Friday, 11 September 2026
SHEIKH WA DODOMA ATOA AGIZO LA DUA MAALUMU MISIKITINI
TANZANIA, MAREKANI KUENDELEZA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA ZA MAENDELEO
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) akisalimiana na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.

Thursday, 10 September 2026
MATUNDA YA AWAMU YA SITA: VETA KUZINDUA SIMU YA ‘UJUZI Pro’
Wednesday, 9 September 2026
WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO YA UBUNIFU UNAOMLENGA MTUMIAJI (HCD) KUKABILIANA NA HABARI POTOFU

Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, amesema mafunzo hayo yanasisitiza umuhimu wa kutumia mtazamo unaomlenga mtumiaji katika kutafuta suluhisho la changamoto ya taarifa potofu.
Amesema mtazamo huo unazingatia mahitaji, matarajio, uzoefu na tabia za wananchi wanaokumbwa na changamoto ya taarifa potofu, hatua inayolenga kuhakikisha suluhisho zinazobuniwa zinakidhi mahitaji halisi ya watumiaji wa taarifa.
Kwa upande wao, washiriki wa mafunzo hayo wamesema yatawasaidia kupata uelewa na mbinu mbalimbali zitakazowasaidia kutambua, kuchambua na kukabiliana na habari potofu na taarifa za upotoshaji katika kazi zao za kila siku.

















































































