Sunday 31 January 2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI “UVUMI WA AJIRA ZA MADAKTARI JWTZ”

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

jwtz
Hivi karibuni kumekuwa na uvumi unaoeleza kuwa JWTZ limetoa nafasi za kazi kwa vijana wenye fani ya Udaktari na kuwataka vijana hao kuripoti Makao Makuu na vyeti vyao kwaajili ya usaili.
Habari hizo si za kweli,JWTZ kama zilivyo taasisi nyingine za serilikali lina mfumo rasmi wa kutangaza habari zake hivyo jeshi linawaomba wananchi wazipuuzie taarifa hizo.
Aidha JWTZ linawataka wamiliki wa mitandao ya kijamii kutotoa taarifa za jeshi bila kuwasiliana na Makao Makuu ya jeshi kinyume na utaratibu huu,unawasababishia wananchi usumbufu usio wa lazima.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano Makao Makuu JWTZ.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARY TAREHE 31/01/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Saturday 30 January 2016

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARY 30 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Share:

Friday 29 January 2016

PICHA:ATHARI YA MVUA DAR ZAANZA KULETA MAFURIKO

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Vijana wakiwa wamekaa nje baada ya nyumba wanazoishi kujaa maji maeneo ya Jangwani jijini Dar es Salaam kufuatia mvua zilizonyesha.
Vijana wakiwa wamekaa nje baada ya nyumba wanazoishi kujaa maji maeneo ya Jangwani jijini Dar es Salaam kufuatia mvua zilizonyesha.
 Kituo cha daladala za kwenda Gongolamboto cha Suwata Kariakoo kikiwa kimejaa maji hivyo  kuleta adha kwa watumiaji kufuatia mvuo hizo.
 Dimbwi la maji likiwa mbele ya jengo la Yanga.
 Daraja la Jangwani na Kituo cha mabasi ya mwendokasi kikiwa kimezingirwa na maji.
 Magari yakipita kwenye dimbwi la maji barabara ya mtaa wa Lindi Ilala.
 Moja ya vibanda wanavyoishi wananchi waliobomolewa eneo la Kinondoni Mkwajuni maji yakipita katikati yake jambo ambalo ni hatari kwa watu wanaoishi ndani humo.
 Nyumba ikiwa imezingirwa na maji eneo la Mchikichini Ilala kufuatia mvua hiyo iliyonyesha leo
Vijana wakiuangalia Uwanja wa Klabu ya Yanga ulivyojaa maji.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger