Tuesday 31 January 2017

BREAKING NEWS:HAYA HAPA MATOKEO KIDATO CHA NNE 2016





 


NECTA yaachia matokeo ya wanafunzi ambaowamemaliza kidato cha nne 2016 ,Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG tunaendelea kutoa huduma ya kuangalizia majina endapo unahitaji kujua matokeo yako;

ILI KUANGALIZIWA FANYA YAFUATAYO;

TAFADHALI FANYA YAFUTAYO KAMA UNATAKA KUANGALIZIWA;
1.TUMA  EXAM NAMBA ya form 4  KWENDA NAMBA 0652740927 mfano:s0710/0119/2016

2.HUDUMA HII UTATOZWA TSHS 1000 AMBAYO UTAITUMA 

KWA MPESA KWENDA NAMBA 0742289379

AU TIGO PESA KWENDA NAMBA 0652740927

UTAJIBIWA BAADA YA DK 1 TU.

TUMA PESA KWANZA NDIO UJIBIWE.

Matokeo yote yapo hapa > BONYEZA HAPA



Share:

Tathmini ya Matokeo ya Kidato cha nne 2016 -Tazama matokeo Hapa


  
Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2016 ambapo umefaulu wa jumla umeongezeka kwa 2.56% kutoka 67.53% mwaka 2015 hadi 70.09% mwaka 2016.

Katibu Mtendaji wa barza hilo, Dkt Charles Msonde amesema kati ya wanafunzi 408,372 waliofanya mtihani, jumla ya wanafunzi 277,283 wamefaulu, wakiwemo wasichana 135,859 sawa na asilimia 67.06 na wavulana 141,424 sawa na asilimia 73.26.

Kwa upande wa watahiniwa wa shule, Dkt Msonde amesema kuwa 244,762 sawa na asilimia 70.35 ya waliofanya matihani wamefaulu ikilinganishwa na wanafunzi 240,996 sawa na asilimia 67.91 waliofaulu mwaka 2015.

Kwa upande wa ubora wa ufaulu, amesema watahiniwa wa shule wenye ufaulu mzuri wa Daraja la kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60

Share:

Wanafunzi 10 Waliofanya Vizuri Zaidi Kitaifa Katika Matokeo Ya Kidato cha Nne 2016

Share:

Shule 10 Bora na 10 za Mwisho katika Matokeo Kidato cha Nne 2016


Leo January 31 2017 Baraza la mitihani Tanzania NECTA limetangaza matokeo ya kidato cha nne ‘CSEE 2016’.
Hapo chini kuna orodha ya shule 10  bora kitaifa na shule 10 zilizoshika mkia
Share:

Monday 30 January 2017

TANGAZO JIPYA LA KAZI MASWAYETU BLOG

Habari zenu,

Maswayetu blog inatafuta vijana 10 ambao watafanya kazi na blog hii kwa kupost habari mbalimbali kila zinapotokea na kushare sehemu mbalimbali.
Share:

MAALIM SEIF:NITAKUWA RAIS WA ZANZBAR

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema mgogoro wa Zanzibarna anaamkni atakuwa Rais Zanzibar.

Amesema, mgogoro visiwani humo utamalizika endapo viongozi wa vyama vyote va siasa watakaa chini kufanya mazungumzo.

Akizungumza katika mahojiano katika kipindi cha Funguka kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Azam, Maalim Seif alisema jambo la muhimu ni viongozi kukubali Zanzibar kuna tatizo.

Alisema anaamini kama kuna nia njema, maridhiano yanaweza kupatikana Zanzibar na migogoro yote ya kisiasa kumalizika.

“Hii naamini kabisa, kama kuna nia njema, kila upande ukubali Zanzibar kuna tatizo, ukubali kuna haja ya viongozi kupata ufumbuzi wa tatizo na watapata vipi, ni kwa kushirikiana pamoja,” alisema Maalim Seif aliyewahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

Alisema Serikali iliyopita ya Umoja wa Kitaifa, ilikuwa na mafanikio makubwa na kwamba anavyoona hakuna kitakachorudisha hali ile, kama si kwa vyama kushirikiana.

“Kila upande ukiona unawakilishwa itasaidia kuleta Wazanzibari pamoja,” aliongeza Maalim Seif.
Aidha, Maalim Seif alisema anajua kuna majaribio makubwa yanafanywa kutafuta ufumbuzi, hivyo ufumbuzi ni vema upatikane ili kuridhisha pande zote, na kwamba kuna njia nyingi ya kupata muafaka na hiyo ni pamoja na kufanyika mazungumzo, lakini ni baada ya kila upande kukubali kuwa Zanzibar kuna tatizo.

Akizungumzia kugombea tena nafasi ya urais mwaka 2020, Maalim Seif alisema ni vema kusubiri ili kuona hali ya kisiasa itakapofika wakati huo.

“Tusubiri kwanza wakati wake tuone kama tunafanikiwa au hatufanikiwi kwenye hili, halafu tutafanya maamuzi,” alisema Maalim Seif ingawa baadaye alisema kuwa karibuni anatarajia atakuwa Rais wa Zanzibar.

“Natarajia muda mfupi ujao, Inshaallah nitakuwa Rais wa Zanzibar,” alisema bila kufafanua anawezaje kuwa rais wakati hakushiriki uchaguzi mkuu wa Machi, 2016.

Akizungumzia mgogoro ndani ya CUF, Hamad alisema Msajili wa Vyama vya Siasa aliruhusu upande wa Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba kuchukua Sh milioni 369 ambazo ni fedha za ruzuku na kwamba baadaye chama kitashindwa kuzijibia matumizi yake.

Kuhusu hilo, alisema wamemwandikia Msajili, Gavana wa Benki Kuu (BoT) na pia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), waangalie hatua ya kuchukua.

Akizungumzia afya yake, alisema anamshukuru Mungu kwamba afya yake ni njema. Hata hivyo alisema tangu aondoke madarakani, amekuwa akijihudumia mwenyewe katika matibabu na si fedha za serikali ikiwa ni pamoja na matibabu nchini India.
Share:

MTUMISHI ASIEWASILISHA CHETI CHAKE IFIKAPO MACHI MOSI MWAKA HUU KAJIFUKUZISHA KAZI

MTUMISHI wa umma atakayeshindwa kuwasilisha cheti cha elimu na taaluma au “Index number” ya mtihani ili zihakikiwe na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), itakapofika Machi mosi mwaka huu, atakuwa kajiondoa kazini mwenyewe, imeelezwa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora), Angellah Kairuki alibainisha hayo mwishoni mwa wiki wakati akifungua Mkutano wa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
“Watendaji wakuu ninawaomba msimamie uhakiki wa vyeti ili watumishi wenu wafanye kazi kwa sifa stahiki,” alisisitiza Kairuki, katika taarifa iliyotolewa na wizara yake.
Aliongeza kwamba serikali ilisitisha ajira mpya ili kupisha kazi ya kuondoa watumishi hewa, ambayo imefika ukingoni na siku za karibuni, ajira zitarudishwa.
Akiwa mjini Dodoma, Septemba mwaka jana, wakati wa kuapishwa kwa wakurugenzi watendaji wapya 13 walioteuliwa Septemba 10, mwaka huu, Kairuki alisema kuanzia serikali imewaondoa watumishi hewa 17,201 kwenye utumishi wa umma na kazi hiyo inaendelea.
Kairuki aliwataka watendaji wakuu kuweka mikakati ya kuepuka watumishi hewa na kusimamia kwa dhati kwa sababu jambo hilo, limeumiza na kupoteza rasilimalifedha nyingi za serikali.
Alisema anatambua kuna wakala zenye upungufu wa watumishi, hivyo zinaingia gharama kubwa za kuajiri wafanyakazi wa mikataba, hata hivyo alielekeza kila Mtendaji Mkuu ajiridhishe kwa kuandaa taarifa ya mahitaji halisi ya watumishi.
Pamoja na hilo, Kairuki alielekeza wakala zenye watumishi wa mikataba zifanye tathmini na kuhakiki kama kweli watumishi hao wanahitajika kwa kuwa eneo hilo ni moja ya maeneo yenye ajira za mashaka kwa baadhi ya taasisi.
Aliongeza kuwa yapo malalamiko kuhusu suala la maadili na uwajibikaji yanayozigusa Wakala za Serikali.
Aliainisha masuala hayo ni pamoja na watumishi hewa, taarifa chafu za watumishi, matumizi mabaya ya madaraka na rasilimali za umma, kutosimamia ipasavyo utekelezaji wa mifumo ya utendaji kazi na wakati mwingine kutotekeleza majukumu ya msingi ya wakala.
Alifafanua kuwa amegundua kupitia taarifa mbalimbali kuwepo kwa changamoto ya mawasiliano hafifu kati ya wizara mama na wakala zilizo chini yao ambapo taarifa kutoka katika wakala hazichambuliwi inavyostahili na hata zinapochambuliwa na wizara mama, hazitoa mrejesho kwenda katika wakala.
Awali, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais (Utumishi), Dk Laurean Ndumbaro alizitaka wakala za serikali kuimarisha eneo la ufuatiliaji na tathmini ili kuimarisha utendaji kazi na kuleta mabadiliko yanayotarajiwa na Watanzania
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARY TAREHE 30.1.2017

Share:

Mahakama Yapiga marufuku amri ya Rais Trump kuzuia Watu Kuingia Marekani

Mahakama moja ya New York Marekani imeridhia ombi la wanaharakati waliokwenda Mahakamani kupinga amri ya Rais Donald Trump wa nchi hiyo, kupiga marufuku Wakimbizi wa Syria na raia wengine wa nchi sita za kiislamu kama Iran, Iraq, Somalia, Sudan, Libya na Yemen wasiingie Marekani.

Mahakama hiyo imeamuru wote waliozuiliwa kupitia amri hizo waachiwe ikiwa ni agizo la lililotolewa saa kadhaa baada ya kuwepo Ripoti kutoka uwanja wa ndege wa John F Kennedy New York kwamba watu kadhaa wamezuiwa kuingia Marekani wakiwemo wale ambao walikuwa wamepewa ruhusa kwenda kuishi Marekani kupitia mpango maarufu wa Green Card.

Tayari pia Raia wawili wa Iraq wameishitaki Mahakamani serikali ya Marekani baada ya kushikiliwa kwenye uwanja wa ndege wa John F. Kennedy New York na kuzuiwa kuingia Marekani ambapo inaripotiwa wakati huo kuna raia wengine 10 walikua wamezuiwa kuingia Marekani muda mfupi tu baada ya ndege kutua.
Share:

Picha: Treni ya abiria yapata ajali ikitokea Kigoma kwenda Dar

Treni ya abiria ya EXPRESS ikitokea Kigoma kuelekea Dar es salaam leo January 29 2017 imepata ajali maeneo ya Ruvu ndani ya mkoa wa Pwani ikiwa ni kilometa kadhaa kabla ya kufika kwenye jiji la Dar es salaam.
Shuhuda ambaye alikua ndani ya Treni hiyo amesema Behewa zaidi ya 10 zimepinduka na watu wanaendelea kuokolewa kwa kupitia Madirishani.

Share:

Friday 27 January 2017

Wazee 2 mbaroni kwa ubakaji, ulawiti watoto 11


WAKAZI wawili akiwemo Mustafa Kassimu (75) ambaye ni mganga wa tiba za asili katika wilaya ya Korogwe mkoani Tanga na fundi wa kushona nguo, Rashidi Singano (70) wa wilayani Lushoto, wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kubaka na kulawiti wanafunzi 11 wa shule za msingi.
Katika tukio la kwanza la Januari 24, mwaka huu, Polisi inamshikilia fundi cherehani huyo ambaye anaishi Kijiji cha Mshwamba Kata ya Lunguza wilayani Lushoto kwa tuhuma za kubaka na kulawiti kwa nyakati tofauti watoto 10 (majina yamehifadhiwa).
Mtuhumiwa huyo inadaiwa alitumia ushawishi wa kuwapa fedha kati ya Sh 300, Sh 600 hadi Sh 1,000 na kuwavizia njiani, kama mbinu ya kuwanasa watoto hao, ambao wote ni wanafunzi katika moja ya shule ya msingi iliyopo Kata ya Lunguza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba alithibitisha tukio hilo kwa kuwaeleza waandishi wa habari kwamba walipata taarifa za ukatili dhidi ya watoto hao kutoka kwa mwalimu wa watoto hao, ambaye jina lake limehifadhiwa.
“Tulipokea taarifa kuhusu tukio hilo kutoka kwa mwalimu wa shule wanayosoma watoto hao, akidai kwamba siku hiyo akiwa shuleni, aligundua kuwa wanafunzi kumi wa kike kati yao sita wote wakiwa wamebakwa, huku wengine wanne wakiwa wamelawitiwa kwa nyakati tofauti na fundi cherehani huyo,” alieleza.
Aliongeza, “Mwalimu huyo alitaja wanafunzi wengine watano na kudai kwamba hao wamenusurika kunaswa kwenye mtego wa kutendewa ukatili huo na Mzee Singano ambaye anaishi maeneo ya jirani na shule hiyo,” alieleza Kamanda Wakulyamba.
Alisema katika uchunguzi, imebainika kwamba mtuhumiwa alikuwa akifanya vitendo hivyo vya kubaka na kulawiti watoto hao ndani ya nyumba anayoishi pamoja na kufanyia shughuli hizo za ushonaji, na aliwapata wakati walipokuwa wakienda kupeleka nguo na wakati wa mchana wanapotoka shuleni kurejea nyumbani.
“Chanzo cha tukio hili kwa kweli ni tamaa mbaya za kimwili alizokuwa nazo mtuhumiwa ambapo alikuwa akiwalaghai wanafunzi hao kwa kuwapa fedha kati ya shilingi mia tatu hadi mia sita wakati wanapopeleka nguo zao kushonwa,” alifafanua.
Tukio la pili linamhusisha mtoto mwingine mwenye umri wa miaka 12, ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu (jina limehifadhiwa) wa Kijiji cha Fune wilayani Korogwe aliyelawitiwa na Kassimu (75) wakati alipokuwa akimpatia matibabu ya asili, yaliyolenga kumwongezea nguvu za kiume.
Share:

MAGAZETI YA LEO TZ NA NJE JAN 27.


Share:

Watu 14 akiwamo Mchina wafukiwa mgodini Geita

Watu 14 akiwemo Mchina, wanahofiwa kufa baada ya kufukiwa katika mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya RZ Union Mining Ltd uliopo Kata ya Nyarugusu mkoani Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga jana alisema watu hao wamefukiwa chini ya mgodi baada ya mlango wa kuingilia kwenye shimo la mgodi kumeguka udongo na kujiziba.

“Usiku wa kuamkia leo (jana) saa tisa kwenye mgodi huo unaoendeshwa na Wachina, mlango wa kuingilia mgodini mmoja ulimeguka na kujifunga watu 14 wakiwa ndani,” alisema Kyunga.

Kyunga alisema kwa mujibu wa kitabu cha orodha ya watu wanaojiandikisha kuingia mgodini, kuna majina ya Watanzania 12 na Mchina.

Aidha, alisema mbali na watu hao 13, pia kuna Mtanzania mmoja ambaye aliingia bila kujiandikisha na hiyo ni kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo hivyo kufanya idadi ya watu waliofukiwa kuwa 14. 
Kyunga alisema tangu jana asubuhi jitihada mbalimbali za kuondoa udongo kuwaokoa watu hao zinaendelea wakitumia mitambo na wataalamu.

“Kwa kusaidiana na Kampuni ya Geita Gold Mine (GGM) na wataalamu wengine, jitihada zinaendelea ili kuhakikisha tunawaokoa watu hao,” alisema Kyunga. 
Alisema wakati huo huo wamefanikiwa kutoboa eneo jingine na kupitisha mabomba ya hewa ya oksijeni ili kuwafanya watu hao wasikose hewa.
Share:

Tanzania na Malawi Kukutana Kujadili Sakata la Watanzania 8 Waliokamatwa

Tume  ya Ushirikiano wa Pamoja ya Kudumu (JPCC) kati ya Tanzania na Malawi, inatarajia kukutana nchini humo kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali, ikiwemo la Watanzania nane kukamatwa nchini humo kwa tuhuma za kuingia eneo la migodini bila kuwa na kibali.

Mbali na kujadili suala la Watanzania hao, lakini pia tume hiyo itajidili mgogoro wa mpaka uliopo baina ya nchi hizo mbili katika Ziwa Nyasa.

Mkutano huo unatarajiwa kuanza Februari 3 hadi 5 mwaka huu nchini Malawi.

Akizungumza Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mindi Kasiga alisema tume hiyo ilikuwa haijakutana kwa muda mrefu, jambo ambalo limesababisha watu kuwa na sintofahamu kati ya ushirikiano wa nchi hizo mbili.

Kasiga alisema mkutano wa tume hiyo, mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2003 jijini Dar es Salaam, hivyo kuwa kimya kwa muda mrefu kuna baadhi ya watu walidhani kuwa ushirikiano wa nchi hizo mbili si mzuri.

“Kikao kama hiki kilikaa miaka mingi kidogo… kuna masuala yaliyochelewa kutekelezwa kutokana na kukaa kwa kikao hiki, lakini kwa sasa yatatekelezwa kupitia vikao hivyo,” alisema Kasiga.

Aliongeza kuwa kwa mara ya kwanza, vikao hivyo vitashirikisha wafanyabiashara kutoka mikoa ya Njombe na Ruvuma, pia wavuvi kutoka katika mikoa hiyo ambao wataeleza namna wanavyofanya shughuli zao kwa kushirikiana na wenzao wa Malawi bila kuingilia.

Mindi alisema katika kikao hicho, ujumbe wa Tanzania utaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk Augustine Mahiga; na mbali na kujadili mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na Watanzania waliokamatwa, pia utajadili masuala mbalimbali katika sekta za biashara, elimu, kilimo pamoja na sekta zingine.

Kasiga pia alikabidhi tuzo za Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) walizoshinda kutoka Umoja wa Afrika (AU). SSRA ambayo imekuwa wa kwanza katika Tuzo za Ubunifu Katika Sekta za Umma Afrika (AAPSIA), ilikabidhiwa kikombe pamoja na cheti cha ushindi.

Ushindi huo wameupata kupitia mradi wao wa Mradi wa Kanzidata ya Taifa ya Sekta ya Hifadhi ya Jamii.
Bi Mindi akimkabidhi Bi. Sarah kombe la ushindi kwa niaba ya Wizara. Bi. Kibonde aliipokea zawadi hiyo kwa niaba ya Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
Meneja wa Mradi wa Mfumo wa Forodha wa TANCIS kutoka TRA akipokea zawadi ya cheti cha ushindi kutoka kwa Bi. Mindi Kasiga.
Share:

Mkuu wa Wilaya ajiuzulu, amwandikia barua Rais Dkt Magufuli

Aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Uyui Bw.Gabriel Mnyele akizungumza na Mwandishi wa habari wa Azam tv Juma Kapipi wakati akiwa ofisi za CCM Wilaya ya Uyui ikielezwa kuwa alikuwa ameitwa na Uongozi wa chama hicho kufuatia kuwepo kwa taarifa kwamba ameamua kuachia ngazi nafasi ya Ukuu wa wilaya hiyo ya Uyui jambo ambalo alilithibitisha kwa Katibu wa CCM wilaya ya Uyui kwamba ni kweli amemwandikia barua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli. 

 *****
Mkuu wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, Gabriel Simon Mnyele amejiuzulu nafasi hiyo leo Alhamisi Januari 26, 2017 na kuwaaga madiwani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano alioufanya wilayani humo.

Akieleza sababu ya kufanya uamuzi huo, Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa alimwandikia Rais Dkt Magufuli barua ya kujiuzulu nafasi hiyo akielezea kusongwa na majukumu binafsi.

Mkuu wa Wilaya, Gabriel Simon Mnyele alikuwa miongoni mwa Wakuu wa Wilaya 139 walioteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 26 Juni, 2016.
Bw.Gabriel Mnyele hakuwa tayari kuelezea maamuzi aliyochukua na kuwataka Waandishi waliokuwa wakihoji hatua ya maamuzi yake wasubiri tamko kutoka juu."Mimi sina la kusema kuhusu hilo nimeamua mwenyewe,kwani mmesikia kuwa nimetumbuliwa?Aliwahoji waandishi.
Share:

Thursday 26 January 2017

AUDIO | Linex Sunday Mjeda - Kiherehere | Download

Share:

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARY 26 2017


Share:

Wednesday 25 January 2017

Magazeti ya Leo Jumatano ya January 25 2017

Share:

NACTE:ORODHA YA VYUO VILIVYO RUHUSIWA KUDAHIRI WANAFUNZI KWA KIPINDI CHA MARCH / APRIL, 2017 KWA MWAKA WA MASOMO 2016 / 2017


 
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
(NACTE)


ORODHA YA VYUO VILIVYO RUHUSIWA KUDAHILI WANAFUNZI KWA
KIPINDI CHA MARCH/APRIL, 2017 KWA MWAKA WA
MASOMO 2016/2017




Share:

NACTE YAANZA KUPOKEA MAOMBI YA WANAFUNZI WANAOTAKA KUJIUNGA NA VYUO VYA AFYA,UALIMU,MIFUGO,KILIMO ETC NGAZI YA CHETI NA DIPLOMA MWAKA WA MASOMO 2016/2017 -MARCH /APRIL INTAKE

BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
(NACTE)

TAARIFA KWA UMMA

KUFUNGULIWA KWA MFUMO WA PAMOJA WA UDAHILI KWA KIPINDI CHA MACHI/APRILI, 2017 KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017 

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), linapenda kuutangazia Umma na wadau wote wa Elimu nchini, kuwa mfumo wa Udahili wa pamoja yaani “Online Central Admission System (CAS)”, umefunguliwa rasmi tarehe 23 Januari, 2017, saa 6 mchana, kwa kupokea maombi ya mwombaji katika kozi mbalimbali, ikiwemo ngazi ya, Astashahada na Stashahada kwa Kipindi cha Machi/April, 2017 kwa mwaka wa masomo 2016/2017.

Namna ya Kufanya Maombi
Maombi yote yafanyike kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) au kupitia chuoni ambapo mwombaji anapendelea kwenda kusoma, ambapo chuo kitamdahili mwanafunzi husika kwenye mfumo wa udahili kupitia “Institutional Panel”.

Tanbihi: Waombaji wa kozi za Afya waliohitimu Astashahada (NTA Level 5), pia wataomba kwa utaratibu ulioelezwa hapo juu.
Mwombaji wa Astashahada na Stashahada anaweza kuomba kwa ajili ya eneo moja au zaidi katika maeneo ya taaluma yafuatayo:
  1. Biashara, Utalii na Mipango, mfano; Uhasibu, Meneja Rasilimali Watu, Wanyama Pori, Mipango.
  2. Sayansi na Teknolojia Shirikishi, mfano; Kilimo, Uhandisi, Mifumo ya Mawasiliano, Usanifu Majengo, Mifugo.
  3. Afya na Sayansi Shirikishi, mfano; Uganga, Maabara, Ufamasia, Uuguzi.
Sifa za muombaji
  1. Awe amehitimu kidato cha nne mwaka 2015 au kabla ya hapo.
  2. Awe na Astashahada ya mwaka 2016 au kabla ya hapo kwa wanaojiendeleza.
  3. Sifa kwa kozi mahsusi ziko kwenye mwongozo wa kozi (Guidebook) ulioko kwenye mfumo (CAS).
Ada ya maombi ni kama ifuatavyo:
  1. Kwa eneo la Afya na Sayansi Shirikishi ada ya maombi ni Tshs 30,000/=.
  2. Kwa eneo moja kati ya maeneo mengine yaliyobaki, ada ni Tshs 20,000/=.
  3. Kwa zaidi ya eneo moja la taaluma, mfano; Afya pamoja na Biashara, ada ni Tshs 30,000/=, ambapo muombaji anaruhusiwa kuchagua maeneo yote.
Mwisho wa kutuma maombi haya ni tarehe 06/03/2017.

Muhimu: Hakutakuwa na muda wa nyongeza wa kufanya maombi. Hivyo waombaji wanashauriwa kuwa makini wakati wa kufanya maombi yao.

Angalizo: Kwa eneo la Mafunzo ya Ualimu na kozi ya Muhudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (Community Health Workers) hayatakuwepo kwenye udahili wa awamu hii.







Imetolewa na: 
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
23 Januari, 2017
Share:

Tuesday 24 January 2017

MSHINDI WA UBUNGE DIMANI AHAIDI KUWA DARAJA

Share:

TCRA YATAHADHARISHA MATAPELI WA NJIA YA SIMU

Share:

WANASIASA WANAOENEZA TAARIFA ZA UONGO KUHUSU NJAA KUKAMATWA

Naibu  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni ameonya kuwa watu wakiwemo wanasiasa wanaoeneza taarifa za uongo za kuwepo kwa baa la njaa, ni kosa na wachukuliwe hatua ikiwemo kukamatwa.

Masauni amesema bado kuna watu wanajichukulia mamlaka ambayo sio yao na kueneza uongo kuwa kuna njaa nchini, hilo ni kosa kwa kuwa kwa kueneza propaganda hiyo kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini.

“Hizo ni propaganda za watu wasioitakia mema nchi hii ….. mtu anapofanya kosa lazima achukuliwe hatua …… Jeshi la Polisi liangalieni hili,” alisisitiza.

Masauni alitoa onyo hilo wakati wa ziara yake ya siku moja aliyoifanya jana mkoani Rukwa ambako Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven alimhakikishia kuwa mkoa huo hauna njaa, bali una ziada ya kutosha.

“Nyie wenyewe mmemsikia mkuu wa mkoa (Zelothe) amethibitisha kuwa hakuna njaa mkoani hapa lakini sio hapa tu, pia mikoa ya Mbeya na Songwe wamenithibitishia kuwa hawana njaa,” alisema Naibu Waziri Masauni na kuongeza: 
“Sasa wapo wanasiasa uchwara wanaeneza propaganda kuna njaa, sio mamlaka yao kutangaza kuwa kuna njaa, kueneza uongo kama huo ni si sawa kwa kuwa kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini, wanastahili kuchukuliwa hatua ikiwemo kukamatwa,” alisisitiza.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe alimweleza Naibu Waziri Masauni kuwa hali ya kiusalama katika mkoa huo ni shwari ambapo amani na utulivu umeshamiri kwa kuwa una chakula cha kutosha.
Share:

WALIMU WATATU WAKAMATWA KWA KUPIGA DILI LA KUPOKEA MISHAHARA PRIVATE NA SERKALINI

Walimu watatu mkoani Mwanza wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la  kukimbia vituo vyao vya kazi na kufanya kazi shule binafsi huku wakiendelea kupokea mishahara ya serikali

Taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa Mwanza imewataja walimu hao waliokamatwa jana asubuhi katika mtaa wa Buhongwa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza,kuwa ni pamoja na Richard Mgendi (30), Rwiza Ntare (27) na Gilbert Makwaya (33).

Walimu hao kila mmoja ana story yake kama ifuatavyo:-

Mwalimu Richard Mgendi alikuwa akifundisha shule ya sekondari ya Misasi wilayani Misungwi, mwaka 2012 alimuaga mkurugenzi wa wilaya hiyo kuwa anakwenda kusoma Masters ya lugha (Linguistic) katika chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino, kwa kipindi chote hicho inadaiwa mwalimu huyo alikwenda kusoma na alipomaliza hakurudi katika shule yake ya awali bali alikuwa akifundisha shule binafsi ya sekondari iitwayo Musabe iliyopo Buhongwa huku akiendelea kulipwa mshahara kutoka serikalini.

Mwalimu Rwiza Ntare alikuwa akifundisha shule ya sekondari iitwayo Kigongo sekondari iliyopo wilaya ya Chato mkoani Geita ambapo mwaka 2015, alimuaga mkurugenzi wake kuwa anakwenda hospitali ya rufaa ya Bugando kupatiwa matibabu ya macho na vidonda vya tumbo lakini hakurudi tena bali inadaiwa alikuwa akifundisha shule binafsi ya sekondari iitwayo Musabe iliyopo mtaa wa Buhongwa huku akiendelea kulipwa mshahara na serikali.

Mwalimu Gilbert Makwaya alikuwa akifundisha Runima sekondari iliyopo maeneo ya Buhongwa na alimuaga mkurugenzi wa wilaya ya Nyamagana tarehe 27/09/2015 kuwa anakwenda kusoma Masters ya Hesabu katika chuo kikuu cha Mwenge kilichpo mjini Moshi lakini hakwenda bali alikuwa akifundisha shule binafsi ya Musabe iliyopo mtaa wa Buhongwa huku akiendelea kupokea mshahara kutoka serikalini.

Walimu wote watatu wapo katika mahojiano na jeshi la polisi na pindi uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani.
Jeshi la polisi linaendelea kuwatafuta baadhi ya walimu ambao wametoroka lakini inadaiwa wapo katika shule hiyo binafsi ya Musabe huku wakiendelea kulipwa mshahara na serikali pamoja na mkurugenzi wa shule hiyo.
Share:

MAJAMBAZI WAWILI 2 WAUAWA JIJINI MWANZA

Watu wawili waliokuwa wakituhumiwa kwa ujambazi wameuawa wakati wakitaka kujaribu kuwatoroka askari polisi wilayani Ilemela mkoani Mwanza

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza amesema kwamba tukio hilo lilitokea  tarehe 20.01.2016 majira ya saa 2:30  usiku, katika mtaa wa kiloleli “A” kata ya Nyasaka mkoa wa Mwanza na kuwataja majambazi waliouawa kuwa ni Eric Magese miaka 22, na aliyejulikana kwa jina moja la Peter miaka kati 25 hadi 27 wote wakazi wa Mecco jijini Mwanza.

Amesema majambazi hao waliuawa wakati wakijaribu kutoroka askari polisi pindi wakiwapeleka mahali ambapo wenzao wamejificha ili waweze kufanya uvamizi.

Amesema kuwa katika tukio hilo pia ilipatikana silaha moja aina ya short gun yenye namba TZ CAR 103283 ikiwa na risasi tatu ambayo inadaiwa walipora kwenye kampuni ya ulinzi iitwayo Malika Security Service Limited

Msangi amesema majambazi hao walikuwa wakitafutwa na polisi baada ya kufanya unyang’anyi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali jijini Mwanza ilikiwemo tukio la Kitangiri mnamo tarehe 19.12.2016 na tukio la tarehe 02.01.2016 katika mtaa wa Nyasaka.

Jinsi walivyouawa
Msangi amesema baada ya upelelezi uliofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao, walikubali kuwapeleka askari katika eneo ambalo walikuwa wamepanga pamoja na wenzao wawili kwa ajili ya kufanya matukio zaidi ya ujambazi.

Amesema walipofika katika eneo hilo, watuhumiwa hao walipiga kelele kama ishara ya kuwatorosha wenzao na kuanza kuwakimbia askari.

Askari walifyatua risasi kadhaa hewani wakiwaamuru wasimame lakini waligoma ndipo waliwafyatulia risasi za mguuni kwa bahati mbaya ziliwalenga maeneo ya juu ambapo walifariki dunia wakati wakipelekwa hospitali.
Share:

WARAKA WA ZITTO KABWE KUHUSU UCHAGUZI WA MARUDIO

Share:

TUNDU LISSU AFUNGUKA KUHUSU UPINZANI KUBURUZWA NA CCM UCHAGUZI MDOGO WA MARUDIO

Share:

KAULI YA MTATAIRO BAADA YA UPINZANI KUANGUKIA PUA UCHAGUZI MDOGO WA MARUDIO

Share:

KAULI YA RAIS MAGUFULI BAADA YA CCM KUSHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI MDOGO WA MARUDIO

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARY TAREHE 24.1.2017

Share:

Monday 23 January 2017

Bulembo amtaka Lowassa Aachane na Siasa

Share:

Hatimaye Jecha Afunguka Kuhusu Kufuta Uchaguzi Zanzibar...

Share:

Bibi Akutwa amekufa Huku akiwa na vibuyu 5 na kuku mweupe

Bibi  mwenye umri wa miaka 60 amekutwa amekufa mkoani Tabora huku amevaa nguo nyeusi aina ya kaniki, akiwa na vibuyu vitano na kuku mweupe, katika mazingira yanayoashiria kushiriki vitendo vya kishirikina.

Aidha, mwili wa mtu mwingine umekutwa pembeni ya mti aliokuwa akichimba dawa.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Hamis Selemani iliwataja waliokutwa wamekufa kuwa ni Nsoma Dotto (60) mkazi wa Kijiji cha Zugimlole Wilaya ya Kaliua na Mayara Marashi (50) ambaye ni mkazi wa Igunga.

Kamanda Selemani alisema Nsoma alikutwa akiwa amekufa umbali wa mita 200 kutoka nyumbani kwake juzi.

Alisema bibi huyo alikutwa amevaa nguo nyeusi aina ya kaniki akiwa na vibuyu vitano huku pembeni yake kukiwa na kuku mweupe. Uchunguzi wa awali wa jeshi hilo, unaonesha kuwa huenda ni imani za kishirikina.

Aidha, alisema Marashi ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Mwakapinga, Kata ya Nanga, aliyekuwa mganga wa kienyeji, mwili wake uliokotwa Januari 16, mwaka huu ukiwa umeanza kuharibika.

Kwa mujibu wa Kamanda Selemani, mganga huyo wa kienyeji aliondoka nyumbani kwake Januari 8, mwaka huu kwenda porini kuchimba dawa, lakini hakurudi kijijini hadi maiti yake ilipookotwa akiwa amekufa.

Alisema Polisi wanaendelea na uchunguzi wa kifo hicho. Aliwaomba wananchi wanaoenda porini kwa ajili ya shughuli zozote zile, wawe wanatoa taarifa kwa ndugu zao ili iwe rahisi tatizo linapotokea.
Share:

Rais wa Uturuki Awasili Nchini Kwa Ziara ya Kikazi

RAIS wa Uturuki Mheshimiwa Recep Erdogan amewasili nchini jana jioni (Jumapili, Januari 22, 2017) kwa ziara ya kikazi ya siku mbili na kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere  na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na niaba ya Mheshimiwa Rais. Dkt. John Magufuli.

Rais huyo ameambatana na mkewe Mama Emine Erdogan pamoja na Mawaziri watatu ambao ni Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Mevlüt ÇavuÅŸoÄŸlu, Waziri wa Uchumi Mheshimiwa Nihat  Zeybekekci na Waziri wa Nishati na Maliasili Mheshimiwa Berat Albayrak

Pia Rais huyo ameambatana na wafanyabiashara wapatao 85 wa nchi hiyo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa   na Rais wa Uturuki, Mheshimiwa Recep Tayyip Erdogan  aliyefuatana na  mkewe, Mheshimiwa Emine Erdogan (kulia) wakifuhia ngoma kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage jijini Dar es salaam baada ya Rais huyo  kuwasili kwa ziara rasmi nchini Januari 22, 2017. Mheshimiwa Majaliwa alimpokea Rais huyo kwa niaba ya Rais John Magufuli. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Share:

Zitto Kabwe Asakwa na Jeshi la Polisi kwa Uchochezi,ACT Wazalendo Wadai Yuko Salama, Wataka Polisi Wafuate Utaratibu

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARY TAREHE 23.1.2017

Share:

Sunday 22 January 2017

MH RAIS MAGUFULI AMTEUA ANNE KILANGO MALECELA KUWA MBUNGE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,  tarehe 21 Januari, 2017 amemteua Anne Kilango Malecela kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Anne Kilango Malecela ataapishwa kwa mujibu wa taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

21 Januari, 2017
Share:

Saturday 21 January 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARY TAREHE 21.1.2017

Share:

Friday 20 January 2017

Donald Trump Kukabidhiwa Leo IKULU Ya Marekani


Mshindi wa uchaguzi mkuu wa mwezi Novemba Donald Trump leo anatarajiwa kuapishwa kuwa rais wa 45 wa Marekani.

Bw Trump wa Chama cha Republican anatarajiwa kuapishwa mbele ya watu 750,000 mbele ya majengo makuu ya bunge la Marekani, Capitol Building, Washington D.C.

Kisheria, rais anafaa kuapishwa kabla ya saa sita mchana saa za Amerika Mashariki ambazo Afrika Mashariki ni saa mbili usiku.

Hii hapa ni ratiba fupi ya matukio yanayotarajiwa siku hiyo.
Saa 17:30 (Saa za Afrika Mashariki) Wanamuziki walioalikwa wataanza kutumbuiza.

19:30 Hotuba za kufungua sherehe zitaanza kutolewa.

20:00 Muda mfupi kabla ya saa Mbili Afrika Mashariki Donald Trump atalishwa kiapo cha kuwa rais wa Marekani na Jaji wa Mahakama ya Juu John Roberts.

Baadaye, kutakuwa na msafara baada ya sherehe ya kuapishwa ambao utaanza katika vidato vya jumba la Capitol Building kuelekea ikulu ya White House kupitia barabara maarufu ya Pennsylvania Avenue.

Bw Trump na mkewe Melania baadaye watacheza dansi katika matamasha matatu, mawili katika ukumbi wa mikutano wa Walter E Washington na jingine katika ukumbi wa Jengo la Makumbusho ya Taifa.

Miaka minane iliyopita, Rais Obama alipokuwa anaapishwa kura rais, waliohudhuria walikuwa watu 1.8 milioni.
 
Siku moja baada ya kuapishwa kwa Bw Trump, wanawake takriban 200,000 wanatarajiwa kuandamana Washington DC na miji mingine kumpinga Bw Donald Trump.

Hillary Clinton na mumewe Bill wamethibitisha kwamba watahudhuria sherehe hiyo, sawa na George W Bush na mkewe Laura.

Wamesema wanataka “kushuhudia kukabidhiwa madaraka kwa rasi mwingine kwa njia ya amani.”

Rais mwingine wa zamani Jimmy Carter atahudhuria pia, lakini George HW Bush, 92, na mkewe Barbara hawataweza kwa sababu za kiafya.

Chanzo: bbcswahili
Share:

TAARIFA KWA UMMA: MAOMBI YA NAFASI 1000 ZA MAFUNZO YA STADI ZA KUTENGENEZA VIATU


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA WAZIRI MKUU

Image result for SERIKALI YA TANZANIA
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger