Tuesday 30 August 2016

Aliyedaiwa kuuawa na polisi azikwa saa 4.00 usiku

...
 
Mwili wa marehemu Stanslausi Kalinga (42) aliyefariki akiwa mikononi mwa polisi ulizikwa saa 4.00 za usiku nje kidogo ya Mji wa Mlowo baada ya ndugu zake kukubali yaishe.
Marehemu ambaye ameacha mke na watoto wanne alifariki akiwa mikononi mwa polisi jambo lililosababisha vurugu kutoka kwa wananchi ambao walitaka mwili uzikwe na polisi wenyewe.
Wananchi hao walisusia mwili tangu Agosti 27 hadi juzi usiku ambapo mwili ulirudishwa kutoka Hospitali ya Rufaa Mbeya ulikopelekwa kwa uchunguzi kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Ernest Paringo.
Hata hivyo hakuna majibu ya uchunguzi yaliyotolewa licha ya ndugu wa marehemu kushiriki katika kuufanyia uchunguzi mwili huo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger