
Rais Mwinyi ametoa pongezi hizo kwenye kilele cha CRDB Bank Marathon kilichofanyika leo Agosti 13 katika viwanja vya The Green vilivyopo Oysterbay jijini Dar es Salaam na kuwashuhudia washindi wakiondoka na mamilioni ya zawadi baada ya kuonyesha kasi kubwa kuliko wakimbiza upepo wengine zaidi ya 7,000 waliojitokeza na kushiriki.

“Fedha zinazokusanywa kutoka kwa washiriki wa mbio hizi za hisani zinaelekezwa kwenye matibabu ya Watoto wenye matatizo ya moyo pamoja na wanawake wenye ujauzito hatarishi. Mwaka huu fedha hizi zitajenga kituo cha afya kule Zanzibar, huu ni mchango mkubwa unaowagusa Watanzania wengi. Nawaomba wadau wengine nao waone namna wanavyoweza kushirikiana na serikali kuboresha huduma za afya,” amesema Rais Mwinyi.

“Benki ya CRDB inashirikiana na washirika wake kufanikisha mbio hizi. Niwapongeze kampuni ya Sanlam ambao niliwaona ikulu kule Migombani Zanzibar. Homgereni Sanlam kwa kuwa sehemu ya mchango huu mkubwa kwa jamii,” amepongeza Rais.

“Mwaka 2020 wakati tunaanza, zaidi ya watu 4,000 walishiriki na kufanikisha kukusanya shilingi milioni 200 zilizofanikisha upasuaji wa moyo kwa watoto 100 katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), pamoja na programu ya utunzaji mazingira ya pendezesha Tanzania,” alsema.

Alifafanua kuwa mwaka jana, jumla ya shilingi milioni 470 zilikusanywa kutoka kwa washiriki 6,000 ambazo zilitumika katika gharama za matibabu ya wagonjwa watoto 100 JKCI na wanawake wenye ujauzito hatarishi na walio na maradhi ya fistula katika Hospitali ya CCBRT.


“Hii si tu imekuwa ni heshima kwa Benki yetu lakini pia ni heshima kwa nchi yetu. Kwa utambulisho huu wa kimataifa, mbio za CRDB Bank Marathon zinavutia wakimbiaji kutoka mataifa mbalimbali ulimwenguni hivvo kuzifanya kuwa sehemu ya kutangaza utalii wa nchi yetu,” alisema Warioba.

Afrika Mashariki wagawana zawadi
Zawadi zenye thamani ya zaidi ya shilingi 100 zilizotolewa kwa washindi wote walioshiriki kilomita 42, kilomita 21, kilomita 10 na kilomita tano pamoja na kilomita 65 kwa waendesha baiskeli zilikwenda kwa wawakilishi kutoka karibu mataifa yote ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Kwenye mbio za kilomita 21 (nusu marathon), Watanzania waling’ara katika makundi yote mawili, yaani wanawake na wanaume baada ya Magdalena Crispin na Josephat Joshua kuongoza. Nafasi ya pili ilikwenda kwa Atalena Napule Gasper wa Sudan na Nangat Willy wa Kenya huku nafasi ya tatu ikikamatwa na Failuna Matanga wa Tanzania na Panuel Mkingo wa Kenya.
Ceclia Panga, Transfora Musa na Neema Kisuda waliwaongoza wanawake kukimbia kilomita 10 huku Shuemery Mohamed, Josephat Tiophil na Jonas John wakifanya hivyo kwa wanaume. John Msigwa, Danidi Kisoni na Justine Mbegu walikuwa moto wa kuotea mbali kwa wavulana waliokimbia kilomita tano.

0 comments:
Post a Comment