Thursday, 5 February 2026

RAIS SAMIA AMEWEKA MCHORO, SASA KAZI IMEBAKI KWA VIJANA WENYEWE



Bunge la 13 limefanya uchambuzi wa hotuba ya kihistoria ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa Novemba 14, 2025. Safari hii, wabunge hawakujadili namba pekee, bali walijadili "uhalisia wa maono."

Kuna watu wanajilalamikia tu bila kufikiri kama nyumbu kwamba wabunge walikuwa wanafanya uchawa, sio suala la 'uchawa' au sifa zisizo na msingi, bali ni kutambua ukweli wa mwelekeo mpya ambao Rais ameuweka kwa ajili ya mustakabali wa asilimia 60 ya Watanzania—ambao ni vijana.

Katika kile kinachoonekana kuwa ni mageuzi makubwa ya kiuongozi, Rais Samia amevunja ukimya na kutekeleza ahadi yake ya kuunda Wizara kamili ya Vijana chini ya Ofisi ya Rais. Hatua hii imepokelewa kwa 'tano' na wabunge, wakibainisha kuwa kuiondoa idara ya vijana kutoka kwenye wizara zilizosongwa na majukumu mengi ni kumpa kijana sauti, mamlaka, na jukwaa rasmi la kushughulikia changamoto zake, hususan ukosefu wa ajira na mitaji.

Wabunge, akiwemo Dk. Emmanuel Nuwa wa Mbulu na Hawa Chakoma wa Viti Maalum, wamethibitisha bungeni kuwa maono haya yameshaanza kuzaa matunda kwa vitendo. Tayari mabilioni ya fedha yameshaanza kutiririka; Shilingi bilioni 10.5 zimepelekwa Benki ya NMB kwa ajili ya mikopo yenye riba nafuu ya asilimia saba, huku Rais akiahidi jumla ya Shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kuimarisha shughuli za kiuchumi za vijana na wanawake. Huu ni ujumbe mzito kwa vijana kuwa "muda wa kulalamika umekwisha, sasa ni wakati wa kuchangamkia fursa."

Mjadala huo bungeni umeweka wazi kuwa ufunguo wa maendeleo ya kijana hautategemea tena 'mikopo umiza' au majukwaa ya kisiasa yaliyopoteza mvuto, bali utategemea sera madhubuti na programu za kimkakati.

Wabunge wamehimiza kuwa wizara hii mpya iwe mhimili wa kuunganisha vijana na sekta za kilimo, madini, na teknolojia ya habari.

Mbunge Agnesta Lambert amesisitiza kuwa hotuba ya Rais imekidhi matakwa ya wananchi wote bila kujali itikadi, akiamini kuwa utawala bora na uwajibikaji ndio utakaofanya matamanio ya Rais yatekelezwe mitaani.

Bunge pia limefanya vyema kwa kutoa rai kwa watendaji na viongozi waliopewa dhamana kuhakikisha "fyekeo" la Rais linafanya kazi kwa wale watakaochelewesha au kukwamisha fedha hizi kuwafikia walengwa.

Kwa uundwaji wa Baraza la Vijana na uimarishaji wa mifuko ya maendeleo, Tanzania inajipanga kuhakikisha nguvu kazi yake kubwa haipotei kwanye vurugu, bali inageuzwa kuwa injini ya uchumi kuelekea Dira ya 2050.

Ni dhahiri kuwa Rais Samia ameweka mchoro, na sasa kazi imebaki kwa vijana wenyewe "kukaa mkao wa kula" na kutumia zana zao, ikiwemo teknolojia, kutafuta na kutumia fursa hizi adimu.
Share:

SPIKA ZUNGU ASEMA HAKUNA MBUNGE ALIYEPEWA KIBALI KUHOJIWA NA TAKUKURU



Na mwandishi wetu, Dodoma

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu, amesema hadi sasa Ofisi ya Spika haijatoa kibali chochote kwa mbunge yeyote kuhojiwa na TAKUKURU. 

Hii ni kufuatia taarifa za vyombo vya habari zikidai baadhi ya wabunge wameitwa kuhojiwa kuhusiana na madai waliyoyatoa bungeni jambo ambalo Spika amekanusha.

Spika amesisitiza kuwa Bunge linaongozwa na Katiba na Kanuni zake, zinazolinda uhuru wa wabunge kutoa maoni bila shinikizo, hofu au kikwazo chochote. Uhuru huu umeainishwa na Ibara ya 100 ya Katiba, ikiwapa wabunge kinga ya kisheria.

Ameongeza kuwa endapo mbunge amekiuka Kanuni, mamlaka ya kuchukua hatua ipo ndani ya Bunge lenyewe kupitia Kiti cha Spika. Bunge litaendelea kulinda uhuru wa wabunge kuchangia masuala ya kitaifa kwa uwazi na ujasiri.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI FEBRUARI 5,2026

Magazeti

 


Share:

Wednesday, 4 February 2026

PROF. SHEMDOE ATETA NA NMB UBORESHAJI MCHAKATO WA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10



Na OWM - TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OWM- TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekutana na uwakilishi wa Benki ya NMB na kujadili namna wanavyoweza kufanya maboresho katika mchakato wa kutoa fedha za mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi kupitia taasisi hiyo ya kifedha.

Prof. Shemdoe amekutana na ujumbe huo leo Februari 03, 2026 ofisini kwake jijini Dodoma, ikiwa ni mwendelezo wa Serikali kutafuta namna bora ya kurahisisha utolewaji wa mikopo hiyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha makundi yote lengwa ya Wanawake, Vijana na wenye Ulemavu yananufaika na mikopo hiyo.

Msisitizo wa Prof. Shemdoe kwa ujumbe huo ulioongozwa na Mkuu wa Biashara ya Serikali wa Benki ya NMB, Bi. Vicky Bishubo umekuwa ni kuhakikisha vikundi vya wanufaika vyenye sifa stahiki vinapata mikopo hiyo kwa wakati.

Sanjali na hilo, Prof. Shemdoe ameipongeza na kuishukuru Benki ya NMB kwa kuiunga mkono Serikali katika uboreshaji wa miundombinu ya afya msingi na elimu msingi pamoja na kurahisisha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa walengwa. 

Akitoa ufafanuzi kuhusu hoja ya walengwa kutakiwa kuweka dhamana ili kupata mikopo ya asilimia 10, Bi. Bishubo amesema kuwa, hoja hiyo si ya kweli kwani mikopo hiyo ni nafuu na inatolewa bila dhamana yoyote, hivyo amewataka walengwa kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo. 

Katika hatua nyingine, uwakilishi huo wa Benki ya NMB umekutana na Naibu Waziri OWM- TAMISEMI, anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, pamoja na Naibu Waziri, OWM - TAMISEMI, anayeshughulikia Afya, Mhe. Dkt. Jafal Seif kama sehemu ya Kuimarisha mahusiano baina ya Benki hiyo na OWM- TAMISEMI.






Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARI 4, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger