Friday, 5 June 2026

TANZANIA: BELGRADE MEETINGS SEAL ARUSHA PREPARATIONS FOR 153RD IPU ASSEMBLY


#Tanzanian delegation confirms readiness after key meetings with IPU leadership and Serbian hosts in Belgrade

By Prosper Makene

Tanzania’s Deputy Permanent Representative to the United Nations in Geneva, Ambassador Dr. Hoyce Temu, joined Tanzanian MPs in Belgrade to engage with the IPU leadership and Serbian parliamentary hosts. In meetings with the heads of the Preparatory Committee from the Parliament of Serbia — Mr. Vladimir and Ms. Vesna — the Tanzanian team exchanged critical lessons on logistics, protocol, and conference management.  

Dr. Temu who also manages the IPU in Geneva, said the engagement was crucial for aligning Arusha’s hosting plans with global standards.  

“After attending five IPU meetings around the world, I can confirm that we are now ready. Arusha is ready and Tanzania is ready,” Dr. Temu posted after the Belgrade sessions. “We have learned a lot about the preparations. Arusha is ready to receive parliamentarians from around the world.”  

On her part, IPU President Hon. Dr. Tulia Ackson, addressed delegates at the IPU Global Conference of Women Parliamentarians in Belgrade, Serbia. She said:

“Today is not a day to talk about anything you haven’t been good in, but for anything good that you have seen in Tanzania, you will get it in abundance,” Dr. Tulia told the assembly.  

She announced that the 153rd IPU Assembly will be held from 5th to 9th October 2026 in Arusha, and assured delegates that Tanzania is ready to host:  

“So I would like to take this opportunity to specially invite all of you, dear women and men parliamentarians of the world, to come to Arusha, to come to Tanzania and enjoy the hospitality of this country.”  

Dr. Tulia further confirmed that President Dr. Samia Suluhu Hassan is ready to receive the global delegation, and that Tanzania has put comprehensive measures in place for safety and health:  

“Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan is ready to receive you, the President of Tanzania, but also Tanzania is ready to receive you. Tanzania is prepared to serve you. We have put in place everything needed to make sure you arrive safely and healthy, and you leave safely and healthy too.”  

In a separate engagement in Belgrade, Dr. Temu assured Dr. Tulia and outgoing Secretary General Martin Chungong that Tanzania has completed its groundwork.  

Arusha to Host 2,000+ Global Delegates  

The 153rd IPU Assembly in Arusha is expected to bring together over 2,000 delegates, parliamentarians, and observers from across the globe, making it one of the largest diplomatic gatherings ever hosted by Tanzania.  

In this context, it is particularly noteworthy that Tanzania will host the 153rd Assembly of the Inter-Parliamentary Union (IPU) in Arusha this October 2026. The announcement has raised expectations as the country positions Arusha — already known as Africa’s diplomatic capital — as a center for parliamentary dialogue, peacebuilding, and multilateral cooperation.  

Tanzania’s Parliament is making final preparations to welcome the world. A high-level delegation of Members of Parliament confirmed the country’s readiness during the World Conference of Women Parliamentarians in Belgrade, Serbia. The delegation, representing the Parliament of Tanzania at the IPU event, met with key IPU officials to ensure the Arusha assembly will be a success.  

The message was echoed by fellow MPs  in Belgrade, including Hon. Rashid Shangazi, Hon. Pindi Chana, Hon. Dr. Zeyana Hamid, and Hon. Kiza Mayeye. The group used the platform to showcase Tanzania’s capacity to host high-level global forums.  

From Geneva to Arusha: A Decade of Parliamentary Diplomacy 
 
Dr. Temu’s role is particularly significant. Based in Geneva where the IPU headquarters is located, she has coordinated Tanzania’s participation in multiple IPU assemblies. Her presence in Belgrade alongside the MPs signals a whole-of-government approach to ensuring Arusha 2026 delivers on diplomacy, organization, and impact.  

With lessons from Belgrade now integrated into the plan, all eyes turn to Arusha. The blueprint is set. The Tanzania Parliament Under the leadership of the House Speaker Mussa Azzan Zungu is Confident and Ready As Dr. Temu said, we are now ready for the IPU meeting in Arusha, the city which is popularly known as the Geneva of Africa.




Share:

TPDC YAKABIDHI KARAKANA YA KISASA YA CNG KWA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.


Dar es Salaam, Juni 5, 2026

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limekabidhi rasmi Karakana ya kuongeza mfumo wa matumizi ya gesi asilia Iliyoshindiliwa kwenye vyombo vya usafiri (CNG Conversion Workshop) kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), hatua inayotarajiwa kuimarisha matumizi ya nishati safi nchini pamoja na kukuza ujuzi wa kitaalamu katika teknolojia ya gesi asilia.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika eneo jijini Dar es Salaam, ambapo TPDC iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Uwekezaji, Bw.Derick Moshi, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC. Kwa upande wa UDSM, karakana hiyo ilipokelewa na Naibu Mkuu wa Chuo Prof. Bernadeta Kilian.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Bw. Derick Moshi alisema kuwa ujenzi wa karakana hiyo ni sehemu ya jitihada za TPDC katika kuunga mkono mkakati wa Serikali wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi na nafuu kwa wananchi.

“Kukamilika na kukabidhiwa kwa karakana hii ni hatua muhimu katika kukuza matumizi ya gesi asilia Iliyoshindiliwa (CNG) nchini. Mbali na kutoa huduma za kuongeza mifumo ya CNG kwenye magari, karakana hii itatumika kujenga wataalamu wazalendo kupitia mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wa uhandisi wa UDSM,” alisema Bw. Moshi.

Aliongeza kuwa mradi huo umegharimu shilingi bilioni 1.52 za Kitanzania na ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano kati ya TPDC na UDSM yaliyowekwa kupitia Mkataba wa Upangishwaji Ardhi uliosainiwa mwaka 2022.

Kwa mujibu wa Bw. Moshi, karakana hiyo ina vifaa vya kisasa vinavyowezesha ufungaji wa mifumo ya CNG kwenye vyombo vya usafiri, ukaguzi wa usalama wa mifumo hiyo pamoja na matengenezo yake, hatua itakayochangia kupunguza gharama za matumizi ya nishati kwa watumiaji wa magari nchini.

Kwa upande wake, Prof. Bernadeta Kilian aliishukuru TPDC kwa kutekeleza ahadi yake ya kujenga na kukabidhi karakana hiyo, akieleza kuwa miundombinu hiyo itakuwa kichocheo muhimu katika maendeleo ya elimu, utafiti na ubunifu wa teknolojia za nishati nchini.

“Kupokea karakana hii ni hatua kubwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Miundombinu hii itawapa wanafunzi wetu nafasi ya kupata mafunzo ya vitendo yanayokidhi mahitaji ya soko la ajira na wakati huo huo kusaidia maendeleo ya sekta ya nishati nchini,” alisema Prof. Kilian

Alisisitiza kuwa UDSM itaendelea kushirikiana na TPDC katika tafiti, ubunifu na maendeleo ya teknolojia zinazochangia matumizi bora ya rasilimali za gesi asilia kwa manufaa ya Taifa.

Karakana hiyo imejengwa ndani ya eneo la Kituo Mama cha kujaza gesi asilia (CNG Mother Station) kilichopo UDSM na inatarajiwa kuwa kituo muhimu cha utoaji huduma za CNG pamoja na mafunzo ya kitaalamu kwa wanafunzi na wadau wa sekta ya usafiri.

Kupitia uwekezaji huo, TPDC inaendelea kutekeleza dhamira ya Serikali ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi, salama na nafuu, sambamba na kuongeza ushiriki wa taasisi za elimu ya juu katika maendeleo ya sekta ya nishati nchini.
Share:

DKT. KIJAJI: NYUMBA ZA IBADA ZIWE CHANZO CHA MSHIKAMANO NA AMANI KWA TAIFA




KONDOA, DODOMA

Mbunge wa Jimbo la Kondoa ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amesisitiza kuwa nyumba za ibada zinapaswa kuwa sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja na amani miongoni mwa wananchi na si kuwa chanzo cha migawanyiko katika jamii.

Dkt. Kijaji ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akifungua rasmi Msikiti wa Filimo uliopo Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.



Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Kijaji amesema kuwa nyumba za ibada zina nafasi kubwa katika kujenga maadili mema, kuimarisha upendo na kukuza mshikamano wa kijamii, hivyo zinapaswa kutumika kwa malengo hayo kwa manufaa ya Taifa.

“Msikiti huu uwe chachu ya mshikamano ndani ya jamii yetu. Nawapongeza viongozi wa dini kwa kusimama katika haki na kuendelea kuhubiri amani na umoja miongoni mwa wananchi,” alisema Dkt. Kijaji.


Aidha, aliongeza kuwa kila mtu ana wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu katika jamii na mbele za Mungu, akibainisha kuwa maendeleo yanayopatikana katika Jimbo la Kondoa yanalenga kuwanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.

"Ninachokifanya ndani ya jimbo letu ni kwa ajili ya maendeleo ya Wakondoa wote. Tunapaswa kuendelea kushirikiana na kuishi kwa upendo ili kuleta maendeleo endelevu,” alisisitiza.



Vilevile , Dkt. Kijaji alitumia fursa hiyo kuwahamasisha waumini na wananchi wa eneo hilo kuendelea kujenga na kuendeleza nyumba za ibada ili zitumike katika kukuza maadili mema na kuimarisha imani katika jamii.

Katika hatua nyingine, amewataka vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vingine vinavyohatarisha mustakabali wao, huku akiwataka viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Pia amesisitiza umuhimu wa malezi bora kwa watoto na vijana, akiwataka wazazi na walezi kuwajenga katika misingi ya maadili mema ili kuwa raia wema na wenye mchango chanya kwa maendeleo ya Taifa.


Share:

Thursday, 4 June 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 5, 2026

Share:

MBEYA CITY EXPO YATUMIKA KUELIMISHA WANANCHI KUHUSU HAKI ZA WALAJI





Na mwandishi wetu

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo, ametembelea banda la Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika Maonesho ya Kimataifa ya Mbeya City Expo 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Uhindini, jijini Mbeya, ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hiyo katika kulinda maslahi ya walaji na kuimarisha ushindani wa biashara nchini.

Katika maonesho hayo, FCC imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi kuhusu haki za mlaji, namna ya kutambua na kuepuka bidhaa bandia pamoja na umuhimu wa ushindani wa haki katika shughuli za biashara.

Elimu hiyo imevutia mamia ya wananchi waliojitokeza kutembelea banda hilo na kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu biashara, ushindani na ulinzi wa walaji.

Akizungumza wakati akifunga Maonesho hayo yaliyodumu kwa siku tisa Mei 30, 2026 jijini Mbeya, Naibu Waziri Londo alisisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya bidhaa bandia, akieleza kuwa bidhaa hizo zinaathiri afya za watumiaji, kudhoofisha biashara halali na kupunguza mapato ya Serikali.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kanda wa FCC - Nyanda za Juu Kusini Bw. Dickson Mbanga, amesema taasisi hiyo imejipanga kuendelea kuimarisha kampeni za utoaji elimu kwa wananchi ili kuwajengea uwezo wa kutambua bidhaa halisi na kuepuka kununua au kutumia bidhaa zisizo na viwango vinavyotakiwa.

Mbanga alisema Maonesho ya Mbeya City Expo yamekuwa jukwaa muhimu la kuifikia jamii kwa karibu na kutoa elimu inayolenga kuongeza uelewa kuhusu sheria za ushindani na hatua zinazochukuliwa dhidi ya wafanyabiashara wanaojihusisha na usambazaji wa bidhaa bandia.

“Tunatumia maonesho haya kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwaelimisha kuhusu hatari za bidhaa bandia na kumlinda mlaji. Lengo letu ni kuhakikisha watumiaji wanakuwa na taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya maamuzi bora wanaponunua bidhaa mbalimbali sokoni,” alisema Mbanga.

Aliongeza kuwa FCC itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa biashara na vyombo vya usalama katika kudhibiti bidhaa bandia zinazoingia sokoni, huku ikiendelea kuhamasisha wananchi kutoa taarifa wanapobaini uwepo wa bidhaa zinazotiliwa shaka.

Maonesho ya Mbeya City Expo 2026 yamewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali za uchumi, biashara na uwekezaji, huku yakitoa fursa kwa taasisi za umma na binafsi kuonesha huduma, bidhaa na mafanikio yao kwa wananchi. Kupitia ushiriki wake, FCC imeendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya kulinda walaji na kujenga mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki .


Share:

MRADI WA FOLUR KUSHUSHA MIONGOZO YA KIMATAIFA MAENEO YA UTENDAJI ZANZIBAR








Na Anangisye Mwateba, Zanzibar

MRADI wa Mifumo ya Chakula, Matumizi ya Ardhi na Urejesho wa Mandhari ya Misitu nchini Tanzania (FOLUR), unatarajia kutoa mafunzo maalum kwa viongozi wa serikali za vijiji na shehia mbalimbali visiwani Zanzibar. Hatua hiyo inalenga kujenga uwezo wa kiutendaji na kuhakikisha jamii inatekeleza shughuli za mradi huo kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.


Akifungua mafunzo hayo kwa maafisa ugani wa kilimo na misitu upande wa Zanzibar, Mratibu wa mradi huo, Bi. Miza Suleiman Khamis, alisema dhumuni kubwa ni kuwawezesha watendaji hao kubaini, kuepuka au kupunguza athari hasi zinazoweza kujitokeza kabla hazijaletea madhara wanajamii na mazingira yao.


Kwa upande wake, Msimamizi wa Kitengo cha Jinsia, Usalama wa Mazingira na Jamii wa mradi huo, Bw. Revocatus Kadoshi, alibainisha kuwa viongozi wa shehia na maafisa ugani watafundishwa miongozo minne mikuu.

Miongoni mwa miongozo hiyo ni Mpango wa Usimamizi wa Mazingira na Jamii (ESMP), unaohusu udhibiti wa matumizi ya rasilimali na kuzuia uhamishaji wa watu usio wa hiari.


Bw. Kadoshi alifafanua kuwa mwongozo huo unalenga kudhibiti na kupunguza athari za kimazingira na kijamii wakati wa utekelezaji wa mradi. Aliongeza kuwa hatua hiyo inaenda sambamba na matakwa ya Mwongozo wa Sera na Taratibu Jumuishi za Ulinzi wa Kijamii za Shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani (WWF).


"Viongozi hawa pia watafundishwa kuhusu Usimamizi Shirikishi wa Visumbufu. Huu unalenga kulinda afya na usalama wa jamii kwa kudhibiti athari zitokanazo na matumizi ya viuatilifu na mbolea," alisema Bw. Kadoshi.


Aidha, mafunzo hayo yatahusisha mbinu za usimamizi wa mazingira zinazohakikisha ustawi wa jamii, usalama mahali pa kazi, pamoja na usafi wa mazingira wakati wote wa utekelezaji wa shughuli za mradi huo.

Vilevile Aliongeza kuwa, ili kuhakikisha usalama wa jamii, mradi umeweka utaratibu maalumu wa kupokea nakufanyia kazi malalamiko kutoka kwa mwanajamii au kikundi cha kijamii kuhusiana na shughuli zinazotekelezwa na mradi. Hii inalwnga kuhakikisha jamii inashiriki vema kwenye shighuli za mradi na wanakuwa na nafasi ya kutoa dukuduku au lalamiko wakati wowote.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUNI 4,2026

Magazeti



Related StoriesView all
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger