Sunday 27 October 2019

MWANAJESHI AWAPIGA RISASI WANAJESHI WENZAKE 10..AUA WANANE

...
Mwanajeshi mmoja wa Urusi amewapiga risasi wanajeshi wenzake wanane na kuwajeruhi vibaya wengine wawili katika kambi ya kijeshi iliopo mashariki, kulingana na maafisa.

Ramil Shamsutdinov ambaye amekamatwa - huenda alikuwa akiugua tatizo la kiakili , wanasema.

Tukio hilo lilifanyika katika kitengo cha kijeshi nambari 54160 katika kijiji cha Gorny , sio mbali na mji wa Chita, siku ya Ijumaa jioni.

Uchunguzi wa mauaji hayo unaendelea.

Je ni nini kinachojulikana kuhusu shambulizi hilo?

Kisa hicho kilitokea mwendo wa saa kumi na mbili na robo , kulingana na kamati ya uchunguzi ya Urusi.

Wizara ya ulinzi mapema ilisema kwamba risasi zilifyatuliwa wakati wa kubadilishana zamu katika eneo la Transbaikal.

Bwana Shamsutdinov , kurutu, aliwaua maafisa wawili na wanajeshi wenzake sita.

Vyombo vya habari nchini Urusi vimeripoti kwamba mshukiwa huyo aliwalenga waathiriwa katika vichwa.
Tume maalum inayoongozwa na naibu waziri wa ulinzi Andrey Kartapolov inaelekea katika eneo hilo ili kuchunguza mauaji hayo.

Kitengo hicho cha jeshi nambari 54160 kinahifadhi makombora.

Kina makombora ya Iskander ambayo yana uwezo wa kubeba vichwa vya kinyuklia.

Huduma za jeshi ni lazima nchini Urusi kwa wanaume wote walio kati ya umri wa miaka 18-27.

Wao uhudumu kwa miezi 12 , na baadaye wanaweza kusaini kandarasi za kitaalam ili kuendelea kuhudumu katika jeshi.

Katika miaka ya 2000, makundi ya haki za kibinadamu yaliripoti ghasia na unyanyasaji kwa jina ''dedovshchina'' dhidi ya makurutu wapya katika jeshi la Urusi.

Lakini katika miaka ya hivi karibuni, Urusi inajivunia kuliimarisha jeshi lake na kuondoa unyanyasaji.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger