Tuesday 22 November 2022

TETEMEKO LA ARDHI LAUA WATU ZAIDI YA 40 INDONESIA

...

Tetemeko la ardhi limekikumba kisiwa kikuu cha Indonesia cha Java na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 40 na mamia kujeruhiwa, wamesema maafisa wa eneo hilo wamethibitisha.


Tetemeko hilo lenye ukubwa wa kipimo cha richa 5.6 lilipiga mji wa Cianjur magharibi mwa Java, katika kina kirefu cha kilomita , kulingana na takwimu za Utafiti wa Jiolojia wa Marekani.

Tetemeko hilo lilisikika katika mji mkuu Jakarta umbali wa kilomita 100, ambako watu waliokuwa katika majengo marefu walihamishwa. Maafisa wanaonya juu ya uwezekano wa kutokea kwa matetemeko mengine huku idadi ya vifo ikitarajiwa kuongezeka.

Eneo ambalo tetemeko hilo lilitokea lina watu wengi na linakabiliwa na maporomoko ya ardhi, huku nyumba zilizojengwa sio imara. Waokoaji wamekuwa wakijaribu kuwahamisha watu kutoka kwenye majengo yaliyoporomoka, na kufanikiwa kumuokoa mwanamke na mtoto wake, kulingana na ripoti za eneo hilo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger