Wednesday 22 July 2015

Kemikali zinavyoathiri sehemu za siri za wanawake

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Wanawake hupenda sana kutumia marashi na vitu vingine kama sabuni zenye kemikali kwa ajili ya kujirembesha.
Baadhi yao wamekuwa wakipenda usafi wao binafsi wakitumia vitu  ambavyo baadhi yake ni hatari kwani wengine wanapenda kusafisha sehemu zao za siri kwa kutumia sabuni zenye kemikali, pafyumu yaani ‘deodorant’ au kupaka mafuta bila kujua madhara yake.
Wanawake hao wanaotumia vitu hivyo wana hatari ya kupata magonjwa ya zinaa au ya kuambukiza. Watafiti katika Chuo Kikuu cha California, Marekani wanasema sabuni ngumu au hata za maji, pafyumu ‘deodorant’ zinaharibu tishu muhimu zilizomo
ndani kabisa ya uke.
Uharibifu huo wa tishu ndani ya sehemu za siri humweka mhusika katika hatari ya kupata malengelenge, fangasi  vitu ambavyo huweza kusababisha kupata Ukimwi ikiwa watajamiiana na watu wenye tatizo hilo.
Sabuni au dawa zinazouzwa na wafanyabiashara zikitangaza kuboresha uke au kuondoa harufu kwenye sehemu hizo nyeti nazo zina madhara.
 Sabuni au mafuta yenye kemikali  huchubua ngozi laini ya uke na ni rahisi vimelea vya magonjwa kuenea kwa urahisi.
Michubuko hiyo ambayo si rahisi kuonekana kwa macho ndicho chanzo cha kuingia kwa maradhi ya kuambukiza.
Kutokana na hayo ni wazi kwamba hakuna haja ya kuweka kemikali, au pafyumu ukeni. Hizo sehemu zinahitaji kuoshwa vizuri kwa maji safi.
Kemikali inapoingia ukeni inavuruga hali ya kawaida na asidi inayolinda sehemu hizo ni vyema wanawake wakaelimishwa kuhusu matumizi ya bidhaa zinaweka harufu nzuri katika sehemu zao za siri, kurudisha bikira au mafuta ya kulainisha uke.
Wanawake wanaofanya usafi sehemu zao za siri kwa kutumia bidhaa au baadhi ya vifaa visivyofaa kutumiwa ukeni huweza kupata saratani ya shingo ya uzazi.
Bidhaa zenye kemikali ya ‘coal tar,’ ambazo mara nyingine huwekwa kwenye sabuni ama manukato na kutumiwa ukeni na wanawake huweza kuchochea saratani hiyo.
Upo ushahidi wa kutosha kuwa kutumia sabuni za kuogea za maji au ngumu katika sehemu za siri za ndani za mwanamke kunaharibu uwiano wa bakteria na kusababisha bakteria kuzalishwa kwa wingi na kumweka mwanamke katika hatari ya maradhi ya  zinaa ya kuambukiza.
USHAURI
Acha kutumia sabuni zenye kemikali au pafyumu sehemu za siri kwani husababisha hayo niliyoyataja hapo juu.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger