Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Wednesday, 25 February 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARI 25,2026



Magazeti




















Share:

Tuesday, 24 February 2026

DC ILALA AAHIDI KUSHIRIKIANA NA FCC KUDHIBITI BIDHAA BANDIA


Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo Akizungumza wakati wa semina ya wahariri iliyoandaliwa na FCC jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu - Dar es salaam.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amesema ataimarisha ushirikiano kati ya ofisi yake na Tume ya Ushindani (FCC) katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia na viwanda bubu ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Amesema hatua kali zitachukuliwa kwa wote watakaobainika kuvuruga uchumi wa soko.

Amesema hayo wakati wa semina ya wahariri iliyoandaliwa na FCC jijini Dar es Salaam, akisisitiza kuwa ofisi yake kwa kushirikiana na halmashauri zote itaongeza udhibiti wa uzalishaji na biashara. Amesema lengo ni kuwabaini na kuwachukulia hatua wanaojihusisha na usambazaji wa bidhaa zisizo halali.

Amesema kumekuwepo na ongezeko la viwanda bubu vinavyozalisha bidhaa feki, hali inayochangia kuvuruga ushindani wa soko, kupunguza mapato ya Serikali na kuhatarisha afya za wananchi. Amesema Ilala ni lango la biashara, hivyo usimamizi wake unapaswa kuwa makini zaidi.

Aidha, amesema FCC inapaswa kuongeza idadi ya watumishi kutokana na majukumu yake kuwa makubwa, hususan katika mipaka na bandarini. Amesema kuongezeka kwa shehena katika Bandari ya Dar es Salaam kunahitaji nguvu kazi ya kutosha kudhibiti bidhaa zinazoingia nchini.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, akizungumza na wahariri wakati wa semina ya wahariri



Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, amesema taasisi hiyo inaendelea kutekeleza maono ya Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha mazingira ya ushindani na kuvutia wawekezaji. Amesema sheria ya ushindani ni kigezo muhimu kwa mwekezaji kabla ya kuamua kuwekeza.

Amesema semina hiyo imelenga kuwajengea uwezo wahariri kuhusu Sheria ya Ushindani ya mwaka 2003 na mabadiliko yanayotarajiwa kupelekwa bungeni. Amesema FCC haiko tayari kuona soko linapangwa kwa namna inayowaumiza wananchi.

Naye Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bakari Kimwanga, amesema ushirikiano kati ya FCC na wahariri ni muhimu katika kutoa elimu kwa umma. Amesema hatua hiyo itasaidia kulinda ushindani wa soko na maslahi ya watumiaji nchini.



Picha za matukio mbalimbali wakati wa semina ya wahariri iliyoandalia na Fcc.
Share:

Monday, 23 February 2026

MFANYABIASHARA ATOA SIRI YA KUREJESHEWA MALI YAKE ILIYOIBIWA NDANI YA SAA 24

Kwa miaka mingi, baba wa watoto watatu huko Kiambu, Kenya, aliishi katika nyumba iliyojaa mabishano yasiyoisha na mvutano wa kihisia. Kile kilichoanza kama kutokubaliana kidogo kati yake na mkewe kiliongezeka polepole na kuwa makabiliano ya kila siku. Watoto walinyamaza na kujitenga, mara nyingi wakirudi vyumbani mwao ili kuepuka kelele. Ukarimu ambao hapo awali uliwakilisha maisha ya familia yao ulitoweka polepole, na kubadilishwa na tuhuma, hasira, na ukimya baridi.

Anaelezea kwamba hata masuala madogo yangeibuka na kuwa migogoro mikubwa. Mawasiliano yalivunjika kabisa, na kila mazungumzo yalionekana kugeuka kuwa lawama na kuchanganyikiwa. Jamaa walijaribu kuingilia kati na kupatanisha amani, lakini utulivu ungedumu kwa siku chache tu kabla ya mzunguko wa migogoro kuanza tena. Msongo wa kifedha na shinikizo la nje vilifanya hali kuwa mbaya zaidi, lakini ndani kabisa, alihisi kulikuwa na kitu zaidi ya kutokubaliana kwa kawaida tu kulikoathiri nyumba yao.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEBRUARI 23,2026

Magazeti ya leo
 





Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger