Thursday 30 April 2020

Bilioni 33 Kutumika Kuimarisha Huduma Za Kijamii Nchini Tanzania

NA WAMJW Dodoma
Wizara ya Afya, kupitia Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii inatarajia kutumia Jumla ya shilingi bilioni 33.195 ili kutekeleza shughuli mbalimbali za kijamii hususani zilizopewa kipaumbele kwa mwaka wa fedha 2020/21.

Akiwasilisha Hotuba ya Wizara ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Mhe. Ummy Mwalimu amesema katika mwaka wa fedha 2020/21 Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii inatarajia kutumia kiasi hicho cha fedha kwa lengo la kuimarisha huduma na mafunzo kwenye Taasisi za Ustawi na Maendeleo ya Jamii, kukarabati makazi ya wazee, kujenga mahubusu za watoto na kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Alisema kuwa bajeti hiyo itasaidia kuimarisha Kujenga kumbi pacha na hosteli katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru ambapo jumla ya shilingi bilioni 2.7 zimetengwa, pia kuboresha utoaji wa mafunzo ya taaluma ya maendeleo ya jamii ili kukidhi mahitaji ya soko sambamba na kukuza ujuzi wa wahitimu ikiwemo kuwajengea uwezo wa kujiajiri na kuajiriwa kwa kutenga jumla ya shilingi bilioni 6.6.

Maeneo mengine yaliyotengewa fedha ni pamoja na ukarabati wa majengo na miundombinu katika makazi ya wazee kwa shilingi milioni 400, ujenzi wa Shule ya Maadilisho katika Mkoa wa Geita shilingi milioni 200, kuimarisha ujenzi wa mahabusu ya watoto katika mikoa ya Kigoma na Mtwara shilingi milioni 700 na kuwezesha Taasisi ya Ustawi wa Jamii kuboresha utoaji wa mafunzo yanayokidhi mahitaji ya soko shilingi milioni 250.

Aidha, jumla ya shilingi milioni 827.95 zimetengwa kwa ajili ya shughuli za kutokomeza ukatili wa kijinsia katika jamii.

“Ili kutekeleza vipaumbele vilivyoanishwa kwa mwaka 2020/21, Wizara kupitia Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii imekadiria kutumia kiasi cha shilingi bilioni 33 kwa ajili ya kutekeleza majukumu mbalimbali ya Wizara ikiwa ni pamoja na uendeshaji wa ofisi na miradi ya maendeleo” alisema.

Mhe. Ummy amesema Wizara imeendelea kukuza ari ya jamii kushiriki katika kujiletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kutumia nguvu kazi na rasilimali zinazowazunguka na kusimamia masuala yote ya ushirikishwaji wa jamii kwenye sekta mbalimbali.


Share:

Safari Za Kwenda Kuwatembelea Ndugu Vijijini Zisubiri Corona iishe:- Dr Subi

Na WAMJW- DSM
Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi ametoa wito kwa wananchi kutosafiri kwenda vijijini kwa lengo la kuwasalimia ndugu katika kipindi hiki ili kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona kusambaa zaidi nchini.

Wito huo ameutoa leo, wakati akiongea na Waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya Jijini Dar es Salaam juu ya mwenendo wa kampeni ya “Mikono safi, Tanzania salama” inayolenga kuelimisha wananchi juu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

“Kwa wanaotaka kwenda kuwatembelea Wazee kijijini, wasubiri Corona iishe, kwasababu tunaona watu watatoka kwenye miji ambayo inamaambukizi wanaenda vijijini kuwatembelea wazazi ambao umri wao umeenda, inawezekana wana magonjwa ya uzeeni, kunauwezekano mkubwa wakuwaambukiza huko” alisema.

Aliendelea kusisitiza kuwa, katika maeneo yote yenye msongamano hususan maeneo ya biashara na huduma za Afya, waweke utaratibu mzuri, utaosaidia wateja kukaa umbali wa mita moja au zaidi pindi wanaposubiri kupata huduma, hali itayosaidia kukata mnyororo wa maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

“Maeneo ya kutoa huduma mbali mbali, ikiwemo Hospitali na vituo vya Afya, waweke utaratibu mzuri, watu wanaokuja kupata huduma wakae katika utaratibu wa mita moja au zaidi ili watu hawa wasiweze kuambukizana maradhi, lengo likiwa kukata mnyororo wa maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine ” alisema

Aliendelea kusema, ni muhimu uvaaji wa Barakoa uzingatiwe katika ngazi zote, hasa katika maeneo yenye mkusanyiko wa watu, huku akisisitiza kuwa, ni muhimu kuzichoma moto Barakoa zilizotumika ili kuepusha usambaaji wa magonjwa ya mlipuko yanayoweza kujitokeza.

“Tunasisitiza uvaaji wa Barakoa, hasa unapokuwa kwenye mkusanyiko wa watu, lakini barakoa sio kitu salama baada ya kumaliza kukitumia, kinakuwa kichafu na maambukizi, kwa mantiki hiyo, hakikisha unaitupa sehemu salama na unachoma moto ili mtu mwingine asiweze kuikokota na kuitumia tena ” alisema

Aidha, Dkt. Subi amesema kuwa, bado elimu ya kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka haijaeleleweka vizuri, hivyo kuitaka timu ya hamasa kuongeza nguvu katika hatua zote tano za unawaji mikono ili elimu hiyo isaidie katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

“Tunaposema kunawa mikono kwa maji safi yanayotiririka na sabuni tunamaana kwamba, unapokwenda kunawa hakikisha sabuni imekolea vizuri kwenye kiganja cha mikono, hakikisha umesugua vizuri, povu la sabuni limeshika vizuri, na hakikisha umenawa vizuri mbele, nyuma, kwenye vidole na kila eneo la mikono vizuri kwa sekunde zisizopungua 20″alisema

Akiwasilisha ripoti ya utendaji kazi wa kampeni ya “mikono safi, Tanzania salama,” Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima ameweka wazi kuwa, mpaka sasa timu hiyo ya uhamasishaji imeshatembelea jumla ya maeneo 145 kati ya 213 yaliopangwa yametembelewa ikiwa ni sawa na asilimia 68.

Mbali na hayo amesema kuwa, licha ya kutoa elimu ya tahadhari, kikosi cha uhamasishaji kimekuwa kikitoa zawadi kwa taasisi na watu ambao wanazingatia maelekezo yanayotolewa na Wizara, vikiwemo vitakasa mikono (Sanitizer), viang’azi (Reflectors) na khanga za Kampeni.


Share:

Serikali Haitopanga Bei Za Mazao Ya Wakulima

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Serikali imesisitiza kuwa haitopanga wala kuingilia bei za mazao ya wakulima nchini badala yake wakulima watajipangia bei na kuuza wenyewe ilihali serikali ikisalia kama msimamizi.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) ameyasema hayo leo tarehe 30 Aprili 2020 wakati akizungumza na viongozi wa TADCOs Co ltd kuhusu hatua iliyofikiwa ya uagizaji wa mbolea katika ukumbi wa KILIMO IV Jijini Dodoma.

Mhe Mgumba amesema kuwa mfumo wa biashara ulivyo unategemea zaidi ujazo wa mazao sokoni, hivyo bei haitolewi kutokana na gharama alizotumia mkulima wakati wa uzalishaji badala yake bei inaendana na soko.

Amesema kuwa wakulima kama wanavyoruhusiwa kuzalisha kadhalika wakulima hao watauza mazao yao popote watakapotaka wao lakini kwa kufuata taratibu na sheria za nchi.

Kuhusu Mfumo wa stakabadhi ghalani Naibu Waziri Mhe Mgumba amesema kuwa mfumo huo ulianzishwa kwa lengo la kumrahisishia huduma za biashara mkulima hivyo utaendelea kutumika kwa mujibu wa matakwa ya kuanzishwa kwake.

Amesema kuwa zipo changamoto nyingi katika utekelezaji wa mfumo huo unaochagizwa na viongozi wanaosimamia hususani wa vyama vya Ushirika kutotekeleza kwa mujibu wa sheria.

“Mtu akipeleka mazao yake ghalani lengo la serikali kwa sababu mazao yote tunategemea msimu wa mvua na upatikanaji wake ni wa wakati mmoja hivyo kuhifadhi kwa pamoja na kupewa stakabadhi itakayomrahisishia kupata mkopo kwa ajili ya kukidhi mahitaji yake wakati akisubiri gharama za mazao zikipanda aweze kuuza kwa bei nzuri” Alikaririwa Mhe Mgumba

Mhe Mgumba ameongeza kuwa mfumo huo ni mzuri endapo utaendelea kusimamiwa vizuri ikiwa ni pamoja na kuendelea kuuboresha zaidi ili uwanufaishe wakulima kote nchini kwani mfumo huo unapunguza gharama za uendeshaji.

Ameeleza kuwa miongoni mwa changamoto waliyokuwa nayo wakulima ilikuwa ni Tija ndogo katika mavuno yao yaliyosababishwa na matumizi madogo ya mbolea hivyo serikali ilitoa elimu ya kutosha kwa wakulima kuhusu matumizi sahihi ya mbolea hivyo katika kipindi cha serikali ya awamu ya tano tija imeongezeka.

Mgumba amesema kuwa matumizi sahihi ya mbolea yameongeza tija katika sekta ya kilimo kwani uzalishaji umeongezeka na wakulima wamekuwa na kipato kikubwa.

Katika kikao kazi hicho Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba amesema kuwa nchi ina mbolea ya kutosha ambapo ina akiba ya zaidi ya Tani 203,000 iliyotokana na uagizaji wa mbolea uliofanywa kwa mwaka mzima wa kiasi cha mbolea Tani 633,197


Share:

Wenye Virusi vya Corona Kenya Wafika 396....Ni Baada ya Wengine 12 Kuongezeka Leo

Idadi ya watu walioambukizwa virusi vya corona nchini kenya, imefikia 396  baada ya wengine 12 kuongezeka leo April 30, 2020

Wizara ya afya nchini humo  imesema kwamba kati hao 12 walioambukizwa, 7 wanatoka Mombasa, 3 Nairobi, Kitui 1 na Wajir 1.

Kwa saa 24 zilizopita, wagonjwa 15 wamepona ikiwa ndio idadi ya juu tangu kutangazwa kwa virusi hivi nchini mno huku wale waliopona wakifikia 144 kwa ujumla.
 
Aidha wawili wamethibitishwa kufariki na kufikisha idadi hiyo kuwa 17.


Share:

Kwanini Baadhi Ya Watu Wana Uzito Mdogo Kupita Kiasi ? ( Kukonda Na Kudhoofu Mwili )

Kuna  idadi  kubwa  ya  watu  ambao wana  kabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  uzito  mdogo kupita  kiasi.

Kwa  mujibu  wa   tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  ni  jambo  linalo weza  kuhatarisha  afya  ya  mhusika.

Kama  ilivyo  kwa  suala  la  kuwa  na  uzito  mkubwa  kupita  kiasi,  suala  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  pia  lina  madhara  mengi  katika  afya  ya  binadamu.

MADHARA   YA KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI  (  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, yafuatayo  ni  madhara  ya  kiafya  yanayo  weza  kumpata  mtu  mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi.

1.    Kupungua  na  kudhoofika  kwa  kinga  ya  mwili
2.    Kuwa  katika hatari  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  ya  mifupa  kwa  sababu  mwili hushindwa  kupokea  na  kutengeneza  virutubisho  muhimu  vinavyo hitajika  katika  kuimarisha  afya  ya  mifupa
3.    Kuwa na  nywele  zisizo  na  afya  (  Kinyonyoki)
4.    Kuwa  na ngozi  isiyo  na  afya
5.    Kuugua  mara  kwa  mara  kutokana  na kuwa  na  kinga  dhoofu  ya  mwili.
6.    Watu  wenye  uzito  mdogo  kupita  kiasi  huwachukua  muda  mrefu  kupona  hata  magonjwa  ya  kawaida  ambayo  hupona  ndani ya  muda  mfupi
7.    Kujisikia  uchovu  muda  mwingi
8.    Kupungukiwa  damu  ambako  huweza  kusababisha hali   kama  vile  kizungu  zungu na  maumivu  ya  kichwa  ya  mara  kwa  mara.
9.    Kwa  wanawake , tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  linaweza  kuathiri  mpangilio  wa  hedhi  ambao  unaweza  kupelekea  matatizo  katika  uzazi.

10.  Na  kwa  mwanamke  mjamzito  mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi, anaweza  kupatwa  na  tatizo la  kujifungua  kabla  ya wakati  yani  kabla  ya  wiki  37.

11.  Tatizo  la  uzito mdogo  kupita  kiasi  huathiri  ukuaji  wa  watoto.  Watoto  wadogo  wanahitaji  kuwa  na  virutubisho  vya  kutosha  ili  waweze  kukua  na  kuongezeka  na kuwa  na  mifupa  yenye  afya.  Ukosefu  wa  vitu  hivyo  maana  yake  ni  kwamba  mtoto  husika  hatoweza  kukua  na  kuongezeka  vizuri .  Vilevile  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  linaweza  kusababisha  tatizo  la  mifupa  kwa watoto  jambo  ambalo  ni  hatari kwa  mustakabali  wa  afya  za  watoto  husika

CHANZO   CHA   TATIZO   LA   KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI ( KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, zifuatazo  ni  baadhi  ya  sababu  kuu  za  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi ( Kukonda  na  kudhoofu  mwili )

1.    Kuugua  magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  ya  kiafya  kama  vile  vidonda  vya  tumbo,presha   na kisukari.

2.    Msongo  wa  mawazo.

3.    Kujinyima  kula  ( Kufanya  diet  ngumu )  au  kukosa  hamu  ya  kula  kwa  muda  mrefu.  Kukosa  hamu ya  kula  kunaweza  kuwa  kumesababishwa  na  eidha  kuugua  magonjwa  na matatizo  mbali  mbali  ya  kiafya  au  kupatwa  na  tatizo  la  msongo wa  mawazo.

SULUHISHO   LA  TATIZO  LA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI( KUKONDA NA  KUDHOOFU  MWILI )
Unaweza  kumaliza  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  kwa  kuzingatia  kula  mlo  kamili  (  Balanced  Diet ) au  kwa  kutumia  DAWA  ZA  ASILI  ambazo  ni  maalumu  kwa  ajili  ya  kumaliza  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi (  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )

DAWA  YA  ASILI INAYO  MALIZA  TATIZO  LA  KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI ( TATIZO  LA  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
Ipo  DAWA –LISHE  YA ASILI  ambayo  INATIBU  na  KUMALIZA  kabisa  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  ambalo  linaenda  sambamba  na  kukonda  na  kudhoofu  mwili.  Dawa  hii  ni  ya asili  kabisa  isiyo  na  kemikali  yoyote  ya  viwandani  na  inayo  saidia  kutibu  na kumaliza tatizo  hili  na  kuurudisha  mwili  katika  afya  yake  ya  awali  ndani  ya  siku  thelathini.

JINSI  YA  KUPATA DAWA  HII:  Jinsi  ya  kupata dawa  hii, fika  katika duka  la  kuuza  dawa  za  asili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM   nyuma  ya  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Wasiliana  nasi  kupitia  simu  namba  0693  -  005  189.
Na  kwa  taarifa  Zaidi  kuhusu  huduma  zetu  nyingine, tutembelee  kupitia  tovuti  yetu :

https://ift.tt/1u8My9X


Share:

UNICEF JOBS: Sub-Saharan Roster of Consultants in Child Poverty, Public Financial Management and Social Protection, including Emergency Cash Transfers

Sub-Saharan Roster of Consultants in Child Poverty, Public Financial Management and Social Protection, including Emergency Cash Transfers Apply Job Number: 531360 | Vacancy Link Locations: Africa: Angola, Africa: Botswana, Africa: Burundi, Africa: Comoros, Africa: Chad, Africa: Gabon, Africa: Liberia, Africa: Benin, Africa: Burkina Faso, Africa: Central Afr.Rep, Africa: Congo, Africa: Cote d’Ivoire, Africa: Congo, Dem. Rep, Africa: Djibouti, Africa: Equatorial… Read More »

The post UNICEF JOBS: Sub-Saharan Roster of Consultants in Child Poverty, Public Financial Management and Social Protection, including Emergency Cash Transfers appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Makonda Atoa Msaada Wa Mabati Yenye Thamani Ya Shilingi Milioni 476 Kwaajili Ya Kuezeka Nyumba 1,000 Za Wajane Waliokumbwa Na Mafuriko Dar

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo April 30, 2020 ametoa msaada wa mabati yenye thamani ya Tsh. 476m kwa ajili ya Kuezeka nyumba 1,000 za Wajane wa mkoa huo ambazo zimeathiriwa na mafuriko. RC Makonda amewataka pia wananchi waliojenga mabondeni kuhama.

RC Makonda amesema hayo wakati wa Ziara ya Kukagua athari za Mvua  na kubaini uwepo wa familia za Wajane ambao Nyumba zao zimechukuliwa na Mafuriko na sasa wanapitia changamoto ya kuhifadhiwa kwa majirani baada ya kukosa makazi ya kuishi hivyo ameona ni busara kutoa msaada huo kama sehemu ya pole kwa adha waliyoipata.

Aidha RC Makonda amewapa siku 10 Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanapitia maeneo ya Mito na Mabonde kukagua athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwashirikisha viongozi wa mitaa ili kwa pamoja watoe mapendekezo ya nini kifanyike kisha wampatie ripoti ya kuonyesha hatua za kukabiliana na Mafuriko ya Mara kwa Mara.

Aidha RC Makonda amesema athari zinazoonekana kwa sasa ni matokeo ya Jamii kuwafumbia macho watu wanovunja sheria kwa kujenga mabondeni, kuchimba mchanga na kuziba mikondo ya maji jambo linalopelekea Mafuriko hivyo ametaka kila mwananchi kuwa mlinzi wa mwenzake.

Pamoja na hayo RC Makonda amesema kwa sasa serikali inaendelea kurejesha miundombinu na madaraja yaliyochukuliwa na Mafuriko ikiwemo ujenzi wa madaraja ya muda mfupi ili kuwezesha shughuli za kijamii kuendelea.


Share:

Country Representative – Tanzania | Global Development Incubator

Company Description Aceli Africa is a market-enabling facility to mobilize over $700M in private sector lending for agricultural SMEs in Uganda, Kenya, Rwanda, and Tanzania by 2025. To achieve this goal, Aceli Africa will provide financial incentives to increase the risk appetite of 20+ financial institutions (both global and local) to make loans ranging from USD $25K-$1.5M to… Read More »

The post Country Representative – Tanzania | Global Development Incubator appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Infectious Disease Specialist at Doctors with Africa CUAMM

Doctors with Africa CUAMM is the first NGO in the healthcare area officially recognized in Italy. Deadline Date: Friday, 15 May 2020 Organization: Doctors with Africa CUAMM Country: United Republic of Tanzania City: Shinyanga Founded in 1950 with the aim of training doctors to work in developing countries, CUAMM is working in Angola, Central African Republic, Ethiopia, Mozambique, Sierra… Read More »

The post Infectious Disease Specialist at Doctors with Africa CUAMM appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WASH Officer-Hygiene Promotion at Danish Refugee council (DRC)

Wash Officer-Hygiene Promotion Categories: WASH Officer-Hygiene Promotion Location: Nduta camp, Kibondo Start Date: ASAP Contract duration: 5 months PURPOSE: The WASH Officer under the management and supervision of the WASH Team Leader will be responsible to implement different activities of DRC related WASH program to ensure the program’s objectives are achieved. The post holder is directly responsible for all Sanitation… Read More »

The post WASH Officer-Hygiene Promotion at Danish Refugee council (DRC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tangazo La Nafasi Za Kazi Katika Shirika La IFAD




Share:

MAMA ALIYEWAPIKIA MAWE WATOTO WAKE APATA MSISIMUKO WA AJABU



Boma la Penina Bahati mtaa wa Mishomoroni, kaunti ya Mombasa.
Prisca Momanyi akiwa na simu mpya ya Penina, pia alimsaidia kufungua akaunti kwenye benki.
***

Mjane Penina Bahati kutoka Mishomoroni eneo la Mlango Saba, kaunti ya Mombasa nchini Kenya ambaye aliwapikia wanawe mawe baada ya kukosa chakula ana sababu ya kutabasamu baada ya kupokea msaada kutoka kwa Wakenya.

Penina Bahati aliamua kupika mawe akiwa na tumaini wanawe ambao walikuwa wanalia njaa watalala hata hivyo hivyo, hatua yake haikufaulu baada ya mwanawe mmoja kuamka na kugundua alikuwa akiwahadaa.

 Baada ya Mtandao wa TUKO.co.ke kuangazia masaibu  ya Penina Bahati Kitsao, wengi walijitokeza na kumpa msaada wa chakula na pesa ambapo sasa anaweza kuwapa wanawe lishe angalau mara tatu kwa siku. 


Akiwa mwingi wa furaha, mama huyo mwenye umri wa miaka 45 alisema watoto wake sasa wanaweza pata mlo angalau mara tatu kwa siku, ambapo kwake ilisalia kuwa ndoto baada ya mumewe kuaga dunia 2019.

 "Nina furaha isiyo na kifani. Siamini Wakenya wanaweza kuwa na roho safi hivi. Nimepokea simu kutoka kote nchini, wengi walitaka kujua jinsi wanaweza kunisaidia," mama huyo alifichua.

 Kupitia kwa msamaria mwema ambaye pia ni jirani yake, Prisca Momanyi, Penina alipata simu na kufunguliwa akaunti ambapo wengi walikuwa wakiitisha ili wamtumie msaada.


"Sijawahi kuwa na akaunti ya benki wala simu, hii ni mara yangu ya kwanza na ninaona ni kama muujiza," aliongeza.

 Prisca alisema aliamua kumsaidia Penina baada ya kupokea habari za kusikitisha kwamba aliwapikia wanawe wanane waliokuwa na njaa mawe.

 Penina ana watoto wanane, kifungua mimba wake ana miaka 28 na kitinda mimba akiwa na miezi mitano.


Penina alisema kwamba mwanawe wa kiume mwenye umri wa miaka mitano ndiye alimshinikiza kupika mawe kwani alikuwa akilia njaa. 

"Watoto wengine ni wazima na wanaelewa wakati hamna chakula, hata hivyo huyu wa kiume ni mgumu hawezi elewa kabisa, alishinda kulia hapa kutwa nzima na ndipo sasa akanifanya nikachukua hatua hiyo," aliongeza.
Chanzo- TUKO NEWS
Share:

WAKILI ALBERT MSANDO ASHIKILIWA NA POLISI KWA KUTOA KAULI ZA UCHOCEZI KUHUSU CORONA

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Koka Moita, amesema kuwa wanamshikilia Wakili wa kujitegemea Albert Msando, baada ya kutoa kauli za uchochezi dhidi ya Serikali juu ya ugonjwa wa COVID-19 kwa madai ya kuwa mkoani humo hali ya maambukizi ni mbaya ili hali yeye hana mamlaka hayo.


Kamanda Moita ameyabainisha hayo leo Aprili 30, 2020, na kusema kuwa Msando alikuwa anaelezea hali mbaya ya ugonjwa wa Corona ndani ya Mkoa wa Arusha kupitia video yake iliyokuwa ikisambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, huku akiwataka waandishi wa habari wawe mstari wa mbele katika kutoa taarifa za ugonjwa huo.

"Hali hii ilitoa wakati mgumu kwa wananchi waliokuwa wanasikiliza, kauli hii aliitoa wakati anatoa vifaa vya kujikinga na Corona katika eneo la kaloleni katika ofisi za Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Arusha, na Serikali ilikwishatoa  maelekezo kuwa mwenye mamlaka ya kutoa tarifa hizo ni Waziri Mkuu, Waziri wa Afya na Mganga Mkuu, hii kauli lazima iheshimiwe" amesema Kamanda Moita.


Share:

Afrika Kusini Yaripoti Maambukizi Mapya ya Corona 354 Ndani ya Masaa 24....Waliombukizwa Hadi Sasa Nchini Humo ni 5350

Idadi ya maambukizi ya virusi vya Corona nchini Afrika Kusini imefika watu 5,350 baada ya visa vipya 354 kuthibitishwa, huku idadi vifo ikifikia watu 103

Taarifa kutoka wizara ya afya imesema visa vipya 354 ni vya juu kuwahi kuripotiwa  nchini humo chini ya kipindi cha saa 24.

Takriban wiki sita zimepita tangu kisa cha kwanza cha Covid 19 kuripotiwa nchini Afrika Kusini, na idadi ya maambukizi imekuwa ikiongezeka .

Hivi karibuniAfrika Kusini ilichukuwa mikakati mipya kupambana dhidi ya Corona katika magereza mbalimbali nchini humo, baada ya wafungwa 59 na wafanyakazi wa gereza 29 kuthibitishwa kuambukizwa katika kipindi cha majuma mawili.



Share:

Rais wa zamani wa Sudan Omar al-Bashir Aomba Kuhamishwa Gereza Baada ya Msaidizi Wake wa Zamani Kupata Corona

Rais wa zamani wa Sudan Omar al-Bashir ametaka kuhamishwa gereza kufuatia habari kwamba mmoja wa wasidizi wake wa zamani ameambukizwa virusi vya Corona. 

Bashir amefungwa katika gereza la Kober pamoja na ofisa wa zamani wa Wizara ya mambo ya ndani Bw. Ahmed Hrouna, ambaye alihamishwa katika hospitali ya gereza baada ya kuthibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona. 

Mkuu wa timu ya ulinzi wa Bashir Bw. Mohamed al-Hassan al-Amin amesema, hali ya Bw. Haroun si mbaya sana.


Share:

Trump Aituhumu China Kwamba Inafanya Kila Mbinu Ili Asichaguliwe Tena Kuwa Rais wa Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kwamba China inampango wa kutumia kila njia ili kumfanya asichaguliwe  tena kwenye uchaguzi mkuu wa Urais unaotarajiwa kufanyika mwaka huu

Katika mahojiano yaliofanyika katika Ikulu ya Whitehouse na chombo cha habari cha Reuters, amesema kwamba China inakabiliwa na athari chungu nzima kutoka kwa Marekani kutokana na mlipuko wa virusi vya corona.

Anasema China ilificha kuhusu ugonjwa wa Corona na hivyo kuufanya usambae dunia nzima na kuleta madhara makubwa. 

Hata hivyo, Trump yeye mwenyewe amekuwa akikosolewa vikali  kwa Jinsi anavyokabiliana na tatizo hilo.

Mlipuko wa virusi vya corona umeharibu uchumi wa Marekani ambao Trump alikuwa akitumia  kama kinga kujipigia debe ili kuchaguliwa tena katika uchaguzi wa mwezi Novemba mwaka huu.

"China inafanya kila mbinu za kutaka nishindwe katika uchaguzi ujao. Wanataka mpinzani wangu mkuu kutoka chama cha Democrat Joe Biden ndo ashinde uchaguzi wa mwezi Novemba."-Trump

Aidha, Trump amepinga vikali utafiti uliofanyika nchini humo na kutoa maoni kwamba mpinzani wake  Biden  ana asilimia kubwa za kuibuka  mshindi.

"Siamini kura hizo za maoni....Naamini  raia wa taifa hili ni watu werevu. Na sidhani kama watamchagua mtu ambaye hawezi kuwasaidia kutatua  changamoto zao''. -Trump


Share:

Mahakama Yaamuru Zitto Kabwe Akamatwe

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, inatarajia kusoma hukumu ya Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe Mei 29 mwaka huu huku ikitoa hati ya kumkamata kwa kutohudhuria kwenye shauri lake bila taarifa.

Amri hiyo ya kumkamata Zitto ambaye anakabiliwa na mashtaka matatu ya uchochezi, ilitolewa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Hukumu ilipangwa kusomwa Mei 29 mwaka huu, baada ya upande wa mashtaka na utetezi kufunga ushahidi na kuwasilisha majumuisho ya mwisho kwa kuirahisishia mahakama kufikia uamuzi.

Wakili wa Serikali Mkuu, Tumaini Kweka, alidai shauri lilitajwa kwa ajili ya kupanga tarehe ya hukumu ambapo mshtakiwa hakuwepo na hakuna taarifa kuhusu kushindwa kufika kwake mahakamani.

”Mheshimiwa Hakimu mshitakiwa hayupo na muda wa mahakama unafahamika ni saa tatu asubuhi na hakuna taarifa yoyote ingawa mshtakiwa hana tabia ya kushindwa kufika mahakamani,” alidai.

Baada ya kudai hayo, Hakimu Shaidi alisema hati ya kukamatwa itolewe, kesi iliahirishwa hadi Mei 29, mwaka huu kwa ajili ya hukumu.

Katika kesi hiyo inadaiwa Oktoba 28 mwaka juzi, Zitto  aliitisha mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika ofisi za Makao Makuu ya ACT Wazalendo, akiwa na lengo la kuleta chuki kwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinyume na sheria na kwamba alitoa maneno ya uchochezi dhidi ya Jeshi la Polisi.


Share:

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira Athibitisha Kuambukizwa Ugonjwa wa Corona

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira ametangaza kuwa ameambukizwa virusi vya corona vinavyosababisha homa ya COVID-19.

Kiongozi huyo amesema, hafahamu ameambukizwa lini virusi hivyo na kwamba aliamua kupima kwa sababu kazi anazofanya zinahusisha muingiliano mkubwa na watu.

“Nimepima na matokeo yamekuja yameonesha nimeambukizwa virusi vya corona, sioni dalili za ugonjwa sina homa sikohoi lakini vipimo vimeonesha, hii ni dalili kwamba Watu wengi tunaweza kuwa tunetembea tukiamini tuko salama kumbe hatuko salama, sijui niliambukizwa lini “ – RC Mghwira


Share:

Maambukizi ya virusi vya Corona yapindukia 500 Jamhuri ya Demokrasia ya Congo

Visa 500 vya maambukizi vya virusi vya corona vimethibitishwa nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Congo, watu 31 wakifariki huku watu 279 wakipona.

Kwa mijibu wa kamati iliyobuniwa kukabiliana na mlipuko huo, gereza la Ndolo limeathirika na mlipuko wa virusi hivyo, huku visa 4 vya maambukizi vikiripotiwa katika gereza hilo na wafungwa wengine 25 wakifanyiwa vipimo.

Mkoa wa Kinshasa unaongoza kwa wagonjwa wengi wa Corona, ukifuatiwa na Mkoa wa Kivu Kaskazini.

Hivi karibuni serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iliwarejesha raia wake 165 walio kuwa wanaishi ugenini na ambao walikuwa wamezuiliwa kurejea nchini humo baada ya nchi nyingi kufunga mipaka kutokana na kuibuka kwa janga la Corona.


Share:

Picha : KASHWASA YATOA MSAADA WA MAPIPA KUONGEZA NGUVU MAPAMBANO DHIDI YA CORONA WILAYA YA SHINYANGA


Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko mapipa 20 yenye lita 210 kwa ajili ya kukabiliana Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ katika wilaya ya Shinyanga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira katika mji wa Kahama na Shinyanga (Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority(KASHWASA) inavyozalisha na kusambaza maji nchini imetoa msaada wa mapipa 20 yenye lita 210 kwa ajili ya kuunga juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ kwenye maeneo huduma za kijamii katika wilaya ya Shinyanga.

Mapipa hayo yamekabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa kwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko leo Alhamis Aprili 30,2020.

Mhandisi Mgeyekwa amesema KASHWASA itaendelea kushirikiana na serikaliH katika mapambano dhidi ya Virusi vya Corona kwani Corona inaweza kuathiri shughuli za kijamii na kiuchumi.

“Tumekabidhi mapipa 20 yenye ujazo wa lita 410 kila moja ambayo yatawekwa kwenye maeneo ya watu wengi katika wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona”,amesema Mhandisi Mgeyekwa

“Katika kuunga juhudi za serikali kwenye mapambano dhidi ya Corona, KASHWASA imechangia mapipa 140 yenye thamani ya shilingi Milioni 11.8 kwa ajili ya wilaya 8 za mikoa ya Shinyanga,Mwanza na Tabora ambako KASHWASA inafanya kazi zake ambapo kati ya mapipa hayo 140, 20 ni kwa wilaya ya Shinyanga”,ameeleza Mhandisi Mgeyekwa.

Akipokea Mapipa hayo, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko ameishukuru KASHWASA kwa mchango huo akibainisha kwa utasaidia kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya Virusi vya Corona.

“Kwa niaba ya wananchi wa wilaya ya Shinyanga ninawashukuru sana kwa kutupatia mapipa haya. Tutayapeleka katika Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ili yakatumike kwenye maeneo ambayo yana mikusanyiko ya watu wengi ikiwemo minada na masoko”,amesema Mhe. Mboneko.

“Mkurugenzi wa halmashauri hakikisheni mapipa/madumu haya yanakuwa masafi na yawe na maji muda. Simamieni pia wananchi wasiweke ndoo tupu bila maji na wanawe kwa maji na sabuni muda wote”,ameongeza Mboneko.

Aidha amesema serikali inaendelea kutoa elimu kuhusu Corona kwa njia mbalimbali huku akiwasisitiza wazazi na walezi kuzuia watoto wasizurure mtaani na wafanyabiashara wasipandishe bei ya vifaa vinavyotumika katika mapambano dhidi ya virusi vya Corona.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Mhe. Hoja Mahiba ameahidi kutunza mapipa hayo na kwamba yatawekwa kwenye maeneo yenye huduma za kijamii ikiwemo minada,masoko,zahanati na vituo vya afya.


ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira katika mji wa Kahama na Shinyanga (Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority(KASHWASA) inavyozalisha na kusambaza maji katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania, Mhandisi Joshua Mgeyekwa akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko mapipa 20 yenye lita 210 kila moja kwa ajili ya kuunga juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ kwenye maeneo huduma za kijamii katika wilaya ya Shinyanga leo Alhamis Aprili 30,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (kulia) akijaribu kufungua koki ya moja ya mapipa 20 yenye lita 210 kila moja yaliyotolewa na KASHWASA kwa ajili ya kuunga juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ kwenye maeneo huduma za kijamii katika wilaya ya Shinyanga. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa.
Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati wa kupokea mchango wa mapipa 20 yaliyotolewa na KASHWASA kwa ajili kukabiliana na Maambukizi ya Virusi vya Corona katika wilaya ya Shinyanga. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akiishukuru KASHWASA kwa mchango wa mapipa 20 kwa ajili kukabiliana na Maambukizi ya Virusi vya Corona katika wilaya ya Shinyanga ambapo alisema mapipa hayo yatapelekwa katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira katika mji wa Kahama na Shinyanga (Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority(KASHWASA) Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza wakati akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (kulia) mapipa 20 kwa ajili ya kuunga juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ katika wilaya ya Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza wakati akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (kulia) mapipa 20 kwa ajili ya kuunga juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ katika wilaya ya Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (katikati) akimkabidhi Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Mhe. Hoja Mahiba (kulia) mapipa 20 yaliyotolewa na KASHWASA ili yakatumike kwenye maeneo yenye huduma za kijamii katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa.
Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Mhe. Hoja Mahiba akizungumza baada ya kupokea mapipa 20 yaliyotolewa na KASHWASA ili yakatumike kwenye maeneo yenye huduma za kijamii katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko.
Muonekano wa mapipa yaliyotolewa na KASHWASA kwa ajili ya mapambano dhidi ya Virusi vya Corona katika wilaya ya Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa (kushoto) akimpa zawadi ya Kalenda za KASHWASA Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko baada ya kukabidhi mapipa 20 kwa ajili ya kuunga juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ katika wilaya ya Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Joshua Mgeyekwa (kulia) akimpa zawadi ya Kalenda za KASHWASA Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Mhe. Hoja Mahiba baada ya kukabidhi mapipa 20 kwa ajili ya kuunga juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ katika wilaya ya Shinyanga.
Picha ya pamoja baada ya makabidhiano ya mapipa 20 yaliyotolewa na KASHWASA kwa ajili ya kuunga juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Corona ‘Covid – 19’ katika wilaya ya Shinyanga.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

BMT kuandaa muongozo kuhusu ukomo wa wachezaji wa Nje nchini.

Na Shamimu Nyaki, WHUSM-Dodoma
Serikali haijatoa ukomo wa wachezaji kutoka nje kushiriki michezo hapa nchini bali imeibua mjadala kwa wadau ili watoe maoni yao.
 
Hayo yamesemwa Jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw.Yusuph Singo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ikiwa ni hatua ya kuboresha na kuimarisha sekta ya michezo nchini. 
 
Ili kutekeleza mjadala huo, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limepewa jukumu la kuendelea kuandaaa mwongozo utakaotumika kukusanya maoni kutoka kwa wadau kuhusu ukomo wa wanamichezo wa nje hapa nchini.
 
“Katika Hotuba ya Bajeti iliyosomwa hivi karibuni Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe, hakuongolea idadi ya wachezaji kutoka nje wanaotakiwa kucheza nchini, bali aliagiza BMT kuandaa mjadala mpana katika kukusanya maoni kwa wadau wa michezo kuhusu namna bora ya kusajili wachezaji wa kigeni katika michezo yote hapa nchini” alisema Bw. Singo.
 
Pamoja na hayo, Mkurugenzi huyo ambainisha kuwa Mhe.Waziri Dkt. Mwakyembe alisisitiza kuwa wanamichezo wote kutoka nje ya nchi wanaosajiliwa hapa nchini ni lazima wawe na ubora pamoja na viwango vinavyotakiwa.
 
Akifafanua suala hilo Bw. Singo amesema kuwa michezo yote ya kulipwa kwa sasa imeendelea kukua duniani kote na nchi yetu pia inayo wachezaji wengi wanaocheza michezo hii ikiwemo Mpira wa Kikapu (Basketball), Kriketi, Mpira wa Miguu na michezo mingine, hivyo, Serikali haijatoa maelekezo ya ukomo wa usajili wa idadi ya wachezaji bali inataka kuwepo kwa mjadala wa wazi utakaotoa mwongozo wa ukomo wa idadi ya usajili wa wachezaji wa kigeni.
 
Aidha, Mkurugenzi huyo alitoa rai kwa wadau wa michezo nchini watakapopata fursa ya kuchangia au kutoa maoni katika mjadala huo wasiegemee katika timu wanazoshabikia, bali watoe maoni ambayo yatasaidia kuendeleza michezo na kuendeleza vipaji vya wanamichezo wetu pamoja na kukuza michezo nchini.
MWISHO






Share:

CCM Watuma Salam za Rambirambi Kifo cha Mbunge Richard Ndassa




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi April 30



















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger