Sunday 31 March 2024

BALOZI DKT. NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU WA KANISA LA NGLCC MKOANI MARA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akisalimiana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, ambaye pia ni Waziri Mkuu wa Tanzania, Ndugu Kassim Majaliwa Majaliwa, alipowasili kushiriki shughuli ya mazishi ya Askofu wa Kanisa la New Life Gospel Community Church (NGLCC), Jimbo la Mara Kaskazini, Fransisca Mwita Gachuma, yaliyofanyika Jumamosi, Machi 30, 2024, huko Komaswa, Tarime Vijijini. Askofu Fransisca alikuwa mwenza wa Ndugu Christopher Mwita Gachuma, ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, kutokea Mkoa wa Mara.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akisalimiana na kuzungumza jambo na Askofu Mkuu wa Kanisa la New Life Gospel Community Church (NLGCC), Dkt. Daniel Ouma (mwenye joho), mara baada ya misa ya kumuombea marehemu, kabla ya mazishi ya Askofu wa NGLCC, Jimbo la Mara Kaskazini, Fransisca Mwita Gachuma, yaliyofanyika Jumamosi, Machi 30, 2024, huko Komaswa, Tarime Vijijini. Askofu Fransisca alikuwa mwenza wa Ndugu Christopher Mwita Gachuma (kushoto mwenye suti), ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, kutokea Mkoa wa Mara. Wengine wanaofuatilia ni viongozi wa Kanisa la NLGCC).
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akishiriki utoaji wa heshima za mwisho, kumwaga mchanga na kuweka shada la maua, wakati wa mazishi ya Askofu wa Kanisa la New Life Gospel Community Church (NLGCC), Jimbo la Mara Kaskazini, marehemu Fransisca Mwita Gachuma, yaliyofanyika Jumamosi, Machi 30, 2024, huko Komaswa, Tarime Vijijini. Askofu Gachuma alikuwa mwenza wa Ndugu Christopher Mwita Gachuma, ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, kutokea Mkoa wa Mara. 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akisalimiana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, ambaye pia ni Mwenyekiti wa UWT Taifa, Komredi Mary Pius Chatanda. Kushoto pichani anayeangalia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Halima Mamuya na aliyeko kulia pichani akiangalia ni Mhe. Christina Mndeme, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Muungano na Mazingira), wakati wa kushiriki msiba wa marehemu Askofu wa Kanisa la New Life Gospel Community Church (NLGCC), Fransisca Mwita Gachuma, huko Komaswa, Tarime vijijini, mkoani Mara, Jumamosi, Machi 30, 2024.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akifurahia jambo wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Issa Haji Usi Gavu (katikati), ambaye pia ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, Oganaizesheni (katikati) na Ndugu Dk. Frank Haule Hawassi, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha (kulia), mara baada ya misa ya kumuombea marehemu, wakati wa mazishi ya Askofu wa Kanisa la New Life Gospel Community Church (NLGCC), Jimbo la Marwa Kaskazini, Fransisca Mwita Gachuma, Jumamosi, Machi 30, 2024, huko Komaswa, Tarime vijijini, mkoani Mara. Askofu Gachuma alikuwa mwenza wa Ndugu Christopher Mwita Gachuma, Mjumbe wa NEC ya CCM Taifa, kutokea Mkoa wa Mara.
Sehemu ya umati wa waombolezaji wakishiriki misa ya kumuombea marehemu, wakati wa mazishi ya Askofu wa Kanisa la New Life Gospel Community Church (NLGCC), Jimbo la Mara Kaskazini, Fransisca Mwita Gachuma, Jumamosi, Machi 30, 2024, huko Komaswa, Tarime vijijini, mkoani Mara. Askofu Gachuma alikuwa mwenza wa Ndugu Christopher Mwita Gachuma, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) Taifa, kutokea Mkoa wa Mara.
Share:

WANAOTOROSHA KOROSHO KWENDA NJE YA NCHI WAONYWA, SIKU ZAO ZINAHESABIKA



Na Oscar Assenga, TANGA.

BODI ya Korosho Tanzania Mkoani Tanga imewaonya wakulima wenye tabia za kutorosha Korosho kwenda kuuza nje ya nchi kuacha mara moja kufanya hivyo kwani siku zao zinahesabika kutokana na vyombo vya dola vinawatambua na watapokamatwa watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Moja ya athari za utoroshaji wa Korosho kwenda nje ya nchi ni pamoja na kutokufikia malengo ya uzalishaji ikiwemo nchi mapato ambayo yangeweza kusaidia katika kuchochea maendeleo kwa wananchi wake.

Onyo hilo na Kaimu Meneja wa Bodi ya Korosho Mkoa wa Tanga Atufigwege Mwakyagi wakati akizungumza na waandishi wa habari namna bodi hiyo ilivyojipanga kukabiliana na vitendo hivyo huku wakiwataka wenye tabia hizo kuacha mara moja

Alisema kwani kufanya hivyo maana yake ni kulihujumu zao hilo pamoja na juhudi za Serikali ni kuhakikisha wakulima wanapata bei nzuri na bora ili kuweza kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo hicho chenye tija.

“Ndugu zangu mnaotorosha korosho kufanya hivyo ni kosa na vyombo vya dola hivyo tambueni siku zenu zinahesabika sisi kama bodi hatutakubali kuona watu wanahujumu zao hilo kwani zinatakiwa kumnufaisha mkulima na Rais wetu Dkt Samia Suluhu ameweka nguvu kuhakikisha mkulima anapata bei nzuri na bora”Alisema

Aidha alisema kwamba wale ambao wanafanya hivyo wanataka kufifisha juhudi za Serikali ambazo ni kuona wakulima wa zao hilo wananufaika nalo na hatimaye kuweza kujikwamua kiuchumi na kubadilisha maisha yao hivyo hawatakuwa tayari kuona zinakwamishwa kwa namna yoyote ile.

Kaimu Meneja huyo alisema mauzo ya korosho msimu uliopita yalikuwa ni tani 741 kwenye mnada uliofanyika wilayani Mkinga na kufanikisha kuingiza fedha kiasi cha Sh.Milioni 703 ambazo wakulima wa zao hilo wameweza kunufaika nalo.

Akizungumzia suala la udhibiti ubora wa zao hilo alisema kwamba wa sasa wamekuwa wakitoa mafunzo kwa wakulima ili kuweza kulima kilimo chenye tija ili kudhibiti ubora kuhakikisha unakuwa mzuri kabla ya kwenda sokoni ambapo wamekuwa wakiuza kwenye mfumo rasmi.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MACHI 31, 2024

 
Share:

UTEUZI; RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI, UTENGUZI NA UHAMISHO WA VIONGOZI MUDA HUU




Share:

Saturday 30 March 2024

SIMBA SC YASHINDWA KUFURUKUTA MBELE YA AL AHLY, YACHAPWA 1-0


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Simba imeshindwa kutamba kwenye uwanja wake wa nyumbani mara baada ya kukubali kupokea kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Al Ahly.

Katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza Al Ahly walifanikiwa kupata bao la Mapema kupitia kwa Ahmed Kouka dakika ya 4 ya mchezo kipindi cha kwanza.

Timu hizo zitarudiana Aprili 5, 2024 ambapo Al Ahly kwenye mchezo huo atakuwa nyumbani mjini Cairo.
Share:

DAWA KIBOKO KWA NGUVU ZA KIUME



Upungufu wa nguvu za kiume ni hali ya kushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu ,shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kutokuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.

CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;

1. Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo

2. Kuvuta sigala na unywaji wa pombe

3. Uzito kupita kiasi na unene uliozidi

4. Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi

5. Kisukari

6. Kuwa na mawazo na wasiwasi

7. Matumizi ya madawa mbalimbali

8. Umri hasa wazee

9. Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili

10. Kuwa na tatizo la kibofu

11. Tabia za kujichua kwa muda mrefu

12. Kutopata usingizi kamili

13. Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa kama kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine

DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni kama;


1. Kuwahi kufika kileleni

2. Kukosa hamu ya mapenzi

3. Kushindwa kurudia tendo la ndoa

4. Uume kusimama kwa ulegevu au kushindwa kusimamisha

5. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo

7. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa)

8. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji


TIBA SAHIHI YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME

FULL POWER
⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50
⇨ Inarutubisha maumbile ya uume na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.

Pia tunatibu Magonjwa mengine kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonda vya tumbo, Kisukari, Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kung’oa


Ndugu mteja Epuka midawa inayouzwa mitaani ambayo sio sahihi kwa matumizi ya binadamu JALI AFYA YAKO OKOA NDOA NA MAISHA YAKO

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27 au 0754568767  utatumiwa sehemu yoyote ulipo
Share:

MBUNGE WA SIMANJIRO OLE SENDEKA ASHAMBULIWA KWA RISASI


Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, Christopher Ole Sendeka inadaiwa amenusurika Kifo baada ya Gari lake kushambuliwa kwa Risasi na watu wasiojulikana.

Taarifa mbalimbali zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zinaeleza tukio hilo  limetokea eneo la Ndaleta, wilayani Kiteto wakati Ole Sendeka akiwa na dereva wake akielekea jimboni kwake Simanjiro.

Jeshi la Polisi Mkoani Manyara kupitia Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Lucas Mwakatundu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo amesema limetokea majira ya jioni leo Ijumaa Machi 29, 2024 na washambuliaji wakitokomea.

Endelea kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa zaidi.

Share:

Friday 29 March 2024

WATANZAMIA TUMIENI FURSA KUPELEKA BIDHAA UINGEREZA


-Dkt. Kijaji: Watanzania tumieni fursa kupeleka bidhaa Uingereza.

Serikali imewashauri watanzania kutumia fursa ya mpango wa biashara wa Nchi zinazoendelea kwa kuhakikisha wanapeleka bidhaa katika nchi ya Uingereza ili kukuza Uchumi pamoja na pato la Taifa.

Mpango huo mpya umeanza kutumika mwaka jana 2023 ambapo Serikali ya Uingereza iko tayari kupokea bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini zikiwemo zenye kulipiwa ushuru na zisizolipiwa.

Waziri wa Viwanda na Biashara,Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema hayo leo Dar es Salaam katika semina ya wafanyabiashara kuhusu fursa ya kuuza bidhaa katika soko la Uingereza na Nchi zinazoendelea (UK- DCTS).

Akizungumza Mhe.Dkt. Kijaji amesema mpango huo wa bishara na Nchi zinazoendelea kwa Tanzania umekuja muda muafaka kwa kuwa Nchi imerekebisha na kuboresha mazingira ya biashara ili kufanya kukuza kipato na biashara nchini.

Amesema kwa mwaka 2022 mauzo ya Tanzania kwenda Uingereza yalifikia sh. bil 44 ikilinganishwa na manunuzi ya sh. trilioni 3.08 ya bidhaa kutoka Uingereza.

Amesema kupitia takwimu hizo ongezeko la mauzo kwenda Uingereza ni ndogo sana ikilinganishwa na ununuzi wa bidhaa kutoka Uingereza Kwenda Tanzania kwani kwa miaka miwili imeongezeka sh. bilioni mbili wakati bidhaa zilizonunuliwa ni zenye thamani ya sh. triloni 1.06.

“Inahitaji nguvu ili kuweza kuvuka na kufikia malengo halisi ya kuanzishwa kwa mpango huo,” amesema Waziri Kijaji.

Aidha, ametolea mfano taarifa ya Kituo cha Uwekezaji nchini ( TIC) kuanzia mwaka 1997-2024 jumla ya miradi 980 ya kampuni ya Uingereza yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 5655.38 zilizotoa ajira za wastani wa watu 126,322 katika sekta mbalimbali ziliwekezwa nchini.

“ Tuweze kutumia mpango huo na kuchochea mapato pamoja na fedha za kigeni, lakini pia kupitia mpango huo Taifa litakuwa na manufaa mbalimbali ambayo ni kupungua kwa masharti ya kupeleka bidhaa na kwa wenye viwanda ni muhimu kuwa na malighafi zitakazochochea ushindani wa bidhaa za Tanzania,” amesema.

Ameongeza pia manufaa ya mpango huo ni kupungua kwa gharama za kufanya biashara kurahisisha upatikanaji wa taarifa za masoko kwa Tanzania na hata kushirikiana na kampuni za Uingereza kuwekeza na kuzalisha bidhaa bora Tanzania.

Amehamasisha wafanyabiashara kuona umuhimu wa uadilifu katika kuziona fursa na kwamba wapeleke bidhaa zinazokidhi soko hilo.

“Serikali yetu ya awamu ya sita imechukua hatua nyingi za kujenga mahusiano ya kidipolomasia na Uingereza ambapo Nchi hiyo pia ilianza kutoa fedha kupitia huduma mbalimbali ambazo zimeelekezwa katika Miradi mbalimbali,” amesema.

Mhe. Dkt.Kijaji ameongeza kuwa mpango huo umezingatia pia sekta ya biashara kwa kuongeza mchango wa sekta ya biashara katika ukuaji wa viwanda.

Akitoa ujumbe kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania David Cancar amesema chini ya mpango huo Tanzania ndio yenye bidhaa zinazotakiwa na Uingereza.

Amesema kupitia mpango huo kwa Pamoja kutakuwa na ongezeko kubwa la biashara kati ya Tanzania na Uingereza.
Share:

NTOBI ANG'ARA... ATOBOA TENA UENYEKITI CHADEMA SHINYANGA

 

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Shinyanga , Emmanuel Ntobi, ameshinda kuwa Mwenyekiti wa Chama hicho mkoani humo, katika uchaguzi wa Machi 28, 2024. 

Katika uchaguzi huo Ntobi alikuwa akichuana na Peter Machaga ambaye alipata kura 26, Ntobi 26 na Thadei Mwati Kura 8. Na ikalazimu kurudiwa kwa duru ya pili ambapo Ntobi alichuana na Machaga na kuibuka na kura 33 sawa na asilimia 55, na Machaga kuibuka na kura 27.

Hivyo Msimamizi mkuu wa uchaguzi Suzani Kiwanga (ambaye ni mjumbe wa kamati kuu CHADEMA) alimtangaza Ntobi kuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga.


Ntobi anakuwa ni Mwenyekiti wa Chama hicho kwa kipindi cha pili 2024 hadi 2029.

Share:

MAADHIMISHO SIKU YA VIWANGO AFRIKA; TBS YATOA ZAWADI KWA WASHINDI WA MASHINDANO YA INSHA.


Shirika la Viwango Tanzania ( TBS ) , Leo Machi 28, 2024 limeadhimisha siku ya viwango Afrika na kutoa vyeti na zawadi kwa Washindi 10 Bora wa Mashindano ya Insha ambapo Washindi wa nafasi tatu za Mwanzo ( waliopewa Zawadi za Fedha Taslimu) watashiriki Mashindano ya Insha Afrika.

Akizungumza katika Hafla iyo iliyofanyika makao makuu ya TBS Jijini Dar Es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Hassan Bomboko ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mhe. Albert Chalamila , amelipongeza Shirika la Viwango Tanzania kwa kazi na Jitihada kubwa za kuhakikisha Watanzania wanafikiwa na Bidhaa zilizo Bora hasa katika kipindi hiki cha Miaka Mitatu ya Serikali ya awamu ya SITA inayooongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

" Niwapongeze TBS kwa kuadhimisha siku hii muhimu kwa namna ya Kitofauti lakini pia niwapongeze washiriki wote zaidi ya 300 waliojitokeza kushiriki mashindano ya Insha hadi sasa tumewapata 10 bora , nyinyi kama wataalamu wetu wa badae wa masuala ya Viwango mmefanya jambo kubwa sana , Juzi wakati tukiadhimisha miaka mitatu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan TBS ni moja kati ya Mashirika yaliyofanya vizuri niwapongezeni sana " alisema Mhe. Bomboko

Akitoa Historia ya Siku ya Viwango Afrika , Mkurugenzi Mkuu TBS , Dkt. Athuman Ngenya amesema
" Shirika la Viwango Afrika lilianzishwa mwaka 1977 likiwa na jukumu kuu la Kuoanisha viwango Afrika ili kukuza biashara na kupunguza vikwazo vya Kibiashara barani Afrika pamoja na kuimarisha ukuaji wa Viwanda Afrika .
Share:

Thursday 28 March 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACHI 29, 2024



Magazeti




 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger