Thursday 30 June 2016

MPYA:MKURUGENZI WA TBS ATUMBULIWA JIPU,PIA MENEJA WA FEDHA APIGWA CHINI


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage leo amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa shirika la Viwango Tanzania TBS Bwana Joseph B. Masikitiko ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili.

Pia Waziri Mwijage ameagiza Bwana Emmanuel M. Ntelya Meneja wa Fedha, Mipango na Utawala wa TBS, asimamishwe kazi mara moja kwa kipindi chote ambacho uchunguzi utakuwa unaendelea. Aidha waziri amemteua Dkt Egid B. Mubofu, Mkuu wa Idara ya Kemia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kukaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania.

index.jpeg
Share:

KESI YA UCHOCHEZI:TUNDU LISSU APEWA DHAMANA,YAHAIRISHWA HADI AGOSTI 12 2016

 Image result for TUNDU LISSU
Mh Tundu Lissu apandishwa kizimbani Muda huu mahakama ya kisutu kwa zile tuhuma za maneno ya kuudhi, nunachokisubiri hapa ni maneno mengine yenye tafsiri nyingine kwa watu wengine atakayoitoa leo baada ya kupata dhamana panapo majaliwa. Ndio kwanza kumekucha mapambano yataendelea.
UPDATES:

Lissu anatetewa na wanasheria 17 wakiongozwa na John Mallya Peter Kibatala na timu nyingine toka makao makao makuu ya Chama.

Viongozi wote wa makao makuu wameshawasili,

Tunasubiri Hakimu tu aingie kwenye ukumbi wa mahakama...

UPDATES,

Tayari Hakimu anayesikiliza shauri ameshawasili, sasa ni utambulisho wa mawakili wa pande zote,

Kesi inaanza kusomwa,

Mwendesha mashitaka: Tundu Lisu anashitakiwa kwa makosa ya uchochezi, mnamo tarehe 28/06/2016 akiwa eneo la mahakama kwania ya kudhalau umma dhidi ya mamlaka yao walioyoichagua kihalali, alisema huyu dikteta uchwara lazima tumpinge kila kona"

Hakimu: Mshitakiwa, unakubali au unakataa?

Lissu: nakataa yote

Mwendesha mashitaka: Mh Hakimu ushahidi wa shauri hili umekamilika, tunaomba tarehe ya kuanza usikilizwa,

Hakimu: Mawakili wa utete mnalololote la kusema?

Wakili: Mheshimiwa kwamjibu wa kifungu cha sheria na.... Mshitakiwa kosa aliloshitakiwa linadhaminika, hapa tunao wadhamini na zaidi mshitakiwa ni mbunge na mwanasheria wa chama, hivyo anadhaminika, na zaidi mshitakiwa aliliripoti mwenyewe mbele ya polisi baada ya kuitwa tu kwa simu. Ni hayo tu mh

Mwendesha mashitaka: Mshitakiwa aliyembele yako, mnamo tarehe 28 mwenzi huuhuu alifikishwa mahakamani kwa kosa...... Aaah nimesahau sina nakala ya mashitaka, na wenzake watatu na kudhaminiwa. Hivyo akatenda kosa hili, huyu ana nidhamu mbovu, ameona kutenda kosa ni kawaida,

Hakimu: Kwanini unamhukumu kwa kosa ambalo mahakama hii haikumtia hatiani...na siajabu akitoka hapa atatenda kosa tena....

Wakili: Mh hakimu nashindwa kujua huyu wakili wa serikali anajipa kazi ya hukumu kwa kesi iliyopo mahakamani, nimshauri arudi kwenye kesi iliyopo mezani kwakuwa kesi ya nyuma ni tuhuma tu na sio hukumu inayoweza kutumika kama kielekezo hapa.

Mwanasheria: Mh huyu mtuhumiwa ni mzoefu wa kutenda makosa...... Watu wanaangua kicheko kwa kwa kwa...

Hakimu..... Wakili

Wakili: Kwanza Mh hakimu naomba ifahamike kwamba upande wa serikali wamekubali kuwa suala la dhamani liko wazi, hili liweke katika kumbukumbu... Haya anayoyaleta sasa huyu mwanasheria hayana msingi, kwani kwa mjibu wa vifungu vya sheria na.....na... Vinampa haki yakupata dhamana, izingatiwe kuwa katika dhamana ya kesi ya mwanzo hakukuwa na mashariti ya mtuhumiwa kutotoa maoni ama kutenda kosa nje ya lile.. Izingatiwe kuwa sababu za kukidhi dhamana tumeshazitoa

Hakimu: Mahakama inaamua kuwa mtuhumiwa apewe dhamana, wadhamini wa mtyhumiwa waje mbele...kuhakiki nyaraka zao

Mwanasheria: Anainuka... Mh Hakimu...

Hakimu anasema Jamhuri haijajenga hoja za kutosha kuzuia dhamana.Kwahiyo hakuna Pingamizi la Dhamana

Anawaita Wadhamini

Wamejitokeza Mbunge Susan Lyimo, Madiwani Humphrey Sambo na Rose Moshi Kwa ajili ya kudhamini

Amepewa dhamana.Asanteni
Share:

UFAFANUZI KUHUSU SIFA, VIGEZO NA MASHARTI YA KUPATA MKOPO 2016/2017

 Tokeo la picha la HESLB
Habari zenu;
Kwanza natumaini mu wazima wa afya,pia kwa upande wangu namshukuru Mungu nipo fresh kabisa.

Leo nimeamua kufafanua kwa kina vigezo na masharti ya Kupata mkopo mwaka wa masomo 2016/2017.

NANI ANAFAA KUPATA MKOPO?

mwanafunzi anaehitaji mkopo lazima akidhi vigezo vifuatavyo;
1.yatima aliepoteza mzazi/wazazi asiezidi miaka 30
2. Mwanafunzi mwenye disiability au mzazi wake hajiwezi asiezidi
     miaka 30 pia awe na cheti
    kinachotambuliwa na doctor wa wilaya.

3.Mwanafunzi anaetoka ktk familia maskini na awe anatambuliwa 
    na jamii.

4.Mwanafunzi ambae alikuwa akisomeshwa na wafadhili kutokana
   na kutokujiweza.


VIGEZO VITAKAVYOKUFANYA UPATE MKOPO 2016/2017.

1.Lazima uwe mtanzania
2.Lazima uombe mkopo thru online system.
3.Lazima uwe umechaguliwa na chuo chochote kikuu either thru TCU au NACTE.
4.lazima awe mwanafunzi aliefaulu na anaendelea na masomo(hii inawahusu waliopo chuoni)
5.Asiwe mwanafunzi anaedhaminiwa na mtu yeyote au organization.

SIFA ZA NYONGEZA ZITAKAZOKUFANYA UPATE MKOPO 2016/2017

1.Kwa form 6 ,Uwe umemaliza kati ya mwaka 2014-2016-DIRECT
2.Kwa  diploma uwe umemaliza kati ya mwaka 2014-2016-INDIRECT

KOZI KIPAUMBELE MWAKA 2016/2017

Zifuatazo ni kozi ambazo ni kipaumbele kwa mwaka wa masomo 2016/2017 ktk kupewa mkopo,kozi hizi zimegawanyika mara mbili Kuna PART A NA PART B

PART A
Priority courses  include: -

i)   Education (Science) and Education (Mathematics);
ii)  Health Sciences (Doctor of Medicine, Dental Surgery,
     Veterinary Medicine, Pharmacy, Nursing, Midwifery, BSc in
     Prosthetics and Orthotics, BSc in  Physiotherapy, BSc in Health
      Laboratory Sciences, BSc in Medical Laboratory Sciences and
     BSc in Radiotherapy Technology) and other Health Sciences;
iii)  All Civil and IrrigationEngineering;
iv)  All Petroleum and Gas Engineering;
 

NOTE:wanafunzi wote mtakaochaguliwa katika kozi hizi za PART A mtapewa mkopo wote bila kuangalia kigezo cha MWAKA ULIOMALIZA SHULE.

 PART B:
wanafunzi hawa wote wanasifa za kupata mkopo,hivyo basi watapewa mkopo kulingana na mahitaji yao waliyonayo tofauti na PART A ambapo wote watapata mkopo bila kuangalia kigezo chochote.

 

Priority courses cluster II include:

i) Engineering Programmes (Civil, Mechanical, Electrical, Mining, Mineral and Processing, Textile, Chemical and Processing, Agriculture, Food and Processing, Automobile, Industrial, Electrical and Electronics, Legal and Industrial Metrology, Maritime Transportation, Marine Engineering Technology, Electronics and Telecommunication, Computer, Computer Science Software, Information Systems and Network, Environmental, Municipal and Industrial Services, and Bio-Processing and Post-Harvest)


iii) Agricultural and Forestry Sciences Programmes (Agriculture, Agronomy, Horticulture, Agricultural Economics and Agribusiness,
Forestry, Aquaculture, Wildlife Management, Life Sciences, and Food Science and Technology)


iv) Animal Sciences and Production


v) Science Programmes (BSc General, BSc in/with Applied Zoology, Botanical, Chemistry, Physics, Biology, Microbiology, Molecular Biology and Biotechnology, Fisheries and Aquaculture, Aquatic Environmental Sciences and Conservation, Geology, Petroleum Geology, Petroleum Chemistry, Mathematics, Mathematics and Statistics, Environmental Science and Management, Environmental Health, Biotechnology and Laboratory, Wildlife and Conservation and Computer)
vi) Land Sciences Programmes (Architecture, Landscape and Architecture, Interior Design, Building Survey, Building Economics, Urban and Regional Planning, Land Management and Valuation, and Geospatial Sciences).


NOTE:wanafunzi wote mtakaochaguliwa kozi hizi ili upate mkopo lazima uwe umemaliza kati ya mwaka 2014-2016


KWA KOZI ZOTE ZA ARTS NA BIASHARA AMBAZO HAZIJAORODHESWA HAPO JUU KTK PART A NA B 

Wanafunzi watakaochagua kozi hizi wanahesabiwa kama wapo katika kozi ambazo ni NON PRIORITY ,hivyo basi WATAPATA MKOPO TU endapo wote waliochagua kozi PRIORITY PART A na B kuwa wamepata.

KAMA UTACHAGULIWA OPEN UNIVERSITY

*wanafunzi wote waliochaguliwa open univeristy watapewa MKOPO wa BOOKS AND STATIONARY ONLY 

ENDAPO UTAPATA MKOPO,HUU NDIO MCHANGANUO

i. Meals and Accommodation charges
ii. Books and Stationery expenses
iii. Special Faculty Requirements expenses
iv. Field Practical Training expenses
v. Research expenses
vi. Tuition Fees


KUHUSU DIVISION I AND II AU UPPER SECOND CLASS KUPEWA MKOPO

Jamani kwa ambao hamuelewi swala hili ni kwamba,hii inawahusu wanafunzi watakaodahiliwa katika kozi za MEDICINE,VETERNARY MEDICINE NA LABORATORY ndio watapewa GRANT,means hawatarudisha pesa yoyote hivyo basi wakimaliza chuo inabidi waifanyie serikali kazi si chini ya miaka 5 kwanza.

JINSI YA KUOMBA MKOPO

A:LIPIA MPESA

1. To get MPESA Menu dial *150*00# (Piga *150*00#)

2. Choose option 4 for Pay by MPESA (Lipa kwa MPESA)
3. Choose option 3 for Choose Business (Chagua aina ya Biashara unayolipa)
4. Enter 8 for Education Services(Ingiza 8 kwa Huduma za Elimu)
5. Enter 2 for HESLB(Ingiza 2 kwa HESLB)
6. Enter 1 for Reference Number (Ingiza 1 kwa namba ya kumbukumbu)
7. Enter Account Number (Ingiza namba yako ya kumbukumbu), which is your formatted 15 character form 4 index number e.g. S0143.0012.2009
8. Enter the amount in Tshs to pay either 30,000 or 10,000 based on your application category
9. Enter your 4 digit PIN
10. Enter 1 to confirm
11. A confirmation Message will be displayed. N.B: Please keep this message privately

B:BONYEZA HAPA KUOMBA>>>>>>>>>>http://olas.heslb.go.tz/index.php/olas/olas/trans_add

MWISHO

Napenda kumaliza kwa kuwapa wito kwamba muombe mkopo kwani deadline ni 31 july 2016,Hivyo basi mtu asikutishe kuhusu kutopewa mkopo ,kikubwa muombe MUNGU akuongoze katika kujaza form,USIDANGANYE wala kusema uongo,kama baba ako ni MKUU WA MKOA,we andika ukweli.kwani hata mwaka hata miaka iliyopita kulikuwa na non priority course na mkopo walipata.

siku zote UKWELI UMUWEKA MTU FREE! 

NAKUTAKIA MAOMBI MEMA,ILA ENDAPO UTAHITAJI USHAURI /MSAADA NITAKUSAIDIA BE FREE!

NADHANI NIMEJIBU MASWALI YALIYOKUWA YANAWAUMIZA WENGI.

SHARE NA MWENZAKO

wako;
BLOGGER BOY
MASWAYETU BLOG TEAM!
Share:

Breaking news:Wabunge wa CHADEMA Joseph Mbilinyi, Kubenea na James Millya wasimamisha kuhudhuria vikao vya Bunge

Wanajamvi wasalaam!
Leo hii kamati ya haki,maadili na madaraka ya bunge leo inataraji kusoma taarifa ya shauri la Mbunge Joseph Mbilinyi baada ya kutoa ishara ya matusi bungeni na kunaswa na kamera za bunge!

Tunataraji Mbunge Mbilinyi kupewa adhabu kali ili iwe fundisho kwa vizazi na wabunge wa aina yake ndani na nje ya bunge!

Kwakuwa Joseph Mbilinyi alitoa ishara ya matusi kwa bunge na wabunge tulitegemea chama chake cha CHADEMA kingempa adhabu lakini wamenyamaza kimya!


Joseph Mbilinyi (Mb) amekiri kunyoosha kidole cha kati juu wakati akitoka bungeni baada ya kusika mbunge amemtusi mama yake. Mh. Mbilinyi amejitetea kuwa ni kweli alinyoosha kidole cha kati juu baada ya kumsikia mbunge wa CCM akimtusi mama yake mzazi hivyo kupata short temper na kujikuta akitenda kosa hilo.

Pia Joseph Mbilinyi amesema kuwa alinyoosha kidole cha kati juu kama kupinga kile kilichokuwa kinafanyika na mbunge huyo wa CCM, alipoulizwa na Kamati ya Maadili inayoongozwa na Mh. Mkuchika, Mh. Mbilinyi alisema kuwa kunyoosha kidole cha kati juu hakina maana ya moja kwa moja hivyo kwa uelewa wake yeye alikuwa anapinga kitendo cha mbunge wa CCM.

Kamati ya maadili imeridhika kuwa kitendo cha Joseph Mbilinyi (Mb) kuonesha kidole cha kati juu ni kosa na kutoheshimu mamlaka ya Spika wa bunge baada ya kupitia matoleo ya maana mbalimbali ya (Kuonesha kidole cha kati juu) nchi tofauti tofauti.

Maazimio ya Kamati Maadili
Bunge limeazimia kuwa mbunge wa Mbeya Mh. Joseph Osmond Mbilinyi asimamishwe kuhudhuria vikao 10 vya bunge la 11 kuanzia kikao cha leo Juni 30 mpaka hapo adhabu itakapokuwa imekamilika. Bunge limepitisha kwa kauli moja adhabu hiyo.
Share:

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUNE TAREHE 30.6.2016

Share:

Polisi Yaua Majambazi Matatu Yaliyokuwa Yamejificha Katika Mapango ya Amboni

POLISI mkoani Tanga imewaua watu watatu katika mapigano ya risasi wanaodaiwa kuhusika katika mauaji ya watu jijini humo wakiwamo watu wanane waliochinjwa katika Kitongoji cha Kibatini, Kata ya Mzizima.

Limewahakikishia wananchi kwamba eneo la Amboni yakiwemo Mapango ya Majimoto yanayodaiwa kutumiwa na wahalifu waliosababisha mauaji hasa ya wakazi wanane wa Kibatini lipo salama, baada ya watuhumiwa wengine watatu na silaha mbalimbali kukamatwa juzi.

Waliokamatwa ni Abdulkarim Singano, Seif Jumanne na Ramadhani Mohamed ambao baadaye walikufa kutokana na majeraha ya risasi wakati wa mapigano katika msitu wa Kibatini wakati askari wakijaribu kuwadhibiti, siku moja baada ya Abuu Seif anayedaiwa kuwa kiongozi wao kuuawa jijini Dar es Salaam.

Silaha zilizokamatwa ni bunduki mbili aina ya SMG, bastola moja, risasi 30, mapanga, majambia ambavyo vimepatikana kupitia msako ulioshirikisha kikosi kazi cha vyombo vya ulinzi na usalama vilivyohusisha askari kutoka majeshi yote.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Leonard Paulo alibainisha hayo wakati akitoa taarifa ofisini kwake jana kwamba, wahalifu hao walikamatwa Juni 28, mwaka huu wakati askari walipokuwa katika harakati za kuwakamata kwenye msitu wa Kibatini jirani na mapango ya Majimoto, Kata ya Mzizima jijini Tanga.

“Majambazi waliohusika kuua wananchi wanane pale Kibatini ndio tumewakamata lakini kwa bahati mbaya watatu kati yao wamekufa wakati wakidhibitiwa na askari,” alisema Kamanda Paulo. 

Alisisitiza wameyakagua yaliyokuwa maficho yao na kujiridhisha kuwa Amboni iko salama na imedhibitiwa.

Mapema wiki hii, Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, walitangaza kumuua Abuu Seif aliyeshiriki katika mauaji ya Tanga, baada ya kumpiga risasi alipokataa kujisalimisha baada ya kubainika kujificha katika nyumba moja jijini Dar es Salaam. Alifariki dunia akipelekwa hospitali.
Share:

Wednesday 29 June 2016

VIDEO:TUNDU LISSU AWEKWA RUMANDE,HII HAPA VIDEO ALIYOMUITA RAIS JPM DIKTETA UCHWARA




June 28 2016 Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu alifikishwa Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kwa ajili ya kujibu tuhuma za uchochezi kupitia gazeti la mawio kwenye habari yenye kichwa kinachosema ‘Zanzibar Machafuko yaja’ dhidi yake na wenzake watatu.
Nje ya mahakama hiyo Lissu alizungumza na waandishi wa habari ambapo alitoa kauli ambayo imewafanya polisi wamuite kwa ajili ya mahojiano, Lissu alisema….
>>>’nchi yetu inaingizwa kwenye giza nene na dikteta uchwara hatuwezi kuongozwa na mtu wa namna hiyo, hata kama kachaguliwa na kuwa Rais

Lissu alifika kituo kikuu cha polisi Dar es salaam kuitikia wito wa polisi na amehojiwa na polisi kwa masaa matatu kutokana na kauli hiyo atalala rumande leo kwa amri ya ZCO baada ya kukosa dhamana na atafikishwa mahakamani kesho.

VIDEO HII HAPA
Share:

BREAKING NEWS: WANAFUNZI 10 CHUO CHA BUGANDO WAFUKUZWA CHUO,BAADA YA KUKIUKA SHERIA ZA MITIHANI

Habari zilizotufikia ni kwamba wanafunzi  10 wa chuo cha Bugando wamefukuzwa chuo kutokana na kukamatwa wakiibia kwenye chumba cha mtihani.

SOMA BARU HII HAPO CHINI;

Share:

Official VIDEO | Msaga Sumu Ft. Dogo Ninja - Unanitega Shemeji | Watch/Download


https://youtu.be/me1KSvEwGkM
Share:

UHAMISHO FORM 5 2016:SERIKALI YAPIGA MARUFUKU



SERIKALI imesema shule zote zenye nafasi za wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano mwaka huu, zimejaa hivyo hakuna nafasi ya mwanafunzi kubadilishiwa shule au mchepuo aliochagua.

Hayo yalibanishwa jana katika taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari mjini hapa na Msemaji wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Rebecca Kwandu.
 
Kwandu alisema baada ya serikali kutangaza wanafunzi waliojiunga na kidato cha tano, baadhi ya wazazi na wanafunzi wamekuwa wakifika ofisi za Tamisemi kuomba kubadilishiwa shule au tahasusi (michepuo) walizochaguliwa.
 
“Tunapenda kuwaarifu kwamba shule zote zenye nafasi za wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2016 zimejaza, hivyo hakuna kinachoweza kubadilishwa,” alisema Kwandu.
 
Aidha, Kwandu alisema vigezo ambavyo vilitumika katika uchaguzi huo ni pamoja na ufaulu na uchaguzi wa wanafunzi wenyewe juu ya masomo wanayopenda kuendelea nayo kidato cha tano na sita.
 
“Kulingana na utaratibu uliowekwa na serikali, mwanafunzi mwenye sifa za kuchaguliwa kuendelea kidato cha tano na vyuo vya ufundi ni yule ambaye ufaulu wake ni kuanzia daraja la kwanza hadi la tatu. Wanafunzi hao wamepangwa kulingana na ufaulu wao masomo waliyochagua na nafasi zilizopo,” alisisitiza.
 
Pia alisema nafasi za shule walizopangiwa wanafunzi zimezingatia miundombinu ya shule husika na uwezo, na kwamba kila shule imepewa wanafunzi kulingana na nafasi zilizopo, hivyo hakutakuwa na nafasi ya kuwabadilisha kutoka shule moja kwenda nyingine kwa sasa.
 
Kutokana na hali hiyo, aliwataka wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi kuripoti katika shule na vyuo walivyopangiwa kama walivyoelekezwa.
 
Alisema mwanafunzi ambaye hataripoti ifikapo Julai 24, ambayo ni tarehe ya mwisho kwa muda uliopangwa, atakuwa amepoteza nafasi yake kwa kuwa itachukuliwa na mwanafunzi mwingine ambaye hakupata nafasi awali.
Share:

AJALI YA BASI:WATU WATANO WAFARIKI ,13 WAJERUHIWA JIJINI MWANZA



WATU watano wamefariki dunia na wengine 13 kujeruhiwa katika ajali ya basi lenye namba za usajili T. 449 BCB mali ya kampuni ya Super Sami lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Mwanza.Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamikia leo katika eneo la Bashini Kata ya Mabuki Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, baada ya gari hilo kugonga jiwe lililokuwa barabarani na kusababisha William Elias, Dereva wa gari hilo kushindwa kulimdu.Watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni Valieth Odede, William Elias (Dereva) huku mwanaume mmoja na wanawake wawili wenye umri wa miaka 25- 30 majina yao bado yakiwa bado hayajafahamika mpaka hivi sasa.
Majeruhi katika ajali hiyo ni 13, ambao ni Sophia Miraji, Kibilo Mwacha, Boniphace Charles na Frank Kunyumi ambao wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya awali kutokana na kujeruhiwa vibaya.
Wengine ni Stanley Zacharia, Sia Dauson, Hellen Leheke, Michael Leonard, Kudra Ibrahim (mtoto wa miaka miwili), Zamda Issa, Marieth Christopher, Elizabeth Simon na Dickson Msamba ambao wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando (BMC) jijini hapa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, akizungumzia tukio hilo, amesema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari hilo kuwa katika mwendo kasi na kusababisha ashindwe kulimdu basi hilo na kusababisha kupinduka.
Msangi, amesema kuwa kutokana na ajali hiyo jeshi la Polisi mkoani hapa linaendelea kuchunguza gari hilo pamoja na kufanya uchunguzi juu ya ajali hiyo iliosababisha vifo vya watu watano kupoteza maisha na wengine 13 kujeruhiwa.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNE TAREHE 29.6.2016

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger