Monday, 16 February 2026

MAVUNDE AZINDUA KISIMA CHA MAJI MSALATO, ASEMA NI UTEKELEZAJI WA AHADI YA 2025

Mbunge wa Jimbo la Mtumba Mkoani Dodoma, Mhe. Anthony Mavunde, ambaye pia ni Waziri wa Madini amezindua kisima cha maji katika Mtaa wa Msalato, Ubalozi wa Catherine Mwajoka, kwa ajili ya matumizi ya wananchi.

Uzinduzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kuhusu kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo.

Akizungumza na wananchi mara baada ya uzinduzi huo, Mheshimiwa Mavunde amewataka wakazi wa Msalato kulinda na kutunza miundombinu ya kisima hicho ili kiweze kudumu na kuwanufaisha kwa muda mrefu.

Amesisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

Aidha, ameahidi kuendelea kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii ya Msalato na Jimbo la Mtumba kwa ujumla, kwa kushirikiana na viongozi wengine wa Serikali.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Mavunde amewashukuru wananchi wa Msalato kwa imani kubwa waliyoionesha kwa kumpigia kura Samia Suluhu Hassan, yeye kama Mbunge pamoja na Diwani wao wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2025, akieleza kuwa ushindi huo unampa nguvu ya kuendelea kuwatumikia wananchi kwa bidii na uadilifu.

Share:

WALIOMHAMASISHA MTOTO KUVUTA SIGARA MIKONONI MWA POLISI

 


Kupitia mitandao ya kijamii kunasambazwa picha mjongeo akionekana mtoto mdogo wa kiume na zikisikika sauti zikimhamasisha kuvuta sigara Kitendo hicho ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za kijamii na nchi. Jeshi la Polisi, limeanza uchunguzi na kuwafuatilia watu hao kwa hatua nyingine za kisheria.

 

Aidha, linatoa wito kwa yeyote anayewafahamu watu hao au mtoto huyo atusaidie kuwafikia na kuokoa afya ya mtoto huyo.


Pia, linatoa onyo kwa watu wenye tabia za kufanya vitendo vya kikatili na vya unyanyasaji kama hivyo na vinavyofanana na hivyo kwa watoto kwa lengo lolote lile ikiwepo msukumo wa kutafuta wafuasi (followers) kwa ajili ya mitandao yao ya kijamii kuziacha kwani halitasita kuwakamata kwa sababu ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za nchi.

Share:

Sunday, 15 February 2026

Video Mpya : MASUMBUKO Ft. NELEMI MBASANDO - NARIDHIKA

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEBRUARI 15,2026



Magazeti
 

   
Share:

Saturday, 14 February 2026

RAIS SAMIA ADHIHIRISHA UPENDO WAKE KWA KUWAJENGEA ICU WANANCHI HANDENI - PROF. SHEMDOE

Na OWM – TAMISEMI, Handeni

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujenga jengo la Wagonjwa Mahututi (ICU) katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni ili kuokoa maisha ya wananchi wa Handeni, kitendo ambacho kinadhirisha upendo wake kwa wananchi hao. 

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Februari 13, 2026 katika Viwanja vya Handeni Square, alipopewa fursa ya kuzungumza na wananchi kabla ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba kuzungumza na wananchi hao, mara baada ya Mhe. Waziri Mkuu kuhitimisha ziara yake ya kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani Handeni. 

“Ndugu zangu wa Handeni tumshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha fedha za ujenzi wa jengo hili la ICU, wengine si rahisi kutambua umuhimu wa jengo hili kwasababu hawajaugua na kulazimika kulazwa ICU, ni jengo muhimu la kuokoa maisha ya mwanadamu,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Kwa kutambua umuhimu wa majengo ya ICU, Prof. Shemdoe amesema  Ofisi ya Rais - TAMISEMI inaendelea kuangalia uwezekano wa kujenga majengo ya ICU Lushoto na Mkinga ili kuboresha huduma za tiba katika maeneo hayo, na kuongeza kuwa ofisi yake inaendelea na jitihada za kuhakikisha hospitali za wilaya ambazo hazina majengo hayo zinapata ili kuokoa maisha ya wananchi.

Kwa upande wake. Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI (Elimu) ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini Mhe. Reuben Kwagilwa amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha ujenzi wa jengo la Wagonjwa Mahututi, Maabara, Huduma za Dharura na na jengo la kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni ambayo miundombinu yake ilikuwa chakavu kwani ilijengwa mwaka 1961.
 
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni, Dkt. Hudi Muradi amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizowezesha kujenga miundombinu katika hospitali hiyo, hivyo amemuahidi Mhe. Rais pamoja na wananchi kuwa, watatoa huduma bora na kuilinda miundombinu hiyo ili  itumike kwa muda mrefu. 

Aidha, kwa niaba ya wakazi wa Handeni Bw. Khalid Hassan Malungula ameishukuru Serikali kwa kujenga jengo la ICU ambalo limeboresha utoaji wa huduma kwa wagonjwa mahututi, na kueleza kuwa kabla ya ujenzi wa jengo hilo wagonjwa wa kawaida na mahututi walikuwa wakihudumiwa  pamoja.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 14,2026

Magazeti
 
     
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger