Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Friday 26 April 2024

WAKULIMA VIJANA WAELEZA FAIDA ZA MATUMIZI YA MBEGU BORA

 
Mkulima kijana kutoka jijini Arusha anayefahamika kwa jina la Edward Jacob anayejihusisha na kilimo cha Mbogamboga na Matunda ameeleza faida za matumizi ya Mbegu bora na matarajio yake kuelekea Bajeti ya Kilimo kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 itakayosomwa Bungeni jijini Dodoma mnamo Mei 02 na Mei 03, 2024.

Miongoni mwa faida nyingi alizoeleza ni pamoja na kupata mazao yenye ubora, yasiyoharibiwa kirahisi na wadudu pamoja na kupata mavuno ndani ya muda mfupi.


Sambamba na faida hizo Edward pia ameeleza matarajio yake kwa Bajeti ya kilimo kwa Mwaka 2024/2025 kuwa ni kuendelea kupata mbegu hizo zinazozalishwa na taasisi zinazotambulika nchini pamoja na kupata pembejeo kwa urahisi zaidi ili kuendelea kupata mazao bora.


Kwa upande wake, Agnes Sachi ambaye pia ni kijana anayejihusisha na Kilimo cha Mbogamboga jijini Arusha ameeleza namna kulima kwa kutumia mbegu na miche bora kulivyomnufaisha na matarajio yake kuelekea bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2024/2025.

Share:

Video Mpya : NELEMI MBASANDO - MAFURIKO

 

Share:

VIJANA 58 WANUFAIKA NA MAFUNZO YA UTENGENEZAJI VIHENGE KUPITIA MRADI WA TANIPAC KUZUIA SUMUKUVU


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Jumla ya Vijana 58 kutoka mikoa ya Tabora, Mwanza, Geita na Simiyu wamehitimu mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa ‘Tanzania Initiative For Preventing Aflatoxin Contamination – TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo wenye lengo la kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii.


Akizungumza leo Ijumaa Aprili 26,2024 wakati wa kufunga Mafunzo ya kutengeneza Vihenge awamu ya tatu, Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban amesema mafunzo hayo yamehitimishwa rasmi baada ya kutolewa katika awamu tatu yakinufaisha vijana 58.

“Mafunzo ya kutengeneza vihenge yalianza tarehe 26,2024 kwa awamu ya kwanza ambapo washiriki walikuwa 19, ikafuatia awamu ya pili ikiwa na washiriki 23 na leo washiriki 16 wamehitimu. Wamefundishwa masuala ya ujasiriamali, utengenezaji wa vihenge kwa nadharia na vitendo, nadharia ya masoko, usimamizi wa fedha na urasimishaji wa biashara”,amesema Taban ambaye ni Afisa Uendelezaji Biashara SIDO Mkoa wa Shinyanga.


“Serikali kupitia mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo imeendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii. Mradi wa TANIPAC unalenga kuwezesha jamii kutumia njia sahihi na za kisasa za uhifadhi wa nafaka hususani mahindi kutokana na sumukuvu”,ameongeza Taban.

Amefafanua kuwa, Serikali imeingia gharama kuhakikisha kuwa vijana wanapatiwa ujuzi wa kutengeneza vifaa vya kisasa na vinavyodumu kwa muda mrefu (vihenge) ili kutimiza adhima ya kupunguza sumukuvu.

Taban amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuhakikisha wanayatumia kwa vitendo kuhakikisha kuwa lengo la mafunzo linatimia ambapo pia yatawezesha kuongeza kipato cha mmoja mmoja, kaya na taifa kwa ujumla.

“Mafunzo haya yametolewa kwa vijana wachache lakini wengi wangependa kupata mafunzo haya,hivyo nitumie nafasi hii kuwaomba mkawe waalimu wa kufundisha vijana wenzenu kwenye maeneo yenu ya kazi ili kwa pamoja tuweze kupambana kwa vitendo kupunguza kama siyo kuondoa kabisa sumukuvu”,amesema Taban.

Akisoma risala kwa niaba ya Washiriki wenzake wa mafunzo, Wanjala Daudi amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha utendaji kazi na kuzalisha bidhaa za vihenge (Silos) na nyinginezo kwa tija ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

“Tunaushukuru uongozi wa SIDO na Wizara ya Kilimo kwa kutoa fursa ya mafunzo haya. Hakika mafunzo haya yametujengea uwezo wa kujiamini na kuamsha ari ndani yetu ya kujiajiri na kuachana na kasumba ya kusubiri ajira”,amesema Daudi.

“Pamoja na ari na motisha ya kujiajiri iliyojengeka ndani yetu, tunakabiliwa na changamoto ya mitaji kwa ajili ya kununua vifaa/vitendea kazi vya kuanzisha shughuli mbalimbali kutokana na fani tulizojifunza”,ameongeza Daudi.

Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa vijana wakati akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa ‘Tanzania Initiative For Preventing Aflatoxin Contamination – TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo - Picha na Kadama Malunde 1 blog
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia) akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kushoto) akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (wa nne mbele kushoto) , viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (wa nne mbele kushoto) , viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo wenye lengo la kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo


Mratibu wa Mafunzo ya Kutengeneza Vihenge Mkoa wa Shinyanga, Misuka Makwaya ambaye ni Mhasibu wa SIDO Mkoa wa Shinyanga akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Mratibu wa Mafunzo ya Kutengeneza Vihenge Mkoa wa Shinyanga, Misuka Makwaya ambaye ni Mhasibu wa SIDO Mkoa wa Shinyanga akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Wanjala Daudi akisoma risala ya washiriki wa mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Afisa Mipango SIDO Shinyanga , Frank Nguyu akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Mwenyekiti wa Mafunzo, Charles Kulwa akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Mratibu wa Mafunzo SIDO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Manyama Lububi akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge


Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban, viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban, viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo

Share:

BENKI YA CRDB YAKABIDHI MADARASA SEKONDARI YA KIKILO, SHULE YA MSINGI ISABE, KONDOA


Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25, 2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na madarasa mengine mawili katika Shule ya Msingi Isabe zote za wilayani Kondoa, mkoa wa Dodoma yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo.

Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.

Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.

Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay wakiwa pamoja na viongozi wengine pamoja na Wanafunzi katika moja ya madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 katika Shule ya Msingi Isabe, iliyopo katika kijiji cha Bukuru, Wilayani Kondoa, katika hafla iliyofanyika Aprili 25, 202.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi (wanne kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay (katikati) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB pamoja na wa Halmashauri ya Kondoa wakiwa katika picha ya paamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikilo, muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili katika shule hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.





Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25, 2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na madarasa mengine mawili katika Shule ya Msingi Isabe zote za wilayani Kondoa, mkoa wa Dodoma yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo.

Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.

Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.

Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.

Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay wakiwa pamoja na viongozi wengine pamoja na Wanafunzi katika moja ya madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 katika Shule ya Msingi Isabe, iliyopo katika kijiji cha Bukuru, Wilayani Kondoa, katika hafla iliyofanyika Aprili 25, 202.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi (wanne kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay (katikati) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB pamoja na wa Halmashauri ya Kondoa wakiwa katika picha ya paamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikilo, muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili katika shule hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.









Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger