Monday 31 December 2018

HII NDIYO SABABU YA BASI LA MWENDOKASI KUUNGUA MOTO

...
Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (UDA-RT) imeeleza chanzo cha ajali iliyoyokea mchana Desemba 25, mwaka huu eneo la Ubungo Maji ilitokana na hitilafu ya mfumo wa umeme.


Taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa UDART, John Nguya kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa basi hilo lenye uwezo wa kubeba abiria 155 ,lilikuwa likitokea Kimara kwenda Gerezani lilishika moto kwenye injini na kuwatia hofu abiria na wananchi wengine.


Alisema kuwa moto huo ulidhibitiwa kwa ushirikiano wa wananchi waliokuwa eneo hilo,Jeshi la Zima Moto na Uokoaji , Jeshi la Polisi na wafanyakazi wa UDART kwa kutumia vifaa vya kuzima moto vilivyomo kwenye magari hayo.


“Tungependa wananchi wafahamu kwamba usalama wa mabasi yote ya UDA -RT umedhibitiwa kwa asilimia 100 kuwa matengenezo take yanafanyika kwa umahiri ,viwango vya kimataifa kwa wasimamizi na watalaam kutoka kampuni ya Xiamen Golden Dragon ya China, Cummings ya Marekani ya kimataifa na Voith ya Ujerumani.


“Ndani ya mabasi hayo eneo la injini vipo vizimia koto vitatu vilivyotengenezwa humor na kuzima moto baada ya koto kuzidi na ndivyo ilivyokuwa wakati wa tukio na pia mabasi makubea kuna vizimia moto vinne vyenye ujazo wa kilogramu tatu katika kila mlango mikubwa ya pande zote mbili kwa akili ya dharura,” alisema Nguya.


Nguya alisema kuwa kwa mujibu wa sheria katika mabasi yote makubwa vipo vizimia moto vine vyenye ujazo wa kilogramu tatu kila kimoja na milango mikubwa pande zorte mbili kwa ajili ya dharura na matumizi ya kawaida.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger