Tuesday 8 February 2022

SERIKALI YAELEKEZA WAFANYABIASHARA KUSHUSHA BEI YA VIFAA VYA UJENZI

...

Serikali imesema tathmini iliyofanyika imebaini ongezeko holela la bei ya vifaa vya ujenzi hususan saruji na nondo linasababishwa na wazalishaji wa bidhaa husika kufanya uzalishaji banifu.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Ashatu Kijaji amesema wamebaini ongezeko limesababishwa na kutokuwa na mfumo wa wazi wa usambazaji wa bidhaa kutoka kiwandani mpaka kumfikia mlaji wa mwisho.

Ameelekeza Wazalishaji na Wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi kushusha mara moja bei za bidhaa walizopandisha kiholela. Mamlaka za Udhibiti zimeagizwa kuchukua hatua dhidi ya walimbikizaji na wauzaji kupitia mlango wa nyuma (black market) wanaosababisha bei za bidhaa kupanda sokoni.



Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger