Saturday 31 August 2019

UDOM- certificate and diploma selection 2019/20- Majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Udom (Cerificate na Diploma) 2019/2020

UDOM-SELECTED APPLICANTS FOR NON-DEGREE PROGRAMMES ROUND ONE FOR 2019/2020, UDOM- certificate and diploma selection 2019/20, UDOM- certificate and diploma selection 2019/20- Majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Udom (Cerificate na Diploma) 2019/2020, udom third round selection, diploma in pharmacy udom, udom second selection, udom diploma courses, diploma udom 2019/2020, udom diploma courses 2019 2020, udom diploma courses in health,… Read More »

The post UDOM- certificate and diploma selection 2019/20- Majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Udom (Cerificate na Diploma) 2019/2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

HALMASHAURI YA BUKOBA YAKUSANYA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI MOJA MWAKA WA FEDHA 2018/2019


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Murshid Hashim Ngeze.
Na Lydia Lugakila - Malunde 1 blog
Zaidi ya shilingi bilioni moja na Milioni mia tatu zimekusanywa na Halmashauri ya wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera Kwa Mwaka fedha 2018/2019 ambazo ni zaidi ya asilimia 97 za mapato kwa mwaka mzima.

Akizungumza leo Jumamosi Agosti 31,2019  katika kikao cha halmashauri hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo kilicholenga kufunga robo ya nne ya mwaka wa fedha 2018/2019,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Murshid Hashim Ngeze,amesema  mafanikio hayo yamekuja kutokana na kasi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kusimamia vizuri rasilimali mbalimbali za nchi.

"Mafanikio hayo yamekuja kutokana na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DkT. John Pombe Magufuli katika kusimamia vizuri rasilimali mbalimbali za nchi na ndo sababu kila kiongozi amewajibika kwa nafasi yake kuanzia ngazi ya juu mpaka ya chini kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania wote ujumla",ameeleza.
 

Ngeze amesema Halmashahuri hiyo imepiga hatua kubwa na kudai kuwa wakati wanaingia madarakani walikuwa wakikusanya zaidi ya shilingi milioni mia sita kwa mwaka lakini mpaka sasa wamevuka malengo kwa 100% kwa miaka minne wakiwa kwenye uongozi.

"Ni jambo la kumshukuru mungu nikikumbuka tulipoanzia hadi sasa ni hatua kubwa hii ni kutokana na juhudi kubwa za Rais wetu za mapambano yenye kuleta maendeleo amesema’’ ,amesema.


Mwenyekiti huyo ambaye pia ni diwani wa kata ya Rukoma amesema tayari ujenzi wa shule ya sekondari umeanza kwenye kata ya Rukoma ili kutatua changamoto inayowakabili wanafunzi wa kata hiyo wanaohangaika kufuata huduma ya elimu umbali mrefu na kulazimika kutembea takribani kilometa 38.

Hata hivyo Ngeze ametoa wito kwa wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla
Share:

WAHUNI WADUKUA AKAUNTI YA TWITTER YA MWANZILISHI WA TWITTER

Wadukuzi walichukua kwa muda udhibiti wa akaunti ya Twitter ya mwanzilishi na mkurugenzi wa mtandao wa kijamii wa Twitter.

Kundi la wadukuzi linalojiita Chuckling Squad limedai kuhusika na udukuzi wa akaunti ya Twitter ya Jack Dorsey.

Akaunti hiyo iliyo wa mashabiki zaidi ya milioni nne ilianza kutumiwa kusambaza taarifa za chuki na kibaguzi kwa kutumia lugha chafu kwa karibu dakika kumi na tano.

Twitter inasema mitambo yake haikufikiwa na wadukuzi na badala yake kulaumu kampuni ya mawasiliano ambayo haikutaja jina lake kwa kusababisha hitilafu hiyo.

"Nambari ya simu inayohusishwa na akaunti hiyo ilivamiwa kutokana na hitilafu ya kiufundi iliyosababishwa na kampuni hiyo ya mawasiliano ," ilisema taarifa iliyotolewa na Twitter.

"Hali hiyo ilitoa fursa kwa watu wasio na idhini ya kutumia nambari hiyo kuanza kutuma ujumbe kwenye mtandao wa Twitter."

Chanzo cha habari kutoka Kampuni hiyo ilithibitishia BBC kuwa wadukuzi walitumia mfumo unaojulikana kama "simswapping" kuchukua udhibiti wa akaunti ya Twitter ya Bw. Dorsey.

Huu ni mfumo ambao inatumiwa kuhamisha nambari halisi ya simu ya Dorsey katika laini nyingine- na kuanza kuitumia.

Wadukuzi mara nyingine hutoa hongo kwa wahudumu wa kampuni za mawasiliano au kuwapotosha kupata namabari halisi.

Kwa kuchukua udhibiti wa nambari hiyo wadukuzi waliweza kuandika ujumbe moja kwa moja katika akaunti ya Twitter ya Bw. Dorsey.

Japo siku hisi watumiaji wengi wa mtandao huo wanatumia programu tumishi kwenye simu zao kutuma ujumbe, awali Twitter ilibuniwa katika mfumo wa kutuma ujumbe mfupi- hali inayoisaidia kudhibiti idadi ya maneno mtumiaji anastahili kuandika.

Wadukuzi waliandika nini?

Ujumbe wa chuki na wa kibaguzi - ulitumwa moja kwa moja kwa kutumia akaunti ya @jack, na wengine wakasambaza ujumbe huo kwa kutumia akaunti zingine.

Ujumbe mmoja uliashiria kuna bomu limetegwa katika makao makuu ya kampuni hiyo.

Chuckling Squad imedai kuhusika na udukuzi wa Twitter za watu mashuhuri,kama vile mwanablogu wa masela ya urembo James Charles miongoni mwa watu wengine.

Japo tukio hilo linaonekana kufanyika nje ya kampuni hiyo, linasalia kuwa aibu kwa mtandao wa kijamii wa Twitter, unaotoa huduma kwa viongozi wenye nguvu zaidi ulimwenguni.
Chanzo- BBC
Share:

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Akutana Na Waziri Mkuu Wa Japan, Rais Wa JICA

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe na kuishukuru Serikali ya Japan kwa ushirikiano inaoutoa kwa Tanzania.

Amekutana na kiongozi huyo leo (Jumamosi, Agosti 31, 2019) katika hoteli ya The New Otani, Tokyo Japan. Amesema Tanzania inaheshimu uhusiano mzuri uliopo kati yake na Japan

Mazungumzo yao yalihusu masuala mbalimbali yakiwemo ya kidiplomasia pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayofanywa kwa ushirikiano kati ya Japan na nchi yetu.

Waziri Mkuu ameishukuru Japan kwa misaada mbalimbali ya maendeleo inayoitoa nchini ambayo imesaidia katika kujenga uchumi na kuwaondolea wananchi kero mbalimbali

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wafanyabiashara na wawekezaji hususan wenye viwanda wawekeze nchini ili washirikiane na Watanzania kukuza uchumi.

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kukuza uchumi na kufikia wa kati ifikapo 2025 kupitia sekta ya viwanda.

“Japan imepiga hatua kubwa katika tekinolojia hivyo naamini kuwa  wafanyabiashara na wenye viwanda  kutoka Japan wakiwekeza Tanzania wataleta tekinolojia yao pia.”

Awali, Waziri Mkuu alikutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Shinichi Kitaoka.

Katika mazungumzo hayo kiongozi huyo wa JICA alisema wameridhia kuwa wataendelea kushirikiana na Tanzania kwa kutia saini mikataba mbalimbali yenye lengo kuinua maisha ya watanzania na kujenga uchumi.

Waziri Mkuu aliishukuru JICA kwa ushirikiano unaoutoa nchini likiwemo suala la kuendelea kuwapokea wanafunzi wa Kitanzania na kuwasomesha katika taaluma mbalimbali. Amesema Tanzania inathamini sana mchango unaotolewa na JICA katika ujenzi wa barabara, huduma za Afya na elimu.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMAMOSI, AGOSTI 31, 2019.


Share:

Waziri Lugola Awataka Maafisa Uhamiaji Kuepuka Rushwa na Kutokuwanyanyasa Wawekezaji Nchini

Na Felix Mwagara, Moshi (MOHA).
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amewataka Maafisa Uhamiaji nchini, kuepuka rushwa na kutokuwanyanyasa wageni na hasa wawekezaji nchini.

Akizungumza katika kikao cha Maafisa Uhamiaji Waandamizi kilichofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Uhamiaji (Trita), Mjini Moshi, leo, Lugola alisema wawekezaji ni watu muhimu katika maendeleo ya nchi, hivyo wanaposumbuliwa kwa kunyanyaswa bila sababu za msingi ni kuvunja misingi ya uadalifu.

Pia Waziri Lugola aliwataka maafisa hao waache kutoa PI (tangazo la kuondolewa mtu asiye raia nchini) zenye utata kwa maslahi binafsi bila kuzingatia athari ambazo nchi inazipata.

“Yapo malalamiko kwamba kuna wageni wanaingia nchini na kuwekeza kwa ubia na Watanzania, biashara inapokuwa inaendelea Watanzania huwazunguka wageni na kuwatengeneza mazingira ya kuwafukuza ili wapate fursa ya kumiliki hizo biashara na hapo ndipo Idara ya Uhamiaji hutumika, acheni hayo mambo kwa kuwa yanatuchafua kama taifa letu,” alisema Lugola.

Aliongeza kuwa, Rais John Magufuli anatafuta wawekezaji kwa nguvu na kuwahakikishia usalama wao na biashara zao lakini baadhi ya watumishi wa umma badala ya kusaidia jitihada hizi wao wanatumika kuwafukuza kwa dhuluma.

Alisema wageni hao wakishafukuzwa na wanaacha uwekezaji wao nchini ambao wanadhulumiwa huko waliko wanaisema nchi vibaya na kwa uzoefu huo wageni wengine hawawezi kuja nchini.

“Tujitathimini, tuzingatie sheria, kanuni, taratibu na miongozo yetu kwa kuzingatia maslahi ya taifa, pia nawasihi sana mumsaidie mheshimiwa Rais kutimiza ahadi zake kwa Watanzania ambazo amezitoa kupitia Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 na ahadi zake nyingine mbalimbali ambazo amekuwa akiahidi na kuzitekeleza,” alisema Lugola.

Aidha, Waziri Lugola kabla ya kukifungua kikao hicho kilichojumuisha Maafisa kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, alisema kikao hicho kitakuwa chachu ya kudumisha maadili ya kazi, nidhamu, utii, na ushirikiano katika maeneo yao ya kazi ili kwenda sambamba na kauli mbiu ya Idara hiyo ya Upendo, Mshikamano, Uwajibikaji na Kukataa Rushwa.

“Ni imani yangu kuwa, mtaendelea kutekeleza majukumu yenu kwa kuzingatia Sheria, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma katika utoaji wa huduma bora kwa Wananchi,” alisema Lugola.

Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala, alisema kikao hicho zitatolewa mada mbalimbali zitakazowasilishwa kuhusu rushwa na Kanuni za Uendeshaji za Uhamiaji za Mwaka 2018 ambazo ndio mwongozo wa utendaji kazi wa  Idara ya Uhamiaji.

“Kwa kuwa Idara yetu ya Uhamiaji inatoa huduma mbalimbali kwa wananchi ikiwemo pasipoti, vibali vya ukaazi, pasi pamoja na viza, hivyo kupitia kikao hiki tutazingatia kikamilifu mada hizo kwa kuwa zitatusaidia katika kutoa huduma bora kwa maslahi ya Idara yetu, Wizara na taifa kwa ujumla,” alisema Dkt. Makakala.


Share:

Taarifa Kwa Umma: Kuhusu Mwenendo Wa Mlipuko Wa Ugonjwa Wa Ebola Ulioripotiwa Nchi Jirani Za Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo Na Uganda.




Share:

Jeshi la Polisi Latoa Onyo Kwa Watakaofanya Vurugu Wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mtaa

Jeshi la Polisi nchini limewatahadharisha wale wote watakaoleta vurugu wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa  na kusema watachukuliwa hatua kali za kisheria

Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini David Misime, ambaye amesema kuwa watu wakifuata sheria chaguzi zote nchini zitabaki kuwa na amani.

“Wale ambao wanahisi watatingisha kiberiti kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa, sisi tumejipanga vizuri kukabiliana nao kwa nguvu zote kwa jinsi ambayo tutazidi kupokea nguvu toka kwao au ubishani toka kwao” amesema Misime.


Share:

Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ afunga ndoa rasmi

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Mhe.Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la SUGU, leo Agosti 31, 2019 amefunga ndoa na Happiness Msonga katika  Kanisa la Katoliki Ruanda, jijini Mbeya.


Share:

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume


Super nzoka  IKEMEKO   TRDITONAL clinic ;

Ni dawa ya Asili  iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 
 
Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji  ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 .
 
Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0789289945.Au whasap/0716343218 TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya mustang


Share:

Wanaoihujumu Serikali na Kusababisha Ndege ya Tanzania Kushikiliwa Afrika Kusini Kufunguliwa Mashitaka

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt Hassan Abbas amesema serikali itawafungulia kesi ya kuhujumu nchi watu wote watakaobainika kuihujumu serikali juu ya kukamatwa kwa ndege ya Tanzania nchini Afrika Kusini, pindi kesi iliyoplekea kukamatwa ndege hiyo itakapomalizika.

Akizungumza mjini Dodoma leo Jumamosi Dk Abbas amesema wapo Watanzania wanaishiriki kuihujumu Serikali  kuhusu ndege hiyo, kwamba kuna siku uhujumu huo utawasaidia.

“Wapo wazawa wanaofanya mawili matatu kuhujumu nchi lakini niwaeleze tusubiri kesi iishe huko Afrika Kusini, tutawafungulia kesi ya kuhujumu nchi yetu.”

“Hakuna Nabii katika historia ya Manabii aliyewahi kuaminiwa kwa asilimia 100, hivyo huwezi kukubaliwa na watu wote, hata hii ndege inayoshikiliwa ikija Tanzania ipo siku wanaochukia watatumia usafiri huo kwenda Afrika Kusini kama sio wao basi watoto wao,” amesema Dk Abbas.

Jana Mawakili wanaoiwakilisha Tanzania katika kesi ya kuzuiwa ndege hiyo waliitaka mahakama Kuu ya Afrika Kusini kutupilia mbali zuio la kuzuia ndege ya shirika hilo ya Airbus A220-300, wakisema ilitolewa kimakosa.


Share:

KIJANA ASULUBIWA KAMA YESU KWA KUPIGILIWA MISUMARI KARIBU NA KITUO CHA POLISI


 Polisi nchini Uganda inachunguza kisa cha mwanamume mmoja aliyeshambuliwa kisha kupigiliwa misumari katika msalaba.

Inadaiwa mwanaume mwenye umri wa miaka 21 alishambuliwa na watu wawili wasiojulikana Alhamisi Agosti 29,2019 kwa madai ya kuunga mkono chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) kinachoongozwa na Rais Yoweri Museveni.

Polisi nchini Uganda ilimtaja mwanaume huyo kuwa ni Baker Kasumba anayedaiwa kushambuliwa na watu hao alipokuwa akitoka kazini kuelekea nyumbani kwake eneo la Kalerwe.

Gazeti la Daily Monitor la Uganda limeripoti kuwa Kasumba alidaiwa alishikwa na kupigiliwa misumaru kwa nyundo na watu hao waliokuwa wamevaa kofia za chama cha NRM zinazovaliwa na wanachama wa chama hicho.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, mwanaume huyo alipata usaidizi kutoka kwa wapitanjia waliomkuta akining’inia katika msalaba huo akiwa amewekewa kofia ya chama hicho katika mikono yake na kumpeleka katika Kituo cha polisi cha Kalerwewa kwa ajili ya kuripoti tukio hilo.

Inadaiwa kuwa mwanaume huyo aliokolewa na wanawake wawili walioshuhudia tukio hilo na kupiga mayowe hatua ambayo iliwafanya washukiwa kukimbia na kumuacha akining’inia.

Mwanaume huyo ambaye ni mfuasi wa chama cha NRM katika maelezo yake aliyoandika polisi alisema watu hao walimueleza kuwa wameamua kumsulubu ili afe kwa ajili ya chama anachokienzi.

Polisi wanadai kuwa kabla ya tukio hilo mwanaume alionywa na mfanyakazi mwenzake kutomuunga mkono Rais Museveni na chama chake.

Tukio hilo limeibua mjadala katika mitandao ya kijamii ambako wananchi wa Uganda wamelaani na kuonya siasa za chuki.

Kupitia mtandao wake wa Twitter, Judith Kukundakwe Asiimwe anadai kuwa hatua hiyo ni njama ya inayoendeshwa na kikosi maalum cha usalama kinachofahamika ili kuchafua sifa ya vijana wa chama cha upinzani.

Roxanne Daphne aliandika “hili ni kosa kubwa sana, sote tuna uhuru wa kuwa na maoni yetu ya kisiasa''aliandika.

Hata hivyo, Naibu msemaji wa polisi mjini Kampala, Luke Owoyesigyire alisema kuwa tayari polisi wameanza msako ili kubaini watu hao.

Tukio hilo la kushangaza kwa mujibu wa Daily Monitor lilitokea karibu mita 30 kutoka Kituo cha polisi cha Kibe na mpaka sasa mwanaume huyo anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali kuu ya Mulago.


Share:

MBUNGE WA CHADEMA JOSEPH MBILINYI 'SUGU' AFUNGA NDOA


Na Godfrey Kahango, Mwananchi 
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu leo Jumamosi Agosti 31, 2019 amefunga ndoa na Happiness Msonga katika Kanisa Katoliki Ruanda jijini Mbeya.

Katika misa hiyo wabunge 10 wa Chadema walihudhuria wakiongozwa na Meya wa Jiji la Mbeya, Mchungaji David Silinde.

Wabunge hao ni Frank Mwakajoka (Tunduma); Anthony Komu (Moshi Vijijini); Lucia Mlowe, Sophia Mwakagenda na Lucy Mollel (wote Viti Maalum).

Wengine ni Joseph Haule (Mikumi); Joseph Selasini (Rombo); David Silinde (Momba); Pascal Haonga (Mbozi) na Wilfred Lwakatare (Bukoba Mjini).

Viongozi wa Chadema walioshiriki misa hiyo ni mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Nyasa, Sadick Malila na katibu wake, Emmanuel Masonga.
Share:

MKUTANO MKUU WA MABALOZI WA USALAMA BARABARANI 'RSA' WAFANYIKA JIJINI MWANZA


Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani Marlin Komba,akizungumza na Mabalozi wa Usalama barabarani Nchini.(RSA ) katika mkutano mkuu uliofanyika Jijini Mwanza Agosti 30,2019 .Picha zote na Vero Ignatus.
John Seka Afisa mtendaji mkuu wa Taasisi ya Mabalozi wa Usalama Barabarani nchini (RSA) akizungumza na mabalozi katika mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika Jijini Mwanza.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani Marlin Komba ,akisisitiza jambo katika mkutano mkuu wa mwaka wa mabalozi wa usalama barabarani uliofanyika Jijini Mwanza.
Mabalozi wa usalama barabarani nchini wakiwa katika mkutano mkuu wa Mwaka uliofanyika Jijini Mwanza 
Moja ya timu wapenzi na marafiki wa Simba Sports Club wakiwa uwanjani kwa ajili ya mchezo wa kirafiki katika Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza
Moja ya timu wapenzi na marafiki wa Yanga sports Club wakiwa uwanjani kwa ajili ya mchezo wa kirafiki katika Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.

Baadhi ya mabalozi wa Usalama barabarani wakiwa katika picha ya pamoja 
Mabalozi wa usalama barabarani wakionekana katika picha ya pamoja 
Na .Vero Ignatus ,Mwanza

Zaidi ya mabalozi 125 kutoka Taasisi ya Mabalozi wa Usalama barabarani( RSA ) wamekutana Jijini Mwanza,lengo kuu likiwa ni kutoa elimu na kuwajengea wananchi uwezo wa kuwa sehemu ya mabadiliko ya usalama barabarani ikiwa ni namna ya kusaidia
kupunguza ajali ,kwani kila raia wa Tanzania anawajibu wa kuwa sehemu ya mabadiliko ya usalama barabarani.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika Agosti 30,2019 jijini Mwanza,Afisa mtendaji Mkuu wa Taasisi ya mabalozi wa usalama barabarani nchini, John Seka  alisema kwa kushirikiana na jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza kikisimamiwa na RTO,Tanroad ,Jeshi la zimamoto, walifanya zoezi za kurudishia alama za barabarani zile zilizopauka ,na kuchora mpya sehemu zinazohitajika.

Seka alisema kuwa kazi zao kubwa kama RSA ni kukemea, kuelimisha ,kutoa taarifa pale dereva anapokwenda kinyume na taratibu na sheria za usalama barabarani ili kuhakikisha kuwa ajali zinapungua kama siyo kwisha kabisa

“Sisi tunafanya kazi zetu kama polisi jamii,macho yetu tunayaelekeza kwa kutambua kuwa jeshi la polisi peke yao hawawezi kwani askari ni wachache na vitendea kazi ni vichache je! sisi kama wananchi hatuna wajibu wa kupunguza?", alihoji Seka.

Mkurugenzi wa tafiti za kisheria kutoka RSA,Augustus Fungo alisema pamoja na kuwa balozi lazima wazingatie sheria za usalama barabarani pia lazima wafuate sheria kama utaratibu unavyoagiza

Alisema hadi sasa RSA wanatekeleza mradi wa Maboresho
ya sheria ya usalama barabarani,wenye lengo la kushawishi serikali na bunge kubadili sheria ya usalama barabarani ya
mwaka 1973 ili ikidhi mahitaji ya wakati huu kwasababu ina mapungufu katika maeneo mbalimbali.

"Mfano wa mapungufu hayo ni pamoja na sheria ya sasa kutomlazimisha abiria kuvaa kofia ngumu,kufunga mkanda,kutokulazimu magari madogo kuwa na vizuizi vya watoto wakiwa ndani ya gari (child restraint) Sheria pia hailazimishi magari yote kusimama kabla ya kuvuka kivuko cha reli isipokuwa magari ya abiria na mizigo",alisema Fungo.

Alisema hadi sasa RSA imefanikiwa kufungua klabu za usalama barabarani kwa wanafunzi katika shule 22,ambapo 10 kutoka mkoa wa Kilimanjaro,12 mkoa wa Pwani, amesema matazamio ya baadaye ni kupanua wigo wa shule zinazopata elimu ya usalama barabarani nchini Tanzania.

“Kwa kuwa tunaamini watoto wakifundishwa tangu wakiwa wadogo ni rahisi wao kuelewa zaidi kwao kutii sheria na
kujiepusha na ajali”,alisema Fungo.

Naye mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, Marlin Komba alimtaka kila balozi kutimiza wajibu wake kwa
kuzingatia maadili,bila kuwa na ushabiki wowote,pasipo kuwatetea wavunja sheria za usalama barabarani,badala yake watumie ubalozi wao kwenye kuelimika na kupata maarifa.

Aliwataka kwenda kuwa mabalozi kwa watu wengine ili kufanya maamuzi sahihi kuzingatia sheria na usalama barabarani ,na kuepuka lugha za matusi kwani ni kosa la jinai,huku akiwaonya baadhi ya mabalozi kutokutumia nembo ya RSA kukashfu watu
wengine.

Mkutano huo uliambatana na michezo mbalimbali ukiwemo mchezo wa mpira wa miguu,kuvuta kamba kufukuza kuku na mbio za magunia ,ambapo michezo yote ilifanyika katika uwanja wa mpira wa Nyamagana Jijini Mwanza.

Kauli mbiu ya Mkutano wa  mabalozi wa usalama barabarani ni 'Uchumi wa Viwanda unahitaji kufanyika kwa mabadiliko ya sheria ya Usalama Barabarani,ili kulinda rasilimali watu dhidi ya ajali'. 

Share:

WAZIRI MWAKYEMBE : SERIKALI IMEJIPANGA KUMALIZA CHANGAMOTO YA MIUNDO MBINU YA VIWANJA VYA MPIRA



Na Lydia Lugakila - Malunde 1 blog
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejipanga kumaliza changamoto ya miundombinu mibovu ya viwanja vya mpira nchini ili kuwezesha sekta ya michezo kufanya vizuri.


Kauli hiyo imetolewa jana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa mkoani Kagera katika mkutano na wadau wa sekta ya habari utamaduni sanaa na michezo uliofanyika katika ukumbi wa mkoa uliopo katika Bukoba manispaa.

Waziri Mwakyembe alisema anatambua sekta ya michezo kuwa sehemu muhimu na kwamba wanamichezo wanafanya kazi kubwa licha ya kukumbana na changamoto ya miundo mbinu mibovu ya viwanja vya michezo.

Alieleza kuwa tatizo la miundo mbinu mibovu ya viwanja limekuwa likipigiwa kelele mara kwa mara na wanamichezo licha ya kuonyesha juhudi kubwa katika michezo kwa kuendana na miundo mbinu hiyo mibovu.

"Changamoto hii itamalizika mwaka huu,   tutalifanyia kazi jambo hili ili kupunguza kelele za viwanja vibovu vya soka nchini",alisema.

Licha ya changamoto hiyo waziri huyo aliwasihi wana michezo kutokata tamaa huku akiitaka Mikoa ya jirani na wana kagera kwa ujumla kujitokeza kwa wingi Septemba 4 wiki ijayo kuishangilia timu ya Taifa Stars inakutana kumenyana na timu ya Burundi,  mchezo ambao ameuataja kuwa ni muhimu sana kwa Watanzania.

"Siri kubwa ya mafanikio ni mazoezi Vijana hakuna kusema kiatu kimebana tunakwenda kuifunga Burundi ninachowaomba wana Kagera, Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mikoa jirani twendeni Burundi tukaishangilie timu yetu", alisema. 

Hata hivyo alisema Rekodi ya Tanzania ni nzuri kwani timu ya watoto wa kike chini ya miaka 17 ilikaribishwa Afrika Kusini kimichezo na kuwabamiza mabao 8-0 na kurudi Tanzania na kombe ikiwa ni mara ya tatu kuchukua ubingwa.
Share:

Mo Dewij awaomba msamaha Mashabiki wa Simba

Muwekezaji wa simba SC  Mohamed Dewij amefunguka na kuonyesha jinsi alivyoumizwa na matokeo mabaya ya timu ya Simba dhidi ya wapinzani wao kutoka Msumbiji UD Songo katika michuano ya klabu bingwa Afrika baada ya kutolewa mapema kwenye michuano hiyo

Hii imekuja baada ya Simba kupata sare ya 1-1 wakati mchezo wa kwanza nchini msumbiji matokeo yalikuwa 0-0, hivyo goli la ugenini liliwabeba UD Songo na Simba kutupwa nje ya michuano licha ya msimu uliopita kufanya vizuri kwa kufika hatua ya robo fainali.

Kupitia kiurasa zake za mitandao ya kijamii Mo Dewij ameandika hivi:-

Wanasimba, mnisamehe kwa ukimya. Maumivu ya matokeo yametupata sote. Naomba tukumbushane: Sisi ni SIMBA! Simba lazima anyanyuke! Hawezi kukata tamaa.

Niwaombe tusivunjike moyo wala kukata tamaa. Hatutaogopa maneno ya watu na hatutaacha kupambana na kujipanga kwa ajili ya malengo yetu. Msimu huu tutautumia kikamilifu kuhakikisha tunaboresha mipango yetu ili msimu ujao turudishe furaha kwa Wanasimba wote.

Tumwombe Mwenyezi Mungu atutangulie katika safari yetu endelevu. Tukumbushane tena: Roma haikujengwa kwa siku moja. Tuwe wavumilivu, tutafika tu Insha’Allah. 🙏🏽


Share:

Kesi Ya Vigogo CHADEMA Yapigwa Kalenda

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,  jana ilishindwa kuendelea na ushahidi katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema, akiwemo mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, kutokana na wakili wa washtakiwa hao, Peter Kibatala kutokuwepo mahakamani.

Kibatala alitakiwa jana Ijumaa Agosti 30,2019 kumhoji shahidi wa saba katika kesi hiyo, Victoria Wihenge ambaye ni Ofisa Uchaguzi kutoka Manispaa ya Kinondoni,  lakini hadi kesi hiyo inaahirishwa alikuwa hajatokea Mahakamani.

Uamuzi wa kuahirisha kesi hiyo ulitolewa na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba ambapo aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 10, 11 na 12, 2019 itakapoendelea.


Share:

Watu 5 wafariki baada ya gari la dangote kugongana na gari dogo Rufiji mkoani Pwani.

Watu watano wamefariki baada ya Gari la Dangote lililokuwa limebeba malighafi ya kutengenezea saruji likielekea Mtwara kugongana na Gari dogo na kupinduka kisha kuwaka moto baada ya kupoteza muelekeo na kugonga nguzo ya umeme ikaanguka na waya wenye moto ukanasa kwenye bodi ya gari hiyo ya Dangote ndipo watu wa 4 wakafariki papo hapo na mmoja aliyekuwa kwenye gari dogo akafariki wakati akipatiwa matibabu, wilayani rufiji mkoani Pwani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji, Onesmo Lyanga  amethibitisha tukio hilo  ambapo ameeleza kuwa gari ndogo Toyota Premio ilikuwa ikitokea kwenye makazi ya nyumba za walimu wa sekondari ya Kibiti eneo la Kinyanya, ikiingia katika barabara kuu inayotoka Dar es Salaam kwenda Mtwara  bila kuzingatia sheria na ndipo ikagongana na gari kubwa la Dangote.

Amesema gari la mzigo la Dangote lilipoteza muelekeo, likaelekea kulia zaidi mwa barabara na kutoka nje na kwenda kugonga nguzo ya umeme, wakati hiyo nguzo ya umeme inadondoka waya wa umeme ukanasa kwenye bodi ya gari na wote waliokuwepo kwenye gari hiyo ya Dangote waliteketea kwa Shoti hiyo ya umeme.


Share:

Aua Mkewe Kwa kumnyonga shingo kisha kujiua kwa kunywa sumu.

Mkazi wa kijiji cha Iponya katika Halmashauri ya Mji wa Kahama, Paschal Clement (32), amemuua mkewe Ashura Paschal (30) kwa kumnyonga shingo kisha kujiua kwa kunywa sumu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Richard Abwao, alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa moja jioni katika kijiji cha Iponya.

Alisema chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi na kwamba kabla ya tukio hilo, wanandoa hao walikuwa na ugomvi huku mume akimtuhumu mkewe kuwa si mwaminifu kwenye ndoa.

Abwao alisema Paschal baada ya kutekeleza mauaji hayo, alijiiua kwa kunywa sumu ambayo mpaka sasa bado haijafahamika ni ya aina gani na kukutwa chumbani kwake akiwa amelala sakafuni.


Share:

Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi aridhishwa na miradi ya SUMA JKT Kanda ya Ziwa

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi amesema anaridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na miradi inayotekelezwa na SUMA JKT kanda ya Ziwa.

Dkt. Mwinyi akiwa kwenye ziara yake ya kukagua miradi inayotekelezwa na SUMA JKT pamoja na makampuni mengine yaliyo chini ya Wizara hiyo kanda ya Ziwa  tarehe 30/08/2019 katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga amesema kwa kiwango kikubwa ameridhishwa na kazi zinazofanywa na sehemu kubwa kazi zimekwenda kwa kiwango kinachotarajiwa na kuwa changamoto zilizopo zitafanyiwa kazi.

“Niwahakikishie Mikoa na Halmashauri zinazohusika na miradi inayotekelezwa na SUMA JKT changamoto zote zitafanyiwa kazi” amesema Dkt. Mwinyi.

Aidha, amemshukuru Mhe. Rais John Magufuli kwa kuiamini kampuni hiyo iliyo chini ya Wizara yake na ndiyo sababu ya yeye kufanya ziara hiyo ili kuhakikisha imani hiyo inadumu pamoja na kuwaomba viongozi wote wa Mikoa na Halmashauri kuendelea kuiamini.

Aidha, amewataka SUMA JKT kuongeza kazi ya ziada mara watakapopata fedha ili kukamilisha jengo la Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambalo ujenzi wake umesimama kutokana na changamoto ya fedha.

Naye Mkurugenzi wa SUMA JKT Kanali Rajab Mabele amesema kuwa, kampuni hiyo imepiga hatua kubwa hasa katika nyanja ya ujenzi lakini pia inajihusisha na kazi nyingine mbalimbali ikiwemo kilimo na ufugaji.

Awali, akimkaribisha Dkt. Mwinyi Mkoani hapa, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemuomba kupitia kampuni ya SUMA JKT kuangalia jinsi ya kuwa na miradi ya kuvuna maji ili wananchi waweze kujishughulisha na kilimo cha umwagiliaji.

“Pamoja na kiangazi kilichopo, tunapata mvua nyingi sana na tunavuna mpunga unaoweza kulisha nchi yote, sasa tuone namna bora ya kuvuna hayo maji na tayari baadhi ya wananchi wameshaanza kuchimba mashimo makubwa ya kuvuna maji, tumeona kama Mkoa tufanye hilo ili wananchi wetu waweze kupata mpunga” amesema Telack.


Share:

Polisi Pwani Yakamata Shehena Ya Vipodozi Feki

NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
JESHI la polisi mkoani Pwani, linamshikilia Albert Kiwia (45) mkazi wa Kimara Dar es salaam kwa kosa la kusafirisha shehena ya vipodozi feki mbalimbali ,kwa kutumia gari aina ya Toyota Nissan.

Katika hatua nyingine, jeshi hilo limefanikiwa kukamata madumu saba ya mafuta ya diezel yakiwa na ujazo wa lita 20 kila moja mali inayodhaniwa kuwa ni ya wizi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani,Wankyo Nyigesa aliwaambia waandishi wa habari kuwa ,mtuhumiwa huyo amekamatwa agost 29 mwaka huu, katika eneo la Mizani ya zamani -Kibaha Mji .

Alifafanua, licha ya tuhuma hiyo ya kusafirisha vipodozi hivyo ,jeshi hilo likamtaka aonyeshe kwa TRA stakabadhi alizolipia ushuru katika mipaka ya nchi wakati akiingiza vipodozi na hakuwa navyo

Aliwataka ,wafanyabiashara wenye tabia ya kuingiza bidhaa zao nchini kwa kukwepa kulipa kodi ,kuacha mara moja .

Wankyo alisema ,wamedhibiti mianya yote kwa wale wanaojaribu kukwepa kulipa kodi katika barabara zote za mkoa na wale watakaokamatwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Hata hivyo, akielezea kuhusiana na tukio la kukamatwa madumu ya mafuta ya diezel ,alisema madumu hayo yamekamatwa ,eneo la Misugusugu ,Kibaha baada ya mtu aliyekuwa na mafuta hayo kuyatelekeza na kukimbia baada ya kuona gari la polisi likielekea mahali alikokuwa .

Wankyo alitoa wito kwa jamii kuacha kuhifadhi madumu ya mafuta aina ya diezel na petrol ndani ya nyumba kwani ni hatari.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi August 31




Share:

Friday 30 August 2019

MWENDESHA BODABODA ALIYEFARIKI KWA AJALI AZUA GUMZO KUACHA WAJANE 6 NA WATOTO 30

Siri nyingi hufichuka wakati ambapo binadamu anafariki kwani licha ya kuwa ni kinyume na itikadi kumuanika aliyeaga dunia, mambo mengine hasa ya kifamilia huwa vigumu kuyaficha. 

Hayo ndiyo yalifichuka baada ya dereva mmoja wa bodaboda aitwaye Hassan Mafabi (51) mkazi wa Nakatundu Kangulumira nchini Uganda kufariki dunia kwenye ajali ya barabarani pikipiki yake kugongana na gari siku ya Jumamosi wiki iliyopita.

Bodaboda huyo alikuwa na wake 6 na watoto 30 licha ya kazi yake yenye malipo ya wastani hali iliyosababisha watu wengi kushangaa ni vipi aliweza kutekeleza mahitaji ya wake hao wote. 

 Wengi wamepigwa na butwaa baada ya matangazo kuwafikia kuhusu mchango wa kusaidia familia ya marehemu kwani ameacha wajane sita na watoto 30.

Hassan Mafabi mwenye umri wa miaka 51 alikuwa akiishi na wake hao sita na watoto wake na kuchapa kazi kama kawaida huku wengi wasijue kuwa alikuwa na familia kiasi hicho.

 Kulingana na Ugandanz.com, Mafibi aliishi katika kijiji kimoja nchini humo tangu kifo chake barabarani ambapo aligongwa na gari. 

Askofu wa kanisa la Mukono nchini humo alidhibitisha kisa hicho na kuwataka marafiki kujitokeza kuisaidia familia ya Mafibi kwani yeye ndiye alitegemewa kuilisha. 

Wengi hata hivyo walishangaa ni vipi mwendesha bodaboda huyo aliweza kuwalisha wake hao pamoja na watoto 30 ikizingatiwa mapato ya biashara ya bodaboda ni ya wastani tu.
Share:

SANAMU TATA YA TRUMP YAZUA GUMZO

Sanamu ya mbao ya Donald Trump, iliyotengenezwa na Tomaz Schlegl, ilisimamishwa wiki kadhaa baada ya sanamu ya Melania Trump

Sanamu ya mbao ya rais wa Marekani imejengwa katika nchi alikozaliwa mkewe ya Slovenia, imeibua maoni tofauti.

Ikiwa na urefu wa karibu futi 26, sanamu hiyo ilijengwa katika ardhi ya kibinafsi na inamuonyesha Donald Trump akiwa na kichwa cha muundo wa mraba na kidevu huku akiwa anyenyenyua kichwa juu.

Msanii aliyeitengeneza amekiambia shirika la habari la AFP kuwa alitaka iwe kama kielelezo cha maoni ya kisasa ya wanaohisi kuwa watawala wa kisiasa hawawajali.

Sanamu hii imewekwa baada ya ile ya mke wa trump, Melania inayomuonyesha akiwa na ulimi uliojaa ndani ya mashabu.

Sanamu ya Melania, iliyochongwa ndani ya mti viungani mwa mji alikozaliwa wa Sevnica, inamuonyesha akiwa amevalia koti la rangi ya blu huku mkno wake ukionyesha angani. baadhi ya wakazi wanaichukulia kama ''aibu'', na wanasema inaonekana zaidi kama katuni kuliko mke wa rais wa Marekani.Mnara huu wa Trump unaripotiwa kujengw ana msanii wa Slovenia Tomaz Schlegl


Sanamu mpya ya rais wa Marekani ilijengwa katika kijiji cha Sela pri Kamniku, yapata kilomita 30 kusini -mashariki mwa mji mkuu wa Slovania -Ljubljana.

Mbunifu wake, Tomaz Schleglameliambia shirika la habari la AFP kwamba alilenga kutoa maoni ya wengi kupitia sanamu.

"Kwa mara ya kwanza ttangu Vita ya II ya dunia ndio mara ya kwanzamaoni ya wengi yanajitokeza kupinga utawala uliopo : Mtazame waziri mkuu wa Uingere za Boris Johnson, tazama Trump, rais wetu au waziri mkuu wa Hungary Viktor Orban. Dunia hii inaelekea wapi ?," alisema. "Tunataka kufungua macho ya watu kuelewa demokrasia ni nini ."
sanamu ya Bwana Trump inamuonyesha akiwa amevalia shati la blu na tai nyekundu, huku akiwa amesimama mithili ya mnara wa uhuru wa New York.

Bwana Schlegl anasema muundo wa ndani ya sanamu ya mbao unairuhusu kubadilika kutoka "sura ya urafiki mnamo siku za kazi za wiki na kuwa na sura ya kutisha sana katika siku za wikendi ", ikiwa ni sihara ya unafiki wa wanasiasa wanaotaka kuonyesha kuwa wanawajali wale wanaohisi kuwa wamesahaulika.

Lakini mnara huu umeibua maoni tofauti . Shirika la habari la AFP ililishuhudia mkazi mwenye hasira akiendesha gari lake la trekta na kugonga mnara huo wa sanamu wiki hii wakati maandalizi ya kuufungua rasmi Jumamosi yakiendelea.

Baadhi ya wakosoaji wa sanamu hiyo wamelalamikia juu ya "uharibifu wa mbao " na wakasema isingepaswa kujengwa .

"Majirani zetu wanadai sanamu hii ina sura mbaya na kwamba haifai katika eneo letu hili zuri tambalale ," Alisema Bwana Mr SchleglMnara huu wa Trump unaripotiwa kujengwa na msanii wa Slovenia Tomaz Schlegl

Watu wa Slovania wana maoni tofauti kumuhusu Rais wa Marekani . Mji anakotoka mkewe Mellania umekuwa ni kitovu cha utalii tangu alipochaguliwa mwaka 2016.

Huku wageni wakija kupata taswira ya mahali alikozaliwa na kuishi enzi za utoto wake , wakazi wametengeneza bidhaa zenye nembo ya melania zikiwemo kandambili, keki na baga zenye sura ya Trump na zilizopambwa na jibini iliyotengenezwa kama " nyweli" za Trump.

Japokuwa sanamu ya Mke wa rais ikiibua ukosoaji mwezi uliopita , mmoja wa wakazi wa eneo hilo ameliambia shirika la habari la AFP n kwamba kazi ya sanaa kuihusu lilikuwa ni " wazo zuri".

"Melania ni shujaa wa Slovenian , amefikia mafanikio ya juu nchini Marekani ," alisema Katarina, mwenye umri wa miaka 66.
Chanzo - BBC
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger