Thursday 31 January 2019

SIMBA YAMUUZA KICHUYA MISRI



Kichuya (kushoto) akiwa na Okwi

Baada ya jana klabu ya Simba kuweka wazi kuwa ipo kwenye mazungumzo ya mwisho na klabu ya Pharco ya Misri juu ya uhamisho wa Kichuya, hatimaye leo dili hilo limekamilika na Kichuya sasa si mchezaji wa Simba tena.

Akiongea na www.eatv.tv Mtendaji mkuu wa Simba Crescentius Magori amesema Kichuya amesaini mkataba wa miaka 4 na klabu hiyo pamoja na malipo mazuri ambayo hata Simba hawakuwa wanamlipa.

''Kichuya ni kijana wetu na klabu imefaidika naye sana hivyo tunafurahi amepata timu ya daraja la pili na itamlipa vizuri na sisi kama Simba tumepata maslahi mazuri kwahiyo tumemuuza'', amesema.

Kichuya ambaye alisajiliwa na Simba akitokea Mtibwa Sugar atacheza ligi kuu ya Misri licha ya kuwa amesajiliwa na Pharco ambapo kwa mujibu wa Magori ni kwamba tayari timu hiyo imemtoa kwa mkopo katika klabu ya Enppi inayoshiriki ligi kuu.

Tayari Kichuya amesharipoti katika timu ya Enppi na kesho Februari 1, 2019 ataanza mazoezi na timu yake ya Enppi kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Misri dhidi ya Al Ahly utakaochezwa Jumanne Februari 5, 2019.

Enppi inashika nafasi ya 14 kati ya 18 zinazoshiriki ligi kuu. Timu hiyo imecheza mechi 20, imeshinda 4, sare 9 na kufungwa mechi 7.
Chanzo - EATV
Share:

YANGA SC YAITOA BIASHARA UNITED KWA MATUTA, YATINGA 16 BORA ASFC


Yanga SC imefanikiwa kwenda hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya ushindi wa penalti 5-4 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90.

Waliofunga penalti za Yanga SC ni Heritier Makambo, Paul Godfrey, Ibrahim Ajibu, Thabani Kamusoko na Matheo Anthony, za Biashara United zilifungwa na Lenny Kissu, George Makang’a, Derick Mussa, Kauswa Bernard, wakati Tariq Seif akapaisha ya nne.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Martin Saanya aliyesaidiwa na Abdallah Rashid na Rashid Zongo, Biashara United ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza 2-1.

Waziri Junior alianza kuifungia Biashara United kwa penalti dakika ya pili tu kufuatia beki Andrew Vincent ‘Dabte’ kumuangusha kwenye boksi George Makang’a.

Yanga SC wakasawazisha kwa penalti pia iliyopogwa na mshambuliaji wake Mrundi, Amissi Joselyn Tambwe dakika ya saba kufuatia Frank Sekule wa Biashara United kumuangusha Nahodha, Ibrahim Ajibu.

Na Biashara United wakapata bao la pili dakika ya 41 kupitia kwa Innocent Edwin aliyemlamba chenga nzuri beki mkongwe Kelvin Yondan kabla ya kumchambua kwa shuti la kitaalamu kipa Ramadhani Kabwili.

Kipindi cha pili Yanga SC waliingia na mchezo wa kushambulia zaidi kusaka bao la kusawazisha na wakafanikiwa kupata bao la pili dakika ya 73 kupitiakwa mshambuliaji wake Heritier Ebenezer Makambo aliyemalizia mpira ulipanguliwa na kipa Nourdine Balora baada ya krosi ya Mrisho Khalfan Ngassa.
 
Kocha Amri Said ‘Stam’ alichukizwa na kipa wake, Nourdine Balora baada ya bao hilo na akamtoa nafasi yake ikichukuliwa na Hassan Robert.

Kocha huyo alionekana akitoleana maneno makali na kipa huyo kabla ya kumsemea kwa refa Saanya aliyemuinua kwenye benchi na kumuamuru atoke kwenye eneo hilo. 

Yanga SC sasa itamenyana na Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi ambayo iliitoa Mighty Elephant.

Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Ramadhani Kabwili, Paulo Godfrey, Gardiel Michael, Kelvin Yondan, Andrew Vincent ‘Dante’, Feisal Salum ‘Fei Toto’, Mrisho Ngassa, Pius Buswita/Thabani Kamusoko dk60, Heritier Makambo, Amiss Tambwe/Matheo Anthony dk76 na Ibrahim Ajibu. 

Biashara United; Nourdine Balora/Hassan Robert dk76, Taro Ronald/Kauswa Bernard dk67, George Makang’a, Waziri Junior/Tariq Seif dk63, Juma Mpakala, Frank Sekule, Innocent Edwin, Lenny Kissu, Wilfred Nkouzima, Derick Mussa na Abdulmajid Mangalo.
Share:

TGNP MTANDAO YATOA MAPENDEKEZO MANNE TUKIO LA MAUAJI YA WATOTO NJOMBE

Mkurugenzi Mtendaji TGNP Mtandao Lilian Liundi

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UKATILI DHIDI YA WATOTO HAUKUBALIKI, HAUVUMILIKI, TUWALINDE WATOTO.

TGNP Mtandao kwa kushirikiana na wadau wa haki za wanawake, watoto  na usawa wa kijinsia tunatoa salamu za rambirambi kwa familia zilizopoteza watoto Mkoani Njombe kutokana na matukio ya mauaji yanayohusishwa na imani za kishirikina. 


Vitendo hivi ni vitendo ambavyo havikubaliki katika jamii kwani ni kinyume cha Azimio la ulimwengu juu ya haki za binadamu (Universal Declaration of Human Rights) la tarehe 10 Desemba 1948. Kifungu cha 3 kinachotamka kwamba “Kila mtu ana haki ya kuishi, haki ya uhuru na haki ya kulinda nafsi yake. Na ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977)  Ibara ya 14 imetamka juu ya Haki ya kuishi sambamba na sheria ya Haki ya kuishi ya mwaka 1984.

Jamii inawajibu wa kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia. Hii ni kwa mujibu wa sheria ya mtoto na. 21 ya mwaka 2009 na mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA), unaolenga kupunguza kiwango cha ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii yetu kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2022.

Matukio kama haya yamesababisha vifo vya wananchi (wanawake, wanaume, wazee na watoto) wasio na hatia kama vile mauaji ya vikongwe, watu wenye ualibino na sasa yanafanyika kwa watoto ambao hawana ulemavu.

TGNP Mtandao, tunatambua jitihada za serikali ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa katika kukabiliana na suala hili, na kamati ya kuchunguza mauaji haya tayari imeundwa. Kwetu sisi tunaona ni jitihada nzuri pamoja na kwamba upelelezi unaendelea, tunashauri yafuatayo:-

⇰ Kamati iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, ilete majibu hayaka iwezekanvyo, na taarifa ya uchunguzi ifanyiwe kazi kwa wakati ili kutokomeza kabisa mauaji haya.

⇰    Serikali na vyombo vya dola visimamie kikamilifu sheria ya kudhibiti uchawi na. 12 ya mwaka 1998(The Witchcraft Act). Ambayo imeainisha adhabu kwa watu wanaoendesha vitendo vya kishirikiana vinavyoweza kudhuru wengine.

⇨ Tunalitaka jeshi la polisi  na vyombo vingine vya dola kuhakikisha watoto wanakuwa salama kwa kuimarisha ulinzi katika maeneo yote yanayotajwa kuwa sio salama katika mkoa wa Njombe ili kuhakikisha watoto wanahudhuria masomo kikamilifu.

    Tunaitaka jamii kutoa  ulinzi wa mtoto kwani ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha ustawi wa watoto. Pia, serikali na wadau kuzijengea uwezo kamati za ulinzi wa watoto ili waweze kutimiza majukumu yao ikiwemo kubaini maeneo hatarishi katika kijiji/ mtaa na kupanga mikakati ya kupunguza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Imetolewa na

Lilian Liundi
Mkurugenzi Mtendaji TGNP Mtandao.
Januari 30,  2019.
Share:

KIKOSI CHA INTELIJENSIA CHAINGIA RASMI NJOMBE KUONGEZA NGUVU YA UPELELEZI WA MAUAJI

Na.Amiri kilagalila Kamishna wa operesheni na mafunzo ya jeshi la polisi nchini NSATO MARIJANI akiwa na wataalamu wengine wa intelijensia wamefika mkoani Njombe ili kuungana na jeshi la polisi mkoani humo katika kupambana na mauaji dhidi ya watoto wadogo. kikosi hicho maalumu kimewasili mkoani Njombe Ikiwa ni siku moja imepita tangu naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi amuagize IGP SIMON SIRRO kutuma kikosi maalumu cha kiintelijensia kuongeza nguvu katika uchunguzi wa watekaji na wauaji wilayani Njombe. Akizungumza katika mkutano wa dharura na wananchi katika kituo kikuu cha mabasi…

Source

Share:

TUNDU LISSU AMJIBU NDUGAI " BUNGE HALIJAWAHI KUNILIPA HATA SENTI MOJA'

Tundu Lissu amesema Bunge la Tanzania halijawahi kutoa hata senti moja kugharamia matibabu yake.

Lissu ambaye ni mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Januari 31, 2019 saa chache tangu Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kusema Desemba 2018, Lissu alikuwa amelipwa Sh207.8 milioni zikiwa stahiki zake na Sh43 milioni zilizotolewa kama mchango wa matibabu kwake.

Lissu amekiri kulipwa Sh43 milioni zilizotolewa na wabunge wenzake kama mchango wao na kwamba kiasi kingine alicholipwa kinachofanya jumla ya fedha hizo kufikia Sh250 ni mishahara na stahiki zake, lakini siyo gharama za matibabu.

Ametoa sababu tatu ambazo Spika Ndugai alizitoa Aprili mwaka jana, kwamba Bunge haliwezi kulipia gharama za matibabu yake.

Lissu amezitaja sababu hizo kuwa hawajapata barua ya kibali ya madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili; hawajapata barua ya kibali cha Katibu Mkuu Wizara ya Afya; na tatu hawajapata barua ya kibali cha Rais (John) Magufuli kuidhinisha malipo hayo.

“Sasa anaposema wamenilipa pesa hizo anapaswa kuulizwa, je, ni lini walipata barua hizo tatu za vibali?” amehoji Lissu na kuongeza:

“Ukweli pekee uliopo ni kwamba Bunge halijawahi kunilipa hata senti moja ya gharama za matibabu yangu. Hata senti moja!”

Na Kalunde Jamal, Mwananchi 
Share:

BAWACHA TAIFA WALAANI VITENDO VYA MAUAJI YA WATOTO NJOMBE

Baraza la wanawake Chadema Tanzania (BAWACHA) wameungana na watanzania wengine hususani wananchi wa mkoa wa Njombe kulaani vitendo vya mauaji ya watoto yaliyotokea hivi karibuni mkoani humo . Katika taarifa iliyotolewa na mwenyekitiki wa Baraza hilo Taifa HALIMA MDEE imeeleza kuwa Kwa kipindi cha takriban mwezi mmoja sasa kumekuwa na habari za kutisha kutoka mkoani Njombe ambapo vyombo vya habari mbalimbali vimeripoti kuwepo kwa mfululizo wa mauaji ya watoto wapatao 10, ambao wametekwa na kuuwawa kwa kuchinjwa katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Mji wa Njombe na Halmashauri ya Wilaya…

Source

Share:

MALORI 8 YALIYOSHEHENI MBAO NA MKAA YAKAMATWA NA TRA NJOMBE KWA KUKWEPA KODI

Na Amiri kilagalila Mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa Njombe inayashikilia Magari makubwa 8 yaliyosheheni mizigo ya Mbao kwa makosa ya kukwepa kulipa Kodi. Akizungumza na waandishi wa habari mapema siku ya leo katika kituo cha ukaguzi wa Magari kilichopo kibena njia panda ya kuelekea lupembe halmashauri ya mji wa Njombe,meneja wa TRA mkoa wa Njombe MUSA SHAABAN alisema kuwa malori hayo yanashikiliwa kwa makosa makuu mawili ikiwemo kuto kuwa na risiti za manunuzi. “Haya malori tumeyakamata kwasababu kuu mbili na sababu ya kwanza tumekagua risiti za manunuzi sasa…

Source

Share:

WEMA SEPETU NA DIAMOND PLATNUMZ USO KWA USO.. WAZUA GUMZO LA AINA YAKE


Msanii wa Bongo Fleva, Wema Sepetu na Diamond Platnumz leo Alhamisi Januari 31, 2019 wamekuwa kivutio katika viwanja vya Leaders Club ambako mkutano kati ya wasanii na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda unatarajiwa kufanyika.

Diamond amewasili viwanja hivyo majira ya saa 9:15 alasiri akiwa katika gari jeusi aina ya BMW X6 huku akiwa amevalia kanzu nyeupe na kilemba.

Akiwa amesindikizwa na walinzi wake, Diamond alipofika alielekea kushoto mwa jukwaa na kusalimia baadhi ya wasanii kabla ya kuelekea jukwaa kuu ambapo Wema na wasanii wengine walikuwa wamekaa.

Alianza kumsalimia ofisa habari wa klabu ya Simba Haji Manara , meneja wake Babu Tale na kisha kumkumbatia mrembo huyo kwa takribani dakika moja kabla hajaenda kusalimia wasanii wengine akiwemo King Kikii, Masanja Mkandamizaji na wengine.

Tukio hilo lilionekana kuwavutia watu waliofika katika viwanja hivyo wakiwemo waandishi wa habari ambao kila mmoja alikuwa akipambana kupata picha.

Na Nasra Abdallah na Hellen Hartley, Mwananchi 
Share:

MABINTI WACHAPANA MAKONDE BAADA YA JAMAA KUWAAMBIA ANAOA MREMBO MWINGINE

Picha haihusiani na habari hapa chini
Mabinti wawili wanauguza majeraha ya kuwekeana baada ya kutwangana makonde wakizozania jamaa mmoja eneo la Kithyoko Kaunti ya Machakos nchini Kenya waliyekuwa wakimmezea mate.

 Inadaiwa kwamba jamaa huyo aliwaalika kwake na kuwaarifu kuhusu mipango yake ya kutaka kuoa karibuni kwani tayari alikuwa amepata binti wa kumuoa. 

 “Mimi nimewaita hapa tukae kama marafiki, lakini cha muhimu ningependa kuwaalika rasmi kwenye harusi yangu itakayofanyika karibuni,” jamaa huyo aliwaambia. 

Katika ripoti ya Taifa Leo la Alhamisi, Januari 31 inadaiwa kuwa, kusikia maneno ya jamaa huyo, mabinti hao walianza kukunja sura zao kwa mshtuko mkubwa huku kila mmoja wao machozi yakimlengalenga. 

 “Loh! Unamaanisha nini? Una hakika unajua unachosema wewe?” Mmoja wao aliuliza kwa mshangao huku ameikunja sura.

 “Najua kila mmoja wenu alitarajia mazuri kutoka kwangu. Lakini poleni sana kwa kuwa hivi sasa nina mchumba nitakayefunga naye pingu za maisha karibuni. Sasa komeni kujipendekeza kwangu na kila mtu ajitafutie maisha yake,” jamaa alisema.

 Inadaiwa mabinti hao walishindwa kujizuia na ghafla wakaanza kutwangana mangumi huku kila mtu akimlaumu mwenzake kwa kumharibia asiolewe na jamaa huyo.

 “Ni wewe… balaa hii yote ni wewe,” mmoja wa mabinti hao alimwambia mwenzake akimwonyesha kidole.

Inaelezwa kuwa binti mwenzake alimjibu kwa maneno ya kukera huku akimkejeli mwenzake aliyekuwa amemwonyesha kidole. 

 “Chunga mdomo wako. Si ulikuwa ukiringa utaolewa naye. Umekula hu!” alisema na wote kupigana na kuangushana hadi sakafuni huku jamaa akiwatenganisha.

 “Tokeni hapa sasa mumezidi. Nimewaambia msijipendekeze kwangu tayari nina mchumba wa kuoa. Sijui mnapigania nini sasa. Hebu! Kila mtu nje mkapiganie huko,” jamaa huyo aliwavuta na kuwaondoa nje kisha akaufunga mlango wake.

 Mabinti hao walizozana nje kwa muda kabla ya kila mtu kushika hasini zake na kutokomea baada ya majirani na watu kujikusanya kuangalia sinema ya bure. 

Via Tuko 
Share:

NDUGAI : NI VYEMA WATANZANIA WAKAJUA HUYU MWENZETU 'ZITTO KABWE' NI MUONGO

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amemtaka Mbunge wa Kigoma mjini Mhe. Zitto Kabwe amwogope Mungu na aache kuwa mwongio kwenye taarifa zake ikiwa ni pamoja na tuhuma za upotevu wa Shilingi trilioni 1.5.

Akizungumza bungeni leo Alhamisi Januari 31, 2019 Ndugai amesema licha ya uongo huo ni mapema mno kumpeleka kiongozi huyo wa ACT katika Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

Amesema Zitto amekuwa akiandika kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Ndugai kuikalia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu upotevu wa Sh1.5 trilioni, jambo ambalo si kweli.

Ndugai amebainisha kuwa taarifa za mbunge huyo kwenye mitandao ya kijamii hazina ukweli na ni uongo mtupu

“Kwa mfano, aliandika katika mtandao wake kuwa nilipokea ripoti ya CAG tangu Januari 8, 2019 nikaikalia wakati mimi nimepokea taarifa hiyo Januari 16, 2019 na Januari 18, 2019 niliwapa kamati ya PAC. Ni vyema Watanzania wakajua huyu mwenzetu ni muongo,” amesema Ndugai.

Amesema Bunge liliweza kujadili habari za Sh300 bilioni kwa nguvu iweje washindwe kujadili kuhusu Sh1.5 trilioni ambazo ni nyingi.

Hata hivyo, amesema CAG, Profesa Mussa Assad alishaulizwa mbele ya Rais John Magufuli kuhusu fedha hizo na kubainisha kuwa hakuna upotevu wa kiasi hicho na hata kamati ya PAC ilishasema hakuna upotevu, lakini anashangaa kuona Zitto analisambaza jambo hilo.
Share:

KESI YA MBOWE NA MATIKO YAPANGIWA HAKIMU MPYA


Kesi inayowakabili baadhi ya viongozi wakuu wa Chama na Wabunge 7 wa Chadema, imeendelea leo ambapo imepangiwa Hakimu mpya anayejulikana kwa jina la Kelvin Mhina.

Hatua hiyo ya kesi hiyo Na.112/2018 kupangiwa Hakimu mpya imekuja baada ya aliyekuwa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Dar es salaam, Wilbard Mashauri kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya kuteuliwa na Rais Januari 28,2019.

Wakati akiwa Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri aliwafutia dhamana viongozi wawili wa CHADEMA, M/Kiti , Mbowe na Mbunge Esther Matiko kutokana na kushindwa kutimiza masharti ya dhamana waliyopewa na Mahakama.

Katika kesi hii ya viongozi wa CHADEMA, Hakimu mpya Kelvin Mhina, ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 14, 2019 itakapotajwa tena baada ya Wakili wa Serikali, Wankyo Simon kutoa taarifa kwamba kesi hiyo ilienda kwa ajili ya kutajwa na kwamba wanasubiri uamuzi wa mahakama ya rufaa.

Ameeleza kwamba upande wa mashtaka ulikata rufaa kupinga dhamana hivyo kesi hiyo itaanza kusikilizwa Februari 18, 2019.

Hata hivyo, Mbowe na Matiko bado wanaendelea kusota rumande kutokana na kufutiwa dhamana.

Chanzo - EATV
Share:

MBUNGE WA CHADEMA GODLESS LEMA ATANGAZA KUJIUZULU


Mbunge wa Arusha mjini (CHADEMA), Godbless Lema.


Mbunge wa Arusha mjini (CHADEMA), Godbless Lema amesema kuwa endapo Spika wa Bunge Job Ndugai atalithibitishia bunge kuhusu kauli yake dhidi ya matibabu ya Lissu, yeye atakuwa tayari kujiuzulu.

Lema ametoa kauli hiyo kwenye ukurasa wake wa 'twitter' ambapo amejibu kauli iliyotolewa na Spika akiwa bungeni leo ambapo amesema kuwa mpaka sasa bunge limegharamia shilingi milioni 250 katika matibabu ya mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

"Bunge halijawahi kumlipia Mh Lissu pesa kwa ajili ya matibabu, alichokisema Mh Spika Ndugai ni upotoshaji kwa jamii na Mungu. Chama kitatoa tamko juu ya hili. Spika akiweza kuthibitisha hili, mimi nitajiuzulu Ubunge, mshahara wa Mbunge sio hisani ya Spika", ameandika Lema.

Akizungumza bungeni leo, Januari 13 Spika Job Ndugai amesema hadi sasa Bunge limeshamlipa Tundu Lissu shilingi milioni 250 kwa ajili ya matibabu yake.
Share:

NDUGAI SASA KU- DILI NA TUNDU LISSU "ADAI AMELIPWA MIL 250 KUTOKA BUNGENI"


Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema kuanzia sasa ataanza kumjibu mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu kwa kuwa ana amini amepona na kwamba tayari ameshalipwa Sh250milioni kutoka bungeni.

Ndugai ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Januari 31, 2019 bungeni mjini Dodoma baada ya kipindi cha maswali na majibu.

Amesema hadi mwishoni mwa Desemba 2018, Lissu alikuwa amelipwa Sh207.8milioni pamoja na Sh43 milioni zilizotolewa kama mchango wa matibabu ya mbunge huyo.

Amesema kwa ujumla hadi sasa Lissu amelipwa Sh250milioni kutoka bungeni.

“Siku za mwanzo sikutaka kujibu maana niliamini kumjibu mtu aliyelala kitandani siyo vizuri kwani kuna vitu huenda vingekuwa vimempita, lakini sasa naamini ni mzima hadi anafanya ziara nje. Nalisema hili akijibu nakuja na mkeka hapa,” amesema Ndugai.

Amesema mbunge huyo amekuwa akilalamika kila wakati kuwa Bunge halimjali kitu ambacho hakina ukweli ndani yake na hakuna madai kama hayo.


Na Habel Chidawali, Mwananchi
Share:

RUFAA YA DHAMANA YA MBOWE NA MATIKO KUANZA KUSIKILIZWA FEBRUARI 18

 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa rufaa ya kupinga dhamana iliyokatwa na upande wa mashtaka dhidi ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko itaanza kusikilizwa Februari 18, 2019 katika Mahakama ya Rufaa.

Taarifa hiyo umetolewa leo Alhamisi Januari 31, 2019 na wakili wa Serikali, Wankyo Simon mbele ya hakimu mfawidhi, Kelvin Mhina wakati shauri hilo lilipokuja kwa ajili ya kutajwa.

Wankyo amedai kuwa kesi lilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba wanasubiri uamuzi wa mahakama ya rufaa.

"Washtakiwa wote wapo mbele ya mahakama yako na kesi ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kuna rufaa iliyopo mahakama ya rufaa ambayo bado haijasikilizwa, hivyo tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa, wakati tukisubiri maamuzi ya mahakama ya rufaa,” amedai Wankyo.

Amedai kuwa rufaa hiyo ya kupinga dhamana iliyokatwa na upande wa mashtaka itaanza kusikilizwa Februari 18, 2019.

Na Hadija Jumanne, Mwananchi 
Share:

MKE AMCHOMA MMEWE KWA MAJI YA MOTO SEHEMU ZA SIRI

Jamaa mmoja mwenye umri wa makamo amekimbizwa hospitalini kaunti ya Kirinyaga nchini Kenya baada ya mkewe kumchoma kwa maji moto kwenye sehemu nyeti/sehemu za siri. 

Inaelezwa kuwa jamaa huyo alipigiwa simu na mmoja wa wateja wake wa kike akimjuza kuhusu nafasi ya kazi ila mkewe alidhani alikuwa akizungumza na mchepuko wake.
 
Mwanamke aliingia hadi jikoni akiwa amejawa na hasira, akachemsha maji na kisha akamumwagia mumewe kwenye sehemu zake za siri na mgongoni.

 "Nilipigiwa simu na mmoja wa wateja wangu wa kike akinieleza kuhusu nafasi ya kazi lakini mke wangu alijawa na ghadhabu na kuanza kunikashifu kwa kutokuwa mwaminifu katika ndoa," Mwathiriwa alisema. 

 "Mke wangu alienda jikoni, akachemsha maji na muda mfupi baadaye alirudi na maji moto kwenye sufuria na kunimwagilia kwenye sehemu nyeti na mgongoni," Jamaa huyo aliongezea.

 Aidha, jamaa huyo ambaye anapokea matibabu katika hospitali ya Kimbimbi alisema mkewe wa miaka 12 katika ndoa amekuwa akitishia mara kadhaa kumchoma. 

Via Tuko blog
Share:

FEDHA ZA TANAPA MILIONI 200 ZALETA KIZAAZAA ,MADIWANI TARIME WATAKA USHAHIDI WA WARAKA.

Na Dinna Maningo,Tarime. Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Tarime mkoani Mara wameitaka halmashauri kuwaonyesha ushahidi wa waraka wa mapokezi ya fedha milioni 140 kutoka Hifadhi za Taifa TANAPA huku wakidai kuwa pesa zilizotolewa ni milioni 200. Agizo hilo limekuja wakati Madiwani wakiuliza maswali ya papo kwa papo ambapo Diwani wa kata ya Nyanungu Ryoba Mang’eng’i (Chadema) alihoji kiasi gani cha pesa kutoka hifadhi za Taifa kilichopokelewa na Halmashauri,fedha ambazo utolewa kama ujirani mwema kutokana na Halmashauri hiyo baadhi ya vijiji vyake kupakana na Hifadhi ya wanyama ya Serengeti. ”…

Source

Share:

WAZIRI UMMY ATOA MABATI 200 KUSAIDIA UJENZI WA SHULE TANO ZA SEKONDARI JIJINI TANGA


Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Hamis Mkoba.
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa.
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Hamis Mkoba
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee
na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Naibu Meya wa Jiji la Tanga Mohamed Haniu baada ya kumkabidhi Mkurugenzi wa Jiji hilo Daudi Mayeji
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa halfa ya kukabidhi mabati 200 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa shule tano Jijini Tanga kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa

***
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ametoa mabati 200 yenye thamani
ya shilingi milioni 4.2 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa shule tano za Sekondari Jijini Tanga. 

Halfa ya makabidhiano hayo yalifanyika mjini Tanga kwenye shule ya Msingi Mwakidila ambapo Mkurugenzi wa Jiji hilo alipokea mabati hayo ikiwa ni mkakati wa Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga kusaidia kuondosha changamoto ya uhaba wa madarasa. 

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mabati hayo, Waziri Ummy aliwashauriwa wazazi na walezi kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya watoto wao jambo ambalo linaweza kuwasaidia kufanya vizuri kwenye masomo yao. 

“Ndugu zangu wazazi na walezi hakikisheni mnafuatilia maendeleo ya watoto wenu wanapokuwa shuleni kwani nyie pia mnaweza kuchangia ufaulu wa mtoto
wako",alisema. 

Aidha pia Waziri Ummy ameahidi kuchangia
ujenzi wa madarasa kwenye shule ya Sekondari Kange ili kuchochea ukuaji wa sekta ya elimu kwa mkoa wa Tanga . 

“Lakini pia niwashukuru watendaji wa Shirika la Tawode kwa kujitoa katika kuchangia maendeleo ya Jamii ya Tanga kwa kutafuta wafadhili mbalimbali wa ndani na nje ya mkoa huu”,alisema.

Share:

MKURUGENZI MPYA BENKI YA CRDB ATAMBULISHWA RASMI MWANZA


Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini (CRDB), Abdulmajid Nsekela (aliyesimama) ametambulishwa rasmi kwa wafanyakazi na wateja wa benki hiyo Kanda ya Ziwa Mwanza na Shinyanga.

Hafla ya kumtambulisha Mkurugenzi huyo aliyechukua nafasi ya Dkt. Charles Kimei imefanyika Januari 29, 2019), katika ukumbi wa Gold Crest Hotel Jijini Mwanza ambapo Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB, Ally Hussein Laay alibeba jukumu la kufanya utambulisho huo.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB, Ally Hussein Laay akizungumza kwenye hafla hiyo.
Wageni mbalimbali wakiwemo wateja na viongozi wa CRDB pamoja na viongozi wa serikali.
Wateja na wafanyakazi wa CRDB wakiwa kwenye hafla hiyo.

Tazama Video hapa chini





Share:

CHANGAMOTO ZAAINISHWA UTEKELEZAJI SERIKALI MTANDAO


Kaimu katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Micky Kiliba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha Serikali mtandao kilichofanyika leo jijini Dodoma
Kaimu katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Micky Kiliba walio kaa (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Serikali mtandao

Picha na Alex Sonna-Dodoma

Serikali imesema kuwa bado kuna changamoto zinazokabili utekelezaji wa serikali mtandao ambapo baadhi ya mifumo ya Tehama kuendelea kutowasiliana na kutobadilishana taarifa ndani ya taasisi na kati ya taasisi na taasisi.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dk, Laurean Ndumbaro kwenye hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na kaimu katibu mkuu Micky Kiliba wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha serikali mtandao kilichofanyika hapa jijini Dodoma.

Dk, Ndumbaro amesema kuwa kuna mafanikio mengi yaliyopatikana kupitia wakala wa serikali mtandao ikiwemo kufanyika kwa uwekezaji mkubwa kwenye miundombinu ya Tehama kama vile mkongo wa Taifa, vituo vya kitaifa vya data na kutenga masafa ya intaneti ya Serikali.

Aidha amesema kuwa pamoja na mafanikio hayo lakini bado kuna changamoto ya urudufu wa mifumo ambapo kila taasisi inakuwa na juhudi za kipekee katika kusimika na kutumia mifumo na miundombinu ya Tehama ambayo ingeweza kutumiwa na taasisi zaidi ya moja.

“Baadhi ya sababu zilizochangia uwepo wa changamoto hizi ni pamoja na kutozingatia miongozo na kanuni za usimamizi wa serikali mtandao zilizopo, upungufu wa wataalamu wa Tehama wenye uwezo na ujuzi wa kutosha, misukumo kutoka kwa wafanyabiashara na wafadhili na uratibu
hafifu wa shughuli za Tehama ndani na kati ya taasisi za serikali,”amesema Dk.Ndumbaro

Hata hivyo Dk.Ndumbaro amebainisha kuwa lengo kuu la utekelezaji wa serikali mtandao ni kuboresha utoaji wa huduma kwa umma, kuimarisha utawala bora na kuongeza tija na ufanisi katika uendeshaji wa taasisi za umma kwa kuhakikisha uwepo wa mawasiliano ya haraka yenye uhakika na salama ndani na taasisi mbalimbali za serikali.

Kwa upande wake Kaimu katibu Mkuu, Micky Kiliba amewataka Watumishi wa umma kuutambulisha mfumo huo kwa serikali mtandao kwa wananchi ili kuwapunguzia gharama za kusafiri umbali mrefu kwa ajili ya kufuata huduma.

Kiliba amesema kuwa wananchi wakielimishwa kuhusiana na serikali mtandao watakuwa wanapata huduma mbalimbali za kiserikali kwa kupitia simu zao za mkononi kwa kuwa lengo la kuanzishwa kwa wakala wa serikali mtandao ni kusogeza huduma karibu na wananchi.

“Hata katika masuala ya uwekezaji hakutakuwa na haja ya wawekezaji kusafiri umbali mrefu kwa ajili ya kupata taarifa za uwekezaji watakuwa wanaingia kwenye mfumo wetu na kujua kila kituwanachokihitaji bila hata ya kuja huku,” amesema Kiliba.

Share:

WADAIWA KUNYWA DAWA ZA ARV BILA KUPIMA VIRUSI VYA UKIMWI

Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Kupambana na Ukimwi Tanzania (Tacaids), Dk Leonard Maboko amesema Watanzania wengi wana mwamko wa kutumia dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi (ARV) kuliko kujua hali zao.

Dk Maboko alibainisha hayo jana wakati akizindua mpango mkakati wa miaka mitano wa taasisi ya kupambana na maambukizi ya virusi vya Ukimwi ya Agpahi.

“Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa asilimia 90 ya wajawazito wanajua hali zao kati yao, asilimia 98 wanatumia dawa za ARV. Hata hivyo, utafiti uliofanyika ilibainika kuna watu hawajui hali zao lakini walipopimwa damu zilionyesha tayari wanatumia ARV,” alisema.

Awali, mkurugenzi mtendaji wa Agpahi, Dk Sekela Mwakyusa alisema kupitia mpango huo wanatarajia kupanua wigo wa huduma ili kufika maeneo mengi zaidi na kuhakikisha maambukizi kwa watoto wanaozaliwa yanakoma.

Na Ephrahim Bahemu, Mwananchi 

Share:

Wednesday 30 January 2019

SOT, PRALENA KUCHANGISHA MILIONI 45

Taasisi ya Michezo ya watu wenye Ulemavu wa Akili Tanzania, Special Olympics inahitaji shilingi milioni 45 kwa ajili ya kuisaidia timu ya Taifa inayotarajia kushiriki michezo ya Dunia itakayofanyika mwezi Machi mwaka huu, Abu Dhabi Falme za Kiarabu (UAE).

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Special Olympics Tanzania (SOT), Charles Rays alisema fedha hizo ni kwa ajili ya tiketi za kwenda na kurudi sambamba na kambi ya maandalizi kuelekea katika michezo hiyo.

Rays alisema kambi ya maandalizi kwa siku 14 inahitaji shilingi milioni 10.5 huku tiketi kwa ajili ya kwenda na kurudi Abu Dhabi ni sh.milioni 34.5.

Aidha Rays alisema ili kufanikisha kushiriki katika michezo hiyo wameomba ridhaa ya Taasisi ya PRALENA Network Ltd ya jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusaidia upatikanaji wa fedha hizo kupitia mfumo wa simu za mkononi.

Naye mwakilishi wa PRALENA, Thabit Said alisema ili kufanikisha upatikaji wa fedha hizo wametengeneza mifumo mbalimbali ambayo wadau watachangia fedha.

Said alisema mfumo huo utatumika kwa kila anayeguswa katika mitandao ya simu ya Tigopesa, M-Pesa na Airtel Money.

“Tunawaomba wadau katika jamii, kusaidia kupatikana kwa fedha hizo kupitia Tigopesa, M-Pesa na Airtel Money kupitia namba ya kampuni 123123 na kumbukumbu namba ni 60024833555,” alisema Said.

Said aliweka bayana kauli mbiu ya ufanikishwaji wa fedha hizo ni ‘Ushindi wao ni ushindi wetu’.

Na Andrew Chale

Mwakilishi wa PRALENA, Thabit Said akizungumza namna ya mifumo mbalimbali ambayo wadau watachangia fedha ili kukusanya kiasi hicho cha Sh. Milioni 45.

Mkurugenzi wa Special Olympics Tanzania (SOT), Charles Rays akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es Salaam wakati wa kuchangisha fedha za tiketi. Kulia ni Mwakilishi wa taasisi ya PRALENA, Bi. Irine Victor na kushoto ni Mjumbe wa bodi ya SOT, Makuburi Ally.

Mkurugenzi wa Special Olympics Tanzania (SOT), Charles Rays akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) mapema leo Jijini Dar es Salaam wakati wa kuchangisha fedha za tiketi.
Share:

POLISI ALIYEUA MKE NA MTOTO AMEJIUA KWA KIPANDE CHA CHUPA

Afisa mmoja wa polisi aliyeshtakiwa kwa madai ya kumuua mkewe pamoja na mtoto mwenye umri wa miaka 5 katika kambi ya maafisa wa kupambana na wezi wa mifugo eneo la Suswa Machi 2018, amejiua. 

Cosmas Kipchumba Biwott, 27, ambaye alikuwa amesimamishwa kazi kwa muda, alijiua Jumanne, Januari 29 katika kituo cha polisi cha Nandi Hills alikozuiliwa kwa mashtaka ya wizi wa kimabavu.

Kulingana na habari zilituzofika katika meza yetu hapa TUKO.co.ke, Kipchumba alimwomba mlinzi wa selo alimokuwa kumsindikiza chooni majira ya saa sita na dakika 10 mchana mita 20 kutoka kwenye selo hiyo. 

Wakiwa njiani, alikiokota kipande cha glasi/chupa na kukitumia kujirarua shingo. 

Alivuja damu nyingi huku akilepelekwa katika hospitali ya Rufaa ya Kapsabet alikothibitishwa kufariki.

 ‘Njiani, mfungwa huyo aliokota kipande cha glasi na kujirarua shingo upande wa kushoto na kuanza kuvuja damu,’’ polisi walisema.

Wakiwa njiani, alikiokota kipande cha glasi na kukitumia kujirarua shingo.

Ilibainika kuwa Kipchumba alizuiliwa kituoni Jumatatu, Januari 28 kusubiri uchunguzi kuhusu kesi nyingine.

 Alikuwa amefikishwa kortini awali lakini hakimu wa mahakama ya Kapsabet akatoa agizo la kuzuiliwa kwa muda. 

Katika kisa kingine, inadaiwa kuwa Kipchumba alimuua mkewe Jane Njoki na mwanawe Shantel Nyambura. 
 Kulingana na ripoti ya polisi, Kipchumba alimpiga mkewe risasi 20 kabla kumgeukia mwanawe na kumuua vile vile. 

Alifikishwa kortini lakini akaachiliwa kwa dhamana kabla kukamatwa tena kwa wizi wa kimabavu.

Share:

SAKATA LA MAUAJI YA WATOTO NJOMBE LATUA BUNGENI…LUGOLA ASEMA NI USHIRIKINA.

Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, Kangi Lugola amesema imebainika kuwa mauaji ya watoto mkoani Njombe ni ya imani za kishirikina. Lugola ametoa kauli hiyo leo Jumatano Januari 30, 2019 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza lililoulizwa na mbunge wa Mufindi Kusini (CCM), Mendrad Kigola. Mbunge huyo amehoji ni mkakati gani umewekwa na Serikali katika kukomesha mauaji ya watoto katika mkoa wa Njombe ili kurudisha amani mkoani humo. Akijibu swali hilo, Waziri Lugola amesema tangu juzi Januari 28, 2019 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni…

Source

Share:

IGP SIRRO AAGIZWA KUTUMA TIMU YA WATAALAMU NJOMBE KUSAIDIA UPELEZI MAUAJI YA WATOTO

Na.Amiri kilagalila Naibu waziri wa mambo ya Ndani ya nchi HAMAD MASAUNI amemuelekeza Inspecta genarali wa polisi SIMON SIRRO kutuma timu ya wataalamu mbali mbali mkoani Njombe ili kusaidiana na jeshi la polisi mkoani humo kupambana na vitendo vya utekaji na mauji ya watoto wadogo. Agizo hilo limetolewa mkoani Njombe wakati waziri wa mambo ya Ndani akizungumza na waandishi wa habari na kutoa tathmini ya ziara yake ya siku tatu mkoani mkoani humo yenye lengo la kupambana na mauaji dhidi ya watoto wadogo yanayoendelea mkoani Njombe. “Namuelekeza IGP kwanza kutuma…

Source

Share:

Tanzia : ALIYEZAWADIWA MILIONI 100 NA JPM KWA KUGUNDUA MADINI YA TANZANITE AFARIKI DUNIA


 
Mvumbuzi wa madini ya Tanzanite, Jummane Ngoma amefariki dunia leo Jumatano Januari 30, 2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mtoto wa marehemu, Hassan Ngoma amesema, “Ni kweli Mzee amefariki leo jioni hii hapa Muhimbili,” amesema Ngoma

Hassan amesema kinachofanyika kwa sasa ni kuuhifadhi mwili wa baba yake kisha baadaye watatoa taarifa rasmi ikiwamo utaratibu wa msiba utakuwa wapi na mazishi yatafanyika wapi baada ya kikao cha familia.

Aprili 6 mwaka jana, Rais John Magufuli akizindua ukuta wa mgodi wa Tanzanite, Mirerani mkoani Manyara alimzawadia Sh100 milioni kama shukrani kwa mchango wake kwa kugundua madini hayo.

Chanzo- Mwananchi
Share:

FACEBOOK KUUNGANISHA WHATSAPP, INSTAGRAM NA MESSENGER

Facebook ina mipango ya kuunganisha huduma zake za kutuma ujumbe katika Instagram, WhatsApp na Facebook Messenger.

Licha ya kwamba huduma zote tatu zitasalia kuwa programu huru zitashirikiana kupitia ujumbe utakaotumwa kutoka huduma moja hadi nyingine.

Facebook imeambia BBC kwamba ndiyo mwanzo wa mchakato mrefu.

Mpango huo kwanza uliripotiwa mjini New York na unaaminika kuwa mradi wa kibinafsi wa mwanzilishi wa facebook Mark Zuckerberg.

Utakapokamilika , ushirikiano huo utamaanisha kwamba mtumiaji wa facebook anaweza kuwasiliana moja kwa moja na mtu ambaye anamiliki akaunti ya WhatsApp.

Hili haliwezekani kwa sasa kwa kuwa programu zilizopo hazina uhusiano.

Hatua ya kuunganisha huduma hizo tatu umeanza , kulingana na gazeti la The new York Times na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2019 ama mapema mwaka ujao.
Je facebook ina mpango gani?

Facebook haikupendelea kuzungumzia kuhusu swala hili katikati mwa kashfa ilioikumba, lakini ililazimishwa na watu waliokuwa wakiwasiliana na New York Times.

Hadi kufikia sasa , WhatsApp, Instagram na Messenger zimekuwa zikifanya kazi kivyake na kushindana kibiashara.

Kuunganisha huduma hizo kwaa kutuma ujumbe kutarahisisha kazi ya facebook.

Haitalazimika kuunda programu mpya kama vile stories ambapo huduma zote tatu zimeongeza katika programu yake bila mafanikio ya kufurahisha.WhatsApp, Messenger na Instagram ni bidhaa huru zinazoshindana

Mawasiliano ya ujumbe kupitia huduma moja hadi nyengine yanaweza kuimarisha biashara katika huduma moja kwa kutuma ujumbe kwa huduma nyengine.

Pia yatairahisishia facebook kugawana data katika huduma zote tatu ili kusaidia juhudi za matangazo yake.

Hatua hiyo pia itaimarisha uwepo wa facebook na kuwa vigumu kuanguka iwapo serikali husika zitajaribu kuivunja kwa manufaa yao ya kibinafsi.
Usambazaji wa data.

Bwana Zuckerberg ameripotiwa kushinikiza ushirikiano huo ili kuimarisha huduma za kampuni yake kuwa muhimu na kuongeza muda wa wakati unaotumika na wateja wake katika huduma hizo.

Kupitia kuunganisha wateja wake katika kundi moja kubwa, facebook itaweza kushindani vizuri na kampuni ya Google na Apple iMessage kulingana na Makena Kelly wa mtandoa wa habari wa The Verge.

"Tunataka kuunda huduma bora zadi ya kutuma ujumbe ilio na ulinzi wa hali ya juu na kufanya kuwa rahisi kuwafikia marafiki na familia kupitia huduma tofauti'', aliongezea.

Taarifa hiyo ilisema kuwa kulikuwa na majadiliano na mjadala kuhusu vile mfumo huo utakavyofanya kazi.

Kuunganishwa kwa huduma hizo tatu kuteleta mabadiliko muhimu katika kampuni ya facebook kwa kuwa imeruhusu Instagram na WhatsApp kufanya kazi kama kampuni tofauti zilizo huru.

Gazeti la the New York Times linasema kuwa hatua ya Bwana Zuckerberg kupigania mpango huo wa kuunganisha huduma hizo umesababisha mgogoro wa ndani.

Inadaiwa ndio sababu ya waanzilishi wenza wa Instagram na WhatsApp kuondoka mwaka uliopita.

Hatua jhiyo inajiri huku facebook ikikabiliwa na uchunguzi na kukosolewa kuhusu vile inavyotunza data za wateja wake.
Chanzo - BBC
Share:

POLISI YAMSHIKILIA MWANAUME NA MCHEPUKO KWA KUMUUA MKE WAKE

Mary Wambui  anadaiwa kuuawa na mume wake Joseph Kori kwa ushirikiano na mwanamke(mchepuko) Judy Wangui.

 Wangui alikuwa mfanyakazi wa zamani wa Kamangara na kulingana na ripoti zilizosambaa ni kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mume wa bosi wake.

 Inadaiwa kulitokea ugomvi uliosababisha kifo cha Kamangara na mwili wake kutupwa katika bwawa la maji Jumamosi, Januari 26.

  Dada wa marehemu Esther Kamangara alisema, dada yake alitaka kufahamu ni nani aliyetaka kuondoka na mtoto wake, Kamangara alitoka nje na kukutana ana kwa ana na Wangui aliyekuwa mfanyakazi wake wa zamani na alikuwa akishuku kuwapo uhusiano kati yake na mume wake.

  Kori alikamatwa eneo la tukio na awali alikuwa ameripoti polisi kuhusu kutoweka kwa mke wake na hata kuwapeleka polisi katika nyumba ya Wangui ambapo matone ya damu yalipatikana. 

 Joseph Kori na  Judy Wangui  wanazuiliwa kwa madai ya kuhusika na mauaji ya mke wake Mary Wambui Kamangara.

Chanzo:Tuko
Share:

TAARIFA ZA SIRI ZA WATU 140,000 WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI ZAIBIWA NA KUVUJISHWA MTANDAONI

Taarifa za siri za watu zaidi ya 14000 waliyo na virusi vya HIV wakiwemo raia wa wageni zimeibiwa nchini Singapore na kuvujishwa mitandaoni.

Udukuzi huo unakuja miezi kadhaa baada ya rekodi za watu milioni 1.5 wa Singapore akiwemo waziri mkuu Lee Hsein Loong kuibiwa mwaka jana.

Taarifa za kibinafsi za wasingapore 5,400 na raia wa kigeni 8,800 zilizokuwa zimeorodheshwa kutoka Januari 2013 huenda zimevujishwa.

Hadi mwaka 2015, raia wa kigeni waliyo na virusi vya HIV hawakuruhusiwi kuzuru nchi hiyo japo kama watalii.

Kwa sasa, mtu yeyote anayetaka kuwa nchini humo zaidi ya siku 90 kwa ajili ya kazi, lazima afanyiwe uchunguzi wa kimatibabu kuhakikisha hana virusi vya Ukimwi.

Nani ilihusika na udukuzi huo?
Singapore ilitoa picha ya Mikhy Farrera-Brochez, raia wa Marekani anayehusishwa na kuvujisha wa taarifa za matibabu za watu binafsi

Mamlaka za nchi hiyo zinaamini aliyehusika na udukuzi huo huenda ni Mmarekani mmoja aliye na virusi vya ukimwi ambaye mpezi wake alikuwa daktari wa ngazi ya juu nchini Singapore

Mikhy Farrera-Brochez alishtakiwa na kufungwa baada ya kupatikana na kosa la ubadhirifu wa fedha na makosa mengine yanayohusiana na dawa za kulevya mwaka 2016.

Alifurushwa kutoka nchini humo mwaka uliyopita. Mpenzi wake Ler Teck Siang raia wa Singapore alishtakiwa kwa kumsaidia Farrera-Brochez kuweka taarifa za uongo katika rekodi zake za matibabu kuficha ukweli kuhusu hali yake ya HIV.

Maafisa wanasema Ler alijitolea kutoa damu yake na kuweka alam katika kitika kibandiko kuwa ni ya Farrera-Brochez ili kumwezesha kuingia nchini.

Katika taarifa, wizara ya afya ilimlaumu Ler kwa kutozingatia sera inayoongoza taarifa za watu binafsi.Singapore imeripotiwa kutafuta usaidizi wa kimataifa katika kesi

Maafisa wanasema kuwa walifahamishwa tarehe 22 mwezi huu wa Januari kuwa Farrera-Brochez huenda bado anashikilia taarifa ya sajili ya HIV.

"Sahamahani mmoja wa mfanyikazi wetu wa zamani ambaye alikua na idhini ya kufikia sajili ya taarifa binafsi za watu wenye virusi vya HIV huenda hakuzingatia mwongozo wa usalama uliyowekwa wa kushughulikia taarifa hizo"alisema waziri wa afya wa Singapore Gan Kim Yong.

Siku ya Jumatatu, maafisa wa afya walisema kuwa wamejaribu kuwasiliana na watu wote walio kwenye orodha hiyo ambao ni raia wa nchi hiyo lakini walifanikiwa kuzungumza na karibu watu 900 pekee kati ya 5,400.

Nambari ya dharura imetolewa kwa wale ambao huenda wameathiriwa na tukio hilo kupewa huduma ya ushauri nasaha.

Katibu wa wizara ya afya Chan Heng Kee amethibitisha hilo na kuongeza kuwa maafisa wanaamini Bw. Farrera-Brochez yuko ughaibuni lakini hawajui ni wapi hasa alipo.

"Kuna hofu huenda akaendelea kuvujisha taarifa hizo za siri mitandaoni," alionya Bw. Chan.
Chanzo - BBC
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger