Tuesday, 14 April 2026

SANGU APIGILIA MSUMARI TUNU ZA TAIFA: ASEMA AMANI NA MARIDHIANO NDIO MUHIMILI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akikabidhi risiti ya benki ya Tsh. Milioni 20,000,000 kwa Padri Didas Nandi, kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Parokia ya Mt. Fransisco wa Asiz iliyopo Msandamungano, mkoani Rukwa, leo Aprili 12, 2026. Pesa hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba,


Katika mkakati kabambe wa kuimarisha mshikamano wa kitaifa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu, ametoa wito mzito kwa Taasisi na Viongozi wa Dini nchini kutosimama kando, bali kuwa mstari wa mbele kushirikiana na Serikali kulinda na kudumisha Tunu za Taifa.

Akizungumza  mkoani Rukwa, Waziri Sangu amesisitiza kuwa Amani, Upendo, Mshikamano, na Umoja wa Kitaifa ndivyo vishikizo vikuu vinavyolishikilia Taifa la Tanzania, na bila misingi hiyo, ustawi na maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana.

Mabilioni ya Harambee na Ishara ya Umoja

Mhe. Sangu aliyasema hayo alipomwakilisha Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, katika harambee ya ujenzi wa Kanisa la Parokia ya Mt. Fransisco wa Asizi, Msandamungano iliyofanyika kanisani hapo leo Aprili 12, 2026. 

Katika tukio hilo la kihistoria lililojaa hekaheka za kizalendo, zaidi ya Tsh. Milioni 53 zilichangwa, huku Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akionyesha mfano kwa kuchangia Tsh. Milioni 20 taslimu—ishara tosha ya namna Serikali inavyothamini mchango wa taasisi za dini katika ujenzi wa nchi.

Dhamana ya Mahusiano na Dira ya 2050

Waziri Sangu ameweka wazi kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu imepewa dhamana nzito ya kuratibu mahusiano kati ya Serikali na makundi ya kijamii ili kuhakikisha maridhiano yanatawala. 

Alibainisha kuwa ushirikiano huo umedhihirishwa kwa vitendo kupitia ushirikishwaji wa viongozi wa dini katika kuandaa Dira ya Maendeleo 2050.

"Dhamira yetu ni kuijenga Tanzania tuitakayo kupitia maono ya pamoja. Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua kuwa viongozi wa dini ni nguzo muhimu katika kulea vijana kiroho ili wawe wazalendo, wenye maadili mema na tabia njema zinazochochea jamii tulivu yenye amani," alisema Waziri Sangu.

Rai kwa Waumini na Viongozi
Waziri huyo hakusita kuwasihi waumini kumuunga mkono Rais Samia kwa vitendo, akisisitiza kuwa ujenzi wa taasisi za dini ni sehemu ya maendeleo ya kijamii ambayo Serikali itaendelea kuyaunga mkono.

 Alimshukuru Paroko wa Parokia hiyo, Padri Didas Nandi, kwa kuratibu vyema harambee hiyo inayolenga kukusanya jumla ya Tsh. Milioni 900 kwa ajili ya kukamilisha nyumba hiyo ya ibada.

Padri Nandi: Sisi ni Kiungo cha Amani
Kwa upande wake, Padri Didas Aisakus Nandi ameahidi kuwa Kanisa litaendelea kuwa kiungo muhimu kati ya waumini na Serikali. Alisisitiza kuwa juhudi zao za kiroho hazitaishia madhabahuni, bali zitakwenda mitaani kuhamasisha amani, ushirikiano na maendeleo endelevu ili kuhakikisha Tunu za Taifa hazitikisiki.







Share:

Monday, 13 April 2026

LALJI FOUNADATION YAENDESHA KAMBI YA MATIBABU YA MACHO BURE KIGOMA


Taasisi ya LALJI FOUNDATION kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Kigoma Hilltop Hotel, Ahlulybayt Academic Center, Vision 4 All Eye Centre pamoja na Supa Foam imeendesha kambi maalumu ya siku nne ya matibabu ya macho bure kwa wakazi wa mkoa wa Kigoma.

Kambi hiyo ilifanyika kuanzia tarehe 03 hadi 06 Aprili 2026 katika viwanja vya shule za Ahlulbayt Islamic Center Manispaa ya Kigoma Ujiji, ilitoa huduma mbalimbali muhimu ikiwemo uchunguzi wa macho, ushauri wa kitaalamu, utolewaji wa miwani, huduma za dawa pamoja na upasuaji wa mtoto wa jicho bila malipo.

Akizumza baada ya kukamilika kwa kambi hiyo mlezi wa Taasisi ya LALJI FOUNDATION Mohsen Lalji amesema Zaidi ya wananchi 6000 walijiotokeza kupata huduma ambapo watu 5079 walifanyiwa uchunguzi wa macho, 2218 walipatiwa miwani ya macho, 518 walifanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho na watu 3215 walipatiwa dawa za macho huku huduma zote zikitolewa bure bila malipo.

Amesema lengo la kambi hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu kwa wakati na ukaribu zaidi.

Akizindua rasmi kambi hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mh Balozi Simon Sirro aliipongeza LALJI FOUNDATION na washirika wake kwa jitihada hizo za kuwafikia wananchi na kuwapatia huduma muhimu za matibabu ya macho, hususan kwa wale wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

Aidha, aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili kunufaika na huduma hizo, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na taasisi zisizo za kiserikali katika kuboresha huduma za kijamii na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Wakizungumza baada ya kupatiwa huduma, wananchi wengi walieleza kuwa walikuwa hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu ya macho, ikiwemo upasuaji na ununuzi wa miwani, hali iliyowafanya kuendelea kuishi na matatizo ya macho kwa muda mrefu.

Wananchi hao pia waliomba juhudi kama hizi ziendelee kudumishwa ili kuwasaidia watu wengi zaidi, hasa wale wa kipato cha chini ambao bado wanakabiliwa na changamoto ya kumudu gharama za huduma za afya.

Kambi hiyo imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za wadau wa maendeleo katika kuhakikisha jamii inapata huduma bora za matibabu ya macho hususan katika maeneo yenye uhitaji mkubwa kama Kigoma.
Share:

AMANI NA MARIDHIANO: NGUZO KUU INAYOIFUNGULIA SIDO MILANGO YA KUWAKOMBOA VIJANA KIUCHUMI


 NA MWANDISHI WETU

KATIKA kipindi hiki ambacho Tanzania inaweka msisitizo wa kipekee kwenye Amani, Upendo, na Maridhiano ya Kitaifa, imebainika kuwa utulivu huo ndio rasilimali namba moja inayoiwezesha Serikali kupitia taasisi zake kama Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Bila mshikamano wa kitaifa, juhudi za kutengeneza mazingira rafiki ya ajira na ujasiriamali kwa vijana haziwezi kuzaa matunda ya kudumu.

Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi mahiri wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeweka kipaumbele cha dhati katika kulinda tunu hizi za Taifa ili kutoa nafasi kwa mashirika kama SIDO kuwafikia vijana na "nyenzo" za kisasa za uzalishaji mali. Hii ni dhihirisho kuwa amani si hali tu ya kutokuwepo kwa fujo, bali ni mazingira wezesha yanayomfanya kijana awe na utulivu wa kubuni, kuzalisha, na kujiajiri.

SIDO na Silaha ya Ubunifu: Kijana Jitambue!

Katika kukabiliana na changamoto ya ajira, SIDO imejipambanua kama kimbilio la vijana wanaotaka kuandika historia mpya ya kiuchumi. Shirika hilo limebeba jukumu la kukuza ubunifu, likiwapatia vijana mbinu za kisasa za utengenezaji bidhaa zinazoweza kushindana ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Mhadhiri na wataalamu wa maendeleo wanasisitiza kuwa kijana mwenye shughuli ya kufanya na kipato cha uhakika ndiye mlinzi mkuu wa amani ya nchi. Kupitia programu za SIDO, vijana wanahamasishwa kuacha utamaduni wa kusubiri ajira za "kuchongwa" na badala yake waingie mitaani kwa hekaheka za uzalishaji zinazochochea utulivu wa kijamii.

Maridhiano ya Kitaifa: Msingi wa Masoko na Uzalishaji

Ushirikiano uliopo sasa kati ya Serikali na wadau mbalimbali umefungua milango ya masoko kwa bidhaa za vijana. SIDO haishii tu kumpa kijana mashine au utaalamu, bali inamsaidia kupata soko—jambo linalowezekana tu ikiwa kuna mshikamano na umoja wa kitaifa. Taasisi mbalimbali zimeunganishwa ili kuhakikisha elimu ya ujasiriamali inawafikia vijana wengi zaidi, ikijenga jamii yenye watu wanaojitegemea na wanaoheshimu tunu za amani na upendo.

Wito wa Uzalendo: Thamani ya Bidhaa na Taifa

Vijana nchini waaswa kuwa mzalendo si tu kulinda mipaka, bali ni pamoja na kuongeza thamani ya bidhaa za kitanzania. Kupitia elimu ya SIDO, vijana wanapata uwezo wa kuboresha ubora wa kazi zao, jambo ambalo ni chachu ya kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Tunapozungumzia maridhiano na umoja wa kitaifa, tunazungumzia pia haki ya kijana kupata fursa. SIDO imetoa rungu hilo kwa vijana; ni wakati wao sasa kulitumia kwa bidii, ubunifu, na uzalendo ili kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa kisiwa cha amani chenye neema ya kiuchumi kwa kila mwananchi.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRILI 13, 2026





 
Share:

Sunday, 12 April 2026

Video Mpya : MAMA USHAURI - MILEMBE

Share:

Saturday, 11 April 2026

Video Mpya : YOGATI - MAISHA

Share:

MOIL ENERGIES YAIPONGEZA TRA KWA MFUMO MPYA WA ULIPAJI KODI YA MAFUTA

 


Kampuni ya Uingizaji na Usambazaji wa mafuta Jamii ya Petrol nchini ya 'MOIL Energies' imesema imefurahishwa kwa kuanzishwa kwa mfumo mpya wa ulipaji kodi ya nishati hiyo kabla ya kuyatoa vituoni na kwenda sokoni (BIL) kwa kiasi kikubwa umesaidia kudhibiti 'ujanja ujanja' uliokuwepo hapo awali.

Akizungumza Dar es Salaam Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo nchini, Dkt. Sajad Habib Rai amesema wao kama Kampuni ya kwanza nchini kutoa mapendekezo ya kuanzishwa kwa mfumo huo kwa EWURA na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) na baadae kuanzishwa rasmi na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), wanajivunia kuona umetekelezwa kwa kuwa dhamira yao ilikuwa kuona huduma ya usambazaji wa mafuta nchini na nje ya nchi unaleta tija kwa Taifa.

"Tumefurahi kuona TRA wameusimamia kikamilifu mfumo huu kwa kuwa unazuia ukwepaji kodi ambao hapo awali ulikuwa ukifanywa na wafanyabiashara, hivi sasa TRA inapata kodi yake mapema kabla ya kuyaingiza mafuta sokoni" amesema Dk Sajad ambaye pia ni Meneja MKAZI wa 'Mansoor Industry Limited'.

Hivi karibuni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitangaza rasmi kuanza kutumika kwa mfumo huo ambao kwa kiasi kikubwa unalezwa kuleta tija kwa Serikali kwa kuwa umesaidia kudhibiti upotevu wa mapato unaotakana na Kodi za uingizaji wa mafuta hayo nchini.

Kupitia mfumo huo mpya na wa kisasa, kila mwagizaji au muingizaji wa mafuta atalazimika kutaja kiasi cha mafuta alichokiingiza nchini ambapo kupitia Shirika la Viwango Tanzania (TBS) watayataweka vinasaba kama alama ya kila mwagizaji kwa lengo la kuwatambua wahusika wote na kiasi alichoagiza ili kuwakadiria viwango vya Kodi wanavyopaswa kulipa.

"Nawapongeza TRA kwa kuona tija na umuhimu wa kuutumia mfumo huu, sisi kama wafanyabiashara tunaozingatia taratibu halali za uingizaji na Usambazaji wa mafuta tunaiona kuwa hatua hii ni kubwa na inayostahili kupongezwa kwa kuwa italeletea manufaa Taifa", ameongeza Dkt. Sajad.

Utaratibu huo wa kikodi unawataka wamiliki wa mafuta hayo kuyalipia kodi kabla ya kuyaingiza sokoni ili yanapoingizwa sokoni yanaendelea na taratibu za uuzwaji hali ambayo inarahisisha usambazaji na kuwafikishia wateja huduma ya mafuta kwa wakati sambamba na kudhibiti kubaki nchini mafuta ambayo kimsingi yanapaswa kusafirishwa kwenda nje ya nchi.

Aidha akizungumza wakati wa ziara yake aliyoifanya hivi karibuni katika bohari za kuhifadhia mafuta zilizopo Jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yusuph Juma Mwenda pamoja na mambo mengine alisema lengo la TRA kuweka utaratibu huo ni kuwezesha biashara kufanyika kwa urahisi na kuondoa changamoto zilizokuwepo hapo awali huku akitoa wito kwa wafanyabiashara watakaokutana na changamoto zozote kuwasiliana na TRA.

Pamoja na mambo mengine pia Kamishina Mwenda alisema Mamlaka hiyo pia umeweka utaratibu wa kufanya kazi kwa Saa 24 ili kuharakisha utolewaji wa huduma kwa walipakodi ambao ni waingizaji, wasambazaji na wauzaji wa mafuta hayo.

Share:

PROF. SHEMDOE AELEKEZA WAFANYABIASHARA SOKO LA SIMU 2000 KUENDELEA NA BIASHARA



Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameelekeza hatua za haraka zichukuliwe kuwarejesha wafanyabiashara wa Soko la Mawasiliano (Simu 2000) ili kuendelea na shughuli za biashara katika soko hilo ambalo lilipata ajali ya moto iliyoteketeza soko hilo Aprili 04, 2026.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Aprili 10, 2026 alipolitembelea soko hilo na kuridhishwa na utekelezaji wa Maelekezo ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba aliyoyatoa Aprili 6, 2026, alipofika kukagua madhara ya tukio hilo la moto na kuelekeza soko hilo kusafishwa mara moja ili kuruhusu wafanyabiashara kuanza taratibu za kurejesha shughuli zao.

“Nimeridhishwa na utekelezaji wa maelekezo aliyotupatia Mhe. Rais na Mhe. Waziri Mkuu, hivyo naelekeza haraka iwezekanavyo wafanyabiashara warejeshwe kuendelea na shughuli zao lakini wasijenge vibanda na badala yake waweke meza pamoja na miamvuli ili kujikinga dhidi ya jua na mvua,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila kusimamia kikamilifu maelekezo aliyoyatoa, huku akimtaka Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando kufanya ufuatiliaji wa kila siku ili wafanyabiashara wa soko hilo warejee haraka kuendelea na shughuli zao.

Aidha, katika hatua nyingine Prof. Shemdoe ameilekeza DART na Mkandarasi anayejenga soko jipya la Mawasiliano kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa viwango ndani ya miezi minne badala ya sita ili wafanyabiashara hao wanaorejeshwa kwa kutumia meza wapate vibanda vya kufanyia biashara.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando kwa usimamizi mzuri wa utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Waziri Mkuu ambayo yanayowezesha urejeshwaji wa haraka wa wafanyabiashara hao walioathirika na ajali ya moto katika soko hilo la mawasiliano (simu 2000). 

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando amesema, ameelekeza ndani ya siku tatu kuanzia leo kufanyike zoezi la utambuzi wa wafanyabishara wote kwa majina matatu na vitambulisho ili kuepuka changamoto ya watu kuchukua vibanda na kuwapangisha wafanyabiasharana kuongeza kuwa atahakikisha wafanyabiashara watakaopata mikopo ni wale waliothirika na janga la moto na wenye sifa na stahiri ya  kupata mikopo.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 11,2026


Magazeti
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger