Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Thursday, 11 December 2025

WATUMISHI WA MAENDELEO YA JAMII TUWAJIBIKE – MHE.MARYPRISCA



Na Jackline Minja WMJJWM- Dodoma.

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amewataka watumishi wa Kituo cha Huduma kwa wateja kuwajibika kwa kuwahudumia wananchi na kutatua changamoto zao.

Mhe. Maryprisca ameyasema hayo leo tarehe 10 Desemba, 2025 alipotembelea kituo hicho ikiwa ni ziara ya kujifunza namna kinavyowahudumia wananchi.

Akizungumza mara baada ya kusikiliza maelezo ya watumishi hao, Naibu Waziri Maryprisca amekiri kuwa kituo hicho kinafanya kazi kubwa na yenye mchango mkubwa katika kuboresha utoaji wa taarifa na huduma kwa umma.

Aidha Mhe. Maryprisca ameahidi kufuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa majukumu katika ngazi zote, ikiwemo kutoa maelekezo mahsusi kwa halmashauri na idara zinazohusika ili kuhakikisha taarifa kutoka katika kituo cha huduma kwa wateja zinashughulikiwa kwa wakati na kuimarishwa kwa utoaji wa elimu kwa umma kuhusu majukumu ya Wizara na namna ya kutoa malalamiko ili kupunguza mkanganyiko unaojitokeza.

Ziara hiyo ya Naibu Waziri Maryprisca inalenga kuboresha mifumo ya uwajibikaji, kuongeza ufanisi wa huduma na kuhakikisha sauti za wananchi zinapokelewa na kufanyiwa kazi kwa uharaka na weledi unaostahili.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI DESEMBA 11,2025

Magazeti

 


Share:

Wednesday, 10 December 2025

POLISI YAONYA WANAOENDELEA KUHAMASISHA MAANDAMANO



Na Mwandishi wetu, Dodoma

Jeshi la Polisi nchini Tanzania kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama nchini wamewahakikishia wananchi kuwa wataendelea kulinda usalama wa Tanzania sambamba na maisha na mali za wananchi ili waweze kuendelea na shughuli zao kwa amani, utulivu na usalama.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime leo Disemba 10, 2025, limeonya pia kuhusu wanaopanga kujitokeza leo kwenye Mitaa mbalimbali ili kufanya kile kinachoitwa maandamano ya amani kutokana na kushindwa kuyafanya jana Oktoba 29, 2025.

"Jeshi la Polisi linaendelea kuwakumbusha, kuwasisitiza na kuwaonya wasifanye hivyo kwani wanachokiita maandamano ya amani yasiyo na kikomo yalipigwa marufuku kutokana na kukosa sifa kulingana na matakwa ya Katiba na sheria ya Polisi na Polisi wasaidizi sura 322." Amesema Misime.

Polisi pia imeeleza kuwa kwa ambaye atakaidi kutii sheria za nchi kwa lengo la kuhatarisha usalama wa nchi ili kusimamisha shughuli za kiuchumi na kijamii zisiendelee, watadhibitiwa ili nchi ibaki salama na watanzania wema na wapenda amani wabaki salama.

Aidha Taarifa ya Polisi imetoa wito pia kwa wananchi kuendelea kufanya shughuli zao na kufuata maelekezo watakayokuwa wanapewa na Vyombo vya ulinzi na usalama katika maeneo yote nchini sambamba na kutii sheria za nchi ili taifa liendelee kuwa salama na kila mmoja kuweza kuendelea na shughuli zake.
Share:

Dial, play, win- How SportPesa Tanzania’s USSD games are transforming betting for millions

A breakthrough is happening in Tanzania’s betting world and it’s not coming from flashy apps or expensive data bundles. It’s coming from a simple dial code. With SportPesa Tanzania USSD betting, fans across the country can now place bets, join jackpots, and check results instantly by dialing *150*87#, making betting more accessible, affordable, and reliable than ever.

In a country where data costs rise, smartphones vary, and network coverage can be unpredictable, SportPesa Tanzania has rebuilt how betting works from the ground up. By launching a seamless USSD betting experience, SportPesa has created a betting ecosystem that works for every Tanzanian, from urban centers to rural villages. No app. No 4G. No downloads. Just dial, play, win.

The rise of USSD betting in Tanzania

Betting in Tanzania is shifting fast. Instead of depending on apps that require a strong internet, fans are now choosing a simpler, smarter path: SportPesa Tanzania USSD betting. With one quick code *150*87# anyone with a basic phone can-

👉Register or log in

👉Deposit via mobile money

👉Explore football betting in Tanzania

👉Join the SportPesa USSD Casino Tanzania

👉Check results instantly

It’s betting engineered for access, speed, and convenience all under one wallet that syncs across USSD, app, and web.

Why Tanzanians are choosing USSD over apps

Kenya and South Africa may be app-heavy markets, but Tanzania is different and SportPesa understands this. USSD solves real issues millions face daily-

1. Zero data required

With SportPesa USSD betting, fans don’t need bundles or Wi-Fi. A student in Iringa, a shopkeeper in Arusha, or a farmer in Morogoro can place bets with the same ease.

2. Works on every phone

Smartphones or kabambe don't matter. Dialing *150*87# works everywhere.

3. No loading screens, no updates

USSD is instant. Menus load quickly even in low-signal areas.

4. Same wallet across all channels

Whether a fan uses USSD, the SportPesa Tanzania official website, or the app, everything syncs automatically.

Real Tanzanian stories behind the wins

USSD isn’t just a feature, it's a lifeline for bettors who want a reliable experience.

A fan from Mwanza explains:

“Sometimes I don’t have data, but I always have my phone. With USSD, SportPesa is always in my pocket.”

Others praise the simplicity:

“I follow the jackpot on USSD every weekend. It’s fast and doesn’t eat my bundles.”

With each story, one truth is clear: SportPesa USSD games connect communities through convenient, local-first technology.

USSD + Responsible Gaming = Trust

SportPesa’s growth is built on responsible gaming in Tanzania. Whether via USSD, app, or web, players are reminded to-

👉Set betting limits

👉Stick to their budget

👉Avoid emotional betting

👉Treat betting as entertainment

This is why SportPesa remains one of the most trusted betting platforms in Tanzania, pairing excitement with structure and safety.

How to join SportPesa via USSD today

You can start playing right now with three simple steps:

Dial the code

Open your dialer and enter: *150*87#

Follow the prompts

Choose to register or log in, then fund your account via mobile money.

Start playing

Access-

👉football betting in Tanzania

👉SportPesa Jackpot Tanzania

👉balance checks

👉live results

All from the same USSD menu.

The future of betting in Tanzania is simple

Tanzania doesn’t need heavier apps, it needs smarter access. SportPesa Tanzania USSD betting brings-

👉Local convenience

👉National reach

👉Affordable participation

👉A safe, responsible ecosystem

👉A unified betting experience

Dial *150*87# pick your matches, place your bets responsibly, and enjoy the most accessible betting experience the country has ever seen.

Share:

Tuesday, 9 December 2025

WAZIRI MKUU AWAKINGIA KIFUA WAFANYABIASHARA WADOGO ATOA ONYO KALI KWA HALMASHAURI ZOTE NCHINI



Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza Halmashauri zote Nchini Majiji kutochukuwa bidhaa halali za Wananchi ambao ni wafanyabiashara wadogo wanaojitafutia riziki zao Barabarani kulingana na mitaji yao hata kama wakikutwa na makosa ushughulikiwe utaratibu tu! na sio kuua mitaji yao midogo

"Huu utaratibu wa kuchukua bidhaa haukubaliki wafautilieni waliochukuwa bidhaa na kama hazipo hao ni wezi kama wezi wengine tusicheze na mitaji ya watu hatutapiga vita umasikini kama hatutaheshimu mitaji ya watu " Waziri Mkuu

Aidha ametumia jukwaa hilo kuwaambia kutangaza Ziara ya majiji yote Nchini kuangazia changamoto za wafanyabiashara hao na kuendelea kuacha utaratibu huo hapo hapo amesisitiza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ni mtu wa haki hivyo watendaji wasimuangushe
Share:

Monday, 8 December 2025

TANZANIA NYUMBA YETU: VIJANA WAASWA KUTUMIA MAZUNGUMZO KUJENGA, SI KUCHOMA NCHI

Wakati juhudi za baadhi ya watu wachache zikielekezwa katika kuhamasisha vurugu na maandamano yasiyo na kibali, viongozi wa kisiasa na jumuiya za vijana wameungana kuwasisitiza Watanzania, hususan vijana, kwamba wajibu wao mkuu ni kuifanya Tanzania kuwa mahali bora pa kuishi kupitia njia za busara, umoja na mazungumzo, na si kwa kuichoma nchi.

Mwanasiasa Peter Daffi alisisitiza kuwa Serikali haiwezi kuruhusu maandamano yasiyo na kibali, akionya kuwa hatua hiyo inaweza kuifanya dunia kushangaa kwa nini Watanzania wanashindwa kukaa, kuzungumza na kukubaliana kama taifa.

"Mnataka turuhusu tena hali ya kushangaza duniani kwamba tumeshindwa kukaa na kuzungumza na kukubaliana?" alihoji Daffi, akisisitiza kwamba juhudi za kuhamasisha vurugu hazikubaliki kwani zinahatarisha usalama wa watu na mali.

Daffi aliwaelekeza wananchi kutumia njia sahihi zilizowekwa na Serikali ili kufikia maridhiano. Alisema waliotaka kutoa maoni yao tayari wametengewa nafasi kupitia Tume iliyoanzishwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

"Rais ameunda tume. Ile tume sasa tuiisikilize ili itekeleze yale tunayodhania na tunayotamani yafanyike," alisema Daffi. Alisisitiza kuwa Tume hiyo ndiyo njia sahihi ya kusikiliza maoni ya wananchi, na kwamba wananchi wanapaswa kutoa maoni yao wanapofika kwenye maeneo mbalimbali ili Serikali iweze kutekeleza wanayoyahitaji.

Vijana Kujenga, Sio Kubomoa

Kauli za wanasiasa ziliungwa mkono na ujumbe mzito kutoka kwa jumuiya ya vijana, wakisisitiza kwamba nguvu za vijana ni za kujenga, si kubomoa. Ujumbe huo uliwakumbusha vijana kuwa Tanzania ni urithi pekee wa thamani unaohitaji kulindwa.

"Tuchague busara, umoja na ustaarabu tunapotafuta 'HAKI' si hasira, wala kutumia vurugu," ulisema ujumbe huo.

Wito huu unaakisi kuongezeka kwa ushiriki wa vijana katika Bunge na katika nafasi za uongozi. Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha, Cecilia Paresso (CCM), ambaye pia ni kijana, alisisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii ili kumsaidia Rais Samia kufikia azma yake ya kuacha tabasamu kwa Watanzania ifikapo 2030, akisimamia misingi ya kazi na utu.

Vijana walisisitizwa kutokuwa chombo cha kuchochewa, kupandikizwa chuki na kufuata mkumbo. Badala yake, wanapaswa kuwa walinzi wa utulivu na mshikamano. Tanzania ni nyumba yetu sote; hatuna nyingine.

Wito kwa Taasisi za Dini

Kama nguzo muhimu, taasisi za dini nazo ziliaswa kuendelea kuwa daraja la upatanisho na si ukuta unaowatenganisha raia na viongozi wao. Waliombwa kutumia maneno yao kuleta matumaini na kurejesha mioyo iliyokata tamaa.

Kwa ujumla, ujumbe mkuu kwa taifa ni kwamba ulinzi wa amani na juhudi za kujenga nchi bora zinapaswa kupitia mazungumzo na taasisi rasmi, huku kila hatua ikielekezwa katika kuijenga Tanzania tunayotaka kuiona kesho.


Share:

Sunday, 7 December 2025

MAHAFALI YA TANO LITTLE TREASURES SECONDARY YANG’ARA, WAZAZI WAHIMIZWA KUWEKEZA KWENYE ELIMU

Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog

Mahafali ya Tano ya Shule ya Sekondari Little Treasures iliyopo Mjini Shinyanga yamefanyika kwa uzito mkubwa na hamasa ya kipekee, yakikutanisha wazazi, walimu, viongozi na wadau mbalimbali wa elimu katika Mkoa wa Shinyanga.

Hafla hiyo iliyofanyika Desemba 5,2025 imeonesha ukubwa wa uwekezaji wa shule hiyo katika kuinua kiwango cha elimu na kujenga kizazi chenye maadili, maarifa na uwezo wa kutimiza ndoto zao.

Akiwasilisha risala ya mahafali hayo, Mkuu wa Shule ya Sekondari Little Treasures, Alfred Mathias, alisema jumla ya wanafunzi 61 wamehitimu masomo yao, wakiwemo wavulana 36 na wasichana 25, huku akisisitiza kuwa shule hiyo itaendelea kujenga misingi imara ya nidhamu na ufaulu.

Mkurugenzi wa Shule za Msingi na Sekondari Little Treasures, Lucy Mwita, alisema wamejidhatiti kuendelea kuwa hazina ya watoto na daraja la mafanikio kwa kuwajengea uwezo, maadili na uelewa mpana wa masomo yao.
Aliwataka wazazi kuendelea kuiamini na kuiunga mkono shule kwa kupeleka watoto wao ili waendelee kupata elimu bora.

Kwa upande wake, Meneja wa shule hiyo, Wilfred Mwita, alisema Little Treasures itaendelea kujituma kwa bidii kuhakikisha wanafunzi wanafundishwa kwa weledi na kuandaliwa kufikia malengo yao ya kitaaluma na maisha, huku akiomba mashirikiano zaidi kutoka kwa wazazi.

Mgeni rasmi kwenye mahafali hayo, Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga, Bakari Ally, aliwataka wazazi kubadili mtindo wa maisha na kuacha kuendekeza starehe zinazopoteza fedha, badala yake wawekeze kwenye elimu ya watoto wao.
Bakari alisema wazazi wengi wamekuwa wakitumia fedha nyingi kwenye sherehe za ubatizo hadi shilingi milioni 3 au sherehe za siku ya kuzaliwa kwa zaidi ya laki 8, lakini wanapofika Januari wakitakiwa kulipia ada za watoto wao, huanza kuomba muda na kusisitiza kuwa hawana fedha.

“Wazazi wekeni vipaumbele vyenu kwenye mambo muhimu na kuacha kupoteza pesa hovyo. Sasa hivi ni mwezi Desemba lakini mtu anafanya sherehe ya ubatizo shilingi milioni 3, au sherehe ya kuzaliwa shilingi laki 8. Ikifika Januari unadaiwa ada unasema huna hela, hivi unadhani walimu watakuelewa kweli?” alisema.
Alisisitiza kuwa elimu ni uwekezaji na wazazi hawapaswi kuchelewesha ada za watoto wao.

“Maji ukiyavulia nguo lazima uyaoge, lipeni ada kwa wakati. Ukweli mchungu, lakini wazazi badilini mtindo wa maisha ,kusomesha mtoto ni kufanya uwekezaji,” aliongeza.

Katika hatua nyingine, Bakari aliitaka Shule ya Sekondari Little Treasures kuanzisha Club ya Sheria, ambayo itakuwa ikipokea wataalamu wa sheria kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga kwa ajili ya kutoa elimu ya sheria shuleni hapo na kuwajengea wanafunzi uelewa mpana wa masuala ya kisheria.

Aliwataka wahitimu kuendelea kudumisha nidhamu, kuwa mabalozi wazuri wa shule hiyo na kuitangaza vyema popote watakapokwenda.
Sehemu ya wahitumu wakicheza muziki

Mtendaji wa Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Bakari Ally akizungumza.
Mkurugenzi wa Shule za Msingi na Sekondari Little Treasures Lucy akizungumza.
Meneja wa shule za Little Treasures Wilfred Mwita.
Mkuu wa shule ya Sekondari Little Treasures Alfred Mathias akisoma Risala ya shule.
Mwakilishi wa wazazi aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizungumza.

Aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akimpongeza mtoto wake Cedric kwa kuhitimu kidato cha Nne shule ya Sekondari Little Treasures.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger