Monday 22 August 2016

PROF NDALICHAKO AVINYOOSHEA KIDOLE VYUO VYA VETA

...

 

WAZIRI wa Elimu, Sayansi naTeknolojia, Profesa Joyce Ndalichako, ametoa mwezi mmoja kwa Mamlaka ya VETA kufanya tathmini ya mafunzo wanayotoa katika vyuo vyote nchini ili kuona kama yanaendana na matakwa ya serikali ya kuwa na wataalamu watakaofanya kazi kwenye viwanda.

Aliagiza hivyo alipofanya ziara katika chuo cha VETA kilichopo Kipawa, Dar es Salaam, ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake ambazo amekuwa akizifanya katika vyuo hivyo ili kuona namna vinavyotekeleza majukumu.Alisema katika vyuo ambavyo ametembelea amekuta changamoto za kuwepo kwa mashine zilizoachwa bila ukarabati kiais cha kushika kutu na nyingine nzima kutotumika wakati kukiwa na vyuo vinavyozihitaji.

“Ni vizuri kukawa na usawa wa mahitaji katika vyuo vyote vya VETA kwenye kila mkoa, kulingana na uhitaji na si vyuo vingine kuwa na vifaa na vingine kuvikosa”,alisema.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger