Monday 28 February 2022

MISS UKRAINE AINGIA VITANI


Miss Ukraine mwaka 2015, Anastasia Lenna
***
Miss Ukraine mwaka 2015, Anastasia Lenna ametangaza kuingia vitani kusaidia nchi yake katika vita ya Urusi.

Anastasia kupitia ukurasa wake wa instagram ame-post video akiwa anajifunza kutumia bunduki na kusema yoyote atakaevuka mipaka atauawa.

Pia ametawaka wanajeshi wa Ukraine waziondoe alama za barabarani ili kupoteza mwelekeo kwa wanajeshi wa Urusi wakitembea ndani ya nchi hiyo.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEBRUARI 28,2022


Magazetini leo Jumatatu February 28 2022

Share:

SIMBA YACHAPWA 2-0 UGENINI



Na Alex Sonna

WAWAKILISHI Pekee wa Afrika Mashariki na Kati Timu ya Simba imeshindwa kutamba ugenini baada ya kuchapwa mabao 2-0 na wenyeji RSB Berkane Mchezo wa Kundi D Michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mchezo uliopigwa uwanja wa Stade Municipal de Berkane nchini Morocco.

RSB Berkane walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Adama Ba akitumia vizuri mpira wa adhabu (Faulo) dakika 32 akipiga na kwenda wavuni moja kwa moja na kumuacha Aishi Manula hana la kufanya.

Mnamo dakika ya 41 Charki El Bahri aliifungia Berkane bao la pili kwa kichwa akitumia vizuri kona iliyopigwa na Badri hadi mapumziko wenyeji walikuwa mbele kwa mabao 2-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa kila timu kufanya mabadiliko huku Simba wakianza kwa kasi na ya kutafuta bao.

Kwa ushindi huo RSB Berkane wamefikisha Pointi 6 na kupanda hadi kileleni mwa msimamo wa kundi hilo,Simba wanabaki nafasi ya pili wakiwa na Pointi 4,US Gendarmerie wakishika nafasi ya tatu wakiwa na Pointi 4 huku ASEC Mimosas wakiburuza Mkia wakiwa na Pointi 3.

Mchezo mwingine wa kundi hilo US Gendarmerie wameutumia vyema uwanja wao wa nyumbani kwa kuichapa mabao 2-0 ASEC Mimosas kwa mechi hizo timu zote zimemaliza mzunguko wa kwanza na zitaanza kurudiana mwezi wa tatu mwaka huu.
Share:

MFALME ZUMARIDI AKAMATWA NA POLISI MWANZA


Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza linamshikilia Dianna Edward Bundala (Zumaridi) mwenye umri wa miaka 39, mkazi wa mtaa wa Buguku kata ya Buhongwa kwa kosa la usafirishaji haramu wa binadamu wapatao 149.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza Ramadhan Ng'anzi amesema watu hao wametolewa na kusafirishwa kutoka sehemu mbalimbali kisha kuwafungia nyumbani kwake ambapo alikuwa akiwatumikisha, kati yao wanaume ni 57, wanawake 92, na miongoni mwao wapo watoto 24 wanaokadiriwa kuwa na miaka kati ya 4 - 17, ambao wamekatishwa masomo kinyume na sheria, hata hivyo amekuwa akiwaaminisha kuwa yeye ni Mungu anayeponya, kufufua watu na kutatua matatizo yao.

Jeshi la polisi lilipokea amri ya mahakama ya mwanzo mkuyuni tarehe 23.02.2022 iliyowataka polisi kumkamata mzazi wa kike wa mtoto Samir Ally Abbas aliyetakiwa kufikishwa mbele ya mahakama hiyo baada ya kesi ya msingi kusikilizwa. 

Katika utekelezaji wa amri hiyo polisi walifika nyumbani kwa mtuhumiwa Dianna Edward Bundala ambapo ilidaiwa yupo mzazi wa kike wa mtoto huyo na mtoto aliyetakiwa kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo baada ya askari kufika eneo la tukio mtuhumiwa aliongoza wafuasi wake kuwashambulia askari na kuwazuia kufanya kazi yao, ndipo askari waliondoka eneo hilo kwa nia ya kuepusha kutumia nguvu ambayo ingeweza kuleta madhara.

 Tarehe 26.02.2022 Askari polisi walirudi nyumbani kwa mtuhumiwa huyo na kufanikisha ukamataji kwa mujibu wa sheria.

Aidha upelelezi wa kina unaendelea ili kubaini kiini cha watu hao kukusanyika katika nyumba ya mtuhumiwa ambayo sio nyumba ya ibadawala sehemu rasmi ya kongamano. Baada ya upelelezi kukamilishwa mtuhumiwa pamoja na washirika wake katika kutenda kosa watafikishwamahakamani ili hatua atahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.
Share:

Sunday 27 February 2022

GEKUL AELEZA MIKAKATI YA KUKUZA RIADHA KILI MARATHONI


********************

Na. John Mapepele

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Pauline Gekul amewapongeza waandaji wa mbio za Kilimanjaro Marathoni huku akifafanua kwamba tukio hilo ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Michezo nchini inayosisitiza ushiriki wa pamoja kati ya Serikali na wadau katika kuendeleza michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

Mhe. Gekul ameyasema hayo leo Februari 27, 2022 wakati akimkaribisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) ili atoe hotuba yake kwenye kilele cha mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon, 2022 kwenye viwanja vya Chuo kikuu cha Ushirika Moshi.

“Sisi familia ya michezo tunajivunia uwepo wa tukio kubwa namna hii linalowaleta pamoja wanamichezo na wapenzi wa riadha kutoka katika maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi yetu, kipekee niwapongeze Kilimanjaro Premium Lager kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kukuza michezo hapa nchini”. Amesema Mhe. Gekul.

Amesema katika kuhakikisha Serikali inaibua na kuendelea vipaji vya michezo ikiwemo mchezo wa Riadha, Serikali imeandaa Mpango Mkakati wa Utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Michezo nchini.

Ameongeza kuwa Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kusaidia maandalizi na ushiriki wa timu za Taifa zikiwemo timu za riadha katika mashindano mbalimbali ya Kimataifa na kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Shilingi Bilioni 1.5 zimetengwa.

Amefafanua kuwa Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya Michezo na mwaka wa fedha 2021/2022 kiasi cha Shilingi Bilioni 10.5 kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Michezo (Sports Centres) katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Geita na kwamba vituo hivyo vitakuwa ni kichochezo kikubwa kwa vijana wetu kushiriki katika michezo.

Pia, amesema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Wizara ya TAMISEMI wameendelea kuratibu michezo ya Shule za Sekondari na Msingi (UMISSETA na UMITASHUMTA), pamoja na kuteua na kuendeleza Shule 56 za Michezo na amesisitiza kuwa Mkakati huo utasaidia kuibua vipaji vya michezo shuleni ikiwa ni pamoja na kuvilea na kuviendeleza vipaji hivyo. Aidha, Mhe. Majaliwa ametoa maelekezo makubwa matatu kwa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na ameitaka kushirikiana na Wizara ya Maliasili Utalii na muandaaji Executive Solution kuona namna bora ya kuandaa tamasha hili kwa miaka ijayo ili kuwaleta watalii wengi pamoja na kuongeza siku na wadau.

Wizara kushirikiana na Shirikisho la Riadha nchini kuandaa kalenda ya mwaka mzima ya mbio nchi nzima na kuandaa vikao vya wadau wote wa riadha nchini ili kupate mawazo ya kuendesha tamasha hili ili liwe na sura ya kimataifa.

Mbio za Kilimanjaro Marathoni za mwaka huu ni za 20 toka kuanzishwa kwake ambapo zimehusisha Kilomita 42, 21 na kilomita tano huku zikiwa na washiriki wengi zaidi kuliko miaka yote ambapo zaidi ya wakimbiaji 12000 wameshiriki kutoka nchi 56 duniani.
Share:

RAIS SAMIA AMTEUA BRIGEDIA JENERALI MABONGO KUWA MWENYEKITI WA BODI TPC


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Brigedia Jenerali Yohana Ocholla Mabongo, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC).

Brigedia Jenerali Mabongo ni Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Uteuzi huu umeanza tarehe 24 Februari, 2022

Zuhura Yunus

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu
Share:

MAPIGANO MAKALI NA MILIPUKO YARIPOTIWA UKRAINE

Mji mkuu wa Ukraine, Kiev umekabiliwa na shambulio makali ya Urusi usiku wa kuamkia leo Februari 27, 2022. Wakati huo huo, mataifa ya Magharibi yanapanga kuiondoaUrusi kutoka kwenye mfumo wa fedha wa kimataifa (SWIFT).

Taarifa ya jeshi la Ukraine imesema kuwa wanajeshi hao wa Urusi pia wanakabiliwa na upinzani mkubwa ikiwa pamoja na vikosi hivyo vya Ukraine kuzuia shambulio la Urusi karibu na mji wa Kharkiv ulio kaskazini, mashariki mwa Ukraine.

Ofisi ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy imesema kumetokea mlipuko kwenye bomba la gesi, kusini mwa mji mkuu wa Kiev mapema Jumapili. Amri ya kutotoka nje imewekwa katika mji huo mkuu wa hadi kesho Jumatatu.

Balozi wa Ukraine nchini Ujerumani Andrij Melnyk ameelezea furaha yake kutokana na uamuzi wa Ujerumani wa kupeleka silaha nchini Ukraine. Balozi Andrij Melnyk ameliambia shirika la habari la Ujerumani (dpa) kuwa hatua hiyo ni ya kihistoria.
th

Sasa kuna ripoti za mapigano katika mitaa ya Kharkiv. Wanajeshi wa Urusi waliingia katika jiji hilo katika saa moja iliyopita, maafisa wa eneo hilo wanasema.

Picha za mitandao ya kijamii zinaonekana kuonyesha baadhi ya vitengo vya jeshi la Urusi katika jiji hilo. Pia kuna picha zinazoonyesha angalau magari mawili ya Kirusi "Tiger" yakiwaka moto katika jiji hilo.

BBC bado haijathibitisha picha hizi.

Maafisa wa Kharkiv asubuhi ya leo wamewaonya wenyeji kukaa katika makazi na kutoka mitaani.

Social embed from twitter

• Licha ya onyo jana usiku kwamba Kyiv ingeshambuliwa na makombora ya Urusi, mlipuko wa angani hauonekani kutokea.

• Milipuko hata hivyo ilisikika karibu na jiji na ghala la mafuta huko Vasylkiv kusini mwa mji mkuu lilipigwa na kuchomwa moto, kulingana na meya wa eneo hilo. Moto huo ulizusha hofu ya moshi wenye sumu na wakaazi walionywa kufunga madirisha na kusalia majumbani

•Mji wa kusini wa Nova Kakhovka umechukuliwa na wanajeshi wa Urusi, meya wa jiji hilo alisema asubuhi ya leo.

• Wakati huo huo, magari ya Urusi yameingia katika jiji la pili kwa ukubwa nchini Ukraine, Kharkiv, wanasema maafisa wa Ukraine. Mlipuko mkubwa pia ulisikika mapema katika mji huo, ambapo bomba la gesi linasemekana kugongwa

• Maeneo ya makazi huko Kharkiv pia yalishambuliwa, kulingana na huduma za dharura. Mwanamke mmoja aliripotiwa kuuawa na makumi kadhaa kuhamishwa kutoka kwa jengo la orofa tisa

• Takriban vifo sita vya raia pia viliripotiwa katika mji wa Okhtyrka, kaskazini-mashariki mwa Ukraine, kulingana na meya wa eneo hilo.

• Katika saa iliyopita Idhaa ya BBC ya Kiukreni iliripoti akaunti mpya za milipuko huko Kharkiv na Kherson kusini-mashariki.

• Katika hatua ya kuiadhibu Urusi, Umoja wa Ulaya, Marekani na washirika wao watakata benki kadhaa za Urusi kutoka kwa mfumo mkuu wa malipo wa kimataifa, Swift. Pia watafungia mali ya benki kuu ya Urusi

• Australia imekuwa nchi ya hivi punde zaidi kutangaza kuwa itafadhili usambazaji wa silaha hatari kwa Ukraine ili kuisaidia kupambana na Urusi. Hatua hiyo imekuja baada ya Ujerumani kuamua Jumamosi kusambaza silaha kwa Ukraine, ikiwakilisha mabadiliko makubwa ya sera

Share:

WATENDAJI SEKTA YA ARDHI WATAKIWA KUZINGATIA UTOAJI HUDUMA BORA KWA WATEJA

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete akisisitiza jambo wakati wa kufunga kikao kazi cha Menejimenti, Wakurugenzi Wasaidizi na Makamishna wa Ardhi wa mikoa kilichofanyika mkoani Arusha Tarehe 26 Februari 2022. Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa kufunga kikao kazi cha Menejimenti, Wakurugenzi Wasaidizi na Makamishna wa Ardhi wa mikoa kilichofanyika mkoani Arusha Tarehe 26 Februari 2022.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi akizungumza wakati wa kufunga kikao kazi cha Menejimenti, Wakurugenzi Wasaidizi na Makamishna wa Ardhi wa mikoa kilichofanyika mkoani Arusha Tarehe 26 Februari 2022.

Kamishna wa Ardhi nchini Nathaniel Nhonge akizungumza wakati wa kufunga kikao kazi cha siku mbili cha Menejimenti, Wakurugenzi Wasaidizi na Makamishna wa Ardhi wa mikoa kilichomalizika tarehe 26 Februari 2022 mkoani Arusha.

Sehemu ya washiriki wa kikao kazi cha Menejimenti, Wakurugenzi Wasaidizi na Makamishna wa Ardhi wa mikoa wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi (hayupo pichani) wakati wa kufunga kikao hicho cha siku mbili mkoani Arusha Tarehe 26 Februari 2022.

*****************

Na Munir Shemweta, WANMM ARUSHA

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amewataka watendaji wa sekta ya ardhi kuhakikisha wanazingatia utoaji huduma bora kwa wateja ili kuondoa malalamiko kwa wanaokwenda kupata huduma kwenye ofisi za ardhi.

Aidha, Ridhiwani aliwataka watendaji wa sekta ya ardhi nchini kufanya kazi kwa kuzingatia taaluma zao na kuacha kufanya kazi kwa kisingizo cha kutekeleza maagizo ya wanasiasa.

Naibu Waziri Ridhiwani alisema hayo tarehe 26 Februari 2022 wakati akifunga kikao kazi cha Menejimenti, Wakurugenzi Wasaidizi wa Wizara ya Ardhi pamoja na Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa mikoa kilichofanyika mkoani mkoani Arusha.

‘’Wakati mnafikiria kutoa huduma kwa wananchi wetu, ‘customer care’ ni jambo la muhimu sana maana yapo baadhi ya malalamiko kutoka kwa wananchi wetu kuhusu ucheleweshaji wa makusudi wa kupatiwa huduma, suala ambalo kama watendaji wakuu tulipaswa kulishughulikia’’ alisema Ridhiwani.

Akitolea mfano wa mama mmoja aliyemfuata akimlalamikia kukwama kupatiwa hati yake kwa muda mrefu, Ridhiwani alieleza kuwa baada kufuatilia kwa kumpigia simu afisa ardhi kwenye halmashauri husika kuhusiana na malalamiko hayo aliambiwa kuwa, mama huyo hakuwasilisha kitambulisho cha taifa jambo lililomfanya kuhoji ni nani anayepaswa kumpa taarifa mama huyo kwa kuwa taarifa za kitambulisho alipewa yeye na siyo mama mhusika.

Alisema, wizara ya Ardhi inapotaka kukusanya vizuri mapato yatokanayo na kodi ya pango la ardhi basi chanzo chanzo ni utoaji hati za ardhi kwa kuwa wanaopatiwa hati wanakuwa sehemu ya walipa kodi. Kwa mujibu wa Ridhiwani, iwapo Wizara haitapima, kupanga na kutoa hati basi kila siku jukumu lake iitakuwa kukumbushana wajibu wa kukusanya mapato wakati uwezekano wa kufikia malengo haupo kutokana na miundombinu iliyopo.

Aliwataka Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa kusisitiza kwa maafisa ardhi wa halmashauri za wilaya, manispaa na majiji kutambua umuhimu wa kufanya kazi sambamba na kutambua kufanya kazi na watu kwa lengo la kuwa karibu ili kuwafanya wafurahi, wapate hati na kupimiwa maeneo yao.

Akigeukia suala la utendaji kwenye kwa watendaji wa sekta ya ardhi, Ridhiwani aliwataka watendaji wa sekta hiyo kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia taaluma zao na kuacha kufanya kazi kwa kisingizio cha kutekeleza maagizo ya wanasiasa.

‘’Msije kutugeuza viongozi wenu kuwa kivuli cha kujitetea katika utendaji kazi wenu, nawaombeni sana na maagizo haya myashushe mpaka kwa maafisa ardhi katika halmashauri, wasifanye vitu vya ovyo kwa visingizio vya wanasiasa’’ alisema Ridhiwani.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi alisema, kupitia kikao kazi waliweza kujadili mapungufu na kubainisha mikakati itakayosaidia kuondoa mapungufu ya kiutendaji.

Alisisitiza umuhimu wa viongozi wa idara na Makamishna wa Ardhi wa mikoa kuwa wepesi katika kufanya maamuzi na kubainisha kuwa, mara nyingi kumekuwa na mzingo kazi unaosababishwa na ulimbikizaji wa kazi na kutaka kuwepo mkakati wa kumaliza au kuondoa kazi za nyuma na zile zinazojitokeza.

‘’Ni muhimu kuwa wepesi katika kutoa maamuzi na kila mmoja anayefanya kazi afikirie ‘Real time solution’ maana mara nying tunakuwa na mzigo wa kazi kutokana na kulundika kazi na ili kuondoa mzigo huo tushughulikie za nyuma na zile zinazojitokeza’’ alisema Dkt Kijazi
Share:

DC MGEMA AWAPONGEZA WADAU WA SEKTA YA UTALII WALIOSHIRIKI MAFUNZO YA COVID-19 SONGEA


MKUU wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya wadau wa Sekta ya Utalii yaliyofanyika kwa siku tano Songea, Mkoani Ruvuma.

Mkurugenzi wa Fedha Mipango na Utawala wa Chuo cha Taifa cha Utalii CPA Munguabella Kakulima akitoa hotuba ya utangulizi juu ya mafunzo hayo wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo na kutunuku vyeti kwa washiriki.

Mratibu wa Mafunzo Mkoa wa Ruvuma Elina Makanja akitoa utambulisho mara baada ya kuwasili mgeni rasmi kufunga mafunzo hayo.

MKUU wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema akimkabidhi Cheti mshiriki wa mafunzo hayo Queen Joseph wakati wa hafla hiyo.

Maajabu mbogo mshiriki wa mafunzo hayo akipokea Cheti chake kutoka kwa MKuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema.

Watumishi na wakufunzi wa Chuo cha Taifa cha Utalii wakiwa katika picha ya Pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema mara baada ya kumalizika kwa hafla ya kufungwa rasmi mafunzo ya watoa huduma katika mnyororo wa Sekta ya Utalii, Songea. (PICHA: NA HUGHES DUGILO).

Na: Hughes Dugilo, SONGEA.

MKUU wa Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma Pololet Mgema amewataka wahitimu walioshiriki mafunzo ya wadau walioko kwenye sekta ya Utalii yaliyokuwa yakitolewa kwa siku tano na  Chuo Cha Taifa cha Utalii kutumia vema mafunzo hayo ili kuleta ufanisi katika kazi zao.

Amesema kuwa mafunzo hayo yamekuja wakati sahihi ambapo Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inachukua hatua za kukabiliana na janga la UVIKO 19 kwa kuweka mikakati mbalimbali ikiwemo kutoa fedha kuwezesha mafunzo hayo.

MKuu wa Wilaya huyo ameasema hayo wakati wa kufunga rasmi mafunzo ya UVIKO 19 kwa wadau wa Sekta ya Utalii yaliyofanyika kwa siku tano Songea Mkoani Ruvuma, ikijumuisha washiriki kutoka katika Wilaya zote za Mkoa huo.

"Mafunzo haya yakawape hamasa na fursa ya kuibua na kutangaza vivutio vilivyosahaulika kwenye Mkoa wetu wa Ruvuma ili mwisho wa siku viendelee kuwa na tija kwa Taifa kwa kuinua mapato ya nchi na mtu mmoja mmoja" amesema Mgema.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Fedha, Mipango na Utawala wa Chuo cha Taifa cha Utalii CPA Munguabella Kakulima  akizungumza wakati wa hotuba ya utangulizi kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa Chuo hicho Dkt. Shogo Mlozi Sedoyeka, amesema kuwa mafunzo hayo yataenda kuboresha Sekta ya Utalii na kwamba kufungwa kwa mafunzo hayo katika Mkoa wa Ruvuma kunatoa fursa kwa mikoa mingine kupata mafunzo hayo  ambayo ni  mikoa ya Iringa na Mbeya.

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufadhili mafunzo hayo ambayo yanakwenda kuikomboa Sekta ya Utalii katika Mkoa wa Ruvuma.

Mafunzo hayo yanalenga kusaidia Sekta ya Utalii kwa kuhakikisha kila mdau anapata uelewa sahihi wa namna ya kukabiliana na janga la UVIKO 19.

 Mwisho.


Share:

Saturday 26 February 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEBRUARI 27,2022

Magazetini leo Jumapili February 27 2022

 

Share:

Picha : RAIS SAMIA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MTAWALA WA DUBAI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Makamu wa Rais ambaye pia ni Waziri Mkuu wa Umoja wa Falme za Kiarabu UAE na Mtawala wa Dubai Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum mara baada ya kuhutubia katika Maonesho ya Dubai Expo 2020 yanayoendelea katika Mji wa Dubai leo tarehe 26 Februari, 2022. PICHA IKULU

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger