Saturday 12 August 2023

Tanzia : MWENYEKITI WA ZAMANI WA SIMBA SC AYOUB CHAMSHAMA AFARIKI DUNIA

...
 

Ndugu Soud Ayubu Chamshama
wa Chang'ombe Dar es salaam 
Anasikitika kutangaza kifo cha Baba 
Yake mzazi,  Mzee Ayubu Salehe Chamshama, 
Kilichotokea tarehe 11 Agosti 2023
nchini India alikokuwa kwa matibabu.

Mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumanne tarehe 15 Agosti 2023 kijijini kwao Kilole, Lushoto, Mkoani TANGA.

Msiba upo nyumbani kwa marehemu Chang'ombe Maduka Mawili Dar es salaam.

Habari ziwafikie Ndugu, Jamaa na marafiki popote pale walipo.

Enzi za uhai wake Marehemu Chamshama alishika nyadhifa mbalimbali. Alikuwa Meneja Mkuu wa kampuni ya Tanzania Tea Blenders, vilevile alihudumu kwa muda mrefu kama Mwenyekiti wa klabu ya Simba SC na pia alikuwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Temeke.

Inna Lillahi wa inna ilayhi raji'un
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger