Wednesday 30 June 2021

SEKTA YA MIFUGO INA MCHANGO MKUBWA KATIKA KUKUZA UCHUMI WA NCHI-PROF.OLE GABRIE

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza wakati wa hafla ya kuwapatia vyeti wauza wa pembejeo sita waliochaguliwa kushiriki katika kutoa huduma za ugani kwa wafugaji walioko maeneo ya Dar es Salaa, Pwani, Morogoro na Tanga.

Mratibu wa Mradi wa AgResults Tanzania Dairly Productivity Challenge Bi.Neema Mrema akizungumza wakati wa hafla ya kuwapatia vyeti wauza wa pembejeo sita waliochaguliwa kushiriki katika kutoa huduma za ugani kwa wafugaji walioko maeneo ya Dar es Salaa, Pwani, Morogoro na Tanga.

Mshirika wa Price Water house Cooper (PwC), Bw.Nelson Msuya wakati wa hafla ya kuwapatia vyeti wauza wa pembejeo sita waliochaguliwa kushiriki katika kutoa huduma za ugani kwa wafugaji walioko maeneo ya Dar es Salaa, Pwani, Morogoro na Tanga.

Mkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw.Steve Michael wakati wa hafla ya kuwapatia vyeti wauza wa pembejeo sita waliochaguliwa kushiriki katika kutoa huduma za ugani kwa wafugaji walioko maeneo ya Dar es Salaa, Pwani, Morogoro na Tanga.

Wadau mbalimbali wa sekta ya mifugo nchiniwakifuatilia hafla ya kuwapatia vyeti wauza wa pembejeo sita waliochaguliwa kushiriki katika kutoa huduma za ugani kwa wafugaji walioko maeneo ya Dar es Salaa, Pwani, Morogoro na Tanga.

Wauza pembejeo waliochaguliwa kushiriki katika kutoa huduma za ugani kwa wafugaji walioko maeneo ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Tanga wakipatiwa vyeti mara baada ya kufanya vizuri katika sekta hiyo.Zoezi la utoaji vyeti limefanyika leo Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Sekta ya mifugo sasa inachangia uchumi wa nchi zaidi ya asilimia 7.4% na mwaka huu wa fedha unaoisha, sekta hii inakuwa kwa asilimia 5% lengo likiwa kufikia mara mbili kwenye mchango wa uchumi na kuweza kufikia angalau asilimia 15 ifikapo mwaka 2025.

Ameyasema hayo leo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel wakati wa hafla ya kuwapatia vyeti wauzaji wa pembejeo sita waliochaguliwa kushiriki katika kutoa huduma za ugani kwa wafugaji walioko maeneo ya Dar es Salaa, Pwani, Morogoro na Tanga.

Amesema uzalishaji wa maziwa nchini umefikia bilioni 3.4 ikiwa maziwa yanayosindikwa ni lita milioni 75 hii inamaana inaleta wawekezaji wengi kuja kuchakata na kuleta thamani kwasababu wateja wananunua maziwa ambayo yameongezwa thamani .

"Takwimu zinaonesha katika lita bilioni 3.4 maziwa yanayotka kwenye ng'ombe wa kienyeji ni lita bilioni 2.38 kwahiyo lita bilioni 1.2 tu zinaonesha zinatokana na ng'ombe wa maziwa". Amesema Prof. Ole Gabriel.

Aidha amesema Tanzania ni nchi ya pili kwa wingi wa mifugo barani Afrika ambapo inazaidi ya ng'ombe milioni 33.9 na mbuzi wameshafika zaidi ya milioni 22 wakati kondoo wamefika takribani milioni 6, kuku wamefikia milioni 87.7.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa AgResults Tanzania Dairly Productivity Challenge Bi.Neema Mrema amesema kuwa kupitia mradi huo wana matokeo mazuri wameyaona ambapo kuna ng'ombe 558 tayari wana mimba na wengine tayari wameshapata watoto pia kuna ng'ombe 336 ambao wameogeshwa kitaalamu na vilevile kuna ng'ombe 62 ambao hao wamepata chanjo kuanzia mbili na kuendelea.

"Wauza pembejeo hawa wameweza kuwafikia wafugaji 2776 na kuuza pembejeo nne ambazo ni vidhibiti vimelea, Chanjo, lishe uhimilishaji pia mpaka sasa tuna ng'ombe 17,000 ambao wamepata huduma mbalimbali za lishe katika kuongeza afya bora na pia kuweza kupata maziwa yaliyobora". Amesema Bi.Mrema.

Amesema kuwa mradi huo una malengo matatu ambapo lengo la kwanza ni kuongeza uzalishaji na tija ya maziwa kwa wafugaji wadogowadogo, kuongeza kipato kwa wafugaji wadogowadogo wa maziwa, kuleta uwiano sahihi na kuboresha mifumo ya uendeshaji wa shughuli katika sekta ya maziwa .

Hata hivyo Bi.Mrema amesema washiriki sita wa mradi huo kutoka sekta binafsi wamepata tuzo na motisha ya dola za kimarekani 27,000 kwa pembejeo 4116 zilizokamilika ili waweze kuendelea kutoa huduma na kuongeza uzalishaji wa maziwa na kukidhi soko la Tanzania.


Share:

Rais Samia Akutana Na Katibu Mtendaji Wa Sekretarieti Ya Eneo Huru La Biashara Afrika



Share:

Maswali 15 Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kwenye Usaili ( Interviews ) na Namna ya Kuyajibu

Usaili wa ajira (interviews) husababisha hofu na msongo wa mawazo kwa vijana wengi kabla au baada ya kutoka chumba cha usaili.

Tatizo hilo hutokana na hofu inayojenga wakati wa kujibu maswali unayoulizwa  na watu ambao wamekuzunguka wakati wa kufanyiwa usaili.

Njia moja ya kuzuia hii kutokea ni kufuatilia mfumo wa kujibu maswali.

Ifuatayo ni orodha yetu ya maswali 15 yanayoulizwa mara kwa mara kwenye interviews( Usaili) na namna ya kuyajibu;

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

1.Jitambulishe(Wewe ni Nani?)
Mara nyingi hili ni swali ambalo mtahiniwa huulizwa mara tu aingiapo kwenye chumba cha usaili. Kwa bahati mbaya watahiniwa wengi hudhani kuwa waajiri hutamani kujua majina yao. Hapana, majina yako wanayafahamu na pengine hata taarifa za ziada. Katika swali hili waajiri uhitaji kujua sifa zako zihusianazo na ajira zitakazo dhihirisha kuwa wewe ni mtu sahihi.

Mfano mtu anaweza kujibu hivi, “Jina langu ni Mti Mkavu, ni Mhitimu wa Shahada ya Masoko ya Chuo Kikuu Dodoma. Ni mtu makini, mbunifu, mchapa kazi na ninayependa watu. Pamoja na hayo ninao ujuzi usio na shaka kwenye masuala ya mawasiliano. Uwezo wangu unadhihirishwa na mrejesho ambao huwa na upata kwa kila mtu ninaye fanya naye kazi”.

Katika swali hili ni muhimu kujua kuwa halihitaji wewe kuzungumzia mambo yasiyo husiana na kazi na ajira. Kwenu mpo wa ngapi,jina la mama yako, mkoa unaotoka, kabila, kazi ya baba au mama yako havihitajiki katika taarifa unazotakiwa. 


2.Kwanini upewe ajira kwetu? | au unaweza ukaulizwa Kwa nini unahisi wewe ni mtu sahihi kwa kazi hii na siyo mwingine?

Kumbuka kuwa usaili wa kazi unahusisha ushindani hivyo swali hili linataka uoneshe utofauti ulionao. Katika kujibu swali hili zingatia mahitaji ya kazi husika kujenga hoja kwani hata kama una utofauti wa aina gani kama hautasaidia katika kufikia  malengo ya taasisi bado itakuwa ni kazi bure.

Mfano, “ Siyo kwamba mimi ni mchapakazi na mbobezi katika uhasibu pekee lakini pia ni mtu ambaye ninaweza kufanya shughuli zangu bila kusimamiwa. Mimi ni mtu wa matokeo hivyo kwa kila ambacho hufanya hulenga kutimiza malengo kwa wakati na kufikia viwango stahiki. 


"Ubora wangu unathibitishwa na tuzo kadhaa nilizowahi kupata ikiwemo mfanyakazi bora wa mwezi mara nne nilipokuwa nikifanya kazi na na Magogo Media. Hii inathibitisha kuwa mkinipa fursa hii hamtakuwa mnajaribu bali mtakuwa mnafanya maamuzi sahihi”.

3.Unajua nini kuhusu sisi?
Siku zote maandalizi ya usaili yanaenda sambamba na kutafuta taarifa sahihi za taasisi husika. Hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa taarifa unazotoa hapa ni sahihi na muhimu katika kudhirisha kuwa ulishafanya utafiti wa kutosha kuhusu taasisi husika.

Mfano, “ Benki yenu ilianzishwa mwaka 1987 ina maono ya kuwa benki bora kuliko zote nchini kwa kutoa huduma za kifedha zinazo aminika na kufikia maeneo mengi nchini. Kwa sasa benki yenu ina matawi 700 na ATMs 500 huku ikiwa na mpango wa kufungua matawi mengine Kigoma hivi karibuni. 


Endapo mtanipa fursa ya kufanya kazi na nyinyi nitahakikisha natumia vyema uwezo wangu katika masuala ya masoko ili kuongeza wateja na kuhaikisha huduma bora mnayotoa inafahamika kwa watu wengi.”

4. Ni vitu gani unavyojivunia?
Katika swali hili waajiri huhitaji kujua mambo kadhaa ambayo unayaona kama mtaji mkubwa katika utendaji kazi. Ni vyema kukumbuka kuwa mambo utakayo yataja hapa ni yale yenye umuhimu katika kuongeza ufanisi au ubora katika kazi husika kwani kila kazi inamahitaji yake ya tofauti na kazi nyingine.

Kwa mfano, “mambo makuu mawili ninayojivunia ni ujuzi na uwezo katika huduma kwa wateja na kujisimamia katika majukumu yangu. Kila ninapowahudumia wateja huwa napokea mrejesho chanya juu ya namna wanavyoridhishwa na huduma yangu hivyo kutamani kuhudumiwa nami tena.


Hii hunifanya nijione kuwa mtu muhimu sana katika taasisi yoyote ninayofanya nayo kazi. Pia, uwezo wangu katika kufanya shughuli bila kusimamiwa au chini ya usimamizi mdogo unanifanya niwe mtu wa kuaminiwa na kutegemewa katika kufanya shughuli zangu.Haya ni baadhi ya mambo mengi yanayonifanya mimi kuwa mtu wa tofauti. Nina amini hamtaacha fursa ya kufanya kazi nami”
 

5.Udhaifu wako ni upi?
Hili ni moja ya maswali ambayo watainiwa wengi huyachukia na kuyaona kama yana lengo la kuwatafutia sababu za kuwanyima kazi. Wengine kwa lengo la kuonesha ukamilifu huthubu kusema kuwa hawana udhaifu wowote-usithubutu kusema hivyo. Kila mtu ana udhaifu wake kwani hakuna aliye mkamilifu.

Suala la msingi ni kujua namna ya kujibu suali hili. Mambo ya kuzingatia ni pamoja na kuchagua udhaifu ambao hauta athiri utendaji wako na pili hakikisha udhaifu huo unahusiana na ujuzi na sio tabia. 


Ujuzi ni rahisi kuutafuata lakini kubadilisha tabia ni ngumu zaidi hivyo usiseme kuwa wewe ni mvivu,mdokozi, na mengineyo ya kitabia. Na unapotaja udhaifu wowote kumbuka kuonesha jitihada ambazo umeshazifanya ili kudhibiti udhaifu huo.

Kwa mfano, kwa kazi ya uhasibu mtu anaweza sema, “Udhaifu nilio nao ni masuala ya ‘graphic designing’ niligundua hili nilipohitaji kuandaa tangazo kwa ajili ya ofisi niliyokuwa nikifanya nayo kazi. Hata hivyo, nimeanza kujifunza mwenyewe kupitia mtandao wa internet na naona napata mabadiliko chanya kila leo”.

Kwa jibu hili ni dhahiri kabisa graphic designing siyo mahitaji muhimu ya kazi ya uhasibu hivyo haita athiti utendaji wa kazi.


6. Kwa nini uliacha kazi yako ya mwanzo?
Hapa unahitajikua makini sana, kumbuka na epuka kuzungumza vibaya kuhusu muajiri yeyote kabla au sasa au uwezo wa muajiri. 


Hapa unaweza ukawajibu tu kwamba;" Kwa sababu ya kuboresha na kuongeza ujuzi, pia natafuta fursa bora zaidi."

7.Unatarajia kupata nini kutokana na kufanya kazi hapa? au unaweza ukaulizwa | Baada ya miaka mitatu wewe mwenyewe utakua wapi?
Ongelea unachotumaini kutimiza ila kuwa mkweli. Pia usiongee kwa ujumla. Chagua kitu maalum ambalo ni muhimu kwa kampuni alafu ilenge. Ila, uwe wazi kwa kusema itachukua muda kujifunza zaidi kuhusu kampuni ili kufanikiwa zaidi.

Kwa mfano; “Nikiwa mwalimu wa kiingereza, lengo langu ni kuongeza asilimia ya wanafunzi wanaofaulu mtihani wa taifa kuwa 85% ya darasa yangu. Najua itachukua muda kujua vizuri changamoto za wanafunzi ila, naamini nitafanikiwa”


Ni vizuri kusema kwamba unatumaini kuona uwajibikaji zaidi  katika kampuni hiyo na kuongeza thamani katika kampuni kwa mchango wako. 

8.Kwanini umekaa muda mrefu bila kupata ajira?

Wajibu kwamba; "Nilikuwa najiendeleza katika taaluma yangu "


9. Eleza namna unavyoweza kujisimamia mwenyewe
Wajibu kwamba: Nitakuwa nafanya kazi niliyopewa nikishirkiana na wasimamizi wangu na viongozi juu ya namna ya kumaliza kazi kabla ya muda uliopangwa.


10. Kitu gani kinakukera miongoni mwa wafanyakazi wenzako?

Wajibu kwamba; "Naamini katika kufanya kazi kwa pamoja. Hata kama nikikerwa na kitu chochote, huwa najaribu kuepuka isipokuwa kama ni kitu cha binafsi."

11.Unategemea kufanya kazi kwa muda gani kama ukipewa ajira?

Wajibu:Kwa muda mrefu kama nitaendelea kuongeza kitu katika taaluma yangu.

12:Je, mwenyewe unajiona kufanikiwa?

Wajibu: Ndio, ukiachana na uwezo wa taaluma yangu, nadhani nimepata watu sahihi wa kufanya nao kazi.

13. Uwezo wako ni upi katika kazi?
Wajibu: Mimi huwa naelewa na kufundishika kwa haraka na ni mchapakazi wa kweli.

14,Unapenda nafasi au cheo gani katika timu unayofanya nayo kazi?
Wajibu: Haijalishi hadi nitakapojifunza kitu kipya kwa kila mradi au kazi.

15.Je, unaswali lolote kwetu? 

Mwishoni wa interview, ni kawaida kwa mwajiri kuuliza kama una maswali kwao. Ukipewa nafasi hii, usiulizie mshaara na faida zingine. Badala yake, uliza:
  1.     Maadili ya kampuni
  2.     Aina ya uongozi
  3.     Wafanyakazi wenzako
  4.     Chochote ambacho hukuelewa kuhusu kazi hiyo.
  5.     Watakupa jibu baada ya muda gani?
==>>USIFANYE HAYA MAKOSA KATIKA SWALI HILO:
- Je, kuna fursa ya kukua / kupandishwa ngazi?
- Nitapata siku ngapi za likizo?

- waajiliwa wanafaidika vipi na kampuni hii. 

==>Tiba bora ya msongo wa interview ni kujiandaa
Ingawa interview inaweza ikakupa misongo mingi, ukijiandaa vizuri Utashangazwa na mafanikio yako.

Interview ni nafasi yako ya mwisho kumvutia mwajiri, na vidokezo vilivyoelezwa hapo juu vitakusaidia na hilo.

Kumbuka, hamna haja ya kuwa na wasiwasi ukiwa umejiandaa. 


 Nakutakia Mafanikio mema kwenye Interview
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

👉Sasa, kwa kuwa umeshajua jinsi ya kujibu vizuri maswali ya Interview, anza kutafuta kazi unayoitaka kwa kubofya hapo chini. 


👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
http://www.ajirazote.com/jobs/

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬


Share:

FAINALI ZA KIHISTORIA UMISSETA 2021 ZAUNGURUMA MTWARA

A.  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Hassan Abbasi (aliyejishika kidevu)

akiangalia  mechi ya nusu fainali baina ya timu ya Mtwara na Dodoma ambapo Mtwara imeshida bao 1 na Dodoma 0. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Dunstan Kyobya kuchoto ni Mkurugenzi wa Michezo nchini Yusuph Singo

A.  Mechi ya nusu fainali ikiendelea baina ya Dodoma (nyekundu) na Mtwara(nyeupe) ambapo Mtwara imeshida bao 1 dhidi ya Dodoma 0.


Penati ikipigwa na mchezaji wa Pemba (kijani) kwa golikipa wa Geita (nyekundu) ambapo timu ya Pemba imeshinda penati 4 dhidi ya penati 3 za Geita.


Mwandishi Maalum, Mtwara

Michezo inayoendelea kwenye Mashindano ya Taaluma na Michezo kwa Shule za Sekondari (UMISSETA) yanafikia fainali Julai 1, 2021 kwenye viwanja mbalimbali vya mjini Mtwara ambapo mashindano hayo yatafungwa rasmi Julai 2,2021.

Kwa mujibu wa Msemaji wa mashindano hayo, John Mapepele fainali ya soka kwa wavulana itakuwa baina ya timu ya Pemba na Mtwara na itachezwa siku ya kufunga mashindano hayo Julai 2, 2021 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona wakati mchezo wa kumtafuta mshindi wa tatu soka utachezwa kesho baina ya timu ya mkoa wa Dodoma na Geita.

Amesema mchezo wa Soka kwa upande wa wasichana utakuwa baina ya timu ya mkoa wa Mwanza na Tabora ambao utachezwa mchana Julai 1,2021 ambapo hadi sasa mshindi wa tatu ni mkoa wa Arusha.  

Pia fainali ya Mpira wa Pete itakuwa dhidi ya timu ya mkoa wa Mwanza na Songwe

Kwa upande wa mpira wa Wavu fainali wasichana itachezwa baina ya mkoa wa Dar es Salaam na Mtwara wakati wavulana itakuwa kati ya Dar es Salaam na Arusha.

Mpira wa mikono fainali wasichana itakuwa baina ya mkoa wa Songwe na Morogoro na kwa upande wa wavulana Unguja watakipiga na Tabora.

Kwa upande wa mpira wa kikapu fainali kwa wanaume itakuwa baina ya Unguja na Dar es Salaam wakati kwa upande wa wanawake itakuwa baina ya Dar es Salaam na Mwanza.

Share:

Majaliwa: Wizara Kilimo Simamieni Kilimo Cha Ngano Na Zabibu


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo isimamie upatikanaji wa mbegu bora katika kilimo cha ngano na zabibu pamoja na kuweka mpango mzuri utakaosimamia na kuendeleza kilimo cha mazao hayo .

 “…Utoaji wa vibali kwa wanunuzi wa ngano na mchuzi wa zabibu ufanywe kwa kuzingatia wale ambao watathibitisha kununua malighafi hizo ndani kwanza. Hakikisheni mnasimamia vizuri makubaliano kati ya wakulima na wanunuzi wakubwa ili tusinunue bidhaa hizo kutoka nje.”

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Juni 30, 2021) wakati akiahirisha mkutano wa tatu wa Bunge la 12, Bungeni jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Agosti 31 mwaka huu.

Akizungumzia kuhusu fursa mpya ya kilimo cha soya, Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Kilimo ihakikishe inakuwa na mpango mzuri wa kuendeleza kilimo hicho kwa kuwapatia wakulima mbegu kwa kuanza na mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma.

Kadhalika, Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu masoko ya mazao ambapo kwa upande wa tumbaku, ameiagiza Wizara ya Kilimo ishirikiane na Wizara ya Fedha na Mipango kukamilisha mazungumzo na wanunuzi wa zao hilo hususan kipindi hiki ambacho bei yake inaonekana kuimarika kwenye soko la dunia.

“Pia nafahamu kuwa tayari tupo kwenye msimu wa pamba. Ninasisitiza kuwa wakulima wa pamba wasikatwe gharama za pembejeo kwa kuwa tayari zipo kwenye mjengeko wa bei. Kwa hiyo, nitoe wito kwa wakulima kupeleka sasa pamba yao kwenye minada ili waweze kunufaika na bei ya sasa.”

Kuhusu kilimo cha mkataba, Waziri Mkuu amesema wameamua kutumia utaratibu huo kwa baadhi ya mazao yakiwemo ya alizeti, ngano, shayiri na soya ili kumpatia tija mkulima, ambapo kwa upande wa soya soko la uhakika lipo nchini China.

“Kwa msingi huo, nasisitiza kwamba Wizara ya Kilimo hakikisheni mikataba inayoingiwa na wakulima inakuwa wazi ikionesha bei na kiwango cha kuuza. Vilevile, simamieni mikataba baina ya wakulima na wanunuzi wakubwa.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuipongeza Wizara ya Kilimo kwa wazo lao la kuwa na maghala kwenye nchi zenye fursa ya masoko. “Wafuateni wateja msisubiri waje kwenu kwani biashara ni ushindani.”

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Majaliwa: Tumepunguza Siku Za Kushughulikia Maombi Ya Vibali


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema utaratibu wa utoaji wa vibali vya ukaazi kwa kutumia mfumo wa kielektroniki umesaidia kupunguza hatua za kuchakata maombi kutoka siku 33 za hadi saba.

Amesema kuwa kwa sasa waombaji hawalazimiki kwenda katika Ofisi za Kazi kwa sababu taarifa zote zinapatikana kwenye mfumo na watajaza fomu moja tu ambayo huwa na taarifa zote za kazi na ukaazi tofauti na awali ambapo wawekezaji walilazimika kujaza fomu mbili.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Juni 30, 2021) wakati akiahirisha mkutano wa tatu wa Bunge la 12, Bungeni jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Agosti 31 mwaka huu.

Amesema miongoni mwa manufaa yaliyopatikana kupitia matumizi ya mfumo huo ni kupungua kwa siku za kushughulikia maombi ya vibali vya kazi kutoka siku 14 hadi siku tatu. “Hali hii, pamoja na mambo mengine, imesaidia kupunguza malalamiko ya kuchelewa kupata majibu ya maombi ya vibali vya kazi.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kupokea maoni kutoka kwa watumiaji wa mfumo kwa ajili ya maboresho na tayari imeshakutana na kupokea maoni ya wadau wa ndani na nje kikiwemo Chama cha Wafanyakazi, Chama cha Waajiri (ATE), Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI), Taasisi ya Sekta Binafsi na kuyajumuisha maoni hayo kwenye maboresho.

Amesema Serikali inakamilisha maboresho ya Sheria ya Kuratibu Ajira za Wageni (Sura 436) kwa kuainisha maeneo yaliyokuwa na changamoto za kiutendaji na kuathiri jitihada za kuimarisha mazingira ya uwekezaji nchini. Mfumo huo unatarajiwa kuzinduliwa rasmi Agosti mwaka huu.

“Sambamba na marekebisho hayo ya sharia, tangu tarehe 23 Aprili, 2021 tumeanza kutumia mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia maombi ya vibali vya kazi kwa raia wa kigeni na katika hatua za majaribio tayari maombi zaidi ya 500 yameshughulikiwa kupitia mfumo huo.”

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema ili kuhakikisha bajeti ya 2021/2022 inatoa matokeo yaliyokusudiwa, Serikali itaimarisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki kwa ajili ya kuongeza uwazi na uwajibikaji na hivyo kudhibiti matumizi ya fedha za umma kwa kuepuka malipo hewa na manunuzi ya umma ya bidhaa na huduma zisizokidhi viwango vya ubora.

Amesema Serikali itahakikisha uwepo wa thamani halisi ya matumizi ya fedha za umma katika utekelezaji wa miradi ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua stahiki tena kwa wakati pale inapobaini ukiukwaji wa sheria, taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za umma.

“Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2021/2022 unakwenda sambamba na Mikakati ya Serikali katika kuimarisha udhibiti wa matumizi ya fedha za umma, utendaji na uwajibikaji kwa viongozi na watendaji wote wa sekta ya umma. Hatua hizo, zinalenga kuhakikisha bajeti hii inatoa matokeo yaliyokusudiwa.”

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasisitiza watendaji wa Serikali hususan wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) wajipange vema na wahakikishe suala la posho za madaraka kwa watendaji wa kata na vijiji kupitia mpango wa halmashauri linasimamiwa na kutekelezwa ipasavyo.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wahakikishe wanatenga maeneo maalumu kwa ajili ya vijana na wafanyabiashara wadogo sambamba na kuwapatia elimu pamoja na kuwashirikisha katika kubaini maeneo yanayoendana na biashara zao. Amewaagiza watendaji hao wasikilize na kushughulikia kero za wananchi kwa wakati ikiwa ni pamoja na kutenga siku maalum kwa ajili hiyo.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Picha : TGNP YAENDESHA KONGAMANO LA TAFAKURI YA SIKU 100 ZA RAIS SAMIA ...'AMETUONESHA MWANGA, TUMPE USHIRIKIANO'

Share:

Waziri Mkuu Awataka Viongozi Waendelee Kusimamia Amani


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefungua mafunzo ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa mikoa na kuwataka viongozi hao waendelee kusimamia amani na utulivu kwenye mikoa yao ili watu waendelee kufanya shughuli zao bila wasiwasi wowote.

“Amani na utulivu ndiyo itatuwezesha kama nchi, tuendelee kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza mitaji yao hapa nchini. Tunakumbushwa sisi viongozi wa Tanzania tuwe wazalendo na tuhakikishe tunaziendeleza rasilimali za nchi hii kwa faida ya Watanzania wote.”

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Juni 30, 2021) wakati akifungua mafunzo ya siku nne yaliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa lengo la kuwaimarisha viongozi ili matokeo ya uongozi wao yawapatie majawabu endelevu wananchi dhidi ya changamoto mbalimbali zinazowakabili kwenye maeneo yao.  Mafunzo hayo yanafanyika jijini Dodoma.

Amesema baada ya mafunzo hayo Serikali inatarajia viongozi hao watasimamia kikamilifu nidhamu katika utumishi wa umma na kuwa kioo katika kuzingatia maadili na miiko bila kubagua jinsia, kabila, dini, rangi ya ngozi, mtu atokako ndani ya nchi ilimradi hajavunja sheria.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa mafunzo yatawawezesha viongozi hao kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika ofisi zao za mikoa na za Mamlaka za Serikali za Mitaa katika maeneo yao ya utawala na kuongeza udhibiti katika ukusanyaji na matumizi ya mapato ya ndani ya halmashauri.

“Mtazingatia kikamilifu mipaka yenu ya madaraka na hatua mtakazozichukua zitazingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Mtasimamia kikamilifu mapambano dhidi ya dawa za kulevya pamoja na kudumisha uhusiano baina yenu na watumishi walio chini yenu, kwa kuzingatia kuwa kila mtumishi anao mchango katika kuboresha utendaji kwenye kituo chake cha kazi.”

Waziri Mkuu amesisitiza viongozi hao kwamba lazima wawe makini muda wote na watumishi wazembe, wezi na wabadhirifu kwenye halmashauri zao lazima wote wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Serikali. Ameagiza ubadhirifu ushughulikiwe mapema kwa weledi na utaalam bila kulazimika kusimamisha utekelezaji wa miradi kwa muda mrefu.

 “Lazima watu wachache ambao wamezoea kupanga njama za kijinai kuiba au kutumia vibaya fedha za umma washughulikiwe kisheria kama upo ushahidi wa wazi kabla hata CAG hajakagua au viongozi wa juu wachukue hatua wakati ninyi mpo. Lazima mianya yote ya ubadhirifu izibwe na tusioneane haya.”

Pia, Waziri Mkuu ametoa wito kwa viongozi hao kuwa wa wakafanyeni kazi kwa uadilifu kulingana na viapo vyao na kila mmoja katika eneo lake awe msimamizi mzuri na kutanguliza mbele maslahi mapana ya Taifa, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Akizungumzia kuhusu miradi ya maendeleo kutokamilika kwa wakati na kwa ukamilifu, Waziri Mkuu amesema kuna changamoto ya baadhi ya miradi katika kutokukamilika kwa wakati na kwa kiwango kilichokusudiwa. “Pamoja na sababu nyingine tumebaini pia kuna baadhi ya viongozi huingilia michakato ya zabuni, manunuzi na ya ujenzi ikiwa ni katika hatua mbalimbali na wengine wanakwenda mbali zaidi kudai wapewe asilimia 10 ya fedha.”

“Nieleze bayana kuwa hili sasa tunalifuatilia kwa karibu na hatutakuwa na uvumilivu pale tutakapowabaini.  Nisistize kuwa Serikali ina macho mengi tutakapopata taarifa za baadhi yenu kujihusisha na vitendo vya ubadhirifu wa fedha za Serikali kupitia fedha zinazoletwa za Miradi ya Maendeleo au zile zinazokusanywa na Halmashauri hatua kali zitachukuliwa dhidi yenu.”

Mafunzo hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, David Silinde, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Festo Dugange.

Wengine ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - TAMISEMI; (Elimu), Gerald G. Mweli, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI (Afya), Dkt. Grace E. Magembe  na Afisa Mtendaji Mkuu, Taasisi ya Uongozi, Kadari Singo.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Serikali Kuendelea Kuunga Mkono Kazi Za Sanaa


Serikali kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) wameahidi kuendelea kuunga mkono kazi mbalimbali za sanaa hapa nchini.

Hayo yamesememwa leo jijini Dar es Salaam na Afisa Sanaa Mwandamizi toka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Abel Ndaga wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya utoaji wa tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali.

“Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wenye zamana na Sekta ya Sanaa kupitia BASATA tutaendelea kutoa ushirikiano na wasanii mbalimbali ili kuweza kufanikisha malengo ya kukuza sekta ya sanaa nchini.

Afisa Sanaa Mwandamizi Ndaga ameongeza kuwa kuelekea siku ya utoaji tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali wanataraji kuwa tuzo hizo zitakuwa zitatoa hamasa kwa vijana wengi hapa nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya utoaji tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali  Joseph Ndalu ameahidi kuwa tuzo hizo zitaweka historia kwa kushirikisha wasanii wa tansia mbalimbali.

“Katika tuzo hizi tunatarajia kuwa na wasanii wa tasnia mbalimbali kama wasanii wafilamu, bongo fleva na sanaa mbalimbali hivyo ni imani yangu tuzo hizi zitakuwa za kipekee sana”alisema Bw. Ndalu.

Tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali zitafanyika siku ya jumamosi Juai tatu katika Kituo cha Mikutano Cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam kuanzia saa moja jioni.


Share:

Basi La Abiria Laacha Njia Na Kugonga Nyumba

Basi kampuni la Ulamaa T 330 DGB lililokuwa likisafiri kwenda Arusha kutokea Mwanza limepata ajali alfajiri ya leo kwa kuacha njia na kugonga nyumba eneo la Mkolani darajani jijini Mwanza.

Imeelezwa kwamba ndani ya nyumba hiyo kulikuwa na Watu 6 ambapo hakuna taarifa za kifo bali Majeruhi tu ambao wamepelekwa Hospitali ya Butimba.

Chanzo cha ajali kinaelezwa kuwa ni baada ya Dereva wa Basi kulikwepa gari dogo kulikosababisha gari kuacha njia baada ya kushindwa kulimudu



Share:

National Individual Consultant at UNICEF

Job no: 541473 Contract type: Consultancy Level: Consultancy Location: Tanzania,Uni.Re Categories: Education, Innovation UNICEF works in some of the world’s toughest places, to reach the world’s most disadvantaged children. To save their lives. To defend their rights. To help them fulfill their potential. Across 190 countries and territories, we work for every child, everywhere, every day, to build a better […]

This post National Individual Consultant at UNICEF has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Bashe Aagiza Ras Tabora Kuwaondoa Watumishi Wa Manispaa Ya Tabora Waliochukua Mashamba Katika Mashamba Katika Skimu Inala


 NA TIGANYA VINCENT
NAIBU Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amemwagiza Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu kuwaondoa watumishi wote wa Manispaa ya Tabora ambao wamejimilikisha mashamba katika mradi wa Umwagiliaji wa Inala.

Alisema wamechukua maeneo hayo na kusababisha wananchi wanaozunguka mradi huo kukosa mashamba kwa ajili ya kulima kilimo cha mpunga.

Bashe alitoa kauli hiyo jana  wakati wa kufungua maadhimisho ya sherehe za siku ya Ushirika Duniani (SUD) ambapo Kitaifa inafanyika Mkoani Tabora na kilele kitakuwa tarehe 3 Julai mwaka huu.

Alisema licha ya Serikali kutumia fedha nyingi kujenga Bwawa hilo bado mradi huo haufanyikazi vizuri kama ulivyokusudiwa kwa sababu ya watumishi wa Manispaa ya Tabora kujimilikisha mashamba ambayo hawayalimi.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri huyo alimwagiza Mrajis wa Vyama Vya ushirika Nchini Dkt. Benson Ndiege kufanya miaka mitatu mfululizo  maadhimisho ya sherehe za siku ya Ushirika Duniani (SUD) katika Mkoa mmoja badala ya kila mwaka kuanga katika eneo jipya.

Alisema hali hiyo itasaidia kuleta matokeo chanya kutokana na Washirika kujifunza katika eneo mmoja kwa kipindi cha miaka mitatu.

Wakati huo Naibu Waziri amewataka vijana kujiunga na ushirika ili kuondoa dhana potofu kuwa Ushirika na wazee na watu waliochoka.

Alisema ushirika ndio silaha pekee itakayowasaidia wakulima kupanga katika masoko na kupata bei nzuri itakayowasaidia kuondoa katika umaskini.

Bashe alisema Serikali itaendelea kuunga mkono Ushirika ili hatimaye uweze kuwa msaada mkubwa kwa wakulima kuchangia katika pato la Taifa kutoka la sasa la asilimia 26 na kuongezeka Zaidi.

Alisema kilimo ndio Sekta inayotoa ajira kwa wananchi wengi ni vema ikachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la Taifa.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya ushirika Duniani mwaka huu ni Ushirika  pamoja tujijenge uya kwa ubora na tija.


Share:

Makamu Wa Rais Dkt.Mpango Awasili Nchini Ufaransa Kuhudhuria Jukwaa La Kizazi Chenye Usawa


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango  Juni 29, 2021 amewasili  Paris nchini Ufaransa  ambako atahudhuria Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa ( Generation Equality Forum) linalofanyika Paris Ufaransa kuanzia Juni 30 – Julai 2, 202.  Makamu wa Rais anamuwakilisha  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Jukwaa hilo.

Aidha, Makamu wa Rais alipata maelezo jinsi Ubalozi wa Tnazania unavyotekeleza Sera ya Diplomasia ya Uchumi katika eneo lake uwakilishi ambalo ni Ufaransa,  Hispania; Ureno; Algeria na Morocco.   Maelezo hayo yalitolewa na Mhe. Samwel Shelukindo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa. Pia Balozi Shelukindo anaiwakilisha Tanzania katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)

Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango amempongeza Balozi Shelukindo kwa uwakilishi mzuri katika nchi hizo na kumuhakikishia serikali itaendelea kutatua changamoto zinazojitokeza katika ubalozi huo. Amemtaka kuendelea kutafuta mahusiano na sekta binafsi zilizopo nchini Ufaransa kwa manufaa ya nchi zote mbili. Hapo kesho juni 30,2021 Makamu wa Rais  anatarajia Kuhudhuria ufunguzi wa Jukwaa la kizazi cha usawa lenye lengo la kuchagiza haki za usawa wa kijinsia kama zilivyokubaliwa katika mkutano wa Beijing wa mwaka 1995.


Share:

Project Coordinator – Covid19 Case Management at Save the Children

Child Safeguarding: Level 3 – The responsibilities of the post may require the post holder to have a regular contact with or access to Pregnant Women, Mothers and Children ROLE PURPOSE: The Project Coordinator will be responsible for delivery of the Save the Strengthening COVID-19 Case Management in Regional Referral Hospitals. He/ She will be […]

This post Project Coordinator – Covid19 Case Management at Save the Children has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Sub Regional Director for Eastern and Southern Africa at Plan International

Location: Nairobi, Tanzania Company: Plan International The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are most affected. Working together with children, […]

This post Sub Regional Director for Eastern and Southern Africa at Plan International has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Office Secretary at TANROADS

Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Executive Agency under the Ministry of Works and Transport, established under section 3 (1) of the Executive Agencies Act (Cap 245) and came into operation in July, 2000. The Agency is responsible for the Maintenance and development of the trunk and Regional road network in Tanzania. The Regional […]

This post Office Secretary at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Work Inspector/Road Work at TANROADS

Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Executive Agency under the Ministry of Works and Transport, established under section 3 (1) of the Executive Agencies Act (Cap 245) and came into operation in July, 2000. The Agency is responsible for the Maintenance and development of the trunk and Regional road network in Tanzania. The Regional […]

This post Work Inspector/Road Work at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

UHURU WA VYOMBO VYA HABARI NA MATARAJIO YA UONGOZI WA AWAMU YA SITA YA SERIKALI YA TANZANIA


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Uhuru wa vyombo vya habari ni miongoni mwa haki za msingi za kila raia wa Tanzania. Haki hii huwawezesha raia kupata na kutoa taarifa, kujieleza ili kutoa maoni yao katika masuala mbalimbali yenye maslahi yao. 

Pia, uhuru wa vyombo vya habari huchochea kukua kwa misingi ya haki za binadamu, demokrasia, na utawala bora.

 Kuwepo kwa misingi hii husaidia wananchi kushiriki katika uendeshaji wa nchi, kuchagua viongozi wanaowataka, kuhoji uendeshaji wa serikali pamoja na kufahamu masuala yanayoathiri maisha yao.

Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwepo na changamoto zinazoathiri au kuminya uhuru vya vyombo vya habari. Taasisi na asasi za kiraia zikiwemo Baraza la Habari Tanzania (MCT), Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA TAN), LHRC, na zinginezo zimeripoti matukio kadhaa kuashiria kuwepo kwa mazingira magumu kwa vyombo vya habari na wanahabari kutekeleza uhuru huu.

 Matukio hayo ni pamoja na kufutwa au kufungia vyombo vya habari, kutoza faini na karipio dhidi ya vyombo vya habari, ukamataji na uwekaji kizuizini kwa waandishi wa habari na vikwazo vya kisheria na kikanuni zinazodhibiti vyombo vya habari na wanahabari kutekeleza wajibu wao kwa uhuru.

Hata hivyo, kuapishwa kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Awamu ya Sita ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kunaleta matumaini ya kuwepo kwa mazingira wezeshi yanayohimiza uhuru wa vyombo vya habari nchini.

 Matumaini haya yanajikita katika nia thabiti ya Mhe. Rais Samia ya kuhakikisha vyombo vya habari vinatimiza wajibu wake wa kuhabarisha umma kwa uhuru.

Akizungumza wakati wa kikao chake na wahariri wa vyombo vya habari kilichoafanyika tarehe 28 June 2021, Mhe. Rais Samia alinukuliwa akihimiza vyombo vya habari vilivyofungiwa kufunguliwa huku akivitaka kuzingatia sheria na miongozo ya serikali. 

Aidha, Mhe. Rais Samia mbali ya kuelekeza kulindwa na kuheshimiwa kwa uhuru wa vyombo vya habari, alitoa hakikisho la serikali yake kuzingatia kuwepo kwa sheria zisizokwaza upatikanaji na usambazaji wa habari nchini.

Ni matumaini ya wanahabari nchini kwamba Mhe. Rais Samia ameonesha dhamira ya wazi ya kuweka mazingira mazuri yanayochagiza uhuru wa vyombo vya habari. 

Hata hivyo, ni wajibu wa kila chombo cha Habari na waandishi wa Habari kuutumia vizuri uhuru huu kwa kutimiza Wajibu kwa kuzingatia weledi na maadili katika kutafuat, kuchakata na kusambaza taarifa na habari mbalimbali zenye maslahi kwa umma.

 Daima watambue kwamba hakuna uhuru bila wajibu.
Share:

Material Engineer at TANROADS

Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Executive Agency under the Ministry of Works and Transport, established under section 3 (1) of the Executive Agencies Act (Cap 245) and came into operation in July, 2000. The Agency is responsible for the Maintenance and development of the trunk and Regional road network in Tanzania. The Regional […]

This post Material Engineer at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Senior Core Banking Systems Administrator at NMB Bank

Job Purpose Perform extensive business analysis and documentation of the requirements of complex product management projects coordinating with cross-functional resources to achieve project objectives. Main Responsibilities Support product life cycle team during product set up in the Core Banking system Partner internal with business stakeholders to understand technical trade-offs and, positioning, requirements architecture to drive […]

This post Senior Core Banking Systems Administrator at NMB Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 30,2021



















Share:

Tuesday 29 June 2021

Video : BAHATI BUGALAMA - UKOO

Share:

TUME YA UTUMISHI WA UMMA YAENDELEA NA MKUTANO WA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2020/2021 JIJINI DAR ES SALAAM

Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma wakiwa katika Mkutano leo 29 Juni 2021: Mheshimiwa Khadija A.M. Mbarak (kushoto) na Mheshimiwa Immaculata P. Ngwale (kulia) wakishiriki katika Mkutano wa Nne kwa mwaka wa fedha 2020/2021 unaofanyika Jijini Dar es Salaam. (Picha na PSC)
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nyakimura Muhoji (kushoto) akiwa na Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, Mhe. Balozi (Mstaafu) Daniel Ole Njoolay (katikati) na Mhe. Balozi (Mstaafu) John Haule wakishiriki katika Mkutano wa Tume leo 29 Juni 2021 unaofanyika Jijini Dar es Salaam.
Maafisa wa Tume ya Utumishi wa Umma: Bw. Peleleja Masesa, Katibu Msaidizi, Idara ya Rufaa na Malalamiko (kushoto), Bw. Evarist Mashiba, Afisa Sheria Mkuu (katikati) na Bw. Charles Mulamula, Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria (kulia) wakishiriki Mkutano wa Tume unaoendelea kufanyika Jijini Dar es Salaam. (Picha na PSC)
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger