Tuesday 29 October 2019

Wanawake Washauriwa Kujitokeza Na Kuogombea Nafasi Mbalimbali Za Uongozi

...
Wanawake Mkoani Kagera wametakiwa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajia kufanyika mnamo septemba 24 mwaka huu.
 
Hayo yamebainishwa na Mbunge wa viti maalumu kutoka Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mh Conchester Rwamulaza wakati akiongea na mpekuzi blog kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mapema mwaka huu.
 
Mh Conchester amesema kuwa wanawake wengi wamekuwa na hofu ya kutotaka kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na kuongeza kuwa wanayo nafasi kubwa yakuweza kugombea nafasi za uongozi kwa mwaka huu  kwa ajili ya maedeleo ya nchi kwa kuwa wana kauli mbiu ya wanawake wanaweza na kusema kuwa isiwe kauli ya maneno bali ata kwa vitendo.
 
Amesema kuwa ushindani wa mwaka huu ni mkubwa na watu wengi wana mwamuko wa kugombea kwa ajili ya maendeleo ya nchi na kuongeza kuwa uongozi unaanzia chini katika ngazi ya vitongoji na vijiji kwa kuwa viongozi hao wanakuwa karibu na wananchi.
 
Aidha Mh Conchester ameongeza kuwa wananchi wajitokeze  kwa wingi mnamo septemba 24 mwaka huu kuweza kupiga kura huku wakitambua umuhimu wa uchaguzi huo na akiwataka wananchi kutobeza uchaguzi huo kwa kuwa ni muhimu sana.
 
Pia mh Conshester amesema kuwa  ili jambo la wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali lifanikiwe inabidi akina baba kutowakataza wanawake  kugombea katika uchaguzi huo ili waweze kutimiza malengo yao.




Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger