Monday, 27 July 2026

JENERALI MSTAAFU JWTZ AWATAKA VIJANA KUWA WAZALENDO NA KULINDA TAIFA

 

Brigedia Jenerali mstaafu Wilfred Kabunda amewataka Watanzania, hususan vijana, kuendelea kuipenda na kuilinda nchi kwa uzalendo mkubwa. 

“Niwasihi Watanzania, hususan vijana wa taifa hili, wawe wazalendo kwa nchi yao kwa sababu hatuna Tanzania nyingine, ni hii tuliyonayo. Tutunze amani tuliyonayo kwa wivu mkubwa sana,” alisema. 

Jenerali Kabunda, alisema hayo katika Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa, Julai 25 katika uwanja wa mashujaa Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma baada ya kukamilika kwa shughuli za kuwakumbuka mashujaa zilizoongozwa na rais Samia Suluhu Hassan ambaye aliweka mkuki na ngao katika mnara wa mashujaa.

Jenerali kabunda ambaye alikuwa mwakilishi wa mashujaa waliopigana Vita ya Kagerahivyo kuweka shoka katika adhimisho hilo , akiwa miongoni mwa makomandoo waliopigana Vita ya Kagera, alisema mafanikio ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika vita hiyo yalitokana na maandalizi madhubuti ya mafunzo na mshikamano wa Watanzania wote.

Alisema Brigade 208 ilikuwa imepata mafunzo ya kutosha kabla ya kuingia vitani, hali iliyowapa uwezo mkubwa wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

“Mbali na mafunzo, hamasa ya Watanzania ilikuwa kubwa. Kila Mtanzania aliunga mkono vita hiyo na kujitolea kwa namna mbalimbali. Hilo lilitupa nguvu na morali ya kupambana hadi ushindi ukapatikana,” alisema.

Kwa upande wake, Brigedia Jenerali mstaafu Mary Hiki alisimulia namna alivyoshiriki Vita ya Kagera akiwa mwanamke pekee katika kundi la mawasiliano. 

Alisema Oktoba mwaka 1978 alikuwa sehemu ya Brigade 201 iliyokuwa ikifanya mazoezi Arusha kabla ya kutangazwa rasmi kwa Vita ya Kagera na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. 

Mary alisema kutokana na umuhimu wa mawasiliano wakati huo, aliendelea kutekeleza majukumu yake kwa kutumia mfumo wa redio, akifanya kazi kuanzia Mutukula hadi ndani ya Uganda kabla ya kurejeshwa nyuma kutokana na mazingira ya operesheni na kuwa mwanamke pekee katika eneo hilo.

“Ukiizingatia wakati ule mawasiliano ilikuwa ni njia ya redio pekee yake, ilikuwa hakuna mawasiliano mengine. Baadaye tukasogea mpaka Mutukula na kisha kuvuka Mutukula pande wa Uganda,” alisema. 

Baada ya ushindi wa vita, alisema aliendelea kufanya kazi nchini Uganda katika Ikulu ya Entebbe kuanzia mwaka 1979 hadi 1980 wakati Tanzania ikiendelea kusaidia kurejesha utulivu nchini humo. 

Alikumbuka mapokezi makubwa yaliyofanyika Bwananyanja Julai 15, 1979 ambapo Baba wa Taifa na Amiri Jeshi Mkuu wa wakati huo, Mwalimu Nyerere aliwapokea wanajeshi waliorejea kutoka vitani huku Watanzania wakisherehekea ushindi huo kwa furaha kubwa. 

Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa huadhimishwa kila mwaka Julai 25 kwa lengo la kuwakumbuka na kuwaenzi mashujaa waliotoa mchango mkubwa katika historia ya Tanzania hususani katika harakati za kupigania uhuru, kulinda mipaka ya nchi na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Sherehe hizo za kitaifa zilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa serikali wakiwemo Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi, Makamu wa Rais, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi na Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba. Pia walikuwapo viongozi wa dini, mabalozi na wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Aidha Sherehe hizo zilipambwa na gwaride la heshima lililopiga ala ya ‘Last Post’ huku wanajeshi wakishusha silaha zao kwa ishara ya maombolezo. Aidha, mizinga miwili ilifyatuliwa na taifa likasimama kimya kwa dakika moja kuwakumbuka mashujaa wote waliopoteza maisha wakitumikia taifa. 

Baada ya kupokea salamu ya heshima ya Rais kutoka kwa gwaride, Rais Samia aliweka mkuki na ngao kwenye mnara huo. Rais Samia alifuatiwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda, aliyeweka sime, huku Kiongozi wa mabalozi nchini, Balozi wa Burundi, Leontine Nzeyimana aliweka shada la maua kuwakumbuka mashujaa hao. 

Viongozi wa dini pia waliongoza sala na dua maalumu kuwaombea mashujaa waliopoteza maisha, huku wakiiombea Tanzania iendelee kudumisha amani, umoja, mshikamano na maendeleo.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 27,2026


Magazeti











Share:

Sunday, 26 July 2026

RC MBONI MHITA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM, 'RAIS SAMIA AMETOA TRILIONI 1.9 SHINYANGA'



Na Marco Maduhu, SHINYANGA

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita, amewasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba, 2025 hadi Juni 2026.

TAZAMA VIDEO👇👇

Amewasilisha taarifa hiyo leo kwa Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Shinyanga ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo Mabala Mlolwa.

Mhita akisoma taarifa hiyo, amesema kwa kipindi cha uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan wamepokea kiasi cha fedha sh. Trilioni 1.9 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo.
Amesema, katika mapokezi ya fedha hizo wananchi wa Mkoa huo, wameshuhudia maendeleo ya haraka katika Nyanja za uzalishaji katika sekta ya kilimo, mifugo, madini, viwanda , biashara, pamoja na huduma za jamii, Afya, Elimu, Nishati na Maji.

UTEUZI WA VIONGOZI

Amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kumteuwa Mheshimiwa Patrobas Katambi kuwa Waziri wa Mambo ya ndani na Mheshimiwa Salome Makamba kuwa Naibu Waziri wa Nishati.


WASIFU WA MKOA

Amesema mkoa huo wa Shinyanga una ukubwa wa kilomita za mraba elfu 18,557 na unajumla ya watu milioni 2,2 wanaume wakiwa milioni 1.102 na wanawake milioni 1.13 kwa mujibu wa sense ya watu na makazi ya mwaka 2022.
HALI YA UCHUMI YA MKOA

Amesema, mkoa huo umeendelee kuimarika ambapo pato halisi limeongezeka kutoka sh. bilioni 7.5 mwaka 2021 hadi sh.bilioni 9.2 mwaka 2026 sawa na ukuaji wa asilimia 22.

PATO LA MTU MMOJA

Amesema, pato la mtu mmoja mmoja limeongezeka kutoka sh. Milioni 1.8 mwaka 2021 hadi Sh.milioni 1.9 mwaka 2026 sawa na ongezeko la asilimia 7.

SEKTA YA AFYA

Amesema katika kuendelea kuimarisha sekta ya afya mkoa huo umepokea kiasi cha fedha sh. bilioni 99.0 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za afya.

Kukamilisha hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo iliyopo Mwawaza, kwa kujenga majengo ya EMD, OPD, Jengo la utawala, Jengo la Uraibu wa Madawa ya kulevya na kituo cha tiba jumuishi, kununua vifaa tiba, ujenzi wa nyumba za watumishi pamoja na kuongezeka kwa madawa na vitendanishi.

ELIMU

Amesema, katika kuinua ubora wa elimu katika ngazi zote Mkoa huo umepokea sh. bilioni 205.2 kwa ajili ya kujenga na kukarabati miundombinu ya elimu na kuongeza idadi ya walimu.

MAJI

Katika kuimarisha upatikanaji wa maji kwa wananchi wote kwamba mkoa huo umepokea sh. bilioni 163.3 ili kuhakikisha kaya nyingi zinaunganishwa na huduma ya maji, na kwamba upatikanaji wa maji kwa wananchi kwa sasa ni asilimia 79 kutoka 63 kwa maeneo ya mijini na vijijini asilimia 68 kutoka 51.

KILIMO

Kwamba wameendelea na ujenzi wa Skimu za bwawa la Nyida na Melenge, kuimarisha huduma za ugani kwa kununua vitendea kazi ikiwamo Pikipiki, vipima udongo na vishikwambi.

MIFUGO

Wameongeza usambazaji wa dawa za ruzuku za kuogeshea mifugo, kuimarisha huduma ugani kwa kugawa pikipiki 534 kwa ajili ya maafisa mifugo, pamoja na kuongeza minada ya mifugo kutoka 25 hadi 30.

MADINI

Kuongezeka kwa utoaji wa lessen kwa wachimbaji wadogo kutoka lesseni 332 hadi 1,766.

MIUNDOMBINU

Kuongezeka kwa mtandao wa barabara za lami kwa kilomita 57 ,barabara za changarawe kilomita 454, na kukamilika kwa ujenzi wa madaraja 18 ,makaravati 2,113, na pamoja na kuendelea kwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kahama- Bulyanhulu kilomita 73 kwa gharama ya sh.bilioni 100.6 na ujenzi umefikia asilimia 78.21.

NISHATI

Amesema Rais Dk Samia ametoa bilioni 426 kwa ajili ya kusambaza umeme vijijini, pamoja kuendelea kwa ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme jua katika kijiji cha Ngunga wilayani Kishapu kwa kuzalisha Megawati 100 kwa awamu ya pili.

UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI

Kuongezeka kwa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo kiasi cha sh. bilioni 11.3 zimetolewa kwa vikundi 941 vya wanawake, Vijana 599 na watu wenye ulemavu vikundi 110.

TASAF

Zimetolewa fedha sh. bilioni 59.5 kwa walengwa elfu 35,055 kutekeleza miradi 77 ya miundombinu ya elimu, afya, barabara, pamoja na kuwezesha walengwa elfu 15,103 kujiongezea kipato kupitia ufugaji na kilimo.

UTAWALA BORA

Mkoa umepokea bilioni 22,2 kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya utawala na nyumba za watumishi, katika Hamashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Shinyanga DC, Ushetu na ujenzi wa Jengo la Ofisi ya mwendesha Mashtaka.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa, amesema wamempongeza Mkuu huyo wa mkoa kwa usimamizi mzuri wa fedha za serikali na kuitendelea haki ilani ya uchaguzi ya Chama hicho.

TAZAMA PICHA👇👇
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba 2025 hadi Juni 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba 2025 hadi Juni 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba 2025 hadi Juni 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba 2025 hadi Juni 2026.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akizungumza.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akizungumza.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa akizungumza,

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger