JESHI
la Polisi Mkoa wa Arusha linamsaka kwa udi na uvumba, muuza nyama
jijini hapa, Lucas Lomayany Molel (37) mkazi wa Ilboru kwa madai ya
kumuua mkewe wa ndoa, Agnes Lucas (24) kwa kumcharanga na sime kwa kile
kinachoelezwa kuwa ni kutokana na wivu wa mapenzi.
Dada wa Lucas Lomayany Molel (37) anayesakwa kwa kumuua mkewe wa ndoa, Agnes Lucas (24), akiwa katika chumba kilichotumika kwa mauaji hayo.Akisimulia kuhusu mauaji hayo, ndugu wa marehemu aitwaye William Lomayany alisema usiku wa tukio, saa 4, mtuhumiwa alirejea nyumbani kwake na kutomkuta mkewe, akamsubiri hadi saa 6 usiku, mke akarejea.
Godoro la kitanda alipokuwa analala marehemu, Agnes likiwa limechafuka kwa damu.William alizidi kusema kuwa, wawili hao walianza kugombana kwa maneno lakini baada ya muda hali ya utulivu ilirejea, ndipo asubuhi ilipopatikana taarifa za kuuawa kwa Agnes jambo lililotafsiriwa kuwa huenda utulivu huo tayari Agnes alishauawa.
Ndoo ikiwa na damu ya Marehemu Agnes Lucas.Ilidaiwa kuwa, baada ya taarifa hiyo, majirani waliingia ndani ya chumba hicho na kuukuta mwili wa marehemu ukiwa umelala kwenye dimbwi la damu huku akiwa mtupu.
Agnes Lucas, enzi za uhai wake, akiwa kwenye picha ya pamoja na mumewe, Bw. Lucas Lomayany Molel.“Nilikwenda kufunga mlango, baba aliondoka bila kusema chochote. Lakini jana usiku (Julai 6) baba alimpiga sana mama na alinipiga na mimi wakati namwambia amsamehe,” alisema Jessica.
Majirani wa wanandoa hao, wamelaani mauaji hayo na kusema Lucas hakupaswa kumuua mkewe badala yake angewashirikisha watu wengine wakiwemo wazazi wamkanye kama alikuwa akimsaliti.
“Kwa jinsi Lucas alivyokuwa mpole sikutegemea kama angemuua mkewe kikatili, kama alikuwa akimsaliti angewaeleza wazazi wake ili wamkanye,” alisema jirani yao ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa, uchunguzi unaendelea na jeshi lake linamsaka mtuhumiwa huyo.
0 comments:
Post a Comment