Saturday, 14 February 2026

RAIS SAMIA ADHIHIRISHA UPENDO WAKE KWA KUWAJENGEA ICU WANANCHI HANDENI - PROF. SHEMDOE

Na OWM – TAMISEMI, Handeni

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujenga jengo la Wagonjwa Mahututi (ICU) katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni ili kuokoa maisha ya wananchi wa Handeni, kitendo ambacho kinadhirisha upendo wake kwa wananchi hao. 

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Februari 13, 2026 katika Viwanja vya Handeni Square, alipopewa fursa ya kuzungumza na wananchi kabla ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba kuzungumza na wananchi hao, mara baada ya Mhe. Waziri Mkuu kuhitimisha ziara yake ya kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani Handeni. 

“Ndugu zangu wa Handeni tumshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha fedha za ujenzi wa jengo hili la ICU, wengine si rahisi kutambua umuhimu wa jengo hili kwasababu hawajaugua na kulazimika kulazwa ICU, ni jengo muhimu la kuokoa maisha ya mwanadamu,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Kwa kutambua umuhimu wa majengo ya ICU, Prof. Shemdoe amesema  Ofisi ya Rais - TAMISEMI inaendelea kuangalia uwezekano wa kujenga majengo ya ICU Lushoto na Mkinga ili kuboresha huduma za tiba katika maeneo hayo, na kuongeza kuwa ofisi yake inaendelea na jitihada za kuhakikisha hospitali za wilaya ambazo hazina majengo hayo zinapata ili kuokoa maisha ya wananchi.

Kwa upande wake. Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI (Elimu) ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini Mhe. Reuben Kwagilwa amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha ujenzi wa jengo la Wagonjwa Mahututi, Maabara, Huduma za Dharura na na jengo la kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni ambayo miundombinu yake ilikuwa chakavu kwani ilijengwa mwaka 1961.
 
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni, Dkt. Hudi Muradi amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizowezesha kujenga miundombinu katika hospitali hiyo, hivyo amemuahidi Mhe. Rais pamoja na wananchi kuwa, watatoa huduma bora na kuilinda miundombinu hiyo ili  itumike kwa muda mrefu. 

Aidha, kwa niaba ya wakazi wa Handeni Bw. Khalid Hassan Malungula ameishukuru Serikali kwa kujenga jengo la ICU ambalo limeboresha utoaji wa huduma kwa wagonjwa mahututi, na kueleza kuwa kabla ya ujenzi wa jengo hilo wagonjwa wa kawaida na mahututi walikuwa wakihudumiwa  pamoja.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 14,2026

Magazeti
 
     
Share:

RC KANALI KIDO RASMI AKABIDHIWA OFISI KAGERA





Na Mbuke Shilagi Kagera. 

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Hajjat Fatma Mwassa amemkabidhi rasmi Ofisi Kanali Yahaya Ramadhan Kido leo Februari 13,2026 katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera uliopo  Manispaa ya Bukoba. 

Akizungumza baada ya makabidhiano Hajjat Fatma Mwassa amesema kuwa Mkoa umefanikiwa kuboresha sekta za huduma zikiwemo sekta za Afya na Elimu. 

Amesema kuwa katika Halmashauri zote saba za Mkoa wa Kagera tayari zipo hospitali za Wilaya ambapo zote zinatumika.

Aidha amemuomba Rc Kanali Kido kutupia jicho la karibu katika hospitali ya Wilaya ya Muleba kutokana na changamoto ya mkandarasi na ubora wa ujenzi.

Akipokea rasmi ofisi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali  Yahaya Ramadhani Kido amesema  kuwa kwa kuwa Mkoa wa Kagera upo mpakani hivyo suala la ulinzi na usalama litakuwa ni kipaumbele namba moja katika Taifa na katika uongozi wake.

"Nitashirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kuendeleza kwa kuendelea kuimarisha usalama kwakua Mkoa wetu unapakana na Nchi jirani", amesema RC Kanali Kido.

Aidha ameongeza kuwa atasimamia miradi yote inayoendelea kutekelezwa na ile inayopangwa kutekelezwa ili iendane na thamani ya fedha zilizotolewa na serikali na kukamilika kwa wakati.

Amesema kuwa amepokea rasmi dhamana ya uongozi ya Mkoa huo akiwa na dhamira thabiti ya kuendeleza yaliyofanywa na mtangulizi wake na yale yote yaliyoelezwa na Mkuu wa Mkoa mstaafu Hajat Fatma Mwassa yatafatiliwa kwa kina na kuhakikisha yanakamilika kwa wakati.






Share:

Friday, 13 February 2026

DKT. GWAJIMA AZINDUA MKAKATI WA KITAIFA WA KISEKTA WA KUTOKOMEZA UKEKETAJI ‎




‎Na Saidi Saidi WMJJWM ,Arusha

‎Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amezindua Mkakati wa Kitaifa wa Kisekta wa Kutokomeza Ukeketaji Nchini (2025/2026–2029/2030) katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Ukeketaji yaliyofanyika Februari 12, 2026, Wilaya ya Monduli mkoani Arusha.
 Uzinduzi wa mkakati huo unalenga kuimarisha juhudi za kitaifa za kulinda haki, afya na ustawi wa wanawake na watoto wa kike.

‎Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Gwajima amesema mkakati huo utaimarisha uratibu na ushirikiano kati ya Serikali, wadau wa maendeleo na jamii katika kuzuia na kutokomeza vitendo vya ukeketaji. Ameeleza kuwa mikoa ya Arusha na Manyara ina viwango vya juu vya ukeketaji, hali inayohitaji hatua madhubuti na ushiriki wa kila mdau.

‎Dkt. Gwajima amesema kuwa katika kutokomeza ukeketaji ni muhimu sana kuwashirikisha wanaume kwa kuwapa elimu, kwani wao ndio wahamasishaji wakuu wa vitendo hivyo.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Dkt. Gwajima pia ameongoza maandamano ya wanaume kama ishara ya kuwataka kupinga ukeketaji.

Aidha, amewashukuru wadau mbalimbali wanaoiunga mkono Serikali ikiwemo Umoja wa Ulaya (EU), Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), C-SEMA, SOS Children’s Village, Compassion International Tanzania na mashirika mengine kwa mchango wao katika mapambano dhidi ya ukeketaji.


‎Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Mhe. Gloriana Kimathi, amemshukuru na kumpongeza Waziri Dkt. Gwajima kwa kuichagua Wilaya ya Monduli kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo, akisema kuwa ujio wake na kufanyika kwa maadhimisho hayo umeamsha ari kubwa ya mapambano dhidi ya ukeketaji.

Ameongeza kuwa Wilaya itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kutokomeza ukeketaji.

‎Naye Katibu wa Viongozi wa Mila Wilaya ya Monduli (Laigwanan), Natuli Letema, amesema viongozi wa mila wataendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Mkoa katika kutoa elimu ya kutokomeza ukatili wa kijinsia na ukeketaji.

Ameeleza kuwa juhudi hizo zitazaa matunda kutokana na ari mpya iliyoamshwa na Waziri Dkt. Gwajima ya kuendelea kupambana na mila hatarishi, akisisitiza kuwa sasa ni wakati wa jamii kubadilika na kulinda watoto wa kike.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARI 13,2026

 
magazeti     Magazeti


  
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger