Monday 31 December 2018

SIMBA YAONESHA UTII

...

Kocha wa Simba Patrick Aussems

Licha ya kukabiliwa na mechi ya klabu bingwa Afrika hatua ya makundi klabu ya Simba, imesema itasafiri siku ya Jumatano ya tarehe 2.01.2019, kuelekea visiwani Zanzibar kwa ajili ya kushiriki mashindano ya kombe la Mapinduzi yanayotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Simba imeeleza kuwa inaondoka na kikosi kamili ili kufanya vizuri kwenye mashindano hayo, na pia kuipa mazoezi timu hiyo ambayo inajiwinda na mechi ya kwanza ya kundi D ligi ya Mabingwa barani Afrika dhidi ya JS Saoura ya Algeria.

Mechi dhidi ya JS Saoura inatarajiwa kupigwa Uwanja wa Taifa hapa Jijini Dar es salaam siku ya Jumamosi ya tarehe 12 Januari saa kumi alasiri.

''Iwapo tutafuzu kuingia nusu fainali ya Mapinduzi, kikosi cha pili kitabaki Zanzibar na baadhi ya wachezaji, huku wengine wakirejea Dar es Salaam kuwakabili JS Saoura'', imeeleza taarifa ya Simba.

Aidha Simba wameeleza kuwa kwa kuwa fainali ya Mapinduzi itafanyika Januari 13, na kama watafuzu kuna uwezekano mkubwa wa baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza kurejea Zanzibar kucheza fainali hiyo.

Kwenye kombe la Mapinduzi Simba ipo kundi A na timu za Chipukizi, Mlandege, KMKM na Simba.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger