Saturday 25 February 2017

Rais Magufuli Ateua Mwenyekiti Wa Bodi Mamlaka Ya Masoko Ya Mitaji Na Dhamana

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli,  amemteua Dkt. John Kedi Mduma kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. John Kedi Mduma umeanza tarehe 23 Februari, 2017.

Dkt. John Kedi Mduma ni Mhadhiri Mwandamizi, Idara ya Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Dkt. John Kedi Mduma anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bi. Grace Rubambey ambaye amemaliza muda wake.
***

Share:

mpya:Taarifa Kuhusu UTAPELI Ajira za JWTZ

Share:

Friday 24 February 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEB 24 2017

Share:

Mahakama Yamzuia RPC Kujibu Swali la Tundu Lissu

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imemzuia shahidi wa kwanza katika kesi inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na wenzake watatu, kujibu swali linalohusu mamlaka ya kikatiba ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC),  kufuta uchaguzi uliofanyika Oktoba 25,2015. Kwa mujibu wa Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba , swali hilo la Lissu halina mashiko.

Lissu alimuuliza shahidi ambaye ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamduni kwamba, Jecha Salim Jecha ana mamlaka gani kikatiba kufuta uchaguzi uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Lissu alimuuliza Kamanda Hamduni kama anafahamu mamlaka yapi ya kikatiba ambayo Mwenyekiti wa ZEC, Jecha aliyatumia kufuta uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na Rais.

Wakili wa Serikali, Paul Kadushi amedai kuwa shahidi huyo amekwenda mahakamani kutoa ushahidi kuhusu maelezo na kwamba si kutoa tafsiri ya kisheria kuhusu Katiba ya Zanzibar.

Kadushi amedai anapinga shahidi wake kujibu swali hilo kwamba Mwenyekiti wa ZEC ana mamlaka ya kufuta uchaguzi ama la na kueleza kuwa shahidi huyo hana ufahamu wa sheria na si mtaalamu wa Katiba na sheria.

''Napinga shahidi kujibu swali hili ambalo kimsingi linamtaka atafsiri sheria, jambo ambalo silo lililomleta na wala hana utaalamu wa kisheria. Hata hivyo, mahakama hii haina mamlaka ya kutafsiri Katiba isipokuwa ni mahakama ya kikatiba na mahakama kuu ndio yenye uwezo huo,'' alidai Kadushi.

Lissu alipinga hoja hizo kwa maelezo kwamba, pingamizi la wakili wa serikali halina maana kwa sababu suala la mamlaka halali au si halali ya Zanzibar limeletwa na upande wa mashitaka wenyewe, kama ambavyo mashitaka ya pili katika kesi hiyo wameeleza kuwa habari iliyochapishwa ingeweze kuleta chuki kwa Wazanzibar kuichukia nchi yao.

Alidai kuwa, masuala ya mamlaka wameyaleta wenyewe wanapaswa kukabiliana nayo, kwa kuwa Sheria ya Ushahidi namba 147, kifungu kidogo cha pili na Sheria namba 157 ya sheria hiyo, vinaweka wazi kwamba shahidi anaweza kuulizwa swali lolote na kwamba si lazima liwe ndani ya kile anachokitolea ushahidi.

Hakimu Simba amesema, mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kuzungumzia Katiba ya Zanzibar.

Amesema mahakama katika kesi hiyo haitazungumzia uhalali au kutokuwa halali kwa Mwenyekiti wa ZEC, Salim Jecha kufuta au kutofuta uchaguzi mkuu Zanzibar.

"Pingamizi la upande wa mashitaka ambao ulipinga masuala ya kikatiba ambayo mbunge huyo alikuwa akimuuliza shahidi kuhusu Jecha ana mamlaka gani kikatiba kufuta uchaguzi uliofanyika Oktoba 25, 2015, ni sahihi na shahidi hatakiwi kujibu swali hilo," amesema Hakimu Simba.

Lissu amedai uamuzi huo hautamuathiri na kwamba anakubaliana nao kwamba haruhusiwi kuuliza swali hilo kwa shahidi hivyo waendelee na ushahidi.

Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 8 na 9, mwaka huu na kuutaka upande wa mashitaka kupeleka mashahidi ili kesi iishe kwa kuwa watu wengi wanaifuatilia hivyo iishe waendelee na shughuli za maendeleo.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mhariri wa gazeti la Mawio, Simon Mkina, mwandishi wa gazeti hilo, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehboob.

Wanadaiwa kati ya Januari 12 na 14, mwaka huu, Dar es Salaam, kwa lengo la kuleta chuki kwa wananchi wa Zanzibar, Jabir, Mkina na Lissu, kwa pamoja waliandika na kuchapisha taarifa‎ za uchochezi zenye kichwa cha habari kisemacho, 'Machafuko yaja Zanzibar'.

Katika mashitaka yanayomkabili Mehboob, anadaiwa kuwa, Januari 13 katika jengo la Jamana, Dar es Salaam, alichapisha gazeti la Mawio lililokuwa na taarifa za uchochezi, pia alichapisha gazeti hilo bila ya kuwasilisha hati ya kiapo kwa Msajili wa Magazeti.
Share:

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Chaipinga TCU.,Chasema Hakijawahi Dahili Wanafunzi Vilaza

Share:

Wednesday 22 February 2017

Tcu: Orodha ya Vyuo na Majina ya wanafunzi waliokosa sifa za kupewa nafasi za vyuo Tanzania 2016/2017


 Image result for tcu tz
Share:

Mahakama Yamkingia Kifua Mbowe,Yaamuru Asikamatwe

Mahakama  Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetoa zuio la muda kuzuia Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe asikamatwe na Polisi hadi maombi yake, aliyoyaomba ya kutaka asikamatwe, yatakaposikilizwa kesho.

Katika kesi hiyo ya kikatiba namba 1 ya mwaka 2017, Mbowe anapinga mamlaka ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Simon Sirro na Mkuu wa Upelelezi wa kanda hiyo (ZCO), Camilius Wambura, ya kutaka kumkamata hadi maombi hayo yatakaposikilizwa.

Maombi ya kesi hiyo yataanza kusikilizwa Februari 23, mwaka huu saa 7:30 mchana katika chumba cha wazi cha mahakama ili kuruhusu watu mbalimbali kusikiliza kesi hiyo.

Jopo la majaji watatu likiongozwa na Sekieti Kihiyo akisaidiana na Jaji Lugano Mwandambo na Jaji Pellagia Kaday lilitoa zuio hilo, hata hivyo walisema Polisi wanaweza kumuita Mbowe kwa mahojiano pindi watakapomhitaji.

Kesi hiyo ambayo ilisikilizwa kwa vipindi vitatu kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana, mahakama iliamuru upande wa wadai ambao uliongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, kurekebisha maombi yao kwa kuwa hawakumuingiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) licha ya kuishitaki serikali.

Hali hiyo ilitokana na mawakili wa upande wa wadai, Lissu ambaye alipinga kitendo cha Mwanasheria wa Serikali, Gabriel Malata kuwatetea wadaiwa hao ambao ni RC, RPC na ZCO katika kesi hiyo kwa kuwa hawajaitaja serikali.

Akijibu hoja hiyo, Malata alidai kuwa waliofunguliwa madai hayo sio Makonda, Sirro wala Wambura, bali ni serikali hivyo ana mamlaka yote ya kuwawakilisha.

Baada ya pande zote kuwasilisha hoja zake, mahakama ilimruhusu Malata kuendelea kusikiliza kesi hiyo ambapo pia iliagiza upande wa wadai kufanya marekebisho ya maombi hayo na kumuongeza AG kama mdaiwa.

Hata hivyo, Lissu aliomba waruhusiwe kufanya marekebisho hayo kwa kumuongeza AG, ombi ambalo halikuwa na pingamizi.

‘’Tutafanya marekebisho ya maombi yetu na marekebisho mengine madogo madogo kwa namna tutakavyoona inafaa siku ya Jumatatu na tutawapa wajibu maombi Machi 6 mwaka huu na Machi 8 mwaka huu itatajwa kwa ajili ya kusikiliza maombi hayo,’’ alidai Lissu.

Mbowe aliwasili mahakamani hapo akiwa na gari lenye usajili namba T 830 aina ya Land Cruiser, saa chache kabla ya kesi yake kuitwa katika chumba namba 64 kwa ajili ya kusikilizwa.

Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro, alifika mahakamani hapo baada ya kutoka Kituo Kikuu cha Polisi saa 7 usiku, alikokuwa anahojiwa na kupekuliwa kuhusu sakata la dawa za kulevya.

Aidha, viongozi mbalimbali wa chama hicho wakiwemo Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, madiwani na wafuasi wao walijitokeza kwa wingi, kusikiliza kesi hiyo huku wakifurahia amri ya mahakama ya kuzuia kutokamatwa kwa mwenyekiti huyo.

Katika kesi ya msingi, Mbowe anaomba mahakama iwazuie wadaiwa kutekeleza azma yake ya kumtia mbaroni, pia itoe amri ya kuwazuia kumkamata hadi hapo kesi hiyo ya kikatiba, itakapomalizika na kwamba polisi wasiendelee na mchakato wowote dhidi yake hadi hapo kesi hiyo itakapomalizika.

Anadai kuwa sheria inayompa Mkuu wa Mkoa mamlaka ya kutoa amri ya kumkamata na kumweka ndani mtu, iko kinyume cha katiba, kwa madai kuwa ilitungwa katika mazingira ambayo hapakuwa na vituo vya polisi vya kutosha.

Pia anadai kuwa kwa mazingira ya sasa, sheria hiyo imeshapitwa na wakati na anaiomba mahakama itamke kuwa ni kinyume cha katiba.

Mbowe pia anadai kuwa hata kama Mkuu wa Mkoa alikuwa anatekeleza mamlaka yake kwa mujibu wa sheria hiyo, basi hakutimiza matakwa ya kisheria, ambayo ni pamoja na kutoa taarifa kwa Hakimu wa Mahakama ya Wilaya au ya Hakimu Mkazi.

Vile vile, anaiomba mahakama kama itaona kuwa Mkuu wa Mkoa alikuwa sawa kutoa amri hiyo, basi imwamuru afuate matakwa ya kisheria, ikiwa ni pamoja na kulinda haki za binadamu katika kutekeleza madaraka yake hayo.
Share:

TCU: ORODHA YA WANAFUNZI WASIO NA SIFA KATIKA VYUO VYA ELIMU YA JUU 2016/2017

TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA
Image result for tcu tz
TAARIFA KWA UMMA
WANAFUNZI WASIO NA SIFA KATIKA VYUO VYA ELIMU YA JUU
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inautangazia Umma kuwa zoezi la uhakiki wa sifa za wanafunzi wanaondelea na masomo kwenye Vyuo vya Elimu ya Juu nchini kwa mwaka 2016/2017 limekamilika katika baadhi ya vyuo. Katika kutekeleza zoezi hilo Tume imebaini kuwa kuna wanafunzi ambao wamedahiliwa katika programu ambazo hawana sifa.
Orodha ya wanafunzi wasio na sifa imeshawasilishwa kwenye vyuo husika. Hivyo, wanafunzi wote wanaondelea na masomo kwenye Vyuo vya Elimu ya Juu nchini wanaweza kutazama matokeo ya uhakiki wao kupitia kiunganisho (link) (Bonyeza Uhakiki wa Sifa za Udahili).
Tume inawaarifu wanafunzi wote ambao majina yao yameorodheshwa wawasiliane na vyuo vyao ili kuthibitisha sifa zao kabla ya tarehe 28 Februari 2017. Wanafunzi ambao hawatafanya hivyo hawatatambuliwa na Tume na hivyo kukosa sifa za uanafunzi.
TCU inatoa rai kwa wanafunzi wote kutembelea tovuti ya Tume (www.tcu.go.tz) mara kwa mara ili kupata taarifa mpya kuhusu uhakiki wa sifa za wanafunzi.
Imetolewa na
Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania

20/02/2017
Share:

Ridhiwani Kikwete ajibu shutuma ya kutajwa kwenye orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya

Mbunge wa jimbo la Chalinze mkoani Pwani kwa tiketi
Share:

WANAWAKE 13 WAHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 2 KWA KOSA LA KUJIUZA HUKO MOROGORO

 Dada poa hao wakitoka  ser
o ya Mahakama ya Nunge wakipanda Difenda  kuelekea Magereza.
Share:

WANAOSOMA CHINA KUISOMA NAMBA,SERIKALI YASISITIZA KUSITISHA FEDHA ZA MIKOPO KWA WANAFUNZI WANAOSOMA NCHINI CHINA

Serikali kupitia wizara ya elimu,sayansi na teknolojia imesisitiza kusitisha pesa za mikopo ya nauli za kwenda masomoni na malipo mengine yote yaliyokuwa yanatolewa kwa wanafunzi wanapata ufadhili wa masomo kutoka kwa nchi rafiki ikiwemo nchi ya China.
Kauli hiyo imetolewa kupitia barua(ya tarehe 7,February,2017) iliyoandikwa na wizara ya elimu ,sayansi na teknolojia kwenda ubalozi wa Tanzania chini China wakati wakijibu barua iliyoandikwa na wanafunzi wanaosoma nchini china kuomba serikali kuangalia vizuri maamuzi hayo.
Takribani miezi miwili iliyopita,Bodi ya mikopo (HESLB) iliauandikia barua ubalozi wa Tanzania nchini china kuueleza maamuzi ya serikali kusitisha utoaji wa fedha za nauli kwa wanafunzi hao.Lakini wanafunzi hao hawakuridhika na maamuzi hayo hivo kuamua kuiandikia barua wizara ya elimu kuangalia vizuri maamuzi hayo.
 
Kwa mujibu wa barua hii ,wanafunzi watatakiwa kujigharamia wenyewe gharama za kwenda na kurudi masomoni kitu ambapo awali walikuwa wanapatiwa na serikali ya Tanzania.
Hii hapa barua mpya uliyosisitiza kutotoa pesa hizo na nauli kwa wanafuni hao
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARY 22,2017

Share:

Tuesday 21 February 2017

 HIZI HAPA HABARI KALI SIKU YA LEO JUMANNE FEB 21 2017

 

MBOWE APEKULIWA USIKU ARUDISHWA POLISI,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/T5jbX8 

 

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEB TAREHE 21.2.2017,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/PHqMKK


SHAMSA FORD AMLILIA MUMEWE ALIEKAMATWA KWA KESI YA MADAWA YA KULEVYA,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/6s58nV


NECTA YAWATAKA WANANCHI KUPUUZA TAARIFA ZILIZOTOLEWA KUHUSU MCHUJO KIDATO CHA KWANZA,SOMA ZAIDI HAPO>>>>https://goo.gl/gmq5ds


AUDIO | Shamba Darasa(Mkubwa na Wanawe) - Mwanamke | Download,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/Ce1kdr 

 

Mahaba Niue!! MZEE WA MIAKA 98 AFUNGA NDOA NA BIBI WA MIAKA 88,SOMA ZAIDI HAPO>>>https://goo.gl/pU13e0

 

 

Share:

Mahaba Niue!! MZEE WA MIAKA 98 AFUNGA NDOA NA BIBI WA MIAKA 88



Mzee Willy Kinyua (98) amefunga ndoa na Joyce Nyambura (88) baada ya wenza hao kuishi pamoja kwa zaidi ya miaka 60.
Share:

AUDIO | Shamba Darasa(Mkubwa na Wanawe) - Mwanamke | Download


Share:

NECTA YAWATAKA WANANCHI KUPUUZA TAARIFA ZILIZOTOLEWA KUHUSU MCHUJO KIDATO CHA KWANZA

Share:

SHAMSA FORD AMLILIA MUMEWE ALIEKAMATWA KWA KESI YA MADAWA YA KULEVYA

Mwigizaji Shamsa Ford ambaye ni mke wa Mfanyabiashara Chidi Mapenzi aliyeitwa Polisi kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya, ameandika yafuatayo ikiwa ni mara ya kwanza toka aitwe Polisi kuhojiwa.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEB TAREHE 21.2.2017

Share:

MBOWE APEKULIWA USIKU ARUDISHWA POLISI

Jana  mchana Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHA
Share:

Monday 20 February 2017

HIZI HAPA HABARI KALI SIKU YA LEO JUMATATU FEB 20 2017

MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEB 20 2017,BONYEZA HAPO>>>>>https://goo.gl/nx8imK

 

 

MANENO YA PRFO.J BAADA YA KWENDA GEREZA ALILOFUNGWA MBUNGE LIJUAKALI,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>>>>>>>https://goo.gl/P00daq 

 

MH.MBOWE ASAKWA NA JESHI LA POLISI KILA KONA APEWA MASAA 48 AJISALIMISHE,SOMA ZAIDI HAPO>>>https://goo.gl/MxB3jP 

 

MKAZI WA MKOA WA MWANZA KWIMBA AANZISHA KIWANDA CHA KUTENGENEZA GONGO,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>>>https://goo.gl/Qh7hOL

 

 


Share:

Siri yafichuka wanawake wengi kujifungua kwa upasuaji



WANAWAKE wengi kwa sasa wanajifungua kwa njia ya upasuaji kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mfumo wa maisha, vyakula, mwili kukosa mazoezi huku baadhi wakiomba wenyewe kufanyiwa upasuaji, imefahamika.
Aidha, imeelezwa kuwa baadhi ya hospitali zinalazimisha upasuaji kama njia ya kutafuta fedha, jambo lililoelezwa kuwa ni kinyume cha maadili ya tiba nchini.
Gazeti hili limezungumza na madaktari mbalimbali, wakiwemo madaktari bingwa wa wanawake na wanajamii kwa ujumla kuhusu sababu mbalimbali zinazohusishwa na hali halisi ya uzazi wa wanawake kwa sasa.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita, Dk Erasto Rite alisema njia ya upasuaji kwa mjamzito inayotumika kuzalisha mtoto mmoja au zaidi (caesarean section), hutumika kipindi ambacho uhai wa afya ya mama na mtoto upo hatarini.
Alisema takwimu zinaonesha kwamba ongezeko kubwa la njia ya upasuaji kwa wajawazito ambapo ni kati ya asilimia 16.4 mpaka 28 ya akinamama wanaojifungua, huku idadi ikiwa juu kwa kina mama wanaoishi mijini ikilinganishwa na wanaoishi vijijini.
Dk Rite alisema hiyo inachangiwa na kubeba ujauzito katika umri mkubwa, kukua kwa teknolojia na baadhi ya kina mama wenyewe kuchagua njia hiyo.
Alisema kwa upande wa kina mama wanaoishi vijijini, njia hiyo imeanza kuongezeka kutokana na baadhi yao kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu (dawa za wepesi), ambazo husababisha wengi kuishia kufanyiwa upasuaji.
Alisema hiyo pia huchangiwa na dawa hiyo kutolewa bila vipimo na pia wengi wanatumia dawa hizo wakati hakustahili kupewa na hivyo kumsababisha kupata uchungu mkali unaohatarisha maisha yake na kulazimika kupasuliwa.
Kwa upande wake, daktari wa magonjwa ya wanawake katika Hospitali ya Regency Dar es Salaam ambaye hakutaka kutajwa jina gazetini, alisema hali hiyo huchangiwa na mfumo wa mabadiliko ya maisha kipindi cha nyuma na ilivyo sasa.
Alisema zamani wanawake walikuwa wakila vyakula vya asili na kufanya shughuli mbalimbali ambazo zilikuwa kama mazoezi ya kumsaidia kuuweka mwili sawa, lakini kwa sasa ni tofauti, wanawake wengi hula vyakula ambavyo havina mpangilio maalumu na hawajishughulishi kuweka mwili sawa.
Aidha, alisema sababu nyingine inayochangia wanawake kufanyiwa upasuaji ni shinikizo la damu au mtoto kukaa vibaya au mtoto kuwa mkubwa na hivyo kushindwa kutoka kwa njia ya kawaida.
Alisema hiyo ndiyo hasa dharura inayotakiwa kuzingatiwa mjamzito kufanyiwa upasuaji na si vinginevyo. Mkazi wa Kinondoni Dar es Salaam, Juliana Joseph ambaye amejifungua watoto wawili kwa njia ya upasuaji, alisema alitamani kujifungua kwa njia ya kawaida, ila tatizo kubwa linalomsumbua wakati akiwa mjamzito ni shinikizo la damu na hivyo madaktari humshauri kwamba ili kuokoa maisha yake na ya mtoto ni lazima kufanyiwa upasuaji.
“Wakati nikiwa hospitali moja ya binafsi nilipokuwa najifungua mtoto wangu wa kwanza, alitokea mama mmoja akiwa ameshapata uchungu, madaktari walimshauri hawezi kujifungua kawaida kwa kuwa mtoto ni mkubwa ila walibishana sasa mama yule alikataa upasuaji akalazimisha kusukuma mtoto.
“Kutokana na hali kuwa mbaya na mtoto kukaa njiani muda mrefu, mtoto alizaliwa amechoka sana na baada ya kuzaliwa alikaa kwenye mashine ya kupumulia siku mbili na ya tatu akafariki, hivyo niliamini kwamba mama yule alichangia kumuua mwanawe, hivyo tunaposhauriwa na madaktari tukubali na tusibishane nao kwa kuwa siamini kama inawezekana mtu mwenye uwezo wa kujifungua kawaida ukalazimishiwa upasuaji, hiyo ni imani potofu,” alisema Juliana.
Naye Amini Salum alisema amejifungua mtoto kwa njia ya upasuaji na hiyo imesababishwa na mtoto wake kukaa vibaya na hivyo kushindwa kutoka kwa njia ya kawaida.
Kwa upande wake, mganga wa wanawake katika Hospitali ya Tumbi wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani ambaye hakuwa tayari kutaja jina gazetini, alisema upasuaji unapaswa kufanyika pale inapotokea tatizo kwa mjamzito na si kitu kinachopendwa na madaktari kumfanyia mtu.
Hata hivyo, alisema zipo taarifa kuwa, baadhi ya wanawake huomba kufanyiwa upasuaji hasa katika hospitali binafsi kwa kile kinachodaiwa hawataki kuharibu maumbile yao ya uzazi.
“Sijui nani aliwaambia maumbile yanaharibiwa kwa kuzaa kwa njia ya asili.
Huo ni utaratibu aliyouweka Mungu mwenyewe hata vitabu vitakatifu vinaeleza.
Uke huwa kama mpira na hutanuka wakati wa kujifungua na baada ya muda mfupi, hurejea katika hali yake, sasa hii dhana potofu sijui wameitoa wapi,” alisema daktari huyo.
Kuhusu hospitali binafsi, alisema wapo wanaowashauri wajawazito kufanyiwa upasuaji kwa tamaa za fedha, jambo ambalo ni kinyume cha maadili ya kazi yao na kuwataka kuzingatia maadili na kufanya upasuaji inapobidi lakini kama mjamzito hana tatizo lolote la dharura linalohitaji upasuaji, aachwe ajifungue kawaida.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake katika Hospitali ya Aga Khan ya Dar es Salaam, Dk Munawar Kaguta alisema wanawake wengi wa mjini wanaomba wenyewe madaktari kuwazalisha kwa upasuaji.
Dk Kaguta alisema hayo hivi karibuni katika mahojiano na gazeti hili kuhusu masuala ya uzazi.
Alifafanua kuwa wanawake wa mjini wanadanganywa na taarifa mbalimbali wanazozipata katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambazo zinaonesha kuwa kujifungua kwa kawaida ni hatari.
“Hawa wanawake wa mjini wanadanganywa na mitandao ambayo wanaingia kutafuta taarifa za uzazi, mwisho wa siku wakija hospitali wanaomba wao wenyewe kufanyiwa upasuaji kutoa mtoto,” alisema Dk Kaguta.
Daktari huyo alisema mbali na taarifa za mitandaoni, pia wanashawishiana na kupeana taarifa nyingine zisizo sahihi, wakielezana athari nyingi zinazoweza kumpata mama anapojifungua kawaida, ikiwa ni pamoja na kupata uchungu mkali wakati wa kujifungua.
Alisema pamoja na sababu zote hizo madaktari wengi huwazungusha na wanapolazimisha sana wakienda hospitali kwa ajili ya kujifungua mwisho wanajifungua wenyewe kwa njia ya kawaida.
Dk Kaguta alisema kila jambo lina madhara yake, alisema mwanamke kupata uchungu wakati wa kujifungua ni kawaida na kwamba hapa nchini hakuna wataalamu wa kutosha kwa ajili ya dawa za kupunguza uchungu.
“Dawa zipo lakini tatizo wataalamu wa kuzichoma, zina utaalamu wake na ambao kwa hapa nchini sio wengi,” alisema Dk Kaguta na kuongeza kuwa wataalamu hao wakipatikana wa kutosha na dawa zifike mpaka katika hospitali za serikali itasaidia kupunguza idadi ya wanaojifungua kwa upasuaji.
Dk Kaguta alisema upasuaji wowote ni hatari kwani dawa zinazotumika kumfanya mtu asipate maumivu wakati wa kufanyiwa upasuaji na pia kumlaza zinaweza kusababisha moyo kusimama ingawa haina madhara mengi kwa mtoto.
“Upasuaji wowote ni hatari, hatari zaidi zile dawa zinaweza kusababisha moyo kusimama, maumivu ya mgongo, kovu kuchelewa kupona na kuendelea kuuma ingawa hakuna hatari zaidi kwa mtoto,” alisema Dk Kaguta.
Hata hivyo, Dk Kaguta alishauri kama mjamzito hana tatizo lolote na pia mtoto amepimwa na kukuta hana tatizo na ana uzito wa kawaida ni bora kujifungua kawaida kwa kuwa ni salama na asili zaidi. Imeandikwa na Regina Kumba, Lucy Ngowi na Hellen Mlacky.
Share:

MKAZI WA MKOA WA MWANZA KWIMBA AANZISHA KIWANDA CHA KUTENGENEZA GONGO


Share:

MH.MBOWE ASAKWA NA JESHI LA POLISI KILA KONA APEWA MASAA 48 AJISALIMISHE

Share:

MANENO YA PRFO.J BAADA YA KWENDA GEREZA ALILOFUNGWA MBUNGE LIJUAKALI

January 11 2017 Mbunge wa Jimbo la Kilombero Morogoro kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ‘CHADEMA’ Peter Lijualikali alihukumiwa na Mahakama ya wilaya kifungo cha miezi sita jela bila kulipa faini kwa kosa la kufanya vurugu kipindi cha uchaguzi wa Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero.

Leo February 19 2017 Mbunge wa Mikumi Joseph Haule maarufu Profesa J amekwenda kumtembelea gerezani Ukonga Dar es salaam na baada ya kutoka hapo akaandika yafuatayo.

‘Nimetoka gereza la Ukonga kumwona Mh. Lijualikali na Patron wa mkoa wa Morogoro kamanda Zinga na wapiga kura wangu watatu kutoka kata ya TINDIGA walifungwa miaka 30, wana afya njema na wanawasalimia sana ila wanalalamika tu hali sio nzuri kabisa kule ndani.. Mungu AWASAIDIE 
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEB 20 2017

Share:

Sunday 19 February 2017

HII HAPA REPORT YA WANASAYANSI KUHUSU KUWEPO KWA BARA LA NANE DUNIANI



Wanasayansi wafahamisha kuwa bara la 8 lawezekana kuwa lipo chini ya bahari ya Pasifiki.


Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa katika jarida la Marekani la 'Geological Society of America' ni kwamba bara hilo limepewa jina la Zealandia .


Bara hilo lililokubalika na wanasayansi linasemekana kupatikana katika upande wa Kusini Magharibi mwa bahari ya Pasifiki.


Liko na ukubwa wa kilomita milioni 5 za mraba sawa na thuluthi ya ardhi ya bara la Australia .


Wanasayansi wamesema kuwa bara hilo limefinikwa na maji ya bahari .
Share:

Zijue Namba Maalum za Magari ya Viongozi, Serikali na Taasisi za Umma kwa Ujumla..!!!

Ukiona mtaani gari zimeandikwa ktk plate number kama ifuatavyo usiumize kichwa jua ni hivi:
1. Ngao-Rais, makamu wa rais na waziri mkuu
2. S-Spika wa bunge
3. JM- Jaji mkuu
4. JR- Jaji wa mahakama ya rufaa
5. JK- Jaji Kiongozi
6. J- Jaji wa mahakama kuu
7. XXXX-Mkuu wa majeshi(CDF)
8. CAG-Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali
9. CS- Katibu mkuu kiongozi
10. W mwanzoni inaashiria waziri kisha kifupi cha wizara yake hufuata
11. NW-Naibu waziri
12. DFP-Donor's Fund project
13. ST-Serikali ya Tanzania kisha herufi nyingine hufuata
14. SMZ-Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar
15. PT-Police of Tanzania
16. SM-Serikali za mitaa
17. CD- Magari ya ubalozini
18. SU-Shirika la umma.
19. gari za jeshi pia zina namba zake ambazo zina vifupi vya JW
20. MT-Magereza Tanzania
21. CGP-Commissioner General of Prison(Mkuu wa Magereza)
22. Gari nyingine za umma zina namba zaidi ya moja kwa kazi maalum
NYONGEZA:
Gari za biashara zina plate number nyeupe na zile za matumizi binafsi plate number ya njano.
Share:

MUGABE ANAWEZA KUPIGIWA KURA HATA AKIWA MAITI...


Mke wa Rais mkongwe wa Zimbabwe, Robert Mugabe, amesema kuwa mumewe ni mashuhuri sana hivi kwamba anaweza kupigiwa kura hata akiwa maiti.
Bwana Mugabe, ambaye atakuwa na umri wa miaka 93 mnamo Jumanne, ametangaza mara kadhaa kuwa atagombea kiti cha Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.
Grace Mugabe ana miaka 40 mchanga kwa mumewe.
Aliambia mkutano wa chama tawala cha ZANU-PF kuwa hata mumewe akifariki, bado jina lake litawekwa kwenye karatasi za kupiga kura.
Alisema watu wa Zimbabwe wanampenda rais wao sana, hivi kwamba wangempigia kura hata akiwa maiti.
Bi Mugabe amekuwa mkosoaji mkuu wa wakosoaji wa mumewe na kwa wale walio na tamaa ya kumrithi.
Inadhaniwa kuwa alikuwa mstari wa mbele wa kumwachisha kazi aliyekuwa makamu wa rais, Joice Mujuru mwaka 2014.
Bwana Mugabe, ambaye siku hizi haonekani sana hadharani, ametawala Zimbabwe tangu taifa hilo kuwa huru miaka 37 iliyopita.
Via>>BBC
Share:

MAELFU WAJITOKEZA KUMZIKA MCHEZAJI BONNY MWANDANJI

Maelfu ya wakazi wa mkoa wa Mbeya wamejitokeza katika mazishi ya mchezaji wa zamani Geoffrey Bonny Mwandanji aliyefariki dunia juzi na kuzikwa katika makaburi ya kanisa Katoliki Makandana wilayani Rungwe.


Akizungumza wakati wa mazishi baba mzazi wa marehemu,Bonifasi Mashamba alisema amepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha mwanae na kuongeza kuwa aliishi na watu vizuri jambo lililochangia watu wengi kujitokeza kumuuguza ikiwa ni pamoja na misaada mbali mbali.

Naye Mjomba wa marehemu, Innocent Sigonda alisema marehemu alikuwa akisumbuliwa na kansa ya mapafu pamoja sukari ilikuwa ikishuka mara kwa mara.


Mwenyekiti wa tawi la Yanga mkoa wa Mbeya Lusajo Kifamba alisema marehemu alikuwa mwanachama wao hivyo uongozi unasikitika kumpoteza mwanachama wake ambaye alikuwa akitoa msaada wa kiufundi kila alipotakiwa.
Naye mwakilishi wa uongozi wa yanga makao makuu Shadrack Nsajigwa alisema marehemu aliishi naye kama ndugu kwani walisaidiana na kupeana ushauri.
Alisema marehemu alikuwa na kipaji cha mpira pia alikuwa anajituma hivyo alikuwa mfano wa kuigwa kwa vijana waliopo.
Aliongeza kuwa wachezaji wa zamani ni hazina kwa taifa hivyo ni vyema wakatunzwa na kuthaminiwa.
 Aidha alitoa wito kwa wachezaji wengine kujipanga kimaisha ili baada ya kustafu wasisubiri kuomba misaada pindi wapatapo matatizo.
Alisema in vyema pia kuanzisha vyama vya kuwasaidia kama wachezaji wastaafu.
Share:

AMIRI JESHI MKUU RAIS DKT MAGUFULI ATUNUKU KAMISHENI KWA MAAFISA WAPYA WA JWTZ IKULU DAR



Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikagua gwaride wakati wa sherehe za Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiweka saini katika hati ya Kamisheni muda mfupi kabla ya Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiweka saini katika hati ya Kamisheni muda mfupi kabla ya Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwasili Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Kikundi cha ngoma cha JWTZ kikitumbuiza kwa ngoma ya Chaso ya Pemba wakati Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipotunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Makamu wa rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa, Waziri wa ulinzi nja Jeshi la Kujenga taifa Dkt Hussein Mwinyi, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Juma Kijazi na viongozi wengine katika picha ya pamoja baada ya Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.PICHA NA IKULU
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEB TAREHE 19.2.2017

Haya hapa magazeti ya leo Jumapili,Februari 19,2017
Share:

Saturday 18 February 2017

Mwanamke asimulia alivyobakwa na askari Msumbiji

Wakati Serikali ikiahidi kufanya uchunguzi wa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika kutimua Watanzania nchini Msumbiji, mwanamke mmoja amesema alibakwa na askari watatu kabla ya kuwekwa mahabausu ambako alikaa siku tatu bila kula. 
Mwanamke huyo, aliyejitambulisha kwa jina la Halima (si jina lake halisi) ni mmoja kati ya zaidi ya Watanzania 180 ambao wamekuwa wakitimuliwa nchini Msumbiji tangu mwanzoni mwa wiki na wengi wakidai wana hati halali za kuishi nchi hiyo jirani na wengine kulalamikia vitendo vya ukiukwaji haki wakati wa utekelezaji wa operesheni hiyo. 
Tayari Serikali imesema kuwa itafanya uchunguzi wa madai hayo, ambayo yanaweza kuharibu uhusiano wa muda mrefu wa Tanzania na Msumbiji. 
Halima anasema walianza kufukuzwa usiku wa Jumamosi ya Februari 11, muda ambao askari hao waliutumia kumfanyia kitendo hicho. 
Halima anasema kuwa alisikia watu wakivunja geti la nyumba waliyokuwa wakiishi na kudhania ni majambazi, kumbe walikuwa ni askari ambao waliwalazimisha kutoa nyaraka zao zote za kuishi Msumbiji pamoja na pesa. 
“Niliwasikia wakivunja geti nikamwambia mume wangu watakuwa ni majambazi kumbe askari, mume wangu akajificha chini ya uvungu, lakini wakamtoa na baadaye kututoa ndani na kuanza kutupiga.” 
Anasema baada ya kipigo walilazimishwa kuzoa mali zao kutoka ndani na zikawekwa kwenye gari la polisi na kisha kuwafunga mikono na baadaye kuwapeleka mahabusu. 
“Cha kushangaza tulibebeshwa vitu wenyewe kuweka kwenye gari pasipo kuelezwa sababu baada ya hapo askari akanivuta nyuma ya nyumba na kuniingilia kimwili. Nikajua ni mmoja, lakini waliendelea hadi wakafikia watatu,” alisema. 
“Ninaona aibu walinibaka kwa njia ya kawaida tofauti na taarifa za wengine wanaosema tulibakwa kinyume na maumbile, si kweli. Nawaomba waelewe hatukubakwa kinyume na maumbile kama wanavyosema ilikuwa kawaida.” 
Hata hivyo anaeleza baada ya hapo waliwekwa mahabusu kwa siku tatu pasipo kula, hali iliyowalazimu kunywa maji yaliyokuwa yamewekwa chooni. 
“Tulikaa mahabusu siku tatu, hamna kula wala kunywa, chooni tulienda kwa mtutu tukalazimika kunywa maji ya chooni kwa sababu hakukuwa na jinsi na njaa ilizidi. Kwa hiyo inabidi useme unakwenda chooni ili ukanywe maji,” alisema Halima. 
Kutokana na hali hiyo, Halima anashangazwa na kauli ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Susan Kolimba kwamba waliorudishwa hawakuwa na nyaraka huku kaimu balozi wa Tanzania nchini Msumbiji akiwatangazia wengine kuondoka ndani ya siku tano. 
“Kweli mtu utathubutu vipi kuishi nchi ya watu bila kibali? Hata kaimu balozi na yeye anatukana, kwamba hatujaingia na documents (nyaraka)? Ilibidi atutetee lakini katukana. Mungu atatulipia,” alisema. 
Mwanamke mwingine aliyewekwa mahabusu kabla ya kurudishwa nchini, Mary Makundi anasema askari wa kiume walimwambia awape fedha na alipowajibu kuwa hana, walimpekua na kuzikuta. 
Anasema walizichukua fedha hizo pamoja na simu kabla ya kumpiga na kutaka kumbaka.
“Walivunja mlango wakanikuta. Wakaniambia niwape nyaraka zangu. Nikawapa nikijua wanazikagua tu na kuniacha, lakini cha kushangaza walizichana mbele yangu na kunitaka niwape pesa na simu. Nikawaambia sina wakanipiga na kunikagua hadi sehemu za siri na kuchukua pesa na simu,” alisema Mary. 
“Baada ya hapo walinipiga kwanza kabla ya kunifunga mkono. Askari mmoja akataka kunibaka, nikamwambia kuwa hata kama hawatutaki nchini kwao, hawawezi kuniingilia bila kinga. 
“Nilipoona hali imekuwa mbaya, nilisema wacha nigombane nife kwa silaha, lakini si kubakwa.” 
Mtanzania mwingine Mohamedi Said ni mmoja wa wafanyabiashara walioambiwa waondoke pasipo kuchukua chochote na anadai kuacha mali zake zote pamoja na nyumba aliyojenga. 
“Polisi walikuja ghafla wakatuambia wageni wote tunatakiwa tuondoke. Hapa nina vibali vyote mpaka leseni ya biashara, lakini imebidi niondoke kwa sababu ya usalama wangu,” alisema Said. 
“Hakuna anayejua sababu mpaka sasa. Nimekuja nyumbani kufuatilia haki yangu kwa sababu mpaka kibali cha kujengea ninacho. 
“Mpaka sasa amekuja kaimu balozi kutoka ubalozi wa Tanzania na amesema kwa ripoti aliyopewa ametupa siku tano tuondoke. Hatujui kwanini siku tano. Utahamishaje vitu kwa siku tano au kumtafuta mnunuzi wa nyumba kwa siku tano kwa sababu imenibidi niache duka kubwa na gari,” alisema Said. 
Akizungumzia tukio hilo, mwenyekiti wa Kijiji cha Kilambo kilichopo mpakani na Msumbiji, Mohamed Mkama alisema wananchi wa kijiji chake wamekuwa wakishirikiana na wanakijiji wa vijiji jirani vya Msumbiji, lakini tukio hilo limewashangaza. 
Amesema mara nyingi wamekuwa wakitembeleana na hata wengine kutoka upande wa Msumbiji kuja kutibiwa Tanzania kutokana na ujirani mwema uliopo. 
“Kijiji changu kina vitongoji vitano ambavyo tumekuwa tukishirikiana na kijiji cha upande wa pili kwa muda mrefu na wengine wana vitambulisho vya uraia mwema, lakini tunashangaa kwanini wanarudishwa pasipo kuelezwa sababu,” alisema Mkama. 
Ofisa uhamiaji Mkoa wa Mtwara, Rose Mhagama alisema idadi ya Watanzania waliorudi na kusajiliwa katika mpaka wa Kilambo ni watu 221 hadi kufikia jana mchana. 
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya February 18

Share:

Vurugu za mgambo na machinga zaibuka tena Jijini Mwanza

Share:

Thursday 16 February 2017

NECTA yasitisha mtihani wa udahili kwa kidato cha kwanza Jambo Blog 10


BARAZA la Mitihani la Tanzania (NECTA) limesitisha mpango wa kuwafanyia mtihani wa udahili wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu katika shule za sekondari za serikali uliokuwa ufanyike Februari 28, mwaka huu.

Naibu Katibu Mtendaji wa Necta, Athumani Salumu alisema hayo juzi kwenye kikao cha wadau wa sekta ya elimu Mkoa wa Morogoro alipokuwa akihitimisha mada yake kwa wajumbe wa kikao hicho kilichoongozwa na mkuu wa mkoa huo, Dk Stephen Kebwe.

Salumu alisema mpango wa kuwafanyia mtihani wa udahili wanafunzi hao ulitokana na matakwa yaliyowasilishwa Necta na baadhi ya wakuu wa shule za serikali wakipendekeza kupitia maofisa elimu wa mikoa na wilaya kuwa wanafunzi wa kidato cha kwanza waliochaguliwa na kupangiwa shule zao wengi hawana sifa na uwezo wa kumudu masomo.

Naibu Katibu Mtendaji wa Necta alisema wakuu wa shule walikuwa wakiomba kupata idhini ya kuwafanyia mtihani wanafunzi ili kubaini uwezo wao na kwamba baraza liliwasiliana na maofisa elimu mkoa na wilaya likiwataka kuwasilisha orodha ya idadi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza waliopangiwa kwenye shule ya zao.

Alisema baada ya kufahamika idadi ya wanafunzi hao, baraza ndilo litatunga maswali ya mitihani yenye kuzingatia mfumo na vigezo maalumu na kutumiwa wakuu wa shule hizo ili kuusimamia kwa lengo la kuweka uzani sawa wa mtihani huo.

Alisema moja ya masharti ni kwamba mtihani huo ulitakiwa ufanyike kwa wanafunzi wa kidato hicho kwa shule zote za serikali siku moja na kwa muda uliopangwa.

Hata hivyo, alisema baada ya kuwatumia masharti hayo, wakuu wa shule hizo walishindwa kuwasilisha orodha ya wanafunzi kwa maofisa elimu wa mikoa na wilaya ili itumwe Necta na kutokana na mazingira hayo, baraza limeamua kusitisha kuwadahili wanafunzi wa kidato cha kwanza na kuitaka mamlaka inayosimamia elimu kuendelea na utaratibu wao wa kawaida.

“Necta imewasiliana na wahusika kwa barua rasmi ya kusitisha mtihani huo ambao ulipangwa ufanyike Februari 28, mwaka huu na wanafunzi wote waliopangiwa kidato cha kwanza shule mbalimbali za serikali zikiwemo za bweni, waendelee na masomo kama yalivyopangwa,” alieleza Naibu Katibu Mtendaji wa Necta.

Novemba mwaka jana, serikali ilitangaza kuwa wanafunzi 526,653 sawa na asilimia 94.8 ya waliofaulu mtihani wa darasa la saba mwaka jana, wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za sekondari za serikali katika awamu ya kwanza huku 28,638 wakishindwa kupangiwa shule katika awamu ya kwanza.

Kati ya wanafunzi hao, wasichana ni 268,052 sawa na asilimia 94.5 ya wasichana waliofaulu na wavulana ni 258,601 sawa na asilimia 95.2 ya wavulana waliofaulu.

Chanzo: Habari Leo
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger