Monday 31 December 2018

ZITTO KABWE AANIKA ORODHA YA VITABU 49 ALIVYOSOMA MWAKA 2018

...
Tangu Mwaka 2012 nimekuwa naorodhesha vitabu nilivyosoma katika mwaka. Si vitabu vyote huviweka hapa kwani vingine huwa nasoma na kuviacha njiani ama kutopendezwa navyo au kwa kusahau tu. 

Vitabu vingine huwa vitabu rejea na huvirudia kwa ajili ya mafunzo ili kufanya maamuzi Fulani Fulani au kwa ajili ya ibada (kwa mfano Quran) au kwa sababu nyenginezo. Nafurahi kuwa hivi sasa kwenye mitandao duniani kote watu wamekuwa wakiorodhesha vitabu ili kujengana katika utamaduni wa kusoma. Barack Obama yeye alianza kuweka orodha yake mwaka 2015 na tayari ameshaweka orodha ya mwaka huu. Obama pia huweka orodha ya muziki aliyopenda mwaka huo. Inavutia.

Mwaka huu nimesoma vitabu 49 (kutoka vitabu 36 + 3 vya mwaka 2017). Wakati natoa orodha yangu 23/12/2017 nilikuwa bado nasoma riwaya za Jumba Maro ya Ally Saleh na The Feast of the Goat cha Mario Vargos Llosa ambazo nilizimaliza nikiwa Maputo, Msumbiji. 

Pia niliweza kuongeza Simulizi iitwayo Zeitoun ya Dave Eggers kuhusu kimbunga cha Katrina huko New Orleans, Marekani. Hii ni simulizi ya wahamiaji kutoka Syria walivyoshiriki kuokoa makumi ya watu kutoka kwenye maafa ya Hurricane Katrina.

Mwaka 2018 nimesoma mchanyato kidogo kuliko mwaka 2017 ambapo dhima (themes) kadhaa ziliniongoza. Hata hivyo bado njaa yangu ya kuwasoma madikteta duniani iliendelea kuniongoza kwa lengo la kupata ufahamu na maarifa ya namna ya kuchangia katika kuzuia nchi yetu kuangukia kwenye utawala wa Imla. Pia nilijaribu kutafuta majawabu ya changamoto hizo. Kwenye dhima hiyo nilisoma:


- The Death of Democracy: Hitler’s Rise to Power
Benjamin C Hett


- The Plots Against Hitler
Danny Orbach


- Franco: Anatomy of a Dictator
Enrique Moradiellos


1 The New Sultan: Erdogan and the Crisis of Modern Turkey
Oner Cagaptey


- How Democracies Die
D Ziblatt and S Levitsky


Kama nilivyopata kusema, ninapenda na kujivunia sana historia ya ukombozi dhidi ya ukoloni barani Afrika na haswa Ukombozi wa Kusini mwa Afrika. 

Mwaka huu niliongeza maarifa katika eneo hilo kwa kusoma sio tu habari nzuri za vyama vya ukombozi bali pia baadhi ya makosa waliyofanya viongozi wetu. SWAPO Captive kilichoandikwa na Bwana Angula ni simulizi muhimu sana kusoma ili kuona namna baadhi ya watu walivyoonewa kwenye harakati za ukombozi. Kwa jina la ukombozi watu huonewa, huteswa na hata huuwawa. Pia nilisoma kuhusu mashujaa wa ukombozi na athari kwa familia zao. Katika dhima hii ya Ukombozi nilisoma:


- Cuito Cuanavale: 12 Months of War That Transformed a Continent
Fred Bridgland


- Africa Tomorrow
Edem Kadjo


- Umkontho we Sizwe: The ANC Armed Struggle
Thula Simpson


- Mozambique: Sowing the Seeds of Revolution
Samora Machel


- 491 Days
Winnie Mandela


- Thabo Mbeki
Adekeye Adebajo


- Umkontho we Sizwe
Janet Cherry


- Chris Hani
Hugh Macmillan


- Being Chris Hani’s Daughter
Lindiwe Hani and Melinda Ferguson


- SWAPO Captive: A Comrade’s Experience of Betrayal and Torture
Oiva Angula


Pia nilisoma vitabu vya hali ya sasa ya Afrika Kusini baada ya ukombozi:


- No Longer Whispering to Power: The Story of Thuli Madonsela
Thandine Gqubule


- How to Steal A City: The Battle for Nelson Mandela Bay, An Inside Account
Crispian Olver


- How to Steal A Country? State Capture and Hope for the Future in South Africa
Robin Renwick


- Coalition Country: South Africa After the ANC
Leon Schreiber


Kama Mtanzania ninayejiandaa kwa majukumu muhimu ya kitaifa nimekuwa nikipenda kupata maarifa Zaidi kuhusu Historia ya Zanzibar. Mwaka 2018 niliongeza maarifa kwa kusoma vitabu kadhaa ikiwemo:


- The Threat of Liberation: Imperialism and Revolution in Zanzibar
Amrit Wilson


- Social Memory, Silenced Voices and Political Struggle: Remembering the Revolution in Zanzibar.
(Ed) W. Cunningham and M. Fouere


Vitabu vinavyofuata ni mchanyato wa riwaya, historia za watu na mataifa mengine, mafunzo ya uchumi na kadhalika. Vitabu vinavyohusu Marekani na utawala wao mpya chini ya Trump ni kwa lengo la kujifunza nini kinaendelea huko. Kitabu cha Deng Xiaoping nilipewa na ndugu yangu Harith Ghassany katika mjadala wa kisomi wa kutafuta modeli sahihi ya kimaendeleo kwa nchi zetu za Afrika.


- Pakistan: Personal Story
Imran Khan


- Making Africa Work: A Handbook for Economic Success
Gregg Mills, O Obasanjo, et al


- Sidetracked
Henning Mankell


- In Praise of Blood: The Crimes of Rwandan Patriotic Front
Judi Rever


- Thomas Sankara Speaks
Thomas Sankara


- A Higher Loyalty
James Comey


- State Secrets: Deathly High Stakes in the Corridors of Power
Quintin Jardine


- Deng Xiaoping and The Transformation of China
Ezra F Vogel


- Gorbachev: His Life and Times
William Taubman


- Tell Tale
Jeffrey Archer


- The Growth Delusion
David Pilling


- CTRL ALT DELETE: How Politics and The Media Crashed Our Democracy
Tom Baldwin


- Unhinged: An Insider’s Account of The Trump White House
Omarosa Manigault


- Fire and Fury: Inside The Trump White House
Michael Wolf


- Why The Dutch are Different
Ben Coates


- The French Revolution: What Went Wrong
Stephen Clarke


- An Extra Ordinary Life: A Passion for Service
V J Mwanga


- Uwajibikaji Ndani ya Kalamu Isiyokuwa na Wino
Ludovich Utouh


- Betting the House: Inside Story of the 2017 Elections
Tim Ross and Tom McTaguwe


- In Defence of Bolsheviks
Max Shachtman


- The Future That Works: Selected Writings of A M Babu
(Ed) Salma Babu and Amrit Wilson


- Our Commonwealth: The Return of Public Ownership in USA
Thomas Hanna


- Democracy, Direct Action and Socialism: A Debate of Fundamentals
Michael Foot and Sean M


Mwaka huu ukiwa unaelekea ukingoni, Wachapishaji wa Vitabu Mkuki na Nyota Publishers walichapisha upya vitabu vya harakati za Willy Gamba, mpelelezi maarufu barani Afrika. Rafiki yangu katika kusoma vitabu Fadhy Mtanga (ambaye pia ni adui yangu kwenye soka – maana yeye ni shabiki mandazi wa Manchester United FC na mimi shabiki wa mabingwa watarajiwa Liverpool FC) alininunulia vitabu vyote 4 vya Mzee Elvis Musiba. Nilikuwa na muda wa kutosha na kuvisoma vyote bila kuweka chini. Namshukuru sana Fadhy kwa zawadi yake murua kabisa. Vitabu hivi ni:


- Kikosi Cha Kisasi
A E Musiba


- Njama
A E Musiba


- Kufa na Kupona
A E Musiba


- Hofu
A E Musiba


Kitabu changu cha mwisho mwaka 2018 ni :


- Dear Ijeawele OR A Feminist Manifesto in 15 Suggestions
Chimamanda Adichie


Vitabu 3 vilivyonigusa sana
The Death of Democracy: Hitler’s rise to power cha Benjamin Hett kilinigusa sana kutokana na namna wanasiasa wanavyoweza kufanya makosa yenye kudidimiza nchi kwa sababu tu ya kulinda madaraka. Katika kitabu hiki somo kubwa ni namna Wabunge wa vyama vyote vya Siasa walivyomruhusu Adolf Hitler kutunga sheria inayompa mamlaka makubwa wakiamini kuwa Hitler ana nia njema na atawalinda. 

Wabunge wa Chama cha SDP ndio pekee walikataa, walizomewa, kuzodolewa na hata kuuwawa. Wengine walikimbilia uhamishoni. Ndani ya miezi michache, hata wale waliomwunga mkono Hitler walishughulikiwa na Taifa la Ujerumani likaingia kwenye taharuki kubwa na hatimaye vita vya pili vya dunia. 

Waliompa madaraka Hitler waliamini kuwa watamdhibiti. Hawakuweza. Historia kama hii ipo lakini wanaadam hatujifunzi tunarudia makossa hayo kila wakati katika nchi mbalimbali duniani.


How Democracies Die cha Ziblatt na Levitsky kilinigusa sana kwa kuwa kinatoa majawabu ya changamoto za demokrasia kuanguka. Licha ya kwamba ni kitabu maalumu kwa muktadha wa nchi ya Marekani, kitabu hiki nilicholetewa na rafiki yangu Rakesh Rajani, kinatazama mifano ya nchi mbalimbali duniani kama Colombia na njia walizotumia kuhami demokrasia (walitumia sana Bunge na Mahakama), Venezuela (jinsi mgomo wa vyama vya upinzani kutoshiriki chaguzi ulivyotoa nafasi ubwete kwa chama tawala) na hata Ujerumani ambayo hali yake nimeeleza hapo awali. 

Somo kubwa kabisa kutoka kitabu hiki ni kwamba ni lazima wadau wote wa demokrasia kushirikiana pamoja kupambana na udikteta bila kujali tofauti ndogo ndogo au kubwa kubwa miongoni mwao. Bila ushirikiano dikteta husaga saga kila mmoja. Ni Kitabu nashauri kila mwana demokrasia akisome.


Dear Ijeawele Or A Feminist Manifesto in 15 Suggestions cha Chimamanda Adichie ni kitabu kidogo sana kwa idadi ya kurasa. Kwa hakika ni barua ambayo Chimamanda kamwandikia rafikiye ambaye amepata mtoto wa kike na anamshauri amkuze vipi mtoto huyu. Kijitabu hiki kimenigusa kwa sababu kinatoa changamoto kadhaa kwa sisi wanaume katika malezi. 

Kuna mambo ambayo tunafanya tunaona kama ni msaada kumbe inapaswa kuwa wajibu kwa familia. Kwa mfano, mara nyingi husikia wanaume tukisema ‘leo nafanya kazi ya kulea mke wangu kasafiri’ ama kwa kimombo ‘baby-sitting’. Chimamanda anatuambia hapa, Baba mtoto hafanyi ‘baby-sitting’ bali anatimiza wajibu wake kama baba. Pia kinachoitwa ‘gender roles’ kwenye nyumba zetu kiasi kwamba tunazuia watoto wa kike kukua na kukuza vipawa vyao vyote. 

Nashauri wenye watoto wa kike wasome kijitabu hiki, wababa na wamama kwani kinaweza kuchangia kubadili mtazamo wako wa namna tunalea watoto wetu wa kike. Mapendekezo 15 ya Chimamanda unaweza usiyakubali yote lakini yana mafunzo mengi ambayo yanaweza kukufaa kwenye malezi ya mabinti zetu.


Heri ya Mwaka mpya 2019


Zitto Kabwe
Dar es Salaam
30/12/2018
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger