Friday 19 April 2024

WAZIRI JERRY SILAA KUONGOZA KLINIKI YA ARDHI TANGA

 

Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI wa Ardhi,Nyumba na Mendeleo ya Makazi Jerry Silaa anatarajiwa kuongoza Kliniki ya Ardhi kwa mkoa wa Tanga itakayofanyika kuanzia Aprili 22 mpaka 28 mwaka huu ikifanyika kwenye maeneo mawili Kijiji cha Miaka 21 Chumbageni Tanga na Korogwe.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kamishna Msaidizi wa Ardhi mkoa wa Tanga Tumaini Gwakisa alisema zoezi hilo litafanyika kwenye maeneo mawili ambapo litaanzia Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Tanga eneo la Kijiji cha miaka 21 Chumbageni kuanzia Aprili 22 mpaka 25 mwaka huu.

Alisema baada ya kumaliza kwa Tanga wataelekea wilayani Korogwe ambapo litafanyika kuanzia Aprili 26 mpaka 28 mwaka hu na uendeshwaji wa program hiyo utasimaiwa na itaongozwa na Waziri wa Ardhi Jerry Silaa akiwa na wataalamu wa Wizara hiyo.

“Nichukue nafasi hii kwaalika wananchi wote wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kupata huduma mbalimbali za sekta ya ardhi katika maeneo ambayo kliniki hiyo itafanyika kwani kutakuwa na utatuzi wa migogoro ya ardhi ambapo Waziri atasikiliza kero mbalimbali za Migogoro hiyo”Alisema

Alisema pia kutakuwa na utolewaji wa elimu kuhusu usimamizi wa ardhi pamoja na uwepo wa kituo jumuishi kitakachotoa huduma ya kupokea maoni mbalimbali na utoaji hati miliki ,ukadiriaji wa kodi ya ardhi na ulipaji wa kodi ya ardhi.

Gwakisa aliwataka wananchi wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kushiriki ambapo Waziri atakuwepo na wataalamu kutoka Wizarani
Share:

Thursday 18 April 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 19, 2024


Share:

FCT YASIKILIZA NA KUTOLEA MAAMUZI MASHAURI 429




Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Daniel Machunda, akizungumza wakati wa semina ya siku moja kwa wadau mbalimbali iliofanyika mkoani 

Kaimu Msajili na Mkuu wa FCT, Kunda Mkenda, akizungumza wakati wa semina ya siku moja kwa wadau mbalimbali iliofanyika mkoani Mwanza.


Baadhi ya washiriki wakimsikiliza Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Daniel Machunda,(hayupo pichani )wakati wa semina ya siku moja kwa wadau mbalimbali iliofanyika mkoani Mwanza


Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Daniel Machunda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungu semina ya siku moja kwa wadau mbalimbali iliofanyika mkoani Mwanza



Na.Mwandishi wetu_MWANZA

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Daniel Machunda amewaomba wadau wote kuendeleza ushirikiano na Baraza la Ushindani ( FCT) katika kuongeza uzoefu, ufanisi katika majukumu mbalimbali.

Hayo ameyasema wakati akifunga semina hiyo Aprili 15 2024 Mkoa wa Mwanza, Machunda, amesema semina hiyo ni muhimu hivyo elimu walioipata itawasaidia kutambua haki na kujua wajibu wao

Amesema ili kusimamisha ushindani wa haki na kumlinda mlaji kwani Sheria zinataka kuwepo na ushindani wa haki na kumlinda mlaji.

"Wadau wamepata fursa ya kutoa ushauri kuboresha mawasiliano na Baraza hili katika masuala mbalimbali na leo ni sehemu ya wao kutatua changamoto mbalimbali za ushindani wa biashara na udhibiti wa soko,"amesema Machunda.

Aidha ametoa shukurani kwa baraza hilo na Wizara ya Viwanda na Biashara kufanya semina mkoani humo na kuwapatia elimu wadau.

Akizungumza Kaimu Msajili na Mkuu wa FCT, Kunda Mkenda wakati wa semina ya siku moja kwa wadau mbalimbali iliofanyika mkoani Mwanza amesema Baraza limesajili jumla ya mashauri 442 kati ya hayo 429 yameishwa sikilizwa na kutolewa maamuzi na baraza hilo katika kipindi cha mwaka 2007 hadi Machi 2024.

Amesema Baraza limefanikiwa kushughulikia mashauri yalioletwa mbele yake kwa asilimia 97.1 huku mashauri 13 yaliobaki yapo kwenye hatua mbalimbali za usikilizwaji.

"Baraza hili limeanzishwa chini ya kifungu cha 83(1), cha Sheria ya Ushindani Na.8 ya mwaka 2003 inayolenga kukuza na kulinda ushindani wa kibiashara na kumlinda mlaji dhidi ya matokeo ya ukiritimba na tabia potofu katika soko,"amesema Mkenda.

Amesema kutokana na changamoto zilizojitokeza za watu wengi kutolijua baraza hilo kwa mara ya kwanza wameamua kufanya semina hiyo kwa wadau mbalimbali mkoani humo ili waweze kujua haki zao, umuhimu wa baraza na kazi zake.

Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa semina hiyo akiwemo Zahara Magambo, ameeleza kuwa kupitia semina hiyo ameweza kufahamu sehemu ya kupata haki zake endapo atakuwa ajaridhishwa na maamuzi yaliotolewa aidha na Tume ya Ushindani(FCC), EWURA, TCRA, TCAA, LATRA na PURA.

"Sijawai kupata changamoto lakini semina hii imenifumbua macho ikitokea nikipata changamoto najua naanzia wapi," ameeleza Zahara.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa wajasiriamali wabunifu Tanzania,Fabiani Semba ameeleza kuwa kupitia semina hiyo ameweza kufahamu wapi pa kwenda kwani katika sekta ya mawasiliano kumekuwa na mambo mengi yakitokea huku wakiwa hawajui wapi pa kwenda kutoa malalamiko.

"Niko tayari kutumia Baraza kama sehemu ya kupata msaada na suluhisho kwani itasaidia kukua kiuchumi hivyo elimu iendelee kutolewa kwa wananchi ili kulifahamu Baraza hilo na kazi zake na kutofautisha na Tume ya Ushindani ili waweze kupata haki zao,"amesema.

Naye Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo(TCCIA),Mkoa wa Mwanza Gabriel Kenene, ameeleza kuwa amejifunza namna ambavyo rufaa zinavyopatikana na kutolewa.

"Nimejifunza kwamba mamlaka hizi za udhibiti ikiwemo EWURA pale inapotokea mtu hajaelewa au utata umetolewa aende wapi,kumbe kuna chombo ambacho unaweza kukata rufaa na kinaondoa utata huo,kinachofurahisha rufaa zinachukua muda mfupi kwani wafanyabiashara hawapendi usumbufu wa kitu kinachochukua muda mrefu hivyo anaona ni bora haki yake ipotee kwa sababu ya muda.

"Nitoe wito kwa wafanyabiashara wanapoona hawajatendewa haki na mamlaka hizi kama LATRA ni vizuri wakafuate haki yao kupitia Baraza hilo kwani gharama zao ni ndogo, nitakuwa balozi kwa kuhakikisha elimu hii nitaipelekwa kwa wadau ambao wanaweza kukutana na kadhia," amefafanua.
Share:

EWURA YATAMBULISHA MFUMO WA MAJIS ULIOBORESHWA




Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Mha.Poline Msuya akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Mamlaka za maji kuhusu mfumo wa kieletroni wa MajIs ulioboreshwa kwa ajili ya kupokea taarifa za utendaji wa sekta ya maji, kilichofanyika EWURA Makao Makuu, Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu_DODOMA

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji EWURA imefanya kikaokazi cha kutambulisha mfumo wa Majis ulioboreshwa kwa ajili ya ukusanyaji wa taarifa kwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira. Kikao hicho kimefanyia EWURA makao makuu Dodoma.

Akifungua kikao hicho kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Mha. Poline Msuya amesema Maboresho yaliyofanyika katika mfumo yalichagizwa pia na maoni ya wadau ambao ni watumiaji wa mfumo. Pia mfumo umeboreshwa kuakisi mabadiliko na maendeleo kwenye sekta ya maji.

Aidha EWURA haitosita kuchukua hatua za kiutawala kwa mamlaka za maji ambazo hazitatekeleza uwasilishaji wa taarifa zao kwa wakati, aliongezea Mha. Poline Msuya.

Akitoa maoni yake muwakilishi wa Wizara ya Maji Mha. Epimack Oscar alisisitiza Mamlaka za Maji zitumie mfumo huo kwa ajili ya kuwa na takwimu sahihi.

Kifungu cha 29(1)(h) cha Sheria ya Maji na Usafi wa Mazingira Sura Namba 272 kinaitaka EWURA kukusanya taarifa za utendaji kutoka mamlaka.


Meneja wa EWURA kanda ya Magharibi Mha. Walter Christopher akiwasilisha mada kuhusu mfumo wa Majis ulioboreshwa kwa ajili ya ukusanyaji wa taarifa kwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira kwenye kikaokazi cha kutambulisha mfumo huo. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano EWURA makao makuu Dodoma.


Mhandisi Mwandamizi wa Maji na Usafi wa Mazingira EWURA, Teophil Sanjawa akiwaelekeza washiriki wa kikaokazi namna ya kujaza taarifa kwenye mfumo wa MajIs ulioboreshwa, leo 17.4.24


Washiriki wa kikao kazi wakifuatilia kwa umakini namna ya kujaza taarifa za utendaji wa mamlaka za majisafi na usafi wa mazingira kwenye mfumo wa MajIs ulioboreshwa.


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Mha. Poline Msuya(katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi watendaji wa Mamlaka za maji za makao makuu ya mikoa na miradi ya kitaifa,wawakilishi kutoka Wizara ya maji na wafanyakazi wa EWURA idara ya Maji muda mfupi baada ya ufunguzi wa kikaokazi cha utambulisho wa mfumo wa Majis ulioboreshwa kwa ajili ya ukusanyaji wa taarifa kwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira,Dodoma.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI APRILI 17,2024






 













Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger