Sunday, 19 July 2026

MASAUNI: UHIFADHI WA UDONGO NI MSINGI WA MAENDELEO ENDELEVU

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, akizungumza na wadau mbalimbali wa mazingira kabla ya kushiriki matembezi yaliyolenga kuhamashisha jamii katika Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira yaliyofanyika Julai 19, 2026 jijini Dar es Salaam.

*************

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaendelea kuimarisha juhudi za kuhakikisha kuwa masuala ya uendelevu wa mazingira yanapewa kipaumbele katika ajenda ya maendeleo ya Taifa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, aliposhiriki matembezi yaliyolenga kuhamashisha jamii katika Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira ‘Save Soil Walkathon’ yaliyofanyika Julai 19, 2026 jijini Dar es Salaam.

Mhe Masauni amesema, ahadi hii inaonyeshwa wazi katika Dira ya Maendeleo ya Tanzania ya 2050, haswa nguzo yake ya Tatu, ambayo inatambua uendelevu wa mazingira na ustahimilivu wa hali ya hewa kama misingi muhimu wa kufikia mabadiliko ya kiuchumi jumuishi ya kijani kibichi na endelevu.

Ameongeza kuwa afya ya udongo ni msingi wa usalama wa chakula, uhifadhi wa mazingira na ustawi wa uchumi wa taifa, hivyo kuna umuhimu wa kila Mtanzania kushiriki katika juhudi za kuutunza.

"Udongo ni rasilimali muhimu inayobeba maisha yetu ya kila siku. Bila udongo wenye afya hatuwezi kuwa na usalama wa chakula, mazingira bora wala maendeleo endelevu. Ni wajibu wa kila Mtanzania kushiriki katika juhudi za kulinda mazingira na kutumia ardhi kwa njia zinazohifadhi uhai wake kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho," amesema Mhe. Masauni.

“Tunapoanza kutekeleza Mpango huu wenye kuleta mabadiliko makubwa, tunaona fursa nyingi za kuimarisha ushirikiano wetu na Jamhuri ya India. Tunatarajia kuendeleza ushirikiano katika nyanja mbalimbali kama vile uhamishaji wa teknolojia, utafiti na uvumbuzi, ujenzi wa uwezo, urejeshaji endelevu wa ardhi, ufuatiliaji wa mazingira, uwekezaji rafiki kwa mazingira na suluhisho zinazozingatia kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.” Amesisitiza Mhe. Masauni.

Kwa upande wake, Rais wa Lions Club of Dar es Salaam Mazingira, Bi. Lion Ramadevi, amesema ‘Save Soil Walkathon’ ni sehemu ya kampeni pana inayolenga kuhamasisha jamii kutambua mchango mkubwa wa udongo katika maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.

"Save Soil Walkathon si matembezi pekee, bali ni harakati ya kuhamasisha mabadiliko ya tabia na kuwajengea wananchi uelewa wa umuhimu wa kulinda udongo. Tunataka kuona jamii, taasisi na sekta binafsi zikichukua hatua za pamoja katika kuhifadhi mazingira kwa mustakabali wa taifa letu," alisema Lion Ramadevi.

Naye Balozi wa India nchini Tanzania Mhe. Lakshay Anand amesema ni jambo jema kuona jamii inatambua umuhimu wa kulinda mazingira na huo ndio msingi wa Maisha ya binadamu ya kuhakikisha kila mmoja anakua sehemu ya kutunza mazingira.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, akizungumza na wadau mbalimbali wa mazingira alipowasili eneo la Swami Vivekananda Culture Centre jijini Dar es Salaam kushiriki matembezi yaliyolenga kuhamashisha jamii katika Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira yaliyofanyika Julai 19, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, akimwakilia maji mti mara baada ya kuupanda ikiwa ni ishara ya kuunga mkono juhudi za utunzaji wa mazingira, wakati aliposhiriki matembezi yaliyolenga kuhamashisha jamii katika Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira yaliyofanyika Julai 19, 2026 jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, akipanda mti ikiwa ni ishara ya kuunga mkono juhudi za utunzaji wa mazingira, wakati aliposhiriki matembezi yaliyolenga kuhamashisha jamii katika Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira iliyofanyika Julai 19, 2026 jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (katikati), akishiriki matembezi yaliyolenga kuhamashisha jamii katika Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira yaliyofanyika Julai 19, 2026 jijini Dar es Salaam.
Share:

KATAMBI: SERIKALI HAITAVUMILIA WANAOTUMIA HAKI ZA BINADAMU KAMA KIVULI CHA KUVURUGA AMANI



Na Mwandishi Wetu, Shinyanga

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amesema Serikali haitaruhusu kundi la watu wachache kutumia hoja za haki za binadamu na demokrasia kama kivuli cha kuvuruga amani na utulivu wa Tanzania, akisisitiza kuwa yuko tayari kufika mahakamani wakati wowote endapo ataitwa.

Katambi amesema kauli na vitendo vinavyochochea chuki, vurugu na machafuko haviwezi kuvumiliwa, huku akieleza kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wanaendelea kuishi katika mazingira ya amani na usalama.

Akizungumza nyakati tofauti na makundi ya walinzi wa amani katika jamii, Polisi Jamii, Sungusungu, wazee, wenyeviti wa mitaa, mabalozi na viongozi wa vitongoji mjini Shinyanga, Waziri huyo alisema wanaomtishia kumpeleka mahakamani wanafanya hivyo kutokana na kushindwa kufanikisha ajenda zao za kuhamasisha maandamano.

Katambi alisema kupotea kwa amani kuna madhara makubwa kwa uchumi wa nchi, ikiwemo kupungua kwa watalii, kukimbia kwa wawekezaji, kusimama kwa miradi ya maendeleo na kudhoofika kwa mahusiano ya kidiplomasia.

"Wanajua wakiichafua Tanzania yetu na amani ikapotea tutapoteza mvuto kwa watalii, nchi inaweza kuwekewa vikwazo, miradi mikubwa ya maendeleo itasimama, wawekezaji wataondoka na mapato muhimu ya taifa yataathirika," alisema Katambi.

Aidha, alihoji kwa nini wanaojinasibu kutetea haki za binadamu hawajawahi kukemea hadharani vitendo vya uchomaji wa shule, vituo vya mafuta, ofisi za Serikali, biashara za watu binafsi pamoja na mashambulizi dhidi ya vituo vya polisi.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, machafuko yanapoibuka waathirika wakubwa huwa ni wananchi wa kawaida, hususan wanawake, watoto, wazee na watu wenye ulemavu.

"Watoto wao na familia zao wako nje ya nchi, lakini machafuko yakitokea ni wananchi wa kawaida watakaobeba mzigo wake. Tanzania ndiyo nchi yetu pekee na hatuwezi kukubali ifikie hatua ya wananchi wake kuwa wakimbizi," alisema.

Katambi alitolea mfano baadhi ya nchi za ukanda wa Afrika zilizowahi kukumbwa na migogoro, akisema Tanzania imekuwa ikiwahifadhi wakimbizi kwa miaka mingi, hivyo hakuna sababu ya kuruhusu mazingira yanayoweza kuisukuma nchi katika hali kama hiyo.

Kuhusu madai ya kuvunja Katiba, Waziri huyo alisema Mahakama ndiyo chombo pekee chenye mamlaka ya kutoa uamuzi kuhusu tafsiri na uvunjifu wa Katiba, na si watu binafsi au taasisi nyingine.

Alisema hadi sasa hajapokea wito wowote wa kwenda mahakamani, lakini akisisitiza kuwa yuko tayari kuitikia wito huo wakati wowote, hata usiku wa manane, kwa kuwa anaamini katika utawala wa sheria na kuheshimu mamlaka ya Mahakama.

Katambi alihitimisha kwa kuwataka Watanzania kuendelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kulinda amani, akisisitiza kuwa utulivu wa nchi ndiyo msingi wa maendeleo, uwekezaji na ustawi wa wananchi.
Share:

Saturday, 18 July 2026

SERIKALI IMEWEKEZA BILIONI 2.8 KUBORESHA AFYA, BARABARA, ELIMU YA AMALI GAIRO - PROF. SHEMDOE


Uwekezaji huo ni sehemu ya zaidi ya Shilingi Bilioni 100 zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita katika wilaya hiyo

Na. OWM–TAMISEMI, Gairo

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza Shilingi bilioni 2.8 katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Kituo cha Afya Chanjale, Barabara ya Confort Pub–Magoweko na Shule ya Amali Kwipipa, hatua iliyoboresha upatikanaji wa huduma za afya, kurahisisha usafiri na usafirishaji pamoja na kupanua fursa za elimu ya amali kwa wananchi wa wilaya ya Gairo.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Julai 17, 2026 katika kijiji cha Kwipipa, kata ya Rubeho, wilaya ya Gairo, baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma.

Prof. Shemdoe amesema miradi hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na maeneo wanayoishi kupitia uwekezaji unaogusa maisha yao ya kila siku.

"Leo nimekagua miradi mitatu muhimu. Mradi wa Kituo cha Afya Chanjale wenye thamani ya Shilingi Milioni 680, Barabara ya Confort Pub–Magoweko yenye thamani ya Shilingi Milioni 470 na Shule ya Amali Kwipipa yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.6.  Miradi hii ni matokeo ya fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kuboresha maisha ya wananchi," amesema Prof. Shemdoe.

Akizungumzia Shule ya Amali Kwipipa, Prof. Shemdoe amesema shule hiyo imebobea katika mafunzo ya uhandisi na itakuwa chachu ya kuandaa wataalamu wenye ujuzi watakaoshiriki katika ujenzi wa taifa na maendeleo ya sekta mbalimbali za uzalishaji na amewataka wanafunzi wa shule hiyo kuitunza miundombinu yake ili idumu kwa muda mrefu na kuendelea kunufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.

Prof. Shemdoe ameainisha kuwa, uwekezaji huo ni sehemu ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita, akieleza kuwa tangu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aingie madarakani, Halmashauri ya Wilaya ya Gairo imepokea zaidi ya Shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Gairo, Mhe. Ahmed Shabiby, amewapongeza wananchi wa kijiji cha Kwipipa kwa kujitolea eneo lililowezesha ujenzi wa shule ya Amali, yenye manufaa kwa wananchi wa Gairo na taifa kwa ujumla, Aidha ameipongeza TAMISEMI kwa kutenga bajeti ya chakula kwa wanafunzi wa shule hiyo, hatua itakayochangia kuboresha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia.

Naye, Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Josephine Kapoma, amesema Shule ya Amali Kwipipa itasaidia taifa kupata wahandisi wazawa wenye ujuzi na tija kwa taifa, hivyo amemuomba Prof. Shemdoe amfikishie salamu Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa wananchi wa Kwipipa wameipokea shule hiyo kwa furaha kutokana na mchango wake katika kuinua elimu ya ufundi nchini.











Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 18,2026 Friday, July 17, 2026


Magazetini Leo





















Share:

Friday, 17 July 2026

How SportPesa Tanzania’s SP Score is changing the way fans follow every match

 

A game of football can change in a heartbeat. One side goes quiet as a late goal is scored and the other goes crazy celebrating. A red card, a missed penalty or a sudden comeback can turn a regular fixture into a story that fans talk about long after the final whistle.


Today, Tanzanian football fans follow the game with the same intensity every day. They want team news before kick-off, live updates during the game and clear results after. SportPesa Tanzania is responding to that demand with the SP Score app, a fast, all-in-one sports companion that brings live scores, fixtures, lineups, stats, match updates and sports news right at fans’ fingertips.

A matchday companion for today’s fans

SP Score gives fans instant access to match information across major sports and competitions. Football fans can follow competitions such as the Tanzania Premier League, the English Premier League and the UEFA Champions League, alongside other major leagues and tournaments. The app lets users follow live scores, fixtures, lineups, results, and match stats, all in one place, eliminating the need to search across multiple platforms.

Tanzanian fans follow football with passion and focus. They want to know who starts, who scores, who gets booked, and how the match shifts after every substitution. Through the SP Score app, SportPesa offers these fans a clearer, more connected way to stay engaged with the game.

“SP Score is about bringing the matchday experience closer to the fans. Whether someone is checking team news before kickoff, following a live score during the game or reviewing the result after full time, the app helps them stay connected to the sports they love” said SportPesa Tanzania Head of Marketing Tracy Humplick.

Live scores that keep fans in the moment

A goal can change a match in seconds. A red card can shift the pressure. A late substitution can turn a close game into a story fans remember. SP Score helps fans follow those moments as they happen.

Get live football scores, match events, results, and updates across leagues and tournaments around the world. Fans can follow their favorite teams, check key match moments, and stay informed even when they cannot watch the game live. That access makes SP Score useful for fans at work, on the road, at home, or in a crowded viewing space.

Stats that help fans understand the game

Today’s fans want more than the final score. They want to understand why a team won, how a player performed, and what changed the match. SP Score supports that habit with useful match statistics and game details.

The app gives fans access to lineups, formations, match stats, and team information. It helps supporters read the game with more context. A fan can follow possession, goals, cards, substitutions, and other key details while the match unfolds.

Built for more than football

Football sits at the heart of many Tanzanian sports conversations, but fans also follow other major sports. SP Score provides updates across football, basketball and tennis, giving users one place to follow scores, fixtures, results and key match information. The platform also plans to introduce cricket and rugby coverage, which will give fans access to an even wider range of sports.

This wider coverage makes SP Score a useful sports results app for daily sports followers. A fan can follow football in the evening, tennis during a major tournament, and basketball when the playoffs heat up. SportPesa Tanzania gives those fans one platform that supports their wider sports interests.

Why SP Score matters during major tournaments

The demand for quick, easy, and precise match updates rises during major competitions. When a goal, red card, comeback, or late equalizer changes the course of a game, fans don't want to wait for delayed scores or search through numerous pages. As the action takes place, SP Score provides users with a single, easy-to-use platform to track fixtures, results, lineups, statistics, and match news.

Every World Cup game has the potential to alter group standings, momentum, or a knockout path. With the speed and context that fans now expect, SP Score enables fans to follow teams from the first games to the championship game. The app makes every phone feel like a matchday screen. SportPesa Tanzania is moving closer to fans by giving them the information they need before, during and after every match.

Turning sports interest into daily fan engagement

The app gives SportPesa a daily role in the life of sports fans, even before a bet is placed. The app delivers value before the match starts, during the action, and after the final result. It helps fans follow sports with greater focus, better context, and faster access to the information they need.

Its impact goes beyond live scores. SP Score keeps fans coming back whenever they want fixtures, lineups, results, stats, or match updates. By supporting fans even before they decide to place a bet, the app builds trusted reliability and makes SportPesa Tanzania an essential part of the full matchday routine.

Conclusion

SportPesa Tanzania’s SP Score gives fans more than just live scores. The app allows you to follow the matches faster, get the key moments and stay connected to football, basketball and tennis. Fans can download SP Score from Apple App Store or Google Play Store. Fans can visit the official SP Score website to find out more and start following their favourite teams and competitions.


Share:

SERIKALI YASISITIZA UKUZAJI TIJA KATIKA SEKTA YA UMMA



Na: OWM (KAM), Dodoma

Watumishi wa umma vijana na wanawake katika wizara na taasisi wamepatiwa mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo katika kukuza tija na kuimarisha utendaji kazi kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utoaji huduma bora na kuchochea maendeleo .

Mafunzo hayo yametolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Korea Kusini (KOICA) jijini Dodoma 16 Julai 2026 ambapo watumishi vijana na wanawake kutoka Ofisi ya Rais Utumishi na Maendeleo ya Vijana pamoja na wanufaika wa programu za KOICA (Almni)

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi Bi. Alana Nchimbi aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Bi.Mary Maganga amesema vijana na wanawake wana mchango mkubwa katika ukuzaji tija kwenye utumishi wa umma.

Bi. Alana aliongeza kusema vijana na wanawake ni sehemu muhimu ya nguvu kazi na kwa kuwa wana uwezo mkubwa wa kuchangia ukuaji wa tija, kuongeza ufanisi na kuboresha utendaji wa sekta ya umma huku ikihakikisha vikwazo vya kiutendaji vinaondolewa

“Yatupasa kwa pamoja kuongeza jitihada za kuondoa vikwazo kwa vijana na wanawake, hivyo Ofisi ya Waziri Mkuu itaendela kushirikiana na Korea Kusini kutoa nafasi za mafunzo ya kuongeza tija kwa watumishi wa umma ili wananchi wapate huduma bora” alisisitiza Bi.Alana.

Kwa upande wake Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania Mheshimiwa Eunju Ahn amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Korea kupitia Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali ya Tanzania katika kuimarisha uwezo wa sekta ya umma kwa kutoa programu za mafunzo kwa vijana na wanawake.

Balozi Ahn aliongeza kusema watanzani wengi wameendelea kufadhiliwa kushiriki mafunzo ya aina mbalimbali nchini Korea Kusini ambayo yamewajengea ujuzi na maarifa ya kukuza tija kwenye utumishi wa umma.

Katika hatua nyingine Balozi huyo aliwapongeza wanufaika wa programu za mafunzo za KOICA kwa kuandaa mafunzo haya nchini Tanzania hatua inayoonesha kwa dhati kukuwa kwa uhusiano baina ya nchi hizi mbili.

Naye mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo ambaye pia ni Mhadhiri Msaidizi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini (IRDP) Dominic Joseph amesema mafunzo hayo yamelenga la kubadilishana uzoefu na kujengeana uwezo wa kukuza tija kwenye utekelezaji wa maeneo yao ya kazi kufuatia mafunzo waliyoyapata nchini Korea Kusini kwa miaka tofauti tofauti.

Kadhalika aliongeza kusema mafunzo hayo yanatarajiwa kuwa chachu ya mabadiliko kwa washiriki waliopata mafunzo kwa kuwapa maarifa na mbinu zitakazowawezesha kuhamasisha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya sekta ya umma na kuongeza mchango wao katika maendeleo ya taifa.





Share:

WAZEE WA KIMILA TARIME WAMWOMBA RAIS SAMIA AMFIKIRIE LISSU, WASISITIZA KULINDWA KWA AMANI



Na Mwandishi wetu, Mara

Wazee wa kimila kutoka koo 12 za Wilaya ya Tarime, mkoani Mara, wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutumia falsafa yake ya 4R (Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi na Kujenga Upya) kumfikiria na kumuachia huru Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, huku wakisisitiza umuhimu wa kulinda amani kwa maslahi ya ustawi na maendeleo ya Tanzania.

Wito huo umetolewa leo Alhamisi Julai 16, 2026, wakati wazee hao walipozungumza na waandishi wa habari ambapo kwa niaba ya Koo ya Nyabasi, Mzee Moris Mung'osi amesema wanaamini Lissu amekaa mahabusu kwa muda mrefu na huenda amejifunza kutokana na yaliyotokea, hivyo akamuomba Rais Samia amfikirie kupitia sera yake ya maridhiano.

"Tunamuomba Rais Samia Suluhu Hassan kupitia falsafa yake ya maridhiano (4R) amfikirie Tundu Lissu ambaye amekaa ndani muda mrefu na huenda amejifunza na kubadili tabia yake ya kutotambua viongozi walioko madarakani. Aachiwe huru." Amesema Mung'osi.

Kwa upande wake, Mzee wa Koo ya Bumera, Joseph Maricha, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kudumisha amani nchini na kuwataka vijana kutokubali kushawishiwa kujiingiza katika vitendo vya uvunjifu wa amani, akibainisha kuwa matukio yaliyotokea Oktoba 29, 2025 yalichangiwa na ushawishi wa watu wasiopenda utulivu wa nchi.

Naye Mzee Charles Mwita Mugogo wa Koo ya Bukimbaru amempongeza Rais Samia kwa juhudi zake za kuleta maendeleo nchini, akisema mazingira ya amani ndiyo msingi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akiwataka wananchi, hususan vijana, kuwakataa wanasiasa wanaohamasisha vurugu na vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa taifa.

Wazee hao walihitimisha kwa kusisitiza kuwa taasisi za kimila zina wajibu wa kuendelea kuhamasisha umoja, mshikamano na amani, huku zikihimiza vijana kushiriki katika shughuli za maendeleo badala ya kujiingiza katika vitendo vinavyoweza kuvuruga utulivu wa nchi.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JULAI 17, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger