Friday, 24 April 2026

Video Mpya : SHINJE ORIGINAL - YA MOTO BALAA

 

Share:

TAMCU YAIMARISHA UCHUMI WA WAKULIMA TUNDURU KWA UNUNUZI WA MALORI MAPYA MATANO

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe.  Denis Masanja watatu kutoka kulia akiwa anakata utepe wakati wa kukabidhi magari hayo mapya matano ya chama cha Ushirika Tunduru (TAMCU) limited Mwenyekiti wa Chama kikuu cha ushirika wilaya ya Tunduru (Tamcu) Musa Manjaule kushoto na meneja masoko wa Benki ya Crdb kanda ya kusini  Emanuel Bigailo wakisaini hati ya makabidhiano ya malori matano mapya yaliyonunuliwa na Tamcu baada ya kupata mkopo kutoka Crdb,nayeshuhudia katikati Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Deni Masanja.

Na Regina Ndumbaro Tunduru-Ruvuma 

Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Tunduru (TAMCU) kimechukua hatua kubwa ya kuongeza ufanisi katika sekta ya kilimo kwa kununua malori matano mapya ya kubebea mazao, hatua inayolenga kurahisisha usafirishaji na kuongeza mapato ya chama pamoja na wanachama wake. 

Uamuzi huo umepokelewa kwa furaha na wakulima wa wilaya hiyo ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikumbwa na changamoto ya ucheleweshaji wa mazao kufika sokoni kutokana na uhaba wa vyombo vya usafiri.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima, Rashid Chibwana amesema kuwa malori hayo yatasaidia kuwafikia wakulima mashambani na kusafirisha mazao yao kwa wakati hadi maghala na hatimaye kwenye minada. 

Amebainisha kuwa hapo awali walitegemea chanzo kimoja cha mapato, lakini uwekezaji huo mpya utaongeza mapato ya chama huku ukipunguza gharama na usumbufu wa usafirishaji.

Mwenyekiti wa TAMCU, Mussa Manjaule, amesema ununuzi wa malori hayo umetokana na maombi ya wanachama waliotaka kuboreshwa kwa huduma za usafirishaji pamoja na kuongeza vyanzo vya mapato. 

Ameeleza kuwa awali walikuwa wanapata changamoto hata katika kusafirisha pembejeo kama viuatilifu kutoka mikoa jirani, lakini sasa hali hiyo itaboreshwa kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake, Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Tunduru, Emanuel Mwasuka, amesema benki hiyo imechangia sehemu kubwa ya fedha zilizotumika kununua malori hayo yenye thamani ya shilingi bilioni 1.5. 

Ameahidi kuendelea kushirikiana na vyama vya ushirika kwa kutoa mikopo, huku akisisitiza umuhimu wa kuyatunza malori hayo ili yadumu na kuleta tija inayokusudiwa.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Denis Masanja, ameipongeza TAMCU kwa hatua hiyo akieleza kuwa ni mfano bora wa maendeleo katika sekta ya ushirika. 

Amesema uwekezaji huo utachochea biashara ya mazao kama korosho, ufuta na mbaazi, kupunguza gharama za usafirishaji na kuongeza kipato kwa wakulima, huku akitoa wito kwa wanachama kushirikiana na viongozi wao ili kufanikisha malengo ya chama.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 24,2026


Magazeti
 
Share:

Thursday, 23 April 2026

HAMU YA MARIDHIANO: VIONGOZI WA DINI NA WANASIASA WAHIMIZA AMANI BAADA YA RIPOTI

 

Viongozi wa dini na wanasiasa nchini wametoa mwito wa dhati kwa Watanzania kudumisha amani, utulivu, na mshikamano kufuatia kukamilika na kuwasilishwa kwa ripoti ya Tume ya Kuchunguza Matukio Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. Ripoti hiyo inawasilishwa leo Aprili 23,2026.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Alhad Mussa Salum, amesisitiza kuwa huu ni wakati wa kujenga imani miongoni mwa wananchi na kuamini uwezo wa ndani katika kutatua changamoto za kitaifa bila kutegemea msaada wa nje. 

Salum amebainisha kuwa tume hiyo iliyoongozwa na Jaji Mkuu mstaafu, Mohamed Chande Othman, ina wajumbe wenye weledi mkubwa, hivyo ni muhimu ripoti hiyo ipokewe, ichambuliwe, na iwapo kutakuwa na upungufu, mifumo iliyopo itumike kurekebisha badala ya kujenga chuki.

Kiongozi huyo wa JMAT ameongeza kuwa kutokuaminiana kati ya wananchi na viongozi wao kunaweza kukwamisha juhudi za kujitawala, akionya kuwa matukio ya Oktoba 29 ya mwaka jana yanapaswa kuwa chachu ya kujenga taifa imara zaidi badala ya kurudia makosa yaliyopita. 

Kwa upande wake, Kiongozi wa Kanisa la Evangelical Fellowship Church Tanzania (EFCT), Askofu Charles Howard, ameeleza hamu yake ya kuiona Tanzania inayojenga misingi ya kusikilizana na kuridhiana hata pale kunapokuwa na tofauti za kifikra. Amesema misingi ya dini zote inahimiza amani na kuheshimiana, hivyo Watanzania hawana budi kutumia maadili hayo kuimarisha umoja wa kitaifa.

Naye Askofu Godfrey Songambele wa Kanisa la Tumaini la Mataifa Yote (HOFAN), amekumbusha kuwa amani ya kweli inapaswa kwenda sambamba na utekelezaji wa haki kwa wananchi, akisisitiza kuwa "amani ni wimbo, lakini haki ni matendo." 

Mtazamo huu wa hitaji la haki na maridhiano umeungwa mkono na Katibu Mkuu wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Hassan Doyo, ambaye amesema mustakabali wa Tanzania unategemea wanasiasa wanaoweza kukaa pamoja na kujadili maendeleo, uchumi, na usalama wa nchi. Doyo ametoa mwito kwa wananchi kutokubali kushawishiwa kufanya vurugu na viongozi wa kisiasa, badala yake walinde tunu ya amani iliyopo.

Katika kutoa mwelekeo wa kisiasa, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Dorothy Semu, amebainisha matarajio yake kuwa ripoti hiyo itasema ukweli mtupu kuhusu nini hasa kilisababisha uvunjifu wa amani uliotokea wakati wa mchakato wa uchaguzi. Maoni haya ya viongozi mbalimbali yanadhihirisha kiu ya Watanzania kuona taifa linasonga mbele kwa masikilizano na kurejea katika hali ya utulivu wa kudumu baada ya taarifa hiyo ya tume ya uchunguzi kuwekwa wazi kwa umma.

Share:

AMANI YATAJWA KAMA MTAJI WA MAENDELEO NA USTAWI WA JAMII



Katika kile kinachoonekana kama mwendelezo wa kusisitiza misingi ya Taifa, watanzania wamekumbushwa kuwa amani ndiyo nguzo kuu inayotoa uhuru wa kweli kwa mwananchi yoyote yule kuweza kufanya shughuli zake za kila siku kwani bila amani na utulivu hakuna uhuru wa Kijamii wala fursa za kiuchumi zinazoweza kuwepo kwenye jamii na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza na mwandishi wetu wa habari leo Jumatano Aprili 22, 2026 Wilayani Ilala Jijini Dar Es Salaam, Bi. Lucy Mgecha, mjasiriamali katika soko la Ilala anasema kwamba amani si tu hali ya kutokuwa na vita bali pia ni mazingira yanayomfanya kila mwananchi kujihisi salama kukuza kipato chake na kushiriki katika ujenzi wa jamii na uchumi wake.

"Amani ni kuwa na uhuru wa kufanya lolote linalokubalika kisheria na kwenda popote unapotaka kwenda, uwe na uwezo huo wa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na ninakumbuka kilichotokea Oktoba mwaka jana tulikosa uhuru kabisa wa kutembea kuanzia sisi watu wazima hadi watoto na hapa ndipo tuliposema amani sasa imevurugika na kwasasa tunamshukuru Mungu amani ipo na tunaendelea na biashara zetu." Amesema Bi. Lucy Mgecha.

Mgecha anaungana na wadau wengine wa maendeleo nchini ambao wanabainisha kuwa amani ni mtaji usioonekana, wakieleza kwamba katika maeneo yenye utulivu, wafanyabiashara, wakulima na wawekezaji hupata uhuru wa kupanga mipango ya muda mrefu na mfupi, uhuru pia ukichochea mzunguko wa fedha na kuongeza fursa za ajira na masoko.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI APRILI 23,2026



Magazeti



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger