Sunday, 25 April 2021

BABA MATATANI KWA KUWACHOMA MAKALIO KWA PANGA LA MOTO WATOTO WAKE

...
Mfano wa panga likiwa kwenye moto
***
Mkazi wa Kata ya Marangu Mashariki wilayani Moshi, Baltazari Mtui anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaunguza makalio kwa kutumia panga la moto watoto wake wawili wa kiume.

Inadaiwa kuwa baba huyo aliweka panga kwenye moto kisha akawaunguza watoto hao ambao ni wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili katika Shule ya Msingi Lyasongoro.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Amon Kakwale alithibitisha kutokea tukio hilo Aprili 16, mwaka huu.

Via Mwananchi
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger