Monday 18 March 2024

MVIWATA KUONGEZA USHIRIKIANO KIUCHUMI KUKUZA KILIMO

...

 

Na Christina Haule,  Morogoro

MTANDAO wa wakulima wadogo Tanzania (MVIWATA) unafanya juhudi za kuongeza 00pushirikiano ya kiuchumi  na kijamii kati ya nchi yetu na mataifa makubwa kama vile China na Brazil ili kuhakikisha wakulima  wanazalisha kwa wingi na kunufaika kutokana na jasho lao kupitia masoko yenye tija.

Hayo yameleezwa mjini Morogoro na Mkurugenzi MVIWATA,  Stephen Ruvuga, wakati akitambulisha taasisi ya Mashirikiano ya kimataifa Baobab  kutoka nchini Ghana na Brazil na taasisi ya Gorduana kutoka nchini China.

Anasema MVIWATA na mashirika hayo wanajadiliana namna ya wakulima wa mazao mbali mbali ikiwemo kahawa wanaweza kuzalisha kwa wingi na  kunufaika moja kwa moja kutoka kwa wanunuzi.

Anasema ushirikiano huo utaendelea kuwa mkombozi kwa kuhakikisha maisha ya wakulima wadogo yanakuwa bora zaidi kwa kuwezesha upatikanaji wa pembejeo na masoko ya mazao ya kimataifa  yenye tija.

Aidha Ruvuga alisema ujio wa taasisi hizo kubwa mbili umelenga kuanzisha ushirikiano kati ya wakulima wadogo wa hapa nchini hususani wanachama wa MVIWATA na wakulima na taasisi nyingine kutoka nchi za Ghana, Brazil  na China na kuboresha suala la kilimo nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo ya utambulisho Mkurugenzi wa taasisi ya Gorduana, kutoka nchini China, Jit Zhou, alisema kuna mahitaji makubwa ya kahawa nchini humo. 

“ China ni nchi yenye idadi kubwa ya watu, na awali hakukuwa na watumiaji wengi wa kahawa, kwa sasa idadi ya watumiaji wa kahawa nchini humo imeongezeka sana, hivyo  bidhaa hiyo inahitajika kwa wingi ili kukidhi mahitaji ya watumiaji. Alisema Zhou.

Naye Katibu Mkuu wa kampuni ya Baobab, Kyeretwice Opoku kutoka nchini Ghana alisema kuwa taasisi yake imepanga kushirikiana na wakulima  wa Tanzania kupitia MVIWATA  ili kuwezesha upatikanaji wa teknolojia ya kilimo na kuwafundisha wakulima kuzalisha mazao kwa kutumia mbolea za asili zisizo na kemikali  huku mkazo mkubwa ukiwa ni kuchechechemua uzalishaji wa mazao mbali mbali ikiwemo kahawa.

Akizungumza kuhusu fursa  hiyo kwa wakulima, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji, ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,  Dk Rose Rwegasira,  alisema  ujio wa mashirika hayo utasiadia kuongeza kasi ya uzalishaji wa mazao kwa kuwa kutaongeza upatikana wa pembejeo za kilimo  na masoko.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger