Sunday, 3 May 2026

RIPOTI YA JAJI CHANDE IMETOA MWANGA MPYA WA MATUMAINI KWA WATANZANIA- DKT. NDILITO



Ripoti ya Tume iliyoongozwa na Jaji Mohamed Chande Othman ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 imeendelea kuzua mjadala mkubwa nchini, huku mchambuzi wa masuala ya uongozi, uchumi na siasa Tanzania, Dk Netho Ndilito (PhD), akiitaja kama nyaraka muhimu iliyofichua mambo makubwa matano yenye maslahi kwa taifa.

Akizungumza kuhusu ripoti hiyo, Dk Ndilito amesema baada ya kupitia maoni ya Watanzania, wanamitandao na wachambuzi mbalimbali, amebaini kuwa taarifa hiyo imeleta mwanga mpya kuhusu hali halisi ya taifa na changamoto zilizokuwa zikijadiliwa kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Dk Ndilito, jambo la kwanza ni kwamba ripoti hiyo imeliponya taifa kwa kueleza ukweli ambao kwa muda mrefu haukupata nafasi ya kujadiliwa waziwazi, ikifichuliwa pia kwa nia na dhamira ovu za baadhi ya watu waliotamani vurugu kabla, wakati na baada ya uchaguzi, jambo ambalo sasa limewekwa wazi kupitia uchunguzi huo.

Aidha, ameeleza kuwa ripoti hiyo imeweka bayana upotoshaji na taarifa zisizo sahihi zilizokuwa zikisambazwa na baadhi ya watu wasiolitakia mema taifa, huku wakitamani kuona nchi ikiingia kwenye machafuko.

Katika hoja ya nne, Dk Ndilito amesema ripoti hiyo imeonesha namna Watanzania wengi wanavyoipenda nchi yao, kuiamini serikali yao na kutokuwa tayari kushawishika kuivuruga amani, umoja na mshikamano wa taifa, huku pia ripoti hiyo ikionesha uimara wa serikali pamoja na ukomavu wa vyombo vya ulinzi na usalama katika kushughulikia masuala ya ndani kwa weledi na utulivu.

Dk Ndilito alitumia nafasi hiyo kuwapongeza Watanzania kwa kuendelea kudumisha umoja, upendo, mshikamano na amani, akisisitiza kuwa huo ndiyo utamaduni uliojenga heshima ya taifa kwa miaka mingi.

“Watanzania wameendelea kuonesha ukomavu mkubwa wa kisiasa na uzalendo. Hii ndiyo desturi yetu kama taifa,” alisema.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 3,2026


Magazeti




Share:

Saturday, 2 May 2026

UNESCO NA MAIPAC WAJA NA MWONGOZO KWA WANAHABARI NA WATENGENEZA MAUDHUI JAMII ZA PEMBEZONI



Mussa Juma mkurugenzi wa maipac Akichangia mada katika maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya Habari jijini Arusha


Dudukwe Saidi kijana maarufu wa kihadzabe akisalimia wanahabari katika Ukumbi wa Mount Meru Hotel jijini Arusha


Na Mwandishi wetu,Arusha

Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kushirikiana na Taasisi ya Wanahabari ya kusaidia jamii za pembezoni (MAIPAC) na Idara ya Habari Maelezo, wanaandaa mwongozo kwa ajili ya watengeneza maudhui katika maeneo ya jamii za pembezoni.

Mwongozo huo, unatarajiwa kuwasaidia Wanahabari na Watengeneza maudhui, kutambua maadili na miiko ya jamii za pembezoni za Wahadzabe, Masai, Datoga na Akie, kabla ya kuandika na kusambaza maudhui kuhusiana na jamii hizo.

Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya MAIPAC, Mussa Juma alitoa taarifa hiyo, jana wakati akizungumza katika mjadala wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo duniani (WPFD) jijini Arusha, kuhusiana na waandaji wa maudhui mitandaoni na matumizi ya akili Unde katika kuboresha kazi zao.

Juma alisema katika siku za karibuni wameibuka watengeneza maudhui wa ndani na nje ya nchi, Kwenda moja kwa moja katika maeneo ya jamii hizo hasa Wahadzabe na kutoa maudhui yao bila ridhaa yao na maudhui mengine ambayo ni kinyume cha maadili.

“Kutokana na changamoto hii, MAIPAC kwa kushirikiana na UNESCO na Idara ya Habari Maelezo wanaandaa mwongozo maalum wa kufanya kazi katika jamii hizi kwa kuzingatia maadili na bila kudhalilisha utu wa jamii hizi”,alisema.

Alisema sambamba na mradi huo, pia MAIPAC kwa kushirikiana na UNESCO ,Maelezo na SAVVY Media, wanatarajia kusaidia jamii hizi kujua matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii lakini pia kuanza kunufaika na matangazo na Habari ambazo zimekuwa zikitangazwa.

“Tutazijengea uwezo jamii hizi, kuweza kutumia vizuri mitandao kwa manufaa yao pia kiuchumi na kutambua haki zao mbali mbali za kidigitali na hivyo kuinua Uchumi wao”alisema


Wakizungumza katika mjadala huo, baadhi ya watengeneza Maudhui mitandaoni na Maafisa wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), walisema matumizi ya mitandao na akili unde vinapaswa kusaidia vijana na jamii badala ya kuogopwa.

Mwenyekiti wa jamii ya Wahadzabe katika eneo la bonde la Eyasi, wilaya ya Karatu, Mdindi Samboga alishukuru MAIPAC, UNESCO, Maelezo na SAVVY Media, kuja na mradi wa kuwasaidia.


Samboga alisema jamii yao imepata umaarufu mkubwa katika mitandao ya kijamii katika siku za karibuni lakini hata hivyo hainufaiki na wanaotengeneza picha na Habari.

“Wanakuja wanatupiga picha na kutuhoji tunasikia mijini tunaonekana sana lakini sisi hatunufaiki zaidi ya kupewa pombe, sasa tunaomba kusaidiwa kunufaika”alisema
Share:

Friday, 1 May 2026

RAIS SAMIA: MSIDANGANYIKE, HAKUNA USTAWI BILA AMANI NA UTULIVU WA TAIFA

  

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wafanyakazi nchini kote kudumisha amani na utulivu akisisitiza kuwa hakuna ustawi wa mfanyakazi unaoweza kupatikana bila kuwepo kwa utulivu wa taifa. 

Aidha amewataka wafanyakazi nchini kuendelea kuchapa kazi na kwamba serikali itaboresha maslahi yao kadri uchumi unavyoendelea kuimarika.

Akizungumza mkoani Njombe kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi), Rais alibainisha kuwa ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha tofauti zilizopo hazigeuki kuwa sababu ya kuhatarisha misingi ya umoja na mshikamano iliyoachwa na waasisi wa taifa.

“Sasa ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba tofauti zetu hazigeuki kuwa sababu ya kuhatarisha misingi ya amani, umoja na mshikamano tulioachiwa na waasisi wetu, tushikamaneni tufanye kazi, tujenge taifa letu na tujenge heshima ya nchi yetu,” alisema.

Alisisitiza kuwa kazi zenye staha ni nguzo imara kwa maendeleo kuelekea Dira ya Taifa 2050 na kuwataka Watanzania kushikamana katika kuijenga heshima ya nchi.

Katika hatua nyingine, Rais Samia alieleza namna Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) wakiongozwa na Rais wa Shirikisho  hilo, Tumaini Nyamhokya walivyompa pole kwenye kikao chao cha pamoja na kumtaka Rais achape kazi, wafanyakazi mwaka huu watafunga mkanda kutokana na mambo iliyopitia nchi baada ya uchaguzi.  lilivyompa pole kwa mambo mazito ambayo nchi imepitia.

“Katika kikao kile walikuja kunipa pole (Tucta)… hawakuwa na madai mapya waliniambia ‘mama wewe chapa kazi tutakuja kukudai mwakani,’ na mimi nikawaambia mwakani ikiwa tutachapa kazi na uchumi utakuwa kwa kiwango kinachoridhisha tutakuja kuangaliana”.

“Nataka niwahakikishie kwamba pamoja na changamoto zilizopo kadri uchumi unavyoendelea kuimarika tutaboresha maslahi ya wafanyakazi wetu, nawaomba tuendelee kuchapa kazi kwa bidii, weledi na uzalendo wa hali ya juu, kwa kufanya hivyo tutaendelea kukuza uchumi wa nchi yetu na kugawana vizuri ile keki ya taifa kama matunda na juhudi ya jasho letu,” alisema.

Alisema serikali ilitumia kiasi kikubwa cha fedha kwenye uchaguzi mkuu kwa vile uligharamiwa na serikali na kwa uharibifu uliotokea baada uchaguzi, kila fedha inayopatikana inatumika kwenye kurekebisha mali zilizoharibiwa na miundombinu iliyoharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha na kulipa madeni ya wafanyakazi na wakandarasi ili utakapoanza utekelezwaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 uanze kukiwa na mwelekeo mzuri unaoleweka. 

“Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kazi na maslahi ya watumishi kwa kadri uchumi utakavyoruhusu, tutaendelea kuchukua hatua zaidi za kuimarisha ustawi wa wafanyakzi na kwa hivyo ndugu zangu chapeni kazi serikali ipo inawasikiliza na inawathamani,” alisema.Licha ya kuyumba kwa uchumi duniani, Rais Samia amewahakikishia wafanyakazi kuwa serikali inathamini mchango wao na itaendelea kuboresha maslahi yao kadri hali ya kifedha itakavyotengamaa. 

Aidha Rais alieleza kwa ufupi mambo makubwa yaliyofanywa katika kipindi cha pili cha serikali ya Awamu ya Sita katika sekta ya kazi ni kutoa ajira 12,000 za ndani katika sekta ya umma ajira 12,000...“hii ni kwa ujumla mbali na ambazo zimetangazwa na watu wanaendelea kuomba,” alisema. 

“Lingine serikali imeendelea kuratibu upatikanaji wa ajira nje ya nchi na vijana wa kitanzania 7,593 tumewapatia ajira nje ya nchi, mipango ya kutafuta fursa zaidi za ajira nje ya nchi inaendelea ili kupunguza changamoto za ajira kwa vijana wetu… na katika hili nakubaliana na Tucta kwamba tunahitaji kuwa na utaratibu wa wazi na usimamizi madhubuti wa Watanzania wanaokwenda kufanya kazi nje ili kuhakikisha haki na maslahi yao yanalindwa ipasavyo,” alisema.

Aliishukuru Tucta kuanzisha kitengo maalumu cha kushughulikia masuala hayo na kuilekeza Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano kuratibu na kusimamia kikamilifu suala hilo kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na balozi.

“...kuratibu na kuharakisha…  najua kuna maombi mengi kutoa nje wanataka wafanyakazi kwa hiyo mratibu na muharakishe vijana wetu wapate kazi nje lakini msimamie maslahi yao,” alisema. 

Vilevile, Rais Dkt. Samia amesema Serikali itaendelea kuweka mkazo katika kukuza ujuzi,hususan kwa vijana, ili kuwaandaa Watanzania kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kisasa unaohitaji maarifa, teknolojia na ubunifu.

“Dhamira ya Serikali ni kuona kila mfanyakazi anafanya kazi katika mazingira salama, yenye heshima, haki na yanayomwezesha kuchangia kikamilifu katika ujenzi wa Taifa,”amesema Rais Dkt. Samia.

Kwa upande wa Waziri Mkuu Dk Mwigulu Nchemba aliyekuwepo kwenye sherehe hizo, aliwataka wafanyakazi kutokana tamaa na badala yake wawe wavumilivu wanapokuwa maeneo ya kazi.  

Akiwasilisha Risala kwa niaba ya Wafanyakazi, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Ndugu Herry Mkunda, amepongeza jitihada za Serikali katika kuboresha maslahi ya wafanyakazi, ikiwemo nyongeza ya mishahara, kuboresha mazingira ya kazi na majadiliano ya wadau wa utatu, huku akiiomba Serikali kuendelea kuimarisha hifadhi ya jamii, usalama kazini na fursa za ajira.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Sangu, amesema hatua zinazochukuliwa na Serikali imeimarisha huduma za jamii na mazingira ya uzalishaji, ikiwemo uwekezaji katika afya, elimu, miundombinu na sekta zakiuchumi zinazogusa moja kwa moja maisha ya wafanyakazi na wananchi.

Naye, Mwenyekiti wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Dkt. Oscar Mgaya, amepongeza hatua za Serikali katika kuboresha mazingira ya biashara na ajira, ikiwemo kuundwa kwaTume ya Rais ya Maboresho ya Kodi, akisema hatua hiyo itaongeza uwekezaji wa sekta binafsi na kutengeneza fursa zaidi za ajira zenye staha.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) Kanda ya Afrika Mashariki, Bi. Caroline Mugala, ameipongeza Tanzania kwa kuimarisha ajenda ya kazi zenye staha, haki za kijamii na majadiliano ya wadau wa utatu katika sekta ya kazi.

Ameongeza kuwa, ILO itaendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kazi zenye Staha, kuimarisha sheria na viwango vya kazi, kukuza ujuzi kwa vijana na wanawake, pamoja na kuimarisha mifumo salama ya ajira kwa Watanzania wanaofanya kazi nje ya nchi.









Share:

WMA YASHIRIKI MAADHINISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI MEI MOSI


Wakala wa Vipimo (WMA) imeungana na wafanyakazi kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali nchi nzima kuadhimisha siku ya Wafanyakazi Duniani.

Siku ya Wafanyakazi Duniani huadhimishwa kila Mwaka tarehe 1 Mei na kaulimbiu ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mwaka 2026 ni "Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050".

Wakala imeshiriki katika maadhimisho hayo Kitaifa Mkoani Njombe ambapo watumishi wa Mkoa huo wameongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA Bw. Alban Kihulla.

Pamoja na ushiriki wa Kitaifa kadharika, WMA imeshiriki kuadhimisha siku ya Wafanyakazi katika ngazi za Mikoa kupitia ofisi za Mikoa za Kivipimo.

Uongozi wa WMA unaendelea kuwahimiza watumishi wake kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanatoa huduma sahihi kwa wananchi kwa kusimamia matumizi sahihi ya Vipimo katika sekta mbalimbali.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 1,2026

Magazeti
 



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger