Monday 2 June 2014

BONGO MOVIE BIFU MWANZO MWISHO,BIFU LA RAY NA JOHARI

...
Ishu! Wakurugenzi wa Kampuni ya RJ Productions, waliowahi kudaiwa kutoka kimalovee, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Blandina Chagula ‘Johari’ wametoa kali ya katika Makaburi ya Kinondoni, Dar, wakati wa mazishi ya mwigizaji mwenzao, Sheila Haule ‘Recho’ baada ya kuombwa kwa pamoja wainuke kuweka shada kaburini lakini wao wakachengana.

Wakurugenzi wa Kampuni ya RJ Productions, waliowahi kudaiwa kutoka kimalovee, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Blandina Chagula ‘Johari’ wakiweka shada za maua kaburini,kila mmoja kivyake bila ya umoja wowowte.

Katika tukio hilo lililoshuhudiwa na mwanahabari wetu, MC Salum Mchoma ‘Chiki’ alisikika akisema kuwa sasa ni zamu ya watu kuweka mashada spesho ndipo akawainua mastaa hao ambapo Ray baada ya kusikia jina lake alionekana kushtuka kidogo kabla hajachukua uamuzi wa kwenda kuweka shada hilo.
Badala ya kuchukua shada moja kila mmoja alichukua lake huku kila mmoja akimchenga mwezake.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger