Thursday 31 March 2022

Breaking : HII HAPA ORODHA YA MAJINA YA MAKATIBU WA WAZAZI CCM NA BAADHI YA WATUMISHI WANAOKWENDA MAKAO MAKUU


KIKAO Maalum cha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichokutana Dodoma tarehe 30, Machi, 2022 pamoja na mambo mengine ikifanya uteuzi wa watendaji wa Jumuiya ya Wazazi ngazi ya wilaya.Sambamba na kufanya uhamisho kwa baadhi ya watendaji wa wilaya na makao makuu kama ilivyoorodheshwa kupitia taarifa hii iliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu Bara, Daniel George kwa niaba ya Katibu Mkuu Umoja wa Wazazi;






















Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 1, 2022



Magazetini leo Ijumaa April 1 2022




















Share:

FREEMAN MBOWE AKUTANA NA RAILA ODINGA


Mwenyekiti wa Chadema Freeman Aikaeli Mbowe jana amekutana na Mheshimiwa Raila Amolo Odinga, Mgombea Urais wa Muungano wa Azimio la Umoja na Mheshimiwa Martha Karua, Kiongozi wa Chama cha NARC Kenya Jijini Nairobi.

Kupitia kwao, Mheshimiwa Mbowe amewataka Wakenya wote kushikamana kuhakikisha kuwa uchaguzi wao unakuwa wa haki, huru na wazi.

Kipekee, amewasihi Viongozi na Wagombea hao kuhakikisha vurugu za uchaguzi zilizotokea nchini Kenya miaka ya nyuma na kusababisha vifo vya Wakenya kamwe havijirudii tena.

Aidha, amewataka kutambua nafasi ya Taifa la Kenya katika kuendeleza Uhuru, Haki na Maendeleo ya watu katika Eneo la Jumuia ya Afrika Mashariki na kwamba wanapaswa wakati wote kulinda na kuendeleza mafanikio hayo.

Mheshimiwa Mbowe amewatakia Wakenya wote mchakato mwema wa Uchaguzi wao wa August 2022.

Share:

Wednesday 30 March 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MACHI 31,2022

Makali ya Rais Samia...
Share:

WIZARA YA ARDHI YASHIRIKIANA NA KOREA KUBADILISHA MIFUMO YAKE KUWA YA KIDIGITALI


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula (Kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mtendaji Mkuu na Rais wa Kampuni ya Hojung Solutions Co Ltd ya Korea Kusini baada yeye na ujumbe wake kumtembelea ofisini kwake eneo la Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 30 Machi 2022.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi akimvisha vazi la kimasai Mtendaji Mkuu na Rais wa Kampuni ya Hojung Solutions Co Ltd ya Korea Kusini baada ya kumtembelea ofisin ya Wizara ya Ardhi eneo la Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 30 Machi 2022.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Korea Kusini ulioongozwa na Mtendaji Mkuu na Rais wa Kampuni ya Hojung Solutions Co Ltd Munseok Lee mara baada ya kumtembelea ofisini kwake eneo la Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 30 Machi 2022.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza na ujumbe kutoka Korea Kusini ulioongozwa na Mtendaji Mkuu na Rais wa Kampuni ya Hojung Solutions Co Ltd Munseok Lee baada ya kumtembelea ofisini kwake eneo la Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 30 Machi 2022.

***********************

Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA

Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa ushirikiano wake na Korea Kusini imeanzisha mkakati wa kuhakikisha inabadilisha mifumo yake upangaji, utumiaji, upimaji na uwekaji kumbukumbu za sekta ya ardhi kutoka analogia kwenda digitali ili kuboresha sekta ya ardhi.

Hatua hiyo inafuatia mifumo mingi ya upangaji, utumiaji upimaji na uwekaji kumbukumbu za ardhi katika Wizara ya Ardhi kuendelea kutumia mifumo ya analogia katika upangaji, utumiaji, upimaji na uwekaji kumbukumbu za sekta ya ardhi.

Katika kufanikisha azma hiyo Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Serikali ya Korea Kusini zimeingia makubaliano ya ushirikiano wa utekelezaji mradi wa ujenzi wa kituo cha Kisasa cha Mafunzo pamoja na uboreshaji miundombinu ya sekta ya ardhi.

Hayo yamebainishwa tarehe 30 Machi 2022 jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi wakati akielezea ushirikiano baina ya serikali ya korea kusini na Wizara ya ardhi katika uanzishaji kituo cha kisasa cha kutolea mafunzo kwa wataalamu wa upimaji pamoja na uboreshaji miundombinu ya sekta ya ardhi.

Uanzishwaji Kituo cha kisasa utagharimu fedha za kitanzania Shilingi Bilioni 5.2 na ule wa ujenzi wa miundombinu utagharimu dola milioni 64.

Akielezea ujenzi wa kituo cha kisasa, Dkt Kijazi alisema uanzishwaji wa kituo hicho siyo tu kwa ajili ya kutumia teknolojia ya kisasa pekee bali ile itakayoendana na wakati ambapo kupitia mradi huo Wizara ya Ardhi itapokea msaada wa kiufundi sambamba na wataalamu wake kupatiwa mafunzo na kuwekewa vifaa vinavyohusu mifumo ya ardhi.

‘’Pamoja na kuwekwa vifaa kwenye kituo lakini pia watumishi watajengewa uwezo pamoja na kukusanya, kuchakata na kutumia takwimu za ardhi katika mipango ya kuendeleza sekta ya ardhi’’ alisema Dkt Kijazi.

Akigeukia sehemu ya pili ya mradi huo, Dkt Kijazi alisema, itakuwa ni ujenzi wa miundombinu itakayowezesha wizara ya Ardhi kutumia teknnolojia ya kisasa katika masuala mazima ya kupanga, kupima na kutumia takwimu za ardhi kwenye maeneo mbalimbali ya nchi..

Mradi mzima utahusisha uandaaji ramani za uwiano mdogo na zile za uwiano mkubwa kwa ile miji mikuu ya mikoa 26 ya Tanzania Bara sambamba na kuweka vituo vya kielektroniki vya upimaji ardhi na kuboresha miundombinu ya kusambaza taarifa za kijografia kwa idara za serikali na watumiaji wote nchini.

Katika hatua nyingine, ujumbe wa wataalamu kutoka Korea kusini uliokuja kwa ajili ya hatua za awali za utekelezaji miradi hiyo ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Hojung Solution Co Ltd Munseok Lee umekutana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula kwa ajili ya kujitambulisha na kumuelezea maendeleo ya utekelezaji miradi hiyo.

Ujumbe huo ulimueleza Dkt Mabula uko tayari kuanza kazi ya utekelezaji mradi huo baada ya maandalizi ya awali ya kutoa mafunzo kwa baadhi ya watumishi nchini.

Kwa upande wake Dkt Mabula aliuambia ujumbe huo kuwa ana imani ujumbe huo ulishiriki vyema hatua zake za awali za maandalizi ya utekelezaji mradi huo na kueleza kuwa matarajio yake kila kitu kitaenda vizuri katika utekelezaji mradi huo.
Share:

RAIS SAMIA AAGIZA TOZO YA SH. 100 KWENYE MAFUTA IREJESHWE


Rais Samia Suluhu ameagiza tozo ya TZS 100 iliyokuwa imetolewa kwenye mafuta irejeshwe kwa sababu hesabu zake tayari zilikuwa zimepigiwa kwenye bajeti. Aidha, amesema kwa mwenendo wa upandaji wa bei ya mafuta duniani, kuondoa TZS 100 hakutasaidia, ila kutainyima serikali mapato.

Rais Samia amesema hayo leo Jumatano Machi 30, 2022 wakati akipokea Ripoti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) ya mwaka 2020/2021 na Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ikulu ya Chamwino, Dodoma.

“Kipindi hiki cha pili mafuta yamepanda kwa Sh. 156 kwa lita Waziri akaona nikitoa Sh. 100 yapande kwa Sh. 56 nitaleta unafuu ndani ya nchi lakini kwa bahati mbaya hakuangalia kwa upana zaidi kwamba ile ilikuwa tayari iko kwenye bajeti iliyopitishwa na bunge.

“Tumekaa kama serikali tumerekebisha ile Sh. 100 iliyotoka nimeagizwa irudishwe, Tathimini tuliyoifanya hata kama ile shilingi tukiitoa kwa mwenendo wa upandaji wa bei ya mafuta duniani bado isingekuwa na impact ila tungejikosesha kile ambacho tunakusanya.

“Bei ya mafuta kwa Tanzania ni ndogo ukulinganisha na nchi za Afrika Mashariki na Kati, lakini wenye sekta wapo kimya hawasemi, tunamsubiria Rais, Nani ni Rais, Rais ni taasisi.

“Mafuta yamekuwa yakipanda bei toka mwaka jana katikati ya mwaka tukachukua hatua ya kupunguza tozo ndani ya mafuta kwa mara ya kwanza ili kushusha bei ya mafuta kwa wananchi lakini mafuta yameendelea kupanda, Waziri akachukua hatua.

“Wabunge katika maeneo yenu nendeni mkawaeleze wananchi wenu kuhusu mambo yanayoendelea kimataifa, mfano vita ya Ukraine na Urusi imechangia kwa kiasi kikubwa bei ya mafuta kupanda, nendeni mkawaeleze wananchi.

“Ukisoma maoni ya Watanzania wengi kwa sasa ni kupanda kwa bei ya bidhaa, itakumbukwa tulikuwa na kipindi cha janga la Uviko-19 na hivyo uzalishaji wa bidhaa ulipungua na kusababisha bei hizo kupanda, angalia sasa uzalishaji unaendelea kuongezeka.

“Waambieni Wananchi yanayoendelea huko duniani… Afrika Mashariki na kati ni Tanzania pekee ambayo bei ya mafuta bado ipo chini kulinganisha na hizo nchi nyingine,” amesema Rais Samia.
Share:

KARIBU JM BUTCHER SHINYANGA MJINI UJIPATIE NYAMA YA NG'OMBE ,SAMAKI NA MAYAI BORA

Habari Njema kwa Wakazi wa Shinyanga na maeneo ya jirani!! JM Butcher inapenda kukutarifu kuwa  tunatoa huduma ya kuuza Nyama ya Ng'ombe, Kuku, Samaki na Mayai bora kwa afya yako!

JM Butcher ipo Nyuma ya Jengo la Benki ya CRDB Mjini Shinyanga..Wasiliana nasi 0753717360 au 0627692212
Share:

AFISA WA AFYA SHIRIKISHO LA SOKA AFRIKA CAF AFARIKI DUNIA


Dr Joseph Kabungo enzi za uhai wake

**

Afisa wa afya wa shirikisho la soka Afrika CAF, Dr Joseph Kabungo amefariki dunia baada ya kupatwa na shambulio la moyo baada ya kumalizika kwa mchezo baina ya Ghana dhidi ya Nigeria na mashabiki kuingia uwanjani kwenye dimba la Abuja International Stadium

Dr Kabungo ambaye alikuwa msimamizi wa mchezo huo kwenye idara ya afya kutokea CAF, taarifa za awali zinasema alipatwa na umauti kutokana na ugonjwa wa shambulio la moyo pindi mashabiki walipoingia uwanjani baada ya mchezo kumalizika dakika 90 huku shirikisho la soka la Zambia likitoa taarifa kusubiri ripoti kamili kutoka CAF na FIFA juu ya chanzo cha kifo cha daktari huyo .

“Ni mapema kusema chanzo kilichosababisha kifo cha Dr Kabungo lakini tunasubiri ripoti kamili kutoka CAF na FIFA kuhusu undani wa tukio hilo” amesema Rais FAZ Andrew Kamanga kupitia mtandao wa Twitter

Enzi za uhai wake alidumu kama daktari wa timu ya taifa ya Zambia “Chipolopolo” kuanzia mwaka 2003 mpaka 2016 huku siku za karibuni alichaguliwa kuwa katika kamati ya matabibu ya FIFA baada ya hapo awali kuwa mjumbe wa kamati ya matabibu wa CAF.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO MACHI 30,2022








Binti aliyekiri kutumwa kuiba watoto afungwa...









Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger