Thursday 13 February 2014

UCHAGUZI MDOGO KALENGA: KAMATI KUU YA CHADEMA KUKUTANA KWA DHARURA FEB 14, 2014

...

http://api.ning.com/files/9pVNH1qXqqxQSKXKvxSGUFMFz9TtxF3Bs*OBQXiDz1wB4BtRN-5TARspxoKApgqvscQTWUMrnSOvL9*XVF-pyW7xqpuA2LO1/Chadema_logo.jpg
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KAMATI KUU YA CHADEMA KUKUTANA KWA DHARURA
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana kwa ajili ya kikao cha dharura, Februari 14, mwaka huu, jijini Dar es Salaam.
Katika kikao hicho, Kamati Kuu itajadili na kufanya uteuzi wa mwisho wa jina la mgombea ubunge wa CHADEMA katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga, mkoani Iringa, unaotarajiwa kufanyika Machi 16, mwaka huu.
Kikao hicho kitafanya uteuzi wa mwisho, baada ya mchakato wa ndani wa kumpata mgombea ubunge wa Jimbo la Kalenga kwa tiketi ya CHADEMA, kuwa umepitia hatua za awali, ambazo ni…
http://api.ning.com/files/9pVNH1qXqqxQSKXKvxSGUFMFz9TtxF3Bs*OBQXiDz1wB4BtRN-5TARspxoKApgqvscQTWUMrnSOvL9*XVF-pyW7xqpuA2LO1/Chadema_logo.jpg
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KAMATI KUU YA CHADEMA KUKUTANA KWA DHARURA
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana kwa ajili ya kikao cha dharura, Februari 14, mwaka huu, jijini Dar es Salaam.
Katika kikao hicho, Kamati Kuu itajadili na kufanya uteuzi wa mwisho wa jina la mgombea ubunge wa CHADEMA katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga, mkoani Iringa, unaotarajiwa kufanyika Machi 16, mwaka huu.
Kikao hicho kitafanya uteuzi wa mwisho, baada ya mchakato wa ndani wa kumpata mgombea ubunge wa Jimbo la Kalenga kwa tiketi ya CHADEMA, kuwa umepitia hatua za awali, ambazo ni pamoja na watu wote wenye nia ya kugombea, kuchukua fomu za uteuzi, tangu Februari 5-10, mwaka huu.
Jumla ya watu 16 waliweza kuchukua fomu za kuwania uteuzi huo, ambapo hadi siku ya mwisho, watu 13 waliweza kurejesha fomu zao na kupita kwenye mchakato wa kura za maoni, zilizofanyika Februari 12, mwaka huu.
Imetolewa leo Februari 13, 2014, Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari- CHADEMA

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger