Thursday 31 December 2020

Results Based Mgmt Specialist at UNDP

Background The UN Resident Coordinator’s Office (RCO) in Tanzania supports the Resident Coordinator in promoting attainment of the Sustainable Development Goals and the Africa Agenda 2063. It provides strategic guidance and coordination assistance for the design and delivery of the UN’s Cooperation Framework, UN Development Assistance Plan 2015-2022 (UNDAP II). Under the direct guidance and […]

The post Results Based Mgmt Specialist at UNDP appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Technical Lead, Family Planning at Americares

TITLE: Technical Lead- Family Planning (TL-FP), Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) project DEPARTMENT:  International Partnerships & Programs REPORTS TO:  Tanzania Project Director, Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) project ASSIGNMENT TYPE:  Full-time LOCATION:  Mwanza, Tanzania LENGTH:  24-months with possibility to extend based on performance and budget ABOUT AMERICARES:  Americares is a health-focused relief and development organization that saves […]

The post Technical Lead, Family Planning at Americares appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Technical Lead, Maternal, Neonatal and Child Health at Americares

TITLE: Technical Lead- Reproductive Maternal Neonatal and Child Health (TL-MNH), Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) Project DEPARTMENT:  International Partnerships & Programs REPORTS TO: Tanzania Project Director, Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) project ASSIGNMENT TYPE: Full-time LOCATION:  Mwanza, Tanzania LENGTH: 24-months with possibility to extend based on performance and budget ABOUT AMERICARES:  Americares is a health-focused relief and […]

The post Technical Lead, Maternal, Neonatal and Child Health at Americares appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Monitoring, Evaluation and Learning Specialist at Americares

TITLE: Monitoring, Evaluation, and Learning (MEL) Specialist, Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) Project DEPARTMENT: International Partnerships & Programs REPORTS TO: Tanzania Project Director, Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) Project ASSIGNMENT TYPE:  Full-time LOCATION:  Mwanza, Tanzania LENGTH: 24-months with the possibility to extend based on performance and budget ABOUT AMERICARES:  Americares is a health-focused relief and development organization that […]

The post Monitoring, Evaluation and Learning Specialist at Americares appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Technical Lead-Community Engagement and Social Behavior Change (TL-CES) at Americares

TITLE: Technical Lead-Community Engagement and Social Behavior Change (TL-CES), Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) Project DEPARTMENT: International Partnerships & Programs REPORTS TO: Tanzania Project Director, Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) project ASSIGNMENT TYPE: Full-time LOCATION: Mwanza, Tanzania LENGTH:  24-months with possibility to extend based on performance and budget ABOUT AMERICARES:  Americares is a health-focused relief and development organization that […]

The post Technical Lead-Community Engagement and Social Behavior Change (TL-CES) at Americares appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Finance Officer at BRAC

Overview BRAC is one of the world’s largest development organisation having extensive development programmes globally. BRAC’s vision is a world free from all forms of exploitation and discrimination where everyone has the opportunity to realise their potential. We use an integrated model to change systems of inequity through social development programmes, humanitarian response, social enterprises, […]

The post Finance Officer at BRAC appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

UONGOZI WA MALUNDE 1 BLOG UNAWATAKIA WASOMAJI & WADAU WAKE HERI YA MWAKA MPYA 2021


Tunawashukuru sana wasomaji na wadau wa Malunde.com kwa ushirikiano mkubwa mliotuonesha katika mwaka 2020 na kuifanya Malunde 1 blog kuwa Blog Bora yenye kuaminika kwa habari na matukio ikiwa na watembeleaji zaidi ya Milioni 49 na Laki 7 hadi kufikia Desemba 31,2020.

Tunawaomba  ushirikiano zaidi katika mwaka 2021 na tunaahidi kuboresha zaidi huduma zetu ili wasomaji na wadau wetu waendelee kufurahia ulimwengu wa Digitali kwa kupata habari na matukio kiganjani mwao kwa wakati muafaka kupitia https://ift.tt/2gKJ5nm na Aplikesheni ya Malunde 1 blog inayopatikana Google Play/ Play store. Pakua <Hapa> au mitandao yetu ya  Kijamii ikiwemo Twitter, Facebook na Instagram

Ili kuboresha zaidi huduma zetu tutumie ushauri,maoni kupitia Email : malundekadama@yahoo.com Phone/WhatsApp +255 757 478 553 ,+255 625 918 527.

Tunaomba Mtusamehe  kama tuliwakwaza kwa chochote mwaka 2020 na Tunawatakia kila lililo jema  na mkatimize mipango mliyopanga kuifanya mwaka 2021....Mungu awabariki sana.

Uongozi Malunde Media


Share:

YANGA SC YANUSURIKA KUCHAPWA SUMBAWANGA...TANZANIA PRISONS WAILAZIMISHA SARE YA 1-1

VINARA, Yanga SC wameendeleza rekodi ya kupoteza mechi katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu huu baada ya leo kulazimisha sare ya 1-1 na wenyeji, Tanzania Prisons Uwanja wa Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.

Kwa ushindi huo, Yanga SC inafikisha pointi 44 baada ya kucheza mechi 18 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi tisa zaidi ya mabingwa watetezi, Simba SC ambao hata hivyo wana mechi tatu mkononi.

Baada ya dakika 45 ngumu za kipindi cha kwanza, Tanzania Prisons wakawashitua Yanga SC kwa bao la Jumanne Elfadhili dakika sita tu ndani ya kipindi cha pili akimalizia kazi nzuri ya Nurdin Chona.

Pilikapilika za Yanga zikafanikiwa kuzaa matunda dakika 12 kabla ya filimbi ya mwisho, mkombozi akiwa na mchezaji mpya kutoka Burundi, Said Ntibanzokiza.

Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Azam FC imeibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Polisi Tanzania bao pekee la Ismail Aziz dakika ya 88 Uwanja wa Chuo cha Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Pamoja na ushindi huo, Azam FC inayofundishwa na kocha wa zamani wa Yanga SC,Mzambia George Lwandamina inabaki nafasi ya tatu na pointi zake 32 baada ya mechi 17.

Uwanja wa Mkwakwani Jijini, bao la dakika ya 76 la Rashid Chambo likawanusuru wenyeji, Coastal Union kulala mbele ya Namungo FC ya Ruangwa mkaoni Lindi iliyotangulia kwa bao la Iddi Kipagwile dakika ya 10 timu hizo zikitoa sare ya 1-1. 

Kikosi cha Tanzania Prisons kilikuwa; Jeremiah Kisubi, Michael Mpesa, Benjamin Asukile, Vedastus Mwaihambi, Nurdin Chona, Jumanne Elfadhil, Salum Kimenya/Ezekia Mwashilindi dk71, Lambert Sibiyanka, Mohammed Mkopi/ Kassim Mdoe dk80, Samson Mbangula na Jeremiah Juma/Marco Mhilu dk9-+4.

Yanga SC; Metacha Mnata, Kibwana Shomari, Yassin Mustapha, Lamine Moro, Bakari Mwamnyeto, Mukoko Tonombe, Tuisila Kisinda, Feisal Salum, Michael Sarpong, Said Ntibanzokiza/Waziri Junior dk86 na Farid Mussa/Deus Kaseke dk61.

 CHANZO - BINZUBEIRY BLOG

Share:

Uchawi Mbeya : MWANAMKE MWENYE UJAUZITO WA MIEZI 9 AJIKUTA HANA MIMBA

Picha ya mwanamke mwenye mimba.

Taharuki imeibuka kwa wakazi wa kitongoji cha Iyula A katika kata Iyula, wilayani Mbozi, baada ya mwanamke mmoja Mariam Mligo (19) anayedaiwa kuwa mjamzito wa miezi tisa, ujauzito wake kupotea katika mazingira tata muda mfupi baada ya kushikwa na uchungu.

Tukio hilo lililozua taharuki kubwa katika Kata ya Iyula, ambapo mama huyo awali alipaswa kujifungua Desemba 25, 2020, na baadaye mama huyo kujikuta hana ujauzito.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Iyula A, Mawazo Mwamlima, amesema kuwa tukio hilo limesababisha taharuki na sintofahamu kwa wakazi wa kitongoji hicho kwa kuwa si tukio la kawaida na kwamba hata mara baada ya kumpeleka hospitali hakuonesha dalili yoyote ya kwamba labda amejifungua.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa wilaya ya Mbozi, Dkt. Mponjoli Mwangosi, amethibitisha kumpokea mwanamke huyo katika kituo hicho cha Afya Iyula akiwa katika hali ya kuchanganyikiwa, ambapo uchunguzi wa awali ulionesha kuwa mama huyo hakuwa na ujauzito.

Aidha Dkt. Mponjoli ameongeza kuwa hali hiyo ipo kwenye mambo ya uzazi kwa akina mama na kuna kitu kinaitwa mimba isiyo halisia ‘Pseudocyesis Pregnance”, hali hiyo huwaingiza watu wengi kwenye migogoro ya ndoa na kuibua taharuki wakisema kuna mambo ya kishirikina, hali hii ambayo hutokana na magonjwa ya wanawake.

Chanzo- EATV
Share:

VITA DHIDI YA UKEKETAJI YALETA MAFANIKIO SINGIDA


Baadhi ya vifaa vinavyotumika kwenye Ukeketaji vikisalimishwa na Ngariba aliyetangaza kuachana kazi hiyo
Mmoja wa Wadau wa kupinga vitendo vya  Ukeketaji, Patrick Kasango  akitoa elimu kwa wananchi

Na Abby Nkungu, Singida


VITA dhidi ya ukeketaji wanawake na watoto wa kike imeanza kuonesha mafanikio mkoani Singida baada ya wazazi na walezi wa kike waliokuwa wanatajwa kuwa kikwazo kikubwa katika suala hilo, kuanza kujitokeza hadharani kupinga mila hiyo potofu yenye madhara makubwa kiafya.

 

Awali, ilielezwa kuwa licha ya juhudi kubwa za Serikali na Mashirika mbalimbali kudumisha usalama na ulinzi wa mtoto kwa kuzuia mila hiyo potofu, wazazi na walezi wa kike waliendelea kuwa kikwazo kwa kubuni mbinu mpya ya ukeketaji watoto wachanga kwa siri ili kukwepa mkono wa sheria.

 

Ilielezwa kuwa baada ya Serikali kutunga Sheria inayotaja ukeketaji kuwa kosa la jinai, baadhi ya wazazi na walezi wa kike walikuja na mbinu mpya ya kufanya kitendo hicho kiovu na cha kikatili kwa siri usiku wa manane kwa kumsugua mtoto mchanga sehemu zake za siri kwa majivu au chumvi aina ya magadi hadi damu itoke au kukata kwa kucha sehemu hiyo ili kutekeleza mila hiyo potofu.

 

Hata hivyo, Mratibu wa Shirika la ESTL linalotekeleza Mradi wa kupinga ukatili wa kijinsia katika Wilaya ya Singida, Filbert Swai anasema baada ya elimu kutolewa kwa wingi, yapo mafanikio yaliyoanza kujitokeza kama vile baadhi ya  ngariba, wazazi na walezi wa kike kuanza kupinga mila hiyo hadharani.

 

“Ikiwa wazazi wa kike na baadhi ya ngariba ambao ndio walikuwa vinara wa kufanya jambo hilo kwa siri usiku wa manane, sasa wameanza kujitokeza mchana kweupe na  kutangaza  kupinga mila hiyo kwenye mikutano ya hadhara ni dhahiri kuwa vita hii tunaenda kushinda” alisema na kuongeza;

 

Pamoja na kudumisha mila,  wengi walishindwa kuacha vitendo hivyo kutokana na dhana potofu kuwa ukeketaji ni tiba ya ugonjwa unaojulikana kienyeji kama 'lawawala'. Baada ya kutumia waatalamu wa afya kutoa elimu kuwa 'lawalawa' inaweza kuzuiwa kwa kuimarisha usafi sehemu za siri za mtoto, baadhi yao wameacha".

 

Ngariba mstaafu, Halima Ntandu (76) Mkazi wa Ntuntu wilayani Ikungi alisema yeye ameacha kabisa kufanya ukeketaji baada ya kupata elimu kupitia vyombo vya  habari na mikutano ya hadhara juu ya madhara ya ukeketaji na hatua zinazoweza kuchukuliwa iwapo mtu atabainika kukeketa.

 

“Tulianza kufanya usiku wa manane lakini nikaja kuambiwa na wajukuu wangu kuwa bibi wameandika hadi kwenye magazeti kuwa mmebadili mbinu, nikasema yuuu nisije kikafungwa bure  na uzee huu, nikaacha kabisa!!” anasema bibi huyo na kutoa mwito kwa ngariba wenzake kustaafu kwa hiari. 

 

 

Daktari Bingwa Mshauri wa magonjwa ya Wanawake na Watoto katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Singida,  Dk Suleiman Muttani alipohojiwa alisema ingawa mila hiyo imeanza kupungua, bado ni kikwazo cha ulinzi na usalama wa mtoto mkoani Singida kutokana na athari za kiafya na kisaikosojia zinazomkuta mhusika ikiwa ni pamoja na athari za  muda mrefu na muda mfupi.

 

"Athari hizo ni kutokwa na damu nyingi sehemu za siri au wakati mwingine kusababisha kifo na maambukizi ya magonjwa ya Ukimwi na mengine. Magonjwa ya kuambukiza ya mara kwa mara yanayoweza kumfanya mtoto kuwa tasa anapofikia ukubwani, uharibifu wa mfumo wa njia ya uzazi, matatizo wakati wa kujifungua na kutofurahia tendo la ndoa wakati wa kujamiana kutokana na kovu linalobaki baada ya majeraha kupona" alifafanua Dk Muttani.

 

Kwa mujibu wa takwimu za utafiti wa Kidemografia na Afya (TDHS), kiwango cha ukeketaji wanawake wenye umri wa miaka 15 - 49 kimekupungua kutoka asilimia 18 mwaka 1996 hadi kufikia asilimia 10 mwaka 2016. 

Share:

Makubwa Haya : JOGOO AGOMA KUUZWA SOKONI


Picha ya jogoo
Wananchi wa kijiji cha Luanda Kaunti ya Vihiga nchini Kenya wameachwa na mshangao mkubwa na kuchanganyikiwa baada ya jogoo anayedaiwa kuibwa katika Kaunti nyingine kukataa kuuzwa licha ya bei yake nafuu.

Mwizi aliyekuwa amemleta jogoo wa kuiba katika soko la Luanda alijikuta katika wakati mgumu baada ya kutaka kumuuza jogoo huyo.

Jogoo alikataa kuuzwa hata baada ya mnunuzi kupatikana wa bei nafuu ambapo hali hiyo iliwafanya watu kumhoji mwizi huyo alikomtoa kuku huyo.

Mdakuzi wetu aliyeshuhudia sinema hiyo anasema kuwa, yeye pia alichanganyikiwa kama walivyochanganyikiwa wengine, baada ya kugundua kuwa, Jogoo huyo kutoka Kaunti ya Siaya, alimkatalia mwizi (kwa jina William) kila mara alipotaka kumuuza. 

Tukio hilo lilitokea na kujirudia mara 4 hadi watu waliokuwa sokoni walipoanza kushuku na kuamua kumkabili mtu huyo.

Walimhoji kumhusu jogoo huyo ambaye bei yake ilikuwa KSh 800, bei ya kutupa.

Wafanyabiashara katika soko hilo, walimhoji William na kutaka kufahamu ni kwa nini jogoo huyo alikuwa akionyesha tabia isiyokuwa ya kawaida. 

Kwa kuwa soko hilo lipo mpakani, inadaiwa mwenye kuku huyo alikuwa amefika katika soko hilo na alikuwa akimsaka kuku huyo.

Baada ya muda wakimhoji, kumbe taarifa ilikuwa imemfikia mwenye jogoo ambaye alifika na hatimaye kumtambua kuku wake aliyekuwa ametoweka. 

Katika hali ya kushangaza sana, mtu huyo alisema amefanya urafiki mkubwa na mifugo wake, na kwamba ni vigumu mtu yeyote kumwibia. 

Aliondoka na kuku wake huku husika wa wizi akiponea kichapo kwa kupigwa kitutu na umma.

Hata hivyo, ilidaiwa mwenye jogoo huyo ni mganga ambaye nguvu zake na dawa zilichangia kuku huyo kukataa kununuliwa kwani sio hali ya kawaida.

Chanzo - Tuko News blog

Share:

MUUAJI HATARI WA KUVIZIA MAKAHABA AFARIKI DUNIA


Samuel Little, mtu aliyetajwa na shirika la kijasusi la FBI kama muuaji mkubwa wa kuvizia katika historia ya Marekani amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80.

Little alifariki dunia katika hospitali ya mjini California siku ya Jumatano, idara ya magereza imesema. Alikuwa akihudumia kifungo cha mauaji ya wanawake watatu.

Lakini kabla ya kifo chake , alikuwa amekiri kuwaua wanawake 93 kati ya mwaka 1970 na 2005.

'Little aliwalenga watu waliokuwa hawawezi kujitetea, wengi wao wakiwa makahaba ama watumiaji wa mihadarati' , walisema maafisa.

Akiwa Bondia wa zamani , Little angewaangusha waathiriwa wake kwa kuwapiga ngumi kabla ya kuwanyonga - ikimaanisha kwamba hakukuwepo ishara zozote , kama vile kuwadunga kisu ama kuwapiga risasi na kwamba mtu huyo alikuwa ameuawa.

Badala yake vifo vyake vingi vilidaiwa kula dawa kupitia kiasi ama vya ajali na havikuchunguzwa.

Baadhi ya miili haijapatikana , kitengo hicho kilisema.

Mwaka uliopita FBI lilisema kwamba wachambuzi wake walisema kwamba madai yote aliokiri kutekeleza yalikuwa ya kweli.

Pia walitoa picha za waathiriwa aliowachora wakati akiwa jela katika jaribio la kuwatafuta aliowaua.
Shirika la FBI lilitoa michoro ya Samuel Little kwa matumaini kwamba waathiriwa watatambulika.

Little alikamatwa mwaka 2012 kwa mashtaka ya kutumia mihadarati mjini Kentucky na kusafirishwa hadi California, ambapo maafisa walitafuta vinasaba vyake .

Tayari alikuwa na rekodi mbaya ya uhalifu akiwa na mashtaka ya wizi wa mabavu hadi ubakaji katika maeneo mbalimbali Marekani.

Vinasaba vya DNA vilimuhusisha na mauaji ya watu watatu ambao hayajatatuliwa kutoka 1987 na 1989 katika kaunti ya mji wa Los Angels.

Alikataa kufanya makosa lakini hatimaye alipatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo cha maisha , bila fursa ya kuachiliwa katika siku za usoni.

CHANZO - BBC SWAHILI

Share:

WANAFUNZI 294 WAKATISHA MASOMO YAO DODOMA, SINGIDA


Mtafiti Jacob Kateri akichukua maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wa elimu Chamwino, Dodoma.
Mtafiti, Jacob Kateri akifafanua jambo kwa wadau wa elimu katika Halmashauri ya Wilya ya Chamwino, Dodoma.

Na Abby Nkungu, Singida
Jumla ya wanafunzi 294 wamekatisha masomo yao katika shule 20 za msingi za halmashauri za wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma na Singida mkoani Singida katika kipindi cha mwaka 2018 kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo mazingira ya shule yasiyokuwa rafiki.

Taarifa ya Utafiti ya Action Aid chini ya Mradi wa Kuvunja vikwazo, Haki kodi na Utoaji huduma kwa usawa wa kijinsia uliojikita katika halmashauri hizo, imebaini kuwa walioacha shule ni sawa na ongezeko la asilimia 2.4 ikilinganishwa na asilimia 1.7 mwaka 2017 ambapo wanafunzi 186 tu waliacha shule.

Akiwasilisha taarifa hiyo kwenye mikutano ya wadau wa elimu katika halmashauri hizo kwa nyakati tofauti, Mtafiti Jacob Kateri alisema kuwa katika utafiti huo uliofanyika Januari na Februari mwaka jana, kati ya wanafunzi 294, Wavulana walikuwa 165 na Wasichana 129.

"Hiki ni kiwango cha juu sana ikilinganishwa na Takwimu za Kitaifa za 'Basic Education Statistics in Tanzania' (BEST) ambapo katika kipindi hicho ni asilimia 0.7 tu ya wanafunzi wote ndio walioacha shule", alisema Kateri.

Alitaja baadhi ya sababu za kuacha shule kuwa ni kupata mimba, baadhi yao kupewa uhamisho, mazingira yasiyokuwa rafiki; hasa kwa wasichana balehe na walio na ulemavu pamoja na utoro ambao takwimu zake zinaonesha kuwa upo kwa zaidi ya asilimia 30.

Alibainisha shule zilizofanyiwa utafiti wilayani Chamwino kuwa ni shule za msingi Buigiri Misheni, Chamwino, Mahama, Makang'wa, Mapinduzi, Matembe, Msanga na Sekondari za Chamwino, Mlowa Barabarani na Msanga.

Shule zingine kutoka halmashauri ya wilaya ya Singida ni shule za msingi Endeshi, Ikumese, Ilongero, Kafanabo, Madamigha, Mghunga, Mtinko na Sekondari za Ilongero, Mtinko na Mwanamwema Shein.

Meneja wa Mradi huo, Karoli Kadege alisema kuwa kuna haja ya kila mdau kuwa na jicho la kijinsia katika kuangalia uandikishaji wa wanafunzi akisisitiza kuwa kila mtoto ana haki ya kupata elimu bila kujali kama ana ulemavu au la.

"Mtoto mwenye ulemavu akisoma anampunguzia mzazi wake majukumu ya kumlea", alisema Kadege huku akiomba wazazi na walezi kuangalia uwezekano wa kuwaendeleza kielimu wanafunzi wanaopata mimba wakiwa shuleni.

Wakichangia hoja hiyo, wadau walisema kuwa kuna haja kwa kila mzazi na mlezi kuhakikisha kuwa mtoto wake anasoma hadi kuhitimu badala ya kuacha jukumu hilo kwa walimu pekee.

Walishauri Wenyeviti wa mitaa na vitongoji kutunza orodha ya wanafunzi wote wanaosoma kwenye maeneo yao na kuwafuatilia kwa karibu ili kuwachukulia hatua wazazi na walezi wanaowaachisha shule kwa ajili ya kuchunga mifugo, kulima au wasichana kupewa mimba na wengine kuozwa.
Share:

Rais Magufuli Arejesha Fomu zake za maadili katika ofisi ya makao makuu ya Sekratarieti ya Maadili ya viongozi


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 31 Desemba, 2020 amewasilisha fomu zake za maadili katika ofisi ya makao makuu ya Sekratarieti ya Maadili ya viongozi Jijini Dodoma.

Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike amekabidhi fomu hizo kwa Kamishna wa Maadili, Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesi.

Leo ni siku ya mwisho ya kuwasilisha fomu za maadili kwa viongozi wote kwa mujibu wa Sheria namba 13 ya mwaka 1995 ya Maadili ya Viongozi wa Umma


Share:

VETA, WADAU WAWEKA MIKAKATI UZALISHAJI WA WATAALAMU MAHIRI WA SEKTA ZA KILIMO, UKARIMU NA UTALII


Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha kati ya VETA na wadau wa sekta za Kilimo, Ukarimu na Utalii wanaotekeleza programu ya Uanagenzi Pacha (Dual Apprenticeship Training System) iliyofanyika mkoani Manyara tarehe 30 Desemba, 2020.
Balozi wa programu ya Uwanagenzi Pacha na Mkulima wa mjini Babati, Ndugu Jitu Son, akichangia mada wakati wa warsha hiyo. 
Washiriki wa warsha wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu (katikati). Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Bi. Stella Ndimubenya na Mkuu wa Chuo cha VETA Manyara Ndugu Felix Ole Ndukai. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Ndugu John Mwanja na Balozi wa programu ya Uanagenzi Pacha na Mkulima wa mjini Babati Ndugu Jitu Son.
Mratibu wa Programu ya Uwanagenzi Pacha VETA, Ndugu Francis Komba, akisisitiza jambo kwa washiriki wakati akiwasilisha mada juu ya wajibu wa wadau hao katika kufanikisha utoaji mafunzo kwenye sekta hizo.
Mmoja wa washiriki akichangia mada wakati wa warsha hiyo.
Washiriki wa warsha hiyo walipotembelea moja ya karakana inayotumika kutoa mafunzo kupitia programu ya Uanagenzi Pacha (Dual Apprenticeship training) katika chuo cha VETA Manyara. 
Washiriki wa warsha hiyo wakijadili jambo juu ya utekelezaji wa programu ya Uanagenzi Pacha (Dual Apprenticeship training)
Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Bi. Stella Ndimubenya akichangia mada wakati wa warsha hiyo.
Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo ambao ni wadau wa kilimo, ukarimu na utalii wakifuatilia mada wakati wa warsha hiyo. 

***************** 

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeendesha warsha kati yake na wadau wa sekta za Kilimo na Ukarimu na Utalii na kuweka mikakati ya kuzalisha wataalam mahiri wa sekta hizo kupitia programu ya Uanagenzi Pacha (Dual Apprenticeship Training System, DATS). 

Akifungua warsha ya wadau hao katika chuo cha VETA Manyara Desemba 30, 2020, Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu amesema kuwa mafunzo kupitia programu hiyo yanamwezesha kijana kupata ujuzi wa fani husika akiwa chuoni na sehemu ya kazi, hivyo kumwezesha kwa kiasi kikubwa kujifunza kwa vitendo na kuendana na mahitaji ya soko la ajira pamoja na kupata uzoefu na uelewa wa mazingira halisi ya kufanyia kazi. 

Amesema wadau hao wana mchango mkubwa sana katika kuhakikisha mafunzo ya ufundi stadi yanatolewa kwa ufanisi na kuzalisha nguvukazi mahiri itakayochangia kuongeza tija na uzalishaji kwenye sekta hizo. 

VETA inatambua umuhimu wa kushirikiana na waajiri kwenye sekta mbalimbali kutoa mafunzo kwa kuwa ushirikiano huo unawezesha kuandaa nguvu kazi mahiri zaidi inayoendana na mahitaji halisi ya viwanda hasa kwa kuzingatia kuwa sehemu kubwa ya mafunzo hayo yanafanyika sehemu za kazi,amesema. 

Kwa mujibu wa Dkt Bujulu,programu hiyo imeendelea kufanya vizuri tangu kuanzishwa kwake mwaka 2012 kwa ushirikiano na Hamburg Chamber of Craft (HWK) ya Ujerumani ambapo jumla ya wanagenzi 448 wamefuzu mafunzo hayo kwenye fani za Ukarimu na Utalii, Ufundi Umeme, Ufundi Magari, Ujenzi, na Ufundi wa zana za kilimo. 

Dkt. Bujulu amewataka wadau hao kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa programu hiyo ili kuweza kuandaa wafanyakazi wenye viwango wanaohitajika katika kuleta mapinduzi katika sekta hizo. 

Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Bi. Stella Ndimubenya amesema warsha hiyo imelenga kuwajengea uwezo wasimamizi wa mafunzo hayo viwandani, juu ya namna bora ya kutekeleza programu hiyo, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zitokanazo na utekelezaji wake. 

Mratibu wa programu hiyo Ndugu. Francis Komba amesema kuwa VETA imeamua kutoa mafunzo ya Uanagenzi pacha katika sekta hizo baada ya tafiti za soko la ajira kufanyika katika mikoa mbalimbali na kubaini mahitaji makubwa ya wataalamu wa hoteli na utalii pamoja na ufundi wa zana za kilimo kwa ngazi ya ufundi stadi. 

Balozi wa programu ya Uanagenzi pacha na Mkulima wa mjini Babati Ndugu Jitu Son ameishauri VETA kupanua wigo wa utoaji mafunzo ya ufundi stadi kupitia programu hiyo na kuwezesha vyuo vingi zaidi kutumia programu hiyo yenye manufaa makubwa kwa wanagenzi na waajiri. 

Mmoja wa wasimamizi wa programu hiyo ya Uanagenzi Pacha kutoka Moivaro Lodges, Serengeti Ndugu Musa Elphas amesema kuwa mfumo huo wa mafunzo umesaidia wenye hoteli kupata wafanyakazi bora zaidi kwa kuwa wenye hoteli wanapata fursa ya kushiriki kuwandaa wakati wa mafunzo. 

Naye msimamizi wa wanagenzi pacha kutoka TPC Ndugu Boniface Mwambaya amesema kuwa kiwanda chake kimefaidika na mafunzo hayo kwa kuwapata wanagenzi wanaofanya kazi kwa weledi na umakini. 

Mmoja wa wanufaika wa programu hiyo katika fani ya Ukarimuna Utalii Ndugu Azizi Ally amesema programu hiyo imemsaidia kupata ujuzi kwenye eneo la hoteli na kufanikiwa kujiajiri ambapo kwa sasa anamiliki Mgahawa wake na amefanikiwa kuajiri vijana wenzake wanne na hata sasa ameamua kupeleka vijana wawili kujiunga na mafuzo hayo kama mchango wake kwa jamii na kuwataka waajiri wenzake kuona umuhimu wa kuendelea kushiriki kutoa mafunzo hayo ya uwanagenzi pacha. 

Mfumo wa utoaji mafunzo ya Uanagenzi pacha unahusisha kuhudhuria mafunzo ya vitendo kwenye karakana na darasani (VETA) na kufanya vitendo zaidi katika sehemu za kazi. Mafunzo hayo ni ya miaka mitatu ambapo kwa kila mwaka mwanagenzi anatumia wiki 20 VETA na wiki 32 kwa mafunzo ya viwandani. 

Mfumo wa mafunzo ya Uanagenzi Pacha ulianzishwa mwaka 2011/12 kwa ushirikiano kati ya VETA na Hamburg Chamber of Crafts (HWK) ya Ujerumani, ambapo kwa sasa unatekelezwa katika vyuo vinne vya VETA vya Moshi RVTSC (Ukarimu na Utalii), Dar es Salaam RVTSC (Ufundi Umeme na Ufundi Magari), Simanjiro DVTC (Uashi) na Manyara RVTSC (Ufundi wa Zana za Kilimo). Viwanda na kampuni zaidi ya 150 zimenufaika na mafunzo hayo.
Share:

Waziri wa Mambo ya Nje wa China kufanya ziara Tanzania


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi amesema mtazamo wa Tanzania kwa Bara la Afrika ni kuona linajitegemea kwa kutumia rasilimali zake kufanya maendeleo.
 
Waziri Kabudi ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wake na Waandishi wa habari, ambapo pamoja na mambo mengine amezungumzia ujio wa Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi Januari 7 mwaka 2021.

Ziara ya siku mbili ya Wang Yi hapa nchini, ni muendelezo wa uhusiano wa muda mrefu baina ya Tanzania na China.


Share:

Vanessa Mdee avalishwa pete ya Uchumba na Mpenzi wake Rotimi


MWANAMUZIKI wa Tanzania, Vanessa Mdee, amevalishwa pete ya uchumba na mpenzi wake Rotimi ambaye ni msanii wa filamu ambapo wote kwa sasa wanaishi nchini Marekani.

‘Videos clips’ ambazo zimepostiwa kwenye mitandao ya kijamii zimeonyesha Rotimi akiwa amepiga magoti mbele ya Vanessa huku akimvalisha pete hiyo ya uchumba, kisha wakakumbatiana na kuanza kupigana mabusu.
 
Vanessa amethibitisha hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameweka video mbili moja ikionesha pete aliyovishwa huku nyingine ikiwa ni kipande cha video ya mahojiano aliyowahi kufanya na moja ya vyombo vya habari na kusema ilimgharimu siku mbili tu kujua kwamba Rotimi ndiye atakayekuja kuwa mume wake.

“Mwaka mmoja na nusu uliopita dunia ilicheka niliposema kuwa nilijua kuwa wewe utakuja kuwa mume wangu muda mfupi baada ya kukufahamu, sikuwalaumu kwani hisia unayoipata pale unapokutana na mpenzi wa maisha yako si ya kawaida na haiwezi kuelezeka lakini pia wao walikuwa wakimfahamu Vanessa ambaye hakuwa na mpango wa kuolewa kwa wakati huo,” ameandika Vanessa.

Rotimi naye kupitia ukurasa wake wa Instagrama ameweka video fupi ya pete aliyomvalisha Vanessa akiambatanisha na ujumbe unaoelezea namna anavyompenda mrembo huyo.

“Unanifanya niwe mwanaume bora. Nina deni kwa Mungu kwa kunipa wewe na nitamlipa kwa kukupenda na kukupa kila kitu unachostahili, nakupenda,” ameandika Rotimi.

Uhusiano wa wawili hao ulianza mwaka 2019 baada ya Vanessa kuachana na aliyekuwa mpenzi wake, mwanamuziki wa Tanzania, Jux.

Kwa sasa Vanessa ambaye mwezi Juni alitangaza kuachana na shughuli za muziki anaishi Marekani pamoja na mwanume huyo na mara kadhaa amekaririwa akimsifia kuwa ni mwanaume aliyefanya aitambue thamani ya maisha yake.

Mwanzoni mwa mwezi wa kumi mwaka 2020, Vanessa  na Rotimi walishea picha mitandaoni zikiwaonyesha wamechorana ‘tattoo’ zenye majina yao kwenye miili yao.



Share:

KARIBU EJOS STATIONARY & GENERAL SUPPY ...TUNAPATIKANA KAMBARAGE SHINYANGA MJINI

 

Share:

REA na TANESCO wapewa miezi mitatu kuunganishia wateja Umeme


 Na Mwandishi Wetu,
Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Medard Kalemani, amewaagiza watendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijjini (REA), kuhakikisha wanawaunganishia umeme wateja wote waliolipia ankara za umeme jijini Mwanza na maeneo ya vijijini ndani ya miezi mitatu kuanzia tarehe 30 Desemba, 2020.

Waziri Kalemani ameyasema hayo, tarehe 29 Desemba, 2020, alipokuwa akizungumza na Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kikao kazi cha pamoja kilichofanyika kwenye ukumbi wa  Benki Kuu jijini Mwanza.

Pamoja na agizo hilo la kuwaunganishia umeme wateja hao ndani ya miezi mitatu, Waziri Kalemani, amewaelekeza watendaji hao kuhakikisha wateja wote walioko katika maeneo ya vijijini na kando kando ya miji, wanaunganishiwa umeme kwa gharama ya Shilingi 27,000 bila kujali umbali wa mita 30 kwani ni wajibu wa TANESCO kuwafikishia wananchi nguzo za umeme ili kuwafikia wateja hao.

“Mnataka kila mwananchi awe mita 30 ndipo muwafikishie umeme? Ni kazi yenu kupeleka nguzo hadi muwafikie wananchi hao. Nisisikie mtu anaongelea suala la mita 30.” amesema Kalemani

Vilevile, Waziri Kalemani, ameitaka TANESCO  kuanzisha madawati ya huduma kwa wateja ili kuhakikisha wateja wanapatiwa huduma bora na kwa wakati ili kuwaondolea adha ya kufuatilia maombi ya kuunganishiwa umeme kwenye Ofisi  za TANESCO wilayani.

Amewataka watendaji wa TANESCO kuwafuata wateja mahali walipo na kuepuka kutumia lugha ya kukatisha tamaa kwa wateja ili kujenga mahusiano mazuri na wateja  jambo litakalopelekea kupanua wigo wa wateja na kuongeza mapato kwa Shirika.

” Masurveyor ndio wanaolalamikiwa sana kwa kutoa lugha zinazokatisha tama, ninawasihi mbadilike kuanzia sasa, atakayebainika anatumia lugha mbaya kwa mteja, huyo tutaachana naye na atachukuliwa hatua za kinidhamu. Wateja wote wahudumiwe bila kubaguliwa, tunataka wateja wote wapate umeme bila kubaguliwa.”Amesema Dkt. Kalemani

Aidha,  Dkt. Kalemani, amewapongeza watumishi wa TANESCO kwa utendaji mzuri na kueleza kuwa kwa zaidi ya asilimia 80 utendaji wa TANESCO ni wa Kuridhisha.

Waziri Kalemani pia ameelekeza watumishi walioajiriwa kwa muda, wanaohusika na kazi za kupimia wananchi  maeneo ya kuunganisha umeme, wanunuliwe pikipiki zitakazowawezesha kuwafikia wateja kwa urahisi.

Vilevile, Waziri Kalemani amesisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa kasi, ubunifu na kwa usahihi na amewataka watumishi wa TANESCO na REA kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari katika kikao kazi hicho, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato, amewataka watumishi wote kuzingatia maelekezo yaliyotolewa na Waziri Kalemani, na kueleza kuwa atahakikisha anasimamia na kufuatilia utekelezaji wake kwa ukamilifu.

Kikao kazi baina ya Waziri  Kalemani na watumishi wa TANESCO na REA, ni kikao kazi cha pili baada ya kufanya  kikao na wafanyakazi wa TANESCO Mkoa wa Geita wiki iliyopita. Lengo la vikao hivyo ni kuweka misingi ya pamoja ya utendaji kazi unaolenga kuleta matokeo chanya na ya haraka katika Sekta ya Nishati.


Share:

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Kusitisha Makongamano Au Mikutano Ya Mkesha Katika Maeneo Ya Wazi Siku Ya Tarehe 31 Desemba, 2020.



Share:

TAWA Yatoa Ufafanuzi Kwa Wanao Sambaza Taarifa Za Uzushi Kuhusu Simba Aliye Uawa Songwe.


Kufuatia taarifa zinazo sambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu askari wa  mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania TAWA kumuua Simba katika kijiji cha Ngwala wilayani Songwe ili kunusuru maisha ya watu na kuonekana kuwa wamekiuka haki za wanyama na kuleta mjadala katika mitandao ya kijamii mamlaka hiyo imetoa ufafanuzi kwamba ilikuwa inatekeleza majukumu yake.
 
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari afisa wanyamapori mwandamizi udhibiti wa wanyamapori wakali na waharibifu TAWA Wilbright Munuo, amesema mamlaka inakemea vikali taarifa za opotoshaji zinazo sambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu udhibiti wa wanyamapori wakali na waharibifu.


Amesema jamii inatakiwa kufahamu kuwa kazi zinazofanywa na wataalam wa TAWA zinafanywa kwa kuzingatia sheria ya uhufadhi ya wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009, hivyo hazipaswi kubezwa kwani kufanya hivyo ni kuingilia majukumu ya mamlaka.
 
Aidha amesema sheria ya uhifadhi wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009 inatambua umuhimu wa kulinda maisha ya watu na mali zao dhidi ya wanyamapori wakali na waharibifu, licha ya mamlaka kutumia mbinu  mbalimbali za kuthibiti wanyamapori hao katika vijiji ikiwemo kutishia kwa risasi.


Pia amesema njia nyingine zinazotumika ni kuwapeleka wanyama wakali na waharibifu katika bustani na ranchi za wanayapori kwa kuzingatia mahitaji Ili kuepusha taharuki kwa wananchi.
 
Amesema mamlaka katika kuhimarisha usalama wa maisha ya watu na mali zao imekuwa ikihamisha wanyamapori waliokuwa wakivamia maeneo ya wananchi na kuwarudisha katika maeneo ya hifadhi.

‘‘Mwezi mei,2017 Tembo wanne walivamii maeneo ya chuo kikuu cha dodoma waliwarudisha hifadhini bila ya kuleta madhara kwa wananchi,pia mwezi February 2020 TAWA kwa kushirikiana na taasisi ya utafiti wa wanyamapori Tanzania TAWILI tuliwahamisha Simba 36 ambao waliua ng`ombe zaidi ya 100 katika Vijiji cha Kwitete,makundusi,iharara,robanda,pakinyigoti,nichoka na maeneo ya hifadhi ’’Alisema Wilbright Munuo.
 
Vilevile Munuo ameongeza kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja wa  2020 pekee jumla ya matukio 993 ya wanyamapori kuvamia maeneo ya wananchi yaliripotiwa katika vituo vya TAWA ambapo wanyamapori hao walirudishwa kwenye maeneo ya hifadhi.



Share:

Jeshi La Polisi Latoa Onyo Kwa Watakaovunja Sheria Siku Ya Sherehe Za Mwaka Mpya



Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi Disemba 31



Share:

Wednesday 30 December 2020

Watoto Watatu Wafariki Dunia Kigoma Baada ya Nyumba Kuteketea Kwa Moto


Wototo wawili wa familia moja wamefariki dunia katika kijiji cha Nyarugisu wilayani Kasulu mkoani Kigoma, baada ya nyumba waliyokuwa wakiishi kuteketea kwa moto.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kigoma, -James Manyama amewataja watoto hao kuwa ni Yumwema Festo na Enifa Festo ambao ni raia kutoka nchi jirani.

Kamanda Manyama amesema kuwa, Jeshi la polisi mkoani Kigoma linaendelea kuwatafuta wazazi wa watoto hao wanaodaiwa kukimbia baada ya tukio hilo, kwa hofu ya kukamatwa kwa kosa la kuishi nchini kinyume cha sheria.

Pia amethibitisha kufariki dunia katika ajali ya moto mtoto mwingine katika kijiji cha Mpeta wilayani uvinza, baada ya nyumba alimokuwa akiishi na Wazazi wake kuungua moto.

Kufuatia matukio hayo, Kamanda Manyama amewataka Wazazi na Walezi mkoani humo kuacha utamaduni wa kuwaacha watoto nyumbani bila uangalizi.

Katika hatua nyingine Jeshi la polisi mkoani Kigoma limewataka Wakazi wa mkoa huo kusherekea sikukuu ya mwaka mpya kwa amani na kuepuka kujihusisha na vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani.


Share:

TECNO Kuwazawadia Wateja Wa Camon 16 Na Spark 5Pro Nchi 55 Ya TV


TECNO inaendelea kuwapa furaha wateja wake hii ni baada ya kukabidhi zawadi kwa Bwana Ramadhani Salim aliyejishindia mashine yakufulia, Jacquline Kaseja vocha ya manunuzi yenye thamani ya sh.500,000 na mshindi wa TECNO Spark 5pro Zee la Vyeti aliyepatikana kupitia challenge ya iliyofanyika twitter. 


Zawadi bado zipo nyingi na TECNO inawakumbusha wateja wake kutembelea maduka yote ya simu ili kuendelea kufurahiya zawadi mbalimbali kutoka TECNO kama vile rice cooker, blender, cattle na gift package pindi ununua apo simu yoyote ya TECNO lakini pia endapo ukinunua camon 16 na Spark 5 pro moja kwa moja utaingizwa katika droo kubwa na washindi kuondoka na Smart TV ya nchi 55, droo hii kubwa itachezeshwa live trh 15/1/2021 kupitia @tecnomobiletanzania.

TECNO camon 16 na Spark 5pro ni matoleo mapya kwa kampuni hii nah ii imepelekea simu hizi kuwa muonekano wenye kuvutia na uimara katika utumiaji. Camon 16 ni simu yenye kamera kali kuzidi simu zote za TECNO nyuma ikiwa na MP 48 na selfie ni MP 16, ukubwa wa memory ni 128GB+4GB RAM na battery lenye kudumu na chaji wa muda mrefu la mAh 5000.


Spark 5 pro ni simu yenye kioo kipana cha nch 6.6, Spark 5pro inakupa nafasi ya kuchukua picha kwa ukubwa zaidi kutoka na kuwa na wigo mpana wa kioo vilevile ina MP16 nyuma na selfie MP 8, memory kubwa GB 64+GB 3 RAM na battery lenye kudumu na chaji kwa muda mrefu mAh5000.


Tembelea https://www.tecno-mobile.com/tz/home/#/ 


 




Share:

Dkt. Ndugulile Aipa Siku 90 Shirika La Posta Kuboresha Utendaji Na Ufanisi Wake


Na Prisca Ulomi, WMTH
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile ameipa siku 90 Shirika la Posta Tanzania (TPC) kuboresha utendaji kazi na ufanisi katika kuhudumia wateja na wananchi kwa ujumla katika shughuli za kila siku za uendeshaji wa Shirika hilo

Dkt.Ndugulile ameyasema hayo kwa Bodi, Menejimenti na wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania wakati wa ziara yake ya kutembelea Shirika hilo, Dar es Salaam ambapo aliambatana na Naibu Waziri wake, Mhandisi Kundo A. Mathew, Katibu Mkuu, Dkt. Zainab Chaula na Menejimenti ya Wizara hiyo kwa lengo la kufahamu utendaji kazi wa Shirika ili kuhakikisha kuwa linahudumia vema wananchi

Ameongeza kuwa TPC ipitie mikataba yake ambayo haina maslahi kwa Shirika na isimamie vizuri rasilimali zake ikiwemo viwanja, ofisi na magari kwa kuwa rasilimali ni mtaji na mtaji sio fedha ili rasilimali hizo zitumike kuongeza mapato ya Shirika

Vile vile ameiagiza  Wizara yake kushirikiana na TPC kufanya mapitio ya sera na sheria ya posta ili ziweke kuendana na wakati kuendana na mabadiliko ya teknolojia duniani ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi

Pia, amewakumbusha kuwa na mahusiano mazuri baina ya viongozi, wafanyakazi, menejimenti na wajumbe wa bodi katika mazingira ya mahali pa kazi ili kuboresha na kuongeza utendaji kazi wa Shirika

Naye Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Kundo A. Mathew amelipongeza TPC kwa kutengeneza Mfumo wa Taarifa wa Posta ambao unasimamia na kufuatilia uendeshaji wa Shirika; malipo na ukusanyaji wa mapato; na taarifa za watumishi

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula, ameueleza uongozi wa TPC kuwa Wizara itaendelea kushirikiana nao ili kufanikisha utendaji kazi wa Shirika katika kuhudumia wateja

Mwenyekiti wa Bodi wa TPC, Kanali mstaafu, Dkt. Haruni Kondo na Posta Masta Mkuu wake, Hassan Mwang’ombe wamemshukuru Dkt. Ndugulile kwa ziara yake na kulitaka Shirika liboreshe utendaji kazi wake na wako tayari kufanyia kazi yaliyoelekezwa


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger