Monday, 10 August 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 10, 2026



Magazetini Leo



Share:

Sunday, 9 August 2026

AGCOT YAMWEZESHA NEEMA KUTOKA MKULIMA HADI MWENYE KAMPUNI YA MAZAO




Na Sheila Ahmadi, Dodoma

Mwanzilishi na Mkurugenzi wa kampuni inayojihusisha na uzalishaji wa mazao ya mboga mboga mkoani Iringa, Neema Mwamoto amesema uwezeshaji alioupata kupitia AGCOT umekuwa sehemu muhimu ya safari yake kutoka kuwa mkulima wa kawaida hadi kuanzisha kampuni inayolenga kukuza uzalishaji na masoko ya mazao ya kilimo.

Neema amesema kuwa safari yake katika kilimo ilianza akiwa mkulima wa kawaida, ambapo alianza kulima mazao mbalimbali kabla ya kuingia katika mfumo wa kilimo cha kibiashara na baadaye kufanya kazi kama mkulima mkataba katika kampuni ya (GBRI) mkoani Iringa mwaka 2015.

mwaka 2017 alianza kulima matikiti, huku mwaka 2019 akiendelea na shughuli za kilimo kupitia kampuni, hatua iliyomuwezesha kupata uzoefu zaidi kuhusu uzalishaji na masoko.

"uzoefu huo ulimsaidia kuona fursa zilizopo katika sekta ya kilimo na kuanza kufikiria namna ya kuanzisha kampuni yake binafsi ili aweze kuzalisha kwa kujitegemea, badala ya kuendelea kufanya kazi kama mkulima mkataba.

Amesema mwaka 2021 changamoto zilizotokana na COVID-19 ziliathiri shughuli zake za kilimo, lakini baadaye alirejea na kuamua kuanzisha kampuni yake mkoani Iringa.

“Nilianza kama mkulima wa kawaida, lakini nilipoanza kufanya kazi kama mkulima mkataba nilianza kuona kuna fursa nyingi katika kilimo. Hapo ndipo nilipopata wazo la kuanzisha kampuni yangu binafsi ili niweze kulima na kukuza shughuli zangu,” amesema Mwamoto"

Katika Hatua nyingine Neema amesema kampuni hiyo ilipoanza, ilijikita zaidi katika kutafuta masoko ya ndani (local market), lakini ndoto yake ilikuwa kufikia hatua ya kuuza mazao katika masoko ya nje ya nchi (export market).

katika kufikia ndoto hiyo, amepitia michakato mbalimbali ya kujengewa uwezo kupitia wadau mbalimbali, ikiwemo AGCOT, ambao umekuwa sehemu ya safari yake ya kujifunza na kuboresha shughuli za kampuni.

uwezeshaji huo umemsaidia kupata uelewa zaidi kuhusu uzalishaji wa mazao kwa kuzingatia mahitaji ya soko, hatua ambayo imeendelea kumjengea uwezo wa kukuza biashara yake na kuwafikia wakulima wengine.

Aidha Dhumuni la sasa ni kuongeza uzalishaji wa mazao ya mboga mboga, kuimarisha masoko na hatimaye kufikia soko la kimataifa.

Vilevile Neema ameongeza kuwa safari yake kutoka kuwa mkulima wa kawaida hadi kuwa mwanzilishi na mkurugenzi wa kampuni imeonyesha umuhimu wa uwezeshaji kwa vijana na wakulima, akisisitiza kuwa elimu, ujuzi, masoko na fursa za kibiashara ni muhimu katika kukuza sekta ya kilimo.

Nitaendelea kutumia uzoefu nilioupata pamoja na fursa za uwezeshaji kutoka kwa wadau kama AGCOT, kwa lengo la kukuza kampuni na kuchangia kuongeza kipato cha wakulima




.
Share:

Saturday, 8 August 2026

WAFANYABIASHARA WA MADUKA YA SIMU KARIAKOO WAPATA FURSA YA KUELEZA CHANGAMOTO ZAO KWA TRA


Kariakoo, 7 Agosti, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kariakoo imeendelea kusogeza huduma karibu na walipa kodi kwa kukutana na wafanyabiashara wa maduka ya simu katika Kijiwe cha Zungu, Kariakoo, kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili na kutoa ufumbuzi wa masuala ya kodi na biashara.

Aidha, wafanyabiashara walipata fursa ya kueleza kwa uwazi changamoto wanazokutana nazo katika shughuli zao za kila siku,ikiwa ni pamoja na ujio wa wageni(wachina) ambao wanauza bidhaa kwa bei rahisi Zaidi huku wakipata ufafanuzi, maelekezo na majibu ya papo kwa hapo kutoka kwa viongozi wa TRA kuhusu namna bora ya kuzitatua.

Hata ivyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafabiashara Bw. Severine Mushi amesema kuwa “Kukutana na TRA kunaondoa hofu na kunatupa nafasi ya kusikilizwa, kuongeza uelewa wa masuala ya kodi na kutujengea imani katika utekelezaji wa majukumu ya kikodi kwa ufanisi zaidi.”

Akizungumza katika kikao hicho, Meneja wa TRA Mkoa wa Kariakoo Bw.Edson Issanya alisema mamlaka itaendelea kuwafikia walipa kodi katika maeneo yao ya biashara ili kutoa elimu, kusikiliza maoni yao, kutatua changamoto wanazokumbana nazo na kuendelea kuboresha huduma kwa lengo la kujenga mazingira wezeshi ya biashara.
Share:

TBS YENDELEA KUTOA ELIMU YA UTHIBITISHAJI UBORA WA BIDHAA NANENANE MOROGORO

Meneja wa TBS Kanda ya Dar es Salaam, Bi. Noor Meghji akitoa elimu ya Viwango kwa Wajasiriamali wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam  katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro

*********

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limewataka wazalishaji wa bidhaa nchini kuhakikisha wanathibitisha ubora wa bidhaa zao ili kuondokana na vikwazo vya kibiashara na kuongeza wigo wa masoko ya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Akizungumza wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki, Meneja wa TBS Kanda ya Dar es Salaam, Bi. Noor Meghji, amesema shirika hilo linaendelea kuwasaidia wazalishaji na wajasiriamali kuhakikisha bidhaa zao zinakidhi viwango vinavyotakiwa, hatua inayoongeza uaminifu wa bidhaa katika soko.

Amesema katika kutambua umuhimu wa kuwawezesha wazalishaji wa bidhaa mbalimbali, TBS kwa kushirikiana na Shirika la Viwango la Afrika (ARSO), imezindua rasmi Alama ya Ubora ya Afrika, ambayo inalenga kusaidia bidhaa zinazokidhi viwango kuingia katika masoko ya Afrika kupitia Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA).

Aidha, amewahamasisha wajasiriamali kuchangamkia fursa ya kuthibitisha ubora wa bidhaa zao kwa kuwa Serikali inagharamia huduma hiyo, hatua ambayo itawasaidia kuondokana na baadhi ya vikwazo vya kibiashara na kuongeza ushindani wa bidhaa zao.

“Hapo awali, bidhaa zilizothibitishwa na TBS ziliweza kuingia katika masoko ya nchi za Afrika Mashariki bila vikwazo vikubwa, lakini sasa wigo wa soko umeongezeka na bidhaa hizo zinaweza kunufaika na fursa zinazotokana na Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA),” amesisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa TBS Kanda ya Mashariki, Mhandisi Cyril Kimario, amewataka wananchi kuhakikisha wananunua na kutumia bidhaa zilizothibitishwa ubora na TBS, huku akiwahimiza kujenga utamaduni wa kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio.

Amesema kufanya hivyo kutawasaidia wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu bidhaa wanazonunua na kuhakikisha wanapata bidhaa zenye ubora unaokidhi viwango.

“Kununua bidhaa zilizothibitishwa ubora wake humhakikishia mwananchi usalama wa afya yake pamoja na uchumi wake, kwani anakuwa amepata kitu bora chenye thamani katika afya na uchumi,” amesema.

Ameongeza kuwa ushiriki wa wananchi katika kuchagua bidhaa zenye alama na taarifa sahihi za ubora ni sehemu muhimu ya kujenga soko lenye ushindani na kulinda afya na maslahi ya watumiaji.
Meneja wa TBS Kanda ya Mashariki, Mha. Cyril Kimario akitoa elimu ya Viwango kwa Wajasiriamali wa Halmashauri ya Kibaha katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro
Meneja wa TBS Kanda ya Dar es Salaam, Bi. Noor Meghji akitoa elimu ya Viwango kwa Wajasiriamali wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam  katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro
Afisa udhibiti Ubora Mkuu (TBS) Bw. Stephen Rwabunywenge akitoa elimu ya viwango kwa wajasiriamali kutoka halmashauri mbali mbali za mikoa ya Tanga, Pwani, Morogoro na Dar es Salaam katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger