Monday, 10 August 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI AGOSTI 9,2026

Magazeti



Share:

WANAFUNZI 85 KWENDA INDIA KUSOMEA ELIMU YA JUU


Na Mwandishi Wetu

WANAFUNZI 85 wanatarajia kwenda masomoni kwenye vyuo vikuu mbalimbali nchini India kuanzia wiki ijayo kupitia Wakala wa Elimu Nje ya Nchi Global Education Link (GEL).

Wanafunzi hao na wazazi wao walihudhuria mkutano uliofanyika katika ofisi za GEL mwishoni mwa wiki kwaajili ya kupewa mafunzo ya namna ya kuishi nchini humo.

Pia walielezwa mambo wanayotakiwa kufanya na wasiyotakiwa kuyafanya wakiwa masomoni nchini humo ikiwemo suala la vibali, bima na makaazi ili waweze kuhitimu masomo yao.

Mbali na mafunzo hayo walipewa tiketi zao za ndege, visa na nyaraka mbalimbali zitakazowawezesha kupokelewa kwenye vyuo wanavyokwenda kusoma nchini India.

Wanafunzi hao wanatarajiwa kuanza kwenda nchini India kuanzia tarehe 21 na 23 mwezi huu.

Akizungumza kwenye mkutano huo wa wanafunzi na wazazi wao, Mkurugenzi Mkuu wa GEL, Abdulmalik Mollel aliwataka wanafunzi hao kusoma huku wakiangalia fursa mbalimbali ambazo zinaweza kuwasaidia wanapohitimu.

“Tunahitaji GPA nzuri lakini pia huko kuna fursa nyingi sana, mtasoma na watoto wa matajiri wenye viwanda tunataka muwe karibu na watu kama hao kutambua fursa ya wewe kupata kazi siyo unamaliza halafu unakuja kuhangaika kutafuta kazi wakati huko kulikuwa na fursa,” alisema

Aliwataka wanafunzi hao kutafuta marafiki ambao wataongeza thamani ya masomo yao badala ya kuwa na marafiki ambao wanapenda starehe na hawahudhuriii masomo madarasani.

“Katumieni muda wenu nje ya kile kilichowapeleka kwa maana ya kujiongeza, tatizo la ajira ni shida ya dunia nzima siyo Tanzania ni wewe tu unavyoona fursa unazoona hata kwa wanafunzi utakaosoma nao huko nje,” alisema

“Kule mtakutana na wanafunzi wa mataifa mbalimbali na hata wa nchi zilizoendelea ulizeni fursa zilizoko kule kwenye mataifa yao ili kama ukimaliza unaweza kwenda kufanya kazi siyo lazima uje kuhangaika baada ya kuhitimu,”

“Mfano mtasoma na watoto wa matajiri wana viwanda ulizeni fursa zilizoko kwa hao watoto kwasababu India watu kuwa viwanda vidogo vidogo nyumbani kwao ni maisha ya kawaida kabisa kuna mtu ana kiwanda chumbani kwake thamani ya mtaji ukiuliza ni Dola 8,000,” alisema

Alisema India kuna viwanda vidogo vidogo ambavyo mtaji wake ni mdogo kiasi kwamba hata ndugu wanaweza kukupa na aliwataka kuondokana na dhana kwamba kuanzisha biashara kunahitaji mabilioni ya fedha.

“India wameendelea sana kwa viwanda tumieni fursa hiyo ila isikutoe kwenye reli ya nasomo yako. Jiulize unasoma kwaajili ya GPA nzuri tu au unakwenda kuhamisha maarifa ya kuchukua telnolojia na fursa za viwanda zinazopatikana kule kuleta hapa Tznania,” alisema Mollel

Alisema kila mwaka wanafunzi zaidi ya 800 wanapitia Global Education Link kwenda kusoma nje ya nchi hivyo kila mmoja akiwa mbunifu na kubaini fursa zilizoko nje ya nchi watapunguza tatizo la ajira wanapohitimu.

Alisema kuanzia mwakani Global Education Link itafungua fursa za ajira kwasababu kuna kampuni kubwa nchini ambazo zimekuwa iwape wataalamu wa aina mbalimbali inaowafahamu.

Alisema India inaongoza kwa kupeleka vijana wao kwenda kufanya kazi nje na si kwa bahati mbaya bali ni kutokana na kuwa na mtandao wa kubaini fursa mbalimbali kwenye mataifa.

“Kule India hawasomi ili wapate GPA wanasoma ili watengeneze fursa wewe unasoma ukimaliza unaanza kulalamika hakuna ajira, hatutaki hilo.Tunatamani mpate zaidi ya GPA mrudi na fursa zinazopatikana huko,” alisema Mollel

“ Ulaya kuna shida kubwa ya rasilimali watu kutokana na wengi kustaafu kwa umri sasa wewe ukisoma uhandisi jiongeze soma na kijerumani au Kifaransa angalia lugha ambayo inaweza kukusaidia kupata ajira,” alisema

Alsiema kwenye mataifa ya Ulaya fursa za kazi zipo ila wanataka mtu anayejua lugha yao kwa hiyo aliwataka wanafunzi hao kuhakikisha wanapata fursa zote wanazoona huko wasiishie kukariri GPA.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 10, 2026



Magazetini Leo



Share:

Sunday, 9 August 2026

AGCOT YAMWEZESHA NEEMA KUTOKA MKULIMA HADI MWENYE KAMPUNI YA MAZAO




Na Sheila Ahmadi, Dodoma

Mwanzilishi na Mkurugenzi wa kampuni inayojihusisha na uzalishaji wa mazao ya mboga mboga mkoani Iringa, Neema Mwamoto amesema uwezeshaji alioupata kupitia AGCOT umekuwa sehemu muhimu ya safari yake kutoka kuwa mkulima wa kawaida hadi kuanzisha kampuni inayolenga kukuza uzalishaji na masoko ya mazao ya kilimo.

Neema amesema kuwa safari yake katika kilimo ilianza akiwa mkulima wa kawaida, ambapo alianza kulima mazao mbalimbali kabla ya kuingia katika mfumo wa kilimo cha kibiashara na baadaye kufanya kazi kama mkulima mkataba katika kampuni ya (GBRI) mkoani Iringa mwaka 2015.

mwaka 2017 alianza kulima matikiti, huku mwaka 2019 akiendelea na shughuli za kilimo kupitia kampuni, hatua iliyomuwezesha kupata uzoefu zaidi kuhusu uzalishaji na masoko.

"uzoefu huo ulimsaidia kuona fursa zilizopo katika sekta ya kilimo na kuanza kufikiria namna ya kuanzisha kampuni yake binafsi ili aweze kuzalisha kwa kujitegemea, badala ya kuendelea kufanya kazi kama mkulima mkataba.

Amesema mwaka 2021 changamoto zilizotokana na COVID-19 ziliathiri shughuli zake za kilimo, lakini baadaye alirejea na kuamua kuanzisha kampuni yake mkoani Iringa.

“Nilianza kama mkulima wa kawaida, lakini nilipoanza kufanya kazi kama mkulima mkataba nilianza kuona kuna fursa nyingi katika kilimo. Hapo ndipo nilipopata wazo la kuanzisha kampuni yangu binafsi ili niweze kulima na kukuza shughuli zangu,” amesema Mwamoto"

Katika Hatua nyingine Neema amesema kampuni hiyo ilipoanza, ilijikita zaidi katika kutafuta masoko ya ndani (local market), lakini ndoto yake ilikuwa kufikia hatua ya kuuza mazao katika masoko ya nje ya nchi (export market).

katika kufikia ndoto hiyo, amepitia michakato mbalimbali ya kujengewa uwezo kupitia wadau mbalimbali, ikiwemo AGCOT, ambao umekuwa sehemu ya safari yake ya kujifunza na kuboresha shughuli za kampuni.

uwezeshaji huo umemsaidia kupata uelewa zaidi kuhusu uzalishaji wa mazao kwa kuzingatia mahitaji ya soko, hatua ambayo imeendelea kumjengea uwezo wa kukuza biashara yake na kuwafikia wakulima wengine.

Aidha Dhumuni la sasa ni kuongeza uzalishaji wa mazao ya mboga mboga, kuimarisha masoko na hatimaye kufikia soko la kimataifa.

Vilevile Neema ameongeza kuwa safari yake kutoka kuwa mkulima wa kawaida hadi kuwa mwanzilishi na mkurugenzi wa kampuni imeonyesha umuhimu wa uwezeshaji kwa vijana na wakulima, akisisitiza kuwa elimu, ujuzi, masoko na fursa za kibiashara ni muhimu katika kukuza sekta ya kilimo.

Nitaendelea kutumia uzoefu nilioupata pamoja na fursa za uwezeshaji kutoka kwa wadau kama AGCOT, kwa lengo la kukuza kampuni na kuchangia kuongeza kipato cha wakulima




.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger