Tuesday 29 October 2019

Muungano wa Tigo na Zantel unavyokusudia kuboresha soko la mawasiliano nchini

...
Sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi imekua kwa kiasi kikubwa sana katika kipindi cha muongo mmoja uliopita.

Katika kipindi hiki cha ukuaji huu makampuni ya simu yametanua wigo wa huduma na matumizi ya simu za mkononi imekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku kwa mamilioni ya Watanzania tofauti na zamani ambapo simu ilikuwa kama anasa na ni wachache tu waliweza kuwa nazo. Maendeleo haya yanazidi kukua siku hadi siku kutokana na kuongezeka kwa ubunifu katika teknolojia. 

Simu ya mkononi sasa imebadilika na kuwa si tu kifaa cha kupiga, kupokea na kutuma meseji baina ya watumiaji lakini pia imeleta mapinduzi katika namna tunavyoweka akiba ya fedha, kulipana, kulipa bili mbalimbali na kuendesha maisha yetu ya kila siku.  
 
Mfano wa namna ambavyo simu za mkononi zimebadili maisha yetu ni kampuni ya Tigo Tanzania. Mfumo wa Tigo Pesa wa kutuma na kupokea pesa unatupa nafasi ya kutumiana na kupokea pesa bila haja ya kwenda na kupanga foleni benki.

Vivyo hivyo wenye maduka na biashara mbalimbali nao wametengenezewa mfumo wa Tigo Pesa Merchant ambao unawapa uwezo wa kupokea malipo kutoka wateja wote wa Tigo Pesa ambao kwa sasa ni zaidi ya watu milioni 16.   

Tigo Tanzania pia ni moja ya makampuni yanayoongoza kwa kutoa huduma ya 4G ambayo ni teknolojia yenye ina kasi zaidi katika mawasiliano nchini.

 Huduma hii inakupa uhakika wa kutazama vitu kama videos mtandaoni bila wasiwasi wa kukwama kwama au hata kufanya mikutano kwa njia ya video (conferencing)

Hata hivyo katika siku za karibuni umekuwepo wasiwasi kwamba sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi imejaa watoa huduma ambao wengi hawana tija na wasiolipa soko afya katika kuhudumia wateja.

Hali hii inaelezwa kuleta changamoto kwa ubunifu na utoaji huduma wenye tija na viwango bora kwa wateja. 

Katika sekta nyingi za uchumi uwepo wa watoa huduma wengi huwa ni faida kwa mteja. Bahati mbaya ukweli huu haupo kwenye sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi. 

Utafiti unaonyesha kuwa kupunguza idadi ya watoa huduma katika sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi huwezesha makampuni machache yalipo sokoni kuongeza faida ambayo huwawezesha kuwekeza zaidi katika mitambo na teknolojia yenye kutoa huduma bora zaidi kwa wateja wake. 

Katika soko la Tanzania, siku za karibuni zimekuwepo hatua mbalimbali za kibiashara kupunguza watoa huduma ili kuongeza uwekezaji kwenye teknolojia na ubora wa huduma kwa wateja.

Makampuni mawili ya Tigo Tanzania na Zantel yamekuwa na mjadala kuungana. 

Hatua hii ya Tigo Tanzania na Zantel kuungana ni habari njema sana kwa wateja wa Zantel. Maana yake ni kwamba sasa wateja hao wa Zantel wataweza kufurahia huduma zote ambazo sasa wateja wa Tigo Tanzania wanazipata.

Muungano huo pia utasaidia sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi nchini kuendelea kuwa bunifu na kutoa huduma bora kwa mamilioni ya wateja wake nchi nzima.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger