Monday, 6 April 2026
Sunday, 5 April 2026
UKOMAVU WA KISIASA: RAIS SAMIA AZIBA MAKOVU YA UCHAGUZI, AKUTANA NA WAGOMBEA URAIS 16 IKULU
.jpg)
Katika hatua inayotajwa kama kielelezo cha juu cha ukomavu wa demokrasia na uongozi wenye busara, Rais Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na waliokuwa wagombea urais 16 alioteuliwa nao katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. 0755844215
Wadau mbalimbali wa siasa, wasomi, na wachambuzi wamemwagia sifa Rais Samia kwa hatua hiyo, wakibainisha kuwa imesaidia "kuziba makovu" yaliyotokana na joto la uchaguzi.
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Juma Ally Khatib, amepongeza kitendo hicho akisema kinaleta tafsiri njema ya demokrasia na kukuza siasa za staha.
Amesema kuwa washindani kukaa meza moja na mshindi ni ishara kuwa maslahi ya Tanzania ni makubwa kuliko itikadi za vyama.
Mwanasiasa mkongwe, Hamad Rashid, amebainisha kuwa mkutano huo ni utekelezaji wa vitendo wa falsafa ya Rais Samia ya 4R (Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi na Kujenga Upya).
Rashid ameshauri utaratibu huu uwe wa kudumu na hata kuingizwa kwenye mfumo wa maandishi kama kanuni ya nchi, huku akitoa mwito kwa upande wa Zanzibar kuiga mfano huo ili kuunganisha wananchi.
Uchambuzi wa wasomi, akiwemo Dk. Paul Loisulie wa UDOM na Goodluck Ng’ingo, unaonesha kuwa Rais amefanya jambo la msingi kwani amani na utulivu ndivyo vinavyotoa nafasi kwa serikali kutekeleza majukumu ya maendeleo kwa wananchi.
Wamesisitiza kuwa siasa za kuheshimiana hupunguza taharuki, hasa katika zama hizi ambapo mitandao ya kijamii hutumika vibaya kuchochea migogoro.
Kwa upande wake, Rais Samia kwa kuitikia wito huo wa wagombea wenzake, amethibitisha kuwa milango yake iko wazi kwa majadiliano yenye tija.
Viongozi hao wa vyama 16 walipata fursa ya kuwasilisha maoni yao kuhusu hali ya nchi, amani, na mshikamano, jambo linalotuma ujumbe mzito kwa ulimwengu kuwa Tanzania ni taifa linalotatua tofauti zake kupitia mazungumzo ya kistaarabu badala ya mivutano.
Saturday, 4 April 2026
MWANAMKE AUAWA KWA KUKATWA SHINGO SHINYANGA
Jeshi la Polisi linawashikilia watuhumiwa wawili kuhusiana na mauaji ya kikatili ya mwanamke Hollo Ruchanganya (60), mkazi wa kijiji cha Bunambiyu wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, huku uchunguzi wa awali ukihusisha imani za kishirikina.
Akizungumza na vyombo vya habari mjini Shinyanga leo Jumamosi Aprili 4, 2026, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Janeth Magomi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa watuhumiwa hao wanahojiwa ili kubaini ukweli wa tukio hilo.
Katika tukio hilo, marehemu Hollo Ruchanganya aliuawa kikatili kwa kukatwa shingoni na mtu asiyejulikana, kabla ya mwili wake kutupwa katika shamba la mahindi jirani na makazi yake.
Kwa mujibu wa taarifa za awali, mtuhumiwa wa mauaji hayo anadaiwa kuwa mgeni aliyefika nyumbani kwa marehemu majira ya saa 3:00 usiku wa Aprili 3, 2026, ambapo alikula chakula pamoja na marehemu na wajukuu wake.
Baadaye marehemu alimsindikiza mtuhumiwa huyo kwa lengo la kumpeleka kwa mtalaamu wa tambiko linalodaiwa kuzuia kupata watoto pacha.
Inaelezwa kuwa muda mfupi baada ya kutoka, mtu huyo alirejea nyumbani na kurejesha tochi, akiwataarifu wajukuu wa marehemu kuwa bibi yao angerudi asubuhi kutoka kwa mganga anayeelezwa kuwa ni ndugu yake.
Mwili wa marehemu uligunduliwa asubuhi na mjukuu wake aliyekuwa akielekea shambani, baada ya kuona damu nyingi na nguo za marehemu njiani. Baada ya kutoa taarifa kwa ndugu, walifanikiwa kuufuatilia mwili huo uliokuwa umetupwa shambani ukiwa na jeraha kubwa la kukatwa shingoni.
Kamanda Magomi amesema uchunguzi unaendelea ili kubaini wahusika wote na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
KAHAMA KUCHEKA KWA NGUVU JUMAMOSI HII !! LIVE COMEDY SHOW UKUMBI WA MALEX 🔥




























