Na Sheila Ahmadi, Ruangwa
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Ruangwa, Kasper Mmuya, amesema Mkoa wa Lindi una fursa kubwa za madini ambazo zinahitaji kufanyiwa utafiti na kutangazwa zaidi ili kuvutia wawekezaji na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa mkoa na Taifa.
Mmuya amesema hayo wakati akizungumza katika Maonyesho ya Madini ya Mkoa wa Lindi yanayofanyika Wilaya ya Ruangwa, akieleza kuwa maonyesho hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kuibua na kutangaza fursa za madini zilizopo mkoani humo.
maonyesho hayo ya siku nne yamehusisha shughuli mbalimbali, ikiwemo ufunguzi, ziara za mabanda, mafunzo kwa wananchi na wadau wa sekta ya madini pamoja na siku ya kilele na kufungwa kwa maonyesho.
Aidha Mmuya amesema wazo la kuanzisha maonyesho hayo lililenga kuonyesha na kutangaza fursa za madini zinazopatikana Lindi ndani ya mkoa, nje ya mkoa na hata nje ya Tanzania.
" juhudi hizo zimeanza kuonyesha matokeo kutokana na kuongezeka kwa wadau wa sekta ya madini wanaofika mkoani humo na kuanza kufanya shughuli mbalimbali" Amesema Mbunge Mmuya
Vilevile Lengo lake lilikuwa ni kuonyesha fursa za madini zinazopatikana katika Mkoa wa Lindi na kuzitangaza ndani ya mkoa, nje ya mkoa na hata nje ya nchi yetu,” amesema Mmuya.
Katika hatua nyingine Lindi haipaswi kutegemea kilimo, uvuvi na ufugaji pekee katika kukuza uchumi wake, bali inapaswa kutumia kikamilifu fursa zinazopatikana katika sekta ya madini.
Hata hivyo mafunzo yaliyotolewa katika maonyesho hayo yamekuwa muhimu kwa wananchi, wachimbaji wadogo na wakubwa pamoja na wawekezaji, kwa kuwa yameeleza namna teknolojia inavyoweza kutumika katika uchimbaji, uchakataji na uongezaji thamani wa madini.
Naye Naibu Waziri wa Madini, Steven Kiruswa, ameongeza kuwa Serikali imeanza kuchukua hatua dhidi ya wamiliki wa maeneo ya utafiti wa madini ambao hawayaendelezi.
Kiruswa amesema katika Mkoa wa Lindi pekee, Serikali ilifuta leseni 98 mwaka uliopita na imefuta nyingine 100 mwaka huu, hatua inayolenga kuachilia maeneo ambayo hayajaendelezwa ili kutoa nafasi kwa wachimbaji na wawekezaji wenye nia ya dhati.
Vilevile Serikali sasa inachambua maeneo hayo ili kubaini kiwango cha utafiti kilichofanyika, huku maeneo ambayo hayajafanyiwa utafiti yakitarajiwa kuingizwa katika mpango wa utafiti wa Serikali.



Magazeti












