Sunday, 30 August 2026

MKURANGA WATAKIWA KULINDA MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Khadija Nassir Ali, amewataka wananchi wa Mkuranga kuhakikisha wanalinda miundombinu ya gesi asilia iliyojengwa katika maeneo yao ili iweze kudumu na kuwanufaisha wananchi pamoja na taifa kwa ujumla.

Amesema ulinzi wa miundombinu hiyo ni jukumu la pamoja, huku akisisitiza wananchi kuendelea kuiunga mkono serikali na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) katika utekelezaji wa miradi ya nishati safi.

Akizungumza katika bonanza la michezo na upimaji wa afya bure lililoandaliwa na TPDC Kisemvule , Mkuranga, Khadija amesema mradi wa usambazaji wa gesi asilia tayari umewezesha zaidi ya nyumba 500 kuunganishwa na huduma hiyo.

Amesema bonanza hilo pia linalenga kuwakutanisha na kuwaunganisha wananchi wa Kisambule na Mkuranga kwa ujumla, sambamba na kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi na ulinzi wa miundombinu.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amesema Mkuranga inajivunia kuwa miongoni mwa maeneo yanayonufaika na uwekezaji mkubwa katika nishati safi, akieleza kuwa matumizi ya gesi asilia yana mchango katika kutunza mazingira, kuokoa maisha ya wananchi na kurahisisha shughuli za kila siku majumbani.

Ameipongeza TPDC kwa kuichagua Mkuranga kutekeleza mradi huo na kuahidi kuwa serikali ya Wilaya itaendelea kushirikiana na shirika hilo kuhakikisha miundombinu hiyo inalindwa na inatumika ipasavyo.

Khadija amesema matumizi ya nishati safi ni miongoni mwa vipaumbele vinavyoendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hivyo wananchi wanapaswa kutumia fursa hiyo kwa manufaa yao na maendeleo ya taifa.

Amesema kuwa serikali inalenga kuona uwekezaji mkubwa unaofanywa katika miundombinu ya nishati ukitoa matokeo chanya kwa wananchi, huku akiwataka wananchi wengi zaidi kujitokeza kutumia huduma hiyo kadri inavyofikishwa katika maeneo yao.

Kwa upande wake Oscar Mwakasege Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi Kutoka Shirika la Petroli Tanzania (TPDC) amesema bonanza hilo na upimaji wa afya bure unalenga kuhamasisha ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia na ulinzi na usalama wa miundombinu ya bomba la gesi asilia huku akisema katika wilaya ya Mkuranga wameshawafungia wananchi gesi asilia nyumba 530 huku kwa mwaka huu wa Fedha 2026/27 wanatarajia kuwafungia huduma hiyo Wananchi zaidi ya 500 pia.

Kwa Upande wao Wananchi wa Kisemvule mkoani Pwani Ally Rajabu na Sharifa Hassan wamelishukukuru Shirika la Petroli Tanzania (TPDC) kwa bonanza hilo na upimaji wa afya bure huku wakisema wamenufaika na gesi asilia wanayoitumia majumbani hivyo kutumia nishati safi ukilinganisha na kipindi cha nyuma walikuwa wanatumia chafu.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA JUMAPILI AGOSTI 30,2026



Magazetini Leo








Share:

Saturday, 29 August 2026

WANANCHI MATONGO NA NYANGOTO KUELIMISHWA KUHUSU UTHAMINI WA FIDIA NORTH MARA


NYAMONGO, MARA

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kupitia wataalamu kutoka Ofisi ya Mthamini Mkuu wa Serikali, imefanya kikao na Kampuni ya Barrick North Mara Gold Mine pamoja na viongozi wa Vijiji vya Matongo na Nyangoto, kwa lengo la kujadili maandalizi ya utoaji elimu kwa wananchi kuhusu zoezi la uthamini wa fidia linalohusishwa na upanuzi wa shughuli za Mgodi wa North Mara.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Diwani wa Kata ya Matongo, Mhe. Godfrey Mwita, amewataka viongozi wa Vijiji vya Matongo na Nyangoto kushirikiana kwa karibu na wataalamu pamoja na wadau wote wanaohusika katika mchakato huo, akieleza kuwa wananchi wa maeneo hayo wanatarajiwa kuguswa na upanuzi wa shughuli za mgodi.

Kwa upande wake, Meneja wa Mahusiano wa Kampuni ya Barrick, Bw. Francis Uhadi, amesema kampuni hiyo iko tayari kuanza mchakato huo kwa haraka, huku akisisitiza dhamira ya kampuni kuhakikisha haki na maslahi ya wananchi yanazingatiwa na kulindwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.

Akifafanua hatua zinazofuata, Mthamini Kiongozi kutoka Ofisi ya Mthamini Mkuu wa Serikali, FRV. Baraka D. Mollel, amesema kikao hicho ni sehemu ya hatua muhimu kuelekea kuanza mchakato wa uthamini, baada ya hatua za awali zilizofanyika kwa kushirikisha Wizara ya Madini, ikiwemo tafiti na maandalizi mbalimbali.

Amesema hatua hizo zinalenga kuhakikisha zoezi la uthamini linafanyika kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu, pamoja na kuwezesha wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu mchakato huo.

Naye Mtunzaji wa Bwawa la Mgodi, Bw. Majuto Kipande, ameeleza kuwa, tafiti za awali zilizofanyika wakati wa uanzishwaji wa mgodi zilionesha kuwa shughuli za uzalishaji zingefikia ukomo mwaka 2027. Hata hivyo, amesema tafiti zinazoendelea hivi sasa zinaonesha uwezekano wa uzalishaji kuendelea hadi kati ya mwaka 2031 na 2040.

Kwa mujibu wa Kipande, hali hiyo imeongeza umuhimu wa upanuzi wa bwawa la kutunza mabaki ya uchenjuaji wa dhahabu kutokana na bwawa linalotumika sasa kutaraji kufikia ukomo wa matumizi mwaka 2031.

Ameongeza kuwa, ujenzi wa bwawa jipya la kutunza mabaki ya uchenjuaji wa dhahabu unapaswa kukamilika kabla ya mwaka 2031, ili kuwezesha shughuli za mgodi kuendelea bila kuathiriwa na ukomo wa uwezo wa bwawa linalotumika sasa.

Mchakato wa uthamini unalenga kuhakikisha wananchi watakaoguswa na eneo la upanuzi wanapatiwa elimu na taarifa sahihi kuhusu hatua zinazochukuliwa, huku zoezi la uthamini wa fidia likitekelezwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi.



















Share:

RC CHALAMILA NAOMBA NISAIDIE KUNA WATU WANATAKA KUNIDHULUMU ENEO LANGU-KIZENGA


Na Mwandishi Wetu

MKAZI wa mtaa wa Unyasini katika Kata ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam Yahaya Kizenga amemuomba Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kupitia kwa Mkuu wa mkoa huo Albart Chalamila kuwasaidia kupata haki ya eneo la aridhi ambalo kuna watu wamevamia wakitaka kuwadhulumu.

Kwa mujibu Kizenga amesema amekuwa katika eneo hiki tangu mwaka 1976 ambalo alipewa na Nyerere wakati wa operesheni ya Nguvu Kazi na anayo hati ya Kijiji lakini cha kushangaza kuna watu wamejitokeza na kudai eneo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Kizinga ambaye ni askari mstaafu wa Jeshi la Polisi amesema alipata eneo wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza na amekuwa akiishi katika eneo hilo tangu mwaka huo wa 1976.

“Nimekuwa nikiishi hapa tangu mwaka 1976 na ninamiliki eneo hili nikiwa na hati ya Kijiji niliyopewa wakati huo. Mbali na kuwa na nyumba yangu lakini nimekuwa nimekuwa nikiliendeleza kwa shughuli za kilimo cha mbogamboga “

Akieleza zaidi kuhusu eneo hilo amesema cha ajabu alitokea mtu aliyekuwa anajulikana kwa jina la Juliana Lyimo ambaye alikuwa anamiliki kampuni ya Oliver beach Resorts akidai hili eneo ni lake.

“Baada ya kujitokeza kwa mtu yule mimi pamoja na majirani wenzangu wanne tuliamua kwenda Serikali ya Mtaa Kawe lakini hatukupata suluhu hivyo tukaenda Mahakamani na tunashukuru Mungu baada ya kuwasilisha vielelezo vyetu tulishinda kesi mwaka 2015.

“Baada ya kushinda kesi mahakamani tulikwenda kukazia hukumu lakini pia ilibidi na twende Wizara ya Aridhi kwasababu miaka ambayo nimekaa tangu tushinde kesi mwaka 2015 tulikaa mpaka 2021 na kila siku tukiuliza tunaambiwa kuna rufaa.

“Lakini nilishutuka kwanini kuna rufaa miaka yote,hivyo nikaamua kwenda Wizara ya Aridhi tena kuangalia na kukuta yule mmiliki ambaye tulimshinda mahakamani ndio amemilikishwa ,hiyo ilikuwa mwaka 2021.Na sasa tumeona watu wamekuja na kuanza kumwaga kifusi katika eneo hili lenye ukubwa wa heka moja na nusu.”

Kizenga amesema kutokana na umri wa utu uzima amekuwa akikabiliwa na maradhi yeye pamoja na mkewe na kutokana na uchumi duni umesababisha wajanja wachache wanataka kuwadhulumu eneo lao na kwamba wanaamini anayeweza kuwasaidia kupata haki yao ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila ambaye tumeshuhudia akitenda haki hasa kwa wake wasiokuwa na uwezo.

“Tunamuomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ,Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni pamoja na Mamlaka zinazohusika na utatuzi wa migogoro ya aridhi watusidie kupata haki yetu,hapa ni kwetu na tuko kihalali lakini leo hii wanakuja watu wanataka kutuondoa sasa wanataka twende wapi?

“Mkuu wa Mkoa tunakuomba utusaidie tupate haki yetu, sisi ni wazee tusio na kitu tunadhulumiwa.Ombi langu kwa mamlaka na viongozi wote watusikie kilio chetu.Wanaotaka eneo langu ni watu ambao wanafanya kila aina ya hila na mbinu na wapo tayari kufanya lolote kudhulumu”

Kwa upande wake Mariam Kizenga ambaye ni mke wa Mzee Kizenga amemuomba Rais DK.Samia Suluhu Hassan kupitia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuwasaidia ili eneo lao lisichukuliwe na watu ambao wameonekana wanafanya ujanja ili kuwadhulumu.

“Tunamuomba Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na viongozi wengine watusaidie kuna mtu amekuja hapa na kuanza kuweka kifusi cha mchanga,anataka kutudhulumu.Tuko hapa kwa miaka 50 tukidhulumiwa tunakwenda wapi? Na sisi hatuna uwezo wa kujenga na makazi yetu yako hapa kwa muda wote .Tunaomba Serikali itusaidie.”
Share:

Friday, 28 August 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AGOSTI 29,2026



Magazeti








Share:

DG NEMC ATUNUKIWA TUZO YA HESHIMA–USIMAMIZI WA MAZINGIRA


-Ni katika hitimisho la Kongamano la FARViBE 2026,lililofanyika Jijini Dar es salaam

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt.Immaculate Sware Semesi ametunukiwa tuzo ya heshima na Naibu Waziri Wizara ya Uvuvi na Uchumi wa Buluu - Zanzibar, Mhe. Mboja Ramadhan Mshenga katika Kongamano la kimataifa la Kisayansi la Utafiti wa Uvuvi na Ufugaji wa Samaki kwa Uchumi wa Buluu Endelevu (FARViBE 2026), lililofanyika kuanzia tarehe 24 hadi 27 Agosti 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC Jijini Dar es Salaam.

Tuzo hiyo iliyopokelewa na Meneja wa NEMC Kanda ya Mashariki Kaskazini Bi. Glory Kombe kwa niaba yake imelenga kutambua mchango alionao katika Sekta ya Mazingira hasa ikizingatiwa suala la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini ndio msingi wa Maendeleo endelevu kufikia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.

Akizungumza wakati wa kukabidhi tuzo hiyo, Naibu Waziri Mhe. Mboja Mshenga amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha juhudi za Uhifadhi na Usimamizi wa mazingira ya bahari, kwani ndio msingi wa maendeleo katika sekta ya uvuvi na uchumi wa buluu huku akisistiza maendeleo ya kiuchumi ili kuhakikisha rasilimali za bahari zinalindwa na kutumika kwa manufaa ya kizazi cha sasa na baadae

NEMC imeshiriki kongamano hilo kwa lengo la kuwasilisha na kujadili masuala ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira hususani Bahari kwa ustawi wa uvuvi na uchumi wa buluu endelevu.

Kongamano hilo lililowakutanisha wataalamu na wadau wa masuala ya bahari kutoka ndani na nje ya Tanzania, lililenga kujadili tafiti, ubunifu na teknolojia zinazoweza kuchangia maendeleo endelevu ya sekta ya uvuvi na uchumi wa buluu.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 28, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger