Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Saturday, 13 December 2025

E- MREJESHO KUKUZA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA UMMA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Wizara hiyo imefanya maboresho mbalimbali ya mifumo yake ikiwemo mfumo wa e- mrejesho, ili kutoa fursa zaidi kwa wananchi wa pembezoni kutoa maoni, malalamiko na pongezi kuhusu huduma zinazotolewa na serikali na Taasisi zake.

Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam, akisema mfumo huo unapatikana kwenye simu za mkononi kupitia nambari *152*00#, ukiwa na module ya sema na Kiongozi, sehemu inayomruhusu mwananchi kutoa maoni kwa Waziri, Mkuu wa Mkoa ama Kiongozi mwingine, akisema mfumo huo utakusanya maoni na kisha kuchakatwa na kufanyiwa kazi.

"Mfumo huu wa e- mrejesho ni kiunganishi cha moja kwa moja cha mwananchi na Kiongozi na hii itatusaidia pale tunapojadili namna ya kuboresha mifumo ya utumishi wa umma na ni mfumo wa kweli huu, hata kama kuna Kiongozi hatojibu sisi tutasimamia kuhakikisha majibu yanapatikana." Amesema Mhe. Ridhiwani.

Aidha Mhe. Ridhiwani amehimiza wananchi kuutumia mfumo huo katika kutoa maoni yao, akisisitiza kuwa maboresho hayo yanaenda sambamba na utengenezaji wa Aplikesheni itakayowezesha wananchi kutoa mrejesho wa haraka na wa uwazi ili kuimarisha uwajibikaji wa watumishi wa serikali.


Share:

SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO LAANZA KUANDAA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO 2026-2031


Shirika la Masoko ya Kariakoo limeanza rasmi maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031, hatua inayolenga kulifanya soko hilo la kimataifa kutoa huduma bora, kwa wakati na kuzingatia mabadiliko ya teknolojia yanayojitokeza duniani.

Mpango huo unakuja baada ya baada ya mpango wa 2021-2025 kumaliza muda wake wa utekelezaji kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi mafunzo ya uchambuzi na uandaaji wa mpango huo, Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashiraf Abdulkarim , amesema maandalizi ya mpango huo umeshirikisha wadau ikiwemo Ofisi Waziri Mkuu TAMISEMI, Wafanyabiashara wa Kariakoo, Wapangaji na wadau wengine ili kuwa na mpango mkakati bora, uliochukua mawazo ya wengi na unaojibu matamanio ya kila mmoja na hivyo kuwa rahisi katika utekelezaji wake.

CPA Abdulkarim ameongeza kuwa katika kuandaa mpango huo, Shirika litazingatia nyaraka mbalimbali ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025-2050, hotuba ya Rais wakati akifungua Bunge la 13, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa, Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025-2030 pamoja na Sheria na miongozo mbalimbali iliyoanzisha Shirika la Kariakoo.

“Mafunzo haya yatafanyika kwa siku tano na yatakuwa endelevu. Lengo ni kuwa na mpango mkakati bora, unaotekelezeka na unaoweza kupimika kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano ambao utalifanya soko la kariakoo kuwa kinara na linalotoa huduma anuai na sio mazao pekee" amebainisha CPA Abdulkarim.

Amesema mpango huo ukikamilika utalibadilisha soko la Kariakoo kuwa kituo cha kisasa cha biashara, chenye mifumo ya kisasa ya uendeshaji na utoaji huduma.

CPA. Abdulkarim amesema kuwa Kariakoo mpya itakuwa na miundombinu ya kisasa kuanzia maeneo ya maegesho ya magari, mifumo ya kuzima moto, maeneo ya dharura, hewa ya kutosha na mifumo ya kiteknolojia ya uendeshaji. Tunataka kuwahudumia Watanzania katika mazingira bora na ya kisasa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mipango na Biashara wa Shirika la Kariakoo, Bi. Mwinga Luhoyo amesema maandalizi ya mpango huo yanahusisha tathmini ya mpango uliopita wa 2021–2025 ili kubaini mafanikio, changamoto na maeneo yanayohitaji maboresho.

Meneja huyo ameongeza kuwa lengo ni kuhakikisha mpango huo unaendana na mikakati ya kitaifa na huku ukilenga kuongeza tija, kuimarisha biashara, na kukuza mchango wa Kariakoo katika uchumi wa taifa.
Share:

WAZIRI HOMERA AZINDUA HUDUMA YA VYETI VYA KUZALIWA KWA MASAA 48 AITAKA TEHAMA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA HAKI

Waziri wa Katiba na Sheria na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo Dkt Juma Zuberi Homera baada ya kutoka kuzindua huduma ya utoaji wa vyeti vya kuzaliwa ndani ya masaa 48.matumizi jijini Dar es Salaam tarehe 12 disemba 2025

Na Mwandishi Wetu Malunde 1 Blog 

Katika kuimarisha utoaji wa haki na huduma kwa wananchi, Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Dkt. Juma Zuberi Homera, amezindua rasmi huduma ya utoaji wa vyeti vya kuzaliwa ndani ya masaa 48. 

Akizungumza wakati wa ziara yake katika Taasisi ya Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Dkt. Homera amesema mpango huo utarahisisha upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi na kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa wakati, hatua ambayo itachangia kuimarisha uchumi wa taifa.

Dkt. Homera amesema masuala kama ndoa, vifo na mirathi yote yanahitaji vyeti ili wananchi waweze kupata stahiki zao, hivyo mpango huo wa masaa 48 utapunguza kwa kiasi kikubwa changamoto zilizokuwa zikijitokeza. 

Amebainisha kuwa utekelezaji wa mpango huu ni sehemu ya maelekezo ya Mheshimiwa Rais, unaolenga kuhakikisha haki inapatikana kwa haraka na ufanisi kwa Watanzania wote.

Katika ziara hiyo, Waziri Homera pia ametembelea Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali pamoja na Roscoe of Tanzania, ambako amezindua magari mapya matatu yaliyotolewa na serikali—mawili kwa ajili ya wakuu wa taasisi na moja kwa matumizi ya wananchi pamoja na watumishi. 

Aidha, amewataka viongozi kuhakikisha wanatoa matamko yenye msingi wa utafiti ili kuepusha hasara na migogoro ya kisheria inayoweza kujitokeza kutokana na kauli zisizo sahihi.

Akiwa katika Shule ya Sheria Tanzania, Dkt. Homera amewasisitiza watendaji kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu, kuacha masilahi binafsi na kuhakikisha taaluma ya sheria inasimamiwa kwa weledi. 

Pia amehimiza matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma, akisisitiza kuwa mifumo ya kielektroniki itasaidia kuharakisha upatikanaji wa haki na kuongeza ufanisi katika taasisi za kisheria nchini.























Share:

Friday, 12 December 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DESEMBA 13,2025


Magazeti




Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA DESEMBA 12,2025

Magazeti
 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger