Wednesday, 29 April 2026

KAGERA KUNUFAIKA NA MPANGO WA MKOA WA AFYA MOJA





Na, Mwandishi Wetu, Muleba – Kagera

KAIMU Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Bw. Salum Kimbau amesema maandalizi ya Mpango wa Afya Moja kwa mkoa wa Kagera utaunufaisha mkoa huo kwa kuzingatia malengo yake ya kuboresha uratibu na utekelezaji wa Dhana ya Afya ya Moja na kuendelea kutatua changamoto zilizopo na zenye mwingiliano kati ya binadamu, wanyama na mazingira


Amezungumza hayo wakati akifungua kikao kazi cha wataalamu wa masuala ya Afya Moja kutoka sekta mbalimbali zikiwemo za afya, mifugo, mazingira, wanyamapori na kilimo ambao wamekutana katika Halmashauri ya Wilaya ya Muleba mkoani Kagera kwa siku tano kuanzia tarehe 27 Aprili hadi 01 Mei, 2026 ili kuandaa Mpango huo utakaotumika kubaini rasilimali zitakazosaidia kutatua changamoto na vihatarishi vya afya ya binadamu, wanyama na mazingira.


Bw. Kimbau amesema kuwa, mkoa utanufaika kwa uwepo wa Mpango huo kwani utaongeza tija katika kutatua changamoto zinazokabili sekta hizo hususan katika kuendelea kutatua changamoto za mwingiliano wa magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu na binadamu kwenda kwa wanyama.

“Tunashukuru kuufikia mkoa wetu wa Kagera, tunajua kuwa asilimia 75 ya magonjwa yanatokana na mwingiliano ulipo kati ya wanyama na binadamu, hivyo kuandaliwa kwa mpango kutasaidia utekelezaji wa Dhana ya Afya Moja kwa kushirikiana pamoja, hivyo utatusaidia kutatua changamoto zilizopo na kuwa na jamii salama,” alisema Bw. Kimbau

Aliongezea kuwa ufanisi wa mpango huu unategemea ushirikishwaji wa sekta zote zinazohusika ili kuleta matokeo chanya.

Naye Mratibu wa Maafa kutoka Idara ya Menejimenti ya Maafa sehemu ya Afya Moja kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bi. Valentina Sanga amesema kuwa, Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Serikali la CIHEB Tanzania kupitia Mradi wa Usalama wa Afya Duniani imeratibu maandalizi ya uwepo wa mpango huo huku akisihi kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuhakikisha utekelezaji wake unaleta matunda yanayotarajiwa.

Aidha, aliwasihi wataalamu wa Masuala ya Afya Moja kutumia fursa hiyo kuja na Mpango utakaoinufaisha Kagera, kwa kuzingatia ni miongoni mwa Mikoa inayokumbwa na majanga ya mlipuko mengine yakichangiwa na mwingiliano wa wanyama na binadamu.

“Dhana ya Afya Moja (One Health) inatoa fursa ya kutambua uhusiano wa karibu kati ya afya ya binadamu, wanyama, na mazingira. Inasisitizwa kuendelea kujifunza zaidi dhana hii ili kutatua changamoto zilizopo zikiwemo za milipuko ya magonjwa na kuweza kuyakabili endapo yanatokea katika maeneo yetu,” alisisitiza Bi. Valentina

Aliongezea kuwa, Mpango huo utasaidia kutatua changamoto za masuala ya kiafya zinazotokea katika Halmashauri za mkoa wa Kagera, kujiandaa na kukabili majanga hayo ili kuwa na jamii salama kwa maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la CIHEB Tanzania, Bw. Mark Lwakatare alisema mradi wa Usalama wa Afya Duniani utaendelea kushirikiana na mikoa husika katika kuimairisha utekelezaji wa dhana ya Afya Moja ili nchi iweze kukabiliana na vihatarishi vya majanga mbalimbali.


“Mradi huu unashirikiana na Serikali kuboresha na kuimarisha utekelezaji wa afua mbalimbali kupitia dhana ya Afya Moja nchini, hivyo mradi utaendelea kushirikiana katika kujiandaa na kukabili athari katika afya ya binadamu, manyama na mazingira,” alisisitiza Lwakatare.

Share:

DKT. MAULID AONGOZA KIKAO CHA BODI YA CHUO CHA MAJI


Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Maji (Water Institute) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dr. Maulid J. Maulid wamekutana Aprili 28, 2026 jijini Dar Es Salaam kwa kikao cha 46 cha Bodi hiyo kujadili masuala ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utoaji wa huduma za kitaaluma na miradi ya maendeleo itakayoboresha ufundishaji na ujifunzaji.

Bodi ya Chuo inaundwa na wajumbe saba ambao ni Dr. Felician Komu, CPA Lucy Mrikaria, Dr. Maulid J. Maulid (Mwenyekiti), Professor Adam Karia (Katibu/Mkuu wa Chuo cha Maji), Professor Said Ally, Ms. Jane Gonsalves na Engineer Charles Mafie (Mkurugenzi wa Usambazaji Wizara ya Maji)
Share:

Tuesday, 28 April 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 29,2026

Magazeti



 



Share:

KUTANA NA MTABIBU WA NY0TA ZA BINADAMU, BINGWA WA TIBA ZA ASILI AFRIKA

 


Kutana na Mtabibu Shariff Majini
Mwenye uwezo mkubwa kutoka kwa Allah  Mtabibu wa nyota za binadamu na dawa za asili za Afrika ✦ Ana uwezo wa kubaini tatizo lako mara tu unapowasiliana naye kupitia njia husika.

Je, unasumbuliwa na matatizo yafuatayo?

Mapenzi
Umeachwa na umpendaye, awe mume, mke au mpenzi, na bado unampenda? Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Wasiliana na Shariff Majini ujionee muujiza wa papo kwa papo ✦ Ana uwezo wa kurudisha mahusiano na kuimarisha ndoa yako ndani ya saa 12 tu.

Mahusiano yaliyovunjika
Umekimbiwa na mumeo, mkeo au mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akusaidie kutatua tatizo hilo.

Ahadi kutimizwa
Atamfanya mhusika atimize ahadi zote kwa muda mfupi.

Matatizo kwa kutumia jina au picha
Shariff Majini hutumia jina la mhusika au picha kusaidia kumaliza tatizo lako.

Huduma nyingine

✦ Kutibu kwa kutumia vitabu vya Qur'an
✦ Dawa za asili za Afrika
✦ Dawa za Kiarabu
✦ Kutafsiri ndoto
✦ Kushinda bahati nasibu
✦ Kusafisha nyota
✦ Kuvutia biashara na mvuto wa mwili
✦ Kinga ya mwili
✦ Zindiko za nyumba
✦ Miguu kufa ganzi
✦ Kufungua kizazi kwa waliofungwa kishirikina
✦ Kupata jini la mali kwa wanaohitaji utajiri bila masharti
✦ Nguvu za kiume
✦ Kumaliza kesi zilizoshindikana ndani ya siku 14 tu

Mawasiliano

+255 756 465 818
📱 WhatsApp: +255 756 465 818

NB: Tiba kwa dini zote na imani zote 

Share:

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA BELARUS AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Belarus, Mheshimiwa Maxim Ryzhenkov, amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia Aprili 28 hadi 30, 2026, kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo.

Mheshimiwa Ryzhenkov amewasili kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, ambapo alipokewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe, pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Belarus nchini Mhe.Dzmitry Krasouski.

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Ryzhenkov anatarajiwa kufanya mazungumzo ya pande mbili na mwenyeji wake, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, Aprili 28, 2026, jijini Dar es Salaam. Aidha, atakutana na viongozi wengine wa Serikali kwa lengo la kuendeleza na kupanua ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Ziara hiyo inalenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Belarus pamoja na kukuza ushirikiano wa kiuchumi katika maeneo yenye maslahi ya pamoja.









Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger