Friday 30 April 2021

Tazama Picha : MKUTANO MKUU MAALUMU WA CCM ...WAJUMBE WAMCHAGUA RAIS SAMIA KUWA MWENYEKITI WA CCM



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa ameshikilia Tuzo yake ya Heshima na Pongezi aliyopewa na Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania (UWT) mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma. PICHA NA IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima kutoka kwa Mwenyekiti wa UWT Gaudensia Kabaka mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.



Viongozi mbalimbali pamoja na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi wakifurahia ndani ya Ukumbi wa Mkutano wa Jakaya Kikwete Convention Centre mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 Jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM baada ya kupigiwa kura zote za Ndiyo na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM uliofanyika leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Samia Suluhu Hassan akiagana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya Mkutano Mkuu wa CCM uliofanyika leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Samia Suluhu Hassan akiwa katika Mkutano Mkuu wa CCM ambao Wajumbe wake Walimchagua kwa Kura zote za Ndiyo kuwa Mwenyekiti Mpya wa CCM leo tarehe 30 Aprili, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.

Share:

SIMBA SC KUCHAPANA NA KAIZER CHIEFS YA AFRIKA KUSINI ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA AFRIKA


Timu ya Simba SC ya Tanzania itakutana na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini katika Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya droo iliyopangwa leo Jijini Cairo nchini Misri.

Mabingwa watetezi, Al Ahly ya Misri nao watamenyana na wapinzani kutoka Afrika Kusini, Mamelodi Sundowns.

Mshambuliaji Mtanzania, Simon Happygod Msuva yeye timu yake, Wydad Casablanca itamenyana na MC Alger ya Algeria. CR Belouizdad ya Algeria pia yenyewe itamenyana na vigogo wengine wa Afrika, Esperance ya Tunisia.

Mechi za kwanza zitachezwa kati ya Mei 14 na 15 na marudiano ni Mei 21 na 22, Simba SC wakianzia nyumbani Dar es Salaam.

ROBO FAINALI
Al Ahly vs Mamelodi Sundowns.
MC Alger vs Wydad Casablanca.
CR Belouizdad vs Esperance.
Kaizer Chiefs vs Simba SC.

NUSU FAINALI
MC Alger / Wydad Casablanca VS Kaizer Chiefs / Simba SC.
CR Belouizdad / Esperance VS Al Ahly / Mamelod Sundowns.
Share:

MWADUI FC YATINGA ROBO FAINALI KOMBE LA TFF BAADA YA KUICHARAZA COASTAL UNION 2-0


TIMU ya Mwadui FC imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Coastal Union ya Tanga jioni ya leo Uwanja wa Mwadui Complex, Kishapu mkoani Shinyanga.

Mabao ya Mwadui FC yamefungwa na Roshwa Rashid dakika ya 14 na Wallace Kiango dakika ya 24.
Mwadui FC inakamilisha orodha ya timu tatu tupu za mikoa inayopakana kufuzu Robo Fainali hadi sasa, nyingine ni Biashara United ya Mara na Rhino Rangers ya Tabora.

Mchezo kati ta wenyeji, Tanzania Prisons na Yanga SC unafuatia hivi sasa Uwanja wa Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.
 Via Binzubeiry
Share:

VIGOGO YANGA WATINGA ROBO FAINALI KOMBE LA TFF BAADA YA KUITWANGA TANZANIA PRISONS 1-0


Vigogo,Yanga SC wamefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Tanzania Prisons Uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga mkoani Rukwa.

Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, mshambuliaji Mburkinabe Yacouba Sogne dakika ya 54 akimalizia pasi ya kiungo Mrundi, Said Ntibanzokiza.

Yanga inaungana na Rhino Rangers ya Tabora, Biashara United ya Mara, Mwadui FC ya Shinyanga na Azam FC ya Dar es Salaam pia kuwa timu zilizotinga Nane Bora hadi sasa.

Michuano hiyo itaendelea kesho kwa mechi kati ya Dodoma Jiji FC na KMC Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na Simba SC na Kagera Sugar Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam wakati keshokutwa JKT Tanzania watamenyana na Namungo FC Uwanja wa Jamhuri, Dodoma kukamilisha Hatua ya 16 Bora.

 Chanzo - Binzubeiry blog

Share:

MANISPAA YA SHINYANGA KUANZISHA MASHINDANO YA USAFI WA MAZINGIRA

 

Mkuu wa idara ya Usafi na Mazingira Manispaa ya Shinyanga Kuchibanda Snatus, akisoma taarifa ya mpango wa kuanzisha mashindano ya usafi wa mazingira kwenye Baraza la Madiwani kwa niaba ya Mkurugenzi. Picha zote na Marco Maduhu
Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi akizungumza kwenye Baraza la Madiwani.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga David Nkulila, akizungumza kwenye Baraza la Madiwani.

***
Na Marco Maduhu, Shinyanga.
Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, inatarajia kuanzisha mashindano ya usafi wa mazingira, kwa ajili ya kuuweka mji huo katika hali ya usafi, pamoja na kupambana na magonjwa yatokanayo na uchafu kikiwemo kipindupindu.

Akisoma taarifa ya mpango huo leo wa kuanzisha mashindano ya usafi wa mazingira, kwenye kikao cha Baraza la Madiwani Manispaa ya Shinyanga, Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira Manispaa hiyo Kuchibanda Snatus, kwa niaba ya Mkurugenzi, alisema lengo la mashindano hayo ni kuhakikisha mji unakuwa safi muda wote.

Alisema mashindano hayo yatajumuisha kata zote 17 za Manispaa ya Shinyanga, Mitaa 55, vijiji 17, Taasisi zote za umma, na binafsi, zikiwamo Shule za Msingi na Sekondari, Masoko, viwanda, ambayo yanatarajiwa kuanza mwezi Julai mwaka huu.

“Maeneo yatakayokaguliwa kwenye mashindano hayo ni usafi wa Kaya, Shule, Masoko, Mitaro, Barabara, Viwanda, na Maeneo ya wazi na utekelezaji utasimamiwa na viongozi wa Serikali za vijiji, mitaa na Kata, kwa kufanya ukaguzi wa usafi wa mazingira kwenye maeneo yote,”alisema Snatus.

“Mshindi wa mashindano haya ngazi ya Kaya na Shule atapewa zawadi ya vifaa vya usafi, Kiwanda na Kata itakayo ongoza watapewa Ngao, Mtaa utapewa Cheti, na watakaofanya vibaya watapewa Kinyago,”aliongeza.

Aidha alisema faida za mashindano hayo ni kuboresha hali ya usafi wa mazingira kwenye maeneo mbalimbali ya Manispaa, kupunguza madharia ya Mbu, pamoja na kutokomeza magonjwa ya kuhara na kipindupindu.

Naye Meya wa Manispaa ya Shinyanga David Nkulila, alisema mpango huo ni mzuri na utasaidia kuondoa kero za uchafu mjini Shinyanga, ambapo mji utakuwa msafi pamoja na kuzolewa uchafu wa kwenye Maghuba kwa wakati, huku akitoa wito kwa madiwani wakatoe elimu ya usafi kwa wananchi.

Nao Madiwani wa Manispaa hiyo ya Shinyanga, walipongeza mpango huo wa mashindano ya usafi wa mazingira kuwa utaleta hamasa kubwa ya kuufanya mji huo kuwa msafi huku kila mmoja akijingamba kupata ushindi.

Pia Baraza hilo la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, limefanya kikao cha siku mbili kujadili ajenda mbalimbali, kwa ajili ya mstakabali wa maendeleo ya Manispaa hiyo.

Madiwani wakiwa kwenye kikao cha Baraza.
Madiwani wakiwa kwenye kikao cha Baraza.
Madiwani wakiwa kwenye kikao cha Baraza.
Madiwani wakiwa kwenye kikao cha Baraza
Madiwani wakiwa kwenye kikao cha Baraza
Madiwani wakiwa kwenye kikao cha Baraza

Na Marco Maduhu- Shinyanga.
Share:

VIJANA WA JKT WALIORUDISHWA NYUMBANI WATAKIWA KUREJEA KAMBINI MEI 7 - 14 , 2021

Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Hassan Mabena akitoa taarifa ya kurejeshwa kwa vijana wa kujitolea katika mafunzo ya JKT kuanzia Mei 7 hadi 14, 2021 baada ya kuwarejesha nyumbani hapo awali.
***
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limewataka vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya kujitolea kuripoti katika makambi waliyopangiwa kati ya Mei 7 hadi 14, 2021 lakini utaratibu huo hautawahusu wenye elimu ya kidato cha sita, cheti, stashahada, shahada na taaluma ya uhandisi.

Kaimu mkuu wa utawala wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Hassan Mabena, amewaambia wanahabari kuwa vijana hao wanatakiwa kuripoti kwenye makambi waliyopangiwa awali.
Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala (JKT), Kanali Hassan Mabena amesema, vijana hao wanatakiwa kuripoti katika kambi walizokuwa wamepangiwa awali kuanzia Mei 7 hadi Mei 14,2021.

“Vijana waliorejeshwa ni wale wenye elimu ya darasa la saba na kidato cha nne, wenye elimu ya kidato cha sita, ngazi ya cheti, stashahada, shahada na wale wenye Taaluma ya Uhandisi wataendelea kusubiri majumbani hadi hapo utaratibu mwingine utakapotangazwa"', amesema Kanali Mabena

Jeshi la Kujenga Taifa ( JKT) limekuwa likiendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo vijana kwa kuwapa stadi za maisha ikiwa ni pamoja na uzalishaji mali, uzalendo, kilimo, ufugaji na kushiriki katika ujenzi wa Taifa.

Mwezi Februari mwaka huu, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) alitangaza kuwarejesha nyumbani zaidi ya vijana 12,000 hadi ambapo wangetangaziwa tena.
Share:

DANIEL CHONGOLO KATIBU MKUU WA CCM, SHAKA ACHUKUA NAFASI YA HUMPHREY POLEPOLE


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimefanya mabadiliko ya viongozi wake wakuu kitaifa ikiwemo nafasi ya Katibu Mkuu iliyokuwa inashikiliwa na Bashiru Ally pamoja na nafasi ya Katibu wa Itikadi na Uenezi iliyokuwa inashikiliwa na Hamphrey Polepole.

Katika Mabadiliko hayo, CCM imempitisha Daniel Chongolo kuwa Katibu Mkuu Mpya wa chama hicho, huku nafasi ya Katibu wa Itikadi na Uenezi ikichukuliwa na Shaka Hamdu Shaka.
Share:

Breaking : LAZARO NYALANDU AIKACHA CHADEMA NA KUREJEA CCM


Lazaro Nyalandu akitangaza kurejea CCM leo
**
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kati, Lazaro Nyalandu ametangaza kurejea Chama Cha Mapinduzi akisema ameamua kurejea nyumbani.

Nyalandu ametangaza kurejea CCM leo Ijumaa Aprili 30,2021 wakati wa Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi Dodoma.

Mara baada ya kutangazwa na Rais wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama hicho Samia Suluhu Hassan kurejea CCM Nyalandu ametoa shukrani zake kwa Mwenyekiti wa Chama hicho,kumpokea ,kumsamehe na kumruhusu kumrejesha katika chama hicho.

“Watanzania wameona nyota yako wamejaa na furaha,Mungu akakuongoze uwepo wangu mbele yako na mkutano huu ni kielezo tosha wewe kuungwa mkono na watanzania wote,”amesema Nyalandu
Share:

SAMIA : SIASA SI UADUI...USHINDI WA CCM 2025 UTATEGEMEA VILE TUTAKAVYOTEKELEZA ILANI YETU


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema Ushindi wa CCM  mwaka 2025 utaletwa kwa namna wana CCM watakavyotekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM huku akisisitiza kuwa  Siasa si uadui hivyo kuviomba vyama vya siasa kutoa ushirikiano katika kuimarisha umoja uliopo.

Mhe. Samia ameyasema hayo leo Ijumaa Aprili 30,2021 wakati wa Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi

Amesisitiza kuwa kazi ya kukiimarisha Chama Cha  Mapinduzi inaendelea kuhusu akibainisha kuwa hatawaangusha wanawake na watanzania kwa ujumla.
Share:

SAMIA SULUHU HASSAN ACHAGULIWA KWA KISHINDO KUWA MWENYEKITI WA CCM


Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi kumchagua kwa kishindo Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Mwenyekiti wa Sita wa CCM kwa kupata kura 1862 hakuna kura ya Hapana hivyo ameshinda kwa asilimia 100.

Nafasi ya MNEC walioshinda ni Happiness Mgongo na Rehema Simba


Share:

PROF. KOMBA ATAKA TSC IONE FAHARI KUHUDUMIA WALIMU WENYE MAADILI

Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Prof. Willy Komba, akifunga mafunzo kwa Kamati za Wilaya za Mikoa ya Kanda ya Ziwa, zinazoshughulikia masuala ya Ajira na Nidhamu kwa Walimu, Aprili 29, 2021 jijini Mwanza.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Mwl. Paulina Nkwama, akitoa hotuba ya kumkaribisha Mgeni Rasmi, ambaye ni Mwenyekiti wa Tume hiyo, Prof. Willy Komba kufunga mafunzo kwa Kamati za Wilaya za Mikoa ya Kanda ya Ziwa, zinazoshughulikia masuala ya Ajira na Nidhamu kwa Walimu, Aprili 29, 2021 jijini Mwanza.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo kwa Kamati za Wilaya za Mikoa ya Kanda ya Ziwa, zinazoshughulikia masuala ya Ajira na Nidhamu kwa Walimu, wakimsikiliza Mgeni Rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Prof. Willy Komba (hayupo pichani), wakati akifunga mafunzo hayo, Aprili 29, 2021 jijini Mwanza.
Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Suzan Nussu kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI (kushoto) na Assela Luena kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa katika mafunzo kwa Kamati za Wilaya za Mikoa ya Kanda ya Ziwa, zinazoshughulikia masuala ya Ajira na Nidhamu kwa Walimu, jijini Mwanza, Aprili 29, 2021.

**********************

Na Veronica Simba – TSC

Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Profesa Willy Komba, ametoa hamasa kwa watendaji wote wa Tume hiyo kusimamia vema suala la maadili kwa walimu ili wajisikie fahari kuwahudumia.

Alitoa kauli hiyo mwishoni mwa juma wakati akifunga mafunzo ya wajumbe wa kamati za wilaya katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, zinazoshughulikia ajira na maadili kwa walimu, chini ya usimamizi wa TSC.

Akifafanua, Prof. Komba aliwataka washiriki wa mafunzo husika, wanaporejea katika vituo vyao vya kazi, kwenda kuwajibika kwa kuwakumbusha walimu maadili na miiko ya kazi yao.

Alisema kuwa, endapo Kamati hizo za Nidhamu zitafanikiwa kuwafikia walimu wote, TSC itafanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya walimu wanaolalamikiwa kukiuka maadili ya kazi yao.

“Sisi sote tuone fahari ya kuwahudumia walimu wenye maadili ambayo watayaambukiza kwa watoto wanaowafundisha na jamii kwa ujumla,” alisema.

Aidha, Mwenyekiti huyo wa TSC aliwasisitiza washiriki wa mafunzo kujenga utaratibu wa kujisomea sheria, kanuni, taratibu, miongozo na nyaraka za serikali kuhusu masuala mbalimbali wanayoyashughulikia ili kujiongezea ufahamu wake.

Vilevile, aliwataka wasisite kuomba ufafanuzi kutoka kwenye Ofisi au Mamlaka nyingine hususan katika masuala yenye changamoto ili kuepuka kukosea katika utendaji wao.

Awali, akitoa hotuba ya kumkaribisha Mgeni Rasmi kufunga mafunzo hayo, Katibu wa TSC, Mwl. Paulina Nkwama alieleza kuwa lengo lilikuwa ni kuwawezesha washiriki kufahamu na kutekeleza majukumu yao ya Tume kwa haki.

Mwl. Nkwama alizitaja mada zilizowasilishwa katika mafunzo hayo kuwa ni pamoja na Kusudi la kuanzishwa kwa Tume ya Utumishi wa Walimu, Muundo na Majukumu ya Tume pamoja na Majukumu ya Tume kuhusu masuala ya Ajira na Maendeleo ya Walimu.

Aliongeza kuwa, mada nyingine zilizowasilishwa ni kuhusu Maadili na Miiko ya Kazi ya Ualimu pamoja na Majukumu ya Mamlaka za Nidhamu na Rufaa kwa Walimu.

Mafunzo hayo ya siku mbili yalifanyika Aprili 28 na 29 mwaka huu jijini Mwanza na kuzishirikisha wilaya zote za Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mwanza, Mara, Kagera, Simiyu na Shinyanga.
Share:

INSTRUCTOR II (ELECTRICAL) at Arusha Technical college

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST INSTRUCTOR II (ELECTRICAL). – 1 POST POST CATEGORY(S) ENGINEERING AND CONSTRUCTION EMPLOYER Arusha Technical college ATC APPLICATION TIMELINE: 2021-04-28 2021-05-12 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To teach up to NTA level 6 and may assist teaching in higher NTA levels; ii. To assist in conducting tutorial and practical exercises for students under […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

LIVE: Mkutano Mkuu Maalum Wa CCM, Dodoma

 LIVE: Mkutano Mkuu Maalum Wa CCM, Dodoma



Share:

Taarifa Ya Kuongeza Kasi Ya Utekelezaji Wa Hatua Za Kujikinga Na Magonjwa Mbalimbali Nchini.



Share:

INSTRUCTOR II (MECHANICAL) at Arusha Technical college

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST INSTRUCTOR II (MECHANICAL) – 1 POST POST CATEGORY(S) ENGINEERING AND CONSTRUCTION WATER, MINING AND NATURAL RESOURCES EMPLOYER Arusha Technical college ATC APPLICATION TIMELINE: 2021-04-28 2021-05-12 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To teach up to NTA level 6 and may assist teaching in higher NTA levels; ii. To assist in conducting tutorial and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

ASSISTANT LECTURER – LIBRARY AND INFORMATION MANAGEMENT SYSTEM(RE-ADVERTISED) at The Mwalimu Nyerere Memorial Academy (MNMA)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST ASSISTANT LECTURER – LIBRARY AND INFORMATION MANAGEMENT SYSTEM(RE-ADVERTISED) – 1 POST POST CATEGORY(S) HR & ADMINISTRATION EMPLOYER The Mwalimu Nyerere Memorial Academy (MNMA) APPLICATION TIMELINE: 2021-04-28 2021-05-12 JOB SUMMARY Candidate should be a person of the highest integrity and professionalism who will work closely with MNMA team to achieve agreed objectives. DUTIES AND RESPONSIBILITIES […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Resident Program Director at International Republican Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Summary Every employee of IRI is responsible for carrying out the Mission of IRI and demonstrating the Core Values in their day to day operations. The Core Values, which are IRI’s foundational building blocks include: Excellence– We believe in quality results delivered by investing in people. Freedom– We believe in exploration and experimentation to be […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Consultant at UN Women

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Background UN Women, grounded in the vision of equality enshrined in the Charter of the United Nations, works for the elimination of discrimination against women and girls, the empowerment of women, and the achievement of equality between women and men as partners and beneficiaries of development, human rights, humanitarian action and peace and security. UN […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Jumbo Operator at North Mara Gold Mine

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POSITION DESCRIPTION: North Mara Gold Mine Limited is seeking to recruit Jumbo Operator to join Underground Production team. The successful candidates for this position will carry out assigned tasks within the guidelines of Company Standard Operating Procedures as well as other assigned tasks within the range of competencies. Key duties are to operate Jumbo drilling rigs […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Retention Assistant (Specific Task) 3 Posts at ICAP

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job no: 495160 Work type: Temporary Full-Time Location: Tanzania – Kagera, Tanzania – Mara, Tanzania – Mwanza, Tanzania – Dar es Salam Categories: Program Management/Implementation/Support ICAP at Columbia University, a global health leader situated within the Columbia University Mailman School of Public Health in New York City, seeks Linkage and Retention Assistants to be based in Mwanza, Mara and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

HIVST Assistant (Specific Task) 2 Posts at ICAP

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job no: 495149 Work type: Temporary Full-Time Location: Tanzania – Dar es Salam, Tanzania – Kigoma Categories: Program Management/Implementation/Support ICAP at Columbia University, a global health leader situated within the Columbia University Mailman School of Public Health in New York City, seeks HIVST Assistants to be based in Kigoma and Dar es Salaam, Tanzania. The HIVST assistant is responsible […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Specialist Trainer – Underground Mine Equipment at Geita Gold Mining

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Geita Gold Mining Ltd (GGML) is Tanzania’s leading gold producer with a single operation in Geita Region. The company is a subsidiary of AngloGold Ashanti, an international gold producer headquartered in South Africa, with operations in more than ten countries, in four continents. The mine is situated in the Lake Victoria Gold fields of North […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 30,2021














Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger