Friday, 8 February 2019

SUMAYE AUGUA GHAFLA KWENYE ZIARA YA CHADEMA TANGA

...

 Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye ameugua ghafla akiwa mkoani Tanga.

Sumaye ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya Chadema amepatwa na tatizo la afya akiwa katika majukumu ya kichama.

Taarifa iliyotolewa leo mchana Ijumaa Februari 8, 2019 na Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Habari wa Chadema, Tumaini Makene imesema, “Sumaye alikuwa mkoani Tanga, akiendelea na ratiba ya ziara ya shughuli za chama kabla ya kupatwa na shida ya afya ghafla leo asubuhi.”

“Baada ya kutibiwa hali yake inaendelea vizuri na sasa amepumzika wakati mipango ya kumsafirisha kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo hii kwa ajili ya uchunguzi zaidi ikifanyika.”

Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger