Tuesday 19 March 2024

KAMATI YA PIC YARIDHISHWA NA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA TANGA UWASA

...







Na Oscar Assenga,TANGA

KAMATI ya Bunge Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC) imeridhishwa na miradi inayotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) huku wakizitaka mamlaka nyengine nchini kwenda kujifunza ubunifu ambao wanautumia katika kutekeleza miradi yao na hivyo kuwawezesha kuondoa changamoto hiyo kwa wananchi.

Hayo yalisemwa  na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Deus Sangu wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua miradi inayotekelezwa na Tanga Uwasa ambapo wameridhishwa na miradi hiyo huku akiipongeza Serikali kwa namna inavyopeleka msukumo kwenye uwekezaji hasa kwenye sekta ya ya maji .

Alisema kamati hiyo imejionea shuguli uwekezaji na kuona ubunifu kamati imekagua mradi huo imerdhishwa na ubunifu huo huku kuwataka mamlaka nyengine ziweze kuiga mfano wa kuona namna ya kutatua changamoto ya maji katika maeneo yao.

“Mradi huu umetekelezwa kwa mkopo kutoka benki ya maendeleo asilimia 75 na sehemu inayobakia kama bilioni 3 ni makusanyo ya ndani hivyo mradi huu zaidi ya Bilioni 10 na umeleta mapinduzi makubwa sana kwa maana mahitaji ya maji jiji la Tanga lita milioni 45,000,000 “alisema

Aidha alisema wao kama kamati wameridhishwa na namna ambavyo Tanga Uwasa walivyoweza kubuni vyanzo vya kufadhili miradi yao na wameona mamlaka za maji wanategemea vyanzo kutoka serikali kuu lakini wao wenyewe wamebuni na kwenda kukopa fedha benki na mapato yao ya ndani wakaleta mapinduzi na kutatua changamoto ya maji karibunia takribinia asilimia 96.

Alisema pia kwanza kuja na hati fungani wamekuja na ubunifu wa kipekee kwa taaswanza Tanzania kuja na hati fungani ya kijani yenye thamani ya bilioni 53 itakayosaidia kuongeza kiwango cha maji kwa kiasi kikubwa huo mradi kwa kikasi kikubwa ilikuwa iongeze hiy ni heshima ya kipekee kwa Tanga Uwasa kuanzisha kwa jambo hilo.

“Sisi kama tunawapongeza na kuzitaka mamlaka za maji kuona namna kujifunza Tanga uwasa kwa jinsi wanavyofanya a Tanga Uwasa walivyotumia mapato yake ya ndani kuweza kwa kutekeleza miradi yake na kuwa na tija kubwa”Alisema

Awali akkizungumza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo aliishukuru hiyo kwa kuwapa ushauri na maelekezo na ushauri wao ndio wameweza kufika hapo hiyo ni sehemu ya awamu ya awali ya mradi ambao baada ya kuchukua mkopo wa awali wa shilling zaidi ya bilioni 7.

Alisema hivyo walikuwa wanajenga uhalali na uzoefu wa kuchukua mkopo mkubwa zaidi na wanataraji kuanzia mwezi wa nne mwaka huu wataanza kutekeleza miradi mingine zaidi ili kufikia lita milioni 60 na kufikia wananchi wote wa Tanga,Pangani,Muheza,Pangani na Mkinga.

“Hivyo niwashukuru bodi kuhakikisha tunakuja na mipango mizuri ya kuhakikisha hkila siku hawalali na kuhakikisha wanakuja na mipango mipaya kuhakikisha wananchi waondokana na gharama za kugharamia huduma mbalimbali”alisema
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger