Friday 22 March 2024

JESHI LA POLISI TANGA LAWAFIKISHA MAHAKAMANI WATUHUMIWA 35 KWA MAKOSA MBALIMBALI

...



Na Oscar Assenga, TANGA

JESHI la Polisi Mkoani Tanga katika kuhakikisha wanaendelea kudhibiti uhalifu wamefanikiwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa (35) ambapo wamehukumiwa vifungo mbalimbali.

Akizungumza leo na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Almachius Mchunguzi alisema watuhumiwa hao waliofikishwa mahakamani na kuhukumiwa vifungo mbalimbali ni.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni wa makosa ya kubaka, ulawiti, wizi na ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani ambapo watuhumiwa 20 walipatikana na hatia na kuhukumiwa vifungo gerezani.

Kamanda Mchunguzi aliwataka waliohukumiwa vifungo vya maisha Jela ni Deogratius Alex (22), Samwel Ghamuga (25) wote kwa kosa la kubaka na Athumani Rajabu (19) akihukumiwa kifungo cha maisha kwa kosa la kulawiti huku Anthony Agunstino na Twaha Rajabu wakihukumiwa miaka (30) jela kwa kosa la kubaka.

Aidha aliwataja watuhumiwa wengine ambao ni Omari Mganga na Hussein Amiry (41) wamehukumiwa kifungo cha miaka nane jela kwa kosa la wizi pamoja ana Salim Jumbe ambaye amehukumiwa miaka 27 jela kwa kosa la kubaka.

Akizungumzia kwa upande wa makosa ya usalama barabarani madereva wawili wameondolewa madaraja kwenye leseni zao za udereva na 1 amefungiwa leseni ya udereva ambapo wengine wamelipa faini mahakamani kwa makosa ya ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani.

Hata hivyo Kamanda Mchunguzi alisema ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuanzia mwezi February 21 hadi Machi 21 Jeshi hilo katika Operesheni ya kuimarisha doria na misako wamefanikiwa kukamata watuhumiwa 94 wakiwa na makosa mbalimbali ikiwemo makosa ya uvunjaji,mauaji,kujeruhi,kusafirisha wahamiaji haramu,kuharibu mali pamoja na kupatikana na silaha sita aina aya Gobole.

Mwisho.

 

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger