Tuesday 1 July 2014

SUAREZ AMUOMBA MSAMAHA CHIELLINI

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Suarez amuomba msamaha Chiellini kwa mara ya kwanza

Mshambulizi wa Uruguay na Liverpool ya Uingereza Luiz Suarez sasa amemuomba msamaha mlinzi wa Italia Giorgio Chellinii kufuatia tukio la kumng'ata timu hizo zilipokuwa zicheza mechi ya mwisho ya makundi huko Brazil.

Suarez aliandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Twitter ''baada ya kuketi nyumbani na familia yangu na kutulia imenijia kuwa tukio la kumng'ata Chellini ni la kusikitisha na kwamba sitarudia tena .
Suarez alimng'ata mlinzi wa Italia Giorgio Chiellini Uruguay ilipowalaza mabingwa hao wa zamani wa dunia 1-0 jumanne iliyopita.“ninajutia sana tukio hilo na ninamuomba msamaha Chellini .ukweli ni kwamba anauguza jereha la kuumwa baada ya kugongana naye katika mechi hiyo .''
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger