Sunday 30 December 2018

MWANAUME AFARIKI KWA KUBANWA KATIKATI YA MAPAJA YA MWANAMKE

...

Mwanaume mmoja katika kijiji cha Gionsaria,kaunti ya Kisii Nchini Kenya amefariki dunia baada ya mwanamke mmoja kumbana /kufungia kichwa cha mwanaume huyo katikati ya mapaja. 




Mkasa huo wa aina yake umetokea siku ya Ijumaa Disemba 28,2018. 


Chifu wa eneo hilo Bwana Oganda Matego amesema mwanaume huyo anayejulikana sana kwa jina ‘Doctor’,ambaye pia ni taniboi wa magari ya kusafirisha majani chaieneo hilo, alishikiliwa kichwa katikati ya mapaja/miguu na mwanamke mmoja huku rafiki wa mwanamke huyo ambaye pia ni mwanamke akiwa ameshikilia miguu ya ‘Doctor’na kumuinua hewani.


Bwana Oganda amesema inashukiwa kuwa wawili hao walikuwa wapenzi na kifo cha ‘Doctor’ kilitokea wakicheza ambapo Baada ya dakika moja mwanaume akaachilia kichwa na kugonga kichwa barabarani



Inaelezwa kuwa wanawake hao walimpeleka ‘Doctor’ katika hospitali ya wilaya ya Nyamache na madaktari walipompima wakabaini kuwa tayari alikuwa amefariki dunia.



Tayari wanawake hao wanashikiliwa na polisi kwenye kituo cha polisi cha Nyangusu huku wakisubiri kufunguliwa mashtaka.



Aidha baada ya habari ya kifo cha ‘Doctor’ kuwafikia majirani wa wanawake hao,waliamua kuchoma nyumba nne zinazomilikiwa na hao wanawake. 


Hali ya utulivu imeshuhudiwa kwa sasa na Chifu wa eneo hilo Bwana Oganda Matego amewasihi wakazi wa eneo hilo kutochukua sheria mikononi mwao kiholela.




Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger