


Tuzo hiyo imetolewa kwa kutambua mchango wake mkubwa katika uongozi na juhudi zake za kuleta maendeleo chanya kwa jamii pamoja na Taifa kwa ujumla.
Kupitia nafasi mbalimbali za kiuongozi, Manumbu ameonyesha uwezo, ubunifu na dhamira ya dhati katika kutumikia nafasi yake na jamii kwa ujumla.
Akizungumzia ushindi huo, Manumbu ameeleza kuwa ni heshima kubwa kwake na kwa Tanzania kwa ujumla, akisisitiza kuwa tuzo hiyo ni motisha ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii, unyenyekevu, na uadilifu kwa manufaa ya jamii.
Hafla rasmi ya ugawaji wa tuzo hizo inatarajiwa kufanyika tarehe 28 Februari 2026 katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma, ambapo washindi kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika watatunukiwa tuzo hizo rasmi.









Kupitia mitandao ya kijamii kunasambazwa picha mjongeo akionekana mtoto mdogo wa kiume na zikisikika sauti zikimhamasisha kuvuta sigara Kitendo hicho ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za kijamii na nchi. Jeshi la Polisi, limeanza uchunguzi na kuwafuatilia watu hao kwa hatua nyingine za kisheria.
Aidha, linatoa wito kwa yeyote anayewafahamu watu hao au mtoto huyo atusaidie kuwafikia na kuokoa afya ya mtoto huyo.
Pia, linatoa onyo kwa watu wenye tabia za kufanya vitendo vya kikatili na vya unyanyasaji kama hivyo na vinavyofanana na hivyo kwa watoto kwa lengo lolote lile ikiwepo msukumo wa kutafuta wafuasi (followers) kwa ajili ya mitandao yao ya kijamii kuziacha kwani halitasita kuwakamata kwa sababu ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za nchi.