Habari wakuu,
Moja kwa moja kutoka bungeni Dodoma, leo tunaanza safari yetu yetu ya hitimisho kuhusu Escrow, japo kuna zuio la mahakama jana spika alisema bunge lina kinga na hakuna atakaezuia bunge lisijadili ripoti. Zitto pia amesema kamati ya PAC itawasilisha ripoti yake kama ratiba ilivyosema. Baada ya pilikapilika za usiku Dodoma tusubiri kitachojiri bungeni leo.

Hakikisha kifaa unachotumia kutembelea JamiiForums kina chaji ya kutosha kutokana na hofu ya TANESCO pia kifurushi chako kiwe kinatosha kuperuzi hii kurasa mara nyingi iwezekanavyo.
============================== ===========================

Kamati ya Uongozi imekutana sasa hivi

Bunge limeanza na aliekalia kiti leo ni mwenyekiti wa bunge, mheshimiwa Zungu kuna maelezo juu ya malalamiko ya walimu, maelezo yanatolewa na upande wa serikali

Swali: Wapo watumishi kama wauguzi wanadai zaidi ya milioni 100, japo kulikuwa na ahadi swala hili litashuhulikiwa, lakini hadi leo, nini kauli ya serikali?