Sunday 31 January 2021

Wakamatwa Kwa Madai Ya Wizi Wa Fedha Kwa Njia Ya Simu


Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Ialla jijini Dar es Salaam linawashikilia watu 10 kwa tuhuma za wizi wa mtandaoni na utapeli.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa Ilala, Janeth Magomi imeeleza kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa katika tarehe tofauti ya mwezi Januari mwaka huu katika maeneo tofauti ya Jiji la Dar es Salaam na wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Aidha, Mgomi ameeleza kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) baada ya wananchi kadhaa kutapeliwa fedha zao. Wananchi hao walitoa taarifa kwa jeshi hilo ndipo ukafanyika msako pamoja na kuweka mtego wa kubaini mtandao wa watuhumiwa hao.

Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi Mkoa wa Ilala limewatahadhariasha watumiaji wa huduma za mitandao kuwa makini na watu ambao mara nyingi wanajifanya ni watoa huduma za mitandao husika na kuwalaghai wananchi ili kuwaibia.

Miongoni mwa watuhumiwa waliotiwa mbaroni ni pamoja na Baraka Makwaya, Fatuma Ayoub, Teddy Njauz, Modesta Njauz pamoja na Gift Makwaya.


Share:

Serikali yakamilisha ujenzi wa kituo cha kupozea umeme wa SGR


Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limekamilisha ujenzi wa miundombinu ya umeme itakayotumika kuendesha treni ya mwendokasi (SGR) kutoka jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro huku awamu ya pili kutoka mkoani Morogoro kuelekea Matukupola mkoani Dodoma ikitarajiwa kuanza hivi karibuni.

Akizungumza mjini Morogoro mara baada ya kutembelea kituo cha kupozea umeme kilichopo Kingolwira nje kidogo ya Manispaa ya Morogoro, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema kwa sasa ujenzi wa miundombinu hiyo yenye urefu wa kilomita 160 imekamilika kwa asilimia 100.

Kwa upande wake Meneja Mwandamizi wa miradi kutoka TANESCO, Mhandisi Emmanuel Manilabona amesema vituo vyote vya kupoza umeme vilivyopo katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro tayari vimeshakalimika.


Share:

IGP Sirro Awataka Polisi Wasaidizi Kufuata Sheria


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewataka Polisi Wasaidizi waliopo kwenye taasisi mbalimbali nchini kuhakikisha wanaheshimu na kuzingatia sheria sambamba na nidhamu wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za kila siku katika kubaini, kuzuia na kupambana na uhalifu.

IGP Sirro amesema hayo jana  jijini Dar es salaam, wakati alipofanya kikao kazi na Polisi Wasaidizi waliopo Kanda Maalum ya Dar es salaam ambapo amesema kuwa, weledi, ufanisi na kujituma kutasaidia kupunguza malalamiko miongoni mwa jamii wanayoihudumia.

Naye Kamishna wa Kamisheni ya Ushirikishwaji wa Jamii Dkt. Mussa Ali Mussa amesema kuwa, uwepo wa Polisi Wasaidizi umesaidia kuwezesha mamlaka na Halmashauri mbalimbali zilizopo nchini kuendelea kuimarika.


Share:

Video Mpya ya Zuchu – Sukari


Video Mpya ya Zuchu – Sukari


Share:

Marekani Yasitisha Mpango wa Chanjo kwa Wafungwa


Wizara ya ulinzi ya Marekani imesema itasimamisha mpango wake wa kuwapa chanjo dhidi ya COVID-19 wafungwa wa makosa ya ugaidi wanaozuiwa kwenye kambi ya Guantanamo kufuatia kuongezeka kwa malalamiko katika wakati ambapo nchi hiyo inajikakamua kuwachanja kwanza watumishi wa afya na wazee. 

Msemaji wa wizara hiyo John Kirby ameandika hayo kupitia ukurasa wa twitter akisema hakuna mfungwa yoyote kwenye kambi hiyo ambaye tayari amechanjwa. 

Kirby amekiri akisema ni kweli rais Joe Biden amesema ana mpango wa kutokomeza virusi vya corona katika siku yake ya kwanza ofisini lakini hakusema atawapa chanjo magaidi kwanza kabla ya Wamarekani.

 Kambi ya Guantanamo iliyoko Cuba inawazuia washukiwa wa makosa ya ugaidi ikiwa ni pamoja na Khalid Sheikh Mohammed, mfuasi wa kundi la Al-Qaeda anayedaiwa kupanga shambulizi la Septemba 11.

-DW



Share:

Tutatenga Fedha Kwa Ajili Ya Huduma Za Ugani- Prof. Mkenda


Wizara ya Kilimo imesema katika bajeti ya mwaka 2021/22 inatarajia kutenga fedha mahsusi kwa ajili kugharimia huduma za ugani ili kuondoa changamoto zinazotatiza ukuaji wa tija kwenye uzalishaji mazao nchini ikiwemo maslahi ya maafisa kilimo ugani.


Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda ametoa kauli hiyo jana (30.01.2021) jijini Dodoma wakati akifunga kikao kazi baina ya wizara yake na maafisa kilimo toka mikoa 26 na halmashauri zote 185 za Tanzania bara uliojadili hali ya upatikanaji huduma za ugani kwenye kilimo.


“Kilimo kimekuwa na maneno mengi utasikia kilimo ni uti wa mgongo ama kilimo cha kufa na kupona.Sasa tunasema maneno yametosha hebu tuanze hatua moja mbele kwa vitendo tuboreshe utoaji huduma za ugani nchini ili wakulima wahudumiwe kwa vitendo” alisema Prof. Mkenda.


Prof. Mkenda alibainisha kuwa wizara yake imeitisha kikao hicho cha siku mbili ili kujadiliana na wataalam wa kilimo wote pamoja na wadau wa sekta binafsi hali ya kuboresha utoaji huduma za ugani na kuweka mikakati ya kuondoa changamoto za ugani


Alisema kuwa suala la kutokuwepo bajeti mahsusi kwa ajili ya watoa huduma za ugani kwenye ngazi za mikoa, halmashauri na vijiji imekuwa ikiathiri utoaji huduma kwa wakulima kushindwa kulima kwa tija.


Katika kikao hicho Waziri wa Kilimo alirejea kueleza dira ya wizara yake kwa sasa na kutaja mambo manne ya kipaumbele ili kilimo kichangie zaidi ukuaji wa uchumi  kwanza ni kuongeza utafiti na uzalishaji mbegu bora za mazao.


Pili, kutoa elimu bora ya kilimo ,tatu kutafuta masoko ya mazao ya wakulima na nne kuhakikisha wakulima na wawekezaji wanapata mitaji yenye riba nafuu toka kwenye taasisi za kifedha nchini.


“Tutawekeza fedha bajeti ijayo na nguvu kukuza utafiti ili tupate mbegu bora zaidi zenye kutoa mavuno bora na tija kwa wakulima” alisisitiza Prof. Mkenda.


Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Charles Mwijage alisema anawapongeza wakulima wa Tanzania pamoja na wataalam wa kilimo kwa kuhakikisha katika kipindi cha miaka mitano ya kwanza ya serikali ya awamu ya tano Tanzania haikupata tatizo la njaa.


“ Kipindi chote kuanzia mwaka 2015 hadi 2020 nchi hii haikupata njaa, tunawashukuru maafisa ugani na wakulima wote wa Tanzania kwa kazi kubwa ya kuhakikisha taifa lina chakula cha kutosha” alisema Mwijage ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.


Mwijage aliiomba serikali kuweka mikakati mizuri na kuongeza bajeti ya kuhudumua watoa huduma za ugani wa serikali waliopo chini ya Ofisi ya Rais Tamisemi na Wizara ya Kilimo ili watatue changamoto za wakulima.


Naye Mwenyekiti wa umoja wa Maafisa Kilimo Halmashauri (DAICOs) Enock Ndunguru aliomba serikali kupitia Wizara ya Kilimo kuwa na mkakati wa kuwahamishia maafisa ugani waliopo halmashauri zote nchini kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa na sasa wawe chini ya Wizara ya Kilimo.


Katika hatua nyingine Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya alisema kwa sasa kuna maafisa ugani kilimo 6700 ambao wanahitaji kuwezeshwa vitendea kazi ili watekeleze majukumu yao ya kusimamia kilimo


Kusaya alisema kwa kuanzia wizara ya kilimo itaendeleza mkakati wa kuwapatia pikipiki maafisa ugani wote 67000 kwa awamu pamoja na kupeleka kifaa maalum cha kupima afya ya udongo (Extension Kit).


Akizungumza kwenye kikao hicho Mbunge wa Musoma Vijijini Prof. Sospeter Muhongo alitoa wito kwa serikali kufanya jitihada za kukifanya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere (Mwalimu Nyerere University of Agriculture) kilichopo Butiama Mara kianze kudahili wanafunzi mwaka 2021/22 ili kifundishwe maafisa ugani.


“Chuo hiki cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere  cha Butiama kimekusudiwa kufundisha wataalam wa ugani ,tunaomba kianze mapema mwaka huu 2021 ili tatizo la upatikanaji wataalam wa kilimo hususan vijijini litatuliwe” alisema Prof. Muhongo.


Mwisho
Imeandaliwa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Kilimo
DODOMA
31.01.2021




Share:

Naibu Waziri Mabula Awabana Watendaji Sekta Ya Ardhi Kuongeza Kasi Utoaji Hati

 Na Munir Shemweta, WANMM MARA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka Watendaji wote wa sekta ya ardhi katika halmashauri kushiriki zoezi la kuandaa hati za ardhi ili kuongeza kasi ya utoaji hati katika maeneo mbalimbali nchini.

Dkt Mabula ametoa agizo hilo mwishoni mwa wiki alipozungumza na wataalamu wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Mara akiwa katika ziara ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi na kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya Serikali kupitia kodi ya pango la ardhi katika mkoa huo.

Alisema, baadhi ya halmashauri nchini zimekuwa na kasi ndogo ya uandaaji hati za ardhi kwa kisingizio cha kuwa na wataalamu wachache wa kuandaa hati wakati halmashauri hizo zina wataalamu mbalimbali wa sekta hiyo na kutolea mfano wataalamu wa Mipango Miji, Warasimu Ramani, Wapimaji na  Wathamani aliowaeleza wamekuwa wakisoma chuo kinachotoa taaluma ya sekta ya ardhi.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliongeza kwa kusema kuwa, iwapo watendaji wa sekta ya ardhi watafanya kazi kwa ushirikiano na kupeana malengo ya kuandaa Hati basi kasi ya utoaji hati itaongezeka na hivyo kuifanya wizara kuongeza makusanyo ya   maduhuli ya serikali kupitia kodi ya pango la ardhi.

“Ninyi nyote mmesoma katika chuo cha aina moja na mnazifahamu kazi za sekta ya ardhi  mnaweza kupeana malengo na kila mmoja akashiriki kuandaa Hati na inapofika hatua ya kukamilisha ndiyo apewe Afisa Ardhi Mteule ili kukamilisha” alisema Dkt Mabula

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, kama watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri hawatakuwa wabunifu na kufanya kazi kwa kujiwekea malengo kasi ya utoaji hati itakuwa ndogo na utaifanya wizara kutofikia malengo yake ikiwemo ya makusanyo ya kodi ya pango la ardhi ambayo kwa mwaka 2020/2021 ni bilioni 200.

Naibu Waziri Dkt. Mabula alieleza kupitia kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Wakurugenzi wa Halmashauri za mkoa wa Mara kuwa, wakati Serikali ikifikia nusu mwaka wa fedha 2020/2021 makusanyo ya kodi ya ardhi katika halmashauri nyingi yako chini ya asilimia 50 jambo alilolieleza kuwa linatia shaka kama halmashauri hizo zitaweza kutimiza malengo katika muda uliosalia.

Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula aliwaambia watendaji hao wa sekta ya ardhi kuwa,  katika robo ya mwaka wa fedha 2020/2021 anataka kuona halmashauri zote zinaongeza kasi ya makusanyo kwa kuhakikisha zinawabana wadaiwa sugu ili kulipa malimbikizo ya kodi ya ardhi na na wale wadaiwa watakaokaidi kulipa basi wafikishwe kwenye Mabaraza ya Ardhi ya Nyumba na Wilaya kwa hatua zaidi.

Aliwaeleza wataalam hao wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Mara kuwa, kwa mujibu wa kifungu Na 48(1) (g) cha sheria ya ardhi, Afisa Ardhi anayo mamlaka ya kufuta umiliki wa ardhi kwa mmiliki aliyekaidi kulipa kodi ya pango la ardhi katika kipindi cha miezi sita baada ya kutumiwa ilani ya madai.  

Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa Mara Jerome Kiwia alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula kuwa, mkoa huo hadi sasa  umeweza kukusanya takriban milioni 890.3 za kodi ya pango la ardhi na kubainisha kuwa, ofisi ya Ardhi katika mkoa huo imejiwekea mikakati  ya kuhakikisha kasi ya makusanyo inaongezeka ikiwemo kusambaza ilani za madai kwa wadaiwa sugu na kutumia vyombo vya habari kuhamasisha ulipaji kodi ya pango la ardhi.


Share:

Serikali Yaokoa Shilingi Milioni 304 Ujenzi Wa Jengo La Dharura

Na. WAMJW-Tabora
Wizara ya Afya imeokoa takribani shilingi milioni 389 katika ujenzi wa jengo la Idara ya huduma za wagonjwa wa dharura linalojengwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora- Kitete ambalo limewekwa jiwe la msingi na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia Dkt. John Pombe Magufuli alipokua akitoa salamu za wizara hiyo kwa wakazi wa mkoa wa Tabora.

Dkt. Gwajima alisema ujenzi wa jengo hilo litakalo wahudumia wakazi wa Tabora, mikoa ya jirani na hata nje ya nchi kutokana na barabara kuu zinazopita mkoani hapo kwakuwa jengo hilo litakua na uwezo kuwahudumia wagonjwa 50 hadi 60 tofauti na awali ambapo walikua wakihudumia wagonjwa 3 hadi 5.

Alitaja gharama za ujenzi wa jengo hilo ni milioni 604.3 ambao zimetolewa kwa ushirikiano na mfuko wa dunia (Global Fund) na ujenzi wake umetumia mfumo wa ‘force Account’ na hivyo limeweza kuokoa fedha hizo na endapo lisingetumia njia hiyo lingegharimu zaidi ya shilingi bilioni moja.

Vile vile Dkt. Gwajima alisema wamepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Mhe. Rais na kuahidi yeye na wizara yake kufanyia kazi ikiwemo kuongeza madaktari bingwa, kuwafuatilia wale walioondoka pamoja na jengo la huduma la mama na mtoto kwa ajili ya kujifungua na ICU.

Miradi mingine ya ujenzi wa Idara ya huduma za wagonjwa wa dharura nchini ambayo wizara inashirikiana na Global Fund inatekelezwa na ipo hatua mbalimbali za kukamilishwa katika mikoa ya Ruvuma, Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Kilimanjaro, Njombe, Mara na Tanga.


Share:

Updates : PAKUA APP YA MALUNDE 1 BLOG ....IMEFANYIWA MABORESHO 2021

Share:

Procurement and Logistics Coordinator at Plan International Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Procurement and Logistics Coordinator Location: Ifakara, Tanzania Company: Plan International The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Crane Operator at Gas Entec Co. L.T.D

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

JOB OPPOETUNITY AT GAS ENTEC CO LTD   PROJECT TITLE: CONSTRUCTION OF 1200 PASSENGER FERRY SHIP DESIGNATION: Crane Operator (1 POST) PLACE OF WORK: MWANZA JOB SUMMARY: Responsible for Crane Operation and maintenance Inspecting equipment, structures, or materials to identify the cause of errors or other problems or defects. Servicing, repairing, adjusting, and testing machines. DUTIES & […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

1500+ Jobs at JVACEE a Joint venture company of Arab Contractors And El-sewedy Electric (Stigler’s Gorge Project)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

JVACEE is a Joint venture company of Arab Contractors and El-sewedy Electric, dealing with the scope of Engineering, Procurement & Construction of Julius Nyerere Hydropower Project in Stigler’s Gorge in Tanzania, which is expected to produce 2,115 MW of installed capacity. Job Title:  Foreman – Welding 9 Job Description: oversees and manages the welding team or individual […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

7 Job Opportunities at Rural Energy Agency (REA)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Opportunities at Rural Energy Agency (REA) Rural Energy Agency (REA) is an autonomous body under the Ministry of Energy and Minerals of the United Republic of Tanzania. Its main role is to promote and facilitate improved access to modern energy services in rural areas of Mainland Tanzania. REA became operational in October 2007. On […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Procurement And Supplies Officer at Rural Energy Agency (REA)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST: PROCUREMENT AND SUPPLIES OFFICER II – 1 POST POST CATEGORY(S) PROCUREMENT & LOGISTIC MANAGEMENT TRANSPORT AND LOGISTICS EMPLOYER Rural Energy Agency (REA) APPLICATION TIMELINE: 2021-01-28 2021-02-10 DUTIES AND RESPONSIBILITIES   Evaluating vendor performance and advices accordingly; Maintaining an up-to-date filing system on pricing and vendors to ensure timely and accurate access to information; Preparing bid documents […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Monitoring And Evaluation Officer at Rural Energy Agency (REA)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST: MONITORING AND EVALUATION OFFICER II – 1 POST POST: CATEGORY(S) BANKING, ECONOMICS AND FINANCIAL SERVICES ENGINEERING AND CONSTRUCTION PROJECT, PLANNING AND POLICY MANAGEMENT STATISTICS AND MATHEMATICS WATER, MINING AND NATURAL RESOURCES EMPLOYER Rural Energy Agency (REA) APPLICATION TIMELINE: 2021-01-28 2021-02-10  DUTIES AND RESPONSIBILITIES Visiting project sites and submit progress reports periodically for projects under implementation and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Project Engineers at Rural Energy Agency (REA)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST: PROJECT ENGINEER II – 5 POSTS POST: CATEGORY(S) ENGINEERING AND CONSTRUCTION EMPLOYER Rural Energy Agency (REA) APPLICATION TIMELINE: 2021-01-28 2021-02-10 DUTIES AND RESPONSIBILITIES Managing projects contracts; Assisting in project identification, Planning, supervision and appraisal; Providing information and statistics on electricity projects carried out; Analyzing and preparing periodic electricity projects performance reports; Monitoring the progress of the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 31,2021













Share:

TADB YAWEZESHA WAFUGAJI KUPATA NG'OMBE WA KISASA WA MAZIWA


Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya Kilimo (TADB) Jeremiah Mhada wa kwanza kulia akimkabidhi hundi ya Sh Milioni 396 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki kwa ajili ya wafugaji mkoani Tanga kupata mbegu ya ng’ombe bora wa kisasa wa maziwa wakiwemo wafugaji 114 kupitia vyama vya msingi 5 kupata mikopo ya ng’ombe wa kisasa wa kwanza kushoto anayshuhudia ni Kaimu Msajili bodi ya maziwa Noely Byamungu
Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya Kilimo (TADB) Jeremiah Mhada wa kwanza kulia akimkabidhi hundi ya Sh Milioni 396 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki kwa ajili ya wafugaji mkoani Tanga kupata mbegu ya ng’ombe bora wa kisasa wa maziwa wakiwemo wafugaji 114 kupitia vyama vya msingi 5 kupata mikopo ya ng’ombe wa kisasa wa kwanza kushoto anayshuhudia ni Kaimu Msajili bodi ya maziwa Noely Byamungu
Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya Kilimo (TADB) Jeremiah Mhada wa kwanza kulia akimkabidhi hundi ya Sh Milioni 396 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki kwa ajili ya wafugaji mkoani Tanga kupata mbegu ya ng’ombe bora wa kisasa wa maziwa wakiwemo wafugaji 114 kupitia vyama vya msingi 5 kupata mikopo ya ng’ombe wa kisasa wa pili kushoto anayeshuhudia ni Kaimu Msajili bodi ya maziwa Noely Byamungu
 
Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya Kilimo (TADB) Jeremiah Mhada akizungumza wakati wa halfa hiyo
Sehemu ya wafugaji wakimsikiliza Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya Kilimo (TADB) Jeremiah Mhada akizungumza wakati wa halfa hiyo

BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imekwisha toa mikopo yenye thamani ya Shilingi billioni 11.80 ili  kuwezesha mnyororo wa thamani wa sekta ya maziwa kote nchini.

Pia imewezesha wafugaji Mkoani Tanga kupata mbegu ya ng’ombe bora wa kisasa wa maziwa wakiwemo wafugaji 114 kupitia vyama vya msingi 5 kupata mikopo ya ng’ombe wa kisasa wenye thamani ya Zaidi ya Tsh 396m.

Akizungumza katika hafla iliyoandaliwa na shirika la kimataifa la Heifer,Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya Kilimo (TADB) Jeremiah Mhada alieleza umuhimu wa ushirikiano wa wadau muhimu katika sekta ya mifugo ili kuongeza tija nakuleta mapinduzi ya kweli katika sekta ya maziwa nchini.

Alisema  kupitia mkopo huu, TADB imeweza kuwajengea wafugaji hao mabanda ya kutunzia ng’ombe 25 na kupata mitamba ya kisasa ili wanufaike na ufugajiwa ng’ombe wa maziwa ikiwemo kupatiwa mikopo naafuaa itakayowawezesha kupata mbegu bora za ng'ombe wa maziwa.

 “TADB ili kuhakikisha wafugaji wananufaika na sekta hii ya maziwa tuliingia katika ushirikiano na shirika la kimataifa la Heifer International kuhakikisha wafugaji wetu wanajengewa uwezo wa namna bora ya ufugaji wa ng’ombe wa maziwa lakini pia kujiunga katika vikundi ili kuweza kupata mikopo kwa urahisi.”Alisema

TADB imewezesha vyama vya msingivya UWAMWA, CHAWAMU, UWAKO, UWAMKI na UWADAKI kuweza kupata jumla ya ng’ombe wa kisasa 156 kwa wafugaji 121 ikiwemo wanawake 39 pamoja na kuwawezesha kupata mkopo huo wafugaji hao tayari wana soko la kuuza maziwa yao.

"Kwa hapa Tanga wataweza kuuza kwa kampuni ya Tanga Fresh ambayo nayo TADB imekwisha iwezesha katika kumudu kuweza kununua maziwa kutoka kwa wafugaji hawa wadogowadogo.” Alisisitiza Mhada.

Kabla ya kufanya makabidhiano hayo,TADB kwakushirikiananaShirika la kimataifa la Heifer International waliendesha mafunzo kwa viongozi wa vyama vya ushirika 26 ambao walijengewa uwezo kwenye namna ya usimamizi bora wa biashara, usimamizi wa fedha, utunzaji wa kumbukumbu, utunzajiwa kumbukumbu na uongozi bora.


“Ufugaji ili uwe na tija nilazima wafugaji wajengewe uwezo na ni muhimu kufahamu namna ya kusimamia fedha, utunzaji wa kumbukumbu,uongozi bora na masuala mengine ya usimamizi wa biashara kwa kuwa na uwezo huu, mfugaji anaweza kuona namna anavyonufaika na mkopo na hata kuweza kufahamu kipato chake.”Aliongezea Mhada.

Alisema Wafugaji wadogo kupitia TADB wanaendelea kunufaika na fursa zilizopo kupitia benki ya kilimo na pia kupitia ushirikiano huo wa TADB nashirika la kimataifa la Heifer.
 
Serikali imeainisha sekta ya maziwa kama moja ya sekta muhimu katika kuchochea uwekezaji katika viwanda jambo ambalo TADB inawawezesha wawekezaji kama kampuni za Tanga Fresh, Kahama Fresh, Njombe Milk na viwanda vingine katika maeneo mbalimbali nchini.

Aliongeza kwamba kupitia uwekezaji katika mnyororo wa thamani wa sekta ya kilimo, pia kama Taifa wanaweza kujihakikishia upatikanaji na usalama wachakula,lishe bora na kipato kwa wafugajina pia kuongezapato la Taifa.

Mhada alisema sekta  ya maziwa nchini inachangia asilimia 1.2% yapato la Taifa huku akieleza ili kuhakikisha wanaongeza kipato kwa wafugaji wadogo wadogo ambao kupitia shughuli hizi za ufugaji huchangia pato la Taifa.

Alisema wamewezesha kupata mitamba ya kisasa na kuwaunganisha na masoko ili kuongeza thamani na kuchochea ongezauzalishaji wa mazi wa nchini.

Share:

Saturday 30 January 2021

WAZIRI MWAMBE AKUTANA NA WAZALISHAJI WA SUKARI NCHINI JIJINI DODOMA

 

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe,akizungumza na Mtendaji Mkuu na Meneja wa kiwanda cha Dangote nchini Tanzania Bw.Abdullahi Baba aliyemtembelea ofisini kwake leo Januari 29,2021 jijini Dodoma

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe,akimsikiliza Mtendaji Mkuu na Meneja wa kiwanda cha Dangote nchini Tanzania Bw.Abdullahi Baba wakati wa mazungumzo ofisini kwake leo Januari 29,2021 jijini Dodoma

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe,akiwa katika picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu na Meneja wa kiwanda cha Dangote nchini Tanzania Bw.Abdullahi Baba mara baada ya mazungumzo ofisini kwake leo Januari 29,2021 jijini Dodoma

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe,akizungumza na wazalishaji wa Sukari nchini na kusikiliza changamoto zao ili kuzitatua na kuongeza uzalishaji wa Sukari leo Januari 29,2021 jijini Dodoma

Baadhi ya wazalisha wa Sukari Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe,wakati wa kikao cha wazalishaji wa Sukari nchini ambapo amesikiliza changamoto zao na kuahidi kuzitatua na kuongeza uzalishaji wa Sukari leo Januari 29,2021 jijini Dodoma

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe,akisisitiza jambo zaidi wakati wa kikao na wazalishaji wa Sukari nchini pamoja na kusikiliza changamoto zao ili kuzitatua na kuongeza uzalishaji wa Sukari leo Januari 29,2021 jijini Dodoma

Afisa Mtendaji Mkuu Utawala TPC Bw.Jaffari Ally akielezea jambo kwa Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe(hayupo pichani) wakati wa kikao cha wazalishaji wa Sukari nchini ambapo amesikiliza changamoto zao ili kuzitatua na kuongeza uzalishaji wa Sukari leo Januari 29,2021 jijini Dodoma

Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Sukari Tanzania Prof.Kenneth Bengesi,akizungumza kwenye kikao cha wazalishaji wa Sukari nchini ambapo Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Geoffrey Mwambe ameahidi kuzitatua changamoto hizo ili kuzitatua na kuongeza uzalishaji wa Sukari leo Januari 29,2021 jijini Dodoma


Na.Alex Sonna,Dodoma

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe,amekutana na wazalishaji wa Sukari nchini na kusikiliza changamoto zao ili kuzitatua na kuongeza uzalishaji na kuhakikisha Sukari inapatikana kwa urahisi wakati wote nchini.

Akizungumza na na wazalishaji hao leo Janauari 29,2021 jijini Dodoma Mhe.Mwambe amesema kuwa Serikali inalenga kuongeza uzalishaji wenye tija kwa kutumia teknlojia na miundombinu ya kisasa ya umwangiliaji.

”Leo nimekutana na nyie kwa leongo la kujifunza na kujua changamoto mlizonazo katika uzalishaji wa sukari nchini na waahidi tutazifanyia kazi”amesema Mhe.Mwambe.

Hata hivyo Mhe.Mwambe amewatoa wasiwasi wazalishaji hao kuwa Serikali itashughulikia changamoto hizo ili kuleta maendeleo na kuongeza uzalishaji zaidi nchini .

Awali Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Geoffrey Mwambe,amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu na Meneja wa kiwanda cha Dangote nchini Tanzania Bw.Abdullahi Baba.

Share:

WAFUGAJI NCHINI WATAKIWA KUFUGA KISASA

Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki akizungumza wakati
wakati wa hafla ya kukabidhi malori na vifaa vya maziwa kutoka shirika la Heifer International kupitia mradi wa usindikaji maziwa Tanzania (TMPP) iliyofanyika katika kiwanda cha Tanga Fresh kilichopo Jijini Tanga kushoto aliyekaa ni Meneja wa Kanda ya Mashariki Benki ya Maendeleo ya kilimo TADB Jeremiah Mhada
Mkurugenzi wa mradi wa usindikaji wa maziwa Tanzania kutoka shirika la Helfer Mark Tsoxoakizungumza wakati wa halfa hiyo
Meneja wa Kanda ya Mashariki Benki ya Maendeleo ya kilimo TADB Jeremiah Mhada akieleza jambo wakati wa halfa hiyo
Kaimu Msajili bodi ya maziwa Noely Byamunguakizungumza wakati wa halfa hiyo
Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki kushoto akikata utepe wakati wa hafla ya kukabidhi malori na vifaa vya maziwa kutoka shirika la Heifer International kupitia mradi wa usindikaji maziwa Tanzania (TMPP) iliyofanyika katika kiwanda cha Tanga Fresh kilichopo Jijini Tanga kulia ni Mkurugenzi wa mradi wa usindikaji wa maziwa Tanzania kutoka shirika la Helfer Mark Tsoxo

Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki kushoto akimshukuru Mkurugenzi wa mradi wa usindikaji wa maziwa Tanzania kutoka shirika la Helfer Mark Tsoxo mara baada ya makabidhiano hayo kulia anayeshuhudia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye pia alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga katika halfa hiyo
Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki akiwasha moja ya magari hayo

WAFUGAJI  nchini wametakiwa kubadilika na kuachana na ufugaji wa mazoea bali wafuge kisasa kwa ajili ya kupata mazao mengi lakini yenye ubora ambayo yataweza kuuzika kwa faida na hivyo kuongeza mchango wa pato la Taifa.

Ushauri huo umetolewa na Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki wakati wa hafla ya kukabidhi malori na vifaa vya maziwa kutoka shirika la Heifer International kupitia mradi wa usindikaji maziwa Tanzania (TMPP) iliyofanyika katika kiwanda cha Tanga Fresh kilichopo Jijini Tanga.

Alisema kuwa licha ya Tanzania kuwa na mifugo mingi lakini sekta hiyo mchango wake kwenye pato la taifa ni asilimia 7.9% pekee  kutokana na ufugaji wa kimazoea  ambao hautoi matokeo bora.

Akizungumzia uzalishaji wa maziwa nchini Waziri Ndaki alisema ni lita Bil 3.01 huku kati ya hizo lita Mil 2.1 zinatokana na ng'ombe wa asili Mil 31 huku ng'ombe wa kisasa Mil 2 wanatoa lita bil 0.9. 

"Kutokana na uzalishaji mdogo wa maziwa hata kiwango cha unywaji wa maziwa kwa mwananchi mmoja mmoja kimekuwa kidogo kwani kwa mujibu wa takwimu ni lita 54 kwa mwaka sawa na kijiko kimoja kwa siku" alisema Waziri Ndaki.

Nae Kaimu Msajili bodi ya maziwa Noely Byamungu alisema kuwa uwepo wa mradi umesaidia kuongeza kasi ys uanzishwaji wa viwanda vya maziwa hadi kufikia vitano ambavyo vinazalisha maziwa kwa kutumia teknolojia ya UHT.

Alisema kuwa bado kumekuwepo na changamoto katika eneo la ukusanyaji wa maziwa kwani kuna kiasi kikubwa yanakuwa hana kosa ubora kabla ya kufika soko hivyo kuwa hasara kwa mfugaji.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uzalishaji na masoko kutoka wizara ya mifugo na uvuvi Steven  Maiko alisema kuwa kutokana na tathimini waliyoifanya 2016/17 inaonyesha kuwa ifikapo mwala 2030/31 sekts hiyo itakabiliwa na upungufu mkubwa raslimali zake za nyama na maziwa kutokana na ongezeko la idadi ya watu.

Hivyo kutokana na changamoto hiyo serikali kwa kushirikiana na wahisani waliamua kuja na mradi huo ili  kuongezs uzalishaji, kudhibiti magonjwa ya mifugo lakini.na kuongeza mnyororo wa thamani wa maziwa ikiwemo kuweka mazingira safi ya kufanyabiashara.

Nae  Mkurugenzi wa mradi wa usindikaji wa maziwa Tanzania kutoka shirika la Helfer Mark Tsoxo alisema kuwa lengo la mradi wa TMPP kuongeza kipato kwa wafugaji wapatao 50, 000 nchi nzima na kwa kipindi cha miezi mitatu pekee tayari wameweza kuwafikia wafugaji 45, 000 kwa kuwapa mafunzo ya ufugaji wa kisasa ili waweze kupata mazao bora na ambayo yataweza kuuza kwa urahisi.

Alisema kwa upande wa wasindikaji waweze kuwawezesha vifaa ili kuhakikisha wanaboresha ukusanyaji wa maziwa na kudhibiti ubotevu wake ili kumuhakikishia mfugaji  soko lenye uhakika.

Nae Meneja wa Kanda ya Mashariki Benki ya Maendeleo ya kilimo TADB Jeremiah Mhada alisema kuwa benki hiyo imewawezesha wafugaji mkopo wa zaidi ya sh Mil 396 pamoja na mitamba bora.

"Ili kuongeza kipato kwa wafugaji wadogo tumewawezesha kupata mitamba ya kisasa na kiwaunganisha ns masoko ili kuongeza thamani na kuchoches kuongeza uzalishaji wa maziwa nchini" alisema Mhada.


Share:

RAIS MAGUFULI AZINDUA MRADI WA MAJI TABORA NA UJENZI WA JENGO LA WAGONJWA WA HUDUMA YA DHARURA HOSPITALI YA KITETE


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na viongozi wengine wakati akizindua mradi mkubwa wa Maji ya Ziwa Victoria utakohudumia miji ya Tabora, Igunga na Nzega. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na viongozi wengine mara baada ya kuzindua mradi mkubwa wa Maji ya Ziwa Victoria utakaohudumia miji ya Tabora, Igunga na Nzega.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maji Jumaa Aweso pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga wakati akikagua ujenzi wa Matanki makubwa ya kuhifadhia maji katika mradi mkubwa wa maji ya Ziwa Victoria katika miji ya Tabora, Igunga na Nzega.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga wakati akikagua ujenzi wa Matanki makubwa ya kuhifadhia maji katika mradi mkubwa wa maji ya Ziwa Victoria katika miji ya Tabora, Igunga na Nzega
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga wakati akikagua ujenzi wa Matanki makubwa ya kuhifadhia maji katika mradi mkubwa wa maji ya Ziwa Victoria katika miji ya Tabora, Igunga na Nzega


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri wa Maji Jumaa Aweso wakati akitoka kukagua ujenzi wa Matanki makubwa ya kuhifadhia maji katika mradi mkubwa wa maji ya Ziwa Victoria katika miji ya Tabora, Igunga na Nzega
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Afya Dkt. Dorothy Gwajima, Mawaziri pamoja na viongozi wengine wakati akiweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la Idara ya Wagonjwa wa Huduma ya Dharura katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora leo tarehe 30 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na viongozi wengine mara baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la Idara ya Wagonjwa wa Hudumaya Dharurakatika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora leo tarehe 30 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na WatotoDkt. Dorothy Gwajima wakati akitoa taarifa ya ujenzi wa jengo la Idara ya Wagonjwa wa Huduma ya Dharurakatika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora leo tarehe 30 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Waziri wa Afya Dkt. Dorothy Gwajima pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Mabula Mchembe mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Idara ya Wagonjwa wa Huduma ya Dharurakatika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora leo tarehe 30 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akitoka kukagua ujenzi wa jengo la Huduma ya Wagonjwa wa Dharura katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora leo tarehe 30 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa mkoa wa Tabora katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora leo tarehe 30 Januari 2021 mara baada ya kuzindua mradi wa maji ya kutoka ziwa Victoria pamoja na jengo la huduma kwa wagonjwa wa dharura.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na wananchi wa Tabora mara baada ya kuwahutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora leo tarehe 30 Januari 2021 mara baada ya kuzindua mradi wa maji pamoja na jengo la huduma kwa wagonjwa wa dharura.
Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi Tabora wakifurahia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufulialipopita kuwaaga mara baada ya kuhutubia wananchikatika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora leo tarehe 30 Januari 2021
Kwaya ya Chuo cha Utumishi Tabora wakiimba Wimbo maalumu mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuwasili katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora leo tarehe 30 Januari 2021 mara baada ya kuzindua mradi wa maji pamoja na jengo la huduma kwa wagonjwa wa dharura.
Kwaya ya Chuo cha Utumishi Tabora wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akihutubia katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora leo tarehe 30 Januari 2021 mara baada ya kuzindua mradi wa maji pamoja na jengo la huduma kwa wagonjwa wa dharura.

PICHA NA IKULU

Soma pia : 

RAIS MAGUFULI AZINDUA MRADI WA MAJI ISAKA- KAGONGWA ...AMPONGEZA AWESO KUFUKUZA WAKANDARASI FEKI



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger