














KATIKA kipindi hiki ambacho Tanzania inaweka msisitizo wa kipekee kwenye Amani, Upendo, na Maridhiano ya Kitaifa, imebainika kuwa utulivu huo ndio rasilimali namba moja inayoiwezesha Serikali kupitia taasisi zake kama Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Bila mshikamano wa kitaifa, juhudi za kutengeneza mazingira rafiki ya ajira na ujasiriamali kwa vijana haziwezi kuzaa matunda ya kudumu.
Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi mahiri wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeweka kipaumbele cha dhati katika kulinda tunu hizi za Taifa ili kutoa nafasi kwa mashirika kama SIDO kuwafikia vijana na "nyenzo" za kisasa za uzalishaji mali. Hii ni dhihirisho kuwa amani si hali tu ya kutokuwepo kwa fujo, bali ni mazingira wezesha yanayomfanya kijana awe na utulivu wa kubuni, kuzalisha, na kujiajiri.
SIDO na Silaha ya Ubunifu: Kijana Jitambue!
Katika kukabiliana na changamoto ya ajira, SIDO imejipambanua kama kimbilio la vijana wanaotaka kuandika historia mpya ya kiuchumi. Shirika hilo limebeba jukumu la kukuza ubunifu, likiwapatia vijana mbinu za kisasa za utengenezaji bidhaa zinazoweza kushindana ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.
Mhadhiri na wataalamu wa maendeleo wanasisitiza kuwa kijana mwenye shughuli ya kufanya na kipato cha uhakika ndiye mlinzi mkuu wa amani ya nchi. Kupitia programu za SIDO, vijana wanahamasishwa kuacha utamaduni wa kusubiri ajira za "kuchongwa" na badala yake waingie mitaani kwa hekaheka za uzalishaji zinazochochea utulivu wa kijamii.
Maridhiano ya Kitaifa: Msingi wa Masoko na Uzalishaji
Ushirikiano uliopo sasa kati ya Serikali na wadau mbalimbali umefungua milango ya masoko kwa bidhaa za vijana. SIDO haishii tu kumpa kijana mashine au utaalamu, bali inamsaidia kupata soko—jambo linalowezekana tu ikiwa kuna mshikamano na umoja wa kitaifa. Taasisi mbalimbali zimeunganishwa ili kuhakikisha elimu ya ujasiriamali inawafikia vijana wengi zaidi, ikijenga jamii yenye watu wanaojitegemea na wanaoheshimu tunu za amani na upendo.
Wito wa Uzalendo: Thamani ya Bidhaa na Taifa
Vijana nchini waaswa kuwa mzalendo si tu kulinda mipaka, bali ni pamoja na kuongeza thamani ya bidhaa za kitanzania. Kupitia elimu ya SIDO, vijana wanapata uwezo wa kuboresha ubora wa kazi zao, jambo ambalo ni chachu ya kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
Tunapozungumzia maridhiano na umoja wa kitaifa, tunazungumzia pia haki ya kijana kupata fursa. SIDO imetoa rungu hilo kwa vijana; ni wakati wao sasa kulitumia kwa bidii, ubunifu, na uzalendo ili kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa kisiwa cha amani chenye neema ya kiuchumi kwa kila mwananchi.

Akizungumza Dar es Salaam Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo nchini, Dkt. Sajad Habib Rai amesema wao kama Kampuni ya kwanza nchini kutoa mapendekezo ya kuanzishwa kwa mfumo huo kwa EWURA na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) na baadae kuanzishwa rasmi na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), wanajivunia kuona umetekelezwa kwa kuwa dhamira yao ilikuwa kuona huduma ya usambazaji wa mafuta nchini na nje ya nchi unaleta tija kwa Taifa.
"Tumefurahi kuona TRA wameusimamia kikamilifu mfumo huu kwa kuwa unazuia ukwepaji kodi ambao hapo awali ulikuwa ukifanywa na wafanyabiashara, hivi sasa TRA inapata kodi yake mapema kabla ya kuyaingiza mafuta sokoni" amesema Dk Sajad ambaye pia ni Meneja MKAZI wa 'Mansoor Industry Limited'.

Hivi karibuni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitangaza rasmi kuanza kutumika kwa mfumo huo ambao kwa kiasi kikubwa unalezwa kuleta tija kwa Serikali kwa kuwa umesaidia kudhibiti upotevu wa mapato unaotakana na Kodi za uingizaji wa mafuta hayo nchini.
Kupitia mfumo huo mpya na wa kisasa, kila mwagizaji au muingizaji wa mafuta atalazimika kutaja kiasi cha mafuta alichokiingiza nchini ambapo kupitia Shirika la Viwango Tanzania (TBS) watayataweka vinasaba kama alama ya kila mwagizaji kwa lengo la kuwatambua wahusika wote na kiasi alichoagiza ili kuwakadiria viwango vya Kodi wanavyopaswa kulipa.
"Nawapongeza TRA kwa kuona tija na umuhimu wa kuutumia mfumo huu, sisi kama wafanyabiashara tunaozingatia taratibu halali za uingizaji na Usambazaji wa mafuta tunaiona kuwa hatua hii ni kubwa na inayostahili kupongezwa kwa kuwa italeletea manufaa Taifa", ameongeza Dkt. Sajad.
Utaratibu huo wa kikodi unawataka wamiliki wa mafuta hayo kuyalipia kodi kabla ya kuyaingiza sokoni ili yanapoingizwa sokoni yanaendelea na taratibu za uuzwaji hali ambayo inarahisisha usambazaji na kuwafikishia wateja huduma ya mafuta kwa wakati sambamba na kudhibiti kubaki nchini mafuta ambayo kimsingi yanapaswa kusafirishwa kwenda nje ya nchi.
Aidha akizungumza wakati wa ziara yake aliyoifanya hivi karibuni katika bohari za kuhifadhia mafuta zilizopo Jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yusuph Juma Mwenda pamoja na mambo mengine alisema lengo la TRA kuweka utaratibu huo ni kuwezesha biashara kufanyika kwa urahisi na kuondoa changamoto zilizokuwepo hapo awali huku akitoa wito kwa wafanyabiashara watakaokutana na changamoto zozote kuwasiliana na TRA.
Pamoja na mambo mengine pia Kamishina Mwenda alisema Mamlaka hiyo pia umeweka utaratibu wa kufanya kazi kwa Saa 24 ili kuharakisha utolewaji wa huduma kwa walipakodi ambao ni waingizaji, wasambazaji na wauzaji wa mafuta hayo.





