Saturday 30 November 2019

SERIKALI YAANZA MCHAKATO WA KUPANDIKIZA FARU WEUPE NCHINI KWA MARA YA KWANZA


Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Khamis Kigwangala  akiwa na baadhi ya wasanii wa muziki na filamu katika hifadhi ya Burigi Chato

Na Ashura Jumapili - Malunde 1 blog 

WIZARA ya Maliasili na Utalii ipo katika mchakato wa kupandikiza Wanyama zaidi wa aina mbalimbali katika hifadhi mpya ya Taifa ya Burigi Chato wakiwemo Faru weupe ili iweze kuwa kivutio kwa watalii mbalimbali ambao wameanza kutembelea hifadhi hiyo.

Akiongoza zoezi la utalii wa kutembea kwa miguu akiwa amefuatana na wasanii wa muziki na filamu katika hifadhi hiyo, mpya iliyopo katika mikoa ya Kagera na Chato Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Khamis Kigwangala amesema kwa mara ya kwanza Serikali ya Tanzania imeamua kupandikiza Faru weupe katika hifadhi ya Burigi Chato.

Alisema utatifi bado unaendelea wa kuangalia namna ambavyo Faru hao weupe wataweza kuishi katika hifadhi hiyo kwa sababu hawakuwahi kuwepo kabisa hapa nchini.

Alisema ,Asili ya Faru weupe wanazaliana kwa wingi na kwa haraka hivyo wakipandikizwa katika hifadhi hiyo watasaidia sana kukuza idadi ya Faru weupe katika nchi na pia kuendelea kuwahifadhi kwa faida ya dunia nzima.

Pia alisema utafiti wa kupandikiza Faru weusi katika hifadhi hiyo umekamilika na malisho yapo ya kutosha na kudai kuwa asili ya hifadhi ya Burigi Chato ni nchi ya Faru historia inaonyesha kulikuwa na Faru wengi.

Alisema pia wamesha peleka familia moja ya Simba kutoka hifadhi ya Serengeti Mkoani Mara na kudai kuwa bado wapo kwenye uzio na wataachiwa rasmi baada ya wiki mbili.

 Msanii wa filamu Steven Mengele maarufu kama (Steve Nyerere) alisema hifadhi ya Burigi Chato ilichelewa sana lakini awamu ya tano imewekezekana chini ya msimamizi wake Khamis Kigwangala na wizara nzima ya maliasili na utalii.

Mengele,alisema Burigi Chato ndio mbuga ya kwanza yenye Twiga warefu na weusi pia ina kila vivutio alivyowahi kuviona.

Single Mtamabile,maarufu kama (Rich )alisema kutembelea hifadhi unapata uzoefu mkubwa sana katika mambo ya uhifadhi wa mazingira na utalii.

“Sisi wenyewe tulikuwa tunaona ni kawaida lakini tulipofika katika hifadhi hii ya Burigi Chato tumeona na kujifunza vitu vingi katika masuala ya Utalii”,alisema Mtambalike.

Alisema kujenga tabia ya kutembelea hifadhi za Taifa unakuwa unalinda asili yako na rasiliamali za nchi kwa kufika kujifunza na kuelewa namna ya kuendelea kutunza na kuhifadhi mazingira.
Share:

Picha : SHIRIKA LA FIKRA MPYA LAENDESHA KONGAMANO KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA




Shirika lisilo la kiserikali liitawalo Fikra Mpya la Mkoani Shinyanga, linalofanya shughuli ya kutoa elimu ya kujitambua kwa mtoto wa kike, limeendesha Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi wa kike kutoka Shule za Sekondari Nane Mjini Shinyanga.


Kongamano hilo limefanyika leo Novemba 30, 2019, kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Ualimu mjini Shinyanga (Shycom), na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo, wakiwemo maofisa ustawi jamii, maendeleo, dawati la jinsia kutoka polisi, walimu, pamoja na wazazi.

Mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya Leah Josiah, amesema wameendesha Kongamano hilo kwa wanafunzi wa kike, ili kutoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia, ikiwemo kutokomeza tatizo la mimba na ndoa za utotoni, ambalo limekuwa likizima ndoto za wanafunzi walio wengi.

Amesema wameendesha Kongamano hilo kama sehemu ya kuadhimisha siku 16 za kupinga Ukatili wa kijinsia, ambayo ilianza kuadhimishwa Novemba 25 mwaka huu na itahitimishwa Desemba 10, kwa kufanya mijadala mbalimbali ya kujadili namna ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto na wanawake.

“Shirika letu tumeamua kuendesha Kongamano hili la kupinga vitendo ya ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi wa kike, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, ambapo tunajadili kwa pamoja na wanafunzi ili kupata suluhu ya kutokomeza ukatili na wanafunzi wapate kutimiza ndoto zao,” amesema Josiah.

“Mkoa wetu wa Shinyanga na Kanda ya ziwa inatajwa kuongoza kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto na wanawake, ambapo takwimu zinaonyesha kuanzia Januari hadi Juni 2019 kanda ya ziwa inaongoza kwa asilimia 38, ikifuatiwa na mikoa ya nyanda juu kusini asilimia 32, Pwani asilimia Tisa (9),

“Kanda ya kaskazini asilimia Tisa (9), Kanda ya Kati asilimia Saba (7), pamoja na Kanda ya Magharibi asilimia Tano (5),”ameeleza Josiah.

Naye mgeni Rasmi kwenye Kongamano hilo Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda, akimwakilisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, amewataka wanafunzi wanapokuwa wakifanyiwa vitendo vya ukatili wasikae kimya, bali watoe taarifa ili wahusika wapate kuchukuliwa hatua na kukomesha vitendo hivyo.

Nao baadhi ya wanafunzi akiwemo Mariamu Charles kutoka Shule ya Sekondari Mwasele, wameshukuru kuendeshwa kwa Kongamano hilo, ambalo wamedai limewasaidia kuwapatia upeo namna ya kupinga vitendo ya ukatili wa kijinsia, pamoja na wapi pa kwenda kutoa taarifa hizo.


TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI

Mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya Mkoani Shinyanga Leah Josiah akizungumza kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia leo Jumamosi Novemba 30,2019. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog

Mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya Mkoani Shinyanga Leah Josiah akizungumza kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Mgeni Rasmi Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda akimwakilisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akizungumza kwenye Kongamano la Kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi wakiwa kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi wakiwa kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi wakiwa kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wageni waalikwa wakiwa kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Mratibu kutoka Shirika la Women Fund Tanzania Mkoani Shinyanga Glory Mbia, akifungua mjadala wa kujadili juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia na kutafuta suluhu ya kuvitokomeza.

Mwenyekiti wa baraza la watoto manispaa ya Shinyanga Rose Matiku akichangia mada kwenye Kongamano hilo la kupinga ukatili wa kijinsia.

Afisa wa Jeshi la Polisi kutoka dawati la Jinsia wilaya ya Shinyanga Joseph Christopher, akichangia mada kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia, wakwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya Leah Josiah.

Mzazi Aida Luben akichangia mada kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Mwandishi wa habari Isack Edward kutoka Radio Faraja, akichangia mada kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia namna vyombo vya habari vinavyosaidia kutoa elimu ya kutokomeza matukio hayo.

Mwanafunzi Verynice Busanga kutoka Shule ya Sekondari Mwasele, akichangia mada kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Mwanafunzi Mariam Charles kutoka Shule ya Sekondari Mwasele akichangia mada kwenye Kongamano hilo la kupinga ukatili wa kijinsia.

Awali wanafunzi wakiingia kwa maandamano kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa Kijinsia.

Mgeni Rasmi afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda akipokea maandamano kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wageni waalikwa wakiwa na mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumaliza Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wageni waalikwa, wanafunzi pamoja na mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya ,wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumaliza Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.


Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog
Share:

SIMBA SC YAMTIMUA KOCHA PATRICK AUSSEMS

Share:

Mbowe Arejesha Fomu yake ya Kugombea Uenyeki CHADEMA, Tundu Lissu Kuwa Makamu Mwenyekiti

Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Tundu Lissu amesema atagombea Makamu Mwenyekiti wa chama hicho katika Uchaguzi unaoendelea kufanyika hivi sasa ndani ya chama hicho.
 

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe wakati akirejesha fomu yake ya kuwania Uenyekiti wa chama hicho kwa Katibu wa Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini.

Mbowe amesema kuwa "Sisi viongozi tunafahamiana historia zetu na umadhubuti wetu, baada ya mashauriano tumemuelekeza Tundu Lissu ajaze fomu ya kuomba nafasi ya Makamu Mwenyekiti, na amefanya hivyo japo hatuzuii mwingine yoyote kujaza nafasi hiyo"

"Kwa sababu Prof. Abdallah Safari (Makamu Mwenyekiti CHADEMA Bara) anaondoka, wamejitokeza Watanzania kadhaa kujaribu kugombea nafasi hiyo, kwa kuwa tunahitaji viongozi" amesema Mbowe


Mbowe alichukuliwa fomu hiyo na wanachama waliochanga Sh1 milioni kulipia gharama na kumkabidhi. Baada ya kuipokea mbunge huyo wa Hai aliikabidhi kwa katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa.

Mara baada ya kukabidhi fomu hiyo, wanachama waliofurika katika ukumbi unakofanyika mkutano huo walishangilia

Kwa sasa chama hicho kimeingia kwenye Uchaguzi wake wa ndani ngazi ya Kikanda ambapo Desemba 18, ndiyo uchaguzi wa nafasi ya Mwenyekiti utafanyika.


Share:

NHIF Yatoa Ufafanuzi Juu ya Taarifa za Ongezeko la Michango ya Wanachama Kutoka 18,000 Hadi 40,000

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umesema hakuna mabadiliko ya michango kwa watumishi kama ambavyo taarifa zinazosambazwa mitandao zinadai kuwa kuna ongezeko la uchangiaji kutoka TZS 18,000 hadi TZS 40,000.


Share:

Madiwani Watano CHADEMA Jijini Arusha Wajiuzulu na Kutimkia CCM

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Dkt. Maulid Madeni amethibitisha amepokea barua za madiwani watano kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutoka ndani ya jii hilo kujiuzulu nyadhifa zao.

Mbali na barua hizo za kujiuzulu, madiwani hao pia wamemuandikia barua katibu wa CCM Wilaya ya Arusha wakiomba kujiunga na chama hicho.

Kutokana na kujiuzulu kwa madiwani hao, Jiji hilo sasa lina madiwani 28 ambapo 20 ni wa Chadema na CCM wanane.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, CCM ilipata diwani mmoja lakini hivi karibuni madiwani saba wa Chadema walijiuzulu na kujiunga na chama hicho tawala.




Share:

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila aagiza mawakala mashine za EFD kukamatwa

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila ameagiza mawakala wa mashine za kutoa risiti za kielektroniki (EFD) mkoani humo, kukamatwa na kuwekwa ndani kutokana na kutohudhuria mkutano wa wafanyabiashara soko la Sido, jijini Mbeya leo Novemba 30, 2019.

Chalamila ametoa agizo hilo leo Jumamosi  katika mkutano wake na wafanyabiashara wa soko hilo kwa ajili ya kusikiliza kero zao.

"RPC  watafute leo Jumamosi wapumzike mahali tutakutana nao Jumatatu, haiwezekani huu ni upuuzi tunawahitaji wao hawapo hata sisi tumeacha usingizi," amesema.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania mkoani Mbeya (TRA),  Jiji la Mbeya lina mawakala wanne kwa sasa ambao walitakiwa kuhudhuria mkutano huo.


Share:

Gari la Coastal Union Likiwa na Mashabiki Walioenda Kumshangilia Bondia Mwakinyo Lapata Ajali

Gari la Coastal Union iliyokuwa imebeba mashabiki kutoka Tanga ambao walienda Dar kumuunga mkono Bondia Mwakinyo limepata Ajali kwa kugongana na lori maeneo ya Bunju ikitokea Dar kurudi Tanga. 

Kwa Mujibu wa Mganga Mkuu Bagamoyo,Dkt Azizi Msuya, majeruhi walikuwa zaidi ya kumi na sita lakini kumi ndio walikuwa na hali mbaya, kati ya hao wawili wamefariki, sita wamepata huduma ya kwanza na wameomba wakatibiwe zaidi Bombo, wawili wamepata rufaa kwenda Muhimbili, na wengine wanaendelea vizuri


Share:

Ajinyonga Baada Ya Mkewe Kumtoroka Usiku na Kwenda Kwa Mwanaume Mwngine

Watu wanne wamefariki dunia katika matukio tofauti wilayani Nkasi mkoani Rukwa, likiwemo la mwanaume kujinyonga kwa kutumia kamba ya nailoni baada ya kugundua mke wake amemtoroka usiku na kwenda kwa mwanaume mwingine.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Justine Masejo, alisema katika tukio la kwanza lililotokea Novemba 24 saa 6 usiku, mwanaume aliyefahamika kwa jina la Rafael Leonard (49) mkazi wa Kijiji cha Bumanda Kata ya Korongwe wilayani Nkasi, alijinyonga chumbani kwake kwa kutumia kamba ya nailoni.

Alisema kabla ya kujinyonga alikuwa amelala na mkewe alipo shtuka usingizini alikuta mke wake ametoroka na kwenda kwa mwanaume mwingine ndipo alipokasirika na kupatwa na wivu wa kimapenzi na kuamua kujinyonga.

Katika tukio la pili lililotokea Novemba 23 saa 8 mchana, katika Kijiji cha Mwai Kata ya Namanyere, kamanda  huyo alisema watu wawili waliofahamika kwa majina ya Japhet Jelazi (25) na Peter Silunde (8) walikufa papo hapo baada ya kupigwa na radi wakiwa wamejikinga mvua chini ya mti.

Alisema Jelazi ambaye alikua akilima shambani na Silunde aliyekuwa akichunga mbuzi baada ya kuona mvua imeanza kunyesha, waliamua kukimbilia chini ya mti ili kujikinga wasilowane na mvua hiyo ndipo radi ilipo wapiga na kufariki dunia papo hapo.

Katika tukio la mwisho lililotokea katika Kitongoji cha Milundikwa Kijiji cha Nkundi, Kamanda Masejo alisema mtoto Emiliana Kauzeni (3) alikufa maji baada ya kutumbukia kwenye dimbwi la maji yaliyokuwa yametuama nyuma ya nyumba yao kufuatia mvua zinazo endelea kunyesha mkoani humo.

Kwa mujibu wa kamanda, mtoto huyo alikuwa akicheza peke yake na kisha kuzunguka nyuma ya nyumba ndipo alipokwenda kwenye dimbwi la maji lililokuwa nyuma ya nyumba na kisha kutumbukia na kufa maji huku mama yake akiwa amelala ndani akijipumzisha kutokana na uchovu wa shughuli za kilimo.

Kamanda huyo alisema kutokana na matukio hayo, hakuna watu wanaoshikiliwa lakini akawahimiza wakazi wa mkoa huo kuwa waangalifu katika kipindi hiki cha mvua za masika ili kujiepusha na madhara yanayoweza kujitokeza.


Share:

Chuo Cha Mipango Chatakiwa Kufanya Utafiti Wa Umasikini Na Utekelezaji Miradi Ya Umma

Benny Mwaipaja, Dodoma
NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, amekitaka Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, kutafiti kwa kina namna wananchi wanavyoweza kuondokana na umasikini wa kipato pamoja namna Miradi mbalimbali ya Serikali inavyoweza kutekelezwa kwa ufanisi na kwa kuzingatia thamani ya fedha kuliko ilivyo sasa.

Dkt. Kijaji ametoa rai hiyo wakati akiwatunuku astashahada na shahada mbalimbali wahitimu 3,182 Wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Kampasi ya Dodoma wakati wa sherehe za mahafali ya 33 ya chuo hicho.

Amesema kuwa matokeo ya tafiti hizo yataisaidia Serikali na Jamii kwa ujumla kupanga mikakati ya namna ya kukabiliana na umasikini wa wananchi hususan wa vijijini pamoja na kuharakisha maendeleo ya nchi kwa kuhakikisha kuwa miradi inayotekelezwa na Serikali inakuwa na tija.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango ambaye pia ni Kamishna Msaidizi wa Bajeti Bw. Pius Mponzi amemwahidi Dkt. Ashatu Kijaji, kwaniaba ya Baraza la Chuo hicho kwamba wataongeza jitihada katika eneo la utafiti na kuhakikisha kuwa matokeo ya utafiti huo yanawafikia wananchi kwa lugha rahisi

Naye Mkuu wa Chuo hicho cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Profesa Hozen Mayaya amesema chuo chake kimetimiza miaka 40 tangu kianzishwe na kimepata mafanikio makubwa kwa kutoa wahitimu mahili na wenye kukidhi mahitaji ya soko.

Amebainisha kuwa Chuo kimeongeza idadi ya kozi kutoka kozi moja mwaka 1980 hadi kufikia kozi 25 mwaka huu, huku idadi ya wanachuo wanaodahiliwa nayo imeongezeka kutoka wanachuo 13 mwaka huo hadi kufikia wanachuo zaidi ya elfu 11 mwaka huu.


Share:

Simbachawene: Matumizi Ya Nishati Mbadala Ni Kitu Cha Muhimu Kwa Maendeleo Ya Taifa

Matumizi ya nishati ya kuaminika na endelevu ni kitu kisichoepukika kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na kwa Taifa lolote duniani hasa tunapoelekea kufikia lengo la Uchumi wa Viwanda ifikapo mwaka 2025. Hayo yamesemwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mh. George Simbachawene alipokua akizindua maonyesho ya  14 ya kitaifa ya nishati jadidifu yaliyofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja , jijini Dar es Salaam.

Aliongeza kuwa changamoto kubwa iliyopo  ni kuhakikisha kuwa masuala yote yanayokwamisha upatikanaji rahisi, ueneaji na ongezeko la matumizi ya Nishati hizi kwa wananchi wote hasa walioko vijijini na hata mijini linashughulikiwa ipasavyo.  ”Ninawashauri muwe tayari kupeleka huduma zenu vijijini kwa kuanzisha matawi ya biashara zenu huko badala ya kunga’ng’ania mijini pekee” alisema Waziri Simbachawene.

Aidha alisititiza kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais inathamini juhudi  za uendelezaji na uhamasishaji wa matumizi ya Nishati jadidifu na udhibiti wa ubora wa vifaa na ufungaji wa mitambo mbalimbali, ili kuwa na Teknolojia endelevu katika ustawi wa Mazingira yetu. Pia amewaagiza TAREA kufanya utafiti kubaini kwa kiasi gani jamii ya Wananchi katika mkoa wa Dar es Salaam wanatumia nishati jadidifu.

“Naye Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania Bwana Jeroen Verheul amemshukuru Waziri Simbachawene lakin pia amesema kuwa wataendelea kufadhili masuala mbalimbali  ya mazingira yakiwemo yanayohusu nishati mbadala kama ambavyo wamefanya kwa TAREA.

Akiongea katika ufungzi huo Katibu wa Jumuia ya Nishati jadidifu Makamu Mwenyekiti wa TARE Bwana Prosper Magali, alimshukuru Waziri Simbachawene kwa kufungua maonyesho hayo na aliongeza kuwa TAREA itaendelea kushughulika na  masuala ya nishati jadidifu lakini pia wanachukua maelekezo ya Waziri aliyowapa na kuyafanyia kazi.

Maonyesho hayo ya nishati jadidifu yameandaliwa na Jumuia ya nishati jadidifu (TAREA) ambapo hufanyika kila mwaka. Kwa mwaka huu maonyesho hayo ymefanyika katika viwanja vya mnazi mmoja na mgeni Rasmi akiwa Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mh. George Simbachawene.


Share:

KAULI YA MWAKINYO BAADA YA KUMCHAPA MFILIPINO ARNEL TINAMPAY


Bondia Mwakinyo akimchapa konde la uso mfilipino Arnel

Bondia Hassan Mwakinyo amesema moja ya sababu iliyopelekea yeye kumshinda Bondia Mfilipino Arnel Tinampay, ni yeye kurusha ngumi nzito huku mpinzani wake akiwa anarusha ngumi nyingi zilizokuwa nyepesi sana.

Mwakinyo ametoa kauli hiyo, baada ya kuisha kwa pambano lake usiku wa kuamkia leo lililofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam, ambapo alimchapa Mfilipino, huyo kwa alama 97-93, 98-92 na 96-96.

Mwakinyo amesema kuwa"sipigi ngumi nyepesi napiga sana madude, kilichomsaidia Mfilipino alishasoma, alikuwa ananificha ukitaka kufanya finishing na yeye anapiga."

"Najua kitu kikubwa kilichokuwa kinambeba alikuwa mvumilivu sana, ila pia Mabondia wengi huwa tunapigwa nje ya nchi kwa namna ambavyo hata yeye mwenyewe amepigwa" ameongeza Mwakinyo
Share:

Mahiga Awataka Wakuu Wa Magereza Nchini Kutumia Ujuzi Wa Wafungwa Kujiendesha Na Kutoa Mchango Wa Gawio Kwa Serikali

Waziri wa Katiba na Sheria Mheshimiwa Balozi Dkt Augustine Mahiga amewataka Wakuu wa Magereza nchini kutumia nguvu kazi na ujuzi wa wafungwa walioko magerezani kubuni miradi mbalimbal ili kuwazalishia fedha zitakazowawezesha kujiendesha bila kutegemea ruzuku kutoka serikalini.

Balozi Mahiga ameyasema hayo jana alipotembelea gereza la Kyela kujionea jinsi Taasisi za Haki Jinai zinavyotekeleza majukumu yake katika mahakama na magereza ikiwemo kutatua changamoto ya mrundikano wa mahabusu katika magereza pamoja na kuboresha mfumo wa utoaji haki na hali ya magereza kote nchini.

“Nguvu kazi za hawa wafungwa ni nyingi na wana ujuzi mbalimbali mnaoweza kuutumia kuanzisha miradi ambayo itawasaidia kupata fedha na mkaweza kujiendesha bila kutegemea ruzuku kutoka serikalini, watumieni. Pale Dar es Salaam natazama yale majengo ya magereza mnajengewa na jeshi wakati mngeweza kujenga wenyewe.”

Kwa upande wake Mkuu wa Gereza la Kyela ASP. Nelson.M. Mwaifani amesema kwamba wao wamejitahidi kuhakikisha kwamba gereza hilo halina msongamano wa mahabusu na kwamba mazingira ya wafungwa na mahabusu ni mazuri salama kwa afya za watu hao kwani wana mabweni na magodoro yanayowatosha wafungwa na mahabusu wote waliopo katika gereza hilo. Pamoja na hayo ASP. Mwaifani amemwambia Waziri Mahiga aliyeambatana na Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka Biswalo Mganga kwamba wameingia mkataba na Halmashauri ya Wilaya ya Kyela ya kuzoa taka ngumu, kuzibua mifereji na kufanya usafi katika hospitali ya Wilaya kwa makubalino ya kulipwa shilingi 6,700,000/- kwa mwezi.

Hata hivyo, Dkt. Mahiga alifurahishwa na uongozi wa gereza la Kyela chini ya ASP. Nelson.M. Mwaifani kwa kuwa wabunifu na kushirikiana vizuri na Halmashauri ya Kyela kiasi cha kufanikiwa kupata tenda ya kufanya usafi katika Halmashauri hiyo jambo linalowaingizia wastani wa cha shilingi milioni sita kwa mwezi. Aidha aliwataka wakuu wote wa Magereza nchini kuiga mfano huo na kwamba siku moja wawe sehemu ya taasisi za serikali zitakazotoa gawio mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt John Joseph Pombe Magufuli.

“Nataka siku moja gereza hili lichangie kwenye mgao wa pesa za Taasisi ya Mahakama kwaajili ya gawio la kwenda serikalini mbele ya Rais, nikisikia, nitafurahi sana. Nina uhakika hivi karibuni tutaulizwa mchango wenu ni nini kwenye gawio la serikali. Najua mnaweza kuwa vyanzo vingi vya kupata pesa hivyo ni matumaini yangu kuwa gawio lijalo Wizara yetu au Taasisi ndani ya wizara yetu itatoa kitu (‘very signficant’) kikubwa, na magereza nina uhakika. Kule sabasaba kila mwaka mnapata zawadi tena nzuri tu, mnaongoza, sasa hapa onesheni mfano mzuri.” Amesema Dkt. Mahiga.

Hivi Karibuni Mheshimiwa Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli azitaka Taasisi za Umma zinazozalisha na kupata faida zitoe gawio kwa serikali na kuzipa siku 60 Taasisi,Mashirika na Makampuni ya serikali ambayo hajatoa yafanye hivyo ndani ya muda huo. Waziri Mahiga ameamua kutumia ziara yake ya siku saba pamoja na mambo mengine kuzipa changamoto Taasisi za utoaji haki jinai kuanza kufikiria namna ya kuweka mikakati madhubuti ili nazo zianze kutoa gawio kwa serikali. Ziara hii iliyoendelea leo katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela na Gereza la Kyela, itaendelea tena kesho katika Wilaya ya Mbarali jijini Mbeya.


Share:

ELIMU YA UMEME KWA WASIOONA YAIPA TANESCO TASWIRA MPYA


 MKUU wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare  akizungumza wakati wa uzinduzi wa wasrha hiyo kushoto ni  Kaimu meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoa wa Morogoro William Masome
 Sehemu ya wanachama wa chama cha wasioona  Tanzania (TLB)  mkoani Morogoro.
 Sehemu ya wanachama wa chama cha wasioona  Tanzania (TLB)  mkoani Morogoro Mkuu wa Mkoa huo ambaye hayupo pichani

 wanachama wa chama cha wasioona  Tanzania (TLB)  mkoani Morogoro.
MKUU wa Mkoa wa Morogoro aliyevaa suti jeusi akiwa kwenye picha ya Pamoja na washiriki wa semina hiyo kushoto ni  Kaimu meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoa wa Morogoro William Masome 

SHIRIKA la Umeme Nchini TANESCO limeendesha semina maalum inayohusu masuala ya Umeme kwa wanachama wa chama cha wasioona  Tanzania (TLB)  mkoani Morogoro.

Akizungumza wakati wa uzinduzi  wa warsha hiyo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  Loata Ole Sanare amesema kuwa Tanesco  imeonyesha mfano mzuri wa kuigwa kwa kutoa elimu hiyo kwa watu wa kundi  maalum katika jamii.

Alisema pia kupitia hili shirika limetoa taswira kuwa mashirika ya Umma yanafuata muelekeo wa Raisi John Pombe Magufuli ambae ni  Raisi wa wanyonge na kwa kujali wateja wake hata wa Makundi maalum kwa kutoa elimuYa Umeme itakayowasaidia katika maisha yao ya kila  siku.

Mkuu huyo wa Mkoa  amewataka wasioona kutokuwa wanyonge kwakudhani kuwa  Serikali haiwatambui na kusema kuwa Serikali ipo pamoja nao na kuwakaribisha katika ofisi za Mkoa, muda wowote watakapokua na changamoto zozote.

Naye Kaimu meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoa wa Morogoro William Masome amesema Kuwa TANESCO chini ya Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Tito Mwinuka imetambua umuhimu wa watu wenye Ulemavu wa kutoona kupatiwa elimu ya Umeme ili waweze kutambua fursa  zitokanazo na umeme zitakazoweza kuwainua kiuchumi lakin pia kuwafundisha jinsi ya kutumia umeme vizuri (matumizi Bora ya umeme)ili wasilipe gharama kubwa
Kwenye kununua Umeme.

Naye kwa upande wake Mratibu wa idara ya maendeleo, Vijana na Chipkizi toka TLB , Bw.Kiongo Itambu ameishukuru TANESCO kwa kuwapatia elimu hiyo
Maalum ambayo itawasaidia hasa katika kujiepusha na matukio ambayo yanaweza kuathiri usalama wao.

Alisema kwani wameshajua athari za kukaa karibu na miundombinu ya umeme  na  kuahidi kushirikiana na TANESCO katika kuwafichua wanaolihujumu Shirika kwa kuiba umeme na kuharibu miundombinu ya Shirika.

Aidha Bw. Kiongo alimuhakikishia Mkuu wa mkoa kuwa wao kama watu wenye ulemavu ni kama watu wengine, ni mara chache kusikika wasioona ikiwa na sifa ya kuliibia shirika la umeme na watakuwa mabalozi wa kuhakikisha Tanesco haiujumiwi ili kukuza kipato chake kwa maendeleo ya Shirika na Taifa kwa ujumla
Share:

ACT- Wazalendo wataka vifurushi bima ya NHIF Visitishwe, Serkali Yawajibu

Chama cha ACT Wazalendo kimeitaka Serikali kusitisha vifurushi  vya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Tanzania (NHIF) kwa madai kuwa vinakandamiza wasiokuwa na uwezo.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dorothy Semu, alipozungumza na waandishi wa habari.

Vifurushi hivyo vilizinduliwa juzi jijini Dar es Salaam na uongozi wa NHIF, ukieleza kuwa vimegawanywa katika makundi matatu yaliyopewa majina ya 'Ninajali Afya', 'Wekeza Afya' na 'Timiza Afya'.

Kwa mujibu wa mpango huo mpya wa matibabu wa NHIF, watu wenye umri wa kati ya miaka 18 na 35 watalipia Sh192,000 kwa mwaka kuwa katika kifurushi cha Najali Afya Premium ama Sh384,000 cha Wekeza Afya ama Sh516,000 cha Timiza Afya.

Kwa wenye umri mkubwa zaidi wa kuanzia miaka 36 hadi 59 watagharimia matibabu ya mwaka mzima kwa kulipia Sh240,000 katika mpango wa Najali Afya Premium au Sh444,000 (Wekeza Afya) au Sh612,000 (Timiza Afya).

Watu wenye umri wa kuanzia miaka 60 na kuendelea wataweza kugharimia matibabu ya mwaka kwa kulipia kati ya Sh360,000 na Sh984,000. Bei za vifurushi hivyo inaongezeka kulingana na idadi ya wanufaika kama mwenza na watoto hadi wanne.

Dorothy Semu alisema  kuwa kitendo cha serikali kujiondoa kwenye kuhudumia raia wake kwenye afya kwa kutangaza vifurushi vipya vya bima, ni kuwatenga wenye kipato cha chini.

Alisema gharama zilizowekwa katika vifurushi hivyo vipya zinajenga matabaka mawili katika utolewaji wa huduma za afya; la wenye nacho na wasio nacho.

“Binadamu hachagui kuumwa au aina ya ugonjwa ambao unapaswa kuugua, utaratibu huu wa vifurushi unachukulia kwamba suala la ugonjwa ni jambo la hiari, kwamba mtu anaweza kuchagua kuumwa ugonjwa huu ama kuukataa ule, hivyo atatibiwa kutokana na chaguo lake.

"Mtazamo wa namna hii ni hatari sana katika ujenzi wa jamii yenye utu, usawa na yenye haki. Duniani kote kuna bima aina mbili, ya binafsi na ya umma. Kiwango cha malipo ya kila mwaka kwa kila mtu ni tofauti kulingana na vigezo tofauti.

"NHIF kimsingi ni skimu ya bima ya afya ya umma, na kwa maana hiyo viwango vya malipo vinatokana na uwiano wa kipato cha mtu na mafao yanapaswa kuwa sawa kwa watu wote bila kujali kiasi cha mchango wanaotoa.

"Kitendo cha kutoa vifurushi vya malipo tofauti, na huduma kutolewa kwa kuzingatia kifurushi, ni kitendo cha kuifanya NHIF kuwa bima binafsi na 'kubidhaisha' afya ya Watanzania," alidai.


Chama hicho kilishauri kusimamishwa kwa huduma ya vifurushi hivyo vipya ili kupunguza matumizi makubwa ya rasilimali fedha.

“Kwa mfano, badala ya kuzuia wananchi wa kipato cha chini kupata huduma mbalimbali kama MRI na CT scan, serikali itoe ruzuku kwa wananchi hao kwa kuwalipia NHIF. Huu ndiyo wajibu wa serikali kutokana na kodi inazokusanya kutoka kwa wananchi,” alisema.


Hata hivyo, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ameyajibu madai ya ACT- Wazalendo kwa kusema kuwa   Vifurushi hivi ni kupitia utaratibu wa HIYARI  na sio lazima. Pia, havijafuta Bima ya Afya ya Jamii (CHF) .

"Tusifanye siasa kwenye hili.  Vifurushi hivi ni kupitia utaratibu wa HIYARI sio lazima. Pili, havijafuta Bima ya Afya ya Jamii (CHF) ambapo kiwango cha kuchangia kwa mwaka ni shilingi 30,000 kwa kaya ya hadi watu 6. Aidha, vifurushi vya watoto, Wakulima nk. bado vipo." Ameandika Ummy Mwalimu katika ukurasa wake wa Twitter wakati akipangua Hoja ya Zitto Kabwe



Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi November 30

















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger