Monday 4 March 2024

ELIMU YA HUDUMA YA KWANZA YAWAKOSHA MADEREVA BODABODA JIJINI TANGA, AMEND WATOA NENO

...



Na Mwandishi Wetu,Tanga

UBALOZI wa Uswisi kupitia ufadhili walioufanya kwa taasisi isiyo ya kierikali ya AMEND kwa ajili ya kutoa elimu ya usalama barabarani ikiwemo elimu ya huduma ya kwanza kwa madereva bodaboda, umewasaidia madereva hao kuwa na uwezo wa kutoa msaada pindi ajali zinapotokea.

Wakizungumza na wandishi wa habari Jijini Tanga baada ya kupewa elimu ya usalama barabarani na taasisi ya AMEND madereva wa kituo cha Mikanjuni hospitali Ally Zuberi na Faky Hamis wamesema ukosefu wa elimu umekuwa chanzo kikubwa cha ajali za barabarani kwa madereva wengi wa bodaboda.

Hivyo wameeleza kwamba elimu waliyoipata kuhusu usalama barabarani itawasaidia kuendesha kwa tahadhari pindi wanapokuwa barabarani na hivyo kuepusha ajali ambazo zimekuwa zikisababisha video na ulemavu wa kudumu.

Akieleza zaidi Mwenyekiti wa Bodaboda Kituo cha Mikanjuni Hospitali Mwin'dadi amesema kutozitambua sheria na alama za barabarani imekua ndio sababu ya ajali ya nyingi kutokea huku akibainisha elimu waliyoipata itawasaidia kujiepusha dhidi ya ajali.

Wakizungumzia kuhusu elimu ya huduma kwanza madereva hao wamesema watakuwa mstari wa mbele kutoa msaada pale ajali itakapotokea ambapo wameendelea kusema kuwa elimu hiyo watawashirikisha na madereva wenzao ili kushiriki katika utoaji wa huduma.

Kwa upande wake Benilda Mtumbuka ambaye ni Ofisa Maendeleo ya Jamii kata ya Magaoni ametoa shukrani kwa Ubalozi wa Uswisi na taasisi ya AMEND kutokana na elimu ya usalama barabarani kwa madereva bodaboda.

Ametoa mwito kwa bodaboda waliopata elimu kuitumia vyema jambo litakalosaidia kupunguza ajali huku akiwata AMEND kuendelea kutoa elimu hiyo kwa madereva wengine.

Wakati huo huo Ofisa Miradi wa AMEND Ramadhani Nyanza amesema elimu ya huduma ya kwanza waliyoitoa kwa madereva bodaboda imeleta mwanga kwa madereva hao kwa kujua namna bora ya kutoa msaada pale kunapotokea ajali.

Nyanza amesema mpaka sasa madereva bodaboda takribani 126 katika Jiji la Tanga wamefikiwa kwa kupatiwa elimu ambapo amebainisha malengo ni kuwafikia madereva 500 kwa mkoa Tanga.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger