Friday 30 September 2022

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 1,2022














Share:

UNISURE GROUP, PHOENIX OF TANZANIA (PART OF MUA) AND SMART APPLICATIONS INTERNATIONAL EXTEND THEIR STRATEGIC PARTNERSHIP INTO TANZANIA


Today marked another important milestone for the insurance industry as The Unisure Group, Phoenix of Tanzania Assurance Co. Ltd (PTAL), (Part of MUA) and Smart Applications International extended their official strategic partnership into Tanzania at a media launch in Dar es Salaam.

Industry leaders, regulators, key stakeholders and members of the media came together to learn more about how this partnership in East Africa and the Indian Ocean Islands, which was first launched in Nairobi, Kenya, in May, will help transform healthcare in the region.

“We are extremely proud to be adding the Tanzanian market to the existing partnership countries. Tanzania is a key market in terms of growth opportunities in medical insurance in particular,” said The Unisure Group’s Deputy Executive Chairman, Stephen Conway.

“This partnership is unique in that three independent organisations – one insurance company, an international administration and assistance provider, and a medical services facilitator – have agreed to partner on projects that will provide access to quality healthcare across multiple African countries in a fully regulated way.

We’re incredibly excited for the long-term collaborations and new business opportunities that lie ahead for our Umatter International Private Medical Insurance (IPMI) plans and look forward to adding additional countries to the four existing partnership countries.”

As The Unisure Group’s Head of IPMI, Daniel van der Merwe, explained, this partnership not only addresses the regulatory requirements that exist with cross-border insurance transactions, but it will bring quality medical insurance and service delivery to a larger number of members who previously would not have had access to this level of international cover.

PTAL’s CEO, Ashraf Musbally, echoed this commitment to greater access for all, and world-class service and customer care.

“This partnership greatly increases our operational footprint, and with this wider geographical scope, we can assure our clients’ seamless health insurance services globally,” he said. “At the end of the day, our top priority with the Umatter product is to ensure our clients receive personalised, world-class health insurance services across the globe.”

In partnering with Smart Applications International, The Unisure Group and PTAL members benefit from Smart’s biometric systems, resolving the challenge that many insurers have with regard to direct access to medical service providers, billing, and potential cases of fraud.

“Our goal has been to transform access to healthcare through the use of foolproof digital solutions and to increase medical insurance penetration,” said Grace Gathuri, Country Manager at Smart Applications International, Tanzania.

“For the last 18 years, Smart Applications Tanzania has been a leading pan-African technology player. With access to over 10 countries using our Biometric Smart system, we believe that our partnership with Unisure and Phoenix Assurance will catapult the provision of international private medical insurance coverage, both in Tanzania and throughout the region.”

The Unisure Group, MUA and Smart’s strategic partnership extends across East Africa and the Indian Ocean Islands. This includes Kenya, Tanzania, Mauritius, and the Seychelles, with Uganda and Rwanda following in the new year.


Share:

TBS YAONYA WAFANYABIASHARA WANAOKIUKA TARATIBU ZA UINGIZAJI WA BIDHAA ZA MABATI NCHINI

Kaimu Mkurugenzi Mkuu ( TBS), Bw. David Ndibalema akiongea na waandishi wa habari alipotembelea ghala la kampuni ya URHOME inayoagiza na kusambaza bidhaa za mabati kutoka nchini China. Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara kutoka Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Bw. Christopher Mramba akizungumza na waandishi wa habari leo alipotembelea ghala la kampuni ya URHOME inayoagiza na kusambaza bidhaa za mabati kutoka nchini China. Mkurugenzi wa Utekelezaji na Uzingatiaji wa Sheria TBS, Dkt. Candida Shirima akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea ghala la kampuni ya URHOME inayoagiza na kusambaza bidhaa za mabati kutoka nchini China. Meneja wa uthibiti wa Shehena zinazoingia na kutoka nchini Mhandisi Saidi Mkwawa akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea ghala la kampuni ya URHOME inayoagiza na kusambaza bidhaa za mabati kutoka nchini China. Mabati yaliyo chini ya kiwango mali ya Kampuni ya URHOME yaliyozuiwa na TBS kwa ajili ya uteketezaji, maeneo ya Sokota, wilayani Temeke, Dar es Salaam mapema leo.

***************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania limeiandikia barua kampuni ya uagizaji na usambazaji wa mabati nchini URHOME Company Limited kuhakikisha ndani ya siku tatu wamewapatia taarifa ya mabati 2176 kati 125280 yapo wapi baada ya kufanyiwa ukaguzi na kugundulika hayajakidhi viwango.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 30 Jijini Dar es Salaam, Meneja wa uthibiti wa Shehena zinazoingia na kutoka nchini Mhandisi Saidi Mkwawa amesema Kampuni hiyo baada ya kuingiza nchini mabati hayo, TBS ilichukua sampuli na kuzipeleka kwenye maabara ya Shirika ili kubaini kama zimeweza kukidhi viwango stahiki kwa mujibu wa sheria .

Aidha baada ya matokeo ya uchunguzi ilibainika kwamba mabati kutoka kampuni hiyo yameshindwa kukidhi viwango vya ubora vilivyotarajiwa, kama ilivyo taratibu za sheria, kulikuwa na njia mbili aidha kurudisha au kuteketeza na mteja alikubaliana na njia ya kuteketeza na zoezi la uteketezaji lilianza.

"Wakati tukiendelea kuteketeza ambapo mabati hayo awali yalikuwa 125280 tukaja tukabaini mabati 2176 hayapo na taratibu za kisheria zimeshaanza". Amesema

Pamoja na hayo Mhandisi Mkwawa amesema watahakikisha mabati yote yanapatikana na zoezi la uteketezaji litaendelea sambamba na mengine.

Nae Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Bw.David Ndibalema amewahimiza wafanyabiashara na waingizaji wabidhaa kutumia vizuri vibali vya masharti kwa kuhakikisha wanazingatia yale masharti ambayo yamewekwa wakati wa kutoa vibali hivyo.

masharti yenyewe ni kwamba kama mzigo bado upo chini ya uchunguzi mzigo huo hautakiwi usambazwe, kuuzwa au kutumiwa kwa njia yoyote ile na tutaendelea kuchukua hatua za kisheria kwa wale ambao wanakiuka akiwemo huyu ambaye ameingiza huu mzigo wa mabati ambayo yamegundulika yapo chini ya viwango

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara Wizara ya Uwekezaji,Viwanda na Biashara Bw.Christopher Mramba amesema wamesikitishwa na tukio hilo na kukemea ukiukwaji wa masharti ya vibali vinavyowekwa na serikali na kuzingatia sheria na kuendelea kujenga utamaduni wakuzingatia masharti ya ubora wa bidhaa na kamwe serikali haitaacha soko la Tanzania liwe dampo kuweka bidhaa zisizo na ubora.

"Tutaendelea kushirikiana na vyombo vya serikali kufuatilia bidhaa ambazo zimeingia sokoni kinyume na sheria na kuchukua hatua stahiki za kisheria na nitoe wito kwa wafanyabiashara wote nchini kuzingatia uaminifu na matumizi mazuri ya fursa zinazotolewa na serikali za kuweka mazingira wezeshi ya biashara ikiwemo hii fursa ya kutoa kibali cha masharti maalumu ya kutoa mzigo bandarini ili bandari yetu iendelee kuwa na ufanisi unaotakiwa na pasiwe na msongamano ili biashara nyingine ziwezee kufanyika". Amesema
Share:

GGML WAZINDUA MASHINDANO YA SOKA KWA WATOTO WANAOZUNGUKA MGODI

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Geita Gold Mining Limited, Terry Strong akisalimiana na timu ya soka ya watoto wanaozunguka kampuni hiyo kutoka Kata za Mtakuja na Nyankumbu zilizopo mkoani Geita. GGML jana imezindua mashindano ya mpira wa miguu kwa watoto hao ili kukabiliana na changamoto ya watoto wanaokwepa kwenda shule na kuingia kwenye eneo la mgodi na kufanya shughuli za uchimbaji bila ruhusa.
Waliosimama kutoka kulia ni Mratibu wa Miradi inayofadhiliwa na GGML kupitia mpango wa Wajibu wa Kampuni kwa Jamii (CSR), Moses Rusasa; Makamu Rais wa AngloGold Ashant-GGML anayeshughulikia miradi endelevu kwa upande wa Ghana na Tanzania, Simon Shayo; Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong; Afisa Tawala wa mkoa wa Geita, Janeth Jonathan na wageni wengine wakiwa katika picha ya pamoja na timu ya soka ya watoto wanaozunguka mgodi wa GGML.
Waliosimama kutoka kulia ni Mratibu wa Miradi inayofadhiliwa na GGML kupitia mpango wa Wajibu wa Kampuni kwa Jamii (CSR), Moses Rusasa; Makamu Rais wa AngloGold Ashant-GGML anayeshughulikia miradi endelevu kwa upande wa Ghana na Tanzania, Simon Shayo; Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong; Afisa Tawala wa mkoa wa Geita, Janeth Jonathan na wageni wengine wakiwa katika picha ya pamoja na timu ya soka ya watoto wanaozunguka mgodi wa GGML.


Na Mwandishi Wetu - Geita

KAMPUNI ya Uchimbaji Madini ya Dhahabu Geita (GGML) imezindua mashindano ya mpira wa miguu kwa watoto wanaozunguka mgodi huo ili kukabiliana na changamoto ya watoto kuingia kwenye eneo la mgodi na kufanya shughuli za uchimbaji bila ruhusa.

Mashindano hayo yanayohusisha kata za Mtakuja na Nyankumbu za Geita Mjini, yanalenga kuwapatia elimu watoto, walezi na wazazi wao madhara ya kuwatumikisha watoto wadogo katika shughuli za uchimbaji na kuwanyima fursa za kupata elimu.

Katika mashindano hayo, watoto kutoka mtaa wa Nyamalembo na Compound walimenyana na watoto kutoka mtaa wa Elimu na Nyankumbu.

Aidha, akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika uwanja wa General Tyre mjini Geita jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Geita Gold Mining Limited, Terry Strong alisema watoto ni sehemu muhimu katika biashara ya kampuni hiyo.

Alisema GGML imewekeza kwenye shule, hospitali na maeneo mengine ambayo watu wanaweza kupata huduma... ikiwa ni sehemu ya Wajibu wa Kampuni kuisadia Jamii inayozunguka mgodi ambapo kupitia mpango huo, GGML ilijenga zaidi ya madarasa 600 mwaka wa 2018.

“Watoto wadogo ndiyo kizazi cha baadaye na ndiyo wa kwanza kunufaika na uwekezaji wetu. Kampuni yetu inafuata kanuni Elekezi za Umoja wa Mataifa kuhusu Biashara na Haki za Kibinadamu na Kanuni za Hiari za Usalama na Haki za Kibinadamu (VPSHR) (UNGP).

“Kwa hivyo, tumekubali kuwalinda watoto dhidi ya hatari zozote zinazotokana na jinsi tunavyofanya biashara,” alisema.

Alisema idadi ya watoto wanaoingia kwenye shughuli za uchimbaji bila ruhusa imekuwa ya kutisha.

“Kwa kawaida sisi hutumia neno "kuwaokoa watoto" badala ya "kuvamia mgodi " kwa sababu watoto wapo chini ya umri wa watu wazima na wanalindwa na sheria za kitaifa na kimataifa.

“Hata hivyo, kutokana na ufuatiliaji wetu ni kwamba watoto wengi waliookolewa baada ya kuingia kwenye eneo la machimbo bila ruhusa, wengi wao tumekuwa tukiwakuta ndani au nje ya leseni yetu ya uchimbaji,” alisema.

Alisema kwa mujibu wa takwimu walizonazo ni kwamba watoto 680 waliokolewa ndani na nje ya eneo la shughuli za mgodi katika mgodi wa GGML kati ya mwaka 2019 na 2020.

Alisema ili kukabiliana na hili, GGML imekuwa ikishirikiana na serikali za mitaa kuzindua mfululizo wa kampeni za uhamasishaji, ikijumuisha ushirikiano wa moja kwa moja na shule za sekondari na msingi.

Aliongeza kuwa katika juhudi za kuwachangamsha watoto, kuwahusisha na michezo na kuwajengea mtindo bora maisha kwa manufaa ya afya zao, tumeamua kuandaa mashindano ya watoto katika kipindi cha likizo katika hali ya uchangamfu na kwenye kipindi chao cha likizo,

“Tunatarajia kuwa vijana wenye vipaji wataibuka kila mwisho wa shindano, na kwamba wataajiriwa na vilabu vikubwa kama Geita Gold Football Club (inayodhaminiwa na GGML) ili kuzidi kuonesha uwezo wao katika uwanja wa Magogo (pia unaodhaminiwa na GGML). Mpango ni kuwaokoa watoto hawa na kuwasaidia kukuza vipaji vyao,” alisema.

Awali, Makamu wa Rais wa AngloGold- GGML anayeshughulikia miradi endelevu kwa Ghana na Tanzania, Simon Shayo alisema moja ya tunu muhimu za kampuni hiyo ni kuhakikisha jamii inayozunguka mgodi huo inanufaika.

Alisema mipango ya kampuni hiyo inalenga kuboresha sekta ya afya, elimu, michezo na utamaduni ili kukuza vipaji vya watoto hao.

Aidha, Afisa utawala wa mkoa wa Geita, Janeth Jonathan akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Geita, Wilson Shimo, alisema wazo la kuanzisha mashindano hayo lilitokana na kamati iliyoundwa ili kukabiliana na wimbi la watoto wanaofanya kazi hatarishi katika eneo la Nyamatagata lenye mlipuko wa madini.

Alisema licha ya kwamba GGML imejenga uwanja, michezo kwa watoto inatakiwa kuzingatiwa ili kuwaondoa katika wimbi hilo la ajira hatarishi hasa ikizingatiwa watoto wanahusishwa zaidi kuchenjua madini kazi ambayo inahusisha kushika kemikali hatari za mercury.

Naye Afisa Kazi kutoka idara ya kazi mkoani humo, Jofrey Oled alitoa wito kwa wazazi kuacha watoto wapate muda wa kusoma badala ya kuwatumikisha kwenye kazi hatari kwani ni kosa kisheria.

Alisem kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini, mzazi atakayepatikana na kosa hilo atapata adhabu ya kulipa faini Sh milioni tani au kwenda kutumia adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja jela au vyote viwili.


Share:

HII NDIO DAWA YA MATAPELI WA VIWANJA

Share:

PAKUA APP YA MALUNDE 1 BLOG TUWE TUNAKUTUMIA HABARI NA MATUKIO BURE

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 30,2022













Share:

Thursday 29 September 2022

KIVULINI YATOA TUZO ZA UJASIRI NA UBUNIFU KWA VIONGOZI VINARA WA KUHAMASISHA JAMII KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA MWANZA


Mkurugenzi Mtendaji Shirika la KIVULINI, Yassin Ally (kulia) akimkabidhi tuzo Sheikh wa Mkoa Mwanza, Hassan Kabeke
Mkurugenzi Mtendaji Shirika la KIVULINI, Yassin Ally (kulia) akimkabidhi tuzo Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa Mwanza, Isack Ndassa.
Mkurugenzi Mtendaji Shirika la KIVULINI, Yassin Ally (kulia) akimkabidhi tuzo Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Amani ya viongozi wa dini mkoani Mwanza.

 ***
Shirika la kutetea haki za wanawake na watoto (KIVULINI) limetoa tuzo za ujasiri na ubunifu wa kuhamasisha jamii kutokomeza ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto kwa viongozi mbalimbali mkoani Mwanza.


Tuzo hizo zimekabidhiwa na Mkurugenzi wa shirika hilo, Yassin Ally Alhamsi Septemba 29, 2022 kwenye kikao kazi cha Kamati ya kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto (MTAKUWWA) Mkoa Mwanza.


Miongoni mwa viongozi waliokabidhiwa tuzo hizo ni pamoja na Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa Mwanza Isack Ndassa, Sheikh wa Mkoa Mwanza Hassan Kabeke, Kamati ya MTAKUWWA Mkoa Mwanza pamoja na Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa Mwanza.
Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mkurugenzi huyo wa shirika la Kivulini Yassin Ally alisema kumekuwa na uelewa wa kutosha kwa wajamii kutonyamazia vitendo vya ukatili wa kijinsia ambapo wamekuwa wakifichua vitendo hivyo katika madawati ya jinsia, ustawi wa jamii na hata kwenye vyombo vya habari.


“Sasa tunashuhudia matokeo ya MTAKUWWA yametoa elimu na wanajamii na viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini hawanyamazii tena vitendo vya ukatili wa kijinsia hususani kwa wanawake na watoto tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo ilionekana ni jukumu la wadau kama KIVULINI”, alibainisha Yassin.


Naye Sheikh wa Mkoa Mwanza Hassan Kabeke alisema katika kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia katika ndoa, BAKWATA imeanza kutoa mafunzo ya misingi ya ndoa kwa wanaume wa kiislamu kabla ya kufunga ndoa ambapo hapo awali mafunzo ya aina hiyo yalikuwa wakitolewa kwa wanawake pekee.


“Hatua hii itasaidia ndoa kudumu tofauti na sasa ambapo ndoa nyingi huvunjika kutokana na wanaume wengi kutokuwa na ujuzi wa namna bora ya kulea ndoa” ,alisema Sheikh Kabeke.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Share:

TBS YATOA MAFUNZO KWA WAFANYABIASHARA WANAOAGIZA NA KUUZA BIDHAA ZA CHAKULA NA VIPODOZI JIJINI MWANZA


Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limetoa mafunzo kwa wafanyabiashara wanaoagiza na kuuza bidhaa mbalimbali za chakula na vipodozi jijini Mwanza ili kuwajengea uwezo kutekeleza shughuli zao kwa kuzingatia Sheria. 

Mafunzo hayo yamefanyika Alhamisi Septemba 29, 2022 yakiwashirikisha wafanyabishara mbalimbali wakiwemo waagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi, wamiliki wa maghala ya kuhifadhia bidhaa na wamiliki wa maduka makubwa ya bidhaa za jumla. 

Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Wilaya Nyamagana mkoani Mwanza Amina Makilagi amewataka wafanyabishara kuwa wazalendo kwa kuhakikisha wanaingiza nchini bidhaa zenye ubora zisizo na madhara kwa watumiaji 

Amesema Mwanza ni jiji la pili kiuchumi nchini na pia kitovu cha biashara katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki hivyo ni vyema wafanyabishara wakatumia fursa hiyo vizuri kwa kuhakikisha wanaagiza bidhaa zenye viwango na kuzihifadhi katika mazingira salama ili zisiharibike kabla ya kumfikia mtumiaji. 

"Serikalini inayoongozwa na Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuboresha miundombi ya usafiri na usafirishaki ikiwemo ujenzi wa meli mpya katika Ziwa Victoria, bandari kavu ya Fela, reli ya kisasa (SGR) hadi jijini Mwanza na uboreshaji wa uwanja wa ndege wa Mwanza ili kurahisisha shughuli za kibiashara" amesema DC Makilagi. 

Katika hatua nyingine, Makilagi ameonya kuwa wafanyabishara wanaouza bidhaa zenye viambata sumu wanaliangamiza taifa na wanaenda kinyume na lengo la Serikali ya kuhakikisha afya ya wananchi iko salama akisema tafiti mbalimbali zinazoendelea kufanyika zinaonyesha magonjwa kama kansa yanasabanishwa na ulaji wa vyakula pamoja na utumiaji wa vipodozi vyenye viambata sumu. 

Pia Makilagi ameipongeza TBS kwa kuendelea kutoa elimu na semina kwa wadau mbalimbali ili kutambua bidhaa zenye ubora na zile zenye viambata sumu zilizopigwa marufuku akisema kila mdau anapaswa kutimiza wajibu ili jamii iwe salama. 

Naye Meneja wa TBS Kanda ya Ziwa, Mhandisi Joseph Mwaipaja amesema Shirika hilo litaendelea kuchukua hatua kali za kisheria kwa wafanyabishara wanaoingiza sokoni bidhaa zilizopigwa marufuku ingawa kabla ya kuchukua hatua hizo TBS inawaelimishwa kwanza. 

Kwa upande wake mmoja wa wafanyabiashara walioshiriki mafunzo hayo, Mohamed Muhan amesema watazingatia elimu waliyoipata ikiwemo kuagiza na kuuza bidhaa zilizosajiliwa kusajiliwa kisheria ili kwa pamoja kwa kushirikiana na TBS wafanikishe jitihada za kuondoa sokoni bidhaa zenye viambata sumu. 

Share:

NHC YATANGAZA MRADI WA “SAMIA HOUSING SCHEME” KWENYE MAONESHO YA MADINI GEITA


Bi. Domina Rwemanyila Afisa habari Shirika la Nyumba la Taifa NHC akitoa maelezo kuhusu mradi wa Samia Housing Scheme unaojengwa Kawe katika jiji la Dar es Salaam kwenye maonesho ya tano ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika EPZA Bombambili mkoani Geita.

…………………………………….

Shirika la Nyumba la Taifa limejipanga kutekeleza mradi wa SAMIA Housing Scheme unaotarajia kujenga nyumba zaidi ya 5000 na kuzalisha ajira zaidi ya Elfu Ishirini na Sita.

Hayo yameelezwa na Daniel Kure Afisa Mauzo na Masoko Mwandamizi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa wakati akizungumzia ushiriki wao katika Maonyesho ya Madini yanayoendelea Mkoani Geita ambapo amesema kuwa wataanza na awamu ya kwanza katika Mkoa wa Dar es salaam na kisha Dodoma.

Afisa huyo amesema kuwa wameshiriki katika maonyesho hayo ili kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu mradi huo na hivyo kurahisisha upatikanaji wa taarifa na kwa wale wote wenye mahitaji ya nyumba waweze kupata kwa wakati.

Amesema kuwa mradi huo umeangalia vipato vya watanzania wote kwa kuangalia madaraja mbalimbali wakiwemo watumishi wa serikali,sekta binafsi pamoja na wafanyabiashara.

‘Mradi huu hadi utakapokamilika katika awamu zote utagharibu Bill 466 na utekelezaji wake utaanzia eneo la Kawe Tanganyika Packers baada ya hapo ndipo utasambaa kwa nchi nzima na tunatarajia tutajenga Nyumba 5000’amesema Daniel

Daniel amewataka wananchi wote wanaohitaji nyumba wahakikishe wanatumia fursa hiyo mapema kwani wataanza kuutekeleza kuanzia mwezi wa kumi na baada ya miezi kumi na mbili watakuwa wameukamilisha.

Aidha Daniel amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika Maonyesho hayo ili waweze kupata taarifa kamili kuhusiana na mradi huo.

‘Nyumba zetu zinakuwa ghali kwa sababu tunapewa eneo na Halmashauri eneo ambalo hakuna miundombinu ,barabara,maji na umeme hivyo mara nyingi sisi ndiyo tunagharamia na hivyo kufanya gharama kuongezaka na kuwa kubwa na watanzania wanaona kama gharama kubwa lakini ukizingatia gharama zote hizo unaona kabisa ubora wa nyumba zanyewe na huduma tunayoitia ’amesema Daniel

Hata hivyo amesema Shirika la Nyumba la Taifa NHC katika kutekeleza hiyo miradi linaingia katika mchakato wa kununua Ardhi pamoja na kuweka miundombinu mbalimbali ili kurahisisha huduma zote.
Afisa Mauzo na Masoko Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw. Daniel Kure akitoa maelezo kuhusu mradi wa Samia Housing Scheme unaojengwa Kawe katika jiji la Dar es Salaam kwenye maonesho ya tano ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika EPZA Bombambili mkoani Geita.
Afisa Mauzo na Masoko Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw. Daniel Kure na Bi. Domina Rwemanyila Afisa habari Shirika la Nyumba la Taifa NHC wakiwa katika picha ya pamoja kwenye banda la shirika hilo.
Bi. Domina Rwemanyila Afisa habari Shirika la Nyumba la Taifa NHC akioneshwa na Bw. Andrew Mwinuka mnufaika wa myumba za mradi wa Bombabili mjini Geita muamala aliolipa kwa ajili ya kununua nyumba yake katika mradi huo.
Bi. Domina Rwemanyila Afisa habari Shirika la Nyumba la Taifa NHC akimfafanulia jambo Bw. Andrew Mwinuka mnufaika wa mradi wa nyumba za NHC Bombambili mjini Geita aliyetembelea katika banda la shirika hilo kwenye maonesho ya madini mjini Geita.
Bi. Domina Rwemanyila Afisa habari Shirika la Nyumba la Taifa NHC akizungumza na mmoja wa raia wa kigeni waliotembelea katika banda la shirika hlo kwenye maonesho ya madini mjini Geita leo.
Muonekano wa nyumba mbalimbali katika picha zitakazojengwa kwenye mradi wa Samia Housing Scheme Kawe jijini Dar es Salaam.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger