Thursday 31 August 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 1, 2023

















Share:

SERIKALI KUANDAA MWONGOZO WA UWIANO WA KIJINSIA ILI KUONDOA UKATILI


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju, akizungumza wakati wa Semina Elekezi ya Usambazaji wa Mwongozo wa Mafunzo ya uwiano wa Kijinsia na Ujumuishaji Jamii katika huduma za ustawi wa Jami kwa Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wizara za Kisekta, Taasisi za Umma na wadau yaliyofanyika leo Agosti 31,2023jijini Dodoma.
Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Nandera Mhando,akizungumza wakati wa Semina Elekezi ya Usambazaji wa Mwongozo wa Mafunzo ya uwiano wa Kijinsia na Ujumuishaji Jamii katika huduma za ustawi wa Jami kwa Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wizara za Kisekta, Taasisi za Umma na wadau yaliyofanyika leo Agosti 31,2023jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi huduma za Ustawi wa jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bi.Subisya Kabuje ,akizungumza wakati wa Semina Elekezi ya Usambazaji wa Mwongozo wa Mafunzo ya uwiano wa Kijinsia na Ujumuishaji Jamii katika huduma za ustawi wa Jami kwa Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wizara za Kisekta, Taasisi za Umma na wadau yaliyofanyika leo Agosti 31,2023jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju (hayupo pichani) akizungumza wakati wa Semina Elekezi ya Usambazaji wa Mwongozo wa Mafunzo ya uwiano wa Kijinsia na Ujumuishaji Jamii katika huduma za ustawi wa Jami kwa Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wizara za Kisekta, Taasisi za Umma na wadau yaliyofanyika leo Agosti 31,2023jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Semina Elekezi ya Usambazaji wa Mwongozo wa Mafunzo ya uwiano wa Kijinsia na Ujumuishaji Jamii katika huduma za ustawi wa Jami kwa Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wizara za Kisekta, Taasisi za Umma na wadau yaliyofanyika leo Agosti 31,2023jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju,akiteta jambo na Kamishna wa Ustawi wa Jamii Dkt. Nandera Mhando, mara baada ya kufungua Semina Elekezi ya Usambazaji wa Mwongozo wa Mafunzo ya uwiano wa Kijinsia na Ujumuishaji Jamii katika huduma za ustawi wa Jami kwa Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wizara za Kisekta, Taasisi za Umma na wadau yaliyofanyika leo Agosti 31,2023jijini Dodoma.

PICHA ZOTE NA ALEX SONNA



Na WMJJWM- Dodoma

Serikali imesema ili kuhakikisha kuna uwiano wa kijinsia katika upatikanaji wa huduma imeandaa mwongozo wa uwiano wa kijinsia ili makundi yote yashiriki katika maendeleo ya jamii lakini pia kuondoa ukatili.

Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju wakati akizungumza na Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wizara za Kisekta, Taasisi za Umma na wadau kwenye mafunzo ya utoaji wa huduma kwa kuzingatia uwiano wa kijinsia ili kufikia kizazi cha usawa, yaliyofanyika jijini Dodoma Agosti 31,2023.

“Mwongozo huu umelenga kutekeleza makubaliano ambayo Tanzania imeridhia katika mikataba yake ya kimataifa lakini pia katiba yetu ya Tanzania inaelekeza kutoa huduma kwa watu wote bila ubaguzi wowote“ amesema Mpanju.

Wakili Mpanju amewasisitiza Maafisa Ustawi hao kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika mafunzo hayo ili maarifa yote yanayopatikana yatumike nchi nzima ili lengo la Serikali kuwa na jamii yenye usawa litimie.

Kwa upande wake, Kamishna wa Ustawi wa Jamii Dkt. Nandera Mhando amesema mwongozo huo umeandaliwa kupitia hatua kadhaa ikiwemo vikao kadhaa na kufanyiwa majaribio kadhaa na wadau na kupitia mafunzo mbalimbali hadi kufikia hatua ya ukamilishaji.

“Malengo ya Semina hii ni kutoa uenezi wa mwongozo huu kwa maafisa ustawi ili utumike nchi nzima na ukazibe mapengo yote yaliyokuwepo kwenye uwiano wa kijinsia nchi nzima” amesema Dkt. Nandera.

Naye Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Subisya Kabuje amesema mwongozo huo utafanikiwa zaidi endapo utasambazwa kwa Maafisa Ustawi wote kutoka mikoa yote na Halmashauri zote na kusaidia kutatua changaoto zilizokuwepo.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Shirika la PACT Tanzania Flora Nyagawa amesema Shirika hilo litaendelea kushirikiana kikamilifu na Wizara kuhakikisha afua zote zinatekelezwa ili kuwa na Taifa lenye uwiano wa jinsia.
Share:

NILISHINDA FEDHA NYINGI ZA KAMARI HADI NIKAWA NATISHIWA MAISHA!



Jina langu ni Shadrack, nilikuwa mtu ambaye niliamini michezo ya kamari, mara kwa mara nilicheza michezo hii kwani niliamini kuwa siku moja ningweza kupata fedha nyingi kutokana na michezo hii.

Marafiki zangu wengi walikuwa wameshakata tamaa kutokana na kuliwa fedha zao tu kila wakati bila wao kushinda, ila kwangu haikuwa hivyo, ama kwa hakika atafutaye hachoki!.

Nilicheza  michezo ya kubashiri mechi kupitia mitandao kama Sportpesa, siku moja niliamshwa na ujumbe wa simu kutoka kwenye kampuni ya Sportpesa kwamba nilikuwa nimeshinda Ksh15 milioni.

Kampuni ile iliniweka kwenye mitandao yao huku vyombo vya habari na mitandao vikitangaza habari yangu, sikuwa na amani kwani katika mtaa wetu nilihofia kwamba watu wenye nia mbaya watakuja kunitoa uhai kwa ajili ya kuchukua fedha zangu.

Nilianza kutafuta namna ya kukabiliana na hali ile kwani nilikuwa nimeshajulikana nchi nzima, nilitaka maisha yangu yasiwe kwenye hatari, sio kila mtu ambaye alikuwa na furaha kufuatia ushindi wangu.

Nilianza kupokea simu za vitisho kwamba watu fulani walikuwa na nia ya kuja hadi nyumbani kwangu kwa ajili ya kunitoa uhai na kuchukua fedha zangu.

Kupitia tovuti www.african-doctors.com niliona jinsi African Doctors alivyokuwa amewasaidia watu wengi kupata usaidizi kutokana na mambo mengi yanayowasumbua maishani.

Sikupoteza muda ambapo nilimpigia simu African Doctors  kwa ajili ya usaidizi wake, nilifika kwenye ofisi yake kwa ajili ya huduma yake, alifanya matambiko yake ya kuwafanya maadui wasiweze hata kunidhuru.

Alinipa hakikisho kwamba hakuna yeyote ambaye ana uwezo wa kutishia maisha yangu, tangu nitoke kwake nimekuwa naisha maisha yangu kwa furaha na utulivu na sasa naendesha biashara zangu bila shida yoyote.

Wasiliana na African Doctors kwa namba; +254 769 404965, tembelea tovuti yao; www.african-doctors.com au watumie email; africandoctorheals@gmail.com

Mwisho.


Share:

Wednesday 30 August 2023

JAMII YATAKIWA KUWAPA NAFASI WANAWAKE KWENYE UONGOZI


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

JAMII imetakiwa kuachana na imani potofu zinazomkandamiza mwanamke ili chaguzi zijazo, wanawake wengi wajitokeze kwa wingi katika kugombea uongozi kwenye nafasi mbalimbali kwani uwepo wao kwenye uongozi inaleta chachu ya maendeleo kwenye jamii.

Ushauri huo umetolewa leo Agosti 30,2023 katika Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) ambapo walikuwa wanajadili nafasi ya mwanamke katika ushiriki kwenye uongozi.

Akizungumza wakati akiwasilisha mada, mwezeshaji Bi. Clara Mcharo amesema kuwa jamii imekuwa haina imani na wanawake katika uongozi kutokana na tamaduni zilizopo kwenye jamii ambazo zinaamini kuwa mwanamke hawezi kuwa kiongozi.

Amesema iwapo dini zetu zikiwashirikisha wanawake katika uongozi basi jamii pia itapata uelewa mkubwa katika kuamini wanawake wanaweza hivyo kuwapa nafasi kwenye uongozi ili kuonesha uwezo wao.


Share:

WAANDISHI WA HABARI SHINYANGA WATEMBELEA BANDARI ZA ZIWA VICTORIA NA BANDARI YA NCHI KAVU ISAKA

Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 30,2023 wametembelea Bandari zinazosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa ajili ya kujionea na kujifunza namna zinazovyofanya kazi. 

Bandari walizotembelea ni pamoja na Bandari ya Nchi Kavu ya Isaka wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga pamoja na Bandari za Ziwa Victoria (Kusini na Kaskazini)


Wakitembelea bandari hizo waandishi wa habari wamejionea namna Serikali inavyowekeza kwa kufanya maboresho makubwa kwenye Bandari hizo na kuchochea ukuaji wa uchumi hapa nchini.

Meneja Bandari za Ziwa Victoria Frednand Nyathi, amesema katika maboresho ya Bandari tatu za Mwanza Kaskazini, Kemondo na Bukoba, Serikali imetenga kiasi cha fedha Sh. bilioni 60 kwa ajili ya kuzikarabati.

Amesema maboresho hayo yataongeza ufanisi wa utendaji kazi wa Bandari pamoja na kuongeza mapato na kukuza uchumi wa nchi.

Afisa Bandari ya Isaka wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Abel Mshana amesema Bandari hiyo Kavu imekuwa ikirahisisha utendaji wa bandari na imekuwa ikihudumia nchi tano kusafirisha mizigo ikiwemo Rwanda,Burundi,Uganda, Sudani Kusini na DRC.

Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga (SPC) iliyoandaa ziara hiyo, Greyson Kakuru amesema katika ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ya uwekezaji wa Bandari ambao ni kichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi hapa nchini ikiwemo maboresho makubwa ya bandari.

Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari

Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari





Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger