
Saturday, 23 May 2026
Ngoma Mpya : MJUKUU WA MWANAMALONDE - MBITI YANE 'Fisi Wangu'

VIJANA LINDENI AMANI YA TANZANIA

Na Vero Ignatus
Mwanadiplomasia na Mratibu wa Makongamano ya Vijana, Ndugu Omary Abdul Punzi, ametoa onyo kwa vijana nchini kuacha kufuata mikumbo isiyo na tija na badala yake waithamini nchi yao kwa kutanguliza uzalendo mbele.
Akizungumza katika mahojiano maalum na Vuka Blog, Punzi amesisitiza kuwa amani ya nchi haitofautiani na utulivu wa kisiasa, bali inategemea kwa kiasi kikubwa jinsi vijana wanavyoheshimu utamaduni wao na kushirikiana kikamilifu na mihimili nane muhimu inayolinda na kulea taifa.
Amewasihi vijana kuwa makini na ushawishi hasi wa utandawazi na makundi yasiyo na maadili yanayotishia mustakabali wa nchi.
Akionyesha masikitiko yake, Punzi amekumbusha kuwa Tanzania ni urithi wa thamani tulioachiwa na waasisi wetu, hivyo hakuna nchi nyingine mbadala ikiwa vijana wataharibu hii iliyopo.
Alibainisha kuwa miongozo na desturi nzuri zilizowekwa na wazee wa kimila tangu zamani hazikuwa za kizamani, bali zililenga kulinda utu na heshima ya jamii.
Alionya kuwa sasa vijana wanatupa dhahabu yao kwa sababu tu inaonekana ya kienyeji na kuokota shaba ya kigeni kwa kuwa inang’aa, jambo linalohitaji mabadiliko ili mila na desturi zilizokubalika zisafishwe na kuendelezwa badala ya kufutwa kabisa.
Katika uchambuzi wake, Punzi alifafanua jinsi mihimili nane ya amani na malezi inavyopaswa kuwa dira kwa kijana mzalendo. Mhimili wa kwanza ni shule ambayo ndiyo msingi wa maarifa, nidhamu na malezi ya awali ya kiakili yanayomfanya kijana kuwa raia mwema.
Hii inaenda sambamba na Jeshi la Polisi ambalo ni chombo cha usalama wa raia na mali zao kinachotegemea ushirikiano wa karibu na vijana kupitia ulinzi shirikishi.
Vivyo hivyo, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) linatajwa kama jukwaa la kuwajenga vijana katika ukakamavu na uzalendo, huku Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) likiwa ngome kuu ya ulinzi wa mipaka ya nchi na alama ya mamlaka ya taifa.
Mihimili mingine inayokamilisha ngome hii ya malezi na ulinzi inajumuisha Idara ya Usalama wa Taifa, chama cha Skauti, taasisi za kidini, pamoja na mila na desturi nzuri ambazo ndizo msingi wa utambulisho wa Mwafrika unaosisitiza heshima, mshikamano na utatuzi wa migogoro kwa njia ya mazungumzo badala ya vurugu.
Punzi amewataka vijana kutokubali kuwa bendera inayofuata upepo wa mambo yanayoonekana maarufu kwenye mitandao ya kigeni, kwani kufanya hivyo ni kupoteza dira.
Alizitaka taasisi zote za elimu, dini na vikosi vya usalama kushirikiana kwa karibu ili kuwatengenezea vijana mazingira wezeshi yatakayowafanya kuwa walinzi namba moja wa amani na maendeleo ya Tanzania.
Friday, 22 May 2026
BOSI WANGU HAKUTAMBUA JUHUDI ZANGU HADI NILIPOPATA KILICHONIFANYA NITHAMINIKE KAZINI
Jina langu ni Elisunguo Martin, mfanyakazi wa kampuni ya utalii jijini Arusha nchini Tanzania, na ninataka kushiriki hadithi yangu ili kumtia moyo mtu yeyote anayehisi hatambuliki kazini. Kwa muda mrefu, nilifanya kazi kwa bidii, niliendelea kujitolea, na kila mara nilitimiza majukumu yangu kwa wakati. Lakini haijalishi ni juhudi ngapi nilizofanya, bosi wangu hakuonekana kuniona.
Kadri muda ulivyosonga, hali hiyo ilizidi kuwa ya kukatisha tamaa. Niliona wenzangu wakisifiwa, kupandishwa cheo, na kupewa fursa huku mimi nikibaki katika nafasi hiyo hiyo. Ilinifanya nijisikie kutoonekana na kutothaminiwa. Nilianza hata kupoteza motisha kwa sababu nilihisi kama kazi yangu ngumu haikuwa na maana.
Rafiki wa karibu aliniambia baadaye kuhusu Mganga wa mashuhuri wa kienyeji mkazi wa Sumbawanga na jinsi alivyomsaidia kupata kutambuliwa na kujitokeza mahali pake pa kazi. Alinitia moyo kuwasiliana nae na kuelezea hali yangu. Baada ya kusikia uzoefu wake, niliamua kuwasiliana na Mganga huyu. Alisikiliza kwa makini na kutoa uchawi wa kutambuliwa na neema ili kunisaidia kujitokeza na kutambuliwa kazini. Pia aliniongoza kwenye hatua za kufuata kwa uvumilivu.
Baada ya muda fulani, nilianza kuona mabadiliko. Kazi yangu ilianza kuvutia umakini, bosi wangu alianza kutambua juhudi zangu, na nilipewa majukumu zaidi. Kwa mara ya kwanza, nilihisi kuonekana na kuthaminiwa.
Leo, ninatambulika mahali pangu pa kazi. Nimepata heshima, fursa bora zaidi, na ninaendelea vizuri katika kazi yangu. Kujiamini kwangu kumeimarika, na sasa ninahisi motisha ya kuendelea kukua.
Ninashiriki uzoefu huu ili kumtia moyo yeyote anayehisi kupuuzwa asipoteze tumaini kwa sababu mabadiliko yanawezekana.
Ninamhimiza sana mtu yeyote anayepambana na ukosefu wa kutambuliwa, kudumaa kazini, au kupuuzwa kazini awasiliane na Daktari Nassoro Tambiku. Anasikiliza, anaongoza, na hutoa suluhisho zinazoleta mwonekano, upendeleo, na ukuaji wa kazi.
📞Simu / WhatsApp Daktari Tambiku: +255766649862
Tovuti:www.doctortambiku.com
Wasiliana na Daktari Nassoro Tambiku anayepatikana Sumbawanga leo na chukua hatua ya kwanza kuelekea kutambuliwa na kusonga mbele katika taaluma yako.
Thursday, 21 May 2026
TAKUKURU KAGERA YAREJESHA ZAIDI YA MILIONI 624, YABAINI DOSARI MIRADI YA MAENDELEO



MCHENGERWA ATAKA USHIRIKIANO WA KIKANDA KUTOKOMEZA MALARIA NA NTDs

MAZISHI YA BOAZ MARTINE KUFANYIKA KESHO MWAWAZA, MSIBA UPO KITANGILI SHINYANGA MJINI
Mazishi ya aliyekuwa Mpiga Picha wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, marehemu Boaz Martine, yanatarajiwa kufanyika kesho Alhamisi Mei 21, 2026 katika makaburi ya familia yaliyopo Mwawaza, Manispaa ya Shinyanga.Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, David Lyamongi, ibada ya kumuombea marehemu itaongozwa na Mashahidi wa Yehova kuanzia saa 7:00 mchana nyumbani kwa marehemu nyuma ya Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kitangili, Manispaa ya Shinyanga.
Baada ya ibada na salamu za rambirambi, mwili wa marehemu utapelekwa katika makaburi ya familia yaliyopo Mwawaza kwa ajili ya mazishi yatakayoanza majira ya saa 9:00 alasiri.
Marehemu Boaz Martine alifariki dunia Mei 19, 2026 kufuatia ajali ya barabarani iliyotokea katika eneo la Samuye mkoani Shinyanga, ajali iliyohusisha gari lililokuwa limebeba waandishi wa habari pamoja na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Akizungumza na waandishi wa habari Mei 20, 2026, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga SACP Janeth Magomi alisema ajali hiyo ilisababishwa na uzembe wa dereva wa gari aina ya Toyota Harrier aliyekuwa akijaribu kulipita gari lililokuwa mbele yake bila tahadhari.
Mbali na marehemu Boaz Martine, watu saba walijeruhiwa katika ajali hiyo ambao ni Frank Mshana wa ITV/Radio One, Johnson James, Koplo Swahiba Msangi, Neema Madono (36), Rehema Edson (45), Shadia Omari (32) pamoja na dereva wa gari la Land Cruiser Laurence Peter (34).
Majeruhi hao wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga na wengine katika Hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza.
Wednesday, 20 May 2026
TANZANIA KUJIFUNZA KUTOKA CHINA KUHUSU MAGEUZI YA MASHIRIKA YA UMMA















































