Wednesday, 4 March 2026

ALIYEKATA TAMAA, ASHANGAA KUPANDISHWA CHEO GHAFLA




Je, kuna kitu kinaumiza kama kufanya kazi kwa bidii halafu ukaonekana kama hauonekani? Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Martin, kijana wa miaka thelathini kutoka Westlands, ambaye alifanya kazi katika kampuni ya bima kwa zaidi ya miaka mitano bila kupandishwa cheo wala kuongezewa mshahara.

Share:

NAIBU WAZIRI WANU AAGIZA CHUO MZENGA KUTOA MAFUNZO YANAYOENDANA NA UCHUMI WA ENEO


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameutaka uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Mzenga, kilichopo Kata ya Mzenga, Wilaya ya Kisarawe, kuhakikisha kinatoa mafunzo katika fani zinazoendana na shughuli za kiuchumi za eneo hilo.

Mhe. Wanu ametoa agizo hilo Machi 03, 2026, wilayani Kisarawe wakati wa ziara ya ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi inayotekelezwa na Wizara katika wilaya hiyo.

Amewataka viongozi wa wilaya na wananchi wa eneo hilo kuona umuhimu wa mafunzo ya ujuzi na hivyo kuhamasisha vijana kujiunga na chuo hicho ili kupata ujuzi utakaowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.

Amesema chuo hicho, pamoja na vyuo vingine vya maendeleo ya wananchi, vinapaswa kuzingatia mahitaji halisi ya kiujuzi ili vijana waweze kujiunga kwa wingi.

“Mmesema hapa mnazalisha zao la korosho, ufuta na mihogo; kwa nini sasa msianzishe kozi ya kusindika mazao hayo? Hii itawamasisha vijana kujiunga na chuo kwa kuwa wanasoma kile wanachofanyia kazi,” amesema Mhe. Wanu.

Aidha, ameutaka uongozi wa chuo hicho kusimamia ipasavyo mifumo ya usimamizi wa watumishi ili kuimarisha uwajibikaji.

Akiwa wilayani humo, Mhe. Wanu pia amekagua ujenzi wa VETA Kisarawe na kusema kuwa Serikali inaendelea kujipanga kupata rasilimali fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa chuo hicho ili malengo ya kutoa ujuzi kwa wananchi yafikiwe.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mhe. Petro Magoti, amemuhakikishia Naibu Waziri Wanu ushirikiano katika kusimamia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa, ikiwemo kuhakikisha huduma za umeme na maji zinafika katika eneo la chuo ili kurahisisha hatua inayofuata ya ujenzi.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO MACHI 4,2026




Magazeti
Share:

Tuesday, 3 March 2026

FCC KUADHIMISHA SIKU YA HAKI YA MLAJI KWA KUTOA ELIMU KWA UMMA



Na Emmanuel Mbatilo, Dar es Salaam

Tume ya Ushindani (FCC) imetangaza kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Haki ya Mlaji Duniani kwa kuendesha kampeni maalum ya utoaji elimu kwa walaji na wafanyabiashara ili kuongeza uelewa wa haki na wajibu wao katika soko.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Khadija Ngasongwa amesema maadhimisho hayo yanalenga kuwawezesha walaji kufanya maamuzi sahihi wanaponunua bidhaa au huduma, pamoja na kuwahamasisha kuchukua hatua pale wanapobaini ukiukwaji wa sheria.

Amesema elimu hiyo pia itawalenga wafanyabiashara kwa kuwajengea uelewa kuhusu wajibu wao wa kumlinda mlaji na kuzingatia matakwa ya sheria katika utoaji wa bidhaa na huduma.

Kwa mujibu wa FCC, kilele cha maadhimisho hayo kitafanyika Machi 31, 2026 katika Hoteli ya Johari Rotana, jijini Dar es Salaam, ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga.

Amesema katika maadhimisho ya mwaka huu, Tume hiyo imejikita kutoa elimu kupitia vipindi vya redio na televisheni, pamoja na majukwaa ya mitandao ya kijamii ili kuwafikia wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, FCC itaendesha kliniki za walaji katika mikoa ya Pwani, Dodoma, Musoma, Njombe na Tanga kwa lengo la kupokea na kushughulikia hoja, malalamiko na changamoto zinazowakabili walaji.

Sambamba na hilo, Machi 10, 2026 Tume hiyo itaendesha semina kwa wafanyabiashara na taasisi zinazotumia mikataba ya walaji (Standard Form Consumer Contracts) katika ofisi zake za Dar es Salaam, ili kuwajengea uelewa kuhusu umuhimu wa mikataba inayozingatia haki za mlaji.

Vilevile, Machi 11, 2026 kutafanyika semina kwa wadau wa sekta ya ujenzi wakiwemo wazalishaji wa nondo, bati, nyaya za umeme na rangi za majumbani, pamoja na vyama vya kibiashara na wadhibiti wa kisekta.

Mbali na semina hizo, FCC itatumia magari ya matangazo (road shows) kufikisha elimu kwa wananchi moja kwa moja katika maeneo yao.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu huyo amewahimiza wananchi wenye changamoto zozote zinazohusiana na bidhaa au huduma kufuatilia vipindi vya elimu vitakavyorushwa na vyombo vya habari, kuhudhuria kliniki za walaji na kutumia fursa hiyo kuwasilisha malalamiko yao kwa ajili ya kupatiwa ufafanuzi au hatua stahiki.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger