Tuesday 25 February 2014

BUNGE LA KATIBA; MWAKIFWAMBA, BATULI WAKWAA SKENDO

BUNGE LA KATIBA; MWAKIFWAMBA, BATULI WAKWAA SKENDO

Stori: Hamida Hassan na Gladness Mallya
WAKATI mchakato wa Bunge la Katiba ukianza leo mjini Dodoma, ishu hiyo imemtia kwenye tope Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba baada ya kukwaa skendo ya ‘kutoka’ na mwigizaji Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ walipotimba mkoani humo.
Yobnesh Yusuph ‘Batuli’.
Kwa mujibu wa staa wa filamu ambaye aliachwa katika safari hiyo ya kwenda kuhamasisha sanaa itambuliwe kwenye mchakato wa katiba mpya, Mwakifwamba alimteua Batuli ili akajiachie naye Dodoma kwa sababu hakuwa na vigezo.
“Akina Monalisa (Yvone-Cherry Ngatikwa) walistahili kwa ukongwe wao kwenye fani, sasa Batuli aliingiaje? Akili za kuambiwa changanya na zako,” alisema msanii huyo.
Akizungumzia skendo hiyo, Mwakifwamba alidai kuwa ameshasingiziwa vitu vingi hivyo anajua nyuma yake kuna kundi linalomchafua kila kukicha lakini ukweli ni kwamba hakumteua Batuli kwa lengo hilo.
“Sasa kama nimemteua kwa sababu hiyo, je, akina Monalisa nao niliwateua kwa kigezo hicho?” alihoji Mwakifwamba huku akikiri kuwa ameshaisikia sana skendo hiyo.
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba.
Kwa upande wake Batuli alifunguka: “Si kweli bwana, wameshatuzushia mambo kibao. Mara kuna fedha tumekula, mara sijui nini…sasa naona wamekuja na hili la mapenzi. Wabongo tuache majungu.
Katika safari ya Dodoma, mbali na Monalisa, wawili hao waliambatana na wasanii wengine wa tasnia mbalimbali wakiwemo Dude, John Kitime, P-Funk Majani na Abdul Salvador ambapo ndani ya bunge hilo linalotarajiwa kutikisa, wanawakilishwa na Paul Mtendah.
Share:

MBONGO ABAKWA CHINA, AFA

Stori: Mwandishi Wetu
AMA kweli dunia hadaa, ulimwengu shujaa! Kumeibuka mchezo mchafu, kuna Watanzania wanawachukua warembo nchini na kuwapeleka China kwa ahadi kwamba wanakwenda kufanya kazi saluni, wakifika kule wanawanyang’anya paspoti na kuwauza kwa wanaume (ukahaba), sasa yamemkuta Mbongo aitwaye Sabrina au Habiba, Ijumaa Wikienda lina mkasa wa kusikitisha.
Sabrina au Habiba enzi za uhai wake.
Habari za uhakika kutoka kwa chanzo chetu nchini humo zilisema kuwa, Sabrina (24), alifariki dunia Alhamisi iliyopita kufuatia kubakwa na wanaume watano, raia wa Nigeria ambao wamo nchini humo kibiashara.
Tukio hilo lilijiri kwenye hoteli moja iliyopo kwenye Mji wa Guangzhou ambao umejaa wageni wengi, wakiwemo Watanzania.
SIKU YA TUKIO
Rafiki wa karibu wa Sabrina, Saada alisema siku ya tukio, marehemu akiwa katika harakati zake za kutafuta wateja alikutana na Mnigeria mmoja ambaye walipatana kulala wote kwa usiku mzima.
“Kumbe yule Mnaigeria alikuwa na wenzake wanne. Usiku walimwingilia wote kwa nguvu kwa kumbaka mpaka akapoteza maisha palepale. Ni ukatili mkubwa.
“Wale watu walipogundua Sabrina amekufa waliuchukua mwili wake na kuutupa chini kutoka ghorofa ya tano,” alisema rafiki huyo.
MAITI YAKUTWA HAINA FIGO, MOYO
Habari zaidi zilidai kuwa mpaka juzi (Jumamosi) madaktari waliokuwa wakiuchunguza mwili wa Sabrina waligundua hauna figo na moyo, jambo linalozidi kuzua hofu juu ya muaji yake.
NI BIASHARA ILIYOIBUKA CHINA?
Ilidaiwa kuwa nchini China imeibuka biashara ya viungo mbalimbali vya binadamu ambapo ili vipatikane ni lazima mwenye viungo hivyo auawe kwa njia yoyote.
SABRINA AFA, MGANDA APOTEA
Mtoa habari wetu alisema wakati Wabongo wakiwa kwenye maombolezo ya kifo cha Mtanzania huyo, mrembo mwingine raia wa Uganda, nchi ambayo imo ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki amepotea katika mazingira ya kutatanisha nchini humo.
Baadhi ya watu wana wasiwasi kuwa kupotea kwa msichana huyo kunahusiana na kushamiri kwa biashara ya viungo vya binadamu.
SABRINA ALIKWENDAJE CHINA?
Mwezi Julai, mwaka jana, Sabrina alikwenda nchini humo akidanganywa na mwanamke mmoja kwamba atapata kazi kwenye saluni ya wanawake lakini baada ya kufika alijikuta akiingizwa kwenye biashara ya ukahaba bila ridhaa yake mpaka alipokutwa na mkasa huo uliopoteza maisha yake.
TAHADHARI KWA WAREMBO WANAOKWENDA CHINA KUFANYA KAZI SALUNI
Imebainika kuwa, kumeibuka wimbi la Wabongo wanaofanya ‘uwakala’ wa kuwachukua wasichana wa Kitanzania kwa kuwadanganya kwamba wanakwenda kufanya kazi za saluni nchini humo.
Mara baada ya kufika, wasichana hao hunyang’anywa paspoti ili washindwe kuondoka nchini humo na kushinikizwa kujiuza (ukahaba) huku waliowapeleka wakipokea fedha kutoka kwa wateja.
KUIKOMBOA PASPOTI
Habari zilisema kuwa mhusika hurejeshewa paspoti yake baada ya malipo yake kwa ‘wakala’ kufikia dola za Marekani 8,000 (kama shilingi milioni 12), ndipo huachiwa ‘huru’ kuendelea na maisha yake.
Wengi wakishaachiwa hushindwa kurejea Bongo na kujikuta wakiendelea kuuza miili katika mahoteli na klabu huku wakikutana na majanga mbalimbali.
MASOGANGE, KAJALA NA DIDA
Watanzania waishio nchini humo wamewatahadharisha mastaa wa Bongo, wakiwemo Mtangazaji wa Radio TimesFM, Khadija Shaibu ‘Dida’, msanii wa filamu Kajala Masanja na Video Queen Agnes Gerald ‘Masogange’ ambao hupenda kwenda nchini humo kwa shughuli zao, kutokubali kuwa karibu na mawakala wa kuchukua wasichana Bongo kwa kuwadanganyia kazi ya saluni kwani wanaweza kujikuta pabaya siku moja.
DIDA
Ijumaa Wikienda lilimsaka Dida siku ya Jumamosi iliyopita na kumuuliza kuhusu kuwepo kwa mawakala hao ambapo alikiri kusikia huku akisema warembo wenyewe wanapaswa kuwa macho na udanganyifu huo.
“Najua wapo Wabongo wanaofanya shughuli hiyo, si China tu hata India, unapelekwa kwa ahadi ya kazi ya saluni, ukifika hamna cha saluni wala nini? Warembo wawe makini jamani, nenda China kama una uwezo wako mwenyewe kufanya ‘shoping’ lakini si kupelekwa,” alisema Dida.
BALOZI WA TANZANIA-CHINA
Juzi, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Balozi wa Tanzania nchini China, Luteni Jenerali Mstaafu Abdulrahman Shimbo ili azungumze lolote kuhusu tukio la Sabrina, lakini simu yake ilionekana kutokuwa hewani kwa muda mrefu.
GLOBAL BADO KAZINI
Magazeti Pendwa ya Global Publishers yanaendelea kuifuatilia habari ya kifo cha Sabrina na yatakuwa yakiwapa wasomaji wake kadiri kitu kipya kinapopatikana.
Share:

USTADH ALIVYOMCHINJA MTOTO

USTADH ALIVYOMCHINJA MTOTO

Stori: Waandishi Wetu
KUFUATIA tukio la Ustadh Mohamed Said Ngulangwa (36), mkazi wa Mbagala-Charambe jijini Dar kumchinja mtoto Jamal Salum Ally (12) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tano kisha na yeye kuuawa na wananchi wenye hasira, Uwazi kama kawaida yake lilichimba tukio hilo na kubaini mengi, twende pamoja.
Mtoto Jamal Salum Ally (12) enzi za uhai wake.
MTOTO AITWA, AENDA
Akizungumza na Uwazi Jumamosi iliyopita msibani Mbagala juzi, mtoto mmoja (jina lipo) alisema yeye na marehemu walikuwa wakicheza michezo ya kawaida, mara akatokea ustadh na kumwita mtoto Jamal.
Ustadh Mohamed Said Ngulangwa (36) enzi za uhai wake.
“Sisi tulikuwa tunacheza, ghafla ustadh akamwita Jamal. We Jamal, njoo. Kwa vile aliita kwa sauti ya kawaida tulijua anataka kumtuma, Jamal akaenda mimi nikawa namsubiria ili tuendelee kucheza, kumbe mwenzangu aliitwa kuchinjwa,” alisema mtoto huyo kwa sura iliyojaa simanzi.
Waombolezaji wakiwa msibani.
KISU KIKALI CHATUMIKA
Mtoto huyo aliendelea kueleza kwa uchungu kwamba, akiwa anamshuhudia Jamal akikutana na ustadh, alishangaa kumwona mwanaume huyo akimdaka kwa haraka na kisha kutoa kisu ambapo alianza kumchomachoma nacho na hatimaye kumlaza chini na kukipitisha shingoni kama anachinja kuku.
Mwili wa ustadh baada ya kuuawa na wananchi wenye hasira kali.
“Nilipiga kelele kuwaambia watu, nikatoka kwenda kuwaita watu huku napiga kelele kwamba Jamal anachinjwa na ustadh,” alisema mtoto huyo huku akionesha sura halisi ya masikitiko ya ndani ya moyo. Inauma sana!
Mwili wa mtoto Jamal baada ya kuchinjwa na ustadh.
MAJIRANI WADHANI ADHABU INATOLEWA
Nao majirani na madrasa ya mtu huyo waliopata nafasi ya kueleza walichojua kuhusu mauaji ya mtoto huyo, walisema kelele za mtoto Jamal kuomba msaada zilisikika, lakini waliamini mtoto anapewa adhabu na mzazi wake.
MAMA WA MAREHEMU AFIKA MBIO
Maelezo zaidi yanasema kuwa, mtoto aliyekwenda kuita watu alifika nyumbani kwa wazazi wa marehemu na kumkuta mama mzazi ambaye alimpa taarifa.
Eneo alilochinjiwa mtoto Jamal.
Mwanamke huyo aliyepewa taarifa hizo, akiwa haamini masikio yake, alitoka mbio na kilio kuelekea eneo la tukio.
Wananchi nao baada ya kusikia maelezo ya mtoto aliyeshuhudia, waligutuka na kutua eneo la tukio lakini kwa bahati mbaya walikutana na kichwa kikiwa miguuni mwa kiwiliwili. Lazima umwage machozi!
Wananchi wakiwa eneo la tukio.
MBALI NA KIWILIWILI NA KICHWA
Wananchi hao waliweza kugundua kuwa, kichwa hicho ni cha mtoto Jamal huku pembeni yake kukiwa na ndoo ambayo walidai muuaji alikusudia kukingia damu (ili iweje?).
VILIO VYATAWALA, USTADH AJIFICHA
Vilio vilianza kutalawa eneo hilo, akina mama, marafiki wa marehemu waliangua vilio vya uchungu baada ya kuuona ukatili huo ambao walisema haujawahi kutokea katika eneo hilo.
Jeneza lenye mwili wa Jamal likiwa mbele ya waombolezaji.
Ilidaiwa kwamba, wakati huo ustadh alikuwa amejificha chumbani kwake ili kuepuka ‘soo’ lake lakini wananchi walishtukia janja yake na kutishia kuvunja dirisha ambapo mtuhumiwa huyo alichungulia akiwa na kisu mkononi kikiwa na mabaki ya damudamu.
WANANCHI WAVUNJA MLANGO, DIRISHA LA USTADH
Bila kujali kisu hicho, wananchi walivunja mlango na dirisha na kuanza kumshambulia kwa mawe, kisha wakamchomoa akiwa uchi wa mnyama mpaka nje huku wakiendelea kumshambulia hadi akakata roho.
Magari ya polisi yakiwa eneo la tukio.
BABA WA MAREHEMU NAYE ANALO NENO LA KUSIKITISHA
Naye baba wa Jamal, Salum Ally alipoongea na Uwazi alitoa simulizi ya majonzi, msikie: “Nilipokea kifo cha mwanangu Jamal kwa huzuni kubwa sana, sikuamini kama yeye ndiye aliyeuawa kikatili namna ile!
“Nilikuwa narudi nyumbani kutoka kazini, jirani na nyumbani nikakuta watu wengi, nikahoji kulikoni? Nikaambiwa kuna mtoto amechinjwa na aliyemchinja ameuawa. Khaa! Nikashangaa!
Baadhi ya watoto waliofika eneo la tukio kushuhudia mwenzao aliyechinjwa.
“Kwa kuwa nilikuwa nimechoka sana, niliona nifike kwangu kwanza ndipo nirudi kwenye tukio. Kabla ya kutua kwangu, nikakutana na mke wangu njiani huku akilia, nilipomhoji kuna nini, aliendelea kulia bila kunipa majibu.
“Ndipo mpangaji mwenzangu akanipasulia kwa kuniambia kwamba mwanangu Jamal amechinjwa mpaka kichwa kutenganishwa na kiwiliwili.
“Nilipatwa na mshtuko mkubwa kwani sikufikiria kama kungetokea tukio la kutisha kama hilo, hata kama mngekuwa ninyi waandishi mngefanyaje jamani?
Mwili wa Jamal ukiombewa kabla ya maziko.
“Nilijivuta hadi eneo la tukio na kukuta mwili wa mwanangu umeshafungwa kwenye nguo na kuwekwa ndani ya gari la polisi, sikuwa na nguvu ya kuangalia sura yake kwa uchungu nilioupata kwani ndiyo mtoto wa kwanza,” alisema Salum.
USTADAH ALIPANGA MAUAJI?
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kuwa, ustadh huyo alijiandaa kutekeleza mauaji hayo kwa vile aliandaa kisu na ndoo kwa ajili ya kukingia damu ya mtoto huyo kwa kile watu walichodai alitaka kuinywa.
POLISI MZIGONI
Baadaye taarifa zilienea maeneo yote ya Jiji la Dar hususan Mbagala-Charambe na polisi walitua eneo hilo na kuchukua miili ya marehemu wote wawili na kupelekwa chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Temeke.
Mwili wa Jamal ukipelekwa eneo la makaburini kwa maziko.
Pale hospitalini, madaktari walitumia saa mbili kichwa cha mtoto Jamal na kiwiliwili.
USTADH ATAJWA KUTOKUWA NA AKILI
Mdogo wa Ustadh Mohamed aliyekuwa msemaji wa familia, Daudi Ngulangwa alisema marehemu kaka yake aliwahi kupatwa na ugonjwa wa akili mwaka 1995/96 kisha kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kutibiwa na akapona.
Maziko ya mtoto Jamal yakifanyika.
MAZISHI YAO
Marehemu Jamal alizikwa Jumamosi iliyopita katika Makaburi ya Mbagala-Charambe jijini Dar (Uwazi lilikuwepo).
Ustadh Mohamed, yeye alizikwa siku hiyohiyo kwenye Makaburi ya Manzese jijini Dar es Salaam.
Share:

FAMILIA YA MISS TZ YAGOMBEA MAITI

FAMILIA YA MISS TZ YAGOMBEA MAITI

Stori: Haruni Sanchawa na Denis Mtima
FAMILIA ya Miss Tanzania 1999, Hoyce Nambuo Temu, inadaiwa kuingia katika mzozo mkubwa wa wapi pa kumzikia mwanafamilia mwenzao, Emmanuel Lewi Nambuo Temu (33) aliyefariki dunia Februari 15 mwaka huu katika Hospitali ya Temeke, Dar.
Marehemu Emmanuel Lewi Nambuo Temu (33) enzi za uhai wake.
Mama wa marehemu Emmanuel, Hilda Lewi Nambuo ameshikilia msimamo kwamba, mwanaye akazikwe kwenye makaburi waliyozikwa mababu zao yaliyopo kwenye Kijiji cha Kikarara, Old Moshi, Kilimanjaro lakini mjomba mtu aitwaye Jacob Nambuo Temu anapinga.
Jacob na Hilda ni mtu na mdogo wake, Hilda akidaiwa kuwa mkubwa. Jacob ni mjomba wa Hoyce na Hilda ni shangazi yake.
Sakata hilo lilifikishwa kwenye Mahakama ya Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam na kupewa jalada namba 7/2014 ambapo mama wa marehemu anaitaka korti iamuru mwili wa marehemu ukazikwe huko kwa kuwa huo ndiyo wosia wa marehemu.
 
Hoyce Nambuo Temu.
“Kutoruhusu mwili huo kuzikwa tunakokutaja kutaongeza uhusiano wa ugomvi wa mama wa marehemu na kaka ambaye ni mlalamikiwa,” imesema sehemu ya hati ya mahakama hiyo iliyosainiwa na Hakimu K. Mkwawa.
Mheshimiwa Mkwawa alisema kutokana na ombi la mama wa marehemu, mahakama hiyo imezuia kuchukuliwa kwa mwili huo kutoka katika Mochwari ya Hospitali ya Temeke, Dar hadi Februari 25, mwaka huu (leo) ambapo atasikiliza pande zote mbili kuhusiana na sakata hilo.
Kwa upande wake mjomba mkubwa wa marehemu, Dk. M. Nambuo Temu aliyeko nje ya nchi ametuma ujumbe akisema ameridhia marehemu akazikwe kwenye makaburi ya mababu huko Old Moshi.
Katika barua yake (nakala tunayo) aliyowaandikia ndugu zake, Hoyce na Rachel Temu na wahusika wengine wa mgogoro huo, Dk. Temu alisema  amesikitika kusikia kuwa, Jacob hataki Emmanuel azikwe nyumbani kwao Old Moshi kama  yeye marehemu  alivyoagiza katika wosia wake.
“Yeye (Emmanuel) mwenyewe kabla ya kufariki dunia aliwahi kumwelezea rafiki yake Noel kuwa akifa akazikwe kwa Watemu (ukoo wa Temu) na si mahali pengine popote pale. Hatuna sababu ya kubishana juu ya mahali pa kumzika Emmanuel,” alisema Dk. Temu.
Dk. Temu alihitimisha waraka wake kwa kusema kuwa, mdogo wake (Jacob) hana haki yoyote ya kudai kuwa shamba la baba yao (marahemu mzee Temu) ni lake yeye kwa sababu hawajaligawa.
Share:

ASKOFU BILIONEA BONGO ATIKISA

ASKOFU BILIONEA BONGO ATIKISA

Stori: Jelard Lucas
ASKOFU na Nabii George David ‘Geordavie’ wa Kanisa la Geordavie Ministry ‘Ngurumo ya Upako’ lililoko jijini Arusha na Kawe, Dar hivi karibuni alifanya mkutano mkubwa na kutikisa nchi  kwa kuwa na magari ya kifahari na ndege aina ya helikopta ‘chopa’ iliyokuwa ikirandaranda juu ya anga kulinda usalama wake, Uwazi lina ushuhuda wa kutosha.
Katika mkutano huo uliofanyika Karatu mkoani Manyara, mwandishi wetu alishuhudia msafara wa Geordavie ambaye hutoa huduma ya uponyaji kwa njia za miujiza, ukiwavutia watu wengi kwa kuwa ulikuwa na ulinzi mkali ambao haujawahi kutokea.
Mbali ya kuwa na chopa iliyokuwa ikiimarisha ulinzi ambayo ameinunua hivi karibuni, askofu huyo alikuwa na msururu wa magari yenye thamani kubwa yanayomfanya kutajwa kuwa tajiri kuliko maaskofu wengine wanatoa huduma katika makanisa ya kiroho Tanzania.
Akiwa Karatu, mbali na ulinzi binafsi, Geordavie alikuwa akilindwa na askari wa jeshi la polisi, askari kanzu, Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na wale wa usalama barabarani.
Mbali na askari hao wa serikali ambao wamekuwa wakimlinda kila anapofanya mikutano yake, pia Geordavie analindwa na askari wake binafsi hali iliyowafanya baadhi ya watu kuamini kuwa ulinzi wake ni kama ule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’.
“Sijawahi kumuona JK akilindwa na chopa lakini mtumishi wa Mungu Geordavie analindwa na ndege katika msafara wake! Hii ni mara yangu ya kwanza kuona,” alisema muumini mmoja ambaye hakupenda kutajwa gazetini.
Hata hivyo, baadhi ya watu walikuwa wakihoji utajiri wa askofu huyo kutokana na fedha nyingi anazozitumia anapofanya mikutano katika sehemu mbalimbali jijini Arusha.
“Tunajua kuwa ni tajiri, lakini anapata wapi fedha za kutumia hivi?” alihoji muumini aliyejitambulisha kwa jina moja la Julius ambaye naye alihudhuria mkutano wa askofu huyo anayetumia kaulimbiu ya Ngurumo ya Upako katika kutoa huduma yake.
Pia, waumini wengine walilalamikia ugumu wanaoupata wanapotaka  kumuona mtumishi huyo wa Mungu kutokana na ulinzi mkali anaopewa.
“Kila mtu alitamani kumuona mtumishi wa Mungu lakini haikuwezekana kutokana na ulinzi wake kuwa mkali, utajiri wake hakuna mfano, hata kule nyumbani kwake Arusha, anaishi kama Mfalme Daud,” alisema Fred Mushi.
Gazeti hili lilimsaka Askofu na Nabii Geordavie kwa lengo la kutaka kujua sababu ya kuwa na ulinzi mkali na kutumia magari ya kifahari ikiwemo chopa katika mikutano anayoifanya lakini simu yake iliita bila kupokelewa.

Share:

DK. CHENI: FREEMASON WANANITESA

DK. CHENI: FREEMASON WANANITESA


MINONG’ONO na uvumi unaotambaa kwa kasi kuwa anajihusisha na taasisi ya wajenzi huru (Freemasons), unazidi kumtesa msanii wa filamu za Kibongo, Mahsein Awadhi Said ‘Dk. Cheni’ kwa madai ya kwamba anajisikia vibaya anaponyoshewa vidole na baadhi ya wadau wa tasnia hiyo.
Dk. Cheni.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, mwandishi wetu alisikia fununu kutoka kwa wadau wengi wa filamu wakiwemo wasanii wenzake wakidai  kuwa Dk. Cheni ni mwanachama halali wa taasisi hiyo ndiyo maana mambo yake ni mazuri kifedha ukilinganisha na wasanii wengine wanaoaminika kuwa na uwezo mkubwa wa kuigiza kuliko yeye.
“Kila dalili inaonesha kabisa Dk. Cheni ni Freemason, angalia mavazi yake mengi ni meusi, machata na alama kibao zinazohusishwa na taasisi hiyo, angali fedha aliyonayo, angalia hata gari lake lilivyojaa alama za ajabu ajabu, huyu jamaa ni Freemason kabisa,” alisema mdau mmoja wa filamu ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alipozungumza na mwandishi wetu.
Kauli kama hizo zimekuwa zikitolewa kwa nyakati tofauti na baadhi ya wasanii wenzake.
Dk. Cheni alipotafutwa kwa njia ya simu Jumapili ya wiki iliyopita na kuulizwa madai hayo alikuwa na haya ya kusema:
“Dah! na wewe umeyapata kaka? Hakika naumia sana na madai hayo, yamevuma sana kwa wadau, tena baadhi yao ni watu ninaowaheshimu sana, jamani mimi siyo Freemason, naigiza, kazi zangu za u-MC zinaniingizia kipato, najiwekea akiba.
“Si mtu wa starehe, nawekeza katika biashara ndogondogo, madai haya ya Freemason yananitesa sana ila namwachia Mungu,” alisema Dk. Cheni.
Share:

Friday 21 February 2014

MATOKEO YA NG'WIGWA SECONDARY SCHOOL 2013 KIDATO CHA NNE


NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2013 EXAMINATION RESULTS

S2571 NG'WIGWA SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 0 DIV-II = 5 DIV-III = 10 DIV-IV = 15 DIV-0 = 12


CNO
SEX
AGGT
DIV
DETAILED SUBJECTS
S2571/0001
F
29
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' PHY - 'D' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'C'
S2571/0002
F
27
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'B' ENGL - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'D'
S2571/0003
F
34
IV
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'E'
S2571/0004
F
42
IV
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0005
F
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'
S2571/0006
F
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'
S2571/0007
F
40
IV
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'E' KISW - 'C' ENGL - 'E' CHEM - 'E' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0008
F
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'
S2571/0009
F
*E
*E
---
S2571/0010
F
*E
*E
---
S2571/0011
F
34
IV
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'C' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'B' B/MATH - 'E'
S2571/0012
F
47
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'E' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'E' B/MATH - 'F'
S2571/0013
F
49
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0014
F
20
II
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S2571/0015
F
28
III
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'B' ENGL - 'C' CHEM - 'D' BIO - 'B' B/MATH - 'F'
S2571/0016
M
30
III
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'C'
S2571/0017
M
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'
S2571/0018
M
*E
*E
---
S2571/0019
M
46
0
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'F' KISW - 'E' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0020
M
42
0
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'F' PHY - 'F' CHEM - 'E' BIO - 'E' B/MATH - 'E'
S2571/0021
M
42
0
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'E' BIO - 'E' B/MATH - 'F'
S2571/0022
M
46
0
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'E' ENGL - 'E' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0023
M
37
IV
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0024
M
49
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0025
M
25
III
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'D' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'D'
S2571/0026
M
*E
*E
---
S2571/0027
M
23
II
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'C' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B'
S2571/0028
M
44
0
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'E' KISW - 'E' ENGL - 'E' BIO - 'E' B/MATH - 'F'
S2571/0029
M
28
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'D' ENGL - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'E'
S2571/0030
M
36
IV
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'F'
S2571/0031
M
30
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'D' BIO - 'B' B/MATH - 'F'
S2571/0032
M
38
IV
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'E' BIO - 'C' B/MATH - 'F'
S2571/0033
M
36
IV
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' CHEM - 'E' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0034
M
*E
*E
---
S2571/0035
M
37
IV
CIV - 'E' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0036
M
39
IV
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0037
M
32
IV
CIV - 'C' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'E'
S2571/0038
M
23
II
CIV - 'B' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'D'
S2571/0039
M
36
IV
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'E' BIO - 'C' B/MATH - 'F'
S2571/0040
M
35
IV
CIV - 'E' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0041
M
41
0
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'E' ENGL - 'E' CHEM - 'E' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0042
M
28
III
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'B+'
S2571/0043
M
35
IV
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'D' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'D'
S2571/0044
M
27
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'C' B/MATH - 'D'
S2571/0045
M
48
0
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0046
M
23
II
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'D' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'C'
S2571/0047
M
35
IV
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'E' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'C'
S2571/0048
M
47
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'E' BIO - 'E' B/MATH - 'F'
S2571/0049
M
48
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'E' ENGL - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0050
M
24
II
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'D'
S2571/0051
M
27
III
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'D'
S2571/0052
M
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'


EXAMINATION CENTRE RANKING
EXAMINATION CENTRE REGION
SIMIYU
TOTAL PASSED CANDIDATES
30
EXAMINATION CENTRE GPA
4.4483
CENTRE CATEGORY
CENTRE WITH 40 CANDIDATES OR MORE
CENTRE POSITION IN ITS CATEGORY(REGIONWISE)
11/75
CENTRE POSITION IN ITS CATEGORY(NATIONWISE)
545/3256
EXAMINATION CENTRE DIVISIONS PERFORMANCE
REGIST
ABSENT
SAT
WITHHELD
NO-CA
CLEAN
DIV I
DIV II
DIV III
DIV IV
DIV 0
52
5
47
5
0
42
0
5
10
15
12
EXAMINATION CENTRE SUBJECTS PERFORMANCE
CODE
SUBJECT NAME
REG
SAT
NO-CA
W/HD
CLEAN
PASS
GPA
REG/RANK
NAT/RANK
011
CIVICS
52
47
0
5
42
20
5.2381
52/141
864/4355
012
HISTORY
52
47
0
5
42
22
5.5238
71/141
1097/4322
013
GEOGRAPHY
52
47
0
5
42
22
5.4048
55/141
903/4352
021
KISWAHILI
52
47
0
5
42
32
4.7857
116/141
2319/4355
022
ENGLISH LANGUAGE
52
47
0
5
42
26
5.2143
97/141
1543/4355
031
PHYSICS
16
16
0
0
16
15
4.1875
4/140
312/3841
032
CHEMISTRY
29
29
0
0
29
20
4.8276
12/140
922/4052
033
BIOLOGY
52
47
0
5
42
31
4.4286
19/141
508/4351
041
BASIC MATHEMATICS
52
47
0
5
42
14
5.9524
40/141

Share:

MATOKEO YA NG'WIGWA SECONDARY SCHOOL 2013 KIDATO CHA NNE


NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2013 EXAMINATION RESULTS

S2571 NG'WIGWA SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 0 DIV-II = 5 DIV-III = 10 DIV-IV = 15 DIV-0 = 12


CNO
SEX
AGGT
DIV
DETAILED SUBJECTS
S2571/0001
F
29
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' PHY - 'D' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'C'
S2571/0002
F
27
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'B' ENGL - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'D'
S2571/0003
F
34
IV
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'E'
S2571/0004
F
42
IV
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0005
F
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'
S2571/0006
F
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'
S2571/0007
F
40
IV
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'E' KISW - 'C' ENGL - 'E' CHEM - 'E' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0008
F
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'
S2571/0009
F
*E
*E
---
S2571/0010
F
*E
*E
---
S2571/0011
F
34
IV
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'C' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'B' B/MATH - 'E'
S2571/0012
F
47
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'E' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'E' B/MATH - 'F'
S2571/0013
F
49
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0014
F
20
II
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'B'
S2571/0015
F
28
III
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'B' ENGL - 'C' CHEM - 'D' BIO - 'B' B/MATH - 'F'
S2571/0016
M
30
III
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'C'
S2571/0017
M
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'
S2571/0018
M
*E
*E
---
S2571/0019
M
46
0
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'F' KISW - 'E' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0020
M
42
0
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'F' PHY - 'F' CHEM - 'E' BIO - 'E' B/MATH - 'E'
S2571/0021
M
42
0
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'E' BIO - 'E' B/MATH - 'F'
S2571/0022
M
46
0
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'E' ENGL - 'E' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0023
M
37
IV
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0024
M
49
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0025
M
25
III
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'D' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'D'
S2571/0026
M
*E
*E
---
S2571/0027
M
23
II
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'C' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'B'
S2571/0028
M
44
0
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'E' KISW - 'E' ENGL - 'E' BIO - 'E' B/MATH - 'F'
S2571/0029
M
28
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'D' ENGL - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'E'
S2571/0030
M
36
IV
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'F'
S2571/0031
M
30
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'D' BIO - 'B' B/MATH - 'F'
S2571/0032
M
38
IV
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'E' BIO - 'C' B/MATH - 'F'
S2571/0033
M
36
IV
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' CHEM - 'E' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0034
M
*E
*E
---
S2571/0035
M
37
IV
CIV - 'E' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0036
M
39
IV
CIV - 'E' HIST - 'D' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0037
M
32
IV
CIV - 'C' HIST - 'E' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'E'
S2571/0038
M
23
II
CIV - 'B' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'D'
S2571/0039
M
36
IV
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'E' BIO - 'C' B/MATH - 'F'
S2571/0040
M
35
IV
CIV - 'E' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0041
M
41
0
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'E' ENGL - 'E' CHEM - 'E' BIO - 'D' B/MATH - 'F'
S2571/0042
M
28
III
CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'B+'
S2571/0043
M
35
IV
CIV - 'E' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'D' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'D'
S2571/0044
M
27
III
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'C' B/MATH - 'D'
S2571/0045
M
48
0
CIV - 'E' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0046
M
23
II
CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'B' KISW - 'C' ENGL - 'D' PHY - 'B' CHEM - 'B' BIO - 'B+' B/MATH - 'C'
S2571/0047
M
35
IV
CIV - 'D' HIST - 'E' GEO - 'E' KISW - 'D' ENGL - 'E' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'C'
S2571/0048
M
47
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'E' BIO - 'E' B/MATH - 'F'
S2571/0049
M
48
0
CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'E' ENGL - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'
S2571/0050
M
24
II
CIV - 'B' HIST - 'B' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'D'
S2571/0051
M
27
III
CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'B' B/MATH - 'D'
S2571/0052
M
-
ABS
CIV - 'X' HIST - 'X' GEO - 'X' KISW - 'X' ENGL - 'X' BIO - 'X' B/MATH - 'X'


EXAMINATION CENTRE RANKING
EXAMINATION CENTRE REGION
SIMIYU
TOTAL PASSED CANDIDATES
30
EXAMINATION CENTRE GPA
4.4483
CENTRE CATEGORY
CENTRE WITH 40 CANDIDATES OR MORE
CENTRE POSITION IN ITS CATEGORY(REGIONWISE)
11/75
CENTRE POSITION IN ITS CATEGORY(NATIONWISE)
545/3256
EXAMINATION CENTRE DIVISIONS PERFORMANCE
REGIST
ABSENT
SAT
WITHHELD
NO-CA
CLEAN
DIV I
DIV II
DIV III
DIV IV
DIV 0
52
5
47
5
0
42
0
5
10
15
12
EXAMINATION CENTRE SUBJECTS PERFORMANCE
CODE
SUBJECT NAME
REG
SAT
NO-CA
W/HD
CLEAN
PASS
GPA
REG/RANK
NAT/RANK
011
CIVICS
52
47
0
5
42
20
5.2381
52/141
864/4355
012
HISTORY
52
47
0
5
42
22
5.5238
71/141
1097/4322
013
GEOGRAPHY
52
47
0
5
42
22
5.4048
55/141
903/4352
021
KISWAHILI
52
47
0
5
42
32
4.7857
116/141
2319/4355
022
ENGLISH LANGUAGE
52
47
0
5
42
26
5.2143
97/141
1543/4355
031
PHYSICS
16
16
0
0
16
15
4.1875
4/140
312/3841
032
CHEMISTRY
29
29
0
0
29
20
4.8276
12/140
922/4052
033
BIOLOGY
52
47
0
5
42
31
4.4286
19/141
508/4351
041
BASIC MATHEMATICS
52
47
0
5
42
14
5.9524
40/141

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger