Tuesday 24 January 2017

MAJAMBAZI WAWILI 2 WAUAWA JIJINI MWANZA

...
Watu wawili waliokuwa wakituhumiwa kwa ujambazi wameuawa wakati wakitaka kujaribu kuwatoroka askari polisi wilayani Ilemela mkoani Mwanza

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza amesema kwamba tukio hilo lilitokea  tarehe 20.01.2016 majira ya saa 2:30  usiku, katika mtaa wa kiloleli “A” kata ya Nyasaka mkoa wa Mwanza na kuwataja majambazi waliouawa kuwa ni Eric Magese miaka 22, na aliyejulikana kwa jina moja la Peter miaka kati 25 hadi 27 wote wakazi wa Mecco jijini Mwanza.

Amesema majambazi hao waliuawa wakati wakijaribu kutoroka askari polisi pindi wakiwapeleka mahali ambapo wenzao wamejificha ili waweze kufanya uvamizi.

Amesema kuwa katika tukio hilo pia ilipatikana silaha moja aina ya short gun yenye namba TZ CAR 103283 ikiwa na risasi tatu ambayo inadaiwa walipora kwenye kampuni ya ulinzi iitwayo Malika Security Service Limited

Msangi amesema majambazi hao walikuwa wakitafutwa na polisi baada ya kufanya unyang’anyi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali jijini Mwanza ilikiwemo tukio la Kitangiri mnamo tarehe 19.12.2016 na tukio la tarehe 02.01.2016 katika mtaa wa Nyasaka.

Jinsi walivyouawa
Msangi amesema baada ya upelelezi uliofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao, walikubali kuwapeleka askari katika eneo ambalo walikuwa wamepanga pamoja na wenzao wawili kwa ajili ya kufanya matukio zaidi ya ujambazi.

Amesema walipofika katika eneo hilo, watuhumiwa hao walipiga kelele kama ishara ya kuwatorosha wenzao na kuanza kuwakimbia askari.

Askari walifyatua risasi kadhaa hewani wakiwaamuru wasimame lakini waligoma ndipo waliwafyatulia risasi za mguuni kwa bahati mbaya ziliwalenga maeneo ya juu ambapo walifariki dunia wakati wakipelekwa hospitali.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger