Tuesday, 10 March 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MACHI 10, 2026

Share:

Monday, 9 March 2026

DAWA ZA UHAKIKA ZA ULINZI WA MWILI NA NYUMBA 'ZINDIKO ZITO'


Je, unahisi kuna nguvu zisizoeleweka zinakufuata?

Je, nyumba yako inakosa amani au biashara haikui?

Dr. Sudai “Ng’wana Gama” anatoa dawa za kienyeji zenye nguvu za ulinzi wa mwili na nyumba, kupitia zindiko la asili lenye nguvu kubwa za kiroho.

Huduma zinazopatikana:
✔ Ulinzi wa mwili dhidi ya nguvu hasi
✔ Kufunga njia za wachawi na majambazi
✔ Kuweka kinga ya kiroho kwenye nyumba au biashara
✔ Kuondoa mikosi na mapepo
✔ Kuvutia mafanikio na baraka

📍 Huduma zinapatikana Maswa – Simiyu
📞 Wasiliana: +255 676 444 408 au 0624333380

Share:

WANAZUONI WAHIMIZA WAISLAMU KUTOA ZAKA KUPAMBANA NA UMASKINI


Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga.

***
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga, amewahimiza Waislamu kutekeleza ipasavyo ibada ya Zaka ili kusaidia kupunguza umasikini katika jamii.

Akizungumza katika kongamano la wanazuoni wa Kiislamu lililofanyika katika ukumbi wa Dar es Salaam Youth Centre (DYCC) jijini Dar es Salaam, Sheikh Ndauga alisema Zaka ni moja ya ibada muhimu inayolenga kuwasaidia watu wenye uhitaji katika jamii.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga.


Alisema kwa mujibu wa mafundisho ya dini ya Kiislamu, Zaka imewekwa mahsusi ili kuwainua watu wasiojiweza pamoja na kuimarisha mshikamano wa kijamii miongoni mwa waumini wa dini hiyo.


Sheikh Ndauga alieleza kuwa Waislamu wakitekeleza ibada hiyo kwa uaminifu na kwa kuzingatia maelekezo ya dini, inaweza kuwa nyenzo muhimu ya kupunguza umasikini na kuboresha maisha ya watu wengi.


Kwa upande wake, Sheikh Ally Zuberi akichangia mada katika kongamano hilo, alisema kumekuwepo na dhana potofu miongoni mwa baadhi ya Waislamu kuhusu walengwa wa Zaka.

Alisema baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa Zaka inapaswa kutolewa kwa yatima pekee bila kuzingatia mafundisho sahihi ya Kiislamu kuhusu makundi yanayostahili kupewa Zaka.


Sheikh Zuberi alifafanua kuwa katika mafundisho ya Kiislamu, yatima hawakutajwa moja kwa moja miongoni mwa makundi ya wanaostahili kupewa Zaka isipokuwa pale wanapokuwa katika hali ya umasikini.


Wanazuoni hao walisisitiza umuhimu kwa Waislamu kujifunza na kuelewa kwa usahihi mafundisho ya dini kuhusu utoaji wa Zaka ili kuhakikisha ibada hiyo inatekelezwa kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa.















Share:

Sunday, 8 March 2026

RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA NDANI WA VIONGOZI WA EAC KABLA YA MKUTANO MKUU




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki katika Mkutano wa Ndani pamoja na baadhi ya Wakuu wa Nchi wa Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kabla ya Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 07 Machi, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Kenya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Mhe. William Somoei Ruto pamoja na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni na Rais wa Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Ndani wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 07 Machi, 2026.
Share:

Saturday, 7 March 2026

WATAALAMU WALIOSOMA JAPAN WACHOCHEA MIRADI YA MAENDELEO NCHINI




Wataalamu wa Kitanzania waliopata mafunzo nchini Japan wameelezwa kuwa rasilimali muhimu katika kuharakisha maendeleo ya sekta mbalimbali kwa kutumia ujuzi na teknolojia walizojifunza nje ya nchi.

Akizungumza katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Msaidizi wa Ofisi ya Rais – Utumishi, Fadhili Mitimingi, amesema ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Japan International Cooperation Agency (JICA) umewezesha Watanzania wengi kupata mafunzo ya kitaalamu nje ya nchi.

Mtimingi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – Utumishi katika Mkutano Mkuu wa Japan Alumni of Tanzania Association (JATA), amesema wahitimu wa mafunzo hayo wamekuwa wakirejea nchini na kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo.

Amesema kupitia miradi hiyo, wataalamu hao wamekuwa wakisambaza maarifa waliyopata kwa wananchi wengine ili kusaidia matumizi ya mbinu bora na za kisasa katika uzalishaji.

“Hatua hiyo imechangia kuboresha maisha ya wananchi kwa kuwahamasisha kutumia teknolojia na mbinu mpya katika sekta muhimu za uchumi,” amesema Mitimingi.

Kwa upande wake, Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mikami Yoichi, amesema mkutano huo ulihusisha mawasilisho ya miradi kutoka kwa washiriki watatu waliowasilisha kazi walizozitekeleza baada ya kurejea nchini.



Naye Mwenyekiti wa JATA, Gregory Mlay, amesema umoja huo unawakutanisha wataalamu kutoka sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, mifugo, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), biashara na afya ili kushirikiana katika miradi ya maendeleo.

Katika hatua Nyingine, Mwakilishi Mkazi wa JICA Tanzania, Ara Hitoshi, amesema lengo kuu la mafunzo hayo ni kuchangia maendeleo ya Tanzania ili kufanikisha hilo, washiriki wanaporudi kutoka kwenye mafunzo wanapaswa kuchukua hatua za kuwasaidia wengine kwa kutumia maarifa na uzoefu walioupata.



Mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo, Godfrey Christopher, amesema wamejifunza mbinu za kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi kupitia usindikaji na uhifadhi bora, hatua inayosaidia kupunguza upotevu wa mazao na kuongeza kipato cha wananchi.










Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger