Monday 29 August 2016

Sekta ya Elimu Yaongoza kwa Watumishi Hewa

...

Image result for Dkt. Ashatu Kijaji
Serikali imeendelea kufanya msako wa kuwabaini watumishi hewa ambapo mpaka kufikia tarehe 20 mwezi huu jumla ya watumishi 16,127 wamebainika kukosa vigezo vya kuajiriwa huku sekta ya elimu ikitajwa kuongoza.
Takwimu hizo zinatolewa na naibu waziri wa fedha na mipango Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa zoezi la ugawaji madawati kwenye kata 21 za halmashauri ya wilaya ya Kondoa ambapo amesema tatizo la watumishi hewa limeigharimu serikali fedha nyingi ambazo zingeweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
 
Awali katika zoezi hilo mkurugenzi wa halmashauri ya Kondoa Falesy Kibasa amesema licha ya zoezi la madawati kufanyika kwa ufanisi lakini bado wilaya hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa pamoja na waalimu.
 
Katika ugawaji huo mwenyekiti wa kamati ya elimu afya na maji ya halmashauri hiyo Zakaria Balajina amesema halmashauri imejiwekea mkakati wa kuyatunza madawati kwa kuwakabidhi kwa mikataba maalum wakuu wa shule ili waweze kuwajibishwa itakapobainika kumekuwepo na uzembe katika utunzaji wake.
 
Katika zoezi hilo jumla ya madawati 2,260 yamekabidhiwa katika hatua ya awali na linatarajiwa kuwa endelevu ili kukidhi mahitaji katika shule zote za msingi na sekondari.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger