Monday, 30 March 2026

TUNAHITAJI MATOKEO YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA PAMOJA.DKT JINGU




Na WMJJWM – Dar Es Salaam

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. John Jingu amasisizitiza kasi katika utekelezaji wa mradi wa kukuza usawa wa kijinsia pamoja na kuleta matokeo yenye tija kwa jamii.

Dkt. Jingu amesema hayo Machi 27, 2026, Jijini Dar es Salaam wakati akiongoza kikao cha Kamati elekezi ya utekelezaji wa mradi wa Kukuza Usawa wa Kijinsia Tanzania (PAMOJA) kwa lengo la kujadili na kuimarisha uratibu na uendeshaji wa mradi huo.

Dkt. Jingu amesema katika utekelezaji wa mradi huo, kila mmoja ahakikishe anatimiza majukumu yake kwa ufanisi kwa nafasi aliyonayo, ili kuleta matokeo tarajiwa ili hatimaye mradi uache alama chanya kwa jamii.

Kwa upande wake Katibu wa Kamati hiyo ambaye ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawaka na Makundi Maalum Victor Nkya amesema mradi huo utawanufanisha wanawake kwa kupitia mikopo ili kuendesha shughuli za kiuchumi na kuongeza kipato cha familia.

“Mradi huu utawafikia wanawake wajasiriamali ili kukuza na kuimaridha Uchumi wa kaya jamii na familia kupitia mikopo yenye masharti nafuu, kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia kuipitia vikundi vya wanawake mtaani na sokoni, pamoja na kuimarisha malezi hatimaye kutakuwa na Watoto wenye maadili na wenye kuleta tija katika jamii” amesema Nkya.

Mradi wa PAMOJA unatekeleza kwa Tanzania bara na Zanzibar, ukilenga kuimarisha usawa wa kijinsia, kupunguza na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia, kuongeza fursa za kiuchumi kwa wanawake, kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kuimarisha malezi nchini.





Share:

Sunday, 29 March 2026

SOAT YAZINDULIWA, YAAHIDI KUONGEZA MAPATO YA UTALII KUFIKIA BILIONI 790

Na Mussa Juma,Arusha.

Jumuiya ya Wawekezaji Mahiri katika maeneo ya Wanyamapori(SOAT) imezinduliwa rasmi jijini Arusha, huku wawekezaji hao wakiahidi kushirikiana na serikali  kuendeleza  Utalii na kuhakikisha ndani ya miaka 20 wanaingizia taifa kiasi cha shilingi Bilioni 790 kutokana uwekezaji wao.

Akizungumza katika Uzinduzi huo, Mtendaji mkuu wa SOAT, Erasmus Tarimo alisema wanachama wa SOAT wanatarajia kuwekeza katika miradi mbali mbali kwa jamii kwa kiasi cha USD 50 milioni kwa kipindi cha miaka ishirini sawa na shilingi bilioni 125.

Tarimo alisema kutakuwa na uwekezaji katika ulinzi wa usiopungua dola milioni 20  ili kukabiliana na majangili kwa kipindi cha miaka 20 na  uwekezaji katika utafiti dola milioni 7.

Alisema SOAT,  inatarajia Kuimarisha mfumo wa udhibiti ili kuhakikisha usimamizi imara na mazingira yanayotabirika ya uwekezaji wa muda mrefu unaotegemea utalii wa wanyamapori.

“ Mheshimiwa mgeni rasmi Dira yetu sisi ni kuunganisha wanyamapori, jamii na Utalii kwa ajili mafanikio endelevu ya kiuchumi  na Misheni ni Kushirikiana kulinda wanyamapori, kuinua jamii katika kuhifadhi na kuendeleza utalii endelevu”,alisema.

Tarimo alisema, Malengo ya jumuiya hiyo kuongeza wigo wa chaguo kwa wateja kuhusiana na shughuli za matumizi na sisizo za matumizi, kutekeleza uwekezaji bunifu kaatika utalii na kuhimiza uwekezaji mbadala na kuendeleza na kutangaza bidhaa za utalii Pamoja na kudumisha ubora wa maeneo ya uhifadhi.

“ Pia tunakusudia kuendeleza uwekezaji toshelezi ili kuwekeza katika kujenga miundombinu stahiki katika maeneo ya hifadhi,kuimarisha uhifadhi , manufaa ya kijamii na kiuchumi pamoja kuzalishamapato zaidi na kutumia rasilimali za wanyamapori kwa kutoa shughuli mbalimbali endelevu za matumizi ya wanyamapori”, alisema.

Akizindua umoja huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA, Meja Jenerali ( Mstaafu) Hamis Semfuko alipongeza wawekezaji hao wa maeneo la Uwekezaji mahiri wa wanyamapori(SWICA) kuanzisha umoja huo ambao utasaidia sana kuimarisha mawasiliano na serikali.

Alisema tangu kuanza utaratibu wa SWICA  Serikali imekuwa ikinufaika sana na uwekezaji mahiri katika maeneo ya Wanyamapori zaidi ya mara tisa kwa sasa.

Alisema Mfumo wa uwekezaji mkakati wa SWICA ulianza kutekelezwa kwa kuanzia na wawekezaji sita Kwa kiasi cha uwekezaji wenye thamani ya USD milioni 278 sawa na shilingii bilioni 696 .

Meja Generali mstaafu , Semfuko alisema awali SWICA ilikuwa na  wawekezaji  sita na sasa kuna wawekezaji 13 na wapo wengine ambao wanataka kuwekeza hatua ambayo inaonesha umuhimu wa uwekezaji huu mahiri katika sekta ya Utalii.

Alisema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa akifuatilia sana uwekezaji katika SWICA na anaamini kuwa unakwenda kulinufaisha sana Taifa lakini pia kuchangia kupunguza migogoro baina ya wanyamapori na binaadamu na kuongeza ajira na mapato.

Awali Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori(TAWA), Mlage Yussuf Kabange alisema alisema maeneo ya SWICA yapo ndani ya maeneo ya TAWA hivyo,SOAT itapewa ushirikiano mkubwa kuhakikisha inafikia malengo yake.

Kamishna  Kabange alisema TAWA inaamini kukiimarishwa ushirikiano, lengo la Serikali kufikisha watalii milioni nane ifikapo mwaka 2030 litafanikiwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa SOAT, Makamu Mwenyekiti Martha Lucumay  alisema wamejipanga kufanyakazi na serikali lakini wanaomba pia changamoto kadha ikiwepo za kikodi kufanyiwa kazi.

Akizungumza katika uzinduzi huo,mmoja wa Wakurugenzi wa kampuni ya Mwiba Holdings Ltd ambayo ni miongoni mwa wanachama waanzishilishi wa SOAT.Nicolaus Negri alishukuru Serikali kufika katika uzinduzi huo na kuahidi SOAT itafanyakazi kwa kushirikiana na Serikali.

Negri pia aliwashukuru viongozi wa chama cha mawakala wa Utalii nchini(TATO) chama cha Wawindaji wa Utalii nchini(TAHOA), Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori(TAWIRI) na wadau wengine wa Utalii kushiriki katika uzinduzi huo amba oni muhimu katika kuboresha sekta ya uhifadhi na Utalii nchini.

Maeneo ambayo yanawekezwa kupitia SWICA  ni Eneo la kaskazini la pori la akiba la Maswa,Maswa Kimali ,Maswa Mbono;Mapori ya akiba ya Grumeti na Ikorongo;.Pori la akiba la Mkungunero,Pori Tengefu la Ziwa Natroni na Kitalu cha LL1 katika pori la akiba la Selous.

Share:

MAHUSIANO YALIVYOGEUKA FURAHA BAADA YA KUTUMIA MBINU HII



Hawa watu wengine hawajui kilichonitokea. Nilikuwa na uhusiano wa mapenzi niliyefikiria ulikuwa wa kudumu. Tulikutana mapema, tulipendana sana na tukapanga maisha yetu ya pamoja. Kila kitu kilionekana kuwa cha ndoto.

Lakini ndani ya miezi michache, mambo yaligeuka kuwa ya kutisha. Kila mpenzi niliyekuwa nikiwa naye alianza kupata matatizo makubwa. Baada ya miezi kadhaa, aliaga dunia kwa sababu zisizoeleweka. Nilishangaa na kuhisi hofu isiyo na kifani.

Share:

KISA CHA MTOTO NELSA CHAREJEA: MAPENZI YA SIRI, FEDHA ZA MICHANGO NA TASWIRA MITANDAONI


Kisa kilichowahi kugusa mioyo ya Watanzania kinarejea tena mezani, kikichorwa upya na mvutano mpya:Mtoto Nilsa enzi za uhai wake (Mungu amrehemu) akiwa pamoja na Baba yake, Simon Bryson Mnyola wanashughulika na mjadala mkali kuhusu matumizi ya fedha za michango ya watanzania na namna taswira ya mtoto inavyo tumika mitandaoni.


Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Kisa kilichowahi kugusa mioyo ya Watanzania kuhusu mtoto Nilsa, aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya kichwa kujaa maji na baadaye kufariki dunia, kimerudi tena katika mjadala wa umma kufuatia kuibuka kwa tuhuma mpya kutoka kwa mama mzazi wa mtoto huyo Jesca.

Kwa mujibu wa maelezo ya mama huyo, aliyewasiliana na chombo hiki kwa njia ya simu, anadai kuwa aliyekuwa mume wake Simon Bryson mnyola (baba nilsa)

alitumia kisa cha mtoto wao kama fursa ya kujipatia fedha kupitia michango ya wananchi, huku akijenga taswira ya kuwa mzazi mwenye upendo mkubwa mitandaoni, jambo ambalo anadai halikuwa halisi.

Jesca anadai kuwa wakati wa ugonjwa wa mtoto, baba huyo alimchukua mtoto na kupiga naye picha ambazo baadaye zilisambazwa mitandaoni kwa lengo la kuibua huruma kwa umma na kuchochea michango ya matibabu.

Kutokana na hali hiyo, Watanzania wengi waliguswa na kuanza kutoa misaada ya fedha.

Hata hivyo, mama huyo anasema baada ya kifo cha mtoto, jumla ya fedha zilizopatikana zilifikia takribani shilingi milioni 17, ambapo anadai alipewa kiasi cha shilingi milioni tatu pekee kwa ajili ya kulipia madeni ya matibabu, huku fedha zilizobaki zikibaki chini ya usimamizi wa baba huyo bila ushirikishwaji wa pamoja.

Aidha, anaeleza kuwa baada ya tukio hilo, mawasiliano kati yao yalivunjika na juhudi zake za kuomba msaada zaidi hazikupata ushirikiano.

Badala yake, anadai kuwa baba huyo ameendelea kutumia jina la mtoto huyo kujitangaza katika shughuli zake za kibiashara mitandaoni.

Katika hatua nyingine, mama huyo anadai kuwa kulikuwa na jitihada za kuonyesha hadharani kuwa wana uhusiano mzuri, ikiwa ni pamoja na kupiga picha pamoja na kuchapishwa mitandaoni, jambo ambalo anasema lilifanyika kwa shinikizo ili kulinda taswira ya baba huyo mbele ya umma.

Wakati huo huo, uchunguzi wa maoni ya mitandaoni unaonyesha kuwepo kwa mgawanyiko wa mitazamo miongoni mwa wananchi, ambapo baadhi wanaendelea kumuunga mkono baba huyo, huku wengine wakianza kuibua maswali kuhusu uwazi wa matumizi ya fedha za michango pamoja na nafasi ya mama mzazi katika mchakato mzima.

Hata hivyo, jitihada za kumpata baba anayehusishwa na tuhuma hizo ili kutoa ufafanuzi wake hazijafanikiwa hadi wakati wa kuchapishwa kwa habari hii.

Hapo chini nimekuwekea baadhi ya maoni ya waliokuwa mashabiki wa Nilsa kwenye mitandao ya kijamii ambapo wengi wameonesha hisia zao moja kwa moja









Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MACHI 29,2026


Magazeti







Share:

Saturday, 28 March 2026

PROF. SHEMDOE AWAASA WALIMU 150 KUZINGATIA MAFUNZO NCHINI INDIA ILI KUWA MAHIRI NA KULETA MAGEUZI YA ELIMU NCHINI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewataka walimu 150 wa Amali za Kihandisi wanaokwenda India kuongeza umahiri kuhakikisha wanajifunza kwa bidii ili watakaporejea wawajengee uwezo walimu wengine, na hatimaye kutoa mchango utaokuwa na tija katika kuharakisha mageuzi ya elimu nchini.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo Machi 26, 2026 kwa walimu hao waliopata fursa ya kwenda nchini India kuongeza umahiri, wakati wa hafla ya kuwaaga walimu hao iliyofanyika Jiji Dar es Salaam.

“Nendeni mkajifunze kwa bidii na nidhamu, mkazingatie maadili, jifunzeni mbinu mpya na muwe tayari kuzitumia mtakaporejea, hivyo tunatarajia mtakaporejea mtakuwa nguzo ya kuboresha elimu ya amali katika shule zenu na chanzo cha maarifa kwa walimu wengine,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesisitiza kuwa mpango wa mafunzo hayo ni utekelezaji wa sera ya elimu ya lazima ya miaka 10, unaolenga kujenga umahiri wa ufundishaji na kuandaa kizazi cha wataalamu wenye ushindani wa kimataifa, huku akiwataka walimu hao kutambua nafasi yao kama daraja kati ya sera na utekelezaji darasani.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameishukuru Serikali chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia walimu hao fursa ya mafunzo, akisisitiza kuwa ni ishara ya dhamira ya dhati ya kuendeleza mageuzi ya elimu, huku akipongeza mshirikiano wa viongozi wa wizara za kisekta katika kulitekeleza kwa ufanisi.

Wanufaika wa mafunzo hayo, akiwemo Mwalimu Judith Faustine wa Uhandisi Ujenzi katika Shule ya Sekondari Mwadui Ufundi na Mwalimu Jacob Mwalyego wa fani ya Uashi katika Shule ya Sekondari ya Ufundi Mbogwe, wameishukuru Serikali kwa kuwapatia nafasi hii ya kipekee. Wamesema ni heshima kubwa na fursa ya kuongeza maarifa yatakayowawezesha kuendeleza mageuzi ya elimu nchini.

Kamishna wa Elimu Dkt. Lyabwene Mtahabwa ameeleza kuwa mafunzo hayo ya mwezi mmoja yamewahusisha walimu kutoka mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na viongozi wa ngazi ya elimu mkoa kutoka mikoa tisa, hivyo
kuiwezesha Tanzania kuandika ukurasa mpya katika historia ya elimu ya ufundi kwa kupeleka walimu 150 wa Amali za Kihandisi nchini India ambao  wakirejea watasimamia kikamilifu uendelevu wa mafunzo nchini.








Share:

Friday, 27 March 2026

SERIKALI YA TANZANIA YASAINI MAKUBALIANO YA UFADHILI WA SAMIA SCHOLARSHIP NA CHUO KIKUU CHA LIMERICK


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Limerick cha nchini Ireland wamesaini hati ya makubaliano ya utekelezaji wa ufadhili wa Samia Scholarship Extended, utakaowawezesha wanafunzi 32 kusoma katika chuo hicho.
Makubaliano hayo yamesainiwa leo Machi 26, 2026 jijini Dar es Salaam, yakishuhudiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Adolf Mkenda pamoja na ujumbe kutoka ubalozi wa Ireland nchini na viongozi wa chuo hicho.

Akizungumza katika hafla hiyo, Profesa Mkenda amesema ufadhili huo ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha elimu kwa kuandaa wataalamu wa sayansi na teknolojia watakaoendana na mahitaji ya dunia ya sasa.

Amesema ushirikiano huo umefanyika wakati muafaka ambapo Tanzania inaendelea kujenga uchumi unaotegemea maarifa na ubunifu, huku ukilenga kuwawezesha vijana kupata elimu bora, uzoefu wa kimataifa na ujuzi wa kisasa.

Aidha, chuo hicho kimetoa punguzo la ada kwa asilimia 50 kwa wanafunzi watakaojiunga kupitia mpango huo.

Profesa Mkenda alibainisha kuwa Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa Samia Scholarship katika fani za Sayansi ya Data, Akili Unde (AI) na taaluma zinazohusiana, ikiwa ni mkakati wa kuwajengea vijana uwezo katika teknolojia mpya.

“Tayari tumewapeleka wanafunzi 34 nchini Ireland, ambapo 32 wanasoma katika Chuo Kikuu cha Limerick na wawili katika Chuo cha Cork,” amesema.

Ameongeza kuwa wanafunzi hao ni sehemu ya ufadhili wa wanafunzi 50 waliofanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita, huku wengine 16 wakiwa tayari wamejiunga na vyuo vikuu nchini Afrika Kusini.

Kwa upande wake, Balozi wa Ireland nchini, Nicola Brennan, amesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika elimu bora ili kukidhi mahitaji ya ajira kwa idadi kubwa ya vijana inayotarajiwa kuongezeka kufikia mwaka 2050.

Amesema Tanzania ina rasilimali watu yenye nguvu na mazingira ya utulivu yanayowezesha maendeleo, lakini uwekezaji mkubwa katika elimu ni muhimu ili kuendana na ongezeko la watu.

Naye Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Limerick, Colin Fitzpatrick, amesema chuo hicho kinajikita katika mafunzo ya vitendo na kuwapatia wanafunzi uzoefu kupitia ushirikiano na kampuni kubwa za kimataifa.

Amesema hatua hiyo itawasaidia wanafunzi kutoka Tanzania kupata ujuzi wa nadharia na vitendo katika mazingira halisi ya kazi, hasa katika sekta ya teknolojia inayokua kwa kasi duniani.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger