Thursday 31 October 2019

Bashe:Serikali Imeamua Kuheshimu Na Kuweka Kipaumbele Sekta Ya Kilimo

Na.Faustine Galafoni,Dodoma.
NAIBU Waziri wa Kilimo,Husein Bashe amesema Serikali imeamua kuheshimu na kutoa kipaumbele mazao ya kilimo kama sekta zingine zinavyothaminiwa kwa kujenga miundo mbinu rafiki kwa mkulima hususani pembejeo bora.

Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa kwenye mkutano wa kitaifa wa wakulima wadogo Tanzania uliofanyika jijini Dodoma kujadili changamoto wanazokumbana nazo ulioandaliwa na Shirika la ANSAF.

Waziri Bashe amesema kuwa sekta ya kilimo imekuwa msaada katika kuinua uchumi wa nchi kutokana na kaya ,jamii kwa ujumla kutumia malighafi nyingi zinazotokana na kilimo mbali na changamoto zinazowakabili wakulima .

Amebainisha tarari serikali imeweka mikakati ya kuboresha miundo mbinu kwa wakulima wadogo katika suala zima la kuongeza maafisa ugani vijijini huku wakishirikana na maafsa watendaji kutembelea wakulima,pembejeo zilizo bora na bei rahisi,upatikanaji wa mbegu nzuri,sheria ya kulinda wakulima,kuwapatia Bima ya mazao ,pamoja na kuongea na taasisi za kifedha kupata mikopo yenye riba nafuu jambo ambalo litasaidia kuleta maendeleo.

"Kama Wizara itaendelea kutangaza  na kuhamasisha wakulima wadogo kuboresha miundo mbinu ili kuwe na kilimo chenye tija  kwani wamekuwa wachangiaji wazuri uchumi wa nchi na jamii imategemea chakula kutoka kwa wakulima wadogo"alisema Waziri Bashe.

Hata hivyo amepiga marufuku kwa viongozi wa Ushirika ambao sio wakulima kuongoza wakulima kutokana na malalamiko yanayotolewa ambapo wao kazi kubwa ni kujinufaisha badala ya kuwasaidia wakulima hao.
"Kuanzia leo kiongozi ambaye sio mkulima hapaswi kuongoza wakulima haiwezekani wewe sio dhehebu ya kiislamu halafu eti uwaongoze waislamu"amesema.

Mbali na hayo amesema wizara imeanzisha Dawati la masoko ambalo litashughulikia wakulima ambao ufanyiwa ukiritimba na TBS huku akisema kutakuwa na huduma bure ya mawasiliano ambayo itawala fursa wakulima kupiga simu kueleza changamoto zao na kutatuliwa hapo hapo.

Nae mwenyekiti kamati ya Bunge kilimo,mifugo na maji Mahamoud Mgimwa amesema wabunge wako tayari kuendelea kuwatetea wakulima ili serikali iweze kutatua changamoto zao lengo ni kufikia asilimia kumi .

Kwa upande wake  Mwenyekiti jukwaa la wakulima wadogo wanawake ,Janeth Nyamayahasi amesema wanakumbana na changamoto ya upungufu wa maafisa ugani vijijini kwenye sekta ya mifugo,kilimo na uvuvi na kwamba baadhi ya wataalamu hao hawatoi ushirikiano na mara utoa ushauri mbovu unaopelekea mazao yao kuharibika.


Share:

Waziri Mkuu Majaliwa Atarajiwa Kuwa Mgeni Rasmi Wiki Ya Azaki.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika wiki ya asasi za Kiraia Tanzania  [AZAKI]itakayofanyika jijini Dodoma kuanzia Novemba 4-8,2019.
 
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma leo Oktoba 31,2019,Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Foundation for Civil Society  [FCS]BW.Francis Kimwanga amesema wiki ya asasi za kiraia nchini itakutanisha zaidi ya asasi za kiraia 500 kutoka nchi nzima Tanzania bara na visiwani Zanzibar.

Mkurugenzi mtendaji huyo wa  FCS]  amefafanua kuwa Wiki ya Asasi za Kiraia [AZAKI]itajumuiya Maonesho  ya kazi mbalimbali zinazofanywa na asasi hizo huku lengo likiwa ni kuimarisha ubia kati ya asasi za kiraia na wadau mbalimbali  katika kutimiza azma ya kuiletea Tanzania Maendeleo.
 
"Lengo la kongamano hilo nikuimarisha ubia kati ya asasi za kiraia na wadau mbalimbali katika juhudi za kutimiza azma ya kuileteaTanzanaia maendeleo," amesema .

Hata hivyo amesema "Kupitia  kongamano  hili asasi  za  kiraia  zitafanya majadilianao juu ya kazi  zao, kubadilishana uzoefu na kuona ni jinsi ambavyo zinaweza kushirikiana wenyewe kwa wenyewe na wananchi, serikali, bunge, wabia  wa  Maendeleo na sekta binafsi," amesema.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti  maalum mkoa  wa Dodoma  Fatma Taufiq ambaye  pia  ni  Mkurugenzi wa shirika  la  WOWAP  amesema wiki hiyo  ni  Wiki  ya kipekee  kwa  mwaka  huu washiriki  mbalimbali  wanatarajiwa kuwepo bila  kuwasahau viongozi  wakubwa kutoka serikalini huku pia akitoa rai kwa vyombo vya Habari kuhabarisha jamii umuhimu wa makundi maalum katika jamii.
 
“Asasi za kiraia zimekuwa na mchango mkubwa katika jamii,AZAKI inatekeleza Malengo 17 ya maendeleo endelevu hivyo nitoe rai kwa asasi ambazo zimekuwa zikienda kinyume na matakwa ya serikali na asasi sio adui zinashirikiana  na serikali .Pia nitoe rai kwa Vyombo vya Habari kuhabarisha umma juu ya Umuhimu wa Asasi hizi.amesema.

Hata hivyo  aliwataka  wananchi  wote kufika  katika viwanja  vya Jamhuri Novemba 4 Hadi 8 ili  kuweza  kuona  na  kujifunza  asasi  za  kiraia zinafanyaje  kazi zao n'a kuachana na  kusikiliza  habari  potofu kuwa  asasi za kiraia zinakula  hela na hazileti Maendeleo yoyote huo ni upotoshaji.

Msajili wa  asasi za kiraia kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,jinsia Wazee na Watoto,Charles Komba amesema asasi za kiraia zimekuwa chachu kubwa ya Maendeleo  na katika kuisaidia serikali.
 
“Asasi za kiraia ni Wadau wetu,ni wadau  wetu wakubwa   sana katika maendeleo ya kijamii,serikali haiwezi kufanya kwa kila jambo lakini sasi za kiraia zmekuwa mstari wa mbele kutusaidia.
 
Aidha,ameongeza kwa kusema ,Mpaka  mwaka 2017 serikali ilishasajili asasi za kiraia zaidi ya 10,000.

Mkurugenzi Mtendaji wa  Taasisi ya Haki,Rasilimali ,Mafuta ,Madini na gesi Rachel Chaganda amesema  taasisi hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kufanya tafiti mbalimbali zinazohusiana na madini,Mafuta na gesi ambapo ni mchango mkubwa kwa serikali  Ya Tanzania.

Naye mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Ulemavu Tanzania[SHIVYAWATA] Ummy Nderiananga amesema katika wiki hiyo ya AZAKI,Kutakuwa na elimu pamoja na miradi mbalimbali  inayofanywa na watu wenye ulemavu huku afisa Uhusiano wa kituo cha sheria na Haki za Binadamu,Legal Human Rights   Centre[LHRC] Michael Malya akisema katika wiki hiyo kituo hicho kitajihusisha na utoaji wa huduma za kisheria.
 
Ikumbukwe kuwa FCS itatoa tuzo za Umahiri wa asasi za kiraia  ili kusheherekea na kutambua ufanisi na michango   za taasisi na watu binafisi  katika uchocheaji na uimarishaji wa sera ya maendeleo ya nchi.
 
Zaidi ya asasi za kiraia 15  zikishirikiana na FCS   Kuandaa wiki ya AZAKI ni LHRC,LSF,Save the children, Wajibu Institute,UN Women,Oxfam,Twaweza,Policy Forum,msichana Initiative,Hakirasilimali, UNA Tanzania, Acountability Tanzania,Sikika,TLS,SHIVYAWATA,na TANGO.
Kaulimbiu  wiki  ya asasi za Kiraia [AZAKI] Mwaka ,2019 ni ubia kwa Maendeleo ,Ushirikiano kama chachu ya Maendeleo.







Share:

Watu 70 wafariki Pakistan kufuatia moto kwenye treni

Watu wasiopungua 70 wameuwawa na dazeni kadhaa kujeruhiwa baada ya jiko la gesi kuripuka ndani ya treni iliyokuwa ikiwasafirisha waumini waliokuwa njiani kwenda kufanya ziara ya kidini nchini Pakistan.

Picha za televisheni zinaonyesha moto unaofuka ndani ya mabehewa matatu ya treni huku vilio vikisikia ndani ya treni hiyo katika eneo la vijijini la mkoa wa kati wa Punjab.

Baadhi ya abiria-wengi wao wakiwa waumini waliokuwa njiani kwenda katika ziara ya kidini katika mji wa mashariki wa Lahore, walikuwa wakipika chakula cha asubuhi pale majiko yao mawili ya gesi yaliporipuka-Ali Nawaz, afisa wa ngazi ya juu wa shirika la safari za reli la Pakistan ameliambia shirika la habari la Ufaransa AFP.

Wapakistan wengi wanabeba vyakula wanapokuwa katika safari ndefu lakini majiko ya gesi yamepigwa marufuku. Ali Nawaz anasema uchunguzi unafanywa kuhusu ajali hiyo.

Televisaheni za Pakistan zimeonyesha jinsi dazeni za watu walivyokusanyika njiani kuangalia jinsi moto unavyofuka ndani ya mabehewa  ambayo yaliachana na sehemu nyengine ya treni.

Waziri Mkuu Imran Khan ameamuru uchunguzi juu yakisa hicho kufanywa mara  moja
 
Vikosi vya  zimamoto vimefika haraka katika eneo hilo karibu na wilaya ya Rahim Yar Khan. Watumishi wa mashirika ya uokozi na wanajeshi pia wameonekana wakisaidia. Miili ya wahanga wa ajali hiyo iliyofunikwa shuka nyeupe imekuwa ikiondolewa.
 
-DW

Share:

TIGO YAINGIZA SOKONI ‘KITOCHI 4G SMART’ ’ YENYE UWEZO WA 4G KWA BEI NAFUU

Share:

TRENI YASHIKA MOTO NA KUUA WATU 65

Takriban abiria 65 wamefariki dunia wakati treni iliyokuwa ikisafiri kutoka mji wa Karachi Pakistan kuelekea Rawalpindi iliposhika moto.

Waziri wa reli, Sheikh Ahmed, alisema kwamba moto huo ulisababishwa na kulipuka kwa mtungi wa gesi uliokuwa ukitumiwa na abiria kupikia kiamsha kinywa mwendo wa asubuhi.

Moto huo unadaiwa kusambaa hadi katika mabehewa matatu, kulingana na maafisa walionukuliwa katika vyombo vya habari vya eneo hilo.

Waathiriwa wengi walifariki walipojaribu kuruka kutoka kwa treni hiyo iliokuwa ikichomeka.

Watu wengine 30 wameripotiwa kujeruhiwa na maafisa wanasema kwamba idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka.

"Majiko mawili aina ya stove yalilipuka. Walikuwa wakipika , walikuwa na mafuta ya kupikia ambayo yalichochea moto huo kuongezeka'', Sheikh Rashid Ahmed alisema.

Abiria wanaoingia na stove katika treni ili kupika chakula wakati wa safari ndefu ni swala la kawaida waziri huyo aliongezea.

Aliongezea kwamba abiria wengi walikuwa wakielekea katika kongamano lililoandaliwa na vuguvu la dhehebu la Kisuni Tablighi Jamaat.

Ajali hiyo ilitokea karibu na Rahim Yar Khan kusini mwa mkoa wa Punjab. Treni hiyo iliokuwa ikisafiri kutoka Karachi kupitia maeneo mengi ya Pakistan hadi Rawalpindi inaitwa Tezgam mojawapo ya treni za zamani ambayo ni maarufu sana.

Inahudumu kila siku na inachukua saa 25 na nusu.

Pakistan ina historia ya ajali za gari moshi zinazosababisha maafa mengi. Waathiriwa huwa wengi kwa kuwa treni hizo hubeba watu wengi zaidi ya viwango vyao.

Tarehe 11 mwezi Julai , watu walifariki katika ajali , huku wengine wanne wakifariki katika ajali nyengine mwezi Septemba.

Mwaka 2007, takriban watu 56 waliuawa na wengine zaidi ya 120 kujeruhiwa katika ajali karibu na eneo la Mehrabpur.

Mwaka 2005, zaidi ya watu 130 waliuawa wakati treni tatu zilipogongana katika mkoa wa Sindh katika kile kilichotajwa kuwa ajali mbaya zaidi inayohusisha treni kuwahi kutokea.
CHANZO - BBC
Share:

Job Opportunity at Coca Cola – Kwanza Limited, Warehouse Team Leader

WAREHOUSE TEAM LEADER (CCB191030-8) Closing date: 2019/11/12 Job Title WAREHOUSE TEAM LEADER Function Logistics, Warehouse & Distribution Company: Coca-Cola Kwanza (Tanzania) Job Type Permanent Location – Country Tanzania Location – Province Not Applicable Location – Town / City Dar es Salaam Job Description  Coca-Cola Kwanza Ltd has an exciting opportunity in Logistics Department. We are looking for a… Read More »

The post Job Opportunity at Coca Cola – Kwanza Limited, Warehouse Team Leader appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Business Performance Lead Job at Diageo Tanzania

Position: Business Performance Lead Location: Dar es Salaam, Tanzania Job Description : Are you looking to grow and develop as your role rapidly increases the value it brings to the organization? The finance functions within Diageo both at the headquarters and in markets has a mission to be great business partners driving great business performance‟. As business partners,… Read More »

The post Business Performance Lead Job at Diageo Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MWANAFUNZI APIGWA VIBOKO MPAKA KUFA DARASANI

Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 14 huko nchini Burundi amefariki baada ya kupigwa na mwalimu wake, baba wa mtoto huyo ameiambia BBC.

Mtoto huyo, Chadia Nishimwe alipigwa viboko kwenye maeneo ya shingo na miguuni , kipigo ambacho kilimpelekea kutokwa damu puani na masikioni, alisema Jean-Marie Misago.

"Alikufa darasani mara baada ya kupigwa na mwalimu wake, na wakaenda kumtelekeza katika ofisi ya mwalimu mkuu," Bwana Misago alisema.

Mkuu wa shule alijaribu kumuwahisha hospitalini mtoto huyo wakati mtoto ameshakufa tayari, aliongeza baba huyo.

BBC imejaribu kutafuta taarifa zaidi katika sekta ya elimu bila mafanikio.

Mtoto huyo aliuwawa siku ya jumanne na kuzikwa siku hiyo hiyo .

Nchini Burundi, adhabu ya kuchapwa kwa mwanafunzi ni kinyume na sheria ingawa bado wanafunzi wanachapwa.
Chanzo - BBC
Share:

WANANCHI KIWALANI WAIPONGEZA SERIKALI KUWAJENGEA SOKO KUBWA...DC MJEMA ASISITIZA UBORA

Share:

DC MJEMA ATAKA WAFANYABIASHARA WALIOHAMA KATIKA VIZIMBA SOKO LA BUGURUNI NA KUFANYA BIASHARA NJE YA SOKO WARUDI MARA MOJA


Mkuu wa Wilaya  ya Ilala Mhe. Sophia Mjema amewataka wafanyabiashara wa soko la Buguruni waliohama katika vizimba na kufanya biashara nje ya soko kwa kigezo cha kuwa na Kitambulisho cha Ujasiriamali warudi mara moja.

Agizo hilo amelitoa Oktoba 30/2019 katika ziara yale kufuatia malalamiko ya baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo ambapo amesema wale watakaokaidi watachukuliwa hatua za kisheria.

Aidha katika kuona suala hilo linafanyiwa kazi, amemuagiza Afisa masoko,Ally Baruani , kufanya kikao na wafanyabiashara hao mara baada ya ziara kumalizika ili kuwarudisha ndani ya soko kwani kitendo hicho kinainyima Manispaa mapato. 

Mkuu huyo wa wilaya amesema soko hilo lipo kwa ajili ya manufaa ya wafanyabiashara wote na sio kwa watu wachache.

"Kwa hili sitowasamehe, mnawaumiza wenzenu, kwaninni mkwepe ushuru wakati wenzenu wanalipa, nataka mrudi haraka na wasiotaka tunawachukulia hatua, " amesema Mjema.

Aidha amesema kutumia vitambulisho vya Mjasiriamali ni kosa kubwa kwani mfanyabiashara yeyote anayefanya sokoni kwa kupangiwa kizimba anapaswa kulipa ushuru kwa mujibu wa sheria za soko na utaratibu, kwani kutofanya hivyo kunaikosesha serikali mapato.

Amesema anatambua wote wafanya biashara lakini kila mfanyabiashara anatambulika kwa mujibu wa sheria na kanuni , hivyo wanaostahili vitambulisho vya Mjasiriamali na mlipa ushuru sifa zao zinatofautiana.

Mbali na wakwepa ushuru amewataka madalali wa biashara waache kuwakandamiza wafanyabiashara badala yake watumie mikataba katika makabidhiano yao ya kibiashara.

Aidha amesema wale madalali watakaoonekana wanakiuka Sheria wataondolewa katika soko hilo.

Kwa upande wa Mkurugenzi Manispaa ya Ilala Mhe. Jumanne Shauri, ameshauri kuwepo kwa mikataba maalumu ya kisheria kati ya mfanyabiashara na dalali ili kila mmoja kuweza kunufaika

Share:

Job Opportunities at Pathfinder International (Director – Monitoring, Evaluation and Learning)

Job Opportunities at Pathfinder International (Director – Monitoring, Evaluation and Learning) Job Title: Director – Monitoring, Evaluation and Learning Location: Dar es salaam Job Summary Pathfinder Overview: Pathfinder International is a global leader in sexual and reproductive health. We place reproductive health care at the center of all that we do—believing that it is not only a fundamental… Read More »

The post Job Opportunities at Pathfinder International (Director – Monitoring, Evaluation and Learning) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Jinsi Ya Kuandika CV Nzuri Ambayo Itamvutia Mwajiri na Kukufanya Upate KAZI Kirahisi

WATU wengi nchini wamekosa ajira  kwa sababu ya makosa wanayoyafanya wakati wa kuandika CV zao.

Kumbuka,  makampuni  karibia yote yanayotangaza nafasi za kazi hupokea wastani wa maombi 200-500 ya kazi kwa tangazo moja la kazi. 

Hivyo, CV yako lazima ikae vizuri ili kumshawishi mwajiri. Utaratibu wa kuomba kazi unaweza ukawa tofauti kati ya makampuni na mashirika, ila yote yatahitaji uwatumie CV.

CV ni nini?
CV ni maelezo ya ujumla kwa kiundani ya historia yako ya kazi na shule. Kawaida, inatumika kwenye maombi ya kazi ya nafasi za kati, za juu na za utafiti.

Mambo yafuatayo yatasaidia kuifanya CV yako iwe bora na hivyo, kukusaidia kupata interview za kazi.

👉Soma na kuelewa maelezo ya kazi
Una ujuzi gani? Mwajiri anatafuta mfanyakazi wa aina gani? Maswali haya ni muhimu kujua kama utaiweza hiyo kazi au la. Pia, ni vizuri kujua nini hasa ni muhimu kwa muajiri na kufanya maombi yako yaendane zaidi na mahitaji ya mwajiri.

Kwa mfano, kama kazi inaweka umuhimu kwenye ujuzi wa kutumia mitandao ya kijamii kwa matangazo, hakikisha CV yako ina kazi zote zilizohitaji matumizi ya mitandao ya kijamii.

👉Andika maneno muhimu yaliyotumika kwenye maelezo ya kazi, uyatumie kwenye CV
Usichukue sentensi nzima kutoka kwenye maelezo ya kazi na ukaitumia vile vile kwenye CV yako. Ila, tumia lugha na baadhi ya maneno yaliyotumika kwenye CV.

👉Fanya utafiti juu ya kampuni iliyotangaza kazi
Pamoja na kuchambua maelezo ya kazi, ni muhimu kufanya utafiti juu ya kampuni yenyewe. Kama wana tovuti au wapo kwenye mitandao ya kijamii, jaribu kujua ni kazi gani na sekta ipi wanayohusika nayo. 

Pia, ikiwezekana jaribu kuwajua wafanyakazi/meneja wa kampuni hiyo. Hii itakusaidia kujua maadili na muelekeo wa kampuni. Hii itakusaidia kuweka maombi yako ya kazi yaendane na kampuni hiyo.

👉Orodhesha ujuzi wako wakufanya kazi
Hapa, usiweke kazi zote ulizozifanya maishani mwako ila, weka zile ambazo zilikuongezea ujuzi utakayo kusaidia kufanya kazi unayoomba.

==>Format/Staili inayotumika zaidi kwenye kuandika CV:
   1. Lengo la CV na ujuzi wako
    2.Ujuzi wako wa kazi
   3. Mafanikio maalum
   4. Elimu
   5. Ujuzi muhimu binafsi

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬
Angalizo:
  1.  Tumia maandishi ya kawaida ya Times New Roman
  2.  Tumia size 9 – 12 ya herufi
  3.   Hakikisha unatumia staili moja ya kuandaa CV kote
  4.   CV isiwe zaidi ya ukursasa 2
  5.   Usitumie sentensi ndefu
  6.  Hakikisha CV yako inasomeka kiurahisi na inawasilisha   mafanikio yako kwa uwazi.
  7.  Anza na kazi yako ya sasa hivi au ya hivi karibuni alafu rudi nyuma.
   ▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 
   ==>.Hakikisha Yafuatayo:
1.Ukiwa unaandika jina la kampuni uliyo fanya kazi, andika jina la kampuni kikamilifu. 
2.Eleza kwa ufupi kampuni yao inahusika na nini. 
3.Tatu, weka muda uliyofanyakazi hapo (mwezi na mwaka).  
4.Baada ya hapo, orodhesha kazi na majukumu yako kwenye hiyo kampuni.
5.Usidanganye

👉Maandalizi ya Mwisho

1.Pitia kila kitu kwa mara ya mwisho
 -Print CV yako alafu ipitie. Hii huwa inasaidia kuona makosa yako.

2.Mpe Rafiki  yako apitie CV
-Muombe rafiki yako apitie CV yako. Macho manne ni bora zaidi ya mawili!

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

Hatua ya kwanza kwenye kupata kazi unayotaka ni kutuma maombi. Tunatumaini kwamba maelezo yaliyoelezwa humu yatakusaidia kuandaa CV bora kwa ajili ya mwajiri.

👉Sasa, kwa kuwa umeshajua jinsi ya kuandika CV nzuri, anza kutafuta kazi unayoitaka kwa kubofya hapo chini.

AU 



Share:

Nafasi za kazi 2019 – Nafasi za ajira zilizotangazwa Leo- Jobs in Tanzania

Browse all latest Jobs Today  in Tanzania:  Here is the list of new jobs advertised in Tanzania, Apply Now!! JOB ADVERTISEMENTS FROM GOVERNMENT, TANZANIA NGOs AND INTERNATIONAL NGOs Tanzania Jobs in October (30-31), 2019 Job Opportunity at ETDCO Limited – Transport Officer Job Opportunity at Sense of Africa, HR Executive Jobs Opportunities at Simba Logistics Limited Ltd (SLL)… Read More »

The post Nafasi za kazi 2019 – Nafasi za ajira zilizotangazwa Leo- Jobs in Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at ETDCO Limited – Transport Officer

Background – ETDCO M/S Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Company (ETDCO) Limited) is a Subsidiary Company of TANESCO Limited established with the Objective of providing reliable electrical services for the TANESCO Transmission and Distribution Infrastructure countrywide and construction of new infrastructure for TANESCO and other companies within the country and beyond the borders. ETDCO Limited hereby… Read More »

The post Job Opportunity at ETDCO Limited – Transport Officer appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at Sense of Africa, HR Executive

Job Title: HR EXECUTIVE  Location: Arusha Job Summary Sense of Africa is a footprint brand of Tourvest Destination Management, a division of the Tourvest Integrated Group of Companies. Sense of Africa operates wholly owned offices in Kenya, Tanzania, Uganda, Namibia and Botswana. In keeping up with our current business needs, we are pleased to  announce the vacancy of… Read More »

The post Job Opportunity at Sense of Africa, HR Executive appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Waziri Mpina Atangaza Neema Kubwa Kwa Wafugaji

Na Mwandishi Wetu, Katavi
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua kampeni ya kitaifa ya uogeshaji mifugo nchini na kutangaza neema kubwa kwa wafugaji ambapo sasa ng’ombe mmoja ataogeshwa kwa shilingi 50 badala ya sh 500 huku Mbuzi na Kondoo wakiogeshwa kwa sh 10 kila mmoja.

Uamuzi huu wa Serikali utawawezesha kuokoa shilingi bilioni 19 ambazo wafugaji wangezitumia kuogesha mifugo yao lakini ambapo sasa itatumika shilingi bilioni 2.16 tu huku Serikali ikiwapatia wafugaji ruzuku ya asilimia 90 ambapo kama wafugaji wangeendelea na bei hiyo ya miaka ya nyuma wangelazimika kutumia sh bilioni 21.6.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa Kampeni ya uogeshaji mifugo awamu ya pili katika Josho la Kikonko wilayani Mlele na baadae mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Majimoto, Waziri Mpina alisema kupitia  mpango huo Serikali itasambaza dawa ya ruzuku lita 12, 546 kwenye majosho yanayofanya kazi 1,733 nchini kote.

Huku Mvua kubwa ikinyesha kwenye mkutano huo, Waziri Mpina alitumia zaidi ya saa moja kuhutubia huku akinyeshewa na mvua na kuwathibishia wananchi kuwa Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuleta mageuzi kwa vitendo hasa katika sekta ya mifugo.

Alisema Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 25 kipengele  inaiagiza Serikali kuhakikisha mifugo yote inaogeshwa ili kuweze kuzuia magonjwa yote yanayoenezwa na kupe ambapo asilimia 72 ya vifo vya mifugo vinasababishwa na kupe.

Hivyo uogeshaji huo utawezesha mifugo kujikinga na maradhi na vifo ambapo Serikali itaogesha michonyo milioni 38 kwa Ng’ombe, michonyo milioni 18 ya Mbuzi, michovyo milioni 7 ya Kondoo, na michovyo 2500 ya Punda hivyo utaliwezesha taifa  kupata mifugo bora ambayo haina magonjwa.

Waziri Mpina alibainisha kuwa katika kipindi kifupi cha mwaka mmoja Serikali imekarabati majosho 400 na kwamba majosho yaliyobaki ambayo  hayajakarabatiwa ni 639 na kusisitiza kuwa yote yatakarabatiwa ili kuongeza kasi ya uogeshaji mifugo.

Waziri Mpina alisisitiza kuwa zaidi ya asilimia 60 ya magonjwa ya binadamu yanasababishwa na mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa hivyo uamuzi wa Serikali kuogesha mifugo pia umelenga kupambana na magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

Hivyo juhudi hizo zinapaswa kuungwa mkono na watendaji wote wa Serikali, wafugaji wote ili kuboresha afya za mifugo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya mifugo ikiwemo nyama, maziwa na ngozi sambamba na kuwakinga wananchi na maradhi yanayoweza kuambizwa kutoka kwenye mifugo.

Kufuatia uzinduzi huo, Waziri Mpina ameagiza kila kijiji nchini kiwe na josho kwenye  vijiji vyote zaidi ya 12,000 ili kila kijiji kiweze kuogesha mifugo na kusisitiza kuwa Serikali ya Rais Magufuli itakuja na mkakati wa kuhakikisha kila kijiji kinapata josho kama sehemu ya kuboresha afya za mifugo.

Pia ameziagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha majosho yote yamekarabatiwa ndani ya mwezi mmoja na wizara itahakikisha inasambaza dawa kwenye majosho yote mabovu.

Aidha amesisitiza wanaokwenda kuogesha mifugo wafuate sheria za uogeshaji kuhakikisha mifugo inaogeshwa lakini kwa fedha ambayo Serikali imeitangaza ya sh 50 kwa kichwa na ng’ombe na sh 10 kwa kichwa cha mbuzi na zoezi hili litafanyika mfululizo kwa kipindi cha miezi 6 na kumuagiza  Mkurugenzi wa huduma za mifugo, Madaktari ya Mifugo wa Mikoa, na Wilaya kuhakikisha zoezi hilo linasimamiwa vizuri kuhakikisha wananchi hawatapeliwi

Pia Waziri Mpina ameweka wazi kuwa Serikali itatangaza bei elekezi ya chanjo ifikapo 15 Novemba mwaka huu na hakuna mtu mwingine atakayekwenda kuwaibia wafugaji tena na kwamba  chanjo ya homa ya mapafu ya ng’ombe itauzwa kwa sh 350 tofauti na siku za nyuma ambapo walichanja kwa sh 2000 kwa kichwa cha ng’ombe.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Komredi Juma Homera amemhakikishia Waziri Mpina kuwa Serikali ya mkoa huo inatasimamia maagizo yote na kwamba hakuna mfugaji atakayeonewa au kudhulumiwa na kwamba bei elekezi iliyotangazwa ya sh 50 kwa kichwa ngombe na 10 kwa mbuzi italeta neema kubwa kwa wafugaji.

Pia kuhusu malalamiko ya wafugaji kupigwa faini kubwa kuuawa kwa mifugo yao amemkabidhi nyaraka za malalamiko hayo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Katavi na kuwakamata watu wote waliotajwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Hezron Nonga amesema zoezi hilo la ugeshaji litafanyika nchi nzima na kuwataka wafugaji kujitokeza kuogesha mifugo yao ili kuikinga na maradhi.


Share:

Waziri Hasunga Awaasa Watumishi Wizara Ya Kilimo Kuwa Waadilifu

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Watumishi wa Wizara ya Kilimo wameaswa kuwa waadilifu na kuzingatia ubora wa kazi wakati wanatoa huduma kwa wananchi.

Mwito huo umetolewa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) jana tarehe 30 Octoba 2019 wakati akizungumza na watumishi Jijini Dodoma alipotembelea ofisi za wizara hiyo eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Mhe Hasunga amesema kuwa udilifu, nidhamu na weledi kwa watumishi wa umma ni kinga dhidi ya matumizi mabaya ya ofisi za umma na ni moja kati ya njia zinazowawezesha watumishi wa umma kuwa wachapakazi hodari.

“Kiwango cha juu cha Ubora wa kazi zetu na utendaji wa kazi unaozingatia weledi vitaweza tu kufikiwa kwa kuajiri watumishi wenye sifa stahiki, maadili, na bidii ya kuchapa kazi na wanaoweza kwenda sambamba na kasi kubwa ya mageuzi katika wizara ya kilimo,” Alisisitiza Mhe Hasunga

Alisema kuwa utekelezaji mzuri wa majukumu yao ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi yam  mwaka 2015-2020.

Amewataka watumishi hao kusimama imara katika kufanya kazi na kutumia weledi wao kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na kwamba uadilifu ndiyo silaha muhimu katika kufanya kazi ya Umma.

Amesema mtumishi atakayetumia vibaya rasilimali za serikali atahesabika adui namba moja wa Serikali na eneo analofanyia kazi huku akibainisha kuwa mtumishi wa aina hiyo kamwe hatohamishwa badala yake ataachishwa kazi.

Ziara ya waziri wa Kilimo kukutana na watumishi hao ilikuwa na lengo la kusalimiana na kusikiliza changamoto zinazowakabili katika utendaji kazi.


Share:

Watu Waliokutwa na tausi wa Ikulu wahukumiwa kulipa Milioni 6

Watu watatu wanaodaiwa kukutwa na ndege aina ya tausi wa Ikulu wamehukumiwa kulipa fidia zaidi ya Sh6.8 milioni baada ya kukutwa na hatia katika kesi ya uhujumu uchumi kwa kujihusisha na nyara za Serikali bila kibali.

Kadhalika mahakama hiyo imetaifishwa ndege hao kuwa mali ya serikali. Pia imewaachia huru kwa masharti ya kutokutenda kosa ndani ya miezi sita.

Hukumu hiyo ilisomwa jana na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salumu Ally, baada ya washtakiwa kumwandikia Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) barua ya kukiri makosa yao.

“Mahakama hii inawaamuru washtakiwa kulipa fidia ya Sh. 6,890,000, ndege hao wanataifishwa kuwa mali ya serikali na inawaachia huru kwa masharti kwamba wasitende kosa la jinai ndani ya miezi sita,” alisema Hakimu Ally wakati akisoma hukumu hiyo.

Awali, washtakiwa walidaiwa kujihusisha na genge la uhalifu, kukutwa na nyara za serikali ikiwamo ndege aina ya tausi watatu wa Ikulu ya Tanzania.

Washtakiwa hao ni David Graha, Mohammed Hatibu na Mohammed Mahamoud, wote wakazi wa jijini Dar es Salaam.

Washtakiwa hao walisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Vick Mwaikambo.

Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi, akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, alidai kuwa shtaka la kwanza, kati ya Juni Mosi, 2015 na Oktoba 14, mwaka huu waliratibu mipango ya uhalifu kwa kujihusisha na biashara ya ndege hao wenye thamani ya Dola za Marekani 1,500 (sawa na Sh. 3,444,150).

Nchimbi alidai katika shtaka la pili, washtakiwa walikutwa na ndege watatu aina ya tausi wenye thamani hiyo ya fedha.


Wankyo alidai katika shtaka la tatu, Oktoba 14, mwaka huu eneo la Mikocheni, mshtakiwa wa tatu Mahamoud alikutwa na tausi hao.
 


Share:

Jafo Atolea Ufafanuzi Malalamiko Yaliyowasilishwa Kwenye Zoezi La Uchukuaji Na Urejeshaji Wa Fomu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo ametolea maelekezo malalamiko yaliyowasilishwa na wadau wa uchaguzi kuwa zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea nafasi za uongozi uzingatie Kanuni za uchaguzi na miongozo iliyotolewa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jioni Ofisini kwake Mtumba Jafo ameelekeza Wasimamizi/Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi, Vyama vya Siasa na wadau wengine woote kuhakikisha kila mmoja kwa nafasi yake anazingatia masharti na miongozo iliyotolewa kuhusiana na uchukuaji na urejeshaji wa fomu.

Amebainisha baadhi ya malalamiko yaliyowasilishwa toka kwa vyama vya siasa kuwa ni kutokuwepo vituoni kwa baadhi ya wasimamizi wa uchaguzi, baadhi ya wasimamizi kutofungua kwa wakati vituo vya kuchukulia fomu, mihuri na masuala mengine ya Kikanuni.

“Malalamiko yaliyopokelewa yanaendelea kufanyiwa kazi, hata hivyo wadau na vyama vya siasa wanapaswa kuwasilisha malalamiko yao kwenye kamati za rufaa zilizopo katika maeneo ya uchaguzi,” alibainisha.


Akieleza maendeleo ya uchaguzi huo jana jijini hapa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo, alisema dosari zilizojitokeza ni chache kwenye baadhi ya mikoa.

Alisema katika Kata 3,959 ni kata 72 pekee ndizo amepokea malalamiko na kutaja maeneo machache kama vile Songwe, Lindi, Sengerema (Mwanza) na Moshi (Kilimanjaro).

Hata hivyo, Jafo alisema malalamiko kuhusu fomu zinazotolewa kwa wagombea kutogongwa muhuri, vyama vya siasa vinapaswa kufahamu kuwa, zitagongwa muhuri   pindi watakaporudisha au wakati wa uteuzi.

Kadhalika, alitoa msisitizo kwa wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi kuzingatia kanuni za uchaguzi kama zilivyowekwa.

Juzi, Waziri Jafo alitangaza wagombea kwenye uchaguzi huo kuanza kuchukua fomu kwenye ofisi za wasimamizi wa uchaguzi hadi Novemba nne mwaka huu.

Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti wa Mtaa, Kitongoji, Kijiji, Wajumbe wa Kamati ya  Mtaa, Waju,mbe wa Serikali ya Kijiji.

Uchaguzi huo ambao ni wa sita tangu kuanza mfumo wa vyama vya siasa nchini, unatarajiwa kufanyika Novemba 24 mwaka huu ambapo wapigakura zaidi ya milioni 19 wanatarajiwa kushiriki



Share:

SUA: BATCH 2 LOAN ALLOCATION FOR SUA STUDENTS (CONTINUING) WHO RECEIVE SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB IN THE ACADEMIC YEAR 2019-2020

SUA: BATCH 2 LOAN ALLOCATION FOR SUA STUDENTS (CONTINUING) WHO RECEIVE SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB IN THE ACADEMIC YEAR 2019-2020 Sokoine University of Agriculture was established on the 1st July, 1984 by parliamentary Act No.6 of the same year, which was repealed by the Universities Act No.7 of 2005 from which the SUA charter was granted in 2007… Read More »

The post SUA: BATCH 2 LOAN ALLOCATION FOR SUA STUDENTS (CONTINUING) WHO RECEIVE SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB IN THE ACADEMIC YEAR 2019-2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi October 31




Share:

WAZIRI MPINA ATANGAZA NEEMA KUBWA KWA WAFUGAJI UOGESHAJI WA MIFUGO

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akishirikiana na wafugaji kuingiza ng'ombe kwenye josho la Kijiji cha Kikonko wilayani Mlele mkoani Katavi wakati wa uzinduzi wa uogeshaji mifugo awamu ya pili na kutangaza ng'ombe mmoja sasa ataogeshwa kwa sh 50 tu badala ya sh 500 waliokuwa wanatozwa miaka ya nyuma.Picha na Mpiga Picha Wetu


Na Mwandishi Wetu, Katavi

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua kampeni ya kitaifa ya uogeshaji mifugo nchini na kutangaza neema kubwa kwa wafugaji ambapo sasa ng’ombe mmoja ataogeshwa kwa shilingi 50 badala ya sh 500 huku Mbuzi na Kondoo wakiogeshwa kwa sh 10 kila mmoja.

Uamuzi huu wa Serikali utawawezesha kuokoa shilingi bilioni 19 ambazo wafugaji wangezitumia kuogesha mifugo yao lakini ambapo sasa itatumika shilingi bilioni 2.16 tu huku Serikali ikiwapatia wafugaji ruzuku ya asilimia 90 ambapo kama wafugaji wangeendelea na bei hiyo ya miaka ya nyuma wangelazimika kutumia sh bilioni 21.6.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa Kampeni ya uogeshaji mifugo awamu ya pili katika Josho la Kikonko wilayani Mlele na baadae mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Majimoto, Waziri Mpina alisema kupitia  mpango huo Serikali itasambaza dawa ya ruzuku lita 12, 546 kwenye majosho yanayofanya kazi 1,733 nchini kote.

Huku Mvua kubwa ikinyesha kwenye mkutano huo, Waziri Mpina alitumia zaidi ya saa moja kuhutubia huku akinyeshewa na mvua na kuwathibishia wananchi kuwa Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuleta mageuzi kwa vitendo hasa katika sekta ya mifugo.

Alisema Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 25 kipengele  inaiagiza Serikali kuhakikisha mifugo yote inaogeshwa ili kuweze kuzuia magonjwa yote yanayoenezwa na kupe ambapo asilimia 72 ya vifo vya mifugo vinasababishwa na kupe.

Hivyo uogeshaji huo utawezesha mifugo kujikinga na maradhi na vifo ambapo Serikali itaogesha michonyo milioni 38 kwa Ng’ombe, michonyo milioni 18 ya Mbuzi, michovyo milioni 7 ya Kondoo, na michovyo 2500 ya Punda hivyo utaliwezesha taifa  kupata mifugo bora ambayo haina magonjwa.

Waziri Mpina alibainisha kuwa katika kipindi kifupi cha mwaka mmoja Serikali imekarabati majosho 400 na kwamba majosho yaliyobaki ambayo  hayajakarabatiwa ni 639 na kusisitiza kuwa yote yatakarabatiwa ili kuongeza kasi ya uogeshaji mifugo.

Waziri Mpina alisisitiza kuwa zaidi ya asilimia 60 ya magonjwa ya binadamu yanasababishwa na mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa hivyo uamuzi wa Serikali kuogesha mifugo pia umelenga kupambana na magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

Hivyo juhudi hizo zinapaswa kuungwa mkono na watendaji wote wa Serikali, wafugaji wote ili kuboresha afya za mifugo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya mifugo ikiwemo nyama, maziwa na ngozi sambamba na kuwakinga wananchi na maradhi yanayoweza kuambizwa kutoka kwenye mifugo.

Kufuatia uzinduzi huo, Waziri Mpina ameagiza kila kijiji nchini kiwe na josho kwenye  vijiji vyote zaidi ya 12,000 ili kila kijiji kiweze kuogesha mifugo na kusisitiza kuwa Serikali ya Rais Magufuli itakuja na mkakati wa kuhakikisha kila kijiji kinapata josho kama sehemu ya kuboresha afya za mifugo.

Pia ameziagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha majosho yote yamekarabatiwa ndani ya mwezi mmoja na wizara itahakikisha inasambaza dawa kwenye majosho yote mabovu.

Aidha amesisitiza wanaokwenda kuogesha mifugo wafuate sheria za uogeshaji kuhakikisha mifugo inaogeshwa lakini kwa fedha ambayo Serikali imeitangaza ya sh 50 kwa kichwa na ng’ombe na sh 10 kwa kichwa cha mbuzi na zoezi hili litafanyika mfululizo kwa kipindi cha miezi 6 na kumuagiza  Mkurugenzi wa huduma za mifugo, Madaktari ya Mifugo wa Mikoa, na Wilaya kuhakikisha zoezi hilo linasimamiwa vizuri kuhakikisha wananchi hawatapeliwi

Pia Waziri Mpina ameweka wazi kuwa Serikali itatangaza bei elekezi ya chanjo ifikapo 15 Novemba mwaka huu na hakuna mtu mwingine atakayekwenda kuwaibia wafugaji tena na kwamba  chanjo ya homa ya mapafu ya ng’ombe itauzwa kwa sh 350 tofauti na siku za nyuma ambapo walichanja kwa sh 2000 kwa kichwa cha ng’ombe.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Komredi Juma Homera amemhakikishia Waziri Mpina kuwa Serikali ya mkoa huo inatasimamia maagizo yote na kwamba hakuna mfugaji atakayeonewa au kudhulumiwa na kwamba bei elekezi iliyotangazwa ya sh 50 kwa kichwa ngombe na 10 kwa mbuzi italeta neema kubwa kwa wafugaji.

Pia kuhusu malalamiko ya wafugaji kupigwa faini kubwa kuuawa kwa mifugo yao amemkabidhi nyaraka za malalamiko hayo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Katavi na kuwakamata watu wote waliotajwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Hezron Nonga amesema zoezi hilo la ugeshaji litafanyika nchi nzima na kuwataka wafugaji kujitokeza kuogesha mifugo yao ili kuikinga na maradhi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger