Wednesday 30 November 2022

NDOTO ZANGU NA MPENZI WANGU ZIMETIMIA, NI KUPATA KAZI NA FAMILIA

Share:

WANAWAKE WANAOSUMBUKA KUPATA MTOTO, TUMIA NJIA HII

Share:

IDADI YA WAGONJWA YAONGEZEKA MLOGANZILA


Idadi ya wagonjwa wanaofika kupata huduma ya matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila imeongezeka kutoka 10854 kufikia 11188 kwa wagonjwa wa nje wakati wagonjwa wanaolazwa 793 hadi 1052 katika kipindi cha miezi miwili kuanzia Septemba hadi Novemba mwaka huu.

Ongezeko hilo limechangiwa na uboreshwaji wa huduma ikiwemo kuhamia kwa Kliniki ya Magonjwa ya Moyo (Cardiology) na Kliniki ya Mishipa ya Fahamu (Neurology) kutoka Muhimbili Upanga ambapo kwa sasa wataalamu wanapatikana muda wote Mloganzila.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya utoaji huduma katika Hospitali ya Mloganzila .

Prof. Janabi amesema pamoja kuhamia kwa kliniki hizo kutoka Muhimbili Upanga lakini Kliniki za Magonjwa ya Ngozi, Upasuaji, Usingizi na ganzi, Masikio, Pua na Koo zinaendelea kama kawaida na wataalamu wapo muda wote.

"Pamoja na kliniki hizo, pia kuanzia tarehe 1 Desemba Kliniki ya Magonjwa ya Sukari na Homoni itahamia hapa Mloganzila, wataalamu waliokuwa wanapatikana Upanga wote watapatikana Mloganzila" amesema Prof. Janabi

Ameeleza kwamba ongezeko hilo limekuja na changamoto ya usafiri, Magari yanayokuja Mloganzila kutoka sehemu mbalimbali yameanza kulemewa hivyo ametoa wito kwa wakala wa usafiri wa mabasi yaendayo kasi DART kuongeza idadi ya magari yanayofika Mloganzila ili kurahisisha huduma za usafiri.

Naye Bi. Marietha John ambaye ni ndugu wa mgonjwa anayehudhuria Kliniki ya Mishipa ya Fahamu ameshukuru uongozi wa MNH kwa kuhakikisha wataalamu wanapatikana muda wote na wagonjwa wanapata huduma kwa wakati.

"Mama yangu ana tatizo la kiharusi, anahudhuria hapa kliniki , kwa kweli nashukuru tunapata huduma nzuri na Mama anapata eneo kubwa na lenye utulivu la kufanyia mazoezi" ameeleza Bi. Marietha
Share:

RAIS DKT. SAMIA ATUNUKIWA SHAHADA YA UDAKTARI WA FALSAFA WA HESHIMA IKIWA NI SHAHADA YA UDAKTARI WA JUU KATIKA HUMANITIA NA SAYANSI JAMII .

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitunukiwa Shahada ya Udaktari wa Falsafa wa Heshima ikiwa ni Shahada ya Udaktari wa Juu katika Humanitia na Sayansi Jamii na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikabidhiwa Cheti mara baada ya kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Falsafa wa Heshima ikiwa ni Shahada ya Udaktari wa Juu katika Humanitia na Sayansi Jamii na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati wa Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022. Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.Adolf Mkenda akizungumza katika Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022.Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Balozi Mwanaidi Sinare Maajar akizungumza katika Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022.Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof.William Anangisye akizungumza katika Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022.Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiwa katika Mahafali ya Hamsini na mbili (52) ya Duru ya Tano ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City tarehe 30, Novemba, 2022.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*******************

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amevitaka Vyuo Vikuu nchini kutimiza wajibu wake wa kutoa mchango katika kuleta maendeleo ya Taifa.

Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa wito mara baada ya kutunukiwa Shahada ya Juu ya Heshima ya Udaktari (Doctor of Letters Honoris Causa) ya Chuo Kikuu cha Dar es katika Mahafali ya 52 ya Chuo hicho yaliyofanyika Novemba 30, 2022 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais ameongeza kuwa jukumu la Taasisi za elimu ya juu katika kuleta maendeleo ni kutoa elimu stahiki, kufanya tafiti na kutoa maoni katika mwenendo wa kulikuza na kuimarisha Taifa.

"Tangu kuingia madarakani Serikali ya Awamu ya Sita imekuwa ikisisitiza kuwa elimu inayotolewa inapaswa kukidhi mahitaji ya jamii katika karne ya 21,"amesema Rais Samia

Ameongeza kuwa mbali ya kuongeza maarifa elimu inayotolewa katika Taasisi za elimu inapaswa kuwawezesha wahitimu kuwa na stadi zitakazowawezesha kujiajiri, kuajiriwa ama kuwa wajasiliamali na kuwa tayari kuchangia maendeleo ya Taifa wanapohitimu masomo.

Akizungumza katika Mahafali hayo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda amesema kuwa tayari Wizara imekamilisha Mapitio ya Sera na Mitaala na kwa sasa hatua inayofuata ni kuyawasilisha kwenye vikao vya ndani vya Serikali kabla ya mjadala wa wazi wa kitaifa kuhusu maoni na mapendekezo hayo.

Kuhusu uboreshaji wa elimu ya juu Prof. Mkenda amesema katika kujenga mazingira mazuri ya utoaji wa elimu ya juu, Serikali kupitia mradi wa HEET itatumia Dola za Kimarekani 425 sawa na fedha za kitanzania Bilioni 972 kupanua na kuboresha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia katika fani za kipaumbele cha Taifa.

Ameongeza kuwa Mradi unatekelezwa katika Vyuo Vikuu 14 vya Serikali,Taasisi 3 za Wizara zinazoshughulikia Elimu ya Juu na Taasisi 5 za Elimu ya Juu zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Aidha, Prof. Mkenda amesema utekelezaji wa Mradi huo utaongeza udahili katika Fani za kipaumbele cha Taifa kutoka 40,000 mwaka 2020 hadi kufikia 100,600 mwaka 2026.

Kuhusu ufadhili wa masomo ya Elimu ya Juu, Waziri huyo amesema Serikali imekuwa ikiongeza bajeti ya Mikopo ya Elimu ya Juu mfululizo kila mwaka ambapo bajeti ya Mwaka wa fedha 2017/18 ilikuwa shilingi bilioni 427 lakini kwa Mwaka wa fedha 2022/23 bajeti hiyo imefikia Shilingi bilioni 654.

Ameongeza kuwa na kama hiyo haitoshi, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameanzisha ufadhili ujulikanao Samia Scholarship kwa lengo la kuhamasisha wanafunzi kusoma masomo ya sayansi na kwamba jumla ya shilingi Bilioni tatu zimetengwa kwa mwaka wa 2022/2023 kwa ajili ya wanafunzi 640.
Share:

WANAFUNZI WAFARIKI DUNIA AJALI YA MOTO KAHAMA


AJALI YA MOTO TENA SHINYANGA YAUA WATU WATATU – WANAFUNZI WAWILI KAMANDA MAGOMI AELEZA



Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Watoto watatu wa familia moja ya Bwana Mathayo Samson katika mtaa wa Igomelo kata ya Malunga Manispaa ya Kahama wamefariki Dunia kufuatia ajali ya moto.

Tukio hilo limetokea leo Novemba 30, 2022 majira ya saa kumi na moja alfajiri ambapo moto uliunguza Nyumba ya Mathayo Samson na kusababisha vifo vya watu watatu wakiwemo wanafunzi wawili.

Akizungumzia ajali hiyo Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi wa Polisi Janeth Magomi ambaye ameeleza juu ya tukio hilo huku akithibitisha vifo vya watu watatu waliofariki katika ajali hiyo ya moto.

“Leo tarehe 30 mwezi wa 11 ilikuwa majira ya saa kumi na moja asubuhi katika mtaa wa Igomelo kata ya Malunga Manispaa ya Kahama Mkoa wa Shinyanga Nyumba ya ndugu Mathayo Samson anaumri wa miaka 39 na mfanyabiashara Nyumba yake iliwaka moto na madhara yaliyosababisha ni vifo vya watu watatu”.amesema Kamanda Magomi

Waliofariki katika ajali hiyo ni Dotto Juma mwenye umri wa Miaka 33 mkulima, Samson Mathayo mwenye umri wa Miaka 13 mwanafunzi wa darasa la sita shule ya msingi ST. Antony of Padua pamoja na Joseph Samson mwenye umri wa miaka 7 mwanafunzi wa darasa la pili shule ya msingi ST. Antony of Padua.

Kamanda Magomi amesema jeshi hilo kwa kushirikiana na jeshi la zimamoto na uokozi limefanikiwa kufika katika eneo la tukio na kwamba jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha moto huo.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 30,2022










Share:

Tuesday 29 November 2022

HATIMAYE WASHINDI WA SHINDANO LA KAMPENI YA TISHA NA TEMBOACARD WATINGA QATAR KUSHUHUDIA KOMBE LA DUNIA


Benki ya CRDB baada ya kuhitimisha awamu ya kwanza ya kampeni yake ya “Tisha na TemboCard” na kuwakabidhi tiketi za kushuhudia mashindano ya Kombe la Dunia wateja wake watatu walioibuka washindi wa jumla wa kampeni hiyo hatimae yawapeleka Qatar.

Wateja hao waliondoka tarehe 25 kupitia uwanja wa Julius Nyerere International Airport na kusindikizwa na baadhi ya wafanyakazi wa Benki hiyo.
Akizungumza kwaniamba ya washindi wenzake katika safari hiyo, Rajabu Dossa Mfinanga aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuwapa kipaumbele wateja wake kwani wanajihisi ni sehemu ya familia ya Benki hiyo, pia alitoa rai kwa watanzania kujijengea utamaduni wa kutumia kadi zao za benki hiyo kwa kuafanya manunuzi na malipo mbalimbali kama bili, usafiri na kadhalika si kwasababu ya kushinda zawadi;

“Niwape wito wateja wenzangu wa Benki ya CRDB na watanzania kwa ujumla tujenge utamaduni wa kutumia kadi kupata huduma mbalimbali badala ya kutumia fedha taslimu. Matumizi ya kadi ni rahisi na inakupa kujiamini zaidi kuliko ukibeba fedha taslimu, unakosa kujiamini kila uendapo unakuwa na wasiwasi kwa kuhofia kuibiwa, lakini ukiwa na Tembocard yako mambo ni burdani”. Aliongeza Mfinanga.

Kwakufahamu namna ambavyo Watanzania wanapenda michezo na hasa msimu huu wa Kombe la Dunia imeona ni vyema ikawa sehemu ya kutimiza shauku ya wateja wao ya kushiriki katika mashindano hayo makubwa duniani.

Katika safari hiyo Benki ya CRDB imewagharamia tiketi za ndege kuelekea Doha Qatar, malazi, pamoja na fedha za matumizi wakiwa huko.
Washindi walioibuka kidedea kwenye safari hiyo ya kushuhudia kombe la dunia ni pamoja na; Haji Athumani Msangi, Erick Boniface Kashangaki, Kelvin Jackson Twissa, na Rajabu Dossa Mfinanga wote wakazi wa Dar es Salaam.

Benki ya CRDB inatarajia kuendesha awamu ya pili ya kampeni hii na kuahidi kuleta mambo mazuri zaidi, hivyo imetoa rai kwa wateja wake kuendelea kutumia kadi zao za TemboCard kulipia manunuzi ili kupata punguzo la bei (discount) au kurudishiwa sehemu ya kiasi walichotumia (cashback) katika maduka mbalimbali.


--
Share:

WATOTO 521,025 KUPATIWA CHANJO YA POLIO SHINYANGA DESEMBA 1 - 4, 2022


Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Faustine Mulutyu akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Novemba 29,2022. 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Watoto walio chini ya umri wa miaka mitano wapatao 521,025 wanatarajia kupatiwa matone ya kuzuia ugonjwa wa Polio Mkoa wa Shinyanga kaya kwa kaya kuanzia Desemba 1 hadi 4,2022.


Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Novemba 29,2022 kuhusu maandalizi ya Kampeni ya utoaji wa matone ya chanjo ya Polio awamu ya nne, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Faustine Mulutyu amesema Mkoa wa Shinyanga umepokea jumla ya chanjo dozi 614,800 pamoja na vifaa vingine (marker pen, chaki, vipeperushhi, rejista) kwa ajili ya kufanikisha Kampeni hiyo.


"Mkoa wa Shinyanga ulitekeleza Kampeni ya Polio awamu ya tatu kwa mafanikio makubwa na kufikia kiwango cha utoaji kukiwa na ushiriki mkubwa wa wadau ambapo walengwa walikuwa 445,681 kuanzia Septemba 1 hadi 4,2022",amesema Mulyutu.


Mratibu wa Chanjo mkoani Shinyanga Timothy Sosoma, amesema Mkoa wa Shinyanga umeshapokea jumla ya dozi ya chanjo ya Polio 614,800 na walengwa wote watafikiwa na timu ya wataalam 1,021 lengo ni kufikia idadi ya watoto 521,025 ili kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa Polio.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Faustine Mulutyu akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Novemba 29,2022 kuhusu maandalizi ya Kampeni ya utoaji wa matone ya chanjo ya Polio awamu ya nne ikayofanyika kaya kwa kaya kuanzia Desemba 1 hadi 4,2022.
Mratibu wa Chanjo mkoani Shinyanga Timothy Sosoma akizungumza na waandishi wa habari juu ya kampeni ya utoaji Chanjo ya Polio awamu ya Nne kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.
Waandishi wa habari wakichukua taarifa juu ya kampeni ya utoaji Chanjo ya Polio kwa njia ya matone dhidi ya watoto waliochini ya umri wa miaka mitano.
Waandishi wa habari wakichukua taarifa juu ya kampeni ya utoaji Chanjo ya Polio kwa njia ya matone dhidi ya watoto waliochini ya umri wa miaka mitano.
Share:

MSANII HI SPEED KUTOKA NIGERIA AACHIA ZAWADI YA ALBUM KWA MASHABIKI


Precious Gift ni album mpya na ya kwanza kutoka kwa msanii wa muziki wa Afro Beat na Hiphop kutoka nchini Nigeria ambaye anafahamika zaidi kwa jina la Hi Speed.

Album ya Hi Speed ina nyimbo 13 ndani yake akiwa ameshirikiana na Mr Raw, Terry Akpala, Seriki, Halima Alao, Jumabee, Shatta Michy , Dj Baddoo, Jesse Jagz, Jay Teaser, Mf Honcho, Di’ja, Eche Ozoku, Dreez, Jahjah, Sharon Sonia, Yonique, Young J, Don Flash, Hajj, Itabreez na Zurezoo.
Lakini pia katika album hii iitwayo Precious Gift imeandaliwa na kuyarishwa na watayarishaji  mbalimbali kutoka nchini Nigeria ambao wamefanikiwa kufanya vizuri kazi mbali mbali akiwemo Mix Monster  pamoja na Don Adah.

Album hii inapatikana katika mitandao yote ya kusikiliza na kupakua muziki unaweza pia kumfuatilia kupitia ukurasa wake wa Instagram @hispeedmusic

Share:

BARAZA HURU LA USULUHISHI WA MALALAMIKO YA WANANCHI VIJIJI VINAVYOZUNGUKA MGODI WA MWADUI LAZINDULIWA


Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akikata utepe wakati akizindua Taratibu za Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy kulia ni Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC).

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui (Williamson Diamonds Limited) kwa njia ya maridhiano kuhusu madhira ,mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu limezinduliwa rasmi mkoani Shinyanga

Uzinduzi wa Baraza la Malalamiko ya Wananchi pamoja na Utaratibu wake katika Mgodi wa Mwadui umezinduliwa leo Jumanne Novemba 29,2022 na Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkude amesema matarajio kupitia baraza hilo ni kuona kutenda haki kwa wananchi waliopata madhara kupitia mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.


“Tunahitaji haki itendeke lakini pia kwa kuzingatia mambo yote tuliyoelezekana ngazi mbalimbali, tuoneshe uhalisia wa haki hizo zinazotolewa na kuwe na tija kwa walengwa wenyewe”,amesema Mkude.


Amesema mara baada ya uzinduzi huo Baraza hilo litaanza kusikiliza malalamiko yaliyowasilishwa na wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa Mwadui.


“Utaratibu wa kuunda Baraza Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi ulivyoandaliwa vizuri ukisimamiwa na kufadhiliwa na Petra Diamonds Ltd. Utaratibu wote uliotumika mpaka kufikia leo umekuwa wa wazi na tumekuwa tukieleweshwa ngazi moja hadi nyingine kwa kushirikisha taasisi mbalimbali kuhusu baraza hili la malalamiko na namna likatavyokwenda kufanya kazi”, ameongeza Mkude.

“Lakini nitumie nafasi hii kupongeza imeonekana kwamba Baraza hili likianza kazi kwa ujumla malalamiko yaliyosajiliwa na wananchi yapo 5575 na wameongeza muda wa kuyasikiliza badala ya miaka mitatu imeenda zaidi, hili ni jambo jema, jambo la kiutu ambalo litasaidia kuangalia kwa undani zaidi haki za watu ambazo wamewasilisha malalamiko yao”,ameeleza.


Mkuu huyo wa wilaya amesema serikali itaendelea kushirikiana Baraza hilo wakati wote na pale ambapo panatokea tatizo au viashiria vya shida au tatizo basi jopo zima lisisite kuwasiliana na uongozi ngazi ya mkoa na wilaya ili kutatua mapema matatizo yanayoweza kujitokeza kabla ya kuleta athari kubwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy amesema wana imani Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi litafanya kazi kwa weledi mkubwa ili haki iweze kupatikana.

“Petra Diamonds Ltd tukiwa ni wamiliki wa Mgodi wa Mwadui tunatambua changamoto zilizokuwepo, tulifanya mabadiliko mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kukidhi matakwa ya sheria za nchi na kimataifa”,amesema Duffy.

Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya Wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala amesema tangu mwaka 2009 hadi 2021 jumla ya malalamiko 5575 yamesajiliwa na usikilizwaji wa hatua ya awali unaanza mara moja kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa.

“Kila mwananchi aliyesajili malalamiko yake na atayesajili malalamiko yake atafikiwa na Baraza hili kuhusu la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi”,amesema Dkt. Nshala.


Naye Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo kuzinduliwa kwa Baraza Huru la Usuluhusihi wa malalamiko ya wananchi yanayotokana nan a shughuli za uzalishaji wa madini katika mgodi wa Mwadui unafungua Ukurasa mpya wa ushirikiano baina ya wananchi na mgodi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu kuruhusu kuundwa kwa Baraza hilo huku akilitaka Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya Wananchi kwenda kufanya kazi kwa weledi na kutenda haki.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akizungumza wakati akizindua Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu
kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema leo Jumanne Novemba 29,2022 Mjini Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akizungumza wakati akizindua Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui.

Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui,Dkt. Rugemeleza Nshala akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui.
Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui ambapo amesema jopo la usuluhishi litaenda kufanya kazi kwa weledi ili jamii ipate suluhisho la malalamiko yao kwa ajili ya kuleta maendeleo katika taifa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui
Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui

Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude (kulia) akikata utepe kuzindua Baraza huru la kushughulikia malalamiko ya wananchi ambao wanazunguka Mgodi wa Almasi Mwadui, (kushoto) ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Petra Diamond Limited Richard Duffy
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude  akikata utepe wakati akizindua Taratibu za Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akionesha Vitendea kazi vya Baraza Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akimkabidhi Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto).
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto) akimkabidhi Katibu Tawala wilaya ya Kishapu, Shadrack Kengese Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akimkabidhi Mbunge wa Jimbo la Kishapu, Boniphace Butondo, Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya  Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto) wakikabidhi vitendea kazi kwa Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala na Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC).

Zoezi la makabidhiano ya Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui likiendelea
Zoezi la makabidhiano ya Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui likiendelea
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu

Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited wakipiga picha na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited wakipiga picha na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger