Monday, 9 March 2026

DAWA ZA UHAKIKA ZA ULINZI WA MWILI NA NYUMBA 'ZINDIKO ZITO'


Je, unahisi kuna nguvu zisizoeleweka zinakufuata?

Je, nyumba yako inakosa amani au biashara haikui?

Dr. Sudai “Ng’wana Gama” anatoa dawa za kienyeji zenye nguvu za ulinzi wa mwili na nyumba, kupitia zindiko la asili lenye nguvu kubwa za kiroho.

Huduma zinazopatikana:
✔ Ulinzi wa mwili dhidi ya nguvu hasi
✔ Kufunga njia za wachawi na majambazi
✔ Kuweka kinga ya kiroho kwenye nyumba au biashara
✔ Kuondoa mikosi na mapepo
✔ Kuvutia mafanikio na baraka

📍 Huduma zinapatikana Maswa – Simiyu
📞 Wasiliana: +255 676 444 408 au 0624333380

Share:

WANAZUONI WAHIMIZA WAISLAMU KUTOA ZAKA KUPAMBANA NA UMASKINI


Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga.

***
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga, amewahimiza Waislamu kutekeleza ipasavyo ibada ya Zaka ili kusaidia kupunguza umasikini katika jamii.

Akizungumza katika kongamano la wanazuoni wa Kiislamu lililofanyika katika ukumbi wa Dar es Salaam Youth Centre (DYCC) jijini Dar es Salaam, Sheikh Ndauga alisema Zaka ni moja ya ibada muhimu inayolenga kuwasaidia watu wenye uhitaji katika jamii.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga.


Alisema kwa mujibu wa mafundisho ya dini ya Kiislamu, Zaka imewekwa mahsusi ili kuwainua watu wasiojiweza pamoja na kuimarisha mshikamano wa kijamii miongoni mwa waumini wa dini hiyo.


Sheikh Ndauga alieleza kuwa Waislamu wakitekeleza ibada hiyo kwa uaminifu na kwa kuzingatia maelekezo ya dini, inaweza kuwa nyenzo muhimu ya kupunguza umasikini na kuboresha maisha ya watu wengi.


Kwa upande wake, Sheikh Ally Zuberi akichangia mada katika kongamano hilo, alisema kumekuwepo na dhana potofu miongoni mwa baadhi ya Waislamu kuhusu walengwa wa Zaka.

Alisema baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa Zaka inapaswa kutolewa kwa yatima pekee bila kuzingatia mafundisho sahihi ya Kiislamu kuhusu makundi yanayostahili kupewa Zaka.


Sheikh Zuberi alifafanua kuwa katika mafundisho ya Kiislamu, yatima hawakutajwa moja kwa moja miongoni mwa makundi ya wanaostahili kupewa Zaka isipokuwa pale wanapokuwa katika hali ya umasikini.


Wanazuoni hao walisisitiza umuhimu kwa Waislamu kujifunza na kuelewa kwa usahihi mafundisho ya dini kuhusu utoaji wa Zaka ili kuhakikisha ibada hiyo inatekelezwa kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa.















Share:

Sunday, 8 March 2026

RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA NDANI WA VIONGOZI WA EAC KABLA YA MKUTANO MKUU




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki katika Mkutano wa Ndani pamoja na baadhi ya Wakuu wa Nchi wa Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kabla ya Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 07 Machi, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Kenya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Mhe. William Somoei Ruto pamoja na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni na Rais wa Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Ndani wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 07 Machi, 2026.
Share:

Saturday, 7 March 2026

WATAALAMU WALIOSOMA JAPAN WACHOCHEA MIRADI YA MAENDELEO NCHINI




Wataalamu wa Kitanzania waliopata mafunzo nchini Japan wameelezwa kuwa rasilimali muhimu katika kuharakisha maendeleo ya sekta mbalimbali kwa kutumia ujuzi na teknolojia walizojifunza nje ya nchi.

Akizungumza katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Msaidizi wa Ofisi ya Rais – Utumishi, Fadhili Mitimingi, amesema ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Japan International Cooperation Agency (JICA) umewezesha Watanzania wengi kupata mafunzo ya kitaalamu nje ya nchi.

Mtimingi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – Utumishi katika Mkutano Mkuu wa Japan Alumni of Tanzania Association (JATA), amesema wahitimu wa mafunzo hayo wamekuwa wakirejea nchini na kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo.

Amesema kupitia miradi hiyo, wataalamu hao wamekuwa wakisambaza maarifa waliyopata kwa wananchi wengine ili kusaidia matumizi ya mbinu bora na za kisasa katika uzalishaji.

“Hatua hiyo imechangia kuboresha maisha ya wananchi kwa kuwahamasisha kutumia teknolojia na mbinu mpya katika sekta muhimu za uchumi,” amesema Mitimingi.

Kwa upande wake, Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mikami Yoichi, amesema mkutano huo ulihusisha mawasilisho ya miradi kutoka kwa washiriki watatu waliowasilisha kazi walizozitekeleza baada ya kurejea nchini.



Naye Mwenyekiti wa JATA, Gregory Mlay, amesema umoja huo unawakutanisha wataalamu kutoka sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, mifugo, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), biashara na afya ili kushirikiana katika miradi ya maendeleo.

Katika hatua Nyingine, Mwakilishi Mkazi wa JICA Tanzania, Ara Hitoshi, amesema lengo kuu la mafunzo hayo ni kuchangia maendeleo ya Tanzania ili kufanikisha hilo, washiriki wanaporudi kutoka kwenye mafunzo wanapaswa kuchukua hatua za kuwasaidia wengine kwa kutumia maarifa na uzoefu walioupata.



Mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo, Godfrey Christopher, amesema wamejifunza mbinu za kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi kupitia usindikaji na uhifadhi bora, hatua inayosaidia kupunguza upotevu wa mazao na kuongeza kipato cha wananchi.










Share:

Friday, 6 March 2026

RIDHIWANI KIKWETE: TUMIENI MFUNGO KULIOMBEA TAIFA AMANI




WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amewataka wadau wa sekta ya bima na Watanzania kwa ujumla kutumia kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuliombea Taifa amani ili kuchochea kasi ya uwekezaji nchini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam katika hafla ya kufuturisha wadau wa bima iliyoandaliwa na Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC), Waziri Kikwete alisema kuwa amani ndiyo msingi mkuu unaoifanya Tanzania kuwa kitovu bora cha uwekezaji, na hivyo ni wajibu wa kila mwananchi kuitunza kupitia fursa za kiroho kama mfungo.

Alibainisha kuwa sekta ya bima ina mchango mkubwa katika kulinda uchumi wa kisasa, kwani inatoa uhakika wa usalama kwa wafanyabiashara na wawekezaji dhidi ya majanga mbalimbali.

Alisisitiza kuwa bila mfumo imara wa bima, ni vigumu kwa Taifa kupata ustawi endelevu wa kiuchumi unaohitajika na serikali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uendeshaji na Utumishi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango (SMZ), Rajab Uweje, alieleza kuwa Shirika la ZIC limekuwa likitekeleza wajibu wake kama kiungo muhimu cha mfumo wa kifedha nchini. Aliongeza kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana na wadau kubuni huduma rafiki zitakazowafikia wananchi wengi zaidi na kusaidia kukuza uchumi wa pande zote mbili za Muungano.
Share:

ACHENI HEKAHEKA ZA MTANDAONI ZENYE NIA OVU, CHANGAMKIENI FURSA





WAKATI baadhi ya vijana wakipoteza muda mwingi mitandaoni kukuza chuki, kulalamika na kushusha hadhi ya nafsi zao, Serikali imewapigia kipyenga wasomi wa vyuo vikuu kutumia akili zao kubuni miradi itakayowaingizia "mkwanja" na kuwafanya mabilionea wa kesho.

Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu, Fatma Mabrouk Khamis, wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka Afrika Mashariki na India.

 Fatma ameweka wazi kuwa Serikali ya Zanzibar Awamu ya Nane imeweka kipaumbele cha kufa mtu kwenye sayansi na teknolojia, ikilenga kuwabadilisha wasomi kutoka kuwa wasaka ajira na kuwa wabunifu wa miradi inayozalisha mali.

“Wasomi wetu, wakati wa kushinda mitandaoni bila tija umepitwa na wakati. Huu ni wakati wa kuongeza ubunifu, kubuni miradi ya uzalishaji na kuingia kwenye ujasiriamali,” alisema Fatma huku akisisitiza kuwa idadi ya wahitimu ni kubwa kuliko nafasi za serikalini, hivyo njia pekee ya ushindi ni kujiajiri kupitia sekta binafsi.

Katika kile kinachoonekana kama "mchongo" wa uhakika, Joseph Evarest kutoka Shirika la UNDP kupitia programu ya FUNGUO, amebainisha kuwa wapo tayari kuviunganisha vyuo vikuu vya Tanzania na mataifa kama India na Uingereza. Mpango huu si wa nadharia tu, bali unalenga kubadilisha mawazo ya ubunifu ya wanafunzi kuwa biashara halisi zinazopata ufadhili wa fedha, ili kijana aweze kusimama mwenyewe kiuchumi badala ya kukata tamaa.

Baadhi ya wanafunzi waliochangamkia fursa hiyo, akiwemo Kelvin Hemu (UDSM) na Happy Weston, wamethibitisha kuwa tayari wapo kwenye mchakato wa kuibua mawazo yatakayowapa fedha za kuendeleza kazi zao. 

Huu ni ujumbe tosha kwa vijana: Badala ya kutumia bando lako kusononeka na hali ya maisha, tumia ubunifu wako kufungua milango ya maendeleo, kwani amani iliyopo nchini ndiyo uwanja mpana wa wewe kujiwekea akiba na kupata tija.



Share:

Thursday, 5 March 2026

NAIBU WAZIRI WA HABARI - WAANDISHI WA HABARI WASIO NA USAJILI JAB WACHUKULIWE HATUA



Na Mwandishi Wetu.

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, ameagiza kuimarishwa kwa udhibiti wa taaluma ya uandishi wa habari nchini ili kulinda hadhi ya tasnia hiyo na kuongeza imani ya umma kwa vyombo vya habari.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati wa ziara yake katika Ofisi za Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Naibu Waziri huyo alisisitiza kuwa ni wakati wa bodi hiyo kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari kwa kuhakikisha wanaojihusisha na kazi za habari wanakuwa na ithibati halali.
Alieleza kuwa kukithiri kwa watu kufanya kazi za habari bila usajili rasmi kunachangia kushuka kwa viwango vya taaluma na kuathiri taswira ya sekta hiyo, hivyo akaitaka JAB kuongeza kasi ya usajili, utoaji wa vitambulisho vya uandishi (Press Cards) na ufuatiliaji wa mienendo ya vyombo vya habari hususan vya mtandaoni.

“Ni lazima kulinda heshima ya taaluma hii. Uandishi wa habari ni mhimili muhimu katika ujenzi wa taifa, hivyo usimamizi wake haupaswi kulegalega,” alisisitiza.
Katika taarifa yake kwa Naibu Waziri, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, alisema katika kipindi cha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa bodi hiyo, hatua kubwa zimepigwa ikiwemo uanzishaji wa mifumo ya kidijitali ya usajili wa waandishi, utoaji wa ithibati na vitambulisho rasmi, pamoja na utoaji wa elimu kwa umma kuhusu maadili ya taaluma.


Hata hivyo, alibainisha kuwa bodi hiyo inakabiliwa na changamoto kadhaa, zikiwemo uhitaji wa rasilimali zaidi na changamoto za udhibiti wa maudhui katika vyombo vya habari vya mtandaoni ambavyo vinaongezeka kwa kasi

Ziara hiyo imekuja katika kipindi ambacho sekta ya habari nchini inaendelea kukua sambamba na mabadiliko ya teknolojia ya mawasiliano, hali inayodai uwajibikaji mkubwa zaidi kwa wadau wote ili kuhakikisha taaluma ya uandishi wa habari inabaki kuwa chombo cha kuhabarisha kwa weledi, maadili na uwajibikaji
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger